Play Gal (Tina Zoa Zoa) Sehemu ya Nne
CHOMBEZO

Ep 04: Play Gal (Tina Zoa Zoa)

SIMULIZI Play Gal (Tina Zoa Zoa)
Play Gal (Tina Zoa Zoa) Sehemu ya Nne

IMEANDIKWA NA : ANDREW CARLOS

*********************************************************************************

Chombezo: Play Gal (Tina Zoa Zoa)

Sehemu ya Nne (4)

Kadri macho yalivyokuwa yanamtoka huyu mke wa Steve ndivyo mwili wangu ulizidi kunisisimka na kunyong’onyea, nilijijaza nguvu za kishujaa nakutoa mkono wangu taaratibu nakuusogeza mpaka shingoni mwake kisha nikamkaba kwa nguvu zangu zote. Macho yake yaliendelea kumbadilika na kwa sasa nilijihisi mikono yangu kama inazidi kuwa laini huku nikihisi kama shingo yake inakuwa kama tope tope. “..Mamaaaa…!! Mamaaaa…!!!” Uzalendo ulinishinda nakujikuta nikitoa sauti ya juu huku ule mwili wa yule mwanamke ukizidi kupukutika nakuwa kama tope tope, ikafika kipindi nikashuhudia mwili wake wote ukimung’unyika mpaka akayeyuka kabisa. Nguvu sikuwa nazo tena zaidi yakuendelea kukaa pale pale chini huku nikitumia mikono yangu kujikokotea mpaka sebuleni kisha nikapumzika. “..amkaaa…?, amkaaa kumekucha..” Ilikuwa ni sauti ya Steve akiwa kavalia bukta yakehuku mkononi akiwa kashikilia mswaki. “..kumekucha, amka ukapige hata mswaki ili unywe chai..” Aliendelea kuongea Steve nakunifanya niendelee kumshangaa tu huku nisiamini yale yote yalionitokea usiku. “…Steve, wifi yuko wapi…?” Nilimuuliza kwa makusudi ili nijue kilichotendeka usiku ule alikuwa ni yeye au nani? “..Yupo jikoni anapika chai, akimaliza ataleta hapa sebuleni utamuona tu, kwani vipi ulkuwa unamuhitaji..?” “..Hapana, nimemuulizia tu kwa maana sijamuona..” Nilizuga nakuchukuwa mswaki kisha nikatoka mpaka nje kwenda kupiga mswaki na nilipomaliza nilijirudia zangu mpaka ndani ambapo tulikunywa chai kisha Steve akaniambia kuwa anaenda kuomba ruhusa kazini kwake hivyo niwe tayari atarudi kunichukuwa. Furaha na amani ya ajabu iliendelea kunitawala ndani ya moyo wangu japokuwa Steve alipoondoka tu ile amani ikatoweka tena ghafla. “..Usiku ulikuwa unataka kufanyaje Malaya wewe..?” Aliongea mke wa Steve nakunifanya niingiwe na uwoga huku mwili wangu ukianza kunisisimka. “..Si naongea na wewe..? Mimi nilijua tu utakuwa mchawi kweli na nimethibitisha ilo usiku Malaya mkubwa wewe tena Yule wa waume wa watu, na umekutana na kisiki hapa nimechanjiwa toka kwetu Kigoma Malaya mkubwa wewe..?” Aliendelea kuniambia maneno ya ukali yule Mama na muda wote sikuongea hata neno zaidi ya kumtizama tu machoni mwake, Alivyoona nazidi kuwa kimya akanisogelea mpaka karibu nilipokuwa nimeketi nakunishika shingoni mwangu, hisia kali nilizipata nakufananisha tukio kama lile la usiku wake alionifanyia. Sikutaka kuonekana dhaifu tena hata kidogo kwani tayari nilishaigundua dhamira yake hivyo nilifanikiwa kuvuta kistuli kilichokuwa karibu yangu pale sebuleni kisha nikamvaa nacho mpaka kichwani mwake akadondoka chini nakupoteza fahamu hapo hapo.

“..huwezi kushindana na mtoto wa mjini..” Nilijisemea kimoyo moyo huku nikimtolea fyonyo la dharau nakuingia mpaka chumbani kwake, nilikagua kagua mpaka nikafanikiwa kuipata pochi yake ambapo nilitoa kiasi kidogo cha pesa kama shilingi elfu ishirini, nikachukuwa nguo zake kwenye kabati lake la nguo nakuvaa. Ndani ya muda mchache tayari nilikuwa nipo nje natafuta njia ya kuelekea kufika mpaka pale kituo cha polisi kwa ajili ya kuonana na Steve. Kumbukumbu za kufika pale kutuo cha polisi sikuwanazo zaidi ya kukodi bajaji kisha ikanipeleka mpaka makaburini pale nilipofumaniwa jana yake asubuhi na nilipofika maeneo ya pale ilikuwa ni rahisi kupakumbuka kituo cha polisi kwani hakikuwa mbali na mitaa ile ya makaburini. “… Za sa hizi jamani…!! Samahanini namuulizia Steve sijui nimemkuta..?” “.. Ahaa mkuu Steve, yupo msubiri hapo pembeni..” Aliongea Polisi mmoja aliyekuwa zamu ambapo hata jana sikumuona na ndio maana hata hana kumbukumbu na mimi. Nilisubiri kidogo tu na punde Steve alitoka ndani ya kile kituo mpaka eneo nililopo. “..OOoooh, Asia umekuja, mbona nilikuahidi nitakuja kukuchukuwa nyumbani huko huko…” “..Hapana, nimeona kama nachelewa na mimi kukaa huku kwenu Bagamoyo naogopa sana yasije yakanitokea kama ya jana..” “..Acha imani potofu bwana, hii siyo Bagamoyo ya wachawi wala wanga kuwa na imani tu, utaishi vizuri na kwa furaha tu, ennheee niambie vipi mke wangu umemuacha au katoka huko..?” “.. Mkeo ameniacha hapo mtaa wa juu, kwani alinisindikiza mpaka mitaa ilee, na hata nguo za kubadilisha alinipa yeye tena asubuhi ulivyoondoka, nimempenda sana anajua kuishi na watu na anaonekana ana huruma..?” “..Ni kweli, mke wangu ni mkarimu sana kwa wageni, anajua matatizo na shida za watu, naishi naye vizuri sana tangu nimemuooa..” Niliguna kimya kimya huku nikimtolea Jicho la kujificha Steve kisha nikauchukuwa mkono yangu nakuikutanisha mikono yangu na yake bila woga wowote. “..Sasa Steve? Si umeshaomba ruksa, nakuomba unirudishe basi Dar es salaam..?” “..Hilo tu usijari, ila embu ngoja nimeshasahau kitu ndani mara moja..” Steve alirudi tena mpaka ndani ya ofisi, ndani ya muda mfupi akarudi na bahasha mkononi. “..Sasa inatubidi turudi tena mpaka nyumbani kwani mke wangu sijamuaga na pia kuna hela natakiwa nimpelekee ili aende kununua vitu sokoni kwani aliniambia kuwa vitu vimeisha..” Nilionesha kukataa lakini Steve hakukubaliana na mimi kabisa hivyo nilipanda tena gari yake nakisha safari ya kurudi nyumbani kwa Steve ikaanza tena. Njia nzima nilitetemeka mithili ya mtu ambaye hajawahi kuoga maji ya baridi na yupo sehemu ya baridi. Niliogopa sana endapo Steve akijua mchezo nilioufanya kwa mke wake. Kadri tuliyokuwa tunaenda ndivyo na mimi mapigo yangu yamoyo yalivyokuwa yakinibadilika na kwenda kasi mno. Hatimaye ndani ya kama dakika kumi tukawa tumeshafika nje kwa Steve, tulijikuta wote mimi na Steve tukitoa macho kwa mshangao tulipofika tu nje ya nyumba yake kwani tulikutana na umati mdogo wakinamama huku kila mmoja akiwa amejifunika khanga na kwa mbaali tulisikia vilio kuashiria kuwa kuna msiba. “..Ulivyoondoka ulikuacha salama huku..?” Alinigeukia Steve nakuniuliza kwa ukali huku amenitolea macho na akitafuta kitu mifukoni mwake.. “..Hao wakinamama ndio nawaona sasa hivi lakini.. Nikiwa bado namuelezea Steve kabla sijamalizia kuongea mara ghafla simu ya Steve ikaita..” “..Mkuu uko wapi…?” “..Ndio naingia kwangu lakini kidogo nahisi hali si nzuri kwani vipi..?” “..Ni kweli na kabla hujafika ni kwamba kuna binti amonekana hapo kwako ametoka kwa haraka sana na inasemekana anahusika na kifo cha mkeo kwani mashuhuda wamemuona akitoka huku amechanganyikiwa na hali tuliyomkuta nayo marehemu mkeo ni kapigwa na stuli eneo la nyuma ya kichwa nakusababisha umauti wake…” Steve alinigeukia huku akitoa machozi na mishipa ya shingoni mwake ikimtoka vilivyo, alitoa pingu nakunifunga mkono mmoja na mwingine akanifunga kwenye msteringi wa gari yake kisha akatoka nakufunga vioo vyote vilivyokuwa na tinted kisha akaloki milango yote akaelekea ndani kwake huku akiniacha peke yangu ndani ya gari.. Bado nilikuwa sijielewi elewi pale ndani ya lile gari, nilijaribu kuangalia huku na kule lakini haikusaidia kitu, kila nikilipenyeza jicho langu kupitia kioo cha mbele ya gari ndivyo hasira nazo zilikuwa zikinijaa. “..Najuta kuja huku Bagamoyo na sitorudia tena eeeh! Mungu niponye tu…” Nilibaki naongea peke yangu huku nikijihisi koo langu limeshikwa na kwikwi na siyo kwikwi ya hasira tu bali kwikwi ya hasira kali niliyokuwa nayo, kwa sasa macho yangu nilijihisi kama yanatoa machozi tena yale machozi ya hasira kila nikiona umati wa wakinamama na wakina baba ukiongozana kuingia mpaka ndani na wengine wakipishana kwa kutoka nje. Ndani ya muda mchache tayari nilishuhudia Steve akiongozana na wenzake kuubeba mwili wa marehemu nakuupeleka mpaka kwenye gari lilokuwa pembeni yangu. Akili ilianza kunichemka huku nikiangalia huku na huku ndani ya gari japo kuambulia chochote niweze kujinusuru katika hatari niliyokuwanayo. Ndani ya muda mchache nilifanikiwa kugundua funguo zikiwa mchanganyio na hata muonekano wake ulionesha wazi hazikuwa funguo za nyumba bali zilikuwa ni funguo kama za pingu japo sikuzijua sana, nilizichukua nakuanza kuzijaribisha moja baada ya nyingine bila ya mafanikio yoyote. Nikiwa bado nashangaa shangaa kuzikagua zile funguo mara nikahisi mtu anagonga kwenye dirisha la kioo. “..nani..? nani…?” Niliongea kwa sauti bila kusikia chochote, nilijijaza moyo wa kijasiri nakuendelea kuzitafuta funguo za kuweza kufungua pingu ambazo zilikuwa zimeshikamana na msteringi wa gari hili la Steve. Nilijitahidi kuzifungua kwa kutumia mdomo waangu na meno huku nikifungua kwa nguvu zote. Sikuweza kufanikiwa kufungua lakini halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi fasta nakuamua nijiweke vizuri nakuliwasha gari kwa kutumia waya kama wafanyavyo wezi wa magari. Ndani ya muda mchache niliweza kuliwasha gari hivyo nikalirudisha nyuma nakuondoka kimya kimya huku nikiamini kwa asilimia zote Steve atakuja kugundua baadaye sana ambapo tayari nitakuwa nimeshafika mbali. Kuwepo kwa barabara nyingi na kona kona za hapa na pale ndicho kilichonisababisha nisielewe njia ya kutokea kuelekea Dar es salaam. Sikutaka hata kufungua vioo zaidi ya kuongoza hivyo hivyo tena nikiwa nimejibana bana mapaja yangu na msteringi nimeukumbatia huku nikitoka kwa mwendo wa kawaida tu. Sikuweza kufika mbali sana kutokana na kuchoka kwanza kwa pingu nilizokuwa nazo na pili sikuielewa haswa barabara ya kuelekea Dar es salaam. Niliisimamisha gari baada ya kutembe kwa mwendo kidogo kutoka lile eneo ambalo alikuwa akiishi Steve na kwa sasa nilikuwa eneo wanaloziba pancha na kutengeneza magari mabovu, pale pale nikafungua mlango nakumuita kijana mmoja. “..Mambo vipi…?” “..Poa tu Sister vipi pancha nini…?” “..Hapana, unaniona hapa mkononi, haya fanya ufanyavyo unitoe hizi pingu sasa hivi na kuhusu pesa wala hata usijali” “..Kwa hilo tu Sister!, wala usihofu tena nafanya mwenyewe, vipi utanipa shilingi elfu kumi na tano..?” “..kuhusu pesa ondoa shaka..” Yule kijana hakutaka kabisa kuchelewa zaidi ya kutoka mbio pale nakurudi na spana mbali mbali ikiwa ni pamoja na msumeno mkubwa. Zoezi la kama dakika tanotu lilikuwa tosha kwa huyu kijana kunitoa pingu ambazo zilishikana na msteringi wa gari. Amani kubwa iliyoambatana na furaha ya ajabu ilianza kuninyemelea ndani na nje ya mwili wangu nakutamani sana nifike Dar kwa muda mfupi. Nilitoa ile pochi ambayo niliichukuwa kwa mke wa Steve nakutoa noti mbili za shilingi elfu kumi kumi nakumpatia Yule kijana kisha akanirudishia chenchi nakuondoka zangu huku nikijidai kuulizia duka maeneo ya pale. Vichochoro viwili vitatu vilinitosha kabisa kutoroka na kulitelekeza gari la Steve huku nikiulizia sehemu ambayo ninaweza japo kupata usafiri wa daladala au hata bajaji.

“..Mpaka stendi shiingi ngapi..?” “..Utanipa buku mbili tu..” Nilichukuwa pikipiki kisha nikampatia hela ya kunifikisha mpaka Dar es salaam kabisa kwani niliamini endapo nitachukuwa daladala itakuwa rahisi sana kushikwa na Steve au mapolisi wenzake. Piki piki ilikuwa iko spidi sana, dereva hakutaka hata kidogo kuchelewa , upepo mkali uliokuwa ukinipuliza njiani, hatimaye tukafika maeneo ya bunju ambapo kwa bahati mbaya pikipiki ikaanza kutoa mlio wa ajabu kuashiria kuwa kuna itilafu ndani yake. Nilimpatia pesa yake lakini alioneka kuchukizwa na mimi kumpatia hela . Sikumuelewa hata kidogo anachomaanisha hadi alipovua kofia na miwani ndipo na mimi nikamgundua. “…waaat, ooohh kumbe ni weweeeeee, noooo…! Noooo…! Noooo…?” “Masikini nimekwisha Tina mimi…!” Niliropoka kwa sauti ya juu baada ya kumgundua yule mtu kuwa alikuwa ni yule mzee alionifanya mpaka nikajikuta nimeamkia makaburini tena uchi wa mnyama kabisa na kwa muda huu kumbe alikuw ni dereva pikipiki na alionesha kuchukizwa baada ya kumlipa pesa yake. “..Ulinitoroka na leo ndioleo na unabahati nilikuwa nakupeleka mpaka kwa wakuu wa mizimu kwa babu zangu Tegeta shetani mkubwa tena malaya usiye na hila wewe” Aliendelea kufoka Yule kijana nakunishika mkono huku akiiacha pikipiki yake nakuniburuta nilijitahidi japo kugoma lakini nilipata makofi na ngumi huku akiniburuta kwa nguvu zake zote tena eneo ambalo hata sikulijua. Kadri alivyokuwa akinivuta ndivyo na mimi nikaanza kupata nguvu za ajabu huku nikijihisi lile eneo la usoni ambalo nilichanjwa kipindi kilee likiniuma sana. “..Hunijui..? leo ndio utanijua vizuri..” Nilijikuta naropoka tena kwa ujasiri wa hali ya juu. Sasa nilishindwa kuelewa kuwa ni nguvu za kichawi alizokwa nazo huyu mzee au la kwani hali ya hewa ilibadilika ghafla kiasi kwamba nikaanza kunyeshewa na mvua tena ile mvua ya mawe, niliendelea kuvutana na Yule mzee japo sikupata msaada wowote kwani sikuweza kumuona mtu yeyote zaidi ya kuwa sisi wawili tu tukisumbuana. “..Sema mwenyewe..?, unataka tukuue au ujiunge na kundi letu..?” “..niacheni jamani.., mie sitaki choc…” Kabla sijamalizia tu kuongea nilishangaa napokea bonge la kibao kutoka kwa mtu ambaye sikumuona lakini sauti tu za watu wengi ndizo nilizisikia zikinihoji. Mwili wangu kwa sasa ulikuwa kama sugu kwani hata yale maumivu sikuyasikia zaidi ya kuhisi tu nimepigwa na mtu nisiyemuona. Maumivu ya kichwa yaliochanganyikana na uchovu huku upepo ukivuma sana nakujikunyata kwa kuhisi baridi kali. Kila nikiendelea kutoa macho nakuliangalia hili eneo bado nilikuwa sipajui ni sehemu gani japo palikuwa ni kama jangwa kumbwa lililojaa michanga tupu, akili yangu yote ilikuwa imenivurugika na kusababisha kumbukumbu zote kunipotea. “..hapa ni wapi..? Nirudisheni kwetu.., Baba yangu yuko wapi..?” Niliuliza kwa sauti ya ukali huku nikimfuata Bibi mmoja aliyekuwa pembeni yangu na kwa muda huu alionesha kuwa yuko ‘busy’ sana, alikuwa peke yake tu, nilimsogelea mpaka karibu na kwa hasira nilizokuwa nazo ukichangia na kutokujitambua vizuri, nilimshika kitenge chake alichokuwa amekivaa nakukivuta kwa nguvu mpaka nikahakikisha amebaki uchi wa mnyama. “..nani aliyenileta huku..? si nakuuliza wewe kibibi..?” Alinitolea macho tu bila kunijibu chochote. “..sasa leo mie nataka mnirudishe kwa wazazi wangu, wapumbavu sana nyie..?” Nilijikuta nachota mchanga kwa hasira huku nikimwagia nao Yule Bibi na mwingine nikimlisha mdomoni, kadri nilivyokuwa nikimtesa huyu Bibi ili japo anioneshe kwa wazazi wangu ndivyo alikuwa akibadilika nakuwa kama ule mchanga niliokuwa nikimwagia. Maskini Tina mimi, nguvu zilianza kunilegea na ule woga ukaanza kunitanda tena katika lile eneo, mara nikahisi kama kuna umati wa watu umetanda japo sikuwaona lakini sauti za watu wakicheka na kujibizana ambao sikuweza kuwaona ndizo zilikuwa zikichochea hisia zangu kwa haraka zaidi. KESHO YAKE ASUBUHI “…Tinaaaa…? Tinaaaa weweeee…? Enheee vipi..? Umekuja saa ngapi shosti..?” Bado nilitoa macho huku na kule huku nisielewe elewe kabisa nimefikaje fikaje hapa chuoni CBE, marafiki zangu walitanda kunishangaa kitandani mwangu wakiongozwa na rafiki yangu kipenzi Aisha. “..Shosti kwani vipi ulifiwa nini..? Pole na umekuja saa ngapi..?” “..Hapana mbona wala hata sikufiwa jamani kwani vipi..?” “..Shosti yani na lijiupara lote hilo bado unatudanganya..? Pole bwana, kwani umefiwa na mzazi yupi..?” Niliona kama wananizungua, niliamka pale kitandani mpaka kwenye kabati langu la vipodozi ambapo kuna kioo kikubwa nikajiangalia. Mchozi ulianza kunidondoka taratibu baada yakujigundua nimenyolewa upara huku uso wangu ukiwa na chanjo chanjo kama kabila lile la wamakonde kutoka Mtwara. Niliumia sana moyoni nabado nilikuwa sina kumbukumbu za kutosha ilikuwaje kuwaje zaidi ya kukumbuka tu nilienda Bagamoyo na huko nilifanikiwa kumuona Steve halafu akanipa hadi nauli nikarudi zangu Dar.. “..nani aliyenichanja…?, nauliza nyie, nani humu bwenini amenifanyia hivi..?” Niliwageukiwa marafiki zangu pale bwenini nakuwauliza kwa hasira zote nakuwafanya waanze kuniogopa tena siyo kwa ukali tu bali kwa sura yangu ilivyokuwa inatisha. “..kuna niliyemchukulia bwana wake humu ndani…? kwanini mnifanyie hivi..? Aisha rafiki yangu nani aliyenifanyia mchezo huu, heee..? Na kwanini mimi tu jamani mnanifanyia hivi.., nimewafanya nini jamani.., au kwakuwa siingiagi darasani mara kwa mara eeenh..?” Niliongea kwa jazba huku nikibubujikwa na machozi, kadri nilivyokuwa nikiongea ndivyo na umati wa wanafunzi wenzangu kutoka mabweni mengine ulikuwa ukijaa ndani ya chumba chetu kuja kunishangaa, hasira zilinizidia zaidi ya pale mpaka nikajikuta nachukuwa nguo zangu kabatini na nyingine nikizitoa kwenye begi pamoja na viatu vyangu vyote huku nakuzikusanya pamoja nakutoka mpaka nje, nikarudi tena mpaka bwenini tena nakukukusanya vipodozi vyangu vyote pamoja na kiberiti nakutoka navyo mpaka nje, nakuanza kuvichoma moto kwa hasira kali niliokuwa nayo. “..Tinaaa, Tinaa rafiki yetu umekuwaje lakini..?” “..Niacheni, si ndiyo mlivyotaka mfurahi haya furahini sasa..?, furahini na mpige na vigele gele kabisa..?” Walinifuata marafiki zangu mpaka nje nakunizuia lakini haikusaidia chochote zaidi ya ule moto kuongezeka kasi huku vipodozi vyangu vikiendelea kuharibika. Niliuacha ule moto ukiendelea kuwaka pale nakutoka mpaka dukani ambapo nilinunua viwembe kama viwili nakurudi tena mpaka bwenini, sikujali makelele ya wanaume wa hapa chuo tena wale waliokuwa wananifuata nyuma nyuma nakunicheka huku wengine wakinizomea. Niliongoza mpaka bwenini na nilipofika nilifungua vile viwembe nakuanza kujichanja zaidi ya nilivyoukuwa mwanzo. “..Hapana Tina usifanye hivyoo, usifanye hivyo..?” “..Embu niacheni, nyie si ndio mmeyataka haya yote nakunifanya hivi.., niacheni nijimalizie mpendwe nyinyi, acha niwe mbaya si mlinichanja niwe mbaya wacha nijiendeleze mwenyewe..?” Tayari niikuwa kama nusu chizi kwa kuchanganyikiwa, walimu wa chuo walikuja mpaka bwenini kuingilia kati swala langu, walinishika lakini nilikuwa na nguvu za ajabu sana, iliwachukuwa muda mpaka kufanikiwa kunifunga kamba mikononi.

“..mpelekeni ofisini huyu..?” Nilisikia sauti ya mwalimu mmoja akiwambia wanafunzi wa kiume wanipeleke mpaka ofisini kwake, wanafunzi walikuwa ni wengi sana wakinishangaa kwa jinsi nilivyokuwa nimebadilika ghafla nakuwa Tina kichaa, kadri walivyokuwa wananivuta nakunipeleka huko ofisini ndivyo na mimi nguvu zilikuwaa zikiniongezeka mara mbili ya pale nakujikuta niking’ata zile kamba mkononi kwa kutumia meno kisha kila mwanafunzi aliyenisogelea alikuwa akiambulia meno tu, nilikuw peku kabisa huku zile nguo nilizokuwa nimezivaa zikawa zimetapakaa damu kidogo, hilo sikulihofia nikakimbia nakuongoza bara bara yakuelekea Buguruni. Kundi kubwa la wanafunzi likichanganyikana na watu wa mitaani na walimu walikuwa nyuma yangu wakinifukuza kwa nia ya kunikamata, nilishindwa hata kujielewa nguvu za kukimbia nilipozitolea kwani nilikuwa na spidi ya hatari. Ndani ya muda mchache nilikuwa nimeshakatisha vichochoro zaidi ya kumi na kwa muda huu sikumuona hata mtu aliyeendelea kunifuatilia kwa nyuma. Nilipofika tu Buguruni nikaingia kwenye daladala ziendazo Gongo la mboto, lengo langu likiwa nikushuka pale uwanja wa ndege ili niende kwa wazazi wangu Mwanza. “..dada nauli yetu ipo wapi..?” Aliongea kondakta baada ya kunishusha uwanja wa ndege. “..unataka nauli tu..? hii hapa chukuwa..?” Nilivua nguo yangu ya ndani nakumfunulia naniii yangu kisha nikavaa nakukimbia zangu kuelekea uwanja wa ndege huu abiria wote nikiwaacha wakicheka kwenye daladala nakuondoka zao. Nilipofika tu uwanja wa ndege, sikuwa na nauli yeyote lakini nilijikuta na imani tofauti huku asilimia zote nikiamini kwa njia yeyote lazima nitapanda ndege na nitafika mpaka nyumbani kwetu Mwanza. Nikiwa bado naangaza huku na kule kuangalia abiria mara.. “..Tinaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa….?” Maskini mwili wangu wote ulininyong’onyea ghafla baada ya kumuona Jerry, na nilishajisahau kama Jerry anafanya kazi uwanja wa ndege… *Sikutaka hata kugeuka nyuma kumuangalia Jerry zaidi ya kumkimbia huku nikiitafuta barabara ya magari na nilipofika tu, uso wangu ukakutana na dala dala bila hata ya kujua ukichangia na woga niliokuwa nao nilijikuta nalivamia daladala nakuingia mpaka ndani. “…dereva simama tumshushe chizi huyu..” “..chizi mama yako?” Nilijikuta namjibu konda tena kwa kujiamini huku abiria wote wakicheka.. “..unamcheka nani wewe? Unamcheka nani..?” Nilimgeukia mzee mmoja ndani ya daladala ambaye alivalia suti huku mkononi kashikilia biblia, nilimpokonya biblia yake nakuichana vipande pande nakumfanya dereva asimamishe gari. “..embu mshusheni huyo mpumbavu, tena apelekwe kituoni tu..” Kitendo cha kusikia neno kituoni tu, nikachoropoka hapo hapo nakukimbia zangu. Njaa kali ilianza kunizidia huku jua nalo likitokomea nakunifanya niwe chizi mara mbili yake, akili yangu moja kwa moja ikanituma nielekee kwenye majalala nakuanza kuokoteza makombo yaliobakizwa na watu.. Sikulifikiria swala la kuugua magonjwa ya mlipuko zaidi ya kufakamia mifuko mbalimbali iliyokuwa na mabaki ya chipsi na mingine mavyakula hata sikuyajua lakini kwa njaa niliyokuwanayo sikuweza hata kushiba, nilitoka pale majalalani nakuongoza mpaka kwenye nyumba zilizokuwa karibu yangu. Kabla sijafika. “..oyaa wee demu unakwenda wapi..?” Alikuwa ni kijana wa kihuni na aliponiona natokea majalalani akaniufuata. Nilivuta nguo yangu vizuri na kuanza kukimbia huku nikikatiza sehemu ambazo wala sikuzijua, kadri nilivyokuwa naongeza mwendo na ndio kwanza na yule kijana naye alizidisha. “..oyaa, wee vipi? Huwezi kufukuzana mbio na kamanda wewe..” Maskini Tina mie nikawa nimeshakamatika tena katika mikono ya kijana muhuni. Nilijitahidi japo kutoa sauti lakini ikawa haitoki, hapo hapo nikatambua huenda sauti ilikatika baada ya kula mivyakula ya ajabu pale jalalani. Nikiwa bado nimezubaa nakujiuliza mwenyewe, nikashuhudia yule kijana akichomoa kisu na kunioneshea. “..hapa kimya tu, ukikukuruka nakupasua nasepa zangu…” Nilijihisi moyo wangu umepasuka, kwani mkojo ulikuwa ukinitiririka ukiambatana na jasho, sikuweza hata kukumbuka ulikuwa ni usiku wa saa ngapi kwani hata watu njiani hawakuwepo kabisa. Yule muhuni alinipeleka mpaka maeneo ambayo sikuyafahamu vizuri na nilipofika tu nilishangaa kukutana na kundi kubwa la wahuni huku wakivuta sigara na bangi na waliponiana walipiga makofi huku wengine wakipiga miluzi. “.. Mwana mtoto bomba huyu umemtoa wapi leo..?” Aliropoka muhuni mmoja huku akinifuata mkononi na sigara yake kisha akanivutisha. Nilikohoa sana kutokana na ule moshi na hapo hapo nikaanza kujihisi kizinguzungu huku miguu ikinilegea. Nilianza kuhisi kama nguo yangu ya ndani inavuliwa lakuni kutokana nakujisikia vibaya nakukosa nguvu hata uwezo wa kutambua ilinibidi niwe kimya tu. Ndani ya muda mfupi tena nikaanza kuhisi kama naingiliwa tena nyuma na mbele kwa kishindo. Maumivu makali nilianza kuyasikia kwani nilihisi kama naingiziwa mikono. Nilijihisi kukata tamaa ya kuishi kwani kwikwi ya ajabu illinishika huku jasho likinitiririka, nilianza kutapa tapa mithili ya mtu anayetaka kufa na hatimaye nikapoteza kabisa fahamu.. Baridi kali ilitetemesha mwili wangu huku nikijihisi maumivu makali kichwani mwangu ambapo bado nilikuwa na upara. Sikuweza kupata kumbukumbu hata kidogo juu ya hili eneo nililopo zaidi kujihisi damu zikinitoka sehemu zangu za siri nakusababisha kitovu kuvuta. Niliangaza huku na kule nikashuhudia kila mtu akiwa bize na mambo yake, niliinuka kwa aibu pale chini huku nikielekea kwenye genge la pembeni yangu na nilipofika tu.. “..hapa ni wapi..?” “..salimia kwanza, chizi nini wewe..” Alikuwa ni Mmama, alivyonijibisha hivyo tu wala sikutaka tena kukaa zaidi ya kusonga mbele huku nikimwacha akinishangaa.. “..vichaa wengine bwana, sijui ndio limetoroka mirembe..” Maneno yale yaliniingia kichwani na kunijaza hasira mara mbili na nilivyokuwa, nilimvamia huyu Mmama nakumkunja huku nikitumia meno yangu na kucha kuuteketeza uso na maziwa yake mpaka nikahakikisha damu damu zinamtoka huku amedondoka chini hajiwezi kabisa , nikachukuwa pesa zake zote za mauzo nikazidumbukiza kwenye matiti yangu nakuondoka. Kelele alizokuwa akipiga pale chini zilifufua umati wa watu huku wengi wao wakiwa ni wakinamama na wakinadada. Sikuijua njia vizuri lakini nilijikuta nikikatiza vichochoro mbalimbali nakutokomea. Mwili wangu wote ulikuwa umechoka, pumzi ziliniishia nakubaki nikihema juu juu, nilijilaza zangu kwenye kibaraza hata sikupajua ni wapi. “..wewe vipi hapo unafanyaje?” Alikuwa ni mzee mwenye nyumba hii hivyo sikutaka hata kumjibisha zaidi ya kuondoka taaratibu nakuonesha sura ya huruma kwa yule mzee. “..embu simama mwanangu nikwambie kitu..” Nilisita nakutaka kukimbia lakini nilijikuta napata moyo wa ajabu wa kumsubiri nakusimama huku nikiendelea kumtolea sura ya huruma.

“..unatokea wapi mwanangu..? Na unaelekea wapi..?” “..natokea kwetu na naelekea chuo..” “..mwanangu embu acha utani we niambie ukweli tu nikusaidie, kwani unaonekana unamatatizo tena makubwa..” “..yaani nimesimama nakajua utaongea vitu vya maana, unaanza ohh eti nina matatizo, ulinipa we? Ningekuwa na matatizo si ningeomba msaada kwako?” Nilimjibu vibaya mpaka mzee wa watu akabaki ananiangalia tu, nikageuka nakuondoka zangu lakini kabla sijafika mbali nilihisi navutwa gauni langu.. “..mwanangu..! Embu nakuomba japo uingie ndani ukanywe chai na pia ukamsalimie na mama yako..” Niliingiwa na moyo wa huruma nakujikuta nikimsikiliza yule mzee kisha nikaongozana naye mpaka kwake tukaingia sebuleni na tulipofika tu.. “..ngoja niende jikoni nikamwite mama yako wewe nisubiri hapo hapo sebuleni..” Nilikaa mda mrefu bila kumuona huyo mzee wala mke wake, nilijitahidi kuwa mvumilivu lakini bado hakukuwa na mtu yeyote, kwa hasira nikainuka nakuelekea mlangoni ili niondoke zangu. Kila nikifungua mlango ukawa haufunguki, niliugonga gonga lakini bado ukawa haufunguki, kwa hasira nikaelekea mpaka huko jikoni napo nilipofika tu sikumuona mtu hivyo nikaanza kumtafuta kwenye vyumba vyake ili anifungulie niondoke zangu. Ile nafungua chumba cha kwanza tu.. “…Mamaa uh uh uh, Mungu wangu..!” Maskini alikuwa yule mzee uchi kama alivyozaliwa tena akiwa amelala kitandani huku akiwa ameganda mithili ya maiti ikiwa monchwari.. Woga ulinitanda nikaanza kurudi kinyume nyume nikitaka kutoroka, kitendo cha kuukaribia mlango tu nikasikia umejifunga wenyewe kisha yule mzee bila kunisemesha akawa ananifuata huku akionesha sura ya huruma na tabasamu.. Nilihisi kama mapigo yangu ya moyo yanabadilika uelekeo, yule mzee alikuwa bado akinifuata taratibu na kwa kunyata huku akiwa uchi wa mnyama na macho yake akiyatoa sambamba na meno yake mithili ya zile sinema za kutisha.. Nikiwa katika hali ya mshangao tena ule mshangao wa kumshangaa huyu mzee, mara tena ule ule mlango wa nyuma yangu ukajifungua na safari hii ulijifungua kwa nguvu. Sikutaka tena kuchelewa zaidi ya kutoka mbio mpaka nje nakutokomea nisikokujua. **** Sikuweza kabisa kujua muda zaidi ya giza likitanda huku nje kukiwa na wapita njia wachache. Baridi kwa mbali lililokuwa likipenyeza ndani ya gauni langu huku meno yangu yakikosa kabisa nguvu kutokana na kutetemeka sana kwa mdomo, nilijihisi kichwa changu kama kimewekewa barafu na hii yote nikutokana nakuwa na upara, machozi yalianza kunilenga lenga haswa baada ya kufikiria maisha yangu yalivyobadilika kutoka Tina wazamani mpaka kuwa Tina kichaa. “..namtaka Mama yangu..? Namtaka Baba..?” Nilijikuta nainuka lile eneo nililopo ambapo palikuwa ni uchochoroni tu, nakuongoza moja kwa moja mpaka barabara kuu huku nisielewe nielekeapo, sikuwa na hata viatu wala ndala hivyo nilikuwa peku. Nilitembea mwendo mrefu bila kupishana na mtu zaidi ya magari yakinipita tu tena yale magari makubwa yakupakia mizigo. Hatimaye baada ya kutembea kamwendo kidogo na giza nikafanikiwa kuyaona malori yakiwa yamepaki eneo la uwazi. Furaha ya ajabu ikanijaa moyoni, sikutaka kujua yanapakia nini na wala yanaelekea wapi, nilichokifanya nikulivizia mojawapo nakupanda kwa nyuma bila ya wao kujua chochote. Huko ndani ya lori ilikuwa ni kero iliyochanganyika na harufu siyo harufu nzuri, ni ile harufu ya ngozi tena za ngozi wanyama, nasikujua walikuwa wanazisafirisha kwenda wapi mimi ilimradi nisafiri tu nitoke katika jiji hili la mikosi na laana lulilonipotezea malengo na maisha yangu kwa ujumla. Muda wote nilikuwa peke yangu ndani ya lile lori kwa upande wa nyuma, nilijikaza na ile harufu kwani nia yangu nikufika mkoa wowote na kama litaelekea kwetu mwanza nitafirahi zaidi. Nilijipa moyo asilimia mia huku nikiamini kabisa nitafanikiwa na safari yangu. “..hata kama halitakwenda mwanza, likinisogeza popote nitafika tu..” Nilijisemea kimoyo moyo huku nikihisi kama gari linawashwa tayari kwa kuondoka. Nilikaa kimya kwa muda mrefu huku nisielewe mwisho wa safari yangu, kutokana na uchovu niliokuwanao nilijikuta usingizi nikiupatia nafasi. ** “…lete jeki..? Lete na spana namba sita..?” Kelele kwa mbaali nilianza kuzisikia na hazikuwa kelele za wapita njia bali zilikuwa ni kelele za konda akijibizana na dereva wake, na safari hii alikuwa amefungua mlango wa nyuma ya lori huku akimulika na tochi kutafuta kitu alichoagizwa na dereva wake, kila nikijitahidi kujizuia ili nisimulikwe haikuwezekana, ndio kwanza yule konda alikuwa ananifuata eneo nililokuwa nimejificha. Nilijitahidi japo kujifunika na mangozi yale yaliokuwa yamekauka lakini haikuwezekana, nilichokifanya nikuuchukuwa mkono wangu wakulia nakuanza kuusogeza mpaka miguuni kwa yule konda. “…Mamaa..? Niache huko..?” Aliropoka yule konda kwa sauti ya chini chini. Nilichokifanya nikujionesha kwa kusimama pale huku akinimulika usoni kwa kutumia tochi yake, nikimfanyia ishara ya kumnyamazisha yani nilimwekea kidole mdomoni kisha nikamsogelea nakumkumbatia huku akiwa hajielewi elewi. “.. Embu niambie hapa ni wapi na gari lenu linaelekea wapi..?” “..hapa tulipo ni mikumi na gari letu linaelekea Iringa kwani wee unaelekea wapi..?” Aliongea yule konda kwa kujiuma uma huku nikisikia kelele za dereva akilalamika nakutufuata eneo tulipo.. Uoga ulianza kunitawala ndani ya halmashauri yangu ya kichwa na kufanya mwili wangu wote kunilegea na kutetemeka si kwa baridi kali, la hasha ni kwa woga niliokuwanao huku nikimwacha yule konda akiendelea kunitolea macho na mdomo wake kuugeuza bubu kwa muda. nikachukuwa ngozi mojawapo nakujificha huku yule konda akibaki na bumbuwazi. “..inamaana wewe leo mgeni humu nyuma ya gari..? Muda wote kutoa jeki na spana tu unatumia dakika zote hizo..?” “..hapana mkuu haya mangozi ndio yamesababisha nisione kiurahisi, lakini nakumbuka niliweka maeneo haya haya..!!” Yule kondakta alikuwa akijibizana nadereva wake, punde nikaanza kuhisi kama wakisogeza zile ngozi kwa kutumia nguvu. Akili ilianza kunichemka nakuona endapo dereva akilijua nipo humu ndani itakuwa vingine kwani hapo ni spana tu lakini anavyomkaripia huyo konda. Walisogeza sogeza yale mangozi huku na kule bila ya kufikia eneo nililokuwa nimejificha, nadhani konda ndio aliyekuwa akimkwepesha, mara kidogo nikasikia kimya kimetanda huku nikihisi kama wanashuka. Nilisogeza ngozi lile nililokuwa nimejifunikia nakuangaza huku na kule. Kulikuwa na giza sana hivyo sikuweza kuambulia chochote zaidi ya kutoka zangu pale huku nikipapasa pembeni kutafuta uelekeo wa lango la kutokea. Nilifanikiwa kuona mlango nakutoka taratibu mpaka nje ambapo kwa muda huu mbalamwezi kali ilikuwa ikiangaza, nikainama uvunguni mwa hili lori nakuwashuhudia konda na dereva wake wakibadilisha tairi. Kwa ushujaa niliokuwa nao Tina mie niliwazunguka nakuelekea mpaka mbele ya gari kisha nikaingia nakuanza kusachi kama nitapata chochote kwani njaa ilikuwa ikilisumbua tumbo langu. Nilifanikiwa kukuta bahasha imevimba japo sikujua kilichopo lakini halmashauri ya kichwa changu moja kwa moja ikatambua kuwa huenda ikawa ni hela, kwa kutumia mwanga wa mbalamwezi na papara nilizokuwanazo niliifungua nakukutana na pesa nyingi sana.

Nikaichukuwa nakuificha ndani ya gauni langu kwenye nguo ya ndani ‘chupi’ kisha nikachukuwa madumu yaliokuwa na maji, nikamalizia na mikate halafu nikatokomea porini bila wao kuniona. Nikiwa nimeuegemea mti mkubwa huku ile njaa kali iliyokuwa imeniandama toka mwanzo wa safari nakusababisha msuguano na muungurumo ndani ya tumbo langu sasa ikawa imekatishwa na mikate pamoja na maji, nilifakamia nakulijaza tumbo haswaa na baada ya hapo nikaanza kuhisi kama kupata usingizi wa ajabu huku nguvu zikiniisha. Kwa mbaali nikasikia lile gari likiondoka. Ile mbalamwezi kali iliyokuwa ikiendelea kuangaza iliendelea kushindana na macho yangu sasa macho yangu yakawa yamesaliti amri nakujikuta nikijiegesha pale pale chini ya mti mkubwa.. “..Leo umependeza Tina mbona watakukoma..?” “..kawaida yangu Aisha na hapa nikijipigilia na mkoba wangu, mbona darasani watanitaka..?” “…hivi si unajua kipindi cha sasa hivi mwalimu anaingia muda si mrefu na leo anatoa ‘test’..?” “..ok, basi Aisha nisindikize uani nikakojoe ‘then’ tuelekee huko darasani..” “..ndio ufanye haraka huko mwalimu atakuwa ameshaingia..? “…Aisha..? Aisha..? Aaaaaisshhaaaaaaaa…?? Nyoka.. Nyoka Aisha mtoe, mtoe naogopaa..!!!” Nilikuja kushtuka bado nipo porini tena kumepambazuka, sauti za ndege zilikuwa zinaendelea kupaa zaidi. Mwili wangu sasa ulikuwa umetawaliwa na wadudu aina ya siafu wale wadogo dogo sana ambao hawaumi, nilijipangusa pangusa, kadri nilivyozidi kujipangusa na mwili wangu ndivyo ulivyokuwa ukiendelea kunitutumka nakuacha maalama alama makubwa kuanzia usoni mwangu, mikononi mpaka mapajani ambapo ndipo walikuwa wakinishambulia zaidi, mara nikashuhudia wadudu wengine wakitambaa kwenye gauni langu, na hawa hawakuwa wadudu wakawaida kwani walikuwa weusi sana na hawakuwa na miguu, wapo kama kono kono. Nilivua gauni langu nakulikung’uta, ile nataka kulivaa nikahisi kwenye bado wapo kwenye nguo yangu ya ndani ‘chupi’, kunacheza cheza. Woga na hasira kali vikanijaa hivyo akili yangu moja kwa moja ikanituma huenda hawa wadudu wananitambalia hadi huku. Hivyo nikaivua nguo yangu ya ndani ‘chupi’ haraka haraka na kwa uoga, nakuitupa kwenye kapori ka pembeni yangu kisha nikalivaa gauni hivyo hivyo. Nilipomaliza nikakaa nakuanza kutafakari ndoto niliyokuwa nimeiota mpaka eti rafiki yangu Aisha ananisubiri chooni ili twende kwenye kipindi darasani. Mchozi ulianza kunidondoka huku nikiinuka taratibu eneo lile nakuanza kutafuta barabara, “..nataka nirudi chuo ama kwetu Mwanza..?” Nilijikuta naongea mwenyewe tena kwa hasira ya hali ya juu. Nikiwa bado njiani na majonzi tele huku dhamira yangu ikiwa nikwenda kupanda basi au gari lolote. “..Mungu wangu..!” Akili ilinicheza ghafla nakugundua kumbe ile nguo ya ndani ‘chupi’ niliyokuwa nimeitupa ilikuwa na bahasha ndani yake. Ile bahasha niliyoichukuwa kwenye lile lori ambapo kulikuwamo na hela. Kwa bahati nzuri, kumbukumbu za nilipoirushia ile chupi nilikuwa nazo hivyo nikarudi mpaka lile eneo niliokuwapo nimelala, kisha nikaingia katika kichaka cha pembeni yake nilichokuwa nimeitupa. “..mhh..!! mhh..!! mhh..!! mhhh..!!” Nilihisi pumzi zinaniishia, huku kojo likitoka lenyewe nakusababisha mchozi unitoke kwa hasira iliyoambatana na kwikwi ya kigugumizi baada ya macho yangu kukutana uso kwa uso kwa mbali na Simba jike akiwa amejifungua huku vile vitoto vyake vikichezea chezea ile bahasha pamoja na noti noti wakizivuruga vuruga huku ile nguo yangu ya ndani ‘chupi’ wakiichanachana vipande vipande… Bado nilikuwa na mshangao wa hali ya juu, machozi ya hasira bado yalikuwa yakinitiririka kwenye paji langu la uso wangu. Nilijisogeza kwa pembeni taaratibu kisha nikaokota jiwe kubwa na kurusha kichaka cha pembeni yangu. Kitendo cha kurusha lile jiwe, kikafanya yule simba asimamishe masikio yake halafu akainuka nakufuata eneo nililokuwapo. Nilitamani ardhi ipasuke nidumbukie kwani mapigo yangu ya moyo yalinibadilika mara mbili na pale na sasa nikajijaza moyo wa kiujasiri nakujificha huku nikihisi kama nimejikojolea tena. “..Mungu saidia..! Saidia..!” Nilijsalia kimoyo moyo kunusuru maisha yangu. Nikiwa bado katika hali ya hofu na. Ya kuzubaa mwenyewe huku nikiendelea kumtolea macho mara yule simba akasimama huku watoto wake wakimzunguka nakumchezea. Alisimama pale kama dakika moja nzima kisha akabadilisha uelekeo nakuondoka zake. Nilishusha pumzi na safari hii akili yangu ikarudi tena mpaka pale nilipokuwa nimetupa bahasha. Sikuwa tena na uoga kwakuwa nilikuwa na uhakika upande alipokuwa ameelekea yule Simba hivyo nikajikongoja taratibu mpaka lile eneo. Niliikuta ile bahasha ikiwa na pesa kidogo huku zile zilizokuwa zimetawanyika niliambulia chache tu, tena kama nne za noti noti ya shilingi elfu kumi. Nikazikusanya nakuzirudishia kwenye bahasha halafu nikafunga katika pindo langu la gauni kwani sikuwa na nguo ya ndani ‘chupi’ nakuondoka zangu huku nukiitafuta barabara ya lami. ** Hali ya hewa ilianza kubadilika kwa asubuhi hii tulivu. Muungurumo wa radi za hapa na pale ndizo zilizoanza kuchochea hali ya hewa nakusababisha mvua kubwa ambayo kwa muda huu ilikuwa ikipenyeza kifuani mwangu mpaka katika gauni langu nakulowana chapachapa. Zaidi ya nusu saa bado nilikuwa nimesimama kando kando ya barabara ya lami huku nikisubiri gari lolote ili niweze kupanda nakuelekea kwetu Mwanza. Furaha ya ajabu ikanirudia tena baada yakuona gari ndogo yakubebea mizigo ikiwa inakuja kwa mwendo wa taratibu sana, niliinua mkono wangu wa kulia nakusimamisha bila ya woga wowote. Hatimaye likapunguza mwendo na liliponikaribia likasimama. “..unaelekea wapi binti..?” “..Mwanza..!” “..Mwanza..? Mwanza unapajua wewe..?” Aliniuliza dereva wa ile gari ambaye alikuwa ni mzee sana. “..embu ingia ndani, sasa na huku unatokea kijiji gani…?” Nilibaki kigugumizi kwa muda huku nikilikwepesha jicho langu lisimwangalie huyi mzee aliyokuwa akiendesha hili gari. Safari ya mimi kutoka mikumi ilianza huku ndani ya gari tukiwa na dereva na wabibi wawili katika siti ya nyuma. Mwendo wa taratibu sana aliokuwa anaendesha huyu mzee ndio ulionijaza hasira na uchovu ndani yake. “..umesema unaelekea Mwanza..? Ila sisi hatufiki huko ila tunaelekea mpaka Kiteto hivyo tutakuacha njia panda ya Kiteto pale karibu na Dodoma..” “..nitashukuru sana..!” Kadri gari lilivyokuwa linatembea ndivyo na hali ya ubaridi ikaanza kiungia katika gauni langu lililokuwa hata halijaanza kukauka yaani bichi bichi. Uhakika wa kusafiri nilikuwa nao japo nilipewa lifti. Ukimya ulliokuwa umetawala ndani ya hili gari ulinifanya nijisikie mwili wangu kuchoka. “..simamisha gari husikii wewe Mzee..?” “..kwani tumefanyaje jamani..?” “..kelele huko..” Nilishangaa napigwa na ubapa wa panga, kisha lile jambazi kuu kati ya watano likaangalia gauni yangu likagundua kitu.. “..umeweka nini hapo kwenye pindo la gauni yako…?” Nilianza kutetemeka nakujiumauma nakuona ndoto zangu zakufika Mwanza ndio zinaishia hapa hapa kwani pesa zote nimezificha kwenye bahasha na niliifunga kwenye pindo la gauni langu. Lile jambazi likaanza kufungua pindo iliyokuwa katika gauni langu kisha akatoa bahasha ile niliokuwa nimeificha. Nillitamani nimpokonye lakini haikuwa na jinsi tena kwani alikuwa na silaha kama panga na bunduki pia alikuwa na

wenzake. Alinifungua gauni langu kwenye pindo nakutoa bahasha nakuzimwaga hela nyingi sana kisha akaniangalia kwa jicho la furaha. “..wewe waweza kwenda kwasababu tumepata hela kutoka kwako. Haya kimbia haraka na nahesabu, 1, 2, 3…” Nilitoka mbio huku nikiwaacha yule mzee na wale wabibi wakiwa chini ya ulinzi wa wale majambazi. Kitendo cha kupiga hatua mbili tatu huku nyuma nikasikia milio ya risasi ikirindima. nikapindisha shingo yangu nakuangalia ndipo nikashuhudia majambazi wakiwateketeza wale wazee nakudondoka papo hapo nakufa. “..Mamaaaa..!! uuh!! Uuh..!! Uuh..!!” Mishipa ya hasira ikaanza kunituna huku nikimtolea macho yule mzee na wale wabibi. Nikaligeuza jicho langu nakuangalia dirishani. Jua kali lilikuwa likiwaka nje ila sikujua tumefika wapi. “Mwanetu vipi tena..? Ulipitiwa na usingizi..” Nilijiangalia mara mbilimbili huku nisiamini ndoto niliyokuwa nikiota eti tumetekwa na majambazi mpaka yakawaua hawa wabibi na mzee. “..eeh Mwenyezi Mungu niepushe na ndoto mbaya hizi..” Nilijisemea kimoyo moyo huku nikiendelea kumwanglia yule mzee aliyekuwa akiendesha gari kwa mwendo ule ule wa taratibu sana. Haraka haraka nikainua mkono wangu wa kulia nakufungua mpaka kwenye pindo la gauni langu nilipokuwa nimeweka ile bahasha ya hela. Ndipo nikaamini sasa kuwa nilikuwa naota baada yakuifungua ile bahasha katika pindo la gauni langu nakuikuta na hela zake. Nilijichekea kimoyo moyo huku nikiirudishia ile bahasha mahala pake. “..hivi mwanangu ulishawahi kuishi Bagamoyo enhh..? Maana sura si ngeni kabisa..!” Aliongea mmojawapo wa wale wabibi nakuniacha njia panda huku nikivuta fikra nakukumbuka sauti kama ya yule bibi aliyekuwa ananifanyia maajabu kule bagamoyo nakuifananisha kabisa na ya huyu. “..sijawah kuishi..” Nilijibu kwa kujiamini, lakini akawa kama anamnong’oneza mwenzake kitu kisha wakaniangalia nakuanza kunicheka kwa sauti ya chini chini. “..ndio wewe mwanetu, sisi pia ni wanachama wenzako, na hizo chanjo mwilini mwako alikupiga huyu mwenzangu..” Wakaangaliana tena wakacheka, mapigo yangu ya moyo yalinibadilika zaidi nakuona kumbe nipo na wachawi tena wale walionitesa sana bagamoyo. Nilijipapasa tena maeneo ya mgongoni mwangu nikahisi bado nina zile chanjo. “siyo huko tu, jiangalie na nyuma ya viganja vyako..” Nilijiangalia nakuziona, kisha kwa jicho la ukali nikawaangalia huku mchozi ukinidondoka wenyewe… “..kwanini kila mkosi Tina mimi tu.. Kwanini..? Eeh mwenyezi Mungu kwanini umeniumba katika dunia hii yenye manyanyaso na masengenyo jamani..? Ni bora nijirushe nje ya hili gari nife tu..” Nilibaki bumbuwazi, mchozi ukiendelea kunitoka huku nikiusemea moyo nakubakiwa na dukuduku kubwa moyoni. Nilijihisi kama mwili wangu hauna tena nguvu za kunyanyuka. Wale wabibi walikuwa bado wakinishangaa na kunong’onezana huku wakinicheka. Niliendelea kuwatolea macho kwa muda mrefu nakuyaelekezea usoni mwao na mwishowe nikajihisi kama macho yao yanabadilika rangi nakuwa ya kijani tena yale yenye miale mikali kama ya radi. Sikutaka kuonekana muoga kwani niliamini nimeshaingia katika himaya ya wachawi tena wale wachawi waliokubuhu, hivyo yanipasa kupigana nao mpaka mwisho kama kufa nife tu. “..Baba Mungu tenda miujiza yako sasa Baba, hakuna jina jina litialo nguvu kama lako… Baba nyosha mkono wako na uniokoe kwa nguvu zako..” Nilipata nguvu ya ajabu nakujikuta nikianza kusali kwa sauti ya chini chini na ya kukemea. Kadri nilivyokuwa nazidisha maombi bibi mmojawapo alianza kujinyonga nyonga kwa kugala gala mithili ya mgonjwa, tena mgonjwa yule wakifafa. Muda wote yule mzee alikuwa bize akiangalia mbele huku akiendesha gari na alikuwa hajui chochote kinachoendelea kati ya mimi na hawa wabibi. Baada ya yule bibi mmoja kujinyongolota kwa muda mrefu pale chini. Yule bibi mwingine akakasirika nakubadilika kucha na nywele zake zikawa ndefu sana na za kutisha huku jasho likimtiririka mwilini mwake mithili ya maji. Kisha akanifuata huku macho yake akiyakaza nakuwa makubwa kama yanataka kutoka. “..ushindwe katika jina la Yesu..! Ushindwe na ulegee..! Shindwaaa..!!” Bado maombi yangu hayakusaidia kitu chochote kwake zaidi yakumuongezea nguvu mara mbili nakunishika shingoni kisha akatoa mkono wake nakunichana upande wa shingoni mfano wa chanjo.. “..niokoeni nakufaaa.. Mzee nisaidie nakufaaa.. Bibi ananiua..?” Nilitoa sauti ya ukali lakini ndio kwanza yule mzee akageuka nyuma nakuangalia kisha akaendelea kuendesha gari na kwa muda huu alibadilisha ile spidi ndogo aliyokuwanayo nakutembea kwa mwendo wa kasi sana. Mwendo wa kasi uliokuwa ukiendelea ulinifanya nishindwe hata kuangalia pembeni wala kujua tunapoelekea. Kizungu zungu nilichokuwa nacho ukiongezea na chanjo nilizokuwa nimepigwa na huyu bibi vilinifanya nishindwe kuinuka wala kuongea chochote. “..hapa ni wapi..?” “..tulia sisi ni wasamalia wema tumekuokota ulitupwa nusu saa iliyopita na gari moja ndogo kisha wakakimbia..” “..wameelekea wapi..?” “..tulia binti, punguza jazba kwanza. Inakubidi twende kwa balozi wetu wa nyumba kumi, ukaoge uondoe hilo tope tope mwilini..” Maskini Tina mimi kumbe nilikuwa nimetupwa. Kumbukumbu zilinirudisha mpaka kwenye gari iliyokuwa inaendeshwa na mzee huku imepakia wabibi wawili lakini sina hata kumbukumbu vizuri ikawaje mpaka nimetupwa hapa.. “lakini waliniambia kuwa watanishusha karibia na Dodoma inamaana ndio hapa..? Na kwanini walinitupa badala wanishushe tu kawaida..?” Bado nilikuwa nausemea moyo kwa maswali mengi sana huku nisijue kilichonisibu Tina mimi. Nilijikagua vizuri nakushuhudia damu damu zilizokuwa zimenigandia mwilini. Wale wanakijiji waliniinua nakunipeleka mpaka kwa balozi wa kijiji chao ambapo nilielekezwa bafuni nakuingia kuoga. Maji yao hayakuwa masafi sana hivyo kila nikijimwagia yalikuwa yakichanganyika na damu damu zilizokuwa zimenigandia mwilini mwangu nakuwa meusi kabisa. Nilipomaliza kuoga nilikung’uta gauni langu nakulivaa lakini kabla sijamalizia kulivaa vizuri kumbukumbu zikanijia kuhusiana na ile bahasha ya pesa niliyokuwa nimeificha kwenye pindo la gauni langu. Niliikuta ile bahasha nikaifungua nakuanza kuangalia ndani yake napo nikazikuta zile pesa zote zipo. Nilitoka bafuni nafuraha tena mpaka nje. “..nahitaji kuondoka leo tena sasa hivi..?” “..kwani unaishi wapi..?” “..kwetu Mwanza, nionesheni barabarani ambapo naweza nikapata mabasi..” Mwili wangu bado ulikuwa na majimaji ambayo hayakukakua vizuri nilipooga, nilisahau maumivu yote. Nilisindikizwa na balozi wao mpaka barabarani. “..lakini binti nauli unayo..? Au utawaomba tu kama msaada wakuchukue..? Maana nijuavyo Mwanza mbali..” “..hapana msijali kwa hilo, nitafika tu ondoeni shaka..” Ilituchukuwa kama dakika ishirini nzima tukiwa tunasubiri basi. Kila basi lililokuwa linapita lilikuwa linaishia Dodoma tu. Hatimaye baada ya kusubiri tena kwa muda mrefu ndipo likapita basi la ‘Mohamed trans’ liendalo mpaka Mwanza. Sikutaka kabisa kuuamini macho yangu lakini moyo wangu uliojaa furaha ndani yake ndio ulionifanya niamini kuwa sasa nipo eneo salama na safi mpaka nitakapofika kwetu Mwanza. Kila abiria alikuwa akinishangaa, si kwa upara wangu uliojaa makovu ya vidonda kichwani, la hasha! Bali ni kwa jinsi gauni langu lilivyokuwa limechafuka kupindukia.

“..Habari yako dada..?” Alikuwa kaka mmoja ambaye nilikuwa nimekaa naye siti moja akiniongelesha. Niligeuza jicho langu kwa dharau zote nakumwangalia kisha nikamjibu kifupi tu. “..salama..!” “..mimi naitwa James, sijui mwenzangu unaitwa nani..?” “..anhaa, James..?” “..hilo ndio jina langu haswaa..!” “..naomba uniache kwani kichwa changu kinamambo mengi sana.. Sawa james…?” James alikaa kimya akinitolea macho tu. “..haya mpendwa katika bwana..” “..Mpendwa..? Mpendwa mke wako..?” Nilimjibu kwa dharau zote nakumfyonza kisha nikaegemea siti nakuwaza zangu. Ndani ya masaa mawili tulishapapita Dodoma na kwa muda huu tulikuwa tunaitafuta. Singida. Uchovu uliokuwa umetawala ndani ya mwili wangu ndio ulisababisha na usingizi kinitawala ndani ya kichwa changu kwani nilianza kipitiwa na usingizi. Usingizi ulinizidia na nilipokuja kushtuka nilijikuta kichwa changu kipo begani kwa James. Niliinuka haraka haraka. “..sorry James..!, nilipitiwa na usingizi nikajik..” Kabla sijamalizia kujitetea, James alidakia.. “..wala usijali lala tu..” “..hapana..!, kwani hapa tumeshapita Tabora..?” “..mbona Tabora tumepapita muda tu na sasa tunaitafuta Mwanza..” Nilijiweka vizuri. Nakwa sasa wala sikujionesha tena kumchukia James zaidi yakupiganaye stori za maisha. Sikuwa namfahamu vizuri James, lakini nilimfahamu nakujua kuwa kumbe James alikuwa ni muinjilisti na tena alikuwa na kanisa lake huko Mwanza tunapoenda. Alitoa biblia yake nakuanza kunichambulia maneno ya Mungu na pia kunishawishi kumrudia Mungu kama bado sijaokoka. Alitoa mkono wake nakuniwekea mpaka kichwani mwangu nakuanza kuhisi nimepata uponyaji sasa kwani niliweweseka sana ikiwa pamoja nakuzimia ndani ya basi na hata nilipokuja kushtuka James aliniambia kuwa nilikuwa na mapepo tena mengi sana mpaka ikabidi wasaidiane na mama wa jirani ambaye alikuwa na yeye ameokoka ndipo wakafanikiwa kunitoa majini manne kwa shida sana mpaka yakatishia kuniua mimi na wakina James. “..amani ya bwana iwe nawe binti..!” Aliongea James. Ni taa ya kwenye basi tu ndio ilikuwa imewashwa lakini upande wote wa nje kulikuwa na giza kali. Kila abiria aligeuka nakuniangalia kwa kunishangaa. “..nipeni maji nasikia kiu..” Niliropoka kwa sauti ya juu huku nikihema juu juu. James alitoa maji ya chupa kwenye mfuko wa nailoni kisha akanipa na nilipomaliza kunywa nilipewa na machungwa nikala. “..haya embu niambie jina lako binti..” “..naitwa Christina..” “..ok, Christina huku Mwanza ndio nyumbani ama..?” “..si nilishakujibu toka mwanzo jamani..?’ “..ok, unakaa sehemu gani kwa huku Mwanza tunapoenda..?” “..Nyamagana..” Nilimjibu kwa kujiamini na baada ya hapo James akanisihi nikalale nyumbani kwake anapoishi na mke wake kwa kuwa gari itafika usiku sana hivyo kesho yake atanipeleka mpaka nyumbani kwetu Nyamagana.. “..Christina..??, Christinaaaaaaaaaa…??” Nilishtuka kutoka usingizini huku nisielewe chochote. Kila mmoja alionekana kuwa busy kumsaidia kumbeba mwenzake. Usiku ulikuwa mnene sana kiasi kwamba ni tochi za simu tu ndio zilikuwa zikiangaza huku na kule kuhakikisha wanaona kinachoendelea mbele ya macho yao. Mikono miwili ilikuwa imeshikilia kichwa changu huku ikiniita kwa jina langu la Christina. Kila nikijitahidi kuvuta kumbukumbu bado ilikuwa ni vigumu. Vilio vya watu ndivyo vilizidi kuchanganya zaidi masikio yangu nakujiona kuwa sina tena bahati ya kuishi. “..wee Christina..? mzima lakini..?” “wewe nani..?” Nilimuuliza kwa sauti ya ukali huku nikimkunjia uso vilivyo, jasho kali lilikuwa likitiririka kupitia usoni mpaka shingoni mwangu. Japo alikuwa ni mwanaume lakini alionekana kulia kama mwanamke tena yule ambaye ameshikwa na uchungu wa kujifungua watoto mapacha. “.. embu amka, mimi mchungaji James..” “..mchungaji James..? wa wapi..? unataka nini kwangu..?” “Kwa uwezo wa mwenyezi mungu aliyetuumba nafarijika kukuona umekuwa mzima wa bukheri. Ulikuwa umepitiwa sana na usingizi huku ukiweweseka kwa mawazo njia nzima. Basi likaanza kuyumba huku likipoteza uelekeo. Abiria wote wakaanza kupiga makelele huku wengine wakimlaani dereva kwa kitendo cha kuendesha gari vibaya. Nilijitahidi kusali sala zangu zote ili tu ninusuru ajali hii lakini kama unavyoona yaliyopangwa na mwenyezi mungu hakika kwa binadamu hawezi kutenganisha. Tumepata ajari kubwa sana na hii yote imesababishwa na lori lililokuwa limepaki vibaya..” “lori..?” Nilishusha pumzi nakurudiwa nakumbukumbu vizuri yakuwa nilikuwa naelekea Mwanza nyumbani kwetu. Nikayapindua macho yangu vizuri huku na kule kwa kutumia mwanga ule ule wa tochi za simu nakuona watu wakilia na wengine wakibebwa. Mwili wangu ulinisisimka ghafla sambamba na kichwa kuniuma huku mchozi ukinidondoka nakujiona laiti kama ningekuwa mimi ndio majeruhi ama maiti. “..kweli mwenyezi Mungu bado ananipenda nakujali..” Nilijisemea kimoyomoyo huku nikimuangalia mchungaji james mara mbili mbili. “..ahsante mchungaji, umeokoa maisha yangu..!” Aliniinuka pale chini nakuelekea nje kabisa ya basi, sijui alienda kufanyaje lakini baada ya muda mfupi alirudi mpaka eneo niliokuwa nimejilaza. Maiti nyingi zilikuwa zimepangwa huku nyingi zikiwa hazina viungo vya mwili. Kuna ambazo hazikuwa na shingo, mikono hata nyingine hazikuwa na miguu. Hakukuwa na msaada wowote kutoka hospitalini zaidi ya wale waliokuwa wazima kuwasaidia wale wenye unafuu kidogo na kuendelea kutoa maiti nakuzipanga kwa nje. “..Kwani hapa mpaka Mwanza ni mbali..?” Nilimuuliza mchungaji james huku nikimuegemea begani mwake kana kwamba mume wangu ama baba yangu na bila yakuogopa kama ni mtu wa mungu. “wala hata siyo mbali sana kwani umbali wake ni sawa na kibamba mpaka kariakoo..” “..twaweza kutembea..?” “..wala tusiwe na haraka kiasi hicho. Kwanza tuhakikishe hawa ndugu zetu wanapata matibabu ya huduma ya kwanza. Pili lazima mawasiliano yafanyike na wote tuje kuchukuliwa na basi jingine wala usiwe na wasiwasi Christina..” Maneno yale yaliniingia sana kichwani nakunitia nguvu nakumuona kuwa mchungaji James ni mtu mzuri, anayejali na kuheshimu watu na hata pia ni msamalia mwema. Aliniinua pale nilipokuwepo. “..mizigo yako unakumbuka ulipokuwa umeiweka..?” “..hapana, wala usihangaike kwani sikuwa na mzigo wowote..!” Kwa muda mfupi tayari gari za polisi wakishirikiana na wanakijiji wa hili eneo walikuwa wakizunguka nakupakiza zile maiti zilizokuwa zimepangwa pembeni ya macho yangu. Sikuwahi kushuhudia maiti zikiwa nyingi kiasi kile zaidi yakuonaga kwenye televisheni tena kwenye taarifa ya habari ama filamu. Machozi yangu yalikuwa karibu sana nakujikuta nikiendelea kububujikwa na machozi huku nikiushikilia kikamilifu mkono wa mchungaji James nakuelekea kwenye basi dogo lililokuwa limekuja kuokoa majeruhi. “…Hapana, sisi ni wazima tunamshukuru mwenyezi mungu tumenusulika, hivyo tupelekeni mpaka kituo cha mabasi ‘Nyegezi’ hapo tutajua jinsi yakufika makwetu..”

Aliongea mchungaji James huku akimsisitizia dereva wa hii gari. Safari yakuelekea stendi kubwa ya mabasi ya Mwanza ‘Nyegezi’ ilianza huku akili yangu yote nikiituliza nakumuachia James kwani alishaniahidi kuwa atahakikisha amenipeleka mpaka nyumbani. Mwendo wa nusu saa ulitosha sana kutufikisha Nyegezi. Hali ya hewa ilikuwa imebadilika sana japo hakukuwa na joto sana wala baridi sana. Mchungaji James muda wote alikuwa amepitiwa na usingizi nadhani hakupata usingizi kabisa zaidi ya njia nzima kushikilia biblia yake nakulichambua neno la Mungu. “..James..?, mchungaji James..?? amka tumefika.!!.” Nilimuamsha kwa kumtikisa lakini bado alionekana mzito kuamka. Baada ya kuendelea kumuamsha zaidi ndipo akaamka. “..haya niambie tunaelekea wapi sasa..?” “..naona kumekucha kabisa, sasa kwa hapa inatubidi tuchukuwe taksi mpaka nyumbani kwangu mtaa wa pili kule halafu tutajua sasa namna yaw ewe kukupeleka kwenu Nyamagana..” Tulichukuwa taksi nakuelekea mpaka nyumbani kwake. Mchungaji James aliuwa na nyumba kubwa sana tena yenye uzio wa ukuta. “..Mama yuko wapi..!” “..Mama, mama hayupo..!!” “..kaenda wapi..?” “..kaenda kanisani..” Mchungaji james alimuuliza mtoto wake baada tu yakupokelewa mizigo. Uchovu niliokuwa nao ukichanganyia na usingizi ni kati ya vitu vilivyokuwa vimeuchosha sana mwili wangu. Tulipoingia tu sebuleni, mchungaji James aliongoza moja kwa moja mpaka chumbani kwake kisha akarudi akiwa kabadilisha nguo. “..samahani Christina. Unaweza kwenda bafuni ukaoga mlango ule, mimi nitaogea chumbani kwangu. Na kwa kubadilisha nguo binti wa kazi huyo hapo atakuelekeza..” “..sawa, wala usiwe na hofu nitaelekea tu kuoga..” Kwa namna alivyokuwa amekuja mchungaji James alinifanya mwili wangu wote ujisikie vibaya kwa kusisimka ovyo. Japo alivaa ‘singlendi’ lakini macho yangu yaliweza kuhakisi nakushuhudia nywele nyingi sana zikiwa zimemjaa kifuani mwake. Hata ile hamu yakuelekea bafuni nikaikosa nakutamani kwenda kuoga naye tena nimuogeshe mimi. Kila nikifikiria kuwa ni mlokole nabaki naumia nakuvunjika moyo. “..lakini mie ndio Tina..!!, tena Tina aliyepinda toka zamani..” Nilijikuta uzalendo unanishinda Tina mie nakutokwa na udenda uliochanganyikwa na hamu ya kutaka kufanya mapenzi na mchungaji. Nilikuwa bado nimezubaa pale sebuleni huku pembeni yangu akiwa mfanyakazi wa ndani akiangalia televisheni. Nikajisachi mifukoni mwangu nakutoa noti shilingi elfu moja kisha nikampa Yule mfanyakazi wa ndani. “..nenda duka la madawa lolote kaninunulie sabuni ya detto, nashindwaga kutumia sabuni nyingine, sawa..?” Yule binti wa watu aliinuka nakuondoka kwenda dukani haraka haraka. “..wafanyakazi kama hawa ndio dawa yao..” Nilijisemea kimoyo moyo huku nikihakikisha Yule mtoto wa James aliyetupokea yupo nje. Nikauloki ule mlango wa sebuleni nakisha nikazivua nguo zangu nakubakiwa mtupu kama nilivyozaliwa, nikazishikilia mkononi nakuongoza mpaka chumbani kwa mchungaji james huku nikijitingisha makalio yangu… Nilipokaribia tu mlango wa mchungaji James kwa ghafla mapigo yangu ya moyo yakabadilika mwendo na kwa muda huu yakawa yanaenda mbio zaidi kama saa yam shale. Hatua chache nikawa tayari natazamana na mlango wa chumbani kwake huku mikono yangu ikinitetemeka mithili ya mtu aliyemwagiwa maji ya barafu. Nilipiga moyo konde huku nikishikilia kitasa tayari kwa kufungua mlango. Sikutaka kuonesha uoga wowote Tina mie kwani mambo kama haya tayari nilikuwa nimeshayazoea tangu zamani. Nilichokifanya nikaufungua ule mlango nakuingia chumbani kwake kisha nguo zangu nikazitupa kitandani mwake nakuanza kugonga sasa mlango wa kuingia bafuni kwa mchungaji James huku nikijidai kama naugonga.. “..my wife..?, unasemaje naoga..?” “.. nifungulie mara moja mume wangu na mimi nataka kuoga..” Maskini mchungaji James alijua kuwa anaongea na mkewe kumbe nilikuwa Tina mie. Alifungua mlango hivyo hivyo akiwa na mapovu ya sabuni usoni huku macho yake akiyafumba. Nikatumia mwanya huo huo na mimi kuongoza mpaka bafuni kisha.. “..haya tuendelee kuoga tu mume wangu..” Bado mchungaji James hakuwa anaelewa chochote kwani mapovu ya sabuni yaliokuwa yamemzunguka mwili wote sana sana eneo la usoni mwake yalimzuia kutoa macho kuangalia nakujikuta akiniruhusu kuingia bafuni huku akidhania kuwa ni mke wake. “..acha tu nikusugue vizuri.., enhe niambie za safari mume wangu..!!” Nilijikaza sauti nakuongea kama mtu mwenye mafua kana kwamba isingekuwa rahisi kwa mchungaji James kutambua ni sauti yangu. Nilimgeuza mgongo huku nikimuogesha na kabla sijamgeuza aniangalie nilimpaka tena sabuni usoni mwake ili niweze kumzuia asione kabisa kwa muda ule. “..yaani mke wangu, tulipata ajali mbaya sana na kwa bahati nzuri na kumshukuru Mungu nimenusulika nipo salama, na nimekuja na binti yuko hapo sebuleni naye amenusulika kwenye hiyo hiyo ajali ambapo watu wengi wamepoteza maisha..” “..mmh pole sana mume wangu, ndio maana nimeona nguo zako zikiwa na damu damu, polee..!!!” “..ahsante sana mke wangu..” Bado nilimfanya mchungaji James asiweze kujua chochote kama anayeongea naye ni mimi mwenyewe Tina. Nilichukuwa mikono yangu na kumtelezesha kuanzia mabegani mwake, shingoni mpaka kiunoni huku nikichukuwa sabuni nakupaka eneo la nanii yake kisha nikaanza kuishika shika kwa kuitekenya.. “..inatosha mke wangu haya nimwagie maji nitoe sabuni hii..” “..tulia kwanza jamani..” “..hapana sabuni inaniwasha machoni, embu nimwagie maji mke wangu..” Nilimshika vya kutosha mpaka nikahakikisha amesimamisha nanii yake ndipo nikamwagia maji tena kwa taaratibu kuanzia mgongoni kisha tumboni na nikammalizia kumwagia usoni na kichwani. Alipofungua macho tu akakutana na sura nyingine kabisa na wala hakuwa mke wake kama alivyoukuwa akifikiria bali nilikuwa ni Tina mimi nilioshindikana. “..we.. wee.. wee ss.. ssiii.. niiili.. ku.. aa..a.. cha.. sebuuuu… leni..? Hapa umefuata nini..?” “…James..? nimeshindwa kuoga peke yangu..!” “..ndio uje chumbani kwangu..? Mke wangu yupo wapi..? Mbona unataka kunivunjia heshima binti..? Hiyo ndio shukrani yako ya kukuleta hapa enh..!!” Mchungaji James alinibadilikia nakuwa mkali kama kifaru tena faru dume mwenye hasira ya kuchezewa watoto wake na mnyama mwingine. “..nakupa dakika mbili uwe umeshavaa nguo zako nakupotea hapa chumbani kwangu ibilisi mkubwa wee uliyetumwa na shetani.., ushindwe..!! nasema ushindwe kwa jina la…” Kabla hajamalizia kuongea nikamziba mdomo wake. Kwa ushujaa niliokuwa nao nikamshika nanii yake nakuanza kumtolea maneno ya hasira. “..James elewa mimi ni mwanamke kama wanawake wengine, nina hisia na nina haki yakutekelezewa kama mwanamke. Najua kuwa wewe ni mchungaji nakuomba unisaidie japo unilale hata kwa bao moja tu nitalizika..” “niiiiiiiniiii??? ..binti..??, umefika mbali.., mbali tena mbali haswa. Una pepo mkubwa wa ngono na unahitaji kuombewa zaidi. Nakuomba tena kwa mara ya pili uende ukavae nguo zako na uelekee sebuleni hapo nitakuja kufanya maombi mazito na wewe. Kwanza hata mke wangu akikukuta umekaa sebuleni atafurahi, embu nakuomaba uende binti pliiz..!!” Maneno yake hayakuniingia akilini hata kidogo. Niliona kama anampigia mbuzi gitaa acheze na tena mziki wenyewe ni ule wa mchiriku. Nikaanza kumfanyia visa. Nilichokifanya nilipumua juu juu nakujifanya nina mapepo kweli kisha nikajiangusha mpaka chini vile vile nikiwa uchi wa mnyama nauanza kutapatapa mithili ya wale wacheza shoo wa kikundi cha THT huku nikitoa mate yenye mapovu mithili ya mgonjwa wa kifafa. Nilitumia kama dakika tatu nzima lakini ni kama mchungaji James alikuwa na bumbuwazi kwani nilijua tu kwa asilimia mia hawezi kuniombea huku akiwa uchi. Alichokifanya alikuwa mpole kisha akainama nakunishika shingo. “..binti, amka na pole kwa matatizo..”

Maneno yale yalinifanya nione sasa atakuwa ameelewa dhamira yangu yakujiangusha nakujigaragaza pale chini kama motto mchanga. Nilinyamaza kimya nakuinuka kisha nikamkaripia. “..nataka jibu moja tu..! unakubali kufanya mapenzi na mimi au la..!” Mchungaji James bado alibaki na kigugumizi kama dakika mioja nzima kisha akanijibu. “..hapana tayari nina mke wangu na licha ya hivyo, maandiko hayaruhusu. Kwani kufanya hivyo nikukiuka maandiko ya neno na kumkosea mungu..” “..sasa nakupa dakika moja tu..!! na usipokubali napiga makelele kwa nguvu zote kuwa unanibaka mpaka nihakikishe umati wa watu umefurika hapa bafuni, sawa..???..” “..no.. nooono.. nooo… usifanye hivyo binti..!!” “..haya unakubali ama..? nianze kuhesabu..?” Kimoyo moyo nilijipa shangwe kwani niliamini sasa nitakuwa nimemuweza mchungaji James na hatakuwa na ujanja kama nitapiga kweli yowe. Mwili wake wote ulionesha kutetemeka kwa uoga, huku nikishuhudia nanii yake ikilala. Nikatumia mwanya huo huo kumtetemesha zaidi.. “..nakuona hujibu uko kimya.., sasa naanza kuhesabu 1.., 2.., 3..?” Mchungaji James alinyong’onyea ghafla huku akionesha sura ya upole na huzuni. Sikutaka kumuonea huruma hata kidogo kwani kifua chake kilichojaa manywele ndicho kilichonivutia nakuingia humu chumbani mwake. Nilichokifanya nikamsogelea karibu kisha nikamkumbatia halafu nikajilaza chini nakumuamuru aanze kufanya mapenzi na mimi.. “..haya ingiza humu ndani kwangu James..??, ingiza basi..? hutaki..?” Jasho jembamba lililoambatana na machozi huku sura ya huzuni ikimtawala mchungaji James kwa kumuamuru kufanya kile kitendo. Bado alikuwa kama mtu mwenye kigugumizi yaani sitaki nataka, kwani alionesha kusita sita muda wote. Tukiwa bado tumezubaa pale chumbani tena kila mmoja akiwa uchi wa mnyama. Mara tukaanza kusikia hodi ikigongwa sebuleni. “..Atakuwa mke wangu huyo amekuja. Pliiz..!!! nakuomba tusitishe zoezi hili na nakuahidi tut…” “..Shiiii. tena ishia hapo hapo…? huyo wala si mkeo lazima atakuwa mfanyakazi wako wa ndani. Kwani nililmtuma sabuni. Nakuhusu kufanya siku nyingine. Utafanya wewe na mkeo. Sawa..?” “..lakini binti..?” “..lakini nini..? haya tuanze mara moja mwenzio nasikia nyege huko…!!” Niliona kama mchungaji James anataka kunicheleweshea muda ili mke wake arudi na tusiweze kuendelea kufanya chochote. Nikaanza upya zoezi la kumshikashika na sasa nilishamlaza chini kabisa na sio kitandani kama tulivyokuwa awali. nikaanza kukitawala kifua chake kana kwamba mume wangu wa ndoa. Nilizilamba chuchu zake sambamba nakukitafuta kitovu chake kilichokuwa kimezungukwa na tumbo. Mchungaji James alikuwa hana ujanja tena kwenye huu mchezo kwani nilikuwa nimeshamlegeza vya kutosha na kwa sasa alikuwa amehamia juu kwangu huku akiniingizia tena kama mtu ambaye hajafanya muda mrefu. Ndani ya dakika nne tulikuwa hoi kila mmoja na tayari tumeshamaliza cha kwanza. “..aha..!! haa..!! haa…!!, unavaa nini..?” “..Christina inatosha bwana..?” “..eti inatoshaa..? Ndio tulivyoafikiana..? hapa mpaka nisuuzike na roho yangu. Na kwa jinsi nilivyokuwa na hamu ya muda mrefu mwenzako. Hivi ujue tangu nizaliwe sijawahi kufanya mapenzi na mchungaji..? Kumbe nyinyi ni watamu kiasi hiki..?” Maneno yale yalizidi kuuchochea ubongo wa mchungaji James si kwa furaha bali ni kwa hasira kali nakujikuta akiunyanyua mkono wake wa kulia nakuanza kunishambulia kwa makofi. Alibadilika ghafla nakua mkali mithili ya simba tena simba dume. Macho yake yalikuwa mekundu sana huku mdomo wake ukitetemeka mithili ya mtu anayenyeshewa na mvua . “..Mpumbavu mkubwa sana. Nimekuvumilia muda wote huo hadi nimekutekelezea ulichokitaka lakini bado huriziki kwanini binti wewe..? Haya kwa sasa nasimama kama mchungaji na vile vile mwanaume lijari. Haya sasa piga kelele zako ulizokuwa unataka kupiga..? Pigaaa..??, pigaa sasa nikuoneshe..??” Ile hali aliyobadilika nayo mchungaji James ilinifanya Tina mie nianze kunyong’onyea nakuona hapa sasa kitakachofuata nikutoka na makovu ama maumivu mwili mzima. Maskini mchungaji James kumbe baada ya kuongea tu yale maneno ya ukali nikamshuhudia akianza kama kutetemeka mwili mzima huku yale macho yake akiendelea kuyakaza nakudondoka mpaka chini. Nilimuwahi pale pale chini nakumshika kifuani kwake ambapo mapigo ya moyo wake yalikuwa yamebadilika ghafla nakwenda mbio kama gari lililokatika breki. Hapo hapo halmashauri yangu ya kichwa ikanituma huenda ana ugonjwa wa moyo au kapata na mshtuko kutokana na kitendo hiki tulichokifanya ukizingatia na nyadhifa aliyokuwa nayo. Nilimtingisha mwili wote mara mbili mbili kuhakikisha lakini bado haikusaidia chochote zaidi ya yeye kufumba macho kabisa kama mtu aliyekata roho. Nilichukuwa kichwa changu huku sikio langu nikiambatanisha sambamba kifuani mwake japo kusikia tena mapigo yake ya moyo lakini haikusaidia kitu zaidi yakutosikia chochote. Woga ukanirudia Tina mimi na sikutaka hata kupoteza muda nilichokifanya nilitoka spidi mpaka chumba cha pembeni nadhani kilikuwa cha yule mfanyakazi wa ndani ama watoto zake mchungaji James. Nilichokifanya kwa haraka haraka nilichagua suruali ya kike nzuri na yakubana mapaja yangu kisha nikatafuta blauzi nzuri nakuzivaa. Kiukweli nilibadilika nakuwa sasa Tina mwingine kabisa kisha nikarudi chumbani kwa mchungaji James. Hali niliyokuwa nimemuacha nayo ndio niliendelea kumkuta nayo na kwa muda huu ni damu za puani ndizo zilikuwa zikimchuruzika nakuwa nyeusi badala ya nyekundu. “..ulale pahala pema peponi mchungaji James..” Nilijisemea kimoyo moyo huku nikimfumba macho yake kwa kutumia mikono yangu nakuanza kutafuta suruali zake nakutafuta hela za kuweza kujinasua kuondoka katika hili eneo pia huu mkasa. Ndani ya dakika ishirini tayari nilikuwa nimemaliza kusachi karibu chumba chote cha mchungaji James na tayari mifukoni nilikuwa niumezishindilia noti noti za shilingi elfu kumi zenye thamani kama ya shilingi laki mbili kisha nikachukuwa shuka nakumfunikia. Safari yangu yakutokea mlango wa jikoni ilianza huku nikiamini kwa asilimia mia endapo nitatokea mlango wa sebuleni ni lazima nitakutana uso kwa uso na mke wa mchungaji James ama yule mfanyakazi wake niliokuwa nimemtuma sabuni ya Dettol. Na hizi nguo zao nilizovaa ndio kabisa watanipigia mayowe. Sikutaka hata kujua ni saa ngapi, kwani kijua tu kile cha asubuhi wazi kilinitambulisha haitakuwa imefika saa sita ama saba za mchana. Kwa muda huu tayari nilikuwa nimeshatoka katika himaya ya kwa mchungaji James nakutokomea nisipopajua. Wazo la kufika nyumbani ‘Nyamagana’ likawa limeishia hapo hapo kwani ndani ya kichwa changu niliamini endapo mchungaji James akiwa hajafa basi itakuwa rahisi kwa mimi kupatikana kwani nilishawahi kumwambia kuwa naishi nyamagana. “..hapa nikurudi Dar es salaam tu..!! kwani hapa Mwanza japo ni jiji lakini nimeshaliharibu nani rahisi kushikwa kuliko Dar es salaam..” Nilijisemea peke yangu kwa sauti ya chini chini huku nikikatiza mitaa ambayo kwa namna moja ama nyingine wala sikuwa naijua ni mitaa gani. Baadhi ya vijana walikuwa wakinitolea macho kana kwamba wamenifananisha lakini hilo waka sikulitilia mashaka kwani nilishajua nilichokifanya cha kuvaa nguo ambazo si za kwangu. Mwendo wa dakika tano nzima ulikuwa tayari umeshanipa jibu nakutambua bararabara kuu ipitayo magari. “..hapa mpaka kituo cha mabasi nyegezi shilingi ngapi..?” “.. elfu kumi tu..” “..twende lakini nakulipa elfu nane..” “..unaua dada.., elewa mafuta yamepanda bei..” Nikiwa bado katika hali ya kuongea na dereva teksi na hata sikuwa nimepanda ile gari wala kupatana naye bei rasmi. Mara kwa ghafla akatokea mwanamama mnene mrefu kidogo. Alikuwa mweusi huku sura yake ikikunjamana vilivyo mithili ya mtu anapopigwa jua la utosi. Macho yake yalionesha kuwa tata kwani mbali na machozi yaliokuwa yakimtoka pia yalikuwa ni mekundu kama mtu aliyefiwa ama kumpoteza mume au mtoto wa kumzaa. “..unakwenda wapi Malaya mkubwa wewe..?”

Aliuliza kwa sauti ya jazba. Sikuwa namtambua zaidi yakumtolea macho mimi pamoja na dereva teksi. Mwili wangu ulikuwa tayari umeshakata tamaa ya kuishi huku nikihisi kama kojo likiteleza ndani ya suruali yangu iliyokuwa imenibana… Uoga uliochanganyikana na kutetemeka mwili mzima ni kati ya vitu ambavyo vilikuwa bado vinasumbua halmashauri ya kichwa changu huku nikibaki njia panda nikiendelea kumkodolea macho yule Mmama alioonesha kunikazia macho vilivyo huku akiendelea kutoa matusi makubwa na mazito. “…na leo ndio utanitambua vizuri..? yaani siku ya nne leo huonekani cha nyumbani wala hujui hata watoto wanaishije huko..? Wewe kazi kuendesha hiki ki teksii chako tena bila hata haya unaongea tu na wanawake shenzii kabisa wewe mwanaume..!” Nilishusha pumzi huku nikinyanyua mkono wangu wa kulia nakushika kifua changu huku nikijihisi mapigo yangu ya moyo yalivyokuwa yakiendelea kunitoka. Nikatoa kitambaa nakuanza kujifuta futa jasho lilikokuwa limeshaanza kupenyeza kwenye uso wangu nakupitilizia shingoni. Kumbe yule dererva teksi niliokuwa naye ndio alikuwa akiongeleshwa na mke wake sijui. Aibu kubwa ikanijaa ghafla Tina mimi nakufikiri kuwa kumbe ningeumbuka kama ndio angekuwa mke wa mchungaji James. “..Naona hapa tena hamna safari..?, embu ngoja nitafute usafiri mwingine…” Niliondoka zangu nakuwaacha pale yule dereva teksi na mke wake wakiendelea kugombana. Nikatafuta teksi nyingine ambapo ilinifikisha mpaka stendi kubwa ya mabasi. Umati wa watu ulikuwa umefurika ndani ya stendi hii ya mabasi huku kila mmoja akiwa yuko ‘bize’ si kwa kubeba mizigo yake bali kwa purukushani za hapa na pale za kugombea tiketi. Nilijisogeza mpaka eneo la karibu na basi la ‘Mohammedi trans’ ambayo ni mabasi maarufu sana kwa safari ziiendazo dar es salaam. “.. Nauli ya hapa mpaka dar shilingi ngapi..?” “..nauli yake shilingi elfu thelathini na nane tu..” Nilichomoa hela kwenye suruali tena hela zenyewe zile nilizokuwa nimeziiba baada ya kufanya mauaji ya mchungaji James. Nikatoa shilingi elfu arobaini na kumpatia yule mkata tiketi. “.. nipe tiketi moja..” “..ya lini..? maana za leo mpaka kesho zote zimejaa…” “..zimejaa..?” “..ndio dada. Zimejaa na hapa unavyoona wanafunzi wengi wa vyuoni haswa wale wa chuo cha Mtakatifu Agustino na chuo cha biashara ndio wamefunga hivyo tangu juzi mabasi yanawabeba wao wanafunzi tu..” “..Ooooh Mungu wangu..!! sasa nitafanyaje jamani na nahitajika Dar es salaamu leo leo hata niingie saa ngapi..?” “..labda usubiri basi letu jingine linatokea Kigoma litapita hapa hivyo kaa pale usubiri..” Kidogo akili yangu ikakaa sawa nakusogea mpaka eneo la kupumzikia abiria nakuanza kusubiri. Ilinichukuwa kama masaa mawili kusubiri huo usafiri wa kutokea Kigoma. Bado hakukuwa na dalili zozote wala hata taarifa zinazotia nguvu juu ya hilo basi litokalo huko kigoma. Jua kali lililochora kivuli kikubwa chini ilimaanisha dhahiri kuwa itakuwa tayari imetimu mchana tena ule mchana wakuanzia saa sita nakuendelea maana jua lilikuwa kali sana. Nilikiwa bado nimezubaa mwenyewe mara ghafla nikahisi kama kuna mtu ananigusa mgongoni taratibu. Sikutaka hata kugeuka kwani niliamini kwa asilimia zote huenda atakuwa ni mdudu ama kweli kuna mtu. Nilichukua mkono wangu wa kulia nakuanza kupapasa papasa kwa nia yakukitoa kitu kinachonigusa kwa begani. Kadri nilivyozidi kukitoa ndipo kilizidi kunibonyeza kwa nguvu na kwa sasa nikaanza kuisikia na muambatano wa sauti ya kike kwa mbali. ”..Samahani dada naomba kukuuliza kitu..?” Alikuwa Mmama mwingine na ni mgeni machoni mwangu kwani hata sikuwahi kumuona maishani mwangu. Sura yake pana iliyokuwa imeng’arishwa na manukato ya zile losheni zinazopendwa na baadhi ya kina dada wa uswahilini na waliokuwa na kipato kidogo. Zile zinazojulikana sana kwa kubadilisha sura yako ya kutoka weusi nakuwa weupe. Wengi wanapenda kuiita ‘carolite’. Na kwa sasa harufu ile ya carolite ilikuwa inapambana na pua zangu zilizokuwa zimenasa harufu hiyo kali na inayochukiwa na baadhi ya wanaume wenye pesa zao. Niliendelea kumtolea macho huku nikijipa maswali mara mbili mbili ndani ya ubongo wangu nakuona sasa huyu huenda ndio akawa Mke wa mchungaji James kweli. Nilimkazia macho nakumjibu. “..uliza tu mama yangu..?” “..haya..! Ujue nakufahamu sana binti japo wewe huwezi kunikumbuka mpaka nikukumbushe..?” “..ni kweli unayosema mama..!” Woga tayari ulishaninyemelea Tina mimi nakuona sasa haya ni majaribu haswa ya dunia. Nilikuwa mpole ghafla nakujidai mtakatifu tena Yule wa kanisani kabisa. Nilijinyenyekeza huku nikimtolea macho na kutega maskio yangu kwa kumsiliziza kwa umakini mkubwa. “..nimekufuatilia muda mrefu.., kwanza kabisa pole na matatizo yaliokukuta kule tuliposafiri wote ikiwa ni pamoja na ajali tuliokuwa tumeipata..” “..pole ya nini tena Mama. Mbona mimi sijasafiri nina muda mrefu nahii leo ndio kwanza nasafiri kuelekea Dar..?” “..wala usitie shaka na mie. Mie nilikuwa mmoja wapo katika lile basi tulikuwa tumesafiri nalo jana kutoka Dar, na nakumbuka kabisa ulipandia kijiji fulani hivi japo kwa jina sikikumbuki na hapo ukapata siti tena kwa bahati nzuri ukakakaa na mchungaji mmoja hivi anaitwa mchungaji James..” Akili yangu ikawa haitaki kabisa kukubaliaana na ukweli aliokuwa anaendelea kuongea huyu Mama. Sura yake kila nikiivutia kumbukumbu bado ilikuwa ni kazi kuikumbuka. Nilichokifanya niliendelea kumkana kama vile Yuda alivyomkana Yesu mara tatu.. “..wewe Mama utakuwa umenifananisha mie..?, embu niondokee hapa..!! Kwanza unavyoendelea kukaa na mimi, hiyo mikarolite yako inazidi kuharibu pua zangu..?” Nilijifanya nimekasirika nakumgeuzia kibao yule Mama. Umati wa watu ukaanza kujaa katika eneo nililokuwa nimekaa na huyu Mama ukinizunguka. Yule Mama aligeuza macho yake huku na huku kana kwamba kafumaniwa ama ameona kitu cha ajabu sana kwangu. “..nakupa dakika moja tu na wala siendelei.. Jibu ndio au hapana..?” kwa muda huu yule mama alikuwa amebadilika sura na sauti nakuwa mbogo kwa muda. Kigugumizi cha ajabu kilichoambatana na kwikwi kali kikaanza kunishika Tina mimi huku nikiwa sina ujanja tena. Nikiwa bado najiandaa kumjibu yule Mama akanishika kwa nguvu ile blauzi yangu nakuanza kuropoka. “..sasa utaeleza vizuri kwanini umemuua mchungaji wetu tena mchungaji James tuliokuwa tukimpenda sana kwa mahubiri yake..?” Maskini Tina mimi nilijikuta nimeshaingia matatani tena, nilijitahidi japo kuzirudisha kumbukumbu kumtambua huyu Mama. Ndipo nikakumbuka kuwa jana wakati nipo safarini siti moja na marehemu mchungaji James aliniambia kuwa nilizimia mara mbili wakati ananiombea na tena wakisaidiana kuniombea na Mmama ambaye alikuwa mtu wa Mungu. Nilihuzunika sana nakuanza kuilaumu nafsi yangu kwa kutokufikiria. Nikiwa bado kwenye mawazo huku watu wakinishangaa mimi na huyu Mama. Mara huyu Mama akatoa sauti ya kuamuru kitu. “.. jamani mapolisi binti mwenyewe ndio huyu hapa..!!, mchukuweni tumpeleke kituoni..” Kumbe na mapolisi walikuwa wamenizunguka eneo lote nililokuwa nimezungukwa na watu ambapo walikuwa wamevalia nguo za kiraia. Walinichukuwa nakunipiga pingu huku umati wa watu ukinisikitikia kwa kitendo nilichokifanya cha kumuua mchungaji wao mchungaji James..****“..inuka twende hukoo..!!, husikii..?” Machozi yangu hayakuwa mbali na uso wangu. Yalianza kunibubujika huku nikijifanya mbishi na king’ang’anizi wa kutokuinuka pale kwenye benchi. Ule umati wa watu ukazidi kuongezeka mara mbili yake nakuanza kupiga makelele ya kuwachochea wale mapolisi huku baadhi yao wakiangua vicheko vya hapa na pale. Sasa Tina mimi nikawa sina ujanja zaidi yakuendelea kushikilia benchi lile la kukalia wageni nikibakiwa na butwaa. “..jamani, sio mimi niacheni..?, mmenifananisha jamani..?” “..akufananishe nani mshenzi mkubwa wewe..? na leo ndio utaenda kuozea jela Malaya wewe..?” Nilijikuta mwili wangu wote unakosa nguvu huku mapolisi wakinibeba juu juu kama vile mzoga wa mnyama tena mnyama mkubwa. Walinipiga kwa ubishi wangu wakugoma kunyanyuka kisha wakaniingiza ndani ya gari yao ya kipolisi huku ule umati wa watu pale stendi ukiwa pamoja nao kunisindikiza kwa makelele na vicheko na baadhi kuhuzunika na nadhani walikuwa wakimpenda sana mchungaji James.

“..kama kufa wacha nife leo leo tu..! Sitapenda nikaozee jela angali bado kijana hivi..?” Nilijisemea kwa sauti ya chini chini nikiwa ndani ya ile gari ndogo ya polisi huku baadhi ya polisi wakiwa wamenizunguka chini ya ulinzi mkali na mikono yangu ikishikamana vya kutosha na pingu. Zile nguo zangu zote nilizokuwa nimezivaa nilihisi kama zimelowa tena chapa chapa na si kwa maji bali kwa jasho na kojo lililokuwa likinitoka ovyo kwa woga wa hali ya juu likiendelea kupenyeza ndani ya nguo zangu zoote. Kila mtu alikuwa akiendelea na shuguli zake. Hakukuwa na baridi sana na wala jua lilichelewa kutoka. Mawingu yaliendelea kuvutana nakuashiria dalili zote za kushuka kwa mvua lakini upepo mkali uliokuwa ukivuma kutoka mashariki kwenda magharibi ndio uliosababisha kukatisha mvua. Makaratasi pamoja na risiti za mabasi zote zilikuwa zimejaa mavumbi yaliosababisha na huu upepo uliojaa vumbi. Milango pamoja na madirisha navyo havikuwa mbali katika kupiga makelele. Kwa sasa macho yangu yalikuwa yamenitoka na niliangaza huku na huku ilikuvuta japo kumbukumbu kujua ni sehemu gani hapa nilipo. Nilijiangalia tena mara mbilimbili nguo zangu kama zimelowa lakini ndio kwanza zilikuwa kavu tena zilizojaa ubaridi. “..Dada..?, basi limeshafika vipi huendi tena..? basi hilo hapo mbele yako limetokea Kigoma..” Amani na furaha tele iliniingia ndani ya moyo wangu nakuanza kuamini kuwa kumbe vyote vile nilivyonitokea muda si mrefu haikuwa kweli bali ilikuwa ni ndoto. Eti mpaka mmama mmoja akanijia tena pamoja na mapolisi wakanichukuwa nakuacha umati wa watu ukipiga makelele kwa vicheko. Nilijisachi vizuri mifukoni mwangu kuangalia kama zile hela nilizochukuwa kwa mchungaji James bado zipo. Kwa bahati nzuri zote zilikuwepo. Nilitoa shilingi elfu thelathini nakumkabidhi konda kisha akanikatia tiketi ya kuelekea Dar es salaam. Njia nzima hadi tunafika Singida bado nilikuwa sijiamini amini Tina mimi. Ndoto niliyokuwa nimeiota ilishanijenga tena vibaya ndani ya halmashauri ya ubongo wangu nakuona sasa nipo katika wakati mgumu. Sikutaka tena kufumba macho kwani niliamini nitaanza tena kuziota zilie zile ndoto mbaya na nitaumbuka humu kwenye basi Tina mie. Siti niliyopata ilikuwa ni ya dirishani na tena nilikuwa peke yangu kutokea Mwanza mpaka tulipofika Dodoma ndipo abiria mwingine akapanda na kukaa pembeni yangu. Alikuwa ni Mmama tu na tena alikuwa na mtoto mdogo anamyonyesha. Mwili wangu wote ukaanza kunisisimka kila nikimwangalia yule mtoto. Alikuwa ni mzuri sana kuanzia macho yake, masikio na hata mdomo wake. Kila mama yake alivyokuwa anambembeleza ndivyo na mie nilikuwa nazidi kusisimka mwili. Hisia kali zilinivuta mpaka nikakumbuka kwa jinsi nilivyoathirika na ukimwi na tena kuhusu kupata mtoto nisahau kabisa milele yote kama alivyoniambia dokta. “…Jerry..?? Jerry..?? Kwanini Jerry umenifanyia hivi mie..?? Kwanini..?” Taaratibu wimbi la matone ya machozi likaanza kunidondoka huku nikiendelea kumwangalia Yule mtoto. Ni Jerry ndio alioaharibu maisha yangu yote japo ni tamaa zangu za mwili ila amechangia kwa kiasi kikubwa kuniharibu kimaisha na kimasomo kwa ujumla. Kwanza yeye ndie alieniambukiza ukimwi. Pili ndio alionisababisha mpaka kwa hasira niache masomo nakuanza kudili na ndugu zake nao kuaambukiza. “..alaaniwe Jerry huko alipo..!! Na ole wake nikifika Dar..?” Nilijikuta uzalendo umenishinda nakuanza kuropoka ndani ya basi. Kitendo changu cha kuropoka japo kwa sauti ya chini chini kilinifanya nianze kujishtukia lakini kumbe hakukuwa na mtu yeyote aliyeniangalia ama kunishtukia. Hata yule mama ndio kwanza aliendelea kupekuwa pekuwa vitu vya mtoto wake vizuri nakuvipanga. Mwendo wa masaa matano na nusu tulikuwa tumeshapapita Morogoro na kwa muda huu tulikuwa tukiitafuta Chalinze. Akili yangu yote sasa nilikuwa nimeielekeza kwa Jerry ambaye ndio chanzo cha kuharibu maisha yangu kwa ujumla. ”..nitahakikisha nimemuua mmoja mmoja kama nilivyomuua mchungaji James..” Niliongea kimoyo moyo huku nikiikaza sura yangu kwa hasira ya hali ya juu. Kwa muda huu yule mtoto mchanga aliyekuwa akilia alikuwa ameshapitiwa na usingizi mkali. Yule mama alikuwa kimya akijisomea kitabu chake huku akihuziunika na kucheka hapo hapo kwa alichokuwa akikisoma. “..mmhh kwa kweli hii hadithi ni nzuri sana sijawahi kuona..” Alinigeukia nakuniongelesha huku akiwa kaendelea kushikilia kitabu kile cha hadithi. “..kwani kikoje..” “..kinaitwa ‘SITAKI TENA’ yaani hadithi ya humu ndani mhh..” “..ikoje kama za shigongo..” “..hapana hii ina muundo fulani hivi lakini inavutia na kuteka hisia zangu. Tangu nimeanza kuisoma nyumbani Dar es salaam bado sijaimaliza na haipiti muda naendelea kuisoma tena, nimekuja huku Dodoma njia nzima bado naendelea tu kuisoma na ndio kwanza bado kurasa kama arobaini ndio niimalize. “..inaonekana ni ndefu eenhh..?” “..anhh ndefu sana..!!, ni ‘novo’ kabisa hii. Yaani kuna binti humu ndani anaitwa Levina. Maskini amepata shida toka mdogo mpaka amekuwa bado anaishi katika mazingira magumu tu..” Kuanzia Chalinze njia nzima ikawa ni yule mama ananihadithia ile hadithi ya Sitaki Tena. Nilianza kutekwa hisia zangu kwani baadhi ya matukio aliyokuwa amefanya yameendana na mimi kabisa. “..enhee ikawaje sasa huyo Levina..” “..yaani hadithi inavyoanza Levina akiwa bado mdogo sana anacheza rede na wenzake na kwa bahati mbaya na haraka haraka kimchezo, Levina anaokota jiwe nakumrushia mwenzake huku akidhania ni mpira. Basi lile jiwe linamfikia mwenzake kwa nguvu nakujikuta mwenzake akikata roho pale pale. Sasa hapo ndio hadithi inaanza sasa..” “ennhh, nipe uhondo japo kidogo..” “..mkasa unaanzia anapelekwa rumande. Huko mapolisi wa zamu wanambaka na kuharibu usichana wake. Kesi yake ilikuwa inasua sua kwani baba yake alipoteza nguvu ubavu mzima kwa mshtuko hivyo kitendo cha kufuatilia kesi kikawa chini ya mama yake na baadhi ya mawakili waliokuwa wanamsaidia. Mwisho wa siku levina akatumikia kifungo cha maisha gerezani..” “..Mungu wangu..!!, ikawaje sasa..?” “..hakukuwa na ujanja tena ikabidi asafilishwe mpaka kwenye gereza la watoto watukutu la mbeya amabapo ndipo maisha yake yakaanza upya..” “..pliiz..!! pliiz..!!, nakuomba uniazime niendelee kupata uhondo halafu tukifika Dar es salaam nitakuachia, wewe si cha kwako,?..” “..usijali..!!, chukuwa, endelea hapa nilipomaliza kukuhadithia..” Akili yangu yote ikawa imebadilika vya kutosha. Mawazo yangu yote nikayahamishia kwenye hii hadithi ya ‘SITAKI TENA’ iliyokuwa imetungwa na mwandishi maarufu na ninayempendaga siku zote ‘ANDY RYN.’ Nilishawahi kusomaga hadithi zake kipindi cha nyuma facebook ila hii sijawahi kuisoma. Mwendo wa masaa mawili na nusu ulinitosha sana kuisoma hadithi robo nzima ya kile kitabu huku nikitamani kujua mbeleni. Sikuwa na ujanja tena kwani tulikuwa tumeshaingia ndani ya hili jiji la Dar es salaam. Giza lilikuwa limeshatanda muda mrefu tu kuashiria kuwa ni usiku japo sikufahamu ni usiku wa saa ngapi. Nilimkabidhi yule mama kitabu chake. Alikuwa na mizigo mingi chini ya basi hivyo akaniomba nimshikie mtoto wake na mkoba wakati wakushuka ili ahakikishe mizigo yake asije akaibiwa. Kwa upande wangu sikuwa na mzigo wowote hivyo nikamsaidia kubebelea mkoba wake na mtoto wake nikambeba kifuani kama mwanangu vile kisha nikaongozana na huyu mama kushuka. Kitendo cha kutangulia kushuka yule mama akapokelewa na mwanaume huku akikumbatiwa. Halmashauri yangu ya kichwa ikafanya kazi haraka haraka nakutambua kuwa inawezekana akawa ndio mumewe. Sikumuona vizuri usoni kwa sasabu ya kukumbatiana na yule mama pia giza giza na mwanga ulikuwepo kidogo tena ile wa ndani ya basi japo kwa sauti zao ndizo ziliweza kupenyeza ndani ya ngome ya masikio yangu. “..mwanangu Brayan yuko wapi..?” “..Si huyo hapo amembeba huyo dada..?” Aliongea yule mwanaume kwa sauti ya ukali naya nguvu akimuuliza mkewe huku akiacha kumkumbatia nakuangaza huku na kule ndipo jicho lake likakutana moja kwa moja na langu. “…Tinaaa..? wewe si Tina wewe..?” Alikuwa ni yule yule mvulana niliokuwa nikimchukia maishani mwangu na ndio yule aliyenipotezea malengo yangu ya kimaisha yote. Si mwingine bali alikuwa ni Jerry. Na kumbe huyu alikuwa ni mtoto wake. Nilijiuliza maswali mengi papo hapo japo sikupata jibu kwani ninavyokumbuka kuwa Jerry aliambiwa kuwa hawezi kumzalisha mwanamke kutokana na kwanza kuathirika na ukimwi na pili tulishawahi kumkata kata nanii yake na viwembe mimi na rafiki yangu Aisha na tulihakikisha tumeikata mirija yake yote inayopitisha mbegu za uzazi na hadi akazimia na kuwahishwa hospitali kipindi cha nyuma. “..Tina mlete mwanangu nimesema..?”

Kwa sasa Jerry alikuwa amebadilika nakuwa mkali sana huku akinisogelea karibu. Mke wake alikuwa akimvuta kana kwamba aniachIe nakuwa mimi ni mtu mzuri tu tangu nimetoka naye safarini. Kila wakijibizana Jerry na mkewe ndipo na mimi nikapata nafasi ya kuwazunguka mpaka kwenye basi jingine nikalizunguka tena basi jingine nakuwatoroka pale pale pale huku nikiwa nimemshikiria mtoto wao. “..ama nife mimi Tina..!, au Jerry..! sitamrudisha huyu motto kamwe..!!” Nilijisemea kwa sauti ya chini chini huku nikitokomea mpaka kwenye geti la nje kabisa na nilipofika nje kabisa ndipo kwa mbaali nikasikia tangazo kuwa kuna dada ametoroka na mtoto na amevaa suruali ya jinsi akiwa na mkoba mweupe. Eti akamatwe popote alipo humu ndani ya stendi.. “..It’s too late Jerry..!! (Jerry umeshachelewa..!!)” Niliongea kwa kujidai huku nikipanda dalaladala yakuelekea Mbagala na nisijue naenda kwa nani na wala itakuwaje huko nieandapo na huyu mtoto.. Ile hali ya woga na kutetemeka ilishaanza kutoweka ndani ya akili na mwili wangu kwa ujumla. Na sasa akili yote nilikuwa nimeielekeza ni jinsi gani nitaishi na huyu mtoto huko niendako. Nilijiona mtu tofauti sana kutokana na kuwa na mtoto japo si wakwangu lakini kwa jinsi nilivyokuwa nambembeleza akilia hata akicheka. Nilikuwa nacheka naye kila abiria allikuwa akinishangaa nakuona ni jinsi gani nilivyokuwa na kipenzi na mtoto wangu japo ukweli si mtoto wa kumzaa mimi. Ilinichukuwa kama lisaa mpaka kufika Temeke. Japo daladala ilikuwa inaelekea mbagala lakini kwa upande wangu kutokana na kuchoka sana mwili na pia mtoto alikuwa kashajisaidia hivyo nilitakiwa nimbadilishe nguo nikaamua kushukia Temeke nakutafuta gesti ya bei nafuu uswahilini. * ‘Mji mwema guest house’ ndio gesti niliokuwa nimefikia Tina mimi na huyu mtoto wa Jerry niliomuiba. Kwa sasa alikuwa amelala hivyo nilipoingia tu chumbani nilimvua nguo zote kisha nikaifungasha vizuri ile pampasi yake iliyokuwa imejaa kinyesi pamoja na mkojo nakuiweka katika mfuko wa rambo nakuvitupia kwa pembeni. Nilipomaliza kumsafisha nilichukuwa pampasi ya akiba ambayo ilikuwa katika huu mkoba mkubwa niliouchukuwa kwa mama yake na huyu mtoto. Usingizi ulikuwa wa shida sana kwangu nadhani hii yote ni kutokana na kuchoka sana mwili na hata akili yangu. Mawazo mengi niliokuwa nayo na mipangilio yangu ya baadaye kuhusu huyu mtoto ni kati ya vitu ambavyo bado vilisumbua sana katika halmashauri ya kichwa changu. Nilifanikiwa kuupata usingizi kwa tabu sana na nilipokuja kushtuka usiku wa manane napo sikuwa na saa wala simu hivyo sikuweza kugundua imetimia muda gani lakini giza bado lilikuwa ni tororo. Mtoto alikuwa anakoroma kuashiria kuwa alikuwa na usingizi sana. Nilitamani japo kupata tena usingizi kwa mara ya pili lakini bado kichwa changu kikaendelea kuwa na mawazo mgando ya kumuwaza Jerry kwa vitendo alivyowahi kunifanyia kipindi cha nyuma. “..Piga ua.! Lazima nije kumtafuta Jerry na nimuue kabisa kwani adhabu ya kumchukulia huyu mtoto wake haitoshi.. yeye ndio aliofanya mpaka nimepoteza ramani ya maisha yangu kwa ujumla..” Nilijikuta naropoka mwenyewe kitandani nakufanya mpaka mtoto ashtuke nakuanza kulia. Nilimtoa pale kitandani nakuanza kumbembekleza lakini haikusaidia kitu zaidi ya kuzidisha kulia zaidi. Nilimchukulia japo ile nyonyo yake ya kunyonyea maziwa ambapo ilibakiwa na vimaziwa kidogo alivyokuwa amevihifadhi mama yake kwenye mkoba lakini bado haikusaidia kitu chochote. Machozi yalikuwa mengi sana nakunisisimua mwili mzima kila nilipokuwa nikimwangalia huyu mtoto. Alibadilika mwili nakuwa mwekundu kutokana na kulia kwa muda mrefu. Nilijitahidi kumbembeleza hata kwa kutoa maziwa yangu nakumdanganyishia kama namnyonyesha ndipo akanyamaza nakuanza kunyonya maziwa yangu ambayo kiukweli hayakuwa yakitoa chochote. “..Sasa huuuuyu mtoto nimuite jina gani..?” Nilibaki nimeduwaa mwenyewe huku nikijisikia raha kwa kunyonywa maziwa yasiotoka na kale katoto mpaka akapitiwa tena na usingizi. Nilijiuliza maswali mengi sana juu ya jina la huyu mtoto kwani Jerry mara ya mwisho alimuita Mama yake na huyu mtoto ‘Mama Brayan’ hivyo moja kwa moja huyu mtoto ndio atakuwa ‘Brayan’. Lakini kwa upande wangu inanibidi nimbadilishe jina huyu motto haraka iwezekanavyo. “..Adrian..!!, Adrian..!! yeees..! nitamwita Adrian tu haina hata ulazima wa kumuita jina la nyumbani kwetu kwani mtoto si damu yangu..?” Niliongea kimoyomoyo huku nikijitandikia vizuri shuka nakujilaza tena kitandani tayari kwa kuutafuta usingizi kwa mara ya pili. ~ BAADA YA WIKI TATU ~ Mtoto Adrian nilishamzoea na nilishamchukulia kama moja ya mtoto wangu wa kumzaa. Pale gesti wahudumu wote wakajua ni mtoto wangu na hata wakanipa jina la Mama Adrian. Uchangamfu wangu wa kuongea na kila mtu ni kati ya vitu ambavyo viliwavutia wengi. Zile hela ambazo nilizichukuwa kwa Mchungaji James nilipomuua kwa sasa zikawa zimeniishia, si kwa kula tu bali hata kwa matumizi ya huyu Adrian. Ilifika kipindi natumia hadi elfu kumi na tano kwa ajili ya matumizi ya mtoto tu. Ilinibidi kila siku niwe na pampasi tatu hadi nne na kopo zima la maziwa ya ng’ombe kwa ajili ya kumnywesha. Sikutaka kujihusisha na marafiki wa mbali nahii gesti kwani niliamini ndipo kujulikana kwangu mpaka kwa Jerry. Habari za nyumbani kwa Baba na Mama yangu sasa nikawa nimezisahau kabisa. Nilianza maisha ya kujitegemea mimi kama mimi tena bila ya kuwa na msaada wowote huku asililimia mia nikiamini endapo baba au mama yangu akagundua kuwa sipo chuoni muda mrefu ataumia sana. Sasa akili yangu yote nikaielekeza katika kufanya mapenzi na watu tofauti tofauti ili tu nipate chochote cha kuniwezesha kujikimu mimi na huyu Adrian. Kuna kipindi nilikubali hata kuingiliwa kinyume na maumbile ili mradi tu nipate chochote na hata wanaume wengine walikuwa wananiingia hivi hivi bila hata ya kutumia kondomu na hata kunilipa. Siri kubwa tatu ndizo zilikuwa zimekaa kichwani mwangu kama sheria na kiapo cha kutokumwambia mtu yeyote mpaka mwisho wa uhai wangu. Siri ya kwanza ni juu ya huyu mtoto si wangu ila wote wanatambua kuwa ni wangu. Siri ya pili ni kuwa hapa nilipo nimejificha na nilishawahi kufanya mauaji hivyo ni wazi natafutwa huko Mwanza na pia natafutwa na Jerry na mkewe juu ya huyu mtoto wao niliotoroka naye. Na siri ya mwisho inayoniumiza sana akili yangu ni juu ya ugonjwa huu wa ukimwi. Ni kweli nimeathirika japokuwa dalili zake sijazipata bado lakini mara ya mwisho niliambiwa hospitali kuwa nimeathirika. Na ndio siri iliyonifanya hata nishindwe kuendelea na masomo kwa kuchanganyikiwa na pia hata niwafiche ndugu, wazazi hata na marafiki zangu wote wanaonifahamu. “..Binti leo nina buku tano tu..” “..Twende tu haina shida ila tunatumia kondomu..” “..aanhaa..!!, kondomu ya nini..?” “..hheee..!!, we vipi..? basi niongezee ziwe elfu kumi twende bila kondomu..” Alikuwa ni mzee mzima kabisa ambaye ana uwezo hata wa kunizaa, na kwa muda huu alikuwa meshazoea kuja kufanya mapenzi na mimi kwa kutumia kondomu sasa leo naona kaja kivingine kabisa na anataka twende naye bila kutumia kinga. Tulikubaliana naye nakuelekea mpaka chumbani kwangu nilipopanga ambapo nilimchukuwa Brayani nakumlaza chini kisha nikapanda kitandani nakuvua nguo zangu zote nakubakiwa na shanga tu kiuononi kwa ajili ya kuwadanganyishia wanaume wapenda ngono. “.. haya nipe changu kabla..?, huna navaa nguo hakuna kufanya chochote..?” “..hilo tu..! ondoa shaka..!!” Yule mzee hakuwa mbishi, alichomoa noti ya shilingi elfu kumi nakunipatia. Niliichukuwa nakuiweka kwenye nguo za Adriani pale chini kisha nikamfuata huyu mzee mpaka kitandani. Nilianza kwa kumchezea kifuani kwake. Hakutaka kuchezewa sana kwani haja yake nikufanya tu mapenzi na mimi hivyo akajiandaa tayari kwa kufanya mapenzi. Akiwa kishavua nguo zote mara tukasikia mlio wa simu yake ikiita.. “.embu naomba simu yangu hapo kwenye suruali..”

Alinituma nimtolee simu yake. Haraka haraka nikainuka na kwenda kumtolea na kisha kumkabidhi.. ile nampa tu simu ikakatika. Akaiangalia namba nakuizima kabisa kisha akanigeukia kwa tabasamu nakuanza kufanya mapenzi na mimi. Nilimuonea huruma sana kwakuwa nimeshaathirika hivyo nilimuona kuwa naye anapoelekea ni huko huko. Kutokana na tamaa zangu za pesa hata sikutaka kumzuia alifanya atakavyo na alipomaliza tu cha kwanza. “..unataka kuongeza..?” Nilimwambia kwa sauti ya taratibu na ya kimahaba huku nikimrembulia macho. Yule mzee alitaka tena hivyo akachukuwa suruali yake akaniongeza elfu kumi nyingine napo tukaanza tena kufanya mapenzi kwa mara ya pili. Tukiwa katikati ya mapenzi mara mwanangu Adrian akaanza kulia kwa sauti yake ya juu. Sikutaka kumbembeleza mpaka nimalizane kwanza na huyu mzee. Hivyo tukaendelea tena lakini kwa safari hii mwanangu Adriani ni kama alikuwa amezidisha kulia kwa sauti ya juu. Bado sikutaka kwenda kumbembeleza. Tukiwa tupo katikati ya mahaba mara tukasikia hodi inapigwa Mlangoni kwangu. Ilipiga kwa nguvu kuashiria kuwa mtu anahasira au anataka kitu cha haraka. Hakukuwa na sauti nyingine yeyote zaidi ya kulia sana kwa mwanangu Adrian na yule mtu kuendelea kupiga hodi kwa nguvu. Nilichokifanya nilimfanyia yule mzee ishara ya kumnyamazisha kwa kutumia kidole changu kukiweka mdomoni, kisha nikamchukua mwanangu Adriani hivyo hivyo akiwa analia nakumtupia uvunguni mwa kitanda na baada ya hapo nikaelekea moja kwa moja mpaka mlangoni tena kwa kujiamini huku nimejifunika khanga nakuufungua mlangu nusu. “eenhe unasemaje..?” Uso wangu kwa sasa ukawa umekutana moja kwa moja na Mmama ambaye sura yake si ngeni kabisa machoni mwangu huku akibubujikwa na machozi yalioambatana na kwikwi na nilipomuuliza tu kuwa anasemaje. Pale pale alinisukuma nakuingia mpaka chumbani kwangu kwa nguvu… *** *** Unavyodhani huyo Mama nii yupi..? Na Tina atafanyaje..? *** Nini hatma ya Tina kimaisha..?

ITAENDELEA

Play Gal (Tina Zoa Zoa) Sehemu ya Tano

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment