Aziza wa Facebok Sehemu ya Kwanza
CHOMBEZO

Ep 01: Aziza wa Facebok

SIMULIZI Aziza wa Facebok
Aziza wa Facebok Sehemu ya Kwanza

IMEANDIKWA NA : NYEMO CHILONGANI

*********************************************************************************

Chombezo: Aziza wa Facebok

Sehemu ya Kwanza (1)

Najisikia nimechoka sana, nimechoka sana kwa sababu nilikuwa nimetoka

kucheza mpira uwanjani huku nikiwa nimechafuka kupita kawaida. Ninapofika

nyumbani, ninaoga na kisha kuchukua simu yangu kwa ajili ya kuangalia

updates za facebook, sikukuta hata meseji

moja zaidi ya notification tu, tena wala hazikuwa nyingi. Nilichokifanya ni kuanza

kuzugazuga hapa na pale na kisha kutulia. Mara ghafla nikaona namba moja

nyekundu kwenye sehemu ya meseji, kulikuwa na meseji imeingia,

nilichokifanya, nikaifungua na kuanza kuchati na mtu huyo huyo.

EDUADO: Mambo vipi Shahruk Khan.

MIMI: Hahahha! Poa. Inakuwaje wewe mtu.

EDUADO: Kama kawa. Nilikuwa nakusubiri sana hewani. Nilikuwa na mzuka na wewe ile mbaya.

MIMI: Duh! Mzuka na mimi! Kuna nini tena?

EDUADO: Kuna bonge la kazi hapa. Unataka?

MIMI: Kwa nini nisitake? Nipe mawasiliano yao niandike barua ya kuomba kazi fasta.

EDUADO: Hahahaha! Kaka unakosea. Niliposema kazi sikumaanisha hiyo.

MIMI: Wewe ulimaanisha ipi sasa?

EDUADO: Kazi moja hivi. Kazi ambayo watu wengi wameishindwa hasa masharobaro.

MIMI: Hahahaha! Itakuwa kubeba zege hiyo watoto wa mama hawaiwezi. Mimi naiweza, hebu niambie ni jengo gani.

EDUADO: Sio kazi ya kubeba zege. Kuna mtu nataka umfanyie kazi.

MIMI: Mtu gani?

EDUADO: Kuna mrembo fulani nipo nae hapa UDSM ni mkali ile mbaya. Yaani mkali

mpaka nashindwa kusema ukali wake unafanana na nini.

MIMI: Hebu acha masihala kaka. Kwa hiyo kama mkali mimi nifanyeje nini?

EDUADO: Huyu mrembo anaringa mbaya. Yaani mrembo ananata utafikiri akanyagi ardhi hii tunayochimbia vyoo.

MIMI: Ok! Wazuri wapo wengi na hata wenye maringo wapo wengi pia. Hebu niambie kuhusu huyo. Kwanza anaitwa nani. Nipe maelezo ya kujitosheleza na sio naanza kumtengeneza mrembo

mkali kichwani mwangu ikawa ndivyo sivyo.

EDUADO: Huyu mrembo anaitwa Aziza Moody, anaishi Msasani, baba yake ni

mfanyabiashara mkubwa sana aisee. Ni mrembo fulani pini…yaani ni pini sana.

MIMI: Hebu acha masihala. Sasa inakuwaje watoto wa kisharobaro wamemshindwa.

EDUADO: Huyu mrembo hafagilii muonekano, ni mrembo fulani ambaye anapenda mtu

anamfuate kama jinsi alivyo. Yaani kama wewe ni mtu wa chini, mfuate hivyo hivyo ila tatizo

watoto wa hapa chuo wanapenda kumfuata kisharobaro kaka.

MIMI: Dah! Kwa hiyo kazi unayotaka kunipa ni ipi?

EDUADO: Umchukue huyu mtoto. Yaani ukifanikiwa, moyo wangu utakuwa mweupeeeeeee

kama theluji.

MIMI: Hahaha! Usitake kunichekesha EDUADO, hivi unamkumbuka Sikitu?

EDUADO: Sikitu yupi?

MIMI: Si yule mrembo wa mwaka jana ambaye ulikuwa unamsifia sanaaaaa kwamba

mkali kumbe wala hakuwa mkali kama ulivyokuwa ukimsifia, mbaya zaidi alikuwa anakaa mbali, Musomaaaaaa.

EDUADO: Acha na hayo, yule msahau kwani mimi mwenyewe alinitumia picha ambayo sio

yake. Ila kaka kiukweli Aziza ni mrembo mmoja mkali sana. Hapa chuo amekuwa

gumzo kila kona, vijana wengi wamechemka.

MIMI: Sasa kama wengine wamechemka mimi nitaweza vipi?

EDUADO: Hahahaha! Kaka ninakuamini sanaaaa, wewe mtu unaweza sana kuongea,

unaweza sana kuandika. Endapo kazi nikakupa na kisha ukashindwa, haki ya Mungu nitajua kweli

duniani kuna wasichana wagumu.

MIMI: Kwa hiyo kazi yako ina malipo au?

EDUADO: Ikitokea umempata, nitakupa zawadi kaka. Yaani ninachokitaka huyu mrembo

umchukue tu, basiiiiiiii. Anaringa sana, ananata sana, yaani sijui niseme vipi.

MIMI: Ila si anaringa kwa sababu mzuri?

EDUADO: Ndio. Ila yeye kazidi.

MIMI: Ila kwa sasa aisee nahisi nimepoteza kumbukumbu zangu za kuongea na hawa

watoto wa kike, sijui kama nitaweza.

EDUADO: Acha kunitania kaka. Nakuamini sana kwamba unaweza kuliko mtu yeyote

na ndio maana nikakufuata wewe. Hivi haujiulizi kwa nini sikumfuata Thomas? Thomas

kwenye kuongea mkali sana ila kwenye kuandika hakuna kitu, ila wewe, aisee una kipaji

kila kona, nafikiri hata ukimtokea kiziwi, hachomoiiiiiiiiii.

MIMI: Hahaha! Hebu acha kunipamba. Hebu niambie, huyo mrembo yupo Facebook?

EDUADO: Amejaa teleeee…yaani kajaa teleeee. Anajiita Aziza M Aziza. Ni mrembo mkali sana.

Hebu mcheki kwanza.

MIMI: Sawa.

Sikutaka kuchelewa, tayari kichwa changu kikaanza kujazwa na sura nyingi za wasichana

wazuri huku nikianza kuzigawanya kimakundi kwamba huyu alikuwa Aziza mwenyewe

huyu hakuwa mwenyewe. Nilikuwa namfahamu EDUADO toka tupo katika shule ya

sekondari, alipokuwa akisema msichana fulani ni mzuri, mzuri kweli japokuwa kwa

Sikitu alikuwa ameniingiza choo cha kike. Sikutaka kuremba, mara baada ya kuona

majina kadhaa, nikamfuata Eduado inbox.

MIMI: Oyaa Akshey.

EDUADO: Vipi ushampata?

MIMI: Wamekuja wakina Aziza wengi hao, mpaka wengine wanakaa India.

EDUADO: Hebu subiri.

Sikujua alikuwa akifanya nini, kwa sababu aliniambia kwamba nisubiri,

wala sikuwa na presha, nikamsubiri nione angeniambia kitu gani baada ya hapo.

Nilimsubiri kwa kipindi kama cha dakika moja hivi, akanijia tena inbox.

EDUADO: Umeiona hiyo picha yenye mdoli wa Barbie?

MIMI: Yeah!

EDUADO: Ndiye yeye huyo. Ibra huyo ni mrembo mkali ambaye sijawahi kuona.

MIMI: Acha utani.

EDUADO: Shua. Unamkumbuka Silvia tuliyesoma nae? Sasa Silvia haingii kwa Aziza.

MIMI: Acha utani kaka. Silvia haingii?

EDUADO: Kweli tena. Tena hagusi hata robo.

MIMI: Sasa mbona hajaweka picha yake, nitamjua vipi kama ni mkali.

Hebu nipe sifa kwanza manake naona picha zake kazipiga pini watu wasio

marafiki zake wasizione.

EDUADO: Kwanza mrembo ni pini sana, mrembo kwao wana mahela ya kumwaga,

chuo anakuja na gari, Verrosa moja nyeusi, mtoto anamiliki laptop aina ya

Apple ile inaayouzwa milioni tatu, mtoto anamiliki anamiliki iPhone

5 huku akisema kwamba iPhone 6 ikianza kuuzwa atataka kuanza kuitumia

kwani anapenda kwenda na wakati.

MIMI: Kaka utakuwa unanitania tu.

EDUADO: Kweli tena. Halafu kuna cha zaidi.

MIMI: Kipi?

EDUADO: Otea.

MIMI: Hebu niambie kipi?

EDUADO: Ugonjwa wako.

MIMI:Unamaanisha nini?

EDUADO: Mtoto Mpemba.

MIMI: Hahahaha! Kaka acha utani, utanifanya nimfuate sasa hivi.

EDUADO: Ndio hivyo. Mtoto ni pini sana, pini ile iliyosimama.

MIMI: Hahaha! Pini kama ya Blackberry vile.

EDUADO: Acha kaka. Mtoto ni pini zaidi ya zile za Blackberry.

Kwanza ukimuona tu, mtoto utampenda. Mavazi yake sasa…weeeeeee.

1

MIMI: Hebu nipe sifa zake kwa ujumla.

EDUADO: Nisikilize. Mtoto ni wa kipemba.

Ana nywele ndefu zinazomfikia chini ya mabega yake,

mtoto ana hipsi zilizopangika, hapa mashavuni mwake ana vijishimo viwili,

lipsi lainiiiii kila wakati zinang’aaaaa.

MIMI: Kingine?

EDUADO: Mtoto ana sura nyembamba, masikio hayaonekani sana,

ifuani hapa kumesimama vizuri sana, mavazi yake huwa ni suruali za jinsi kwa sana.

MIMI: Umesema anaishi wapi?

EDUADO: Anaishi Masaki.

MIMI: Halafu mimi naishi uswahilini Tandale. Umesema anamiliki simu gani?

EDUADO: Anamiliki iPhone 5.

MIMI: Halafu mimi namiliki Nokia ya Tochi. Umesema baba yake ana gari?

EDUADO: Yeah! Yeye mwenyewe analo.

MIMI: Mimi sina gari na baba yangu hana hata gari.

EDUADO: Acha kujizarau Ibra. Mtoto unang’oa huyu.

MIMI: Usijali. Ushawahi kufika kwao?

EDUADO: Yeah kaka. Kwanza hiyo nyumba yao….duh! Kuna watu wanakufuru. Kwanza bonge la nyumba. Limezungushiwa ukuta, jumba lina fensi kwa juu, ndani kuna kamera, nyumba vigae, ukiingia ndani unakutana na bwawa la kuogelea. Kuna ungo wa Dstv, kuna bustani kali ya maua mbalimbali, kuna walinzi wawili ambao wanalinda kwa bunduki kutoka Knight. Yaani wapo full.

MIMI: Ok! Mimi naishi Tandale. Nyumba yetu ndogo, haina ukuta wala fensi, haina mlinzi na kama kuogea, tunaogea bafuni na si kwenye bwawa. Mpaka hapo, nimeshamkosa.

EDUADO: Ibra. Usiniangushe. Yaani mimi lengo langu umchukue huyu mtoto tu.

MIMI: Una namba zake za simu?

EDUADO: Hapana.

MIMI: Basi ngoja nifanye mishe halafu nione itakuwaje. Ila wasiwasi wangu ule ule tu, itakuwa kama Sikitu.

EDUADO: Usijali kaka. Huyu sio kama Sikitu. Kwanza yule demu mwenyewe alinitaka nikaamua kukurushia wewe. Mimi na mrembo wa mkoa wapi na wapi. Ishi Dar tuwe tunamalizana, mambo ya mikoani haya, tigo pesa zinatumika sanaaaa. Hapa hapa Bongo ndio kuzuri, ukimtaka tu,

nauli yako sh 400 kwenda, 400 kurudi. 600 soda yako, 600 soda yake. Mwisho wa siku kwa

gharama zote ukitoa buku tano, michenji inarudi mingi mpaka mfuko unaomba poo kwa kuzidiwa uzito.

MIMI: Hahaha! Umeonaeeeee. Hakuna gharama kabisa. Ila poa, usijali. Ngoja nimtumie friend request halafu nianze kumfanyia uninja. Ila niandalie zawadi yangu.

EDUADO: Usijali kaka. Wewe fanya yako, ukimaliza, niache nami nifanye yangu. Au sio?

MIMI: Poa. Mia mia. Ngoja nianze kazi.

EDUADO: Shwari. Ngoja nifanye yangu. Nataka nimfuate mtoto Magreth hapa.

MIMI: Ndio yupi huyo?

EDUADO: Si yule wa facebook wa kipindi kileeeee.

MIMI: Kwani ushang’oa?

EDUADO: Chezea mimi wewe. Mimi noma…kama ni wembe basi Gilette.

MIMI: Sasa mbona hujamkata Aziza kama ni Gilette.

EDUADO: Aziza ana chembechembe za chuma. Ningemkataje? Huyo nakuachia kama wewe mwenye yale maji ya kuyeyushia vyuma ndio utakwenda nae sawa.

MIMI: Basi poa. Acha nikufanyie kazi yako mkurugenzi. Kazi hii niliachana nayo zamani sana ila kwa ajili yako, navaa gwanda nikukamilishie halafu nisepetue.

EDUADO: Mia mia.

Hapo nikatulia kwanza. Nikaanza kujifikiria ni kwa jinsi gani nilitakiwa kuanza kumfuata msichana Aziza. Kitu ambacho kilikuwa kikiniumiza kichwa changu kwa wakati huo ni kwamba hata Aziza mwenyewe sikuwahi kumuona kwa hiyo niliogopa kuuziwa mbuzi kwenye kiroba kama ilivyokuwa kwa Sikitu. Ngoja nikupe kijistori changu na huyu Sikitu.

Eduado alinifuata inbox na kuniambia kuhusu Sikitu, alimsifia na kumpamba sana, alinifanya nivutiwe nae sana na yeye alitaka nimchukue, nikasema poa. Mzee nikaanza mishemishe zangu kama Michael Scotfield wa Prison Break na kweli ndani ya wiki mbili, mtoto akawa mikononi mwangu. Unajua jinsi mtu anavyokwambia kwamba msichana mzuri hata kama wewe mwenyewe haujamuona unaanza kumtengeneza msichana wako kichwani, hivyo ndivyo nilivyofanya kwa Sikitu. Nikamtengeneza Sikitu wangu kichwani, kumbe nilikuwa namuumba Sikitu wa tofauti bila kujua. Siku aliponitumia picha yake inbox niione mara baada ya kumlazimisha sanaaa, akanitumia. Alikuwa mrembo lakini hakuwa na urembo kama ambao Eduado aliniambia. Nikaachana nae.

Sikitu hakukoma, chating zangu nzuri za inbox za maneno ya hapa na pale alikuwa akizipenda sana, hivyo alitaka tuendelee kuchati. Haikuwezekana tena, nilimkatia maguu mara baada ya kuniambia kwamba anaishi Musoma, mbaya zaidi huku Dar hakuwa hata na ndugu kwa hiyo hakuwa na ndoto za kuja Dar, sasa mimi ningeonania nae wapi? Yaani nisafiri mpaka Musoma kwa ajili yake? Niliona kuwa suala gumu sana kufanyika. Basi ndio hivyo, tukapotezana potezana na hatimae mapenzi kutoweka, siku hizi simuoni, bila shaka, kaniblock.

Baada ya miezi miwili, leo Eduado kaja na mpya, kaja na mrembo mpya ambaye wala sijawahi kumuona, huyu anaitwa Aziza. Sikutaka kufanya vitu kwa presha sana, nilichokifanya ni kumuomba urafiki na kisha kuanza kusubiria majibu. Kila siku nilipokuwa naingia facebook, hakuwa amenikubalia, sikuwa na shaka, niliendelea kusubiria zaidi na zaidi na baada ya siku mbili, akakubali kuwa rafiki yangu, furaha iliyoje? Hapo ndipo nilipoamua kuuanza mchezo wangu, mchezo ule ule ambao ulimfanya Sikitu kuchanganyikiwa kwangu, ila kwa hapa, kutokana na sifa ambazo niliambiwa na Eduado, ilinipasa nitumie mbinu kubwa zaidi, mbinu ambazo zingeendana na uzuri wake, mtoto wa kipemba bwana, hakutakiwa kufuatwa kikawaida, nami nikaanza kumfuata kipemba kipemba na mapenzi ya Kihindi….mtu mzima nikawa najiona kama Shahruk Khan vile.


Mtu mzima nikaingia kazini kwa ajili ya kuanza kazi yangu ambayo nilikuwa nimepewa ya kuhakikisha kwamba mtoto wa Kipemba, Aziza anakuwa wangu. Ni kweli kwa mambo ambayo alikuwa amenieleza Eduado yalikuwa yamekwishanitenga kwa kiasi kikubwa sana kutoka kwa Aziza lakini ilitakiwa pia nifanye yangu katika kipindi hicho.

Kitendo cha Aziza kuukubali urafiki pamoja nami kilionekana kuwa kitu kizuri sana, kwa hiyo nilichokifanya nikajifanya bonge la bwege, nikamfuata kwa wall yake na kuandika ‘Asante A’ na kisha kusikilizia.

Kweli, kama alivyosema Eduado ilikuwa vile vile, mrembo hakuiLIKE asante yangu wala kuitolea comment, nikaona poa, vyote hivi ni mwanzo wa kumbukumbu zangu nitakazompa hapo baadae. Kwa upande wa Eduado, hakutaka kujishika, kila siku alikuwa akinisumbua tu kwa inbox.

EDUADO: Kaka vipi?

MIMI: Kuhusu nini?

EDUADO: Mtoto. Hujaniambia chochote kile. Umefanikiwa au?

MIMI: Wewe umeniambia mambo mengi kuhusiana na huyu mrembo, unadhani ningeweza kumamilisha ndani ya siku tatu?

EDUADO: Hapana. Nilikuwa nauliza manake nimeona hapa sasa hivi u rafiki yake.

MIMI: Yeah! Ni rafiki yangu ila kila kitu kinatakiwa kufanywa kimahesabu.

EDUADO: Usiniangushe basi Sharukh Khan.

MIMI: Hilo usijali.

Katika kipindi hicho nilikuwa nafikiria mambo mengi sana, huyu mtoto kwangu alionekana kuwa na pozi ajabu, yaani nilikuwa nikizipitia post za kizushi alizokuwa akiziweka, watu walikuwa wakicomment halafu yeye hatokei. Hata kama kaweka picha ya mdoli, watu walikuwa wakicomment halafu yeye hatokei na mbaya zaidi kulikuwa na watu wengi wanaolike na kucomment jambo lililonifanya kugundua kwamba kuna siku huyu msichana alikwishawahi kuweka picha na hivyo wanaume kujua ni mzuri na kisha kuzitoa.

Bado kiu yangu ilikuwa ni kuwasiliana na Aziza tu ambaye alionekana kuwa mtu wa mapozi sana. Sikujua ningeanzia wapi ila nilichokifanya ni kuanza kumtumia meseji nione kama angeijibu au kuipotezea.

2

MIMI: Mambo!

Niliituma meseji hiyo, siku ya kwanza, ya pili, ya tatu mpaka wiki hadi mwezi lakini meseji ile moja haikujibiwa, mbaya zaidi nilikuwa namuona yupo hewani. Sikukoma kidume mimi, bado nilikuwa nikimtumia meseji za kumsalimia lakini hali ilikuwa vile vile, hakujibu.

Mtu mzima nikaona naumbuka, kama nilikuwa naitwa Sharukh Khan basi ilibidi niwaonyeshe watu kwamba hawakukosea kuniita jina hilo, nilitaka kuwaonyeshea dhahiri kwamba mama yangu alikuwa mtu wa Tanga, kule ambapo mapenzi yalikuwa yamenogeshwa kwa kuwekewa makorokocho. Nilichoanza kukifanya ni kuanza kumtag picha. Hapa ni lazima ugundue, picha ambazo nilikuwa nikimtag ni zile ambazo zilikuwa na muonekano wa kimapenzi tu. Picha ambazo zilikuwa zikiwaonyesha wapenzi wakibusiana na kukumbatiana, ndizo ambazo nilikuwa nikimtag, tena yeye peke yake.

Hahaha! Ule ukaonekana kama ujinga vile kumbe kwa wakati huo nilikuwa na target zangu kichwani. Niliendelea na mtindo ule ule mpaka siku ambayo akaonekana kuchoka na kukasirika, kwa mara ya kwanza akaja inbox, ila sio kiamani kama nilivyotaka, alikuja kibifu.

AZIZA: Naomba usiwe unanitag mapicha yako.

Niliisoma meseji ile. Kwanza nikacheka, kilichonifanya kucheka ni kwa kumuona kwamba alikuwa msichana mjinga sana, kitendo cha yeye kuniandikia meseji kilionekana kuwa kama kosa kubwa sana, nilichokifanya, nikaanza kuandika meseji ndefu, meseji ambayo ingemfanya kunijibu, meseji ambayo isingemfanya kubaki kimya.

MIMI: Kuna vitu kadhaa Aziza itakupasa uelewe na ninatumaini vitakuongoza katika maisha yako yote. Jitahidi kuishi lakini kamwe usiwe mbinafsi. Unapopata kitu, usitake kukaa nacho, jaribu kuchangia pamoja na wenzako. Unapopata chakula, jaribu kumwangalia yule asiye na chakula na kumgawia, milele atakushukuru kwa ulichomfanyia siku moja tu alipokuwa na njaa. Unapomuona mtu hana nguo, mgawie nguo na ataendelea kukushukuru maisha yake yote. Unaniona mimi, mimi si mbinafsi hata mara moja, katika maisha yangu nimekuwa nikiwapa watu vitu fulani vitu ambavyo hawana katika maisha yao, nikakuangalia wewe, nikakuona kwamba u masikini sana, ukijiangalia, unajiona kuwa tajiri, mwenye fedha labda, lakini bado ni masikini, masikini wa kitu kimoja ambacho ulihitaji mtu mwenye kitu hicho akusaidie, nikakusaidia lakini unaonekana kuukataa msaada wangu. Kuwa makini Aziza, mara nyingine msaada huja mara moja na kupotea, unapoutafuta, inawezekana usiuone tena.

Kwanza nikashusha pumzi nzito, nikaiangalia meseji ile na kisha kuirudia rudia mara nyingi nyingi na kisha kuituma. Niliiona kuwa meseji kali ambayo isingemfanya kubaki kimya kwa kutaka kujua ni kitu gani ambacho alikuwa amekosa katika maisha yake, kilichonifurahisha, akatuma meseji. Kuna nini tena? Meseji ya pili hiyo, hakujua kwamba ndio mwanzo wa chating yetu.

AZIZA: Umemaanisha nini?

MIMI: Nimemaanisha kwamba wewe ni masikini. Tena yule fukara kabisa. Hiyo ndio maana yangu.

AZIZA: Sijakuelewa.

MIMI: Hebu isome vizuri hiyo meseji, utaielewa tu.

AZIZA: Nimeirudia zaidi ya mara tano, sijaielewa, naomba uniambie umemaanisha nini.

MIMI: Nikuulize kitu kimoja?

AZIZA: Niulize.

MIMI: Unaweza kugundua ni umasikini wa aina gani umekuwa nao?

AZIZA: Hapana na ndio maana nikauliza.

MIMI: Inawezekana ukawa na magari, nyumba na fedha ila bado ukawa masikini, unakubaliana nami?

AZIZA: Hapana.

MIMI: Kwa sababu gani?

AZIZA: Mtu ana kila kitu, atakuwaje masikini.

MIMI: Hahahah! Aziza. Ukisema hivyo unakosea. Kuwa na kila kitu haimaanishi kwamba wewe si masikini. Unaniruhusu nikuulize kitu?

AZIZA: Niulize

MIMI: Unaamini katika fedha?

AZIZA: Yeah!

MIMI: Fedha inaweza kukupa kila ukitakacho?

AZIZA: Yeah!

MIMI: Unakosea sana Aziza.

AZIZA: Unapokuwa na fedha unanunua gari ulitakalo, unanunua chakula, unanunua nyumba na mambo mengine. Kwani nimekosea?

MIMI: Umepatia. Ila unavyoona kila mtu mwenye fedha huwa na furaha?

AZIZA: Inawezekana.

MIMI: Umekosea. Umekwishawahi kuwasikia wale matajiri wanaojiua?

AZIZA: Yeah!

MMI: Sasa wamekosa nini wale katika maisha yao? Wana fedha, wanaweza kununua kila kitu, wana magari, wanaweza kwenda sehemu yoyote ile. Ila swali linakuja kwa sababu gani wanajiua?

AZIZA: Mmmh! Sijui.

MIMI: Hahaha! Jibu rahisi sana. Walikosa furaha, amani, wakakosa mapenzi na mambo mengine. Unapokuwa na fedha, utanunua gari ila kumbuka hautoweza kununua furaha, unapokuwa na fedha utaweza kumnunua msichana mtaani lakini ukashindwa kununua mapenzi. Umenipata hapo?

AZIZA: Kidogoooo.

MIMI: Yeah! Kila mtu hunipata kidogo, ila tukiendelea kuchati, utanipata sana tu. Utaniruhusu niwe nachati nawe kwa ajili ya kukuambia mengi usiyoyajua?

AZIZA: Yeah! Ila huwa siwi hewani muda wote.

MIMI: Hilo si tatizo. Unachotakiwa ni kunishtua kila unapokuwa hewani. Utakwenda kufahamu mengi ambayo haujayajua. Kwani unaishi wapi?

AZIZA: Nipo Masaki Dar es Salaam.

MIMI: Ndio maana.

AZIZA: Kwa nini?

MIMI: Usijali. Mtaa unaokaa ndio nitakaoanza nao siku tukianza kuchati. Kwa sasa nahitaji kusoma, naomba uniruhusu niondoke.

AZIZA: Ila pleeeaseeee naomba uniambie.

MIMI: Sijakataa. Nitakwambia tu wala usijali. Wewe ni rafiki yangu, pamoja kuwa na kila kitu, yakupasa kupata vitu vingine ambavyo haupaswi kuvinunua. Nitakwambia namna ya kuvipata na inawezekana hata marafiki zako wakakushangaa.

AZIZA: Mmmh!

MIMI: Usigune. Huo ndio ukweli. Usiku mwema Aziza.

AZIZA: Nawe pia.

ITAENDELEA

Aziza wa Facebok Sehemu ya Pili

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment