Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034 Sehemu ya Kwanza
KIJASUSI

Ep 01: Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034

SIMULIZI Vipepeo Weusi Mkakati Namba 0034
Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034 Sehemu ya Kwanza

IMEANDIKWA NA: THE BOLD

*********************************************************************************

Simulizi: Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034

Sehemu ya Kwanza (1)

Muhimu: Simulizi hii inaakisi namna ambavyo kila mmoja wetu anaguswa na mambo ya siri yanayofanywa na watu wenye nguvu na ushawishi. Pia simulizi hii inajitahidi kugusia ulimwengu wa hatari wa “conspiracies” na Ujasusi. Pia msimuliaji anaonyesha namna ambavyo nguvu ya mapenzi inaweza kuokoa nafsi ya mtu na kumfanya kuwa bora kwa wanomzunguka na nchi yake.

Kumbuka simulizi hii ni ya kutunga. Wahusika, matukio na visa vyote vinavyosimuliwa ni vya kufikirika, hivyo mfanano wowote na mtu katika maisha halisi ni bahati mbaya.

Tafadhali si ruhusa kutumia andishi hili mahali popote pasipo ruhusa ya muandishi.

VIPEPEO WEUSI: MKAKATI NAMBA 0034

“Nipe mahali pa kusimama na ndoano mkononi mwangu, naweza nikainua dunia.” – The

MIAKA 3 ILIYOPITA, Dar es Salaam.

Nimezaliwa miaka 29, miezi minne, wiki mbili, siku tano, masaa 18, na dakika 40 zilizopita. Jina langu naitwa Rweyemamu Charles Kajuna, lakini marafiki na wanafamilia hupendelea kuniita kwa kifupi, Ray.

Nakumbuka miaka mitatu iliyopita. Siku ya kwanza waliponifuata. Siku ya kwanza nilipo fahamu kuwa wanataka niwe mmoja wao au angalau yafaa kusema niwe kibaraka wao.

Ilikuwa siku alhamisi, jioni yapata majira ya saa kumi na mbili kasoro, walifika wakiwa ndani ya gari nyeusi aina ya Land Ceuiser V8. Nilikuwa nimelala kitandani lakini niliamka baada ya kumsikia Shangazi akiongea nao nje.

Nyumba yetu ilikuwa pembezoni mwa barabara ya mtaa katika maeneo ya Mwembe Chai, na nyumba yetu haikuwa na uzio. Hivyo nilivyo amka kutoka kitandani na kuchungulia dirishani niliweza kuwaona wageni waliokuwa wanaongea na Shangazi.

Walikuwa wamepaki gari yao nyeusi ng’ambo ya barabara. Watu wawili walishuka kutoka kwenye gari na kuja mpaka mlangoni mwa nyumba yetu. Wakagonga mlango na shangazi akatoka kuwasikiliza.

Haya yote nilikuwa nayaona kupitia dirishani. Kitu cha kwanza kilichoisumbua roho yangu baada ya kuwaona watu hawa ilikuwa ni gari waliyokuja nayo. Kichwani mwangu nilishawishika kabisa gari hii naifahamu na nimewahi kuiona lakini kumbukumbu ilikuwa haiji ni wapi niliiona au naifahamu vipi.

Nikahisi labda kuna mahusiano na bahasha niliyoipokea wiki mbili zilizopita, nikiwa ofisini Morogoro ililetwa na mtoto anayeuza machungwa akidai kuwa amepewa na mtu nje ya jengo letu la ofisi na akaambiwa aje amkabidhi mtu anayeitwa Ray.

Ndani ya bahasha hii nilikuta simu na kikaratasi kimeandikwa “speed dial 1”, ikimaanisha nibonyeze kwa muda kitufe namba moja cha simu ili simu ipige. Suala hili nilikuwa sijalifanya mpaka leo hii na sikuwa na mpango wa kulifanya kwani ni uchizi kutii maagizo ambayo hata haufahamu yaliko toka.

Hisia zangu zikaendelea kufikiri labda watu hawa wana uhusiano na bahasha ile. Lakini pia roho yangu ilizidi kusumbuka kila nilipoiangalia ile gari waliyokuja nayo. Kadiri nilovyoiangalia ndivyo nilivyozidi kushawishika kuwa naifahamu, lakini bahati mbaya sikuweza kukumbuka niliiona wapi.

Nikiwa bado niko dirishani nachungulia kuangalia kinachoendelea mara shangazi akaniita kutokea nje, “Ray.!!”

“Naaaam.!” Nikamuitikia huku nikisogea kwenye dirisha sikuataka wajue kuwa nilikuwa nawachungulia mda wote huu.

“Kuna wageni wako nje hapa”

“Nakuja” nikajibu huku navaa pensi mda wote huu nilikuwa nimevaa bukta ya kulalia na singlendi.

Kabla sijatoka chumbani kwangu, nikachukua begi la mgongoni ambalo lilikuwa pembeni ya kitanda na kufungua zipu kisha nikatoa bahasha pamoja na simu nilivyovipokea wiki mbili zilizopita. Nikaiweka simu ndani ya bahasha na kuikunja ili niweze kuishika mkononi.

Baada ya kufungua mlango na kutoka nikiwa sebuleni shangazi naye alikuwa ndio anaingia kutoka nje. Nikamuuliza “kwanini hujawakaribisha ndani wageni”.

“Wamesema hawakai wana haraka” akanijibu kwa ufupi huku akielekea chumbani kwake. Nikafungua mlango nikatoka nje. Wageni wangu walikuwa ni watu wawili, mmoja alikuwa ni muhindi, mtu mzima kiasi mwenye umri kati ta miaka 40 hadi 42 na mwenzake alikuwa ni mswahili na kijana zaidi kwa makadirio ya umri kuanzia miaka 34 hadi 36.

Yule muhindi alikuwa amevalia shati, suruali ya jinzi na viatu vyeusi, na yule mwenzake mswahili alikuwa amevalia suti ya kaunda. Jamaa huyu mswahili alikuwa na mwili uliojengeka kimazoezi kiasi kwamba hata suti ilikuwa imemkaa sawia. Kwa mtazamo wa haraka nikahisi kwamba jamaa huyu mswahili alikuwa ni mlinzi binafsi wa huyu muhindi.

“Hujambo Ray?” Yule muhindi alisalimia huku anatabasamu mara tu nilipofika walipokuwa wamesimama.

Sikutaka kuitikia salamu yao, nikaenda moja kwa moja kwenye hisia zangu “mmefuata mzigo wenu?” Nikawauliza huku nawaonyesha bahasha niliyotoka nayo ndani.

Yule muhindi akatoa tabasamu kubwa na kuniuliza “nini kinachokufanya uhisi huo ni mzigo wetu na ndicho kilichotuleta?”.

“Kama sio mzigo wenu niambieni niurudishe ndani alafu nije niwasikilize hicho kilicho waleta?” Nikaongea kwa kujiamini huku nimemkazia macho yule muhindi.

Akaichukua bahasha kutoka mkononi mwangu kisha akampa yule mswahili aishike, kisha akaniuliza kwa kifupi tu “kwa nini haukupiga simu?”.

“Mimi sio mpumbavu nifuate maelekezo nipige simu wakati hata sijui hiyo bahasha ilikotoka!” Nikamjibu haraka huku nikijitahidi kuonyesha kujiamini. Yule muhindi akatabasamu tena huku akitingisha kichwa “ndio maana tumeamua tuje ili tuongee kwa mdomo, relax” akaongea yule muhindi.

“Siwezi kurelax wakati siwafahamu hata nyinyi ni kina nani, mnatokea wapi na mnataka nini.” Nikajitutumua zaidi. Rohoni nilijisikia raha kwasababu nilijihisi kama nimeshika usukani wa haya maongezi.

“ooohh usijali, mimi naitwa Sultan na mwenzangu anaitwa Kevin”

Nikamkazia macho yule muhindi huku, na yeye akinikodolea macho kana kwamba anajaribu kusoma ninachofikiria.

“Mmejitambulisha wawili tu, kwanini hamjamtambukisha mtu wa tatu mliyekuja naye?” Nikamuuliza huku nimemkazia macho kwa kujiamini.

Yule muhindi Sultan akageuka wakatazamana na yule mswahili Kevin kisha akanitizama mimi, “Ray mtu gani wa tatu unamuongelea”

Sikupepesa macho wala kutazama pembeni, nikaendelea kumkazia macho na nikasogea hatua moja mbele kuelekea aliposimama Sultan. Kisha nikamuangalia moja kwa moja machoni kwa kujiamini na kumueleza, “nimewaona tangu mnakuja, mlipofika hapa na gari lenu wewe ulishuka kwenye gari kwa mlango wa kushoto wa mbele, na huyu mwenzio alishuka kutoka mlango wa nyuma, kwahiyo nina hakika kuna aliyekaa upande wa kulia mbele ambaye ndiye anayeendesha gari na hajashuka!”

Nilipowaambia maneno hayo wote macho yetu kwa pamoja yakaelekea kwenye gari lililokuwa wamepaki ng’ambo ya barabara. Gari ilikuwa na vioo vyeusi visivyoonyesha ndani. Kutokana na pale tulipokuwa tumesimama nikafanikiwa kuona namba za gari, T 228 CNL. Namba hizi zikazidi kuniaminisha hisia zangu kuwa gari hii naifahamu lakini bado kumbukumbu zangu haziji kuelewa gari ile niliwahi kuiona wapi.

Sultan akaangaliana na mwenzake Kevin kisha Kevin akatingisha kichwa kumpa kama ishara ya kukubali. Kisha akaniangalia mimi, “ok Ray, twende tukamsalimu”.

Tukavuka barabara mpaka mahali walipopaki gari. Tulipofika Kevin akagonga kwa kidole kioo cha gari. Kioo kikafunguliwa taratibu na kilipofunguka chote mpaka chini, ndipo hapa nikaelewa kwanini kumbukumbu zangu ziliniambia kuwa nalifahamu hili gari.

Ndani ya gari kwenye siti ya dereva alikuwa ameketi Dr. Boniface Shirima.

Dr. Shirima ni mwalimu wangu wa Uchumi, au yafaa kusema alikuwa mwalimu wangu wa uchumi Chuo Kikuu cha Mzumbe kabla sijahairisha masomo miezi minne iliyopita ili niweze kujizatiti katika shughuli zangu za taasisi niliyoianzisha.

Nilimuangalia kwa mshangao kwa dakika kadhaa bila kuongea chochote.

Bumbuwazi langu lilikatishwa na Dr. Shirima ambaye alitabasamu na kunisalimu “hujambo Rweyemamu?”

“Shikamoo dokta, tafadhali nieleze kinachoendelea hapa sielewi” nikamjibu haraka haraka ndani ya nafsi yangu nikihisi kuwa labda walau sasa kuna mtu ninaye mfahamu anaweza kunieleza mini kinaendelea.

“Usijali Ray, kwanini haukupiga simu wiki mbili zote hizi” Dr. Shirima alikwepa swali langu na kuniuliza swali lingine.

“Dokta nimeshawaeleza hawa wenzako nimeletewa bahasha katika mazingira ya kutatanisha na ndani nakuta simu yenye kikaratsi chenye maelezo kwamba nipige simu!

Mimi sio mpuuzi kiasi hicho kufuata maelezo nisiyoyajua yalikotoka” nikamjibu Dr. Shirima, kwa mbali hasira zilinza kunishika kwenye nafsi. Nilianza kuchoshwa na hiki kilichokuwa kinachoendelea.

Kana kwamba Dr. Shirima alisoma akili yangu kwa haraka akendeleza maongezi, “Ray, hauna haja ya kuogopa wala kuwa na wasiwasi. Inawezekana haujafikiria hili lakini nchi hii inahitaji vijana wenye maono kama yako. Sisi ni marafiki, pia tuna pambana usiku na mchana kuhakikisha nchi inasonga mbele”

Kwa muda wa sekunde chache nikajaribu kutafsiri maneno yake kichwani ili niweze kuelewa kile ambacho labda alimaanisha na alikuwa hakitamki. Nikatafakari maneno kadhaa ‘nchi inahitaji vijana wenye kama yako’, ‘tunapambana usiku na mchana kuhakikisha nchi inasonga mbele’!

Kiasi nikahisi kama nimemuelewa anachojaribu kukisema, hivyo nikataka nipate uhakika nikamuuliza, “Dokta kama mko na Idara ya Usalama wa Taifa, sidhani kama huu ndio utaratibu wa kurecruit watu ku….”

“No no no no hatuko na Usalama wa Taifa” Dr. Shirima alinikatsha kabla sijamalza nilichotaka kusema.

“Kama sio Usalama wa Taifa, nyinyi ni akina nani?” Nikamuuliza nikionyesha wazi mshangao wangu.

Dr. Shirima hakunijibu moja kwa moja akaingiza mkono kwenye begi dogo lilikuwa pembeni yake na kutoa simu inayofanana kabisa na ile niliyoletewa wiki mbili zilizopita niliyo wakabidhi Sultan na Kevin. Akanikabidhi simu na kunambia, “ni rahisi sana kukujibu sisi ni akina nani na kwanini tunakuhitaji, unachotakiwa kufanya, leo ikifika saa nne usiku bonyeza ‘speed dial’ namba 1”

Nikaipokea simu, nikaiangalia na kuigeuza geuza, nikijiuliza kichwani nimrudishie au nifanyeje?

“Na kama sitopiga simu hiyo saa nne?” Nikamuuliza.

Dr. Shirima akainamisha kichwa chini kama anafikiria kitu hivi kisha akaniangalia usoni, “kama hutopiga simu basi tutaachana nawe, lakini kabla haujafanya uamuzi huo kumbula kitu kimoja, nafahamu ni kiasi gani unapata tabu kutafuta funds za kuendesha program yako ya ‘Sote Hub’! Tuna uwezo wa kukusaidia kwenye hilo, we can point you to the right direction upate hizo funds” Dr. Shirima alinieleza huku amenikazia macho, alijua wazi kabisa ni kiasi gani maneno haya yatakuwa yamenigusa moyoni.

Moyo wangu ulilipuka niliposikia anataja kuhusu ‘kuniwezesha kupata funds kwa ajili ya ‘Sote Hub’. Nikamuangalia usoni, Dr. Shirima akatabasamu, nilikuwa na uhakika kuwa amefahamu ni kiasi gani maneno aliyoyasema yamenigusa.

Akatabasamu, “Ray, fikiria kwa makini uamuzi ni wako, leo saa nne usiku fanya uamuzi sahihi.” Akanieleza kwa kifupi huku akiwapa ishara wenzake Sultan na Kevin ambao mda wote walikuwa wamesimama kando yangu wakifuatilia mazungumzo yetu mimi ma Dr. Shayo. Wakapanda kwenye gari na mimi nikaanza kuondoka.

“Hey Ray..” Dokta aliniita, nilikuwa nataka kuvuka barabara na wao walikuwa wameshawasha gari. Nikageuka.

“Yes..” Nikamuitikia

“Msalimie cheupe!” Dr. Shirima akaniambia kwa utani huku anatabasamu. Na mimi nikashindwa kuzuia tabasamu usoni, nikamuitikia tu kwa kutingisha kichwa. Kichwani mwangu nikawaza “hawa washenzi wanafahamu vitu vingapi kuhusu mimi?”. Nikatabasamu.

Wakawasha gari na kuondoka na mimi nikavuka barabara na kurejea nyumbani.

Nilipoingia ndani nikamkuta shngazi sebuleni na aliponiona tu akaanza kuniangalia kwa macho ya udadisi.

“Uko sawa?” Akaniukiza huku bado ananitazama kwa kijicho cha udadisi.

“Yeah shangazi, niko poa tu” nikamjibu kwa mkato huku nikielekea chumbani, sikutaka kubaki sebuleni hata dakika moja maana namfahamu shangazi yangu, ungeanza mfululizo wa maswali ambayo nilikuwa sitaki kuyajibu mda huu. Lazima angeanza kuniuliza Wale kina nani, wamesemaje, wanataka nini, unafahamiana nao vipi??

No, sikutaka kujibu maswali haya sasa, nikapitiliza mpaka chumbani kwangu na kufunga mlango.

Nilipofika chumbani nikajitupa kitandani kifudifudi, “aaaaaaarrrrggghh”. Nikajiungurumia mwenyewe. Kichwa kilikuwa kinauzunguka nikitafakari mambo kadhaa kwa wakati mmoja.

Kitu kikubwa zaidi nilichokuwa nakiwaza na kikijirudia tena na tena akilini mwangu ilikuwa ni kauli ya D. Shirima, “tunaweza kukusaidia kupata funds kwaajili ya ‘Sote Hub'”. Nilitabasamu kila nilipofikiria kauli hii. Nikajiuliza ni kama ni kweli wana uwezo wa kufanya hivyo au ilikuwa ni mbinu ya kunipata na kuniingiza katika mipango yao waliyo nayo ambayo bado sikuijua mpaka muda huu.

Lakini jambo moja lilikuwa bayana, kwamba ndani ya mwezi mmoja ujao kama sitoweza kupata funds kwa ajili ya program ya Sote Hub sitakuwa na chaguo lingine zaidi ya kutii amri ya serikali ya kufunga ofisi.

Kila nilipofikiria dhana ya kufunga ofisi moyo wangu uliniuma na kulipuka. Nikikumbuka jinsi nilivyo vuja jasho na ‘damu’ mpaka kuanzisha Sote Hub, hakika kufunga ofisi itakuwa moja ya mapigo yatakayo niuma zaidi kwa maisha yangu yote.

Nikikumbuka jinsi safari ya kuanzisha Sote Hub ilivyo moyo wangu uliuma.

Safari hii ilianza mwaka mkoja uliopita nikiwa kama mwanafunzi wa mwaka wa kwanza chuo kikuu cha Mzumbe nikichukua shahada ya ‘Economics and Project Planning’.

Nilipata wazo la kusaidia wanafunzi wenye talanta ya ujasiriamali. Nikaanzisha shindano la michanganuo ya biashara. Shindano hili nililiita ‘Anzisha Business Competition’. Nikapata ufadhili kutoka kampuni ya Coca Cola.

Wanafunzi kutoka vyuo mbali mbali Tanzania walituma michanganuo yao ya mawazo ya biashara. Kisha mimi pamoja na panel yangu akiwemo Dr. Shirima ambaye alikuwa ni mwalimu wangu wa uchumi na moja ya watu ninaowahusudu sana kitaaluma kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuona mambo kwa mtazamo mpana zaidi, tulichagua wanafunzi thelathini wenye mawazo bora zaidi kisha tukawashindanisha na kuwachuja na kubaki na wanafunzi kumi pekee ambao waliingia raundi ya mwisho ya fainali.

Fainali za shindano hili la Anzisha Business Competition zilirushwa kwenye televisheni ambapo washiriki walijieleza juu ya idea zao hizo na namna gani zitakavyo tekelezeka na kuleta faida za kiuchumi kwao na kuajiri vijana wengine.

Mshindi wa kwanza alipewa shilingi milioni kumi kutoka kampuni ya Coca Cola na mshindi wa pili alipatiwa milioni tano na watatu milioni mbili.

Miezi mitatu baadae tulipotembelea washindi hawa kufanya tahimini ya shindano tukakuta wote biashara zao walizianzisha lakini zimekufa.

Ndipo hapo katika kikao chetu cha majumuisho, nakumbuka Dr. Shirima akaeleza kuwa kumpatia mtu fedha pekee haisaidii bali anahitaji pia apatiwe mafunzo afahamu ulimwengu wa ujasiriamali ukoje, afundishwe kuhusu kutambua masoko, branding ya bidhaa yake na hata apate ‘mentor’ wa kumjenga kisaikolojia kuhusu biashara.

Ndipo hapa nikiwa mwanafunzi wa mwaka wa pili, nikachukua hatua ya kuanzisha kituo cha kukuza biashara za vijana wenye ideas za tofauti na zenye uwezo wa Kukuwa kuwa kampuni kubwa.

Nilidhamiria kituo hiki kichukue vijana wenye mawazo bora kabisa ya kibiashara, kisha wapewe mafunzo kuhusu masoko na ‘branding’, watafutiwe mentors na mwishoni wapemwe mtaji wa kuanzisha biashara zao (seed capital).

Sisi kama kampuni tunaowasimamia tutachukua asilimia ndogo za hisa katika kampuni zao watakazo zianzisha.

Nikasajili kituo/kampuni hii kama ‘Sote Hub’ (SOTE – startup operations and trainings in Entrepreneurship).

Nikavuja jasho kuhangaika usiku na mchana kutafuta wafadhili wa kusaidia kuanzisha program hii. Baada ya miezi kadhaa ndipo nikafanikisha kuingia mkataba na Vodacom kudhamini hii programu. Ambapo kwa mwaka wa kwanza watatoa kiasi cha shilingi milioni 120 ambazo zitatolewa kwa awamu tatu, milioni 40 kila baada ya miezi minne.

Kwakuwa nilikuwa bado mwanafunzi chuo kikuu mzumbe, hivyo kituo hiki nikakianzisha Morogoro mjini na ofisi zake zilikuwa katika ghorofa la Hajram Mtaa wa Boma Road.

Ofisi na programu yenyewe zikazinduliwa kwa sherehe kubwa ya kufana mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Wilaya Morogoro. Ikarushwa katika taarifa za habari za televisheni mbali mbali na kutokea kwenye magazeti.

Vodacom wakanipa awamu ya kwanza ya funding, shilingi milioni 40. Utekelezaji wa programu ukaanza. Vijana kutoka kila pembe ya nchi wakatuma michanganuo ya biashara. Tukatumia takribani miezi miwili kupitia michanganuo yote na hatimae kupata vijana watano ambao ndio watakuwa chini ya programu hii kwa awamu hii ya kwanza.

Tukafanya press conference kuwatangaza. Vijana wakasafiri kutoka walipo wakaja Morogoro. Lengo lilikuwa ni ‘kuwapiga msasa’ kuhusu masuala ya kibiashara kwa miezi mitatu kisha mwishoni wanapatiwa seed capital ya milioni 10 kila mmoja.

Kutokana na kuwa bize sana kusimamia shugjuli za programu ikanibidi nihairishe masomo chuoni.

Vijana wakapatiwa mafunzo kwa mwezi wa kwanza. Ilipofikia mwanzoni mwa mwezi wa pili wa Programu, kukatokea mabadiliko makubwa ya kisera na uongozi ndani ya Vodacom. Uongozi mpya ukasitisha mikataba mingi ya udhamini ukiwepo mkataba wao na Sote Hub.

Hapa ndipo mushkeli ulipoanza katika maisha yangu. Nikahangaika usiku na mchana kutafuta sponsor mwingine wa kusaidia kuifikisha mwisho programu tuliyoianza lakini hakukuwa na mafanikio yoyote.

Sasa leo hii napata wageni tata, ambao ni dhahiri wana agenda ya siri na mimi na wanaahidi “tunaweza kukusaidi upate funding kwaajili ya Sote Hub”.

Nilibaki na alama ya kuuliza kichwani. Niliwaza na kuwazua kwa masaa kadhaa. Nikaangalia saa kwenye simu ilionyesha ni saa tatu na dakika tano.

Nikachukua simu nimpigie Hasnat. Yes, Hasnat. Roho ya roho yangu. Mtu pekee ambaye nikisikia sauti yake hata niwe nimepaniki kiasi gani kila kitu kinakuwa shwari. Hasnat, mwanamke wa maisha yangu. Mwanamke niliyempenda na tunapendana tokea utotoni, na mwanamke pekee ambaye nataka niendelee kumpenda kwa maisha yangu yote duniani. Hasnat, mwanamke anayenifahamu pengine kuliko hata mimi ninavyojifahamu.

Nikachukua simu na kumpigia.

“Nambie kichwa” Sauti ya Hasnat iliongea kutoka upande wa pili wa simu. Taratibu taharuki yangu ikaanza kuyeyuka.

“Fesh tu, uko poa cheupe”

“Niko poa baba, nimechoka choka tu nilikuwa discussion ndio naingia room sahizi hapa wakati unapiga”

“Ok, skia cheupe! I have some bad news and worse news, what do you want first?”

“Hahahaha no i want the good news”

“OK! Kuna watu wamekuja home leo wanataka kunisaidia nipate funding kwaajili ya Sote Hub, the problem is I don’t trust tem..”

“Are you kidding me, that’s really a good news, kwanini unasema ni habari mbaya and kwanini huwatrust?”

“Sijui nisemeje but nadhani its better nichukulie hii positively, unakumbuka ile stori nilikwambia kwenye nchi za Asia wanaamini ukitembea barabarani kipepeo akikugusa hiyo inaashiria baraka, labda ndio vipepeo wenyewe hawa hahaha.”

“Yeah but sio kila kipepeo ana rangi za kupendeza, vipepeo wengine ni vipepeo weusi majanga tupu hahahaha kidding honey, I think you should take the deal”

“Yeah kesho nitaenda kuonana nao”

“That’s ma boi, good luck honey mi wacha nilale nimechoka kinyama yani”

“Poa! Usiku mwema cheupe, nakupenda”

“love you more kichwa”

Hasnat alikuwa na miujiza ya aina yake au labda ni kutokana na kumpenda kupindukia, kwani kusikia sauti yake tu kulifanya taharuki yote iliyokuwepo ndani yangu kuyeyuka. Lakini kuna maneno aliyoyatamka yaliendelea kujirudia kichwani mwangu na kufanya kuanza kurudiwa na hofu. “Sio kila kipepeo ana rangi ya kupendeza, kuna Vipepeo weusi pia”. Maneno haya yalijirudia tena na tena kichwani.

Nikaangalia tena saa kwenye simu, ilikuwa ni saa nne na dakika mbili. Nikajipa moyo, “fu*k it! Wawe na rangi ya kupendeza au nyeusi, kipepeo ni kipepeo tu”

Nikachukua simu niliyopewa na Dr. Shirima na kubonyeza speed dial namba moja na kuweka sikioni.

“Halo!” Nikasubiri kusikia sauti kutoka upande wa pili.

“Una peni na karatasi hapo” sauti nzito upande wa pili wa simu iliongea bila hata kuitikia salamu yangu wala yeye kunisalimia. Haraka haraka nikafungua zipu kwenye begi la mgongoni lililokuwa pembeni mwa kitanda na kutoa kalamu.

“Ndio ninavyo” nikamjibu haraka haraka.

“Kesho saa kumi na nusu, PPF House, ghorofa ya saba, Unimax Marketing, jina lako ni Ally Hassan” ikaongea sauti upande wa pili wa simu bila nukta, haraka haraka.

“What, jina langu ni Rweyem…..” Kabla sijamaliza kuongea simu ilikuwa imekata.

Nikaangalia taarifa nilizokuwa nandika kwenye kikaratasi nilipokuwa natajiwa na ile sauti kwenye simu. ‘Saa kumi na nusu. PPF House. Ghorofa ya Saba. Unimax Marketing. Ally Hassan.’

“What the fu*k is this?” Nikajisemea kimoyo moyo..

Nikakikunja kile kikaratasi nikakiweka kwenye begi la mgongoni pembeni ya kitanda, kisha nikajilaza nikitafakari hiki kinachoendelea. Na baada ya kama dakika ishirini usingizi ukanipitia.


Saa kwenye simu ilikuwa inanionyesha ni saa tisa na dakika arobaini. Nilikuwa nje nimesimama nasubiria taxi. Nilikuwa nimempigia simu Musa, dereva taxi maarufu maeneo ya mwembechai ninaye mfahamu toka niko nasoma sekondari.

Kama dakika tano baadae Musa aliwasili na bila kuchelewa kama ilivyo ada yetu waswahili nikafungua mlango wa mbele na kukaa pembeni ya dereva badala ya kukaa siti ya nyuma ambapo ndipo haswa anapotakiwa kukaa abiria.

“Niaje kichwa?” Musa akinisalimu kwa uchangamfu na tabasamu kama ilivyo kawaida yake.

“Poa tu, mishe vipi” nikamjibu na kumuuliza.

“Mishe mwanana tu mwanangu! Adimu sana kichwa vipi mtoto mzuri gani kakuficha mwanangu hahaha!” Kama kawaida Musa akaanza masikhara na kucheka kama kawaida yake.

Musa alikuwa na desturi ya kupenda masihara na mara zote yeye mwenyewe ndiye anakuwa wa kwanza kucheka kwa sauti kubwa hahahaha.

“Nifichwe wapi mwanangu! Kutafuta ugali tu.” Nikamjibu.

“Nakuaminia sana baharia wangu! Alafu unajua j’mo tunawakalisha kama watoto”

Daah ndio akanikumbusha kuwa jumamosi kuna mechi kali ya Barcelena na Madrid. Mawazo niliyokuwa nayo yalinisahalisha kabisa kuwa kuna mambo mengine yanayoendelea duniani.

Musa alikuwa mnazi wa Barcelona na mimi nilikuwa mnazi wa Madrid.

“Mumkalishe nani wachumba nyinyi, subiri uone tunavyowapakata” nikamjibu nikijitahidi kuwa natural kuficha mawazo niliyo nayo kichwani.

“Tunaelekea wapi babu?” Hatimaye akaniuliza.

“Stesheni mwanangu, PPF House.”

“Mia mia”

Safari ikaendelea pamoja na utani wa hapa na pale, na dakika ishirini baadae tukafika PPF.

Nikatoa noti mbili za elfu kumi nikampatia Musa. “Ya uchakavu hii mwanangu” nikampatia

“Shukrani” Musa akajibu huku anatoa shilingi efu tano anirudishie chenji.

“Zuia hiyo mwanangu usijali” nikamzuia asinipe chenji.

“Dah shukrani kichwa”

“Mia”

Tukaagana na kushuka kwenye gari nikaingia ndani ya jengo la PPF House.

Jengo hili nalifahamu vizuri sana, kuna shemeji yangu alikuwa anafanya kazi hapa miaka ya nyuma, nimewahi kufika hapa mara kadhaa lakini sikuwahi kusikia kampuni ya Unimax Marketing kuwa na ofisi katika jengo hili. Nilikuwa najua PPF wenyewe, Sumatra na kampuni nyingine kutumia jengo hili lakini sio Unimax Marketing. Na si hivyo tu bali pia hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuisikia kampuni ya Unimax Marketing.

Nikaenda mpaka kwenye meza ya kuandika majina ya wageni.

Mlinzi akaniuliza “Mfanyakazi au mgeni?”

“Mgeni” nikamjibu kwa mkato.

Akanisogozea kaunta book lililokuwa limefunguliwa liko juu ya meza.

Nikalivuta karibu na kabla sijaandika nikapitisha macho haraka haraka na niliangalia zaidi kwenye jedwali watu wanapoandika ofisi anayo kwenda. Nikaona majina tu ya PPF, Sumatta, BUMACO yakiwa yanajirudia rudia lakini sikuona Unimax Markering hata sehemu moja.

Nikaandika jina langu, kisha nikapita kwenye Mashine ya ukaguzi na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye lifti. Kwenye lifti nikabonyeza kitufe namba saba na ndani ya dakika moja mlango wa lifti ukafunguka nikiwa ghorofa namba saba.

Nilitoka na kusimama koridoni na mbele yangu kulikuwa na mlango wa kioo ulioandikwa Unimax Marketing. Nikaufungua na kwenda moja kwa moja mpaka kwenye meza ya mapokezi.

“Habari yako dada” nikamsalimu mdada mrembo aliyekuwa mapokezi.

“Salama tu, nikusaida nini kaka” akaniuliza.

Nikashikwa na kigugumizi kwa sekunde kadhaa. Sikujua nimjibu nini. Anisaidie nini??.

“Aaaah natakiwa niwe hapa jina langu naitwa Ally Hassan” nikakumbuka jina nililotajiwa jana kwenye simu na nilijitahidi kujieleza kwa kumung’unya maneno.

“Subiri hapo kwenye kiti tafadhali”

Yule dada alinijibu haraka baada ya kumtajia jina la Ally hassan akionekana ameelewa ninachozungumza. Nikasogea pembeni na kukaa kwenye kiti cha wageni.

Dada akainua simu ya mezani na kumpigia mtu. “Amefika” alimwambia kwa kifupi huyo aliyekuwa anaongea nae. Baada ya hapo akawa bize anaendelea na shughuli zake. Dakika moja baadae akaja mdada mrefu, mrembo haswa amevalia sketi fupi nyeusi na shati jeupe.

“Habari, yako? Nifuate tafadhali”

Dada alinisalimu na kabla sijamjibu akanipa maelezo nimfuate.

Nikainuka na kumfuata. Kulikuwa na milango kadhaa ya ofisi yote ikiwa ya vioo, tukakata kushoto na kufuata korido iliyoenda moja kwa moja na mwishoni kulikuwa na mlango wa mbao. Yule dada akaufungua tukaingia. Ndani kulikuwa kama chumba cha daktari au theater. Nikaanza kushikwa na hofu kiasi.

Baada ya kuingia tu, akaingia mwanamama mwingine amevalia suti amebeba kibriefcace kidogo.

“Jina langu ni Zuhura na huyu mwenzangu anaitwa Jeniifer, atakufanyia utaratibu wa kawaida ili tuweze kuendelea na ratiba nyingine.” Aliongea yule dada mrefu. Siku sema chochote nilibaki tu nawakodolea macho.

Yule mama aliyetambulishwa kama Jennifer akaweka kibriefcase chake juu ya meza na kukifungua. Akatoa gloves na kuzivaa mkononi. Mapigo ya moyo yakaanza kuniaenda mbio. Nikaanza kujutia kwanini hata nimekuja hapa.

Mara akatoa bomba la sindano na pamba. “Naomba mkono wako wa kushoto” yule mama akaongea.

“Hey wait!” Nikafoka huku namuangalia yule dada aliyejitambulisha kama Zuhura. “Unaweza kinambia nini kinaendelea hapa.” Nikamuuliza huku natetemeka.

“Sikiliza Ray, tunaweza kuendelea na utaratibu au unaweza kufungua mlango na kuondoka” alinijibu huku amenikazia macho bila kuyapepesa.

Nikajishangaa mpaka mimi mwenyewe, Zuhura aliniruhusu kama sitaki kuendelea na ‘utaratibu’ wanaoufanya basi naweza kwenda,

lakini jambo la ajabu kuna sehemu kubwa ya nafsi yangu ilikuwa haitaki kuondoka, inataka kufika mwisho wa hili jambo. Ni kama unapotamani usinywe pombe lakini nafsi yako inashindwa kujizuia. Nikajifariji moyoni kuwa nimeshakula ng’ombe mzima wacha nimalizie mkia.

“Fu*k it!” nikajikuta nimetamka kwa nguvu na kumnyooshea mkono yule mama Jennifer. Atumia sindano kunitoa damu kiasi kwenye mkono wa kushoto na kisha sindano ile yenye damu akaihifadhi kwenye kifaa kama kimkebe na kurudisha kwenye briefcase yake. Kisha akatoa kifaa kama simu ya ‘tablet’ na kuanza kuniscan viganja vya mikono, akaanza na mkono wa kulia na kisha mkono wa kushoto. Nikaelewa alikuwa anachukua alama za vidole.

Akipomaliza akaweka vifaa vyake vyote kwenye briefcase na kuondoka.

“Tumemaliza tunaweza kuendelea sasa, nifuate” aliongea yule dada Zuhura huku akigeuka kuanza kuelekea kwenye mlango. Nikainuka na kumfuata. Tukapita tena koridoni kwenye milango ya vioo ya ofisi na kukata kushoto tukatokea mapokezi. Hapo tulimkuta jamaa ambaye jinsi alivyo vaa na umbo lake anafanana kabisa na Kevin ambaye alikuja Jana nyumbani.

Alikuwa na umbo la miraba minne na alikuwa amevalia Kaunda suti. Alipotuona akasimama. Tulipo mkaribia akafungua mlango na wote kwa pamoja mimi, Zuhura na huyo jamaa tukatoka nje kuelekea kwenye lifti.

Tukashuka chini na jamaa akatuongoza mpaka kwenye parking ya magari.

Tukapanda gari nyeusi inayofanana kabisa kabisa na waliyokuja nayo nyumbani Dr. Shirima na wenzake jana. Land cruiser V8 nyeusi.

Safari ikaanza tukaikamata Morogoro Road moja kwa moja mpaka Ubungo. Ubungo tukapinda kulia Kuifuata Barabara ya Sam Nujoma moja kwa Moja mpaka mwenge.

Kwenye makutano ya barabara tukanyoosha moja kwa moja na mbele kidogo tukakata kushoto kisha kulia. Nikaelewa kuwa tunaelekea Mikocheni B, kitu ambacho sikuwaelewa ni kwanini tumezunguka sana. Hii tayari ilikuwa imefika saa mbili usiku.

Mikocheni B tukapita Kanisa la Mlima wa Moto, tukaenda mbele kidogo mtaa wa nyuma yake. Tukaifikia nyumba moja iliyokuwa imejitenga kiasi na nyingine. Ilikuwa na uzio wa ukuta mrefu na juu una waya za umeme na geti kubwa.

Tulipofika nje ya geti hili bila kupiga honi geti likafunguliwa. Pembeni ya geti kwa ndani kulikuwa na watu wawili ambao walionekana walikuwa ni walinzi lakini walinzi hawa walikuwa na tofauti. Walikuwa wamevalia sawa kabisa na jamaa huyu tuliyeongozana nae kuja hapa na Kevin aliyekuja jana nyumbani. Wote wana miili ya mazoezi na walivalia Kaunda suti.

Nyumba hii ilikuwa na ghorofa moja na moja kwa moja jamaa akaenda kupaki gari ambapo hapa tulikuta karibia gari ishirini za aina tofauti. Range Rovers, V8, BMW, n.k. moja kwa moja nikajua gari hizi si za mtu mmoja bali kuna watu wamekuja nazo kama sisi. Hii ilimaanisha kulikuwa na kikao hapa. Na kwa muonekano wa gari hizi za gharama ni dhahiri kilikuwa ni kikao kizito.

Tukashuka kwenye gari, yule jamaa tuliyekuja naye akaelekea getini kwa ‘wenzake’ na Zuhura akaniongoza kuingia ndani ya Jumba hilo. Kadiri tulivyokuwa tuna pig a hatua kuingia ndani moyo wangi ulizidi kulipuka kwa hofu. Nilikuwa kwenye taharuki kubwa kiasi kwamba nilianza kutokwa jasho.

Baada ya kuingia ndani tukapandisha ngazi zilizokuwa zinaelekea juu ghorofani.

Tulivyofika juu, tukakutana na korido ndefu ambaye tuliifuata mpaka kufika katikati ilikuwa inaungana na korido nyingine ndogo mkono wa kushoto. Tukipokata kushoto kulikuwa na mlango mkubwa. Zuhura akaufungua na kunikaribisha ndani.

Kilikuwa ni chumba cha mikutano lakini hakikuwa na mtu. Kulikuwa na meza ndefu ya mikutano ya kiofisi na viti vinne kila upande.

Zuhura akaniashiria niketi.

“Subiri hapa” akanieleza kwa mkato tu kisha akatoka nje.

Ndani nikabaki peke yangu. Upande mmoja wa chumba hiki ulikuwa ni kioo tupu, hii iliniwezesha nione kwa urahisi kinachoendelea nje.

Baada ya kama dakika kumi hivi, nikaona nje geti linafunguliwa na gari tatu aina ya Range Rover ziliingia zikiwa zimeongozana. Baada ya kuingia hazikwenda kupark bali zilienda mpaka mlango wa mbele wa kuingia ndani ya nyumba. Magari mawili kati ya yale matatu, milango ilifunguliwa na watu wakashuka lakini gari la katikati milango haikufunguliwa kwa muda wa takribani dakika moja.

Wale walioshuka ambao wote wamevalia suti, waliangaza macho kila upande. Kisha wakafungua mlango wa nyuma wa gari ile ya kati kati na kuna mtu akashuka na wakaanza kuingia ndani ya jengo. Walitembea katika mtindo ambao yule mtu alikuwa katikati mbele yake kulikuwa na watu wawili, nyuma watu wawili na kulia na kushoto watu wawili wawili. Wakaingia ndani ya jengo. Nilijitahidi kadiri niwezavyo nione sura yake lakini sikufanikiwa kutokana na Giza na jinsi alivyozungukwa na walinzi.

Nikabaki nikitafakari sehemu hii nilipo. Nini kinaendelea, na kwenye hiki kitu nilichojiingiza. Nikajiuliza tena na tena, hawa watu ni akina nani, malengo yao ni nini na wanataka nini kutoka kwangu.

Niliwaza na kuwazua, nikasimama na kuanza kutembea kutoka upande mmoja wa chumba mpaka upande mwingine, tena na tena.

Baada ya kama dakika 45 msafara wa yule mtu mwenye walinzi ulitoka na moja kwa moja wakapanda kwenye gari zao na kuondoka. Kama dakika kumi baadae nikaona watu wengine karibia kumi na tano wanatoka na kwenda kupanda kwenye zile gari tulizozikuta wakati tunafika. Wote walikuwa wamevalia suti nadhifu na zote zilikuwa rangi nyeusi.

Nikajaribu kuwatazama kwa umakini niweze kung’amua walau watu wachache.

Nilipata mshtuko nilipoweza kuwang’amua watu wawili.

Wa kwanza alikuwa ni mfanyabiashara maarufu nchini na mmliki wa vyombo vya habari. Mzee Bernard Shayo

Wa pili alikuwa ni mbunge kijana na mwanasiasa mashuhuri nchini, Zephania Zuberi.

Presha ilinipanda na mshtuko nilioupata nikaanza kutokwa jasho mpaka shati nililolivaa kikaanza kulowa.

Nikakaa chini kwenye kiti. Nikitafakari, na kuwaza lakini akili ilikuwa haifanyi kazi kabisa kutokana na mshangao niliokuwa nao.

Mara mlango ukafunguliwa. Nilipigwa na butwa nilipomuona aliyeingia. Alikuwa ni Dr. Shirima akiwa amevalia suti nadhifu ya rangi nyeusi kama wale wengine niliowaona. Pia katika ukosi wa koti la suti usawa wa mfuko alikuwa ameweka pini kama ile inayovaliwa na viongozi wa kiserikali ikiwa na bendera ya nchi. Lakini pini hii ilikuwa tofauti, ilikuwa na rangi nzuri ya zambarau na kwa ndani ilikuwa na mchoro kama wa kichwa cha simba ambao ulikuwa na rangi ya dhahabu.

“Hujambo Ray?” Alinisalimia Dr. Shirima kwa tabasamu, mkononi alikuwa ameshika bahasha.

“Hapana dokta siko ok, nimeenda kwenye ofisi ambayo sijawahi kuisikia, nimetolewa damu, nimechukuliwa alama za vidole alafu naletwa hapa jumba lenye mazingira ya kutatanisha, so yes am not ok dr. Labda unieleze kinachoendelea.”

Kama kawaida yake, Dr. Shirima akatabasamu “Relax Ray.” Akaongea huku ananipa bahasha aliyokuwa ameishika mkononi.

Nikaipokea na kuiweka juu ya meza.

“Naomba upitie hizo document zilizomo ndani, kuna mambo namalizia kidogo nitarudi baada ya nusu saa! Zisome na uzielewe.” Dr. Shirima aliongea huku ananitazama usoni kwa udadisi. “Unaonekana kama una swali Ray, uliza.”

“Who are you people?” Nikamuuliza huku nimemkazia macho, nikiwa namaanisha kweli kweli.

“The Board! Karibu sana Ray.” Dr. Alinijibu kwa ufupi na kutoka nje.

Nilikuwa nimebaki tena peke yangu ndani ya chumba hiki ma nikiwa na nusu saa tu kupitia hizi document kabla Dr. Shirima hajarudi tujadiki hicho anachotaka tujadili. Nikaifungua ile bahasha. Ndani kulikuwa na karatsi zipatazo kumi na karatasi ya juu ilikuwa na kichwa cha habari T.B.F.Q Strategy # 0034.

Nikaketi kwa utulivu, nikavuta pumzi ndani na kuzishusha kwa taratibu. Akili ikakaa sawa. Nikaanza kuzisoma.

Leo June 20, 2016. Morogoro

Kwa kawaida nikiamka asubuhi lazima nifanye mazoezi ya kukimbia walau kilomita tatu. Nilikuwa ndio nimerejea kutoka kwenye kukimbia na nimeshamaliza kuoga niko najiandaa kwa ajili ya kuianza siku nyingine ya utafutaji na kujenga taifa.

Kwa karibia miaka mitatu huwa najaribu kuishi siku zangu nikijitahidi kadiri niwezavyo niishi kana kwamba tukio lililotokea miaka mitatu iliyopita kana kwamba halikuwahi kutokea. Kikao changu na The Board. Siku niliyopelekwa katika jumba lao la kukutania na wakanionyesha nyaraka zenye kichwa cha habari T.B.F.Q 0034.

Kwa kiwango kikubwa nimefanikiwa kuishi kana kwamba siku hiyo haikuwahi kutokea, lakini ni siku kama ya leo ndizo ambazo zinanifanya nikumbuke kila sekunde ya siku ile miaka mitatu iliyopita, nikumbuke kila hatua niliyopiga kuelekea kwenye kikao kile. Ni siku kama ya leo ambayo natamani niifast forward nijikute nimeamka kesho yake pasipo kuiishi siku ya leo.

Nilikuwa nimeletewa Ujumbe na mtu kuwa Dr. Shirima anahitaji tuonane. Mara ya mwisho kuonana naye ilikuwa ni miezi mitatu iliyopita. Alinipa maelezo ya kufanya, na leo hii naamini naenda kupewa ‘maelezo’ mengine.

Toka siku nimehudhuria kikao chao kule Mikocheni B Dar es Salaam Dr. Shirima amekuwa akitaka tuonane anaandika kikaratasi na kumpa mtu aniletee. Niliwahi kumuuliza kwanini asinipigie simu, akanijibu kuwa kwa mtu makini kamwe usipitishe taarifa muhimu kwa njia za kielektroniki. Haijalishj unahisi kompyuta au simu yako iko salama kiasi gani, akipatikana mtu mwenye weledi wa kutosha anaweza kuidukua hiyo taarifa kwa urahisi tu.

Jana nililetewa kikaratasi nyumbani kwangu mtaa wa Mazimbu. Kikaratasi kiliandikwa kwa kifupi tu;

“Kesho. 10:00 PM. Nashera Hotel

D.S. 13″

Leo tukikutana kitakuwa ni kikao chetu cha kumi na tatu mimi na yeye Dr. Shirima (D.S) tangu siku nilipoingizwa kwenye mkutano wa The Board ingawa mpaka sasa bado nilikuwa sielewi wananihesabia kama nani kwao. Mwenzao, mshirika wao au kibaraka wao.

Binafsi siwezi kujihesabia kama mmoja wao kwa kuwa sijawahi kuhudhuria hata kikao kimoja toka siku ile ya kwanza au yafaa kusema sikuwahi kualikwa tena.

Kwa miaka mitatu yote mtu pekee ambaye nimekuwa nikikutana naye ni Dr. Shirima. Na kila nikionana naye alikuwa akinipa maagizo, fanya hiki, fanya kile.

Kila nilipomuuliza mimi wananichukulia kama nani, kama kawaida yake alitabasamu na kunijibu kwa utulivu “Wewe ni mwenzetu Ray”!

Bullsh*t.! Kama mimi ni mwenzenu kwanini na mimi sihudhurii vikao vyenu vya mafichoni, kwanini na mimi siji kwenye mikutano yenu nimevaa suti nyeusi na kipini cha dhambarau na kicha cha simba cha dhahabu kwenye ukosi wa koti la suti kama nyinyi?? Sikuwahi kumtamkia mdomono lakini hayo ndiyo yalikuwa mawazo yangu kila mara aliponijibu kuwa “wewe ni mwenzetu Ray”.

Nilimalizia kujiandaa nifunga mlango ili nianze safari ya luelekea Nashera Hotel.

“Habari ya asubuhi Ray” Baba Bite alinisalimia.

Huyu alikuwa ni mpangaji mwenzangu. Nyumba yetu ilikwa imejengwa katika mtindo ambao, Kulikuwa na nyumba ndogo tatu (apartments) ndani ya uzio ila kila moja inajitegemea. Nyumba mbili zilikuwa ni nyumba za vyumba viwili na sebule, pamoja na jiko, na vyoo. Nyumba moja ilikuwa ni ya vyumba vitatu na sebule na jiko na vyoo.

Nyumba zote hizi Tatu zilikuwa ndani ya uzio mmoja wa ukuta.

Baba Bite na familia yake walikuwa wanakaa kwenye apartment ya vyumba vitatu. Alikuwa na mkewe, mtoto mmoja wa kike wa miaka minne aliyeitwa Beatrice lakini tulizoea kumuita Bite.

Apartment nyingine inayofanana na yangu yenye vyumba viwili na sebule, waliishi jamaa mmoja na demu wake. Yes demu wake kwa maana “wamewekana kinyumba” tu hawana ndoa. Walikuwa ni wahitimu wa Chuo miaka michache iliyopita. Hawa walikuwa wanaakisi kabisa maisha ya vijana wengi wa kitanzania waliomaliza vyuo na kufanikiwa kupata kazi. Walikuwa na ratiba ya kila ‘bata’ hapa mjini Morogoro. Kuna kipindi mpaka huwa najiuliza wanafanyaje kazi? Maana kila jumatatu wanaamka na ‘hangover’ sijui huko ofisini kwao wanafanyaje kazi. Ikifika ijumaa, bata linaanza mpaka jumapili usiku mnene. Kwahiyo siku pekee niliyokuwa na uhakika labda wanafanya kazi kwa uhakika ilikuwa ni Jumanne, Jumatano na alhamisi.

Mwanaume ni afisa mikopo FINCA na ‘demu’ wake yupo Ofisi za Tigo Huduma kwa Wateja hapa Morogoro.

Lakini Baba Bite na familia yake walikuwa tofauti sana. Walikuwa wanaakisi familia ambayo kila mtu angelipenda kuwa nayo. Walikuwa ni wacha Mungu pia. Sijawahi kumuona Baba Bite amechelewa kurudi kwake. Sikuwahi kuwasikia wanagombana, labda wagombane kimya kimya wenyewe kwa adabu. Tofauti na ‘bwana yule’ na demu wake, kila baada ya siku mbili utasikia anamfokea demu wake “we fala ntakuzibua ujue”.

Baba Bite alikuwa na duka ‘hardware” mjini na mkewe Mama Bite alikuwa mwalimu wa shule ya Sekondaei Kihonda. Ingawa walinizidi umri lakini hawakuwa watu wazima, Baba Bite mwenyewe kwa muonekano alikuwa hazidi miaka 36 na Mama Bite hazidi miaka 32.

“Salama kabisa, mmeakaje?” Nikaitikia salamamu ya baba bite.

Tukasalimiana na kuongea mawili matatu kisha nikawasha gari na kuondoka. Saa ilikuwa inaonyesha saa tatu kasoro robo. Nilikuna saa moja na dakika 15 kabla ya kikao changu na Dr. Shirima.

Nikaendesha gari huku nikiwaza kuhusu jirani yangu Baba Bite. Kuna jambo lilikuwa linanisumbua rohoni mwangu kuhusu yeye lakini sikujua ni kitu gani.

Labda ni kwasababu mara kadhaa nikiwa mjini nimewahi kupita kwenye duka Alilonielekeza kuwa ni lake, lakini karibia mara nne zote nilizofika ili nimsalimie nikajibiwa “ametoka”.

Labada ni kwasababu sijawahi kumsikia ana pilika pilika za kwenda kununua mzigo mpya, kitu ambacho kilinishangaza. Tanzania hii wafanyabiashara wetu hata akiwa anauza soksi lazima akutambie “kesho nasafiri naenda kuchukua mzigo”

Sikujua ni nini kiliisumbua roho yangu kuhusu Baba Bite.

Labda ni kwasababu siku moja majirani zetu, yule jamaa na demu wake baada ya kuanzisha ugomvi huko kwenye bata zao, ‘wazee’ wakawasweka lock up. Kwa vile hawakuwa na ndugu hapa Morogoro, tukapigiwa simu sisi wapangaji wenzao. Nakumbuka namna ambavyo nilimbembeleza OCD awaachie nikafikia hatua mpaka ya kutaka kutoa rushwa, kwa ajabu OCD akanibadilikia na kutaka kunitia mimi pia lockup kwa kutaka kumuhonga. Nakumbuka dakika chache baadae akaja Baba Bite, akaingia ofisini kwa OCD. Sikujua waliongea nini, lakini kama dakika kumi baadae walitoka wakiwa wanatabasamu na OCD akiongea naye kwa heshima kubwa. Nakumbuka jinsi OCD alivyoamuri askari wake wawaachie mara moja wapangaji wenzetu wala bata na tukarudi nao nyumbani.

Kuna jambo lilikuwa linanisumbua sana rohoni kuhusu Baba Bite, lakini sikuweza hata kuhisi ni jambo gani.

Dakika kumi baadae tayari nilifika ofisini, ghorofa la Hajram mtaa wa Boma Road. Ofisi yetu ilikuwa gorofa ya tatu.

Dr. Shirima na wenzake walikuwa wametimiza ahadi yao ya kunitafutia wafadhili. Na kwa miaka miatu sasa ofisi yetu inekuwa inapokea funds kiasi cha dola laki mbiki kila mwaka kutoka mfuko unaoitwa Alice Cartz Foundation ya nchini Australia kwa ajili ya kuendesha projects za kusaidia vijana wajasiriamali na kuendesha ofisi, yaani kulipa mishahara, pango na kadhalika. Mpaka sasa ofisi ilikuwa na wafanyakazi wa kudumu nane.

Nikafika mapokezi na kumsalimia Dada Hadija, mdada wetu wa reception kisha nikafungua mlango wa kuingia ofisini. Ofisi yetu tuliitengeneza katika mtindo ambao ukiingia tu unakutana na ukumbi ambao kuna cubic za wafanya kazi, au yafaa zaidi kusema meza za wafanya kazi. Tulikuwa tunapata funds za kutosha hivyo pia tulijitahidi kuitengeneza ofisi ivutie haswa.

Kila meza moja ilikuwa na wafanyakazi wawili waliokaa huku na huku. Na kila meza ilikuwa ni ‘department’. Ukiingia mbele yako mkono wa kushoto unakutana na meza yenye wadada wawili, hii ilikuwa ni department ya ‘Marketing and Branding’, mbele yake kuna meza yenye mkaka na mdada hii ilikuwa ni department ya ‘Monitoring and Evaluation’.

Upande wa kulia mwanzoni kuna meza yenye mdada na mkaka pia hawa ndani ya ofisi tuliwatunga jina ‘anchors’, kazi yao ilikuwa ni kusaka vijana wenye Idea za tofauti na kuwaunganisha na ofisi yetu. Mbele yake kulikuwa na meza yenye wakaka wawili, hii ilikuwa ni idara ya fedha na uhasibu.

Nikawasalimia wote, tukataniana mawili matatu kisha nikaingia ofisini kwangu. Ofisi yangu ilikuwa inajitegemea, ina mlango wa kioo ambao unaweza kuona hata ukiwa nje na upande wa dirisha, ukuta karibia wote ulikuwa ni dirisha la kioo.

Nikaketi katika kiti na kabla sijafanya chochote akaingia Hadija mdada wa reception. Kama ilivyo kawaida alikuwa ameniletea magazeti ya siku ya leo.

“nikuandalie chai?” Akaniuliza baada ya kuweka magazeti kwenye meza. “Yeah, ya rangi, and ya mkono mmoja tu” nikamjibu nikiamaanisha anipe chai tupu ya rangi.

Alipotoka nikaanza kupitia magazeti, na cha kwanza nilichokiona kwenye magazeti yote ilikuwa ni kuungwa mkono kwa hoja binafsi ya Mbunge Zephania Zuberi huko bungeni Dodoma. Karibia wiki mbili zilizopita Mbunge machachari, Mheshimiwa Zephania Zuberi aliwasilisha bungeni hoja binafsi aliyoiita “Uwezeshaji wa kimkakati kwa Makampuni ya Vijana Wazawa”.

Katika hoja hii Mheshiwa Zephania aliitaka serikali kupitia waziri mkuu, wakubaliane na hoja yake na kuweka mkakati wa makusudi kuhakikisha kuwa vijana waliothubutu kuanzisha kampuni ndogo za kibiashara wanapewa sehemu ya mikataba serikalini na katika sekta binafsi.

Hoja yake ilikuwa kwamba, kwa mfano tuseme kuna kampuni ya kichina imepewa tenda na serikali kujenga barabara, linapokuja suala la kununua kokoto kwa mfano, kampuni hiyo ipewe sharti kuwa lazima waingie mkataba na kampuni inayomilikiwa na vijana wazawa kwa ajili ya kusupply kokoto hizo.

Vivyo hivyo kwenye halmashauri za wilaya, Mheshimiwa Zephania akamtaka Waziri |Mkuu aiagize TAMISEMI kuamuru halmashauei zote nchini ziwe zinatoa walau 20% ya tenda kwa kampuni za vijana wazawa. Yaani kwa mfano halmashauri ikitaka kununua vifaa vya ofisi na kuna vijana wana miliki kampuni ya stationaries kwenye wilaya husika basi tenda hiyo wapewe vijana hao.

Hoja hii iliungwa mkono kila kona ya nchi na kila mtu. Asasi zisizo za kiserikali zikaandaa mijadala kuunga mkono hoja ya Mheshimiwa Zephania. Wanaharakati wakapaza sauti kuishinikiza serikali kukubaliana na hoja hiyo. Kwa mara nyingine tena mheshimiwa Zephania akawa shujaa katika nchi.

Nilipokuwa nasoma habari ya kukubaliwa kwa hoja hii na serikali, nilitabasamu. Nikacheka. Nikajisemea kimoyo moyo “kumekucha”.

Kimsingi The Board kupitia Dr. Shirima walikuwa hawanitamkii moja kwa moja mipango yao. Lakini uzuri ni kwamba mimi mwenyewe sikuwa mtu wa mchezo mchezo kichwani. Niliweza “kuconnect dots”.

Miezi mitatu iliyopita katika kikao chetu cha 12 mimi na Dr. Shirima alinipa maagizo kadhaa.

Katika kipindi hicho ndani ya SOTE HUB tulikuwa na mchakato wa kuchagua vijana ambao watapata ufadhili wa miradi yao kwa mwaka huu 2016.

Dr. Shirima alinipa maelezo kuwa kuna kuna “vijana” watatu wataomba kuwepo chini ya SOTE HUB natakiwa niwapitishe. Nakumbuka tulibishana sana kwani katika programu yetu tunachukua vijana watano pekee kila mwaka, hivyo akisema nichukue “watu wao” watatu hii inamaanisha tutabakia na nafasi mbili pekee kuweka vijana wenye uhitaji halisi.

Dr. Shirima akakomalia hoja yake kuwa tutafanya hivi kwa miaka miwili pekee kisha watatuacha tuendelee na mipango yetu vile tunavyotaka. Mwishoni sikuwa na namna zaidi ya kukubaliana kupitisha “vijana” hao wanaowataka.

Vijana hao walikuwa ni Maximilian Anga, huyu alikuwa ni “mchawi” wa kompyuta. Alikuwa ameanzisha kampuni yake ya teknohama aliyoiita Max tech.

Wa pili alikuwa ni George Ole Nangoi. Huyu alikuwa ni kijana wa kimasai aliyeanzisha kampuni ya ulinzi iliyohusisha ulinzi binafsi, na ulinzi wa mali. Kampuni yake ilijikita zaidi kutumia Morani wa kimasai badala ya walinzi wa kawaida wanao beba silaha za moto. Kamapuni yake iliitwa Moran Warriors Security.

Kampuni ya tatu ilikuwa ni ya kijana wa kike aliyeitwa Aisha Mzava, muhitimu wa chuo kikuu SUA shahada ya Agribusiness. Alikuwa amewachukua wahitimu wenzake wengine watatu na kuanzisha kampuni ha kutengeneza na kuuza madawa na mbegu za kilimo.

Hao ndio “vijana” watatu akionitaka niwapitishe miezi mitatu iliyopita tulipoonana na nikitekeleza hilo.

Leo hii nakutana na habari iliyopamba kurasa za mbele za kila gazeti kuhusu hoja ya Mheshimiwa Zephania “Uwezeshaji Wa Kimkakati Kwa Vijana Wazawa”. Nikahisi hapa kuna kitu The Board wamelenga, ubaya ni kwamba hawawezi kunieleza. Pia nikashangaa jinsi habari hii ilivyopewa kipaumbele kwenye media zote. Nikawa na hakika lazima Mzee Bernad Shayo amehusika kuipatia umaarufu hii habari.

Swali nililojiuliza, wanalenga nini? What’s their plan??

Wakati nikiwa bado napitia magazeti na kutafakari hili na like, Hadija akarudi na chupa ya chai na kikombe. Nikaangalia saa, ilikuwa saa nne kasoro dakika tano.

“Sh****ttt” nikajikuta nimeropoka. “Sory Hadija sitaweza kunywa chai nina appointment na mtu saa nne kamili na nishachelewa”. Nikaongea huku nanyanyuka haraka haraka na kutoka nje.

Dakika kumi baadae nilikuwa napaki gari ndani ya Nashera Hotel. Baada ya kushuka tu kuna gari ikaniwashia taa mara mbili. Nilipoiangalia nikagundua ni V8 ya Dr. Shirima.

Nikaifuata na kufungua mlango na kuingia ndani.

“Well, this is new! Leo kikao kwenye parking ya magari?” Nikaaanza kufungua maongezi kwa swali kabla hata ya salamu.

“Well, Ray mimi mtaalamu wa uchumi na uchumi is all about namna ya kumanage rasilimali na naomba nikwambie wengi wanadhani fedha ndio rasilimali kubwa zaidi lakini ukweli ni kwamba hakuna rasilimali adhimu kama muda!! Umechelewa dakika tano, nilikuwa nataka kuondoka.” Dr. Shirima akiongea kama kawaida yake huku anatabasamu.

“Ok ok ok, nice speech! Am here now.. Shikamoo!”

“Marhaba, umesoma magazeti ya leo” akaniuliza.

“Yeah nimemsoma shujaa wenu jinsi alivyoishawishi serikali, i guess ndio sababu tunaonana hapa leo”.

“Yeah na kwakuwa umechelewa naomba niende moja kwa moja kwenye agenda.”

“Ok..” Nikamjibu kwa kifupi huku namuangalia nikisubiri maagizo kwa shauku kubwa. Nilikuwa natamani walau nipate clue ya nini wanakilenga.

“Ok, nadhani unafahamu kuwa kampuni za vijana zilizo chini yenu hawawezi kuomba kandarasi wala kusaini mkataba pasipo SOTE HUB kuridhia, so ninachotaka mfanye ni kwamba muombe kandarasi hizi kwa zile kampuni tatu nilizo kueleza uzipitishe kikao chetu kilichopita.” Dr. Shirima akaongea huku anatoa makaratasi kwenye mkoba na kunikabidhi.

“Hizo ni tenda za serikali na kampuni binafsi hazijatoka bado lakini zinatangazwa wiki ijayo, hiyo ya kwanza ni tenda kutoka kampuni ya Swala Energy, naamini unaifahamu?” Akaniuliza.

“Yes, naifahamu” nikamjibu, naifahamu vizuri sana Swala Energy, kampuni inayofanya utafutaji wa mafuta katika bonde la ufa eneo la Kilosa.

“Ok, siku chache zijazo watatangaza tenda kwa ajili ya kuhitaji ulinzi katika maeneo yao huko kilosa nataka muombe tenda hiyo kwa niaba ya George Ole Naiko na kampuni yake ya Morani Worriors Security” Dr. Shirima akaongeza.

“Ok..” Nikamjibu kwa kifupi huku naipitia haraka haraka ile document ya tenda ya Swala Energy.

“Hiyo document nyingine ni tenda ya benki kuu pamoja na hazina, wanataka kampuni ya kuwasaidia kuboresha mifumo yao ya kompyuta.” Akaongea huku anatabasabu akijua wazi nitakuwa na swali.

“Benki kuu na hazina wana wataalamu wao wa IT sijawahi kusikia wanatoa kandarasi kwa kampuni binafsi” nikamuuliza kwa mshangao.

“Usijali kuhusu hilo Ray, tenda itatangazwa wiki ijayo na unatakiwa umuombee Maximillian Anga Yule kijana wa Max tech.”

“OK..” Nikamjibu tena kwa mkato.

“Hiyo tenda ya mwisho ni ya wizara ya kilimo, actually ni kama tangazo maana maombi yenyewe yanatumwa kwa mkuu wa mkoa, lakini wiki ijayo litatoka tangazo kwa kampuni za kilimo kuomba zabuni ya kusambaza mbolea na mbegu za kilimo, nataka umuombee Aisha na kampuni yake, na uombe mkoa wa Lindi.”

“Hahahah Dokta naheshimu sana weledi wako lakini lazima ukumbuke kuwa hizi kampuni bado ni changa hata kama serikali inataka kuanzaka kuzingatia hiyo sera mpya iliyopendekezwa na Mhe. Zephania lakini sidhani kama wanaweza kutoa zabuni kubwa hivyo kwa kampuni changa.” Nikamueleza huku nikicheka kicheko chepesi.

“Ray, jukumu lako ni kuomba hizo zabuni suala la kukubaliwa liache kwetu.” Akaongea akiwa serious. Baada ya sekunde kadhaa akaanza tena kutabasamu na aligundua nina swali. “Uliza Ray, najua una swali.”

“What’s your plan?? Najua hamuhitaji hivi vijihela vya chai, mna mpango gani?” Nikamuuliza basi tu kwa vile nilishindwa kukaa nalo rohoni lakini nilijua fika hawezi kunijibu.

“Ray, unajua siwezi kukujibu hilo swali or at leats nor here.” Dokta akajibu huku anatabasamu.

“Ok kama huwezi kunijibu hapa unaonaje sasa mkiniruhusu nije kwenye vikao vyenu ili nami nielewe kinachoendelea?” Nikamjibu huku naonyesha kukereka.

“Ray, huwezi kuja kwenye kikao kwasababu Chairman hajakualika” Dokta akanijibu kwa kifupi.

“Chairman, chairman, kila siku chairman hivi mara chairman vile! Who is this guy anyway? Ndiyo yule aliyeingia na msafara na walinzi kama Mkuu wa nchi siku ile?? Who is this guy??” Nikaongea kwa kukasirika na kukereka.

“Ray, inabidi niende sasa tafadhali shughulikia hayo niliyokueleza ASAP.” Dr. Shirima akaongea huku amerelax na kutabasamu huku anawasha gari.

Tukaagana nikashuka kwenye gari na kureje kwenye gari yangu. Nikasubiri kama dakika tano hivi baada ya dakika kama tano baada ya dokta kuondoka na mimi nikawasha gari na kuondoka.

Njiani nikawaza sana ni nini kilikuwa kinapangwa na The Board. Kwa hakika hawakuwa wanahitaji hizo zabuni kwa sababu ya pesa, kuna jambo kubwa walikuwa wamelipanga nyuma yake. Ni nini hasa lengo lao?? Nikawaza na kuumiza kichwa bila majibu. Nikaunganisha haya matukio bado sikupata jibu kabisa.

Katika kuwaza huku nikakumbuka tukio lililotokea mizezi sita iliyopita ambapo kwa wakati ule nililiona la kawaida lakini sasa lilianza kunitia mashaka kama lina mahusiano na kinachopangwa kufanywa na The Board.

Miezi sita iliyopita baba yake Hasnat, cheupe wangu, Mhandisi Jaffar Kumbea alichaguliwa kuwa mjumbe wa bodi ya TPDC, shirika la mafuta nchini.

Sikuona kama kuna uhusiano wowote na zabuni nilizoambiwa niombee vijana wetu wizara ya kilimo, benki kuu na hazina lakini sasa nilianza kuona uhusiano japo kwa mbali na maagizo niliyopewa na kumuombea George Ole Nangoi wa Morani Worriors Security, tenda ya Ulinzi katika kampuni ya utafutaji mafuta ya Swala Energy.

Nikarudi ofisini. Kazi zikaendelea. Wiki mbili zikapita, matangazo ya zabuni yakatoka. Tukawaombea vijana na kampuni zao, hapa niseme hata wenzangu walinishangaa kuomba zabuni hizo ila walishindwa tu kunizuia kwa kuwa nilikuwa bosi wao. Tukaomba, na kusubiri majibu.


Zilikuwa zimepita takribani wiki tatu toka nionane na Dr. Shirima. Kwa kiasi fulani maisha yalikuwa yamerejea katika hali ya kawaida.

Niliamua siku ya leo nitoke out na cheupe wangu na ili out yetu iwe ya kufana niliamua kuomba ushauri kutoka kwa majirani zangu pale nyumbani, yule jamaa na demu wake, wala bata ‘profesheno’.

Nakumbuka kauli ya jamaa alivyo nijibu “ishu za kumpeleka demu wako kwenye ‘nice dinner’ hizo tabia za kike na umbulura. kama unataka dinner si mpike tu wali nyama mle mlale, kama tunaenda out inabidi iwe ni kula bata la uhakika”.

Kwa kuwa yeye ndiye profesheno kwenye sekta hii nikafuata ushauri wake.

Kwa pamoja wote, mimi na cheupe na jamaa na demu wake tukaenda ‘kula bata’. Jamaa anaitwa Tony na demu wake anaitwa Grace.

Tulipokuwa tunatoka cheupe, alianza kuwa na wasiwasi kama hili lilikuwa na wazo zuri! Lakini kadiri usiku ulivyokuwa unayoyoma nilimuona anaanza kuinjoi. Tulianzai Down Town Club, tukavuruga vya kutosha kisha presheno Tony akashauri twende Nyumbani Park au kama watoto wa Moro wenyewe wanavyopaita, “samaki samaki”. Nako tukavuriga vya kutosha. Mishale ya saa saba kasoro ilibidi kuwalazimisha Tony na Grace kweli kweli mpaka wakakubali tuondoke kurudi nyumbani.

Kwa kawaida huwa sinywi pombe wala cheupe wangu naye hatumii, lakini usiku huu nilijikaza nikabugia Windhoek mbili, na shots kadhaa za whisky nisiyoijua ninachokumbka ni profesheno Tony alikuwa analeta kila baada ya dakika kadhaa. Cheupe naye alikunywa bia mbili ila pombe kali nikampiga marufuku asiguse. Nikakumbuka jinsi alivyo na “kichwa chepesi” asije akaanza kuharibu.

Tony na demu wake sijui walimaliza kreti ngani, sijui ndio nilikuwa nimelewa au maluwe luwe tu, maana nilimuhesabia Tony na demu wake karibia kreti mbili kasoro walimaliza.

Siku ikaenda vizuri kabisa.

Tukaanza safari ya kuondoka Samaki Samaki kurejea mazimbu. Japo kuwa nilikuwa na pombe kiasi kichwani lakini huwa simuamini mwingine yeyote aendeshe zaidi yangu katika mazingira ya namna hii, walau mimi nilikuwa na afadahali. Dakika kama kumi na tano tayari tulikuwa Tumefika Mazimbu FK mtaani kwetu. Kana kwamba Baba Bite alikuwa anatusubiri, alifungua geti hata kabla hatujapiga honi.

“Asante sana Mkuu.” Nilimshukuru Baba bite nikiwa naingiza gari ndani. Baba Bite hakuitikia. Sikujua kama ni pombe ama nilikuwa naona sahihi, nilipoangalia usoni kwa Baba Bite niliona hali Fulani hivi ambayo sijawahi kumuona nayo tangu nimfahamu. Alikuwa kama na hali ya wasi wasi, Iliyochanganyika na huzuni pamoja na hasira. Nilitamani nimuulize lakini kwa kuwa tunaheshimiana sikuona vyema kuongea naye nikiwa na pombe kichwani.

Nikapaki gari tukashuka wote, Tony na demu wake wakaingia ndani kwao na ndani ya dakika chache tu nikasikia wanaanza kutukanana.

Na mimi na cheupe wangu tukaingia ndani. Nikajitupa juu ya sofa na cheupe wangu akanirukia akakaa juu yangu. Na macho yenye ulevi kwa mbali akaniangakia moja kwa moja ndani ya macho kwa muda mrefu sana, “thank you kichwa” hatimae akaongea..

“For what?” Nikaongea nikijibalaguza kama sielewi. Moyoni tu nikitamani kusikia anayatamka maneno yale tena na tena.

“For today, for every day, for being my man! Nakupenda sana kichwa?” Akaongea huku anashusha kichwa chake taratibu mdomo wake ukikaribiana na wa kwangu.

“Nakupenda zaidi cheup…” Kabla sijamaliza midomo ilikuwa imekutana.

Kabla sijafaidi zaidi utamu wa lips na mate yake Mara akainuka “hey, ngoja nijimwagie maji kichwa chepesi kinoma usije ukaniua hahahah” akainuka kutoka juu yangu na kuanza kuondoka sebuleni. Nikamsindikiza kwa macho yenye ulevi kwa mbali huku natabasamu. “What?” Cheupe akasimama na kuniukiza.

“Leo utajuta kunifahamu” nikamwambia kwa utani huku nikijitahidi kuongea kimahaba.

“Hahahaha dooh” cheupe akacheka na kuingia bafuni.

Baada ya cheupe kutoka kwenda kuoga sijui ni kiherehere gani kikanikuta nikachukua simu na kuanza kuperuzi mitandaoni. Nikaingia instagram, hakuna kilichonivutia, nikaingia facebook, yale yale. Nikaingia mtandao wa jamii forums.. Baada ya kuingia tu nikaenda moja kwa moja kwenye ‘Recent Posts’. Juu kabisa kama kawaida nikaona mada za “kila siku”, sikumbuki vizuri lakini nahisi kulikuwa na mada “Natafuta Mume”, chini yake kulikuwa na nyingine “Mkewangu ana wivu sana nifanyaje?”. Nikaendelea kushuka chini. Kama post ya nne au ya tano hivi nikaona post ilifanya moyo wangu ulipuke. Iliandikwa “BREAKING NEWS: Waziri ameuwawa mda huu”.

Kwa haraka sana nikaifungua. Ndani ilikuwa imeandikwa mistari aliyepost alikuwa na nia ya kuwa wa kwanza kuleta habari hiyo; “Habari za uhakika nilizo nazo, Waziri wa Nishati amevamiwa na watu wasiojulikana na kupigwa Risasi mda huu hapa Ubungo mataa, source: Mimi mwenyewe”

Nikashusha chini nione ‘comments’ za watu na comment ya kwanza iliandikwa na mtu ambaye nilishindwa kulisoma jina lake lote, niliambulia herufi za kwanza tu, GENTA….. aliandika “mods ondoeni huu uzushi”!

Nikashuka chini kuangalia comments nyingine, zote zilikuwa na mtazamo huo huo.

Ikabidi nirudi juu nione jina la mleta habari, nikakuta anajiita MSAGA SUMU.

“Pumbavuuuuuuu” nikajikuta naongea mwenyewe na kuanza kucheka. Moyo wangu ukatulia, presha ikashuka. Maana nilishaanza kuwaza mengine kabisa kichwani.

Mara nikasikia mlango unagongwa. “Nani?” Niliuliza huku bado nimeketi kwenye Sofa.

“Baba Bite” alijibu aliyekuwa anagonga.

Nikaangalia saa kwenye simu, ilikuwa saa saba na dakika ishirini. Nikajiuliza jirani yangu anataka nini au ana shida gani usiku wote huu. Nikaenda kufungua.

“Vipi mkuu salama?” Nikamuiliza baada ya kufungua mlango.

“Salama tu, vipi umepafa taarifa?” Akanijibu huku akiwa anaonekana amepaniki kiasi.

“Taarifa gani?”

“Waziri wa Nishati amepigwa risasi ubungo mida hii” akanieleza huku ana hema juu juu.

Nikatabasamu na kumuuliza “umesoma jamii forum?”

“No hapana nimepigiwa simu na rafiki yangu yuko gazeti la Mwananchi, ni habari ya uhakika” Baba Bite akanijibu huku yuko serious kabisa.

Nilijihisi kama nataka kuanguka. Nikatoa simu yangu tena na kurejea kwenye ile habari Jamii forum nikakuta imeongezewa ‘link’ na maneno mbele yake “source: Millard Ayo.”

Nikajishika mlangoni, nilitaka kuanguka mwili wote uliishiwa nguvu. Sikuamini nilichokiona na kukisikia. Sikujua hata ni mda gani Baba Bite aliniaga na kurudi ndani kwake.

Kama mtu aliyenyeshewa mvua nikarudi na kuketi kwenye Sofa. Kichwani dots zilianza kuungana. Kama kweli Waziri wa Nishati ameuwawa nilianza kuhisi mkakati wa The Board ulihusu nini na ulikiwa unaelekea wapi. Niliogopa hata kukiwaza nilichoanza kukielewa.

Upande mwingine, nilijuta kwanini sikuwahi kumwambia cheupe kuhusu The Board na jinsi ninavyoshirikiana nao. Toka siku ya kwanza nilivyomueleza kuwa kuna watu wanataka kunitafutia wafadhili ila siwaamini, sikuwahi kuongea nae tena suala hili. Sasa nilijisikia kujuta kwanini sijawahi kumwambia, kwasababu kadiri dots zilivyokuwa zina connect kichwani mwangu nikang’amua kuwa hata baba yake aliyeteuliwa kuwa mjumbe wa bodi ya TPDC miezi michache ikiyopita alikuwa hatarini.

Sikumsikia hata cheupe alipotoka bafuni, nilikuja kugundua tu amesimama mbele yangu.

“Ray, are you ok?” hatimae nilimsikia anauliza, nahisi alianza kuongea mda tu lakini sikumsikia.

“Waziri Japhet kipanju amepigwa risasi mda huu ubungo.!” Nikamjibu bila kumuangalia.

“Ooh my god, una uhakika.”

“Asilimia mia” nikamjibu

“Aisee, inauma na naihurumia familia yake, but sielewi kwanini imekugusa kiasi hiki.” cheupe aliniuliza kwa mshangao.

Sikujua nimjibu nini au nianzie wapi. Sikujua nianze vipi kumuelezea kosa kubwa nililolifanya, sikujua nianze vipi kumuelezea nilichokuwa nahisi kimepangwa na The Board na ambacho nilikuwa na hakika moyoni kilikuwa ninaelekea kutokea.

“Am so sorry hasnat” ndicho pekee nilichoweza kukitamka. Hasnat alikuwa amesimama mbele yangu na alikuwa na mshangao mkubwa usoni na alikuwa ameanza kutetemeka kwa woga.

“Sorry for what?” Aliniuliza huku bado akiwa kwenye mshangao mkubwa.

Kabla sijamjibu simu yake ya mkononi ikaita. Hasnat alikiuwa na mazoea ya kuongea na simu ikiwa kwenye “loud speaker” hivyo alivyo ichukua simu mezani na kuanza kuongea nayo nikawa nasikia kila kitu.

“Shikamoo mama! Vipi kwema? Mbona usiku usiku.” Hasnat aliongea haraka haraka akiwa na woga mkubwa.

“Wamemchuka baba yako Hasnat!” Sauti ya upande wa iliongea ikiwa na mtetemo ikionekana dhahiri alikuwa analia.

“Nani aliyemchukua mama, na kwasababu gani?” Hasnat aliuliza sauti ikitetemeka kuashiria alikuwa anajikaza asilie kwa sauti.

“Polisi wamemchukua baba yako kama nusu saa iliyopita, wanasema anahusika na tukio la kupigwa risasi Waziri Mpanju usiku huu” mama yake hasnat aliongea na kushindwa kuzuia kilio chake.

Hasnat akishindwa kuendelea kuongea na simu, alipigwa na butwaa akabaki ameganda amenikodolea macho kana kwamba ni mara yake ya kwanza kuniona. Kuna kitu alikuwa anataka kusema lakini anashindwa ila ni machozi tu yakaendelea kutoka. Nikabaki nimesimama tu mbele yake sijui nifanye nini au niseme nini! Sikumbuki mara yangu ya mwisho kulia ilikuwa lini, lakini hii inaweza kuwa mara ya kwanza kwa miaka mingi. Nikajikuta machozi yananitoka bila kuelewa.

“Ray, whats going on here?” Hasnat aliongea huku anatetemeka kwa woga na hasira.

Nikajikuta nainua uso na kuangalia juu na kufumba macho kwa uchungu. Kisha nikafumbua macho na kumuangalia Hasnat moja kwa moja.

“Hasnat ma love, nataka nikwambie kitu but you are not going to like it.”

Kwa karibia dakika tano Hasnat alinitazama kwa mshangao akiwa amepigwa na bumbuwazi.

“What’s going on Ray?” Hatimaye akaniuliza tena akiwa amenikazia macho.

Niliwaza haraka haraka nianze vipi kumueleza nilichokuwa nimepanga kumuambia. “Hey, calm down ma love! Please kaa chini nikueleze kwa utaratibu.” Nikamueleza bila kujiamini na nikaanza kuona jinsi alivyokuwa anapandwa na hasira huku machozi yanamtoka.

“Ray, naomba unieleze kinachoendelea!” Cheupe akaongea bila kukaa chini kama nilivyomuomba na alikuwa amefura kwa hasira.

“Ok! Hasnat, nina sababu za kuamini kuwa watu walionitafutia wafadhili kwa ajili ya Sote Hub ndio wanaohusika na mauaji ya Waziri Kipanju na nina amini wanahusika na kukamatwa mzee wako!” Nikamueleza kwa hofu kubwa huku nikijaribu kuchunguza reaction yake usoni. Hasira nilizokuwa naziona zikabadilika na kuwa ‘confusion’. Akafumba macho kwa sekunde chache akijaribu kuelewa nilichokuwa najaribu kumueleza.

“What the fu*k are you talking about? Ninavyofahamu ni Dr. Shirima mwalimu wako ndio amekusaidia kupata wafadhili.” Akaniuliza bado akiwa na mshangao mkubwa usoni.

“It’s much bigger than that?” Nikamjibu na kufumba macho kwa kujisikia aibu kwa nilichotaka kumuekeza. “Dr. Shirima ni sehemu ya watu wanaojiita The Board, sifahamu hasa wana malengo gani, lakini wao ndio wamenisaidia kupata wafadhili!” Nikajikuta nimeinamia chini nikiwa namueleza mambo hayo. Nilijisikia aibu kumueleza mambo haya leo.

“And..?” Hasnat akauliza kwa kifupi tu na nilihisi hasira iliyokuwa kwenye sauti yake.

“Well, wamekuwa wananipa maelekezo tu mambo ya kufanya, vijana gani niwaingie kwenye projects Sote Hub, project gani waanze nazo na mambo kama hayo” nikamueleze nikiwa najitahidi nirelax lakini ndani nikiwa na hofu kubwa kwani nilianza kuona hasira inarejea usoni kwa Hasnat.

“And hukuona umuhimu wa kunieleza yote haya miaka miatatu yote hii.” Hasnat akauliza sauti ikiwa na hasira kweli kweli.

“Am so sory! Sikuona umuhimu wowote wa kukueleza mambo ambayo hata mimi mwenyewe siyaelewi vizuri. Na sikuwahi kuhisi yana ubaya wowote ule mpaka leo hii. Natamani nirudishe siku nyuma nifanye kitu sahihi. Am so sorry”

“Ray, I don’t give a fuk wewe na hao wenzako wa Freemason, sijui The Board mnafanya nini! I don’t give a fuk of what you do! Please muacheni mzee wangu, please please sitaki mzee wangu apotee please Ray! Kwanini umenifanyia hivi Ray.” Hasnat akaongea kwa hasira ambayo sikuwahi kumuona nayo tangu nimemfahamu. Alikuwa anaongea huku amenifuata mpaka niliposimama na kuanza kunipiga vingumi. Uzuri vilikuwa vingumi vya kike, yes nilikuwa nimemkosea sana lakini pia vingumi hivi vilikuwa vya kudeka. Katika wakati mgumu kama huu nilijua ni kiasi gani alikuwa ananihitaji. Ni kiasi gani natakiwa kuwa imara kwa ajili yake.

Nikamvuta karibu yangu, akijitahidi kujitoa katika mikono yangu lakini nikamshinda nguvu! Nikamvuta kwa nguvu na kumkumbatia, akajitahidi kukukuruka atoke mikononi lakini nilizidi kumkumbatia kwa nguvu mpaka akatulia na kitu pekee alichoweza kukifanya ni kulala kifuani kwangu na kuanza kulia. Sidhani kama nimewahi kujisikia uchungu kiasi kile katika maisha yangu, nikajikuta nataka kutamka maneno lakini nikashindwa na kitu pekee nilichomudu kukifanya ni kumkumbatia zaidi.

“Am sorry honey! Am so sorry.” Ndio maneno pekee nilifanikiwa kuyatamka na nikajikuta nayatamka tena na tena.

Nikamchukua Cheupe, nikaenda nae mpaka kwenye Sofa pembeni na nikampakata kama katoto kadogo. Mda wote huu alikuwa analia tu bila kusema chochote na mimi sikutaka kumzui kulia, nilijua kiwango cha uchungu ambacho atakuwa alikuwa nacho moyoni, nikaache atoe uchungu huo kwa machozi. Takribani dakika ishirini alilia na hatimae akanyamaza. Zilipita karibuni dakika kumi nzima baada ya kunyamaza lakini hakuna aliyesema chochote. Alilala tu kifuani, na mimi nilikuwa nimemkumbatia tu.

Kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu niliogopa kuanzisha maongezi na Cheupe wangu. Na yafaa zaidi kusema nilitamani tusiongee chochote kile. Tubakie hivi hivi milele. Alale kifuani kwangu, nimkumbatie namna hii milele. Tusiseme chochote, mioyo yetu tu isemeshane katika ulimwengu tusiouona. Niliogopa neno lolote, au sentesi yoyote nitakayo tamka inaweza kuanza kumliza tena Cheupe, na hakuna maumivu makubwa kama kushuhudia mpenzi wako wa maisha analia kwa uchungu na sababu ni wewe umemkosea.

Mara Hasnat akainua kichwa na kunitazama “so, you are one of them? The Board?” Akaniuliza huku akizungusha macho alipoitaja ‘The Board.’

“No I’m not! Sio mwenzao mimi.” Nikamjibu nikionyesha kukereka kwa kufikiria tu kwamba na mimi ni mwanachama wa The Board.

“Ray, unawezaje kukataa sio mwenzao wakati unashirikiana nao mwaka wa Tatu huu sasa?”

“Its complicated” nikamjibu kwa kifupi tu.

“So Mzee wangu anahusikaje kwenye……” Nikamkatisha kabla hajamaliza kuongea nikihisi muda si mrefu atapaniki tena.

“Ssshhh.! Please naomba tusiongee haya mambo sasa hivi. Please hasnat naomba pumzika. Tutaongea kila kitu asubuhi. Najua unaweza kuwa huniamini sasa lakini najua huwezi kutilia shaka kuwa nakupenda kuliko kitu chochote kile. So please naomba ulale, kutakucha asubuhi na nakuahidi kila kitu kitakuwa sawa! I promise you.” Nikaongea kwa hisia za hali ya juu. Hasnat hakusema chochote kile, akaniangalia machoni kwa karibia dakika nzima kisha akashusha kichwa na kukilaza tena kifuani. Nikamkumbatia. Nikambusu paji la uso. Dakika chache baadae wote tukapitiwa na usingizi.


Japokuwa tulichelewa sana kulala, lakini saa kumi na moja na nusu nilikuwa nimeamka.

Tulikuwa tumelala pale pale kwenye sofa mimi na cheupe na alikuwa amelala juu yangu kifuani kama tukivyolala Jana usiku. Kwa hiyo nikajitahidi kuamka taratibu nisimshitue cheupe na nikamuacha aendelee kulala.

Nikaingia bafuni na kuoga haraka haraka kisha nikaingia chumbani na kuanza kupanga vitu kwenye begi dogo la mgongoni. Wakati nikiendelea kuweka vitu kwenye begi nikahisi mtu amesimama nyuma yangu mlangoni.

“Unataka kunitoroka?” Hasnat akaniuliza macho yakiwa bado yamelegea kutokana na usingizi kwasababu ya kulala mda mfupi.

“No najiandaa inabidi twende Dar, so ni vizuri uanze kujiaandaa pia” nikamueleza na hakunijibu nikamuona amegeuka tu na kuelekea bafuni.

Takribani dakika kumi tu baadae tulikuwa tunafunga mlango wa nyumba yetu na tunaekekea kwenye gari. Ajabu ni kwamba ilikuwa ni saa kumi na mbili kasoro kama dakika kumi hivi lakini tulimkuta baba bite yuko nje kibarazani kwao anabrush viatu. Nikajiuliza sana kama nimewahi kumuona mwenye duka yeyote duniani anabrush viatu asubuhi kama mwalimu au polisi anataka kuwahi ofisini. Nikahisi alikaa tu pale nje atuone tunavyotoka. Nikaona wacha nimfanyie mind game.

“Za asubuhi Mkuu!” Nikamsalimia kwa bashasha. Nikamuona kama ameshtuka hivi kwa kuniona niko kawaida. Nika note kitu kichwani.

“Salama kabisa Ray, shemeji za asubuhi?” Akanijibu na kumsalimia Hasnat.

“Nzuri shemeji, shikamoo” Hasnat akamjibu. Uzuri wa cheupe wangu huwa anajua kusoma akili yangu. Ingawa sikumwambia chochote ila usalimiaji wangu ule wa bashasha akahisi ‘kuna jambo’. Hivyo na yeye akijitahidi kuwa kawaida na kusalimia kwa uchangamfu.

“Daaahh mkuu habari ya Waziri imekuwa kubwa kweli kweli, vipi hujasikia tetesi zozote kuhusu muhusika wa tukio?” Nikamuuliza.

“Hapana Mkuu sijajua bado” alijibu kwa kugugumizi kwa mbali na nikamuona amemuangalia Cheupe kwa kama nusu sekunde hivi. Nikanote kitu ningine kichwani.

“Daaahh yatapita bhana, and… Aaah sorry naelekea dar sahizi naweza kupitia gazeti la Mwananchi kuna tangazo la ofisi naweza kupeleka pale watuchapie kwenye gazeti lao, so ukinisaidia namba ya yule jamaa yako anayefanya kazi pale utakuwa umenisaidia sana, si unajua watanzania bhana tunaishi kwa kujuana hahahhah” nikamtega na kucheka kinafiki.

“Aaah daaahh Mkuu simu imezima chaji kabisa, itabidi nikutumie labda baadae” baba bite akajibu na nikimuona kabisa ameanza kuwa uncomfortable.

“Ooohh haina shaka Mkuu nipe tu hata jina lake.” Nikamtega tena.

“Aaaahh anaitwa… aahh John! Yeah anitwa John.! John Joseph.” Baba bite akanijibu akiwa totally uncomfortable.

“Nashukuru sana Mkuu” nikamjibu huku nabonyeza bonyeza simu nikijifanya kusevu nilichoambiwa.

Tukapanda kwenye gari na kuondoka. Tulipotoka tu nje ya geti Cheupe akaniangalia huku ana tabasamu.

“What the fu*k was that?”

“Hahahaha usijali, nikielewa nitakwambia maana hata mwenyewe bado sijaelewa mpaka sasa” nikamjibu na kucheka.

“Damn jamaa hajui hata kusema uongo” Cheupe akajibu huku akipokea simu.

Nikafarijika kuwa na cheupe ameona kuwa Baba Bite alikuwa anadanganya. Nikaanza kufikiria tena maongezi yangu na Baba Bite.

Nimemsalimia kwa bashasha lakini akashtuka. Kwahiyo alitegemea habari ya kifo cha waziri inishtue! Kwanini?

Nimemuuliza kama anajua kuhusu muhusika wa mauaji, akanijibu kwa wasiwasi huku anamkata jicho Cheupe! Yawezekana alifahamu kuhusu kukamatwa kwa Babake Hasnat, swali amefahamu vipi wakati habari hiyo bado haijawekwa wazi kwa vyombo vya habari.?

Pia nimemuomba namba na majina ya rafiki yake wa gazeti la Mwananchi na amenidanganya! Kwanini jana anidanganye kuwa taarifa ameipata kutoka kwa rafiki yake wa Mwananchi? Kwanini anifiche source yake? Anafahamu vipi mambo haya?

Nikamuweka kiporo.

“Tunaweza kuongea sasa kuhusu kinachoendelea?” Cheupe aliniuliza na kunizindua kutoka katika kumuwaza Baba bite.

“Yeah! Nikueleze tu juu juu maana na mwenyewe sifahamu kwa undani sana” nikaanza kumuelezea cheupe kila kitu. Kuhusu siku ya kwanza wakivyokuja nyumbani mwembe chai. Kuhusu nilivyotolewa damu. Kuhusu kikao chao mikocheni B. Na kuhusu karatasi za mkakati namba 0034.

“Oohh my god! So huo mkakati unahusu nini hasa?” Hasnat aliniuliza kwa mshangao baada ya kumueleza yote haya.

“Actually sifahamu sana! Nilipewa karatasi kama kumi hivi lakini sehemu kubwa zilikuwa kama zimefutwa hivi. Si unaonaga vile kwenye televisheni zile karatasi za top secret zinavyokuwa zimefutwa futwa na wino mweusi na kuacha mistari michache? Yes, zilikuwa namna hiyo. Kitu pekee ambacho nilikiona ni mkakati wa kuwezesha vijana, pia kuna karatasi ilihusu Sote Hub, kuna karatasi ilihusu sera mpya ya kuwezesha vijana, nahisi ndio hii iliyowasilishwa bungeni na Mhe. Zephania. Na karatasi ya mwisho ilikuwa na figures tu zinainyesha kiwango cha gesi na mafuta vilivyogunduliwa mpaka sasa na vitalu vyote vilivyopo pamoja na makampuni yanayomiliki vitalu hivyo.!”

“Aiseeeee! So unadhani hii inahusiana vipi na kuuwawa waziri kipanju na mzee wangu kuchaguliwa bodi ya TPDC na kukamatwa kwake”.

“Siku ile Dr. Shirima alivyonieleza niwaombee vijana tenders, nilijiuliza sana why wametarget idara hizo za serikali na kampuni ya swala Energy. So nikaanza kufatilia kampuni ya Swala Energy, hawa jamaa wamepewa licence na serikali kufanya utafutaji wa mafuta kwenye bonde la ufa eneo la kilosa na kilombero toka mwaka 2008! Katika kufukunyua kwangu nikakuta kuwa thamani za hisa zao zimeporomoka sana kwenye masoko ya hisa miaka hii miwili. Pia mwaka huu walitakiwa wafanye drill ya kisima kipya kwenye eneo lao huko kilosa lakini ikahairishwa. Sasa licence yao ya kufatuta mafuta walipewa na serikali mwaka 2008 na inaisha mwakani 2017. Kwa mwenendo huu lazima serikali itakataa kuwapa licence mpya ya miaka minane mingine. Kwahiyo ninachokihisi ni kwamba The Board wanajaribu kushinikiza TPDC kubariki taarifa za uongo kuhusu maendeleo ya utafutaji mafuta huko kilosa na kilombero ili Swala Energy wasipoteze wawekezaji na serikali wasijue hali mbaya waliyo nayo ili iwape tena licence mwakani. Kwa hiyo ninachohisi mzee wako aliwekwa TPDC ili kusaidia kushawishi kukubalika kwa taarifa hizo za kupika! Ninachojiuliza je alikubali kutumiwa na The Board? Pia nahisi Waziri Kipanju aligundua hii ishu au akupewa taarifa nyeti kuhusu hili suala na alikuwa anazipeleka sehemu au alikuwa anataka kuzifanyia kazi mara moja ndio maana wakamzimisha fasta fasta! Maana wangeweza kutumia njia nyingine kumuondoa, lakini assasination ya dizaini hii inaonyesha suala la kumuondoa lilikuwa urgent kuzuia asifanye alichokusudia kukifanya kwa haraka. Pia bado sijaelewa kusudi la kunambia niwaimbee tends Morani Warriors kulinda Swala Energy.”

Nilimueleza Cheupe kwa kina kile ninachokihisi. Aliganda kwa dakika kadhaa akitafakari kile nilichomueleza.

“Ooohh my gorsh! This is insane” Cheupe akaongea huku anafumba macho kwa uchungu.

“Be strong cheupe” nikamtia moyo.

Niliendesha kwa fujo kiasi kwamba ndani ya masaa mawili tu tulikuwa tumefika ubungo. Moja kwa moja tukaelekea ubungo plaza. Nilikuwa nimempigia simu school mate wangu Issack niliyesoma naye sekondari. Huyu alikuwa mtundu mtundu wa kompyuta. Hakuwa mchawi kiasi kile cha wale wa kwenye televisheni lakini alikuwa na utundu wa kutosha tu na uzuri chuoni alichukua shahada ya masuala ya kompyuta.

Tulipofika tu baada ya salamu nikamueleza nilichomuitia.

“Issack hii simu kuna mtu alinipa, naomba ufanye utundu wako nipate taarifa ya chochote utakachofanikiwa kukipata kuhusu simu hii” nilimkabidhi Issack simu niliyopewa na Dr. Shirima miaka mitatu iliyopita.

“Pia hii ni namba ya akaunti ya shirika linaitwa Alice Cartz Foundation, lipo Australia naomba pia taarifa zao zote ambazo utafanikiwa kuzipata hasa hasa donors wao na bodi ya wakurugenzi”

Nikamkabidhi kikaratasi kilichoandikwa namba ya akaunti ya wafadhili wangu wa SOTE HUB shirika la Alice Cartz Foundation pamoja na anuani yao ya ofisi.

Baada ya maongezi hayo kwa haraka tukaondoka kuelekea kituo cha polisi Oysterbay ambapo tuliambiwa baba yake Hasnat alipelekwa baada ya kukamatwa. Nje tulimkuta mama Hasnat na ndugu wengine na wakatueleza kuwa askari waliowakuta hapo wamekataa kuwajibu chochote mpaka pale mkuu wa kituo akifika.

Hatukuwa na jinsi tukasubiri mpaka majira ya saa nne mkuu wa kituo akawasili. Akatuomba radhi kwa kuchelewa kwani alikuwa na majukumu mengine. Baada ya kumueleza shida yetu kuwa tumefika kumuona ndugu yetu Mhandisi Jaffar Kumbea, akatujibu kwa mkato tu kuwa hayupo hapo kituoni kwao alishakuja kuchukuliwa na afahamu amepelekwa wapi.

Tulipomuuliza ni nani aliyemchukua? Akatujibu tu “watu wa serikali” wamemchukua. Wengine hawakuelewa ila binafsi nilimuelewa. Nilielewa “watu wa serikali” ni akina nani.

Tulitoka nje na kuanza kujadili nini tufanye. Wengine wakashauri tufanye press conference kushinikiza serikali iseme walipompeleka Mhandisi Jaffar Kumbea, wengine wakashauri tuende Wizara ya Mambo ya ndani tukaombe maelezo zaidi. Kama ilivyo ada kukiwa na tatizo alafu kikaitishwa kikao cha ndugu, kila mtu anakuwa mjuaji zaidi, hivyo Mjadala ulikuwa mkali haswa. Mpaka saa nane mchana bado tulikuwa kwenye mgahawa karibu na kituo cha Oysterbay ‘tunajadili’.

Mara simu yangu ikaita, alikuwa ni Issack! “Give me some good newz!” Nilimjibu Issack baada ya kupokea simu na kusogea pembeni.

“Oohh yeah nina habari njema haswaaa! Hii simu bado nahaingaika nayo ila ile akaunti nimepata vitu verrrryyy interesting.” Aliongea Issack kwa sifa kama kawaida yake.

“Really?” Nikamuuliza

“Yeah, nadhani vizuri uje hii sio ya kuongea kwenye simu!”.

Nikakata simu. Nikamuita Cheupe pembeni, nikamueleza nilichoambiwa na Issack. Kisha nikamuaga na kuwasha gari Kuelekea Upanga kuonana na Isaack.

Issack alikuwa anaishi Upanga mtaa wa Mindu kwa wazazi wake. Tumefahamiana kwa miaka mingi sana tangu tunasoma sekondari Kibaha Boys. Tangu kipindi hicho alikuwa ni mtundu mtundu sana wa kompyuta. Nakumbuka siku za weekend tulikuwa tunatoka shuleni maeneo ya Tumbi mpaka Maili Moja kwenye hoteli ya Njuweni kulikuwa na Internet Café.

Wenyewe wamiliki wa Internet Café walikuwa na utaratibu unalipia hela ambayo ilikuwa shilingi mia tano kwa nusu saa kisha unakaa kwenye kompyuta iliyowekewa program ya ‘time watcher’ ambapo inasetiwa kujizima mara tu nusu saa ikifika.

Nakumbuka tulikuwa tunalipia nusu saa na tukisha wekewa muda na muhudumu kuondoka Issack anabonyeza bonyeza button za keypad na baada ya mda pale juu alama ya ‘time watcher’ inaondoka na tunatumia hata masaa mawili kisha anabonyeza bonyeza tena ile time watcher inarudi tena na kompyuta kujizima.! Uzuri kulikuwa na kompyuta nyingi hivyo hatukuwahi kushitukiwa na muhudumu.

Nilikuwa nimeshafika Nyumbani kwao na tulikuwa tumeketi kwenye meza ya chakula namsikiliza maelezo yake.

“Ujue muda ule ulikuwa upo na mtoto mzuri nikashindwa kukuliza nini tatizo mpaka unataka kuwachunguza wafadhili wako.” Issack akauliza huku usoni akiwa na tabasamu la ‘kikomedi’ kama desturi yake.

“Its a long story Issack, ila kwa ufupi labda niseme siwaani! Nahisi kuna vitu wananificha, so tell me umeona nini?” Nikamueleza kwa mkato tu nikijihami kuepuka kumpa taarifa ambazo hazimuhusu.

“OK! Unajua kwenye system za bank kuhack na kufanya transfers ndio ishu ngumu, so nilitamani niwaibie ila itachukua muda kidogo hahahah.” Issack akaanza utani.

“Come on, kuwa serious basi! Umeona nini?” Nikamuuliza nikiwa serious nikitaka aache utani tuongee mambo ya maana.

“Ndio nilikuwa nakuja huko, as i said kuhack na kufanya transfers ndio ishu ngumu so nilichokifanya ni kuhack na kuchukua statemnt yao kuonyesha transactions zilizofanyika, nikaangalia transactios walizozifanya kutuma hela sijaona chochote cha kushtua then nikaanza kuangalia transactios za kupokea fedha kutoka kwa donors hapo ndipo nikakuta maluwe luwe” akaongea huku ananipa karatasi.

Nikapokea karatasi na kuitazama tu nikiwa bado sijaelewa point yake. Karatasi ilikuwa na orodha ndefu sana ikionyesha miamala.

Issack nandhani akaona bado sijaelewa au sikuona alichotaka nikione kwenye karatasi hiyo.

“Cheki hapa!” Akanionyesha sehemu kwenye karatasi. Moyo ukanipasuka! Katika kati ya miamala kulikuwa na muamala wa kutumiwa fedha kutoka kwa NDESHEMA SAFARIS (UK). Moyo ukalipuka.

“Cheki na hizi” akanikabidhi karatasi nyingine kama tano hivi.. Zote zilikuwa ni bank statements zikionyesha miamala. Kwenye kila karatasi kulikuwa na miamala kadhaa kutoka kwa NDESHEMA SAFARIS (UK).

Kuna kipindi inatokea mtu unaona jambo mbele yako lakini ubongo wako unakataa kuamini! Ndio nilikuwa katika hali hiyo. Mikononi mwangu niliona jambo dhahiri kabisa lakini nilishindwa kuamini.

Ndeshema Safaris ikikuwa ni kampuni inayomilikiwa na Eric Kaburu. Licha ya kampuni yake kuwa kubwa ilijizolea umaarufu zaidi miaka miwili iliyopita baada ya yeye mwenyews Eric Kaburu kukabiliwa na kesi ya mauaji ya mpenzi wake. Mwishoni mwa kesi alikutwa na hatia ya kuua bila kukusudia na akahukumiwa miaka saba gerezani.

Kampuni yake ilikuwa na makao makuu nchini Tanzania, na ilijihusisha na kutoa huduma za masuala ya utalii lakini pia ilikuwa na matawi ya uwakala nchini marekani na nchini uingereza! Na tawi hili la Uingereza ndilo linaloonekana hapa kuwa moja ya donors wa Alice Cartz Foundation.

Nikapepesa tena macho kwenye zile karatasi. Kulikuwa na majina ya watu binafsi, makampuni ambayo yakikuwa yanachangia fedha kwenda Alice Cartz Foundation, lakini katika orodha yote hii Ndeshema Safaris ndio walionekana kuwa wachangiaji wakuu na wakitoa kiwango kikubwa zaidi cha fedha.

Nikajiuliza kichwani kama hii ilikuwa ni coincidence au ina maana gani. Sikuwahi kusikia au kuona kampuni ya kitanzania ikisaidia shirika la nje kwa kiwango kikubwa namna hii alafu shirika hilo hilo lije tena Tanzania kusaidia jamii. Nikahisi kuna jambo hapa.

“Hivi unakumbuka kaburu yuko gereza gani?” Nikamuuliza Issack ambaye muda wote huu alikuwa amenikodolea macho ananishangaa nilivyokaa kimya najaribu kuelew kinachoendelea

“Well, baada ya kukuta hayo mauza uza kwenye statement nikaanza kutafuta taarifa za Eric Kaburu, yuko gereza kuu Morogoro” Akanijubu Issack na kuongeza “Ray, unaweza kunieleza kinachoendelea hapa? Maana sielewi elewi hivi nahisi” akauliza akiwa ameacha kabisa utani kama kawaida yake na akikuwa serious kabisa usoni.

“Issack i promise nitakueleza kinachoendelea but its a long story naomba tuongee siku nyingine kwasasa naomba niende nikalifanyie kazi hili.”

Nikamshukuru na kumuaga haraka haraka na kuondoka.

Tayari ilikuwa imeshafika saa kumi na mbili jioni. Nikampigia simu Cheupe kumuuliza wamefikia wapi na majadiliano na familia, na akanieleza kuwa walienda wizara ya mambo ya ndani na wakaelezwa kuwa hawawezi kupewa taarifa zozote kwa sasa kuhusu Mhandisi Jaffar kumbue lakini waliombwa kuwa watulivu na warudi baada ya siku tatu.

Baada ya yeye kunipa mrejesho huo na mimi nikamueleza kuhusu kikao changu na Issack na kitu ambacho amefanikiwa kukipata.

Pia nikamuekeza kuwa sitaonana nae kwani naelekea Morogoro usiku huu na nia yangu ni kwenda kuonana na Eric Kaburu gerezani. Nikamueleza kuwa nilikuwa na imani na hakika kabisa kuwa lazima kunaconnection kati ya Kaburu na The Board maana haiwezi kuwa conicedence kwa kampuni yake kusaidia shirika nchini Australia alafu shirika hili lije linisaidie mimi na taasisi yangu na ukizingatia kuwa wafadhili hao nimetafutiwa na The Board.

Tukaagana, nikakanyaga mafuta kuelekea Morogoro.

Niliingia Morogoro saa nne kasoro usiku na nilipofika nyumbani Mazimbu na kupaki gari ndani nikashangaa mabadiliko niliyoyaona. Kwanza nilifunguliwa geti na mla bata Tony tofauti na kawaida ambapo mara nyingi ni Baba Bite huwa ananifungulia geti. Pia ndani kuliwa kumepooza mno.

“Vipi kiongozi wazima hapa?” Nikamsalimia Tony baada ya kushuka kwenye gari.

“Salama kabisa! Rafiki yako Baba Bite amehama leo ghafla tu hahahah” akaongea Tony huku anacheka.

“Whaaat? Baba bite si nimemuacha hapa leo asubuhi na hakunambia chochote kuhusu kuhama?” Nikauliza kwa mshangao mkubwa.

“Hata mwenye nyumba ameshangaa maana ghafla tu na kodi yake bado miezi minne hahahahah! Watu na mipango yao bhana huwezi jua” Tony akajibu huku anaingia ndani kwake.

Nikashangaa kweki kweli! Inawezekana vipi mtu ahame haraka haraka namna hii? Huyu baba bite ana nini anakificha? Nikazidi kuongeza mashaka juu yake.

Nikafungua mlango wa ndani kwangu na kuingia kulala tayari kwa kwenda kumuona Kaburu kesho gerezani.


Tayari nilikuwa nimefika gereza kuu la Morogoro. Gereza hili liko karibu kabisa na katikati ya mji njia ya kuelekea Kilakala. Nilikuwa sijaingia bado ndani, nilikuwa nje nawashawishi maaskari niingie na walikuwa ‘wananikazia’ kwa kuwa haikuwa weekend.

Nilitumia karibia nusu saa kuwashawishi maaskari magereza wamuite Kaburu na Kuniruhusu kuongea naye lakini wakanikatalia.

Baadae akaja askari mwingine ambaye alionekana kuwa na cheo kuliko wale niliokuwa naongea nao na akatuuliza nini tatizo.

“Mkuu nimekuja kumuona ndugu yangu hapa, natokea mbali sana, naishi dar na leo hii baadae natakiwa nisafiri kwenda nyumbani kigoma na nina maongezi muhimu sana na ndugu yangu! Nashangaa hawataki kuniruhusu kitu kidogo kama hichi wanataka nije weekend!” Nikaongea uongo huku najiamini kweli kweli.

Yule askari mwenye cheo cheo akawageukia kama anawashangaa hivi, “yani ishu ndogo hivyo ndio mnabishana mda wote huu, eboo! Hebu saidianeni bhana, mruhusuni kuonana na ndugu yake na wewe dogo hebu tuachie ya vocha.” akaongea kwa makeke na kujiamni.

Nikazama mfukoni, nikachukua wallet na kutoa noti tano za elfu kumi na kumkabidhi yule askari mwenye cheo.

Akazikunja noti tatu na kuziweka mfukoni kisha akawapa noti moja moja wale maaskari mwingine.

Baada ya hapo, nikaruhusiwa kuingia ndani na kuongozwa mpaka kwenye kichumba cha wageni kuongea na wafungwa. Kilikuwa ni kichumba kidogo ambacho kilitenganishwa pande mbili katikati likitengenezwa kama dirisha kubwa la nyavu kutenganisha chumba hicho pande mbili ambapo mnakuwa ndani ya chumba kimoja na mnaweza kuonana lakini hamuwezi kugusana.

Nikasubiri kama dakika kumi hivi ndipo upande wa pili wa chumba akaingia mtu mzima wa makamo kwa makadirio ya kama miaka 54 hadi 56! Alikuwa na mwili wenye afya nzuri tu na kichwani alikuwa na mvi kwa mbali.

Alikuwa amevalia mavazi ya rangi ya chungwa, sare ya kifungwa!

Hatimaye Eric Kaburu alikuwa mbele yangu.

Nikamsubiri akae na awe comfortable kisha nikafungua maongezi.

“Shikamoo mkuu” nikaamkia kwa heshima.

“Sidhani kama nakufahamu!” Kaburu akajibu bila kuitikia salami yangu akiwa amenikazia macho.

“Yeah! Aaahh jina langu naitwa Ally l! Aaahh Ally Hassan Nina shida kidogo nataka kuzungumza nawe.” Nikaongea tena kwa heshima.

Kaburu hakujibu chochote kile. Akiniangalia tu. Nikaelewa kuwa alikuwa anasubiria niongee shida yangu.

“Kampuni yako tawi la London linafadhiki Shirika ambalo linatoa msaada katika kampuni yangu na hivi karibuni nadhani ime…..”

“Sikiliza kijana, ukitaka msaada kwa mtu kwanza unatakiwa umuheshimu! Na dalili ya kwanza ya kumuheshimu mtu ni kuwa mwaminifu! Umeanza maongezi yako kwa kusema uongo, jina lako sio Ally Hassan! Nafahamu unaitwa Rweyemamu Charles Kajuna!! Na kabla hujaniuliza chochote naomba nikupe majibu kabisa… Sina explanation ya swali lako lolote na sitaki kukuona tena ukija hapa kuniona, kwa usalama wangu na wako.”

Kaburu aliongea akiwa amenikazia macho na alikuwa serious kweli kweli. Hakusubiri niseme chochote, akainuka na kuondoka.

Nilipigwa na bumbuwazi na kubaki nimeganda kama nimemwagiwa maji. Mwili wote uliganda kama barafu.

Sikujua nilikaa namna ile kwa muda gani, nilikuja kuzinduliwa na askari magereza akiniita nitoke.

“Oya vipi umelala au niaje? Ndugu yako ametoka muda tu nashangaa wewe bado uko ndani.”

Nikazinduka kutoka kwenye bumbuwazi na kutoka nje. Sikukumbuka kuaga wala kuwashukuru wale askari walioniruhusu kuingia. Nikatoka na kuingia kwenye gari moja kwa moja na kurudi nyumbani Mazimbu. Nilipofika nyumbani nikamkuta Tony nje, sikumbuki kama alinisakimia au vipi lakini nakumbuka kuwa sikuitikia kama alinisalimia.

Nikafunga mlango. Nikazima simu.

Sikutaka kuongea na yeyote, au yafaa kusema sikuweza hata kuongea chochote. Mshangao na mshtuko niloupata nilishindwa hata kuwaza kichwani. Eric Kaburu ananifahamu!! Inawezekana vipi??

Nikajihisi kama niko kwenye dimbwi lenye tope na kila ninapojaribu kukuruka kujiokoa ndivyo ninavyozidi kuzama. Kila hatua na kila ninachokifanya kinazidi kuniiingiza kwenye sintofahamu kubwa zaidi.

Nikafumba macho. Sikuweza kuwaza. Usingizi ukanipitia.

Nilikuja kushtuka mida ya jioni. Kuna mtu alikuwa ana gonga mlango nadhani alikuwa Tony. Sikuweza kumuitikia. Kitu pekee kilichokuwa kinajirudia tena na tena kichwani mwangu ilikuwa ni kauli ya Eric Kaburu gerezani. “Nakufahamu unaitwa Rweyemamu Charles Kajuna.” “Naomba usirudi tena hapa kuonana nami kwa usalama wako na wangu”

“What the fu*k is going on??” Niliwaza. Nikatamani kulia lakini machozi hayakutoka.

Nikabaki na bumbuwazi tu. Nikafumba macho. Usingizi ukanipitia.


Nilipokuja kuamka ilikuwa ni saa kumi na mbili asubuhi. Njaa ilikuwa inaniuma kweli kweli. Nilikuwa sijala toka jana asubuhi.

Huwa sipendi kupika. Hata chai tu sipendi kupika. Nikawaza labda niwashe gari mpaka mjini maeneo ya Kaumba nikanunue chips maana maeneo hayo haijalishi ni saa ngapi watu wako macho na chips kibao zinapikwa.

Nikiwa katika kuwaza kuhusu kula nikakumbuka kuwa simu nimeizima toka jana mchana na nilikuwa nimeshasahau kama simu iko off.

Nikaichukua haraka haraka na kuiwasha. Baada ya kuiwasha tu meseji kama thelathini hivi zikaingia, nyingi zilikuwa za Cheupe. Jicho likaona moja ya meseji hizo.

“Baby am worried! Are you ok?”

“Sh*t” nikabofya simu kumpigia haraka. Nikagundua kiasi gani atakuwa na wasiwasi kwa kunikosa hewani siku nzima.

“Hey love” nikamsalimia baada ya kupokea simu.

“What the hell? Siku nzima sikupati, are you ok?”

“Niko poa kabisa, nitakupa mrejesho tukionana! Vipi huko nini kinaendelea?”

“Jitahidi ufike haraka kabla ya saa nne, tumeitwa wizara ya mambo ya ndani” akaongea cheupe haraka haraka.

“Duh! Am on my way”

Nikakata simu na kujiandaa haraka haraka. Nikawasha gari na kuanza safari ya kurejea tena dar.

Nilipofika maeneo ya Nane Nane kwenye kituo cha mafuta cha Camel Oil nikaingia ili kujaza mafuta. Wakati najaza mafuta nikaona gari ya kijivu aina ya Land Cruiser ikapaki pembeni yangu nayo ikawa inajaza mafuta.

Baada ya kumaliza nikaendekea na safari na masaa mawili na nusu baadae nikwa nimefika ubungo. Niliposimama kusubiri taa ziruhusu nilipotizama katika kioo cha dereva nikaliona tena lile gari land cruiser niliyoiona Nane Nane Morogoro.

Nikahisi gari hiyo inanifuatilia. Kwahiyo taa ziliporuhusu nikanyoosha moja kwa moja Morogoro Road kuelekea mjini.

Nilipofika maeneo ya Magomeni Kagera nikaangalia tena nyuma, ile Land Cruiser ilikuwepo.

Nikakata kushoto bara bara ndogo inayoenda kutokea Magomeni Popobawa. Nikaongeza mwendo na kuangalia nyuma ile Land Cruiser bado ipo.

Nilipotokea Popobawa, nikakata kulia kufuata barabara inayotoka sinza kwenda kukutana na barabara ya Ali Hassan Mwinyi. Nikatazama nyuma, ile land cruiser ipo na sasa zilikuwa mbili. Ile ya kijivu na nyingine nyeusi.

Nikaongeza mwendo lakini ile Land Cruiser ya kijivu ikanizidi kasi na kuja kuniziba mbele yangu ikipunguza mwendo taratibu na kunilazimu na mimi kupunguza mwendo. Mwisho ikasimama na kuniziba njia mbele na mimi nikasimana.

Haya yote yanafanyika “mchana kweupe” au tuseme asubuhi kweupe maana ilikuwa ni majira ya saa nne asubuhi.

Baad ya magari yote kusimama, wakashuka watu wawili kutoka ile Land Cuiser ya kijivu, mmoja amevaa suti nyeusi na mwingine amevalia suruali na shati amechomekea.

Wakaja mpaka kwenye gari yangu na kunionyesha ishara nishuke. Nikajiuliza sana nifanyeje. Kama ilivyo desturi yetu waswahili tayari watu walianza kushangaa na kujikusanya. Moyoni nikapata ujasiri. Nikafungua mlango nikashuka.

Yule mmoja aliyevaa suti akanisogelea karibu na kunionyesha kitambulisho.

“Afisa Usalama wa Taifa, naomba ufuatane nasi” akaongea haraka, na hakusubiri jibu langu akanishika mkono kwenye kiwiko na kunipeleka kwenye ile land cruiser ya kijivu, tukapanda ndani akafunga milango.

Yule Afisa mwingine akaingia kwenye gari yangu. Kisha nagari yote matatu yakageuza kwa kasi kuifuata Barbara inayoelekea sinza.

Nikajisemea kimoyo moyo, “nimekwisha!!”

Ndani ya gari niliwekwa katika siti ya nyuma na yule jamaa aliyenipandisha kwenye gari akakaa siti ya mbele kwenye usukani na kuendesha gari.

Kule nyuma nilikowekwa siti ya pembeni yangu alikuwepo mdada wa makamo anayeelekea kwenye umama ambaye kwa makadirio hawezi kuvuka miaka 34. amevalia suti ya kike ya rangi ya bluu. Alikuwa mwembamba, mrefu na sura yake ilikuwa nyembamba kama ya Kinyarwanda, au tuseme ya Kitusi kwa ufasaha zaidi.

Hakunisemesha chochote na mimi sikusema chochote. Nilibaki naduwaa tu kuangalia kile kilichokuwa kinaendelea.

Magari yote yakaendeshwa kwa kufuatana kuelekea barabara inayoelekea sinza. Tukiwa tunakaribia maeneo ya sinza, simu ya mkononi ya yule dada aliyekaa pembeni yangu ikaita.

“Hello.!” Yule dada akapokea simu na nikagundua lafudhi ya kifaransa katika utamshi wake.

“Oui… ok… ok… d’accord.!” Yule dada akawa anamuitikia tu anayeongea naye kwenye simu huku anachanganya maneno ya kingereza na kifaransa kisha akakata simu.

“..il que nous allions directement à la maison..” Yule dada akaongea kifaransa haraka haraka akimwambia dereva.

“..est-il là?” Dereva akamuuliza

“..oui.!” dada akamjibu

Baada ya kuwasikia maongezi yao ndipo hapa nikaafikiana na hisia zangu kwamba yule dada ni Mnyarwanda. Aliikicharaza kifaransa kwa ufasaha kabisa. Uzuri nakifahamu kifaransa kwa kiasi. Yule dada alipokata simu alikuwa amemueleza dereva kuwa huyo mtu aliyekuwa anaongea naye ataka tuelekee moja kwa moha “nyumbani”. Na dereva alikuwa amemuuliza kama huyo mtu amefika tayari hapo nyumbani (huyo aliyekuwa anaongea naye) na yule dada akamjibu kuwa amefika.

Nikabaki na maswali kichwani. Yule jamaa wa mbele anayeendesha gari anakifahanu vizuri tu kiswahili na anaonekana ni mtanzania na kipindi wananichukua alijitambulisha kwangu kama Afisa wa Usalama wa Taifa na niliamini moyoni mwangu kweli walikuwa ni Usalama wa Taifa kutokana na haiba zao.

Jambo nililokuwa sielewi ni huyu dada mnyarwanda anausikaje na hawa Usalama wa Taifa maana anaonekana ni kama “mwenzao”.

Nikiwa katika kuwaza huko tayari tukawa tumetokea Mwenge na tulipofika kwenye makutano ya barabara wakaendesha magari yote matatu kuifuata Old Bagamoyo Road. Moyo ukanipasuka. Nikaanza kuwaza moyoni “napelekwa mabwepande”. Jasho likaanza kunivuja kwa mbali. Nikaanza kukumbuka kuhusu sakata la yule daktari kupelekwa Mabwepande kufanyiwa “usafi wa kinywa” na “usafi wa kucha”. Nikahisi hicho ndicho kilikuwa mbele yangu. Joto la mwili likapanda kweli kweli jasho likanitoka haswa.

Tulipo fika maeneo ya Lugalo nikageuka kumtazama yule dada. Kumbe muda wote huu ananiangalia tu jinsi ninavyopaniki. Nilivyomuangalia tu na macho yetu kukutana akatabasamu. Nilikereka kweli kweli, nilitamani nimtemee mate. Alionekana kuinjoi jinsi nilivyo paniki.

“..où m’emme-vous?” (mnanipeleka wapi) nikamuuliza kwa kifaransa changu cha kuunga unga.

Yule dada akatabasamu tena na kunijibu kwa mkato tu, “..domicile!” (Nyumbani).

Nikajiinamia. Nikahisi naanza kuchanganyikiwa. Nyumbani??, nikajiuliza. Nyumbani wapi wanaponipeleka? Nyumbani kwetu Mwembe Chai, nyumbani kwetu Morogoro, huku nyumbani wapi wanaponipeleka? Au wanamaanisha “nyumbani kwangu kwa milele”. Daammn it! Nikijisikia hasira na kuchanganyikiwa kila mara neno “Mabwepande” lilipokatiza kichwani mwangu.

Tulipoofika maeneo ya Mbezi Beach Jogoo magari yote yakakata kulia kutoka barabara kuu kufuata njia ya vumbi.

Nikajikuta nimeshikwa na mshangao wa ajabu. Presha ikashuka, lakini mshangao nilioupata ulikaribia kunipandisha tena presha. Ni kama vile mtu ameingiza mkono mfukoni ukitarajia atoe kisu na kukudhuru badala yake anatoa pipi.

Nikageuka na kumuangalia yule dada pembeni yangu kwa butwaa. Akatabasamu tu. Nahisi alikuwa anajua kinachoendelea akilini mwangu.

Mshangao niliokuwa nao ilibakia kidogo tu nimuulize “hatuendi Mabwepande?”.

Presha na hasira zikashuka kiasi. Walau nilijua siendi kufanyiwa “usafi wa kinywa na kucha”. Walau moyo ulipoa, lakini bado nilikuwa najiuliza wananipeleka wapi.

Gari zote zikaendeshwa mpaka mbele kidogo kuna barabara nyingine ndogo inaingia kulia kwenda kanisa la Agape, tukaicha hiyo tukanyoosha mpaka mbele kidogo. Mitaa hii ilikuwa na utulivu sana, labda kwa vile wanaishi watu wa kipato cha juu. Maana mda wote huu sikunbuki kama tulimpita mtu yeyote barabarani. Tulikuwa tunapita tu majumba ya kifahari yenye mageti makubwa.

Mbele kidogo tukakuta barabara nyingine inaingia kushoto. Tukaifuata hiyo barabara mpaka tulipotokea mbele ya nyumba moja kubwa. Nayo ilikuwa ya kifahari kama nyumba nyinginezo pale mtaani. Ilikuwa kubwa na uzio mkubwa wa ukuta. Geti likafunguka. Nadhani lilitunia rimoti au sijui teknolojia gani ya siku hizi maana sikuona mtu kufungua.

Tukaingia ndani na wakapaki magari. Mda wote huu nilikuwa sijamuona Afisa au maafisa waliokuwa kwenye ile Land Cruiser nyeusi. Waliponichukua pale magomeni popobawa ni maafisa waliokuwa kwenye land cruiser ya kijivu iliyonizibia njia mbele ndio walishuka kwenye gari na mmoja aliyevaa suti kunichukua mpaka kwenye gari yao na yule alivaa suruali na shati akaendesha gari yangu. Ile land cruiser nyeusi hakushuka Afisa yeyeto ulitufuata tu kwa nyuma.

Tulipopaki hapa ndani ya hii nyumba ndio nikaona Afisa aliyekuwemo kwenye ile land cruiser nyeusi. Alishuka kijana mdogo tu wa makamo yangu. Kwa muonekano tu alikuwa hazidi miaka 29. Kwa kumkadiria haraka haraka nilihisi atakuwa na miaka 28 au 29.

Alikuwa amevalia suruali na jinzi ya bluu iliyopauka kidogo na na raba nyeupe. Juu alikuwa amevaa sweta yenye mistari mistari.

Nikamuangalia kisha nikajisemea kimoyo moyo “hawa ndio mafala wanaotugongea mademu zetu vyuoni, wanajifanya ‘wajasiriamali’ kumbe wazee wa kitengo”.

Uzuri niliyasema hayo kimoyo moyo, nikamkata tu kijicho cha hasira kisha nikaangalia mlangoni tulikokuwa tunaelekea.

Yule dada akafungua mlango tukaingia ndani. Nilipokanyaga tu ndani kitu cha kwanza nilichokiona na kunishtua nusura nizimie haikuwa sebule kubwa ya kifahari, haikuwa seti za sofa zilizopangiliwa vizuri pale sebuleni, na wala haikuwa meza kubwa ya kioo katikati ya sebule.

Kitu cha kwanza nilichokiona na kunishitua mpaka karibu roho iruke, alikuwa ni Baba Bite. Alikuwa amevalia suti nyeusi na amekaa kwenye sofa la watu wawili na laptop mapajani.

Mshtuko nilioupata ilinibidi nisimame pale nilipokuwa ili nisiweze kudondoka. Maana mapigo ya moyo yalienda mbio kiasi kwamba ningepiga hatua moja tu ningeweza kudondoka. Nikabaki nimesimama tu namkodolea macho.

“Karibu sana Ray!” Baba bite akanisalimia kwa tabasamu na kusimama.

Kwa kipindi chote ambacho niliishi nae kule Morogoro Mazimbu siku zote Baba Bite alikuwa ni mtu mwenye furaha, lakini leo hii nilimuona na muonekano tofauti kabisa ambao sikuwahi kumuona nao kabla. Baba Bite niliyemuona leo alikuwa relaxed, alikuwa comfortable na alikuwa ana jiamini haswaa.

Nikatembea na kwenda kukaa kwenye sofa mojawapo ya watu wanne. Yule jamaa tuliyekuja naye aliyevakia suti nyeusi ambaye ndiye alikuwa anaendesha gari niliyokuwemo mimi akaja kukaa pembeni yangu. Baadae nilikuja kujua jina lake anaitwa Fredy.

Yule Afisa kijana wa makamo yangu ambaye baadae alikuja kutambulishwa anaitwa Hassani pamoja na yule Afisa aliyeendesha gari yangu ambaye baadae nikamfahamu anaitwa Mbena wakakaa kwenye sofa ya watu watatu.

Yule dada wa kitusi ambaye nilivyokuja kutambulishwa baadae jina lake sikuweza kulishika kichwani kutokana na lilivyokuwa gumu akaenda kukaa pale alipokaa Baba Bite lakini hakukaa kwenye sofa kabisa bali alikaa juu kwenye sehemu ya kuwekea mikono.

Zilipita karibia dakika tatu toka wote tuketi hakuna mtu aliyeongea chochote, nilikuwa nimekodoa macho tu kwa Baba Bite.

“Habari yako Ray” Baba Bite akavunja ukimya uliokuwa umetawala.

“Wewe Baba Bite ni Usalama wa Taifa??” Nikamuuliza kwa mshangao.

“Well, hilo ni swali au? Nadhani umeshaligundua hilo toka jana uliponishtukiza na maswali yako ya mtego” Baba Bite akanijibu huku anatabasamu. Nilichukia jinsi alivyokuwa relaxed ukinzingatia mimi nilikuwa katika paniki na mshangao mkubwa.

“Is that right? Ndio maana sikuwahi kukutata ‘dukani kwako’ hata siku moja. Ndio maana ulikuwa na taarifa ya kifo cha waziri kabla taarifa kufika kwenye media. Na ndio maana kwa miezi minane tuliyoishi pamoja ulijenga ukaribu na mimi. Kwa fikra za haraka haraka naamini muda wote huo ulikuwa unanichunguza! Swali language ni why? Kwanini Afisa wa Usalama wa Taifa upoteze miezi yote hiyo kunichunguza?” Nikamuuliza swali nikiwa katika hali ya utulivu. Taharuki na mshangao wangu vilikuwa vimeshaisha na sasa nilijisikia hali ya utulivu ndani ya nafsi.

“Well, hiyo naamimi ndio sababu kwanini wote tuko hapa! Why? Kwanini tukuchunguze? Ray, jibu lake ni jepesi tu.. Tunahitaji kujua uhusika wako kwenye kitu kinachoitwa The Board!!” Akaongea huku uso umebadilika ukiwa seruous kweli kweli hasa alipouliza swali la uhusika wangi kwenye The Board.

“Sifahamu chochote kuhusu The Board” nikamjibu kwa kujiamini. Sikutaka kutoa taarifa nisizokuwa na uhakika nazo kirahisi rahisi namna hiyo.

“Ray, nakuuliza kwa ustaarabu na kibinadamu kwa kuwa ni kijana ninayekufahamu! Nisingependa kutumia nguvu kupata hizo taarifa kutoka kwako” Baba Bite akaongea usoni akionyesha dhahiri ameanza kupatwa na hasira.

Mara simu ya mkoni ya yule dada wa kitusi ikaita. Wote tukanyamaza na nikaona wote wamegeuka kumuangalia yeye. Akapokea na kuweka sikioni.

“Hello!” Akaongea kwa lafudhi yake ya kinyarwanda.

“oui.. oui!” akamuitikia aliyekuwa anaongea naye kisha akakata simu na kuwatazama wenzake.

“le ministre est arrivé” (Waziri amewasili) akawaambia wenzake na kunyanyuka na kutoka nje.

Nikajiuliza kichwani, Waziri?? Waziri anakuja kwenye hiki kikao? Nikaacha nione kitakacho fuata!

Pia niligundua kuwa yule Dada anakielewa kiswahili ila hawezi kukizungumza kwani muda wote tunaongea alikuwa anafuatilia kwa makini na hakuna aliyekuwa anamtafasiria.

Dakika moja baadae akarejea akiwa ameongozana na Mhe. Charles Wangwe, Waziri wa Mambo ya Ndani.

Kama kawaida yake Mhe. Wangwe alikuwa amevalia suti nyeusi na shingoni amejifunga ‘scarf’ yenye rangi za bendera ya Taifa.

Alipoingia tu wote tukajikuta tumesimama mpaka mimi mwenyewe nikijikuta tu nimesimama. Mheshimiwa Wangwe ni moja kati ya viongozi wa nchi ninaowashimu sana na kuwahusudu, pia ni moja kati ya watu ninao waangalia kama mfano wa kuwaiga. Yes, nilikuwa natofautiana na baadhi ya misimamo yake hasa hasa kujipambanua kwake kwa itikadi za kichama, lakini alikuwa ananikosha kweli kweli kutokana na uzalendo wake na utendaji wake ambao binafsi nauona umetukuka.

Akatusalimia wote kisha akanifuata nilipokaa na kunipa mkono, “habari yako kijana” akanishika mkono.

“Nzuri tu, shikamoo Muheshimiwa” nikasalimia kwa bashasha nikifurahi kwa sekunde kadhaa nikisahau kuwa niko kwenye matatizo makubwa.

“Sijui nimechelewa? Mmefikia wapi” akauliza akiwa anakaa mahali ambapo Hassani yule Afisa kijana aliinuka na kumpisha.

“Hapana hujachelewa Muheshimiwa ndio tulikuwa tunaanza na Ray hapa anatueleza kuwa hafahamu chochote kuhusu The Board” akaongea Baba Bite huku anatabasamu.

Waziri Wangwe akatabasamu na kutoa kicheko fulani hivi kifupi kama ‘anacheka kwa dharau’ hivi lakini kwa sauti ndogo.

“Dogo mambo vipi” akaniangalia na kuniliza.

“Safi muheshiwa shikamoo” nikajikuta nimemuakia tena, damn it!

“Nadhani umesikia kuhusu kifo cha waziri wa nishati? Si ndio? Na tunafahamu kuwa kwa mara kadhaa umekuwa unakutana na mtu ambaye tuna hakika ni wakala wa The Board na jana tu ulienda gerezani kuonana Eric Kaburu gerezani! Sasa kabla hatuja kuunganisha kama moja ya watuhumiwa ni vizuri ukatupa maelezo ya kuridhisha” akaongea Waziri Wangwe kwa msisitizo na kwa mamlaka.

Nikajifikiria moyoni niwaeleze au niendelee kukataa? Nikahisi kuwa yaweza kuwa kosa kubwa kuongea hata kile kidogo ninachokifahamu kuhusu The Board. Lakini kwa upande mwingine nikakumbuka jinsi ambavyo mimi mwenyewe kwa siku mbili zilizopita jinsi nilovyoanza kuwa na mashaka makubwa kuhusu The Board. Na pia nikajipa moyo, kwanini niwafiche taarifa watu wa serikali na kuwalinda watu ambao Nina mashaka nao? Bora nimwage mchele tu.!

“OK! Nitaeleza kile ninachokifahamu” nikamwambia Waziri Wangwe.

Nikaanza kuwaeleza stori yote kuanzia ile miaka mitatu iliyopita. Jinsi nilivyopokea simu kwenye bahasha Morogoro ofisini. Jinsi walivyokuja nyumbani Mwembe Chai, jinsi nilivyopelekwa PPF House, jinsi walivyo nitoa damu na kuchukua alama za vidole. Nikawaeleza pia jinsi walivyonipeleka kwenye kikao chao Mikocheni B… Nilipowaeleza kuhusu kikao cha Mikocheni B niakona wameshtuka kidogo.

“Unataka kusema kuwa ulihudhuria kikao chao, unakumbuka wahudhuriaji walikuwa akina nani?” Baba Bite akaniuliza kwa shauku kubwa..

“Hapana sifahamu wahudhuriaji walikuwa akina nani, niliwekwa tu kwenye chumba fulani nikimsubiri Dr. Shirima.” Nikamjibu huku nikificha kumwambia ukweli kuwa niliwang’amua wahudhuriaji wawili wa kikao usiku ule, Mbunge Zephania Zuberi na Mzee Bernard Shayo. Nikajisemea moyoni kuwa sio busara kuweka karata zangu zote mezani kwa wakati mmoja.

“Ok! Unakumbula hiyo nyumba ilikuwa wapi?” Akauliza Baba Bite huku kila mmoja wao akichukua peni na karatasi kuanza kuandika.

Nikawaelekeza mahali nyumba ilipo kule Mikocheni B. Baada ya kuwapa maelekezo hayo wakapeana ishara fulani hivi na nikawaona yule dada wa kitusi na yule Afisa aliyeiywa Mbena wakinyanyuka na kuondoka. Nikaamini wanafuatilia hiyo nyumba niliyowaelekeza.

“Enhe endelea” Baba Bite akanikumbusha kuwamalizia maelezo yangu.

Nikawaeleza kuhusu vikao vyangu na Dr. Shirima na nilipofikia kuwaeleza kuhusu vikao vyangu viwili vya mwisho, kile ambacho Dr. Shirima alinipa maelekezo kuhusu vijana wa kuwachagua kwenye programu ya Sote Hub kwa mwaka huu na pia kikao cha wiki mbili zilizopita ambapo alinipa maelezo ya kuwaombea tenda vijana hao, nilipowapa maelezo haya umakini wao uliongezeka nikagundua kuwa walikuwa hawajui suala hili. Hivyo wakaniuliza majina ya vijana hao nilioambiwa niwapitishe, majina ya kampuni zao na tender nilizowaombea. Nikawatajia na wakaandika kwenye makabrasha yao.

Baada ya hapo nikawaeleza kuhusu nilivyogundua namna ambavyo Ndeshema Safaris wanatoa msaada kwa Alice Cartz Foundation na hatimaye nikawaeleza kuhusu kumtembelea Eric Kaburi gerezani Morogoro na kitu alicho nijibu. Nikamaliza.

“Aiseeee!” Waziri Wangwe akashusha pumzi, “asante sana kijana kwa taarifa hii” akaongea huku anaendelea kuandika kwenye notebook yake.

“Umetuongezea vitu kadhaa ambavyo tulikuwa hatuvifahamu kuhusu The Board lakini pia la muhimu nadhani maelezo yako yanathibitisha ripoti ambazo alikuwa anatupa Justin (baba bite) kwamba wewe sio mwanachama wa The Board bali itakuwa wanakutumia tu” akaongeza Waziri Wangwe.

“Sijakuelewa Mheshiwa” nikamuuliza kwa uso wa alama ya kuuliza.

“Well, takribani mwaka mmoja umepita toka tugundue juu ya vikao vyako na Dr. Shirima ambaye tunamfahamu muda mrefu kuwa wakala wa The Board. Ndipo miezi minane iliyopita Justin akahamia mahali unapoishi kwa ajili ya kuchimba taarifa zako na baada kama ya miezi minne kwenye ripoti zake akatueleza kuwa wewe sio mwanachama wa The Board bali labda utakuwa unatumika tu so ni vizuri tusikuchukulie kama adui bali tukugeuze kuwa asset!” Akaongea Waziri Wangwe akimalizia kuandika kwenye notebook na kuniangalia usoni.

“Asset? Una maana gani kuwa niwe asset?” Nikauliza ingawa moyoni nilishakijua anachokimaanisha.

“Tunataka utusaidie kuichinguza The Board na tunaihitaji kufanya hivyo haraka sana!” Akaongea tena Waziri Wangwe.

“Kabla sijakubali au kukata hilo, sidhani kama The Board wataniamini tena, kwanza nimedukua akaunti ambayo nina amini wanahusika nayo, nimeenda kumuona Kaburu gerezani na niko hapa naongea na nyinyi watu wa serikali! Sidhani kama wataniamini tena” nikaongea kwa msisitizo kabisa nikiwakatisha tamaa kuhusu hoja waliyoiibua.

“Kuhusu sisi kukutana na wewe hawafahamu na hawawezi kufahamu tumejitahidi kuwa makini! Kuhusu kudukua taarifa za akaunti na kwenda kumuona Kaburu hawawezi kukutema kwenye mipango yao kwasababu hiyo! Naamini Dr. Shirima atakuita na kukukemea uache kufukunyua na mipango yenu itaendelea! Hawawezi kukutema kiraisi hivyo, naamini kutokana na kukuficha mambo yao wanexpect kijana mwenye utashi kama wewe ufukunyue mambo kuwafahamu” akaongea Waziri Wangwe akiwa na uhakika kabisa na kujiamini.

“Ok! Ok, kabla sijaanza kufikiria kuhusu hilo suala la kuwachunguza mnaweza kunieleza walau kidogo hawa The Board ni watu gani hasa maana nahisi mnawafahamu zaidi kuliko mimi”

“Ray sidhani kama kuna umuhimu wa kukupa taarifa ya namna hiyo”

“Mheshimiwa Waziri, kwa heshima zote kabisa naomba kukuambia kwamba nimewapa taarifa zote mnazohitaji na bado mnanitaka nianze kuwachunguza hao watu! Sasa nasema hivi, siwezi kuanza kuchunguza watu ambao siwafahamu na wala sifahamu ubaya wao! Kwa miaka mitatu hao The Board wanamtuma dokta kunipa maelekezo Fanya hiki fanya kile, lakini wameniweka gizani kuhusu shugjuli zao na unaweza kuona jinsi zilivyoniingiza kwenye majanga! Sasa na nyinyi mnataka kunituma kazi zenu na mnakuja na mtindo ule ule wa kutaka kuniweka gizani! sasa nasemaje, eidha niachieni niende nyumbani, au niswekeni rumande kama mtuhumiwa kama mlivyonitishia awali lakini nawahakikishia siwezi kufanya hicho mnachokitaka pasipo kunipa maelezo ya kutosha!!” Nikafoka kwa hasira nikimuangalia Waziri Wangwe.

Tukabakia tunaangaliana machoni kwa karibia nusu dakika.

“Justin naomba files za The Board” Waziri akamuagiza Baba Bite na Baba bite akainuka na kuingia chumba kimoja wapo mle ndani na dakika mbili baadae alirudi na mafailu kama saba hivi mkononi akayaweka mezani mbele ya Waziri Wangwe.

Waziri Wangwe akachukua faili moja na kulirusha mezani mbele yangu, nikalichukua na kuanza kufungua ndani kulisoma huku namsikiliza akinipa maelezo.

“The Board, hatufahamu mengi sana kuwahusu so nitakueleza machache tunayoyafahamu mpaka sasa” akaanza kunipa maelezo Waziri Wangwe

“Mtu ambaye tunahakika kwa asilimia mia kuwa ni mwanachama wao ni Dr. Shirima, mwalimu wa Uchumi Chuo Kikuu cha Mzumbe! IHuyu anatumiwa kama mtu wa mikakati na kuwa wakala wa kuwaunganisha The Board na vibaraka wao katika sekta mbali mbali. Na kuna watu watatu wengine ambao tume wafahamu hivi karibuni kuwa ni wanachama, wa kwanza ni Bernard Shayo naamini unamfahamu vizuri ni mmiliki vyombo vya habari Vingi hapa nchini… Vituo vya televisheni, vituo vya redio, magazeti na kampuno ya kusindika maji na soda. Mtu wa pili ni mfanyabiashara maarufu sana ambaye naamini unamfahamu na alikuwa mbunge kabla ya kujiuzuru miaka michache iliyopita, Bw. Khalid Mohammed na watatu ni Askofu Eliyah Kamei wa Uzima Ministries moja ya makanisa makubwa zaidi ya kilokole hapa nchini. Kwa hiyo hawa ndio watu wannepekee ambao tuna hakika kuwa ni wanachama wa The Board lakini kwa taarifa zetu za intelijensia tunaamini kuwa The Board ina wanachama wasiopungua ishirini na tano! Lakini taarifa zao ni za siri mno ila tunapambana usiku na mchana tuweze kuwatambua wanachama wao wengine na hasa hasa tunatamani kumjua kiongozi wao ambaye hatumjui jina bado ila wenyewe wanapenda kumuita Chairman “

Sikushangaa kuyasikia majina ya Dr. Shirima na Mzee Bernard Shayo kwani hawa nilikuwa nafahamu kuwa ni wanachama wa The Board lakini nilishtuka kusikia jina la Khalid Mohammed na nilipigwa na butwaa zaidi kusikia jina Askofu Eliyah Kamei wa Uzima Ministries.

Na pia nikawaza moyoni kuwa kumbe hawajui Mbunge Zephania Zuberi ni mwanachama pia wa The Board. Nikatamani kuwaambia lakini nikaimbia tena nafsi yangu kuwa si busara kuweka mezani karata zangu zote kwa wakati mmoja. Nikanyamaza na kuendelea kusikiliza maelezo ya Waziri Wangwe.

Waziri Wangwe akaendelea na maeleza, “tanahisi kuwa The Board ilianzishwa zaidi ya miaka arobaini iliyopita! Tunaami kuwa ilianza na wanachama kumi na mbili pekee na wamekuwa wakiongeza wanachama kwa kadiri ya mahitaji ya wakati husika. Tunaamini kuwa lengo lao kuu ni kushika uchumi wa nchi na kufanya ushawishi nchi iende vipi na ili kutekeleza malengo hayo wamekuwa wakiratibu matukio mengi makubwa katika nchi kwa miaka mingi sana”

Akaongea Waziri Wangwe na kuchukua faili lingine na kunirushia mbele yangu kwenye meza. Nikalichukua na kuanza kulipitia. Juu lilikuwa limeandikwa T.B. Strategy # 008. Waziri Wangwe akaamza kunipa maelezo.

“Tunaamini kuwa The Board kwa kushirikiana au kutumiwa na baadhi ya nchi za nje ndio walioratibu mpango mzima wa kuondoa sera na itikadi ya ujamaa nchini”

Akachukua faili lingine na kulirusha mbele yangu, hili lilikuwa limeandikwa T.B. Starategy # 0012. Waziri Wangwe akaendelea na maelezo.

“Tunaamini kuwa The Board ndio walioratibu mkakati wa kushusha thamani ya shilingi kwa mara ya kwanza kabisa na kusababisha mgogoro wa kiuchumi nchini mpaka mzee wetu kipindi kile akaachia madaraka kutokana na umaarufu wake kisiasa kushuka kutokana na kupingana na mipango hii. Usiniulize kushuka thamani ya shilingi iliwanufaisha vipi, baadae ukipitia hiyo file utapata majibu”

Akachukua faili lingine na kulirusha mbele yangu. Hili lilikuwa limeandikwa T.B. Strategy # 0021. Waziri Wangwe akaendelea na maelezo.

“Tunaamini kuwa kstika miaka ya tisini na elfu nbili mwanzoni The Board kwa kushirikiana au kutumiwa na IMF waliratibu mkakati wa ubinafsishaji wa viwanda, mali na mashirika ya umma nchini.”

Akachukua tena faili lingine na kunirushia mbele yangu. Hili lilikuwa limeandikwa T.B. Strategy # 0031. Waziri Wangwe akaendelea tena na maelezo ila safari hii yalikuwa maelezo mafupi tu. Kwasababu nilipofungua faili na kutazama ndani nikakuta maelezo lakini juu take kulikuwa na picha ya kiongozi mstaafu. Nikainua macho kumuangalia Waziri Wangwe. Naye akaongea kwa kifupi tu,

“Uchaguzi mkuu 2005, tunaamini The Board walimuingiza huyo mgombea madarakani”

Nikainama kuangakia faili na kuangalia Picha ya yule kiongozi mstaafu. “Aiseeee!” Nikajikuta nimetaka neno hilo tu.

Waziri Wangwe akachukua faili lingine lakini safari hii hakunirushia mbele yangu kwenye meza bali akiendelea kulishikilia mkononi na kuanza kunipa maelezo.

“Tunaamini kuwa kwa miaka yote hii zaidi ya arobaini toka kuanzishwa kwa The Board wamekuwa wakitekeleza mkakati mmoja baada ya mwingine, hiyo niliyokuonyesha ni mifano ya mikakati michache tu waliyoitekeleza lakini tunaamini jumla ya mikakati hiyo ambayo wameitekeleza tayari mpaka sasa iko thelathini na tatu! Na kwa sasa wako wanatekeleza mkakati wa thalathini na nne” akaongea akinionysha lile faili alilolishika mkononi mwake.

“Dogo, sasa hapa ndio naomba unisikilize kwa makini kweli kweli maana ndipo tunapohitaji utusaidie”

Nikakaa sawa sawa kwenye sofa na kutega masikio yangu kwa shauku kubwa.

“Nakusikiliza Mheshimiwa!” Nikamwambia Waziri Charles Wangwe nikiashiria niko tayari kuyasikia hayo maelezo ya mkakati wa thelathini na nne na kitu gani wanataka nisaidie kukifanya

Mhe. Wangwe akaweka faili mbele yangu na kuanza kunipa maelezo.

“Kwa taarifa ambazo tumeweza kuzikusanya mpaka sasa tuna kila sababu ya kuamini kuwa mkakati namba 0034 unalenga kuhakikisha wanachama wa The Board wana asilimia kubwa katika umiliki wa vitalu vya gesi na mafuta”

Akaacha kuongea na kutulia kidogo.

“What? Sidhani kama mko sahihi kwa kadiri ninavyo fahamu vitalu vyote vya gesi viko chini ya makampuni ya kigeni na msimamo wa Waziri wa nishati unajulikana kuwa hataki watu wa ndani ya nchi wahusike katika utafutaji na kuchimba gesi na mafuta” nikamuuliza Waziri kwa mshangao.

“Yes, Ray! That’s exactly why wakaja na mkakati namba 0034”

“Mheshimiwa, ili kuepuka yote haya sioni sababu kwanini msiwaruhusu wazawa kuhusika katika kutafuta na kuchimba gesi na mafuta, sioni kama kuna ubaya wowote” nikamuuliza tena kwa mshangao.

“Of course, uko sahihi kabisa Ray! Tunapaswa kuruhusu wazawa kuhusika katika sekta ya gesi na mafuta.. But hatutaki kuwaruhusu The Board! Sijui unanielewa, tunataka kuwaruhusu wazawa lakini hatutaki kuruhusu The Board! Hawa watu hatuna imani nao, kila jambo na kila mkakati walioutekeleza umekuwa na manufaa kwao binafsi lakini hakuna manufaa kwa nchi! Kama nilivyokueleza awali hawa watu lengo lao ni kushika uchumi wa nchi na kujiongezea ushawishi katika mwenendo wa nchi! So, no Ray hatuwezi kuruhusu The Board watushinde tena akili kwenye hili.” Waziri Wangwe akaongea huku ananiangalia usoni akiwa serious haswa.

“Ok! So, mnahisi mpango wao ni upi ukizingatia karibia vitalu vyote viko chini ya makampuni ya nje” nikamuuliza Waziri.

“Nitakupa mfano mmoja kukuwezesha kuelewa kuelewa angalau kiasi wanachokipanga kwenye mkakati huu 0034” Waziri Wangwe akaongea huku akikaa sawa kwenye sofa na kuinama mezani kwenye lile faili aliloliweka na kuanza kunipa maelezo.

“Nitakupa mfano wa kampuni ya Quebec Energy inayofanya utafutaji mafuta kwenye bonde la ufa kilosa na kilombero mkoani Morogoro. Kampuni hii imepewa zaidi ya hekari 440 katika sehemu ya bonde la ufa lililopita Morogoro. Walipewa licence na serikali toka mwaka 2008 na mwaka 2009 wakaanza rasmi shughuli za utafutaji mafuta. Mwaka 2013 wakapata mafanikio makubwa ya shughuli zao” Waziri Wangwe akanyamaza akatoa ukurasa mmoja kutoka kwenye faili, ukurasa huu ulikuwa unaonyesha michoro na picha za miamba.

“Hizi ni 2D sesmic data inaonyesha kwamba katika sehemu ya chini kabisa pembezoni mwa miamba ya bonde kuna vitu viko deposited” Waziri akaongea na kuweka karatasi ile chini na kuchukua nyingine.

“Hii nyingine inaonyesha data za sesmic stacking velocities kutokana na tafiti katika bonde la kilombero na kilosa data hizi zinahakikisha kuwa chini ya bonde umbali wa mita elfu tatu kwenda chini kuna miamba ya kale ya kipindi kijografia kinachoitwa Neogene-age.! Characteristics hizi ziko sawa kabisa na eneo la bonde la ufa lilipopita katika Ziwa Albert nchini Uganga ambako kumegundulowa kuwa na deposit ya karibia mapipa bilioni nne pia characteristics hizo hizo ziko sawa sawa kabisa na eneo la Lockchar nchini kenya ambako pia kimepita bonde la Ufa na kiwango kikubwa cja mafuta kimegunduliwa.! Kwahiyo tuna hakika Vitalu hivi vya Kilombero na Pangani vilivyo chini ya Quebec Energy vina kiwango kikubwa pia cha mafuta ardhini.” Akaeleza Waziri Wangwe na kuendelea.

“Sasa basi, katika mikataba mingi ya utafutaji mafuta na gesi, kitalu kinakabidhiwa kwa kampuni moja lakini ndani yake kunakuwa na na makampni mawili, matatu au zaidi! Kwa maana ya kwamba kwenye kitalu kinakuwa na kampuni ambayo tunaita kuwa ni Operator, huyu ndiye anayekabidhiwa kitalu. Lakini huyu Operator anakuwa na financers! Huyu Operator yeye ndiye anayeendesha shughuli za kila siku za utafutaji kwenye kitalu na ndiye mwenye mitambo. Hawa financers wao ndio wanahakikisha kuwa kuna rasilimali fedha kwa ajili ya kuendesha zoezi zima la utafutaji mafuta”

“Sasa hawa Quebec Energy wao ndio operators wa eneo la utafutaji wa mafuta katika bonde la ufa eneo la kilombero na Pangani lakini financiers wao ni kampuni inayoitwa Matas Associates ambayo imesajiliwa katika visiwa vya Canyon Islands.”

Waziri wangwe akatulia kidogo na kuniangalia.

“Tuko pamoja Ray?” Akaniuliza.

“Tuko pamoja Mheshimiwa” nikamjibu, nilikuwa niko makini kweli kweli nikisikiliza neno kwa neno, sentensi kwa sentensi.

“Ok, vizuri” akanijibu waziri huku akikaa vizuri tena kwenye sofa aendelee kunipa maelezo.

“Ray, unapaswa kufahamu kuwa katika sekta hii ya mafuta na gesi kuna ujanja mwingi sana na moja wapo ya wajanja wa kubwa ni hawa financers, ndio maana wengi wanaenda kusajili kampuni zao katika nchi ambazo zinaficha taarifa za kifedha za watu kama nchi ya Canyon Islands. Kwa taarifa tulizo nazo hawa Matas Associates ni ‘shell company’! Ni kampuni ambayo iko kwenye makaratasi tu.. Tunaamini kuwa kuna mzungu mmoja mjanja akaianzisha kwa mtaji wa dola milioni moja ili aweze kuingia mkataba na Quebec Energy. Tunaamini kuwa mwaka mmoja uliopita Khalid Mohammed mmoja wa wanachama wa The Board aliinunua kampuni ya Matas Associates lakini hakununua yeye direct, alitumia mlolongo wa majina ya kampuni anazoziliki huko Oman. Na ndipo hapa mchezo mzima unaponoga.” Waziri Wangwe akatulia tena kuniangalia kama tuko pamoja kisha akaendelea.

“Tunafahamu kuwa huyu aliyeanzisha Matas Associates katika mkataba wake na Quebec Energy alikubali apewe asilimia ndogo sana za ubia katika mkataba wao ndio maana hata ikawa rahisi kwa Quebec Energy kumchagua yeye kama financier na kuwaacha wengine. Lakini tunaamini kuwa lengo la mmliki wa Matas Associates ilikuwa ni kiuza kampuni yake kwa faida mara tu ikigundukika kuwa kuna deposits za mafuta huko kilombero na pangani na lengo lake hili limetimia mara baada ya Khalid Mohammed kununua kampuni yake ya Matas. Sasa usidhani kwamba Khalid na The Board ni wajinga walikuwa wanajua wanachokifanya kuwa wananunua kampuni ya kwenye makaratasi na mtaba wa kampuni hiyo na Quebec Energy unawapa asilimia chache katika ubia. Licha ya hayo yote lakini walikuwa bado na nguvu moja muhimu! Wao ndio financiers wenye jukumu la kutoa fedha shughuli ziende. Hapo ndipo walipoanza kuhujumu Quebec Energy.” Waziri akachukua faili lingine na kuliweka mbele yangu.

“Nikukumbushe kitu, Quebec Energy walipewa licence mwaka 2008 na licence ilikuwa inaisha mwezi january 2016. Lakini mpaka kufika january mwaka huu 2016 walikuwa bado hawajafanikiwa kufanya drilling ya kisima ili kuhakikisha kuwa kuna mafuta kama jinsi data zilivyokuwa zinaonyesha… Ndipo hapa serikalo ikaamua kuwaongeza muda na kuwapa extension ya mwaka mmoja hadi january 2017. Lakini Miezi miwili baada ya Matas associates kununuliwa na Khalid Mohammed wakafungua kesi mahakama kuu kumshitaki mbia wao Quebec Energy. Wakatumia hoja za kipuuzi tu zilizoandikwa kwa lugha tamu za kisheria na walichokuwa wanadai ni kuwa Quebec Energy imefanya uzembe kwa kushindwa kufanya drilling ndani ya kipindi rasmi cha licence hivyo kuongeza mwaka mkoja mwingine ili kufanya drilling hii itasababisha gharama za uendeshaji kuongezeka tofauti na ilivyopangwa awali, hivyo basi katika shauri lao hilo wakawa wanaitaka Quebec Energy itoe asilimia kadhaa za ubia wake na kukabidhi kwa kampuni nyingine ili ije kuwa operator katika kipindi hicho cha extension ya mwaka mmoja ulioongezwa na serikali!” Waziri Wangwe akanichambulia kwa makini kisha akatulia kidogo kuniangalia.

“Bado tuko pamoja Ray?”

“Tuko pamoja Muheshimiwa” nikamjibu.

“OK, sasa…” Waziri akaendelea “lengo la The Board na Khalid Mohammed kupitia Matas Associates kufungua kesi ni kuinyima fedha Quebec Energy wao wakiwa kama financiers ili hatimae hatua ya drilling isifanyike na shughuli zote zikwame na Quebec Energy ipokonywe licence au isipiwe extension nyingine mara baada ya extension ya kwanza ikiisha 2017, January” Waziri akanyamaza tena kidogo nadhani alihisi kuwa nina swali.

“Whaaat?? Quebec wakipokonywa licence hii inamaanisha kuwa na Matas hawana chao tena katika utafutaji huo wa mafuta kilombero na Pangani!” Niakamuuliza kwa mshangao.

“Yes ndio maana yake” Waziri naye akanijibu kwa kifupi.

“Siku zote hizi mimi nilikuwa nahisi labda The Board wanafanya manipulation ya taarifa za utafutaji mafuta huko kilombero ili kuongeza thamani ya hisa za Quebec katika masoko duniani” nikauliza tena kwa mshangao.

“Hapana wanacholenga ni Quebec wapokonywe licence au ikifika January mwakani 2017 wasipewe extension nyingine” akanijibu Waziri Wangwe.

“Wao wananufaikaje na hili” nikauliza kwa mshangao mkubwa.

“Swali zuri sana ray!” Waziri akaanza kunijibu.

“Kumbuka nimekueleza kuwa mkakati namba 0034 tunaamini unalenga sekta ya gesi na mafuta, pia kumbuka kuwa kampuni Matas Associates iloyonunuliwa na Khalid Mohammed kwa niaba ya The Board ilikuwa na asilimia chache sana kwenye ubia wake na Quebec Energy hivyo basi tunaamini kuwa lengo kuu la The Board lillikuwa ni kufanya sabotage ili Quebec wapoteze vitalu hivi vya Kilombero na pangani ili baadae vije virudi mikononi mwa The Board kwa kutumia kampuni nyingine! Hii inawezekanaje?” Waziri akanyamaza kidogo na kukaa vyema kwenye sofa aendelee na maelezo.

“Katika nchi yetu tunaamini kuwa kuna deposits za mafuta baharini lakini ni Kilombero na Pangani pekee ndiko tunaimani kwa asilimia kubwa kuwa kuna mafuta na tunaamini hiyo ndio sababu kwanini The Board wameamua kuanza nako. Sasa nini kitafuata baada ya wao kufanya hii sabotage kwa Quebec? Duniani kuna system mbili za kutoa licence kwa kampuni za kutafuta mafuta na gesi. Kuna Bid System na kuna Grant System. Bid system inatumika hasa na nchi za ulaya ambapo kampuni zinashindana kuomba licence katika kitalu specific na kwa muda specific! Lakini sisi hapa nchini tumefuata mtindo wa nchi za kiarabu ambao ni Grant system, ambapo serikali inakuwa na orodha yake ya vitalu na makampuni yanaomba tu serikalini kuwa yanataka kufanya utafutaji mafuta na gesi kisha serikali wao ndio wanavigawanya vitalu kwa makampuni vile ambavyo serikali wao wanaona kampuni gani ikae kitalu gani na kwa muda gani!! Hii ni grant system.. Sasa endapo Quebec watapokonywa licence january 2017 maana yake viatalu vya Kilombero na Pangani vitaingizwa katika mkupuo ujao wa ugawaji vitalu.. Sasa ingesaidia kama tungekuwa na Bid System coz tungeweza tu kuyamonitor makampuni yatakayoomba vitalu vya Kilombero na Pangani na tungegundua kampuni gani nyuma yake kuna The Board! Lakini ubaya hii grant sustem ni serikali ndiyo inayopangia kampuni gani ikae kitalu gani.! Na bahati mbaya taarifa zetu za intelijensia hatujaweza kufahamu The Board wamepanga kutumia mbinu gani ili kuwachanganya serikali wagawe Kitalu cha Kilombero na Pangani kampuni wenye masilahi nayo!! Ndipo hapa sasa tunahitaji kujua mkakati 0034 kinaga ubaga.. Inabidi Tuupate kabisa wote mkononi tuusome! Na ndio sababu ya kukuita wewe hapa!” Waziri Wangwe akamaliza kunipa maelezo na kuniangalia.

“Wooooooww! Aiseeeee” nikajikuta nashindwa kupata neno la kuongea. Nikashusha pumzi na kuinamisha kichwa sekunde kadhaa nikifikiri, kisha nikainua kichwa na kumuuliza waziri;

“Kwanini msiwakamate hao wanachama wa The Board ambao mmeshawatambua na kuwahoji kwa kutumia ‘mbinu’ zenu ninazozisikiaga” nikamuliza waziri.

Waziri Wangwe akatabasamu, “Ray, usiamini kila unachosoma kwenye magazeti na mitandao, sisi sio watesaji! Unajua ubaya wa torture? Ukimtesa mtu kama ni muoga atakupa taarifa unayoitaka haraka tu. Lakini mwingine utamtesa mpaka anakufa hakwambii chochote! Sasa hebu imagine watu mashuhuri kama wanachama wa The Board ije kujulikana amefia mikononi mwetu hiyo skendo itakuwaje?? Si itatutafuna mpaka tuishe?? Lakini usisahau pia ukimtesa mtu anaweza kukwambia hata kile ambacho hakijui, ataropoka tu chochote ili mradi uache kumtesa! Kwa hiyo taarifa inayo patikana kwa kutesa mtu hainaga uhakika na thamani. Tunachokifanya sasa ni sawa sawa na ukimuona panya ana randa randa chumbani kwako, usifanye haraka ya kumuua! Mfatilie taratibu tu, muda si mrefu atakupeleka mpaka kwenye shimo lake na humo ndimo utawakuta mama zake, watoto zake, babu zake na ukoo wote! Hicho ndicho tunachokifanya Ray.” Akaongea Waziri huku anatabasamu.

“Na Mhandisi Jaffar Kumbea anahusikaje kwenye hill?” Nikamuuliza huku nimemkazia macho.

“Hiyo ni taarifa ya ndani sana ila wacha nikupe ili tujengeane uaminifu zaidi” akaongea Waziri Wangwe huku anatabasamu zaidi.

“Mda mchache kabla ya Waziri Japhet Kipanju Kuuwawa alitoka nyumbani kwake Masaki majira ya Saa mbili usiku akaelekea moja kwa moja Mawasiliano Tower, hatujui alienda kuonana na nani ila waliomuona wanadai alifika hapo mikono nitupu ila dakika kadhaa baadae alipokuwa anapanda gari kuondoka alikuwa ameshika begi dogo la mkononi linaloonekana lilokuwa na makaratasi. Baada ya kutoka hapo akaelekea Land Mark Hotel karibu na River side ubungo. Akiwa hapo akaongea kwa takribani lisaa lizima na Mwandisi Kumbea na alipotoka hapo na kufika Ubungo akisubiri taa kumruhusu ndipo akapigwa risasi na kufariki. Like begi alilokuwa amepewa Mawasiliamo Tower, halikukutwa kwenye gari. Hivyo tunamshikiria Muhandisi kwa kuwa tunahisi anahusika na kifo hiki, au anahusika na kupotea kwa hizo nyaraka, au labda anajua kilichopo kwenye hizo nyaraka au yote matatu! Kitu pekee kitakachosaidia kuachiliwa kwake ni endapo tutazipata hizo nyaraka na kuoanisha na kile anachotuambia, tukiona kuna ukweli nasi hatutakuwa na budi kumuachia!”

“Ni kitu gani alichowaambia?” Nikamuuliza waziri haraka haraka.

“Samahani Ray hiyo taarifa siwezi kukwambia” akanijibu Waziri Wangwe huku anatabasamu.

“Ok! Nadhani tumeongea kila tulichopaswa kuongea, ni vizuri niende sasa sidhani kama kuna la ziada” nikawaeleza huku nikianza kusimama.

Nukaona wameangaliana na kupeana ishara fulani hivi kisha Baba bite akaongea.

“Hakuna shaka Ray, unaweza kwenda najua ni kiasi gani Cheupe yuko kwenye wakati mgumu kutokana na mzee wake kukamatwa kwa kesi ya mauaji na najua ni kwa kiasi gani hii inakuathiri hata wewe hivyo naomba ukumbuke kuwa kupatikana kwa haraka kwa taarifa kuhusu mkakati mzima namba 0034, au kupatikana kwa nyaraka zilizopotea kutoka kwenye gari la Marehemu Waziri Kipanju, au taarifa yoyote muhimu kuhusu The Board ndivyo itakavyo harakisha kuachiwa kwa Muhandisi Kumbea! Hivyo basi ukipata taarifa yoyote muhimu naomba tuwasiliane haraka iwezekanavyo” aliongea Baba bite huku ananipa mkono.

“Tunawasiliana vipi wakati mmesema hamtaki ijulikane kuwa nashirikiana na nyinyo” nikauliza huku tukipeana mikono na baba bite na wengine.

“Ni rahisi sana Ray, ukiwa na taarifa muhimu na unataka tuonane, nenda mpaka Mlimani City duka la Skolastika bookshop, chagua kitabu chochote cha bei ghari kisha ukienda kulipia kaunta mpe hela ndogo kama elfu tano hivi mfano na akikwambia hela haitoshi mjibibu “kuna hela yangu huku” kisha atakuacha uende.! Baada ya hapo nenda jizungushe zungushe kama nusu saa rudi umwambie akubadilishie kitabu akupe kingine kwa sababu kile labda kina kurasa zimechanika au mpe sababu yoyote ile then atakubadilishia kitabu na kukupa kitabu kingine ambacho ndani yake utakuta maelezo ni namna gani tuonane” akaniekeza Baba Bite

“Oooohh Ok.!” Nikaitikia tu kwa kifupi.

Nikaagana nao. Wakanikabidhi funguo yangu ya gari, nikatoma nje na kuwasha gari na kuondoka.


Nilikuwa nimepaki gari maeneo ya pembeni kidogo ya kituo cha fire karibu na shule ya sekondari ya jangwani. Nilikuwa hapa namsubiri Isack aje akitokea kwao pale pale karibu tu, Upanga mtaa wa Mindu. Pia nilikuwa nimempigia simu Cheupe atoke kwao Tegeta anisubiri Ubungo kwasababu inabidi turudi Morogoro! Alilalamika kweli kweli lakini uzuri Cheupe wangu anajua kunisikiliza na kilichomtuliza zaidi ni nilivyo muambia kwa kifupi tu “I have a plan”.

Kichwani nilikuwa nawaza jambo moja tu ni namna gani tutamnusuru Mhandisi Jaffar Kumbea na kesi nzito iliyoko mbele yake kuhusishwa na mauaji ya Waziri mwandamizi wa serikali.

Hilo tu ndio lilisumbua akili yangu na kuninyima raha. Hata njaa nilikuwa sisikii. Akili ilikuwa imevurugika. Huo ugomvi wao wa viatalu vya mafuta haunihusu! Its a dog fight..

Niliumia sana jinsi Cheupe wangu nilipokuwa namuona akiwa kwenye maumivu mazito kutokana na jambo hili. Na si hivyo tu Mhandisi Kumbea licha ya kuwa baba mkwe wangu mtarajiwa, bali pia alikuwa ni rafiki yangu, baba yangu na mtu aliyenisaidia vitu vingi sana kwenye maisha. Sikuwa tayari Mhandisi Kumbea apokwe uhuru wake kirahisi hivi, sikuwa tayari Cheupe wangu aishi na maumivu na simanzi maisha yake yote, sikuwa tayari mimi mwenyewe kuishi na maumivu kama ninayoyasikia sasa kwa maisha yangu yote yaliyobaki. I must do something. Kwa muda huu nilijihisi kuwa nimezaliwa ili niweze kuimaliza changamoto hii pekee. Nothing else matters. Maisha ya watu wengi yako mikononi mwangu, naweza kuwanusuru. Mhandisi kumbea, hasnat, mama yake na mimi mwenyewe.

“I have a plan”, nikajisemea mwenyewe tena moyoni. Ubaya ni kwamba nilikuwa na hakika hakuna ambaye angekubali nitekeleze plan hiyo. Hakuna ambaye angekubali nifanye kitu cha hatari nilichokuwa nimekipanga kichwani. Lakini sikuwa na namna nyingine!

“I have a plan” nikajisemea tena moyoni nikijipa moyo.

Mara kigari aina Vitz kikapaki karibu yangu! Isack.

Akashuka kwenye gari yake na kuingia ndani ya gari yangu. Baada ya salamu na kumpa mrejesho wa yaliyojiri kuhusu ufuatiliaji wa ishu ya Mhandisi Jaffar Kumbea Wizara ya mambo ya ndani (sikumwambia chochote kuhusu “kutekwa” kwangu na Usalama wa Taifa), nikaenda moja kwa moja kwenyd point yangu.

“Hivi kuna kifaa chochote cha kuzuia mtu asikusikie endapo amekuwekea ‘bug’ ya kunasa sauti nyumbani kwako au kwenye gari au kwenys nguo?” Nikamuuliza Issack

“What? Aaaahh i guess kipo aaaahh! Hey what the fu*k is going on man? Nadhani imefika mda uache kunificha kinachoendelea!!” Issack akabwata.

“Come on man, I promise nakwambia, nijibu basi hicho kifaa kipo kuzuia ‘bug’ iendelee kuwepo ila mtu asikusikie?” Nikamuukiza kwa msisitizo.

“Aaaahh yeah kipo! Kinaitwa aaaahh dah jina limenitoka kidogo, aaaahh kinaitwa pink noise generator! Yes, kinaitwa pink noise generator!” Akajibu Isack huku ana tabasmu baada ya kukumbuka jina.

“Ndio kinafanyaje?” Nikamuulza

“Well, aaaahh unajua vile mfano ukiwa unatafuta station ya radio alafu redio kuna mda kama ‘inapiga miluzi’ hivi, yes the same thing pink noise generator inaingilia frequency za ile ‘bug’ yule anayekusikiliza kule anakuwa anasikia kama miluzi ya redio tu sauti yako wewe haisikii hata tone!” Isack alijibu huku anatabasamu, huyu rafiki yangu anapenda sana kumuelekeza mtu jambo

“Nakipataje?” Nikamuuliza

“Well, kibongo bongo ngumu but unaweza kukinunua eBay kwa mfano, inachukua kama siku tano au sita mpaka kifike bongo” akanijibu Isack

“Ok then, agiza vinne au zaidi”

“Ok, but for what??” Akauliza kwa mshangao.

“Nimeshakwambia nitakueleza! Hilo jambo la kwanza, la pili unakumbuka Jana tumeongea kuhusj Eric Kaburu?”

“Yes nakumbuka vizuri tu”

“Ok! Nataka ukae chini utulie uchimbe historia yake, chochote utakachokipata kuanzia utotoni mpaka utu uzima.. Pia weka mkazo zaidi kwenye kesi yake ta mauaji ya mpenzi wake miaka miwili iliyopita! Chimba kila kitu kuhusu ile kesi.. Mpenzi wake ni nani, walikutanaje, kifo chake kilikuwaje, mpelelezi alikuwa nani, Jaji wa kesi alikuwa nani, mashahidi walioletwa akina nani na kadhalika! Pia chimba kuhusu kampuni yake ya Ndeshema Safaris! Kila kitu kitu utakachokipata.!” Nikamueleza haraja haraka.

“Ok, but what the fu….”

“Sijamaliza!” Nikamkatisha, “leo funga funga vitu vyako kesho uje Morogoro, na kuanzia kesho nakupa ajira rasmi Sote Hub! Congratulations!” Nikamwambia kwa utani lakini nikimaanisha..

Isack akabaki ameduwaa tu! Sijui alikuwa anafikiria nini kichwani mwake.

“Hey Isack namuwahi Cheupe Ubungo, tafadhli anza kuyafanyia kazi hayo niliyokuambia”

“Kichwa! What the fu*k is going on man?” Isack akauliza bado akiwa na mshangao.

“I have a plan! Jitahidi kesho ufike Moro mapema” nikamueleza Isack huku nikilazimisha kutabasamu nikikumbuka jinsi wazo langu lilivyo la kiwendawazimu.

Isack akatoka na kuelekea kwenye gari yake. Na mimi nikakanyaga mafuta kuelekea Ubungo kumchukua Cheupe tuanze safari ya Moro.

“I have a plan!” Nikajisema tena moyoni. Nikajipa moyo. Nikakanyaga mafuta.

Tayari tulikuwa tumefika Mazimbu Morogoro. Na tulikuwa tupo sebuleni mimi na Cheupe.

Njiani tukiwa tunatoka Dar kuja Morogoro, nilimsimulia Hasnat kila kitu ambacho kilitokea.

Kuanzia kuchukuliwa na watu wa Usalama kutoka kwenye gari yangu maeneo ya Magomeni Popobawa na kupelekwa Mbezi Beach, kukutana na maafisa wao akiwemo Baba Bite, uwepo wa Waziri Charles Wangwe katika kikao hicho na kila kitu walichonieleza kuhusu mikakati ya The Board na wanachohisi kuhusu mkakati namba 0034.

Pia nikamueleza kuhusu kwanini Usalama wa Taifa wanamshikilia Baba yake Muhandisi Jaffar Kumbea. Nikamueleza kuhusu Mhandisi kumbea kukutana na Waziri Kipanju muda mfupi kabla ya Waziri kupigwa risasi maeneo ya Ubungo na kupotea kwa nyaraka alizokuwa nazo.

Safari yetu yote kutoka Dar mpaka Morogoro nilikuwa namuelezea mambo haya kwa kina na kwa utaratibu. Nilikuwa nataka ayaelewe mambo haya kwa ufasaha kutokana na mpango wangu niliokuwa nimeupanga kichwani.

Sasa nilikuwa nimeshamaliza kumueleza kila kitu na alikuwa ameelewa kwa ufasaha kabisa na tulikuwa tumeshafika Nyumbani mazimbu, tumeoga na tumekaa sebuleni na kulikuwa na swali moja tu mbele yatu.

“So what’s your plan Ray?” Akaniuliza Cheupe. Tulikuwa tumekaa kwenye Sofa dogo la watu wawili na tumevuta meza karibu yetu na nilikuwa nimeweka makaratasi kadhaa juu ya meza nayachambua chambua.

Nikaacha kuchambua yale makaratasi nikakaa sawa na kumuangali.

“Cheupe, sasa hivi sitaki kufanya chochote kwa ajili ya kusaidiana na The Board wala watu wa Usalama. Kilichopo akilini mwangu ni namna gani tunaweza kusaidia Mzee wetu asipatwe na matatizo makubwa ya kukabiliwa na kesi ya mauaji! Hayo masuala yao ya ugomvi wa vitalu vya gesi na mikakati yao sitaki kujisumbua nayo! Thats their business not mine” nikaongea nikiwa nimemsogelea cheupe.

“Nimekuelewa hilo baba toka mwanzo” Cheupe akanijibu.

“Kwahiyo sasa, ninachokiona ni kwamba jambo la kwanza kabisa ili kuelewa kwanini Waziri Kipanju aliuwawa inatupasa tuelewe wanachokipanga The Board, na hii inaweza kutoa mwanga nyaraka zilizoibiwa siku Wazriri alipouwawa zilihusu nini na pengine inaweza kutuwezesha kumjua muuaji halisi” nikamueleza Cheupe sasa nikiwa nimemkaribia karibu yake kabisa.

“Ok! That make sense! So umepanga tunafanikishaje hilo?”

“Ninachokiona uwezekano pekee kwangu kuelewa kilichopangwa na The Board ni kuanza kwenye source iliyonifanya niingie kwenye mipango yao.. Hapa naongelea Alice Cartz Foundation, na nikiwaongelea wao nawagusa donors wao Ndeshema Safaris na nikiongelea Ndeshema Safaris tunamuongelea mmliki wake Eric Kaburu.” Nikanyamaza kidogo.

“Nakusikiliza baba” akaongea Cheupe huku ananiangalia kwa macho ya udadisi.

“Tunachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kuwa Eric Kaburu anazungumza nasi! Na hili kufanikisha hili natakiwa nikae nae kwa muda mrefu kumshawishi kwa kutumia details zozote ambazo tutakuwa nazo juu yake ambazo zinaweza kumfanya asiwe na jinsi nyingine zaidi ya kuongea nasi” nikamueleza huku namtazama machoni. Cheupe alianza kupepeaa macho, alikuwa na desturi akianza kupaniki anapepesa macho haraka haraka, akiyafumba na kuyafumbua.

“Well, kama hukumbuki wacha nikukumbushe! Ni juzi tu umetoka gerezani kuongea naye na amekataa na akakuambia kwa usalama wake na wako usiende tena kumtembelea ili uongee naye” akaongea Cheupe huku kupeoesa macho kukiwa kumeongezeka.

Nikavuta pumzi ndani na kuzishusha taratibu. Nikajikaza kiume ili nipate ujasiri kumuambia “bomu” nililokuwa nimelipanga kichwani. Nikamuangalia machoni Cheupe na ‘kutumbua jipu’.

“Cheupe, nataka niingie gerezani nikiwa kama mfungwa au mahabusu” nikamueleza huku nimemkazia macho hasa.

“Whaaaaaaaaaaattt.!!?? I knew you had a crazy idea lakini sikudhani litakuwa wazo baya kiasi hiki! No no no no nooooo Ray, you are not going anywhere! Unanisikia? You are not going to do that”

Cheupe aliongea kwa hisia huku akianza kulengwa lengwa na machozi. Alijua fika kuwa haijalishi angenisisitiza kiasi gani lazima ningetekeleza wazo hilo.

Alijua udhaifu wangu. Nikishapataga wazo kichwani mwangu, inakuwa ni impossible to talk me out of it! Lazima nitalitekeleza. Nikamuona akianza kulia.

“Hasnat please I have to do this.. Kesho Issack anakuja hapa Morogoro na mimi nikishaingia gerezani mtashirikiana kukusanya taarifa kuhusu Kaburu then mtakuwa mnaniletea gerezani ili zinisaidie kumshawishi aongee na sisi” nikaongea kwa taharuki.

Wote tulikuwa tumesimama. Hasnat alikuwa analia akishindwa aniambie nini ili nielewe. Nilitamani nibadili mawazo yangu, lakini kila nilipofikiria kubadili mawazo nikajikuta najiuliza. Je, kuna alternative nyingine? Na nikajijibu mwenyewe hakuna!

Hasnat alikuwa ana bubujikwa na machozi. Roho iliniuma kweli kweli. Nikamshika na kumsogeza kwangu na kumkumbatia kwa nguvu.!!

“Please don’t do this to me Ray, please don’t!” Hasnat alilia na kuongea kwa sauti ndogo.

“I have to do this honey! I have to do this kwa ajili ya Mzee, kwa ajili yako, kwa ajili yangu, kwa ajili yetu sote! I have to do this honey, I’m so sorry!!” Nikamkumbatia kwa nguvu zaidi.

Hasnat akaendelea kulia na kadiri muda ulivyokuwa unaenda kilio chake kilijuwa kinapungua. Zikawa kama kwikwi hivi. Nikaendelea kumkumbatia kwa nguvu.. Akalala kifuani kwangu tukiwa bado tumesimama pale pale katikati ya sebule.

“Hasnat nadhani nikueleze sasa jinsi nilivyo panga kuingia………” Kabla sijamaliza kusema nilichotaka akanikatisha.

“Please Ray, usiseme chochote kingine! Just hold me tight” akaongea akikilaza tena kichwa chake kifuani na mimi nikamkumbatia kwa nguvu.

Nikamsogeza kwenye sofa kubwa ya watu watatu. Tukajilaza. Akalala kifuani kwangu huku nimemkumbatia kwa nguvu.

Tukakaa hivyo kwa takribani dakika kumi bila yeyote kati yetu kusema chochote.

Mara Hasnat akainua kichwa na kunitazama.

“Honey I’m scared!” Akaongea huku ananitazama ndani ya macho.

“Unaogopa nini mama?” Nikamjibu huku namdekeza kwa kupitisha vidole vyangu kwenye nywele na kumkumbatia kwa nguvu.

“Gerezani sehemu ya hatari baba, I’m really scared” akaongea huku bado ananitazama machoni.

“Usijali mama, its going to be fine” nikamjibu kiume nikimuondoa hofu kisha nikaweka mkono nyuma ya kichwa chake na kumvuta taratibu nikimuashiri aendelee kulala kifuani.

Akalala ingawa kichwa hakikulala kifuani exactly kilikuwa juu kidogo ya mabega yagu na kufanya uso wake uwe umenigusa shingoni.

“Nakupenda sana Kichwa!” Akaongea taratibu sana kama ananinong’oneza na dizaini kama ananibusu kwa taratibu sana shingoni. Nikaanza kusikia kama cheche kwa mbali zinapita mwilini.

“Nakupenda zaidi cheupe wangu” nikamjibu kwa sauti ya taratibu pia huku nami nikipitisha vidole kwenye nywele.

Yale mabusu yake ya taratibu shingoni yakaaanza kugeuka na akanza kuninyonya shingoni kwa taratibu.

Zile cheche nilizokuwa nazisikia mwilini zikaanza kuongezeka na “jambazi Mkuu” wa toka utotoni bolo yanki nikaanza kumsikia anaamka kutoka usingizini.

Nahisi Cheupe alihisi jinsi nilivyosisimka, na akataka ‘kunitesa’ zaidi. Akapenyeza mkono ndani ya pensi taratibu akamshika jambazi kuu. Bolo yanki hanaga utani akiguswa tu anachachamaa, nikamsikia alivyosimama mara baada ya kuguswa. Cheupe ili kumpandisha hasira zaidi bolo yanki akaanza kuchezea mayai yake.

Daaaammmnn, nikaanza kusikia mwili jinsi ulivyokuwa unaitikia uchokozi unaofanywa na cheupe. Na kwa kuwa cheupe alidhamiria ‘kunitesa’ zaidi akatoka mkono kutoka kwenye pensi.. Mda huo mimi tayari nishaanza kuwa hoi, alafu alaniangalia moja kwa moja machoni.

Akawa kama anatabasamu hivi, alafu akakipaka mate kiganja chake cha mkono kwa mtindo kama anakilamba hivi kisha akaingiza tena mkono ndani ya pensi. Combination ya vile vitendo alivyonifanya nilisikia raha na kusisikwa nikajikuta nimemkamata kama katoto na kumvuta kwa nguvu nikaanza kuinjoi kunyonya lips zake na mate.

Mkono wake bado ulikuwa ndani ya pensi unamfanyia fujo bolo yanki.

Na mimi nikapenyeza mkono wangu taratibu ndani ya top ya kuanza kuziminya ‘konzi’ kifuani kwake.

Nikaanza kumsikia jinsi alivyoanza kuhema juu juu kwa haraka.

Ghafla tu cheupe akajivuta na kushuka chini akaanza kunisaidia kuvua pensi. Na mimi niakavua tisheti ‘fasta fasta’ na alipomaliza kunivua pensi akavua top yake.

So, mimi nilikuwa kama nilivyozaliwa na yeye alikuwa kifua wazi ila akiwa amebakia na kikaptula tu ambacho alikuwa amekivaa mda wote.

Nikiwa nimelala pale kwenye sofa, Cheupe akashuka na kupiga magoti.

Jambazi kuu bolo yanki mnara ulikuwa uko juu kweli kweli lakini baada ya cheupe kupiga magoti ili ampooze kwa ‘kumtesa’, kitu kikaenda dede zaidi mnara unasoma 4G.

Cheupe akaanza kucheza na jambazi kuu na mdomo wake. Kwa kila aina ya utundu na ufundi. Mara acheze na kichwa tu cha mnara, mara atumie mikono tu. Katika mda huu nikasahau matatizo yote duniani, kuna mda unasikia raha mpaka hujui urespond vipi! Nilichokifanya ni kumshika kichwa tu na kumuacha cheupe aendelee ‘kudili’ na jambazi kuu.

Baada ya kuridhika kumpooza jambazi kuu, cheupe akaanza kufanya utalii taratibu kwenye mwili wangu huku akibusu na kunyonya kila palipomvutia. Kuanzia tumboni, kifuani mpaka akafika mdomoni.

Nikamuinua na kumgeuza yeye akawa amelala juu ya sofa na mimi nikasimama. Nikamuinua miguu juu kisha nikamvua taratibu kikaptula chake na kuanza kuubusu mguu mmoja mmoja, kuanzia kwenye vidole mpaka kwenye mapaja, nikafanya hivyo pia kwenye mguu mwingine.

Kila nilipokuwa nashuka chini nikimbusu mapajani, pumzi zilimuishia cheupe wangu akaanza kuhema juu juu. Sikumchelewesha. Nikakata tiketi ya bombadia, nikaenda uvinza kuchimba chumvi.

Kila alipokuwa anakaribia kutaka kufika kibo na mawenzi nikawa naacha ‘kuchimba’ chumvi.. Makusudi tu ili ‘nimtese’..

“Ray pleeeeeeeeeeaaassse” alijinyonga nyonga na kulia kila mara.

Nikainuka na kuanza kuzinyonya ‘konzi’ kifuani kwake, kisha nikahamia shingoni, na kisha mdomoni.

Nikiwa naendelea kutalii mdoni kwake, nikamuinua mguu mmoja na kuuweka begani kisha nikamruhusu jambazi kuu aingie alipe kisasi cha kuteswa mda wote huu.

Nikaanza kwa kupiga ‘punch’ za taratibu tu lakini zilizo shiba dona na sato.

Nilikuwa natoa dozi huku sibanduki kumnyonya mdomoni kwake na shingoni. Cheupe wangu akawa anagala gala tu kwa raha. Nilipoanza kumpa dozi mikono yake nilikuwa nimeishika na kuibana kwa kuigandamiza kwenye sofa.

Lakini kadiri utamu ulivyomkolea alikuwa anahangaika aitoe mikonoanikumbatie. ‘Nikamtesa’ hivyo kwa muda na baadae nikamuachia, akanikumbatia kwa nguvu akihaha asijue ashike wapi. Mara ashike kiunoni, mara anipapase mgongoni, mara anishike shingoni na kunivuta kwa nguvu nimnyonye mdomoni. Ili mradi tu raha ilikuwa imemkolea.

Nilipoona raha imemkolea zaidi na anakaribia kufika mawenzi, nikaongeza uzito wa ‘punch’! Nikaanza kumpa punchi nzito nzito. Mimi mwenyewe wazungu nilishaanza kuwasikia wanakuja, nikajikaza ili niwaachie waende kwao mda ule ule cheupe akiwa juu ya mawenzi. Cheupe mwenyewe anasemag “hakuna raha duniani kama kufika pamoja”.

Nikaanza kusikia jinsi mwili wake ulivyokuwa kama unavunjia vipande vipande, akijinyongorota kwa kila namna na amenishikilia kiuno kwa nguvu kweli kweli. Ooohh yeah, alikuwa anawasili mlimani, na mimi hapo hapo nikawaruhusu wazungu waende kwao.

Hakika hakuna raha kubwa kama kufika juu pamoja. Kwa jinsi ambavyo tuling’ang’aniana na kila mmoja sauti aliyoitoa! Hakunaga kama zile sekunde ishirini na tatu za kufika juu ya mlima.

Nikajitupa juu ya Cheupe niko hoi! Akawa ananipapasa tu mgongoni. Baada ya muda nikalala pembeni yake, bila kuongea chochote tukiendelea kunyonyana mate kwa karibia dakika kumi na tano.

Baada ya muda kidogo Cheupe akakumbuka maongezi yetu tuliyokuwa tunaongea kabla ‘hatujaondoka duniani’ na kurudi tena.

“Thank you honey! Nakupenda sana kichwa” akaongea huku anashika shika kidevu.

“Anything for you hny! Nakupenda zaidi cheupe” nikamjibu huku namuangalia machoni.

“So tell me hiyo plan yako ya namna utakavyoingia gerezani” cheupe akaniuliza.

“Ni simple tu” nikamjibu na kukaa sawa kuanza kumueleza.

Morogoro Central Police Station

Nilikuwa nimeshamaliza kuchukuliwa maelezo na askari aliyejitambulisha kama Sajenti James Bidebu wa kitengo cha ‘Fraud’ ndani ya jeshi la polisi.

Ofisi za kitengo hiki zipo ghorofa ya pili katika kituo hiki kikuu cha mkoa wa Morogoro. Mwanasheria wangu Hemedi Bantu wa kampuni ya Bantu & Associates alikuwa pembeni yangu muda wote huu nikiwa nachukuliwa maelezo. Issack na Cheupe walikuwa ‘ground floor’ eneo la mapokezi ambapo waliambiwa wasubiri kipindi nachukuliwa maelezo kwa kuwa wao ndio walalamikaji hivyo hawaruhusiwi kuwepo nikiwa nachukuliwa maelezo.

Baada ya kuchukuliwa maelezo nilichokuwa nasubiri ni kupelekwa ‘lockup’ kwa kuwa hakukuwa na mtu wa kunidhamini na hata mwanasheria wangu sikutaka anidhamini.

Nikaanza kukumbuka matukio kadhaa yaliyotokea mpaka kunifikisha hapa.

Ni usiku wa jana tu ambapo nilikuwa na usiku mwanana kabisa na mpenzi wangu Cheupe na mara baada ya kufanya yanayopaswa kufanywa na wakubwa wakati wa giza, ndipo nikamueleza juu ya mpango wangu wa kuingia gerezani na namna gani nimepanga kufanikisha hilo.

Asubuhi kulipokucha, majira ya saa nne Issack alikuwa ameshawasili Morogoro. Alikuja nyumbani na nikamueleza mpango wangu wa kuingia gerezani. Kama ilivyokuwa kwa Hasnat mwanzoni aliipinga lakini baadae ikabidi akubaliane nami baada ya kuona hakuna namna ambayo ataweza kunibadilisha mawazo.

Baada ya hapo wote watatu tukaelekea ofisini kwangu mtaa wa Boma road ghorofa la Hajram. Nikafanya kikao cha dharura na wafanyakazi wote. Nikawaomba radhi kwa kuto kutulia ofisini kwa takribani wiki nzima na pia nikawaeleza kuwa nimepatwa na dharura hivyo inanipasa kuchukua likizo ya mwezi mzima. Pia nikatumia fursa hiyo kumtambulisha Issack kwao na kuomba waridhie Issack kukaa katika nafasi yangu kwa kipindi hiki ambacho nitakuwa ‘likizo’.

Uzuri ofisi yetu wote tunaishi na kufanya kazi kama ndugu hivyo hawakuwa na pingamizi lolote. Wakamkubali Issack na tukaondoka kuelekea Nyumbani na Issack alipaswa kwenda kuripoti ofisini na kuanza kazi kesho yake.

Tukiwa nyumbani tukapeana maelekezo ya mwisho mwisho na kuagana. Nikambusu cheupe wangu, na kumkubatia kwa muda mrefu na kisha akanipa naneno ya faraja sana na kuniambia tena na tena kiasi gani ananipenda.

Baada ya hapo nikachukua simu yake na mkoba wake wa mkononi ambao ndani yake kulikuwa na walet yake ya kike yenye kadi zake za benki. Nikaondoka na kuwaacha nyumbani.

Nikaelekea moja kwa moja kwenye mashine za ATM za benki ya Barclays iliyopo katikati ya mji nikatoa fedha kwa kutumia kadi za benki za Hasnat, nilipomaliza hapo nikaelekea kwenye ATM nyingine ga Barclays iliyopo karibu na soko kuu, nikatoa tena fedha. Kisha nikaelekea ATM nyingine ya Barclays iliyopo katika stendi kuu ya msamvu nako nikatoa fedha nyingine.

Nilipokuja kuhesabu nilikuwa na karibia Shilingi milioni moja na laki sita mkononi. Nikasema imetosha.

Nikawasha gari na kuelekea club/baa maarufu ya Vibe au kama watoto wa Morogoro wenyewe wanavyoiita, Viber! ambayo ipo pembezoni mwa Dodoma road ukiwa unaelekea kihonda. Nikaanza matanuzi “ya kufa mtu”. Kila aliyekuwemo ndani ya baa nilimnunulia kinywaji chochote alichokuwa anahitaji. Uzuri ilikuwa ni mida ya saa kumi hivi hivyo club haikuwa na watu wengi. Wengi walikuwa wanakula chakula wakishushia taratibu na vinywaji. Baada ya kumnunulia kila aliyekuwemo ndani ya club mda mchache ghafla Malaya karibia sita wakaja kukaa pamoja na mimi mezani. Mmoja akaja kuninong’oneza sikioni kwa sauti ya kimahaba ya ‘kufoji’, “twende ndani VIP”.. Nikajitoa akili nikamjibu kwa sauti ya juu, “hapa hapa kummaeeee, mwaga radhi unyeshewe na mvua ya hela, DJ ongeza sautiiiii kumameeee”

Haya matanuzi yote na kujitoa ufahamu niliyafanya makusudi ili kujenga saikolojia na mazingira fulani kwa ajili ya kitu kitakachofuata.

Kama nusu saa baadae, kwa mbali barabarani nikaona difenda ya polisi imepaki na wakashuka maaskari wanne walivalia kiraia wakiwa wameongozana na Hasnat pamoja na Issack.

“Ni huyu hapa” Hasnat akapiga kelele huku anaanza kulia walipoingia ndani ya club.

Moja ya wale maaskari ambaye alikuwa ‘mbavu’ kweli kweli akajakuninyanyua kwa nguvu kwa kunishika mkononi. Mimi sio mwembamba sana na wala sio mnene, nina mwili wa kawaida na umejengeka kiasi chake kutokana na utamaduni wa kukimbia na ‘push ups’ kila asubuhi lakini kwa jinsi yule askari alivyoninyanyua ilikuwa kana kwamba ananyanyua karatasi.

“Watoto wa siku hizi mmekuwa waseng* waseng* sana, yani unamuibia demu wako ili uje utumie na Malaya” akafoka yule askari huku wananitoa nje.

Tulipofika nje wakachukua funguo zangu za gari na askari mmoja akaanza kuipekua gari yangu. Baada ya muda akatoka.

“Kila kitu alichoibiwa huyo dada kipo humu, simu, mkoba, walet, kadi za benki na kuna pesa taslimu milioni moja na laki nbili” akaongea yule askari.

Kisha Askari mmoja akakaa upande wa dereva kwenye gari yangu, hasnat akakaa siti ya mbele na mimi, Issack na askari mwingine tukakaa siti za nyuma kisha safari ya kuelekea Central ikaanza huku ile difenda inatufuata nyuma yetu.

Ndipo sasa tuko hapa kituoni nikiwa nimeshamaliza kuandika maelezo.

“Ray ungenambia hata kidogo hicho ulichokipanga kichwani mwako ingenisaidia walau na mimi nisiwe gizani” akaongea Wakili wangu Hemedi Bantu.

“Usijali kaka, nitakueleza muda muafaka ukifika wewe hakikisha tu kesho napelekwa mahakamani” nikamjibu kwa kifupi.

Mara Sajenti James Bidebu ambaye alikuwa ametoka kidogo akarejea.

“Naona maPP wote wameshaondoka nyumbani si unajua muda wa kazi umepita, ila nitajitahidj kesho asubuhi mapema wakifika tu niwape faili waandike mashtaka na kesho hiyo hiyo mteja wako apelekwe mahakamani” akaongea Sajenti James Bidebu huku anaakaa kwenye kiti mbele yetu na kuweka faili la kesi yangu juu ya meza.

“Nitashukuru sana, naomba tuende kwa kuheshimu Sheria, mnapaswa kumfikisha mahakamani mteja wangu ndani ya masaa ishirini na nne sitegemei mniletee zile drama zenu” Hemedi Bantu akaongea akiwa amerelax kabisa nikahisi wameshawahi kukumbana na huyu askari kwenye kesi nyingine tofauti na hii.

“OK, sasa hebu fanya mpango niweke vocha niwasisitize kesho wawahi mapema kesi iende mahakamani” Sajenti James Bidebu akaongea huku anatabasamu kwa uroho.

“Hahaha ushaanza mambo yako” wakili wangu akatoa kicheko kidogo kisha akaingiza mkono kwenye mfuko wa suruali wa nyuma akatoa wallet na kuchomoa noti mbili za elfu kumi kumi akampatia Sajenti Bidebu.

“Kwahiyo dogo ana lala lock up??” Sajenti bidebu akauliza huku anakunja zike noti na kuweka kwenye mfuko wa shati.

“Yap! Analala lock up” Wakili Bantu akamjibu kwa kifupi tu.

“Daaaahh aisee! Nina miaka kumi na mbili sijawahi kukutana na mshtakiwa anakataa dhamana hii ni mara yangu ya kwanza” akaongea Sajenti Bidebu huku ananitazama.

“Well, kutokana na kilichotokea mteja wangu anaamini hayuko Salama akiwa huko nje! Kwa hiyo ni bora usiku wa leo akalala hapa kwenu” akaongea Wakili Bantu huku anatabasamu.

“Ok! Twendeni basi mida ishaenda sana nataka niondoke nyumbani” akaongea Sajenti huku ananyanyuka.

Tukashuka ngazi kutoka ghorofa ya pili mpaka ground floor. Kisha tukanyoosha na korido moja kwa moja tukizipita ofisi zilizokuwa nyingi zimeshafungwa tayari na chache zikiwa wazi na maaskari walikuwa wanamalizia kazi zao kabla ya kuondoka.

Mwisho mwa korido mkono wa kushoto kuna reception/kaunta ya kipolisi na mkono wa kulia kwa mbele kidogo kuna geti la nondo linaloekekea kwenye vyumba vya lockup.

Issack na Cheupe walikuwa wamekaa kwenye benchi pembeni. Hasnat alikuwa amevaa top na suruali ya kumbana na alikuwa amejifunga khanga kwa juu. Issack kama kawaida yake alikuwa amevalia sweta na suruali ya jinzi.

Tulipokutanisha macho tu na Hasnat akainama kuuficha uso wake kwenye mapaja! Alikuwa analia kimya kimya. Nikasikia uchungu sana moyoni, nikatamani nimkimbilie na kumkumbatia. Issack akanikodolea macho tu akionekana haamini kile kinachotokea.

“Mahabusu mpya” Sajenti akaongea akimwambia askari wa kike kabinti kadogo hivi ambacho nahisi labda nimekazidi hata miaka miwili. Mwenzake mwingine askari wa kiume akamsogezea Sajenti daftari fulani hivi kubwa kubwa. Sajenti akandika andika kwa takribani dakika nzima kisha akawa amemaliza akamrudishia yule askari daftari.

“Haya dogo twende” akaongea yule askari mwingine wa kiume huku anachukua lundo la funguo zilizoning’inizwa kwenye ‘key holder’ kama bangili hivi.

“Subiri kidogo nitete na mteja wangu” Wakili Bantu akaongea huku amemnyooshea mkono ishara ya ‘stop’ yuke aaskari mwenye mifunguo ‘ya kutisha’.

“Kesho mahakamanu umejiandaaje? Wadhamini unao au nikatafute?” Wakili Bantu akaninong’oneza.

“Sina wadhamini na naomba usitafute?” Nikamjibu kwa sauti ya chini huku nikimwangalia kwa macho serious.

“What the fu*k man, what’s going on here?” Bantu akaniukiza huku ‘amemaindi’.

“Don’t worry man, we will talk about it!” Nikamjibu kwa kifupi tu. Uzuri wa Hemedi Bantu licha ya kuwa Wakili wangu lakini pia alikuwa mshkaji, na alikuwa ni kijana tu amenizidi kama miaka sita pekee.

“Ok! Poa, all the best man!” Akaongea Bantu huku anamruhusu yule askari anichukue.

Nikageuka alipokaa cheupe na Issack. Cheupe wangu alikuwa ananiangalia kwa macho ya huruma na kuogopa.

Nikampa ishara yetu. Ishara Ambayo huwa tunaitumia mimi na yeye tu kuelezana hisia zetu.

Nikakunja ngumi kisha nikakunjua kidole cha pili (kidole cha shahada/index finger), kisha nikakunjua kidole cha kati, kisha nikakunjua kidole cha pete.

Na yeye akafanya hivyo hivyo na akashindwa kuzuia hisia zake, akajiinamia mapajani na kuanza kulia tena.

Ingawa ulikuwa wakati wa huzuni kubwa na hatari, lakini baada ya kupeana ishara ile nilijisikia kujiamini na ujasiri.

Ishara hii ya kukunja ngumi na kukunjua kidole kimoja kimoja tulimaanisha; ukikunjua kidole cha shahada kiliwakilisha herufi “I”, na kidole kinachofuata kilIwakilisha “love”, na kidole cha pete kiliwakilisha “you”. Kwahiyo ukikunja ngumi na kuanza kukunjua kidole kimoja kimoja kwa mtiririko, tulikuwa tunaambiana “I LOVE YOU”.

Yule askari akanichukua na tukaelekea kule mbele upande wa kulia kwenye geti la nondo. Akafungua geti tukaingi.

Kulikuwa na korido ndefu yenye vyumba kila upande, huku na huku. Vyumba vyote vilikuwa vina milango ya geti za nondo ambayo inafanana kabisa na milango ya nondo ya magereza ambayo huwa tunaona kwenye televisheni. Zinakuwa ni nondo tu zimepita toka juu mpaka chini.

Jumla kulikuwa na vyumba sita. Vitatu kushoto na vitatu kulia na vyote juu vilikuwa na namba. Zilisomeka “MEN CELL 1”, “MEN CELL 2”, “MEN CELL 3” ……… na kuendelea mpka namba sita. Mbele mwishoni mwa korido kulikuwa na geti lingine la nondo na kwa ndani nikaona vyumba viwili vimeandika “WOMEN CELL 1” na “WOMEN CELL 2”.

Ajabu ni kwamba wakati tunaingia watu walikuwa wanaongea kwa sauti ya chini tu kawaida, ila tulipoingia tu wakalipuka na na kuanza kuongea kwa sauti za juu kama wanashindana, “Afandeee…. Afandeeee…. Afande Fanya mpango wa fegi…… Afande ndugu yangu hajaja?…… Afande kuna boya anazingua humu…….. Afandeeeee…… Afandeeee……” Kila mtu alikuwa anapiga kelele anaongea lake.

Inaonekana askari mwenyewe alikuwa ashazoea hii hali, kwani hata hakujisumbua kuwasikiliza wala kutilia maanani alichokuwa anafanya alikuwa anachungulia selo moja baada ya nyingine. Nahisi alikuwa anaangalia ipi ambayo haijajaa sana aniweke humo.

Kisha nikamuona anafungua selo ambayo iko karibu na mlangoni juu imeandikwa “MEN CELL 2”.

“Ingia” akaniamuru baada ya kumaliza kufungua mlango wake wa nondo.

Nikaingia, akafunga lile geti la nondo kisha nikamsikia anafunga lile geti kubwa la nondo na akaondoka.

Mara tu baada ya yule askari kuondoka, kelele zile zikapoa na watu wakaendelea kuongea kwa sauti ya kawaida.

“Mambo vipi…. Niaje Mkuu.. Mambo… Niaje… Mambo vipi” nikaanza kuwasalimia ‘wenyeji’ wangu niliowakuta mle mmoja baada ya mwingine.

Niliwahesabu wahesabu haraka haraka, selo ilikuwa na watu kumi na mbili. Selo haikuwa kubwa sana lakini nilishukuru haikuwa ndogo kiwango kile nilichokuwa nafikiria nitaikuta. Ilikuwa na ukubwa wa kama chumba kimoja na nusu kwa ukubwa wa vyumba vyetu vya uswahilini. Lakini hiyo nusu imetengwa kidogo na ukuta uliojengwa nusu na kutengeneza kama kijichumba hivi ambacho kilikuwa ni choo. Uzuri wa hiki choo nilipokuja kukifumia baadae hakikuwa kile cha kujisaidia kwenye ndoo (mtondoo) kama nilivyokuwa nimejenga picha kutokana na stori za mtaani lakini pia nilishukuru kwa kuwa hapa ni Central Police kwasababu kama ningepelekwa kituo kidogo lazima ningekumbana na kisanga cha kujisaidia kwenye mtondoo.

Choo hapa kilikuwa na sink (sio sink la kukaa, ni lile ‘sink’ kuchuchumaa alafu unamwaga maji na ndoo).

Pia selo ilikuwa na kidirisha kidogo kabisa ambacho naaminj walikiweka kwasababu ya kupitisha hewa na sio mwanga. Kidirisha kilikuwa kidogo kiasi kwamba hata ukifanikiwa kutoa nondo walizoziweka kikabaki kidirisha chenyewe huwezi kupita kutokana na udogo wake.

Pia kulikuwa na mabenchi ya zege yaliyojengwa kuunganishwa kwenye ukuta ambayo hawa wenyeji wangu walikuwa wamekaa wanapiga stori.

Ila nilipoingia na kuwasalimia mmoja mmoja wote wakakaa kimya, wengine wakaitikia na wengine wakakaa kimya tu.

Nikatafuta sehemu kwenye banchi ya mkono wa kushoto nikakaa. Wote bado walikuwa wananiangalia mimi. Mbele yangu benchi ya mkono wa kulia alikuwa amekaa ‘dogo’ ambaye kwa kumkadiria alikuwa hazidi mika 25. Inaonekana alikuwa anasubiri nikae nitulie aanze kuniongelesha.

“Niaje mani?” Akaniuliza baada ya kuona nimetulia. Watu wote walikuwa kimya wanatusikiliza.

“Poa poa! Ishu vipi?” Nikamuitikia

“Fresh tu mwanangu! Karibu sana jisikie upo nyumbani”

Watu wote wakaanza kucheka. Dogo mwenyewe naye akaanza kutabasamu.

“Vipi una msala gani mwenzetu?” Akaniuliza yule dogo.

“Aaaahh.. Aaahh” nikawa najitahidi kutafuta sentensi nzuri, “aaaahh kuna mwanamke ananisingizia eti……” Kabla sijamaliza akanikatiza.

“Usijali mwanangu hata sisi wote tumesingiziwa, mpaka hao wengine kwenye hizo selo huko wote nao wamesingiziwa! Daaaahh hawa raia wanasingizia sana siku hizi” akaongea ‘kikomedi komedi’ watu wakaanza kucheka tena.

Ila nikamuelewa alichokuwa anajaribu kunambia. Alikuwa anataka niache kujifanya mtakatifu niwaambie ukweli tu kwasababu hata wao pia ni wahalifu, kwahiyo hakuna haja ya kujishtukia.

“Hahaha! Ok, aaaahh kuna malaya nimenpiga hela” nikaongea kwa lugha ya kihuni ila moyo uliuma kwa mbali niliposema ‘malaya’, kwasababu huyo malaya ninayemsema ni Cheupe wangu.

“Duh! Kama shi ngapi hivi” kauliza kwa udadisi.

“Kidogo tu! M mbili kasoro”

Nikasikia watu kadhaa wametoa miluzi ya ‘appreciation’.

“Daaaaaahh! Mwana wewe ni nyok*, ko huyo malaya ni demu wako unamaanisha si ndio?” Akauliza tena yule dogo.

ITAENDELEA

Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034 Sehemu ya Pili

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment