Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Pili
CHOMBEZO

Ep 02: Dokta Mimi Siumwi Huko

SIMULIZI Dokta Mimi Siumwi Huko
Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Pili

IMEANDIKWA NA: 2JIACHIE

*********************************************************************************

Chombezo: Dokta Mimi Siumwi Huko

Sehemu ya Pili (2)

“Mimi Sulee, una akili kweli au? Kwa nini unifikirie hivyo jamani?”

“Akili ninazo tena nyingi sana Monica. Sasa ile kukurukakara ya viti kutoa mlio ilikuwa nini? Ndiyo matibabu yenyewe?”

“Sasa je? Madokta we Sulee unawajua, wakimpima mwanamke mara wamshike makalio, mara watamani kumbusu, kama hukutumia akili yako unaweza kujikuta umemalizwa.”

“Mh! Mi siamini Monica.”

“Kwa nini huamini? Kwanza naomba nikuulize Sulee, umekuwa ukiniwekea wingu kuonana na dokta, kwani ni nani yako?”

Sulee alishtuka kwa swali hilo hasa alipokumbuka kwamba, mumewe na mume wa Monica ni marafiki na wao pia ni marafiki. Mambo yanaweza kufika mbali…

“Mi nimeuliwa tu, si nani wangu wala nini!”

“Sasa ni kwa nini umenitolea mimacho kwamba nimetembea na dokta kisa ulisikia viti vikilialia ndani?”

“Maana yangu usije ukamsaliti shemeji.”

“Mmmh! Au wewe siku ulipotembea naye mliliza viti? Sema ukweli Sulee.”

Ilibidi Sulee acheke ili kupoza mambo, akabalaguza kwa kuanzisha hoja nyingine kabisa nje ya hiyo.

Lakini Monica alishapata ujumbe, aliamini kuna kitu kati ya Sulee na Dokta Kisarawe…

“Amekupa dawa lakini?” aliuliza Sulee.

“Ndiyo, amesema nitumie hizo kisha niwasiliane naye.

Walifika kwanza nyumbani kwa Sulee, baadaye Monica akaenda nyumbani kwake.

Alifikia kwenye kiti akiwa amechoka sana kwa purukushani za Dokta Kisarawe…

“Lakini kama asingetumia nguvu walahi vile asingenipata, ana bahati sana, kidogo nimpigie kelele…

“Lakini lo! Dokta anayajua mambo yule, sijui ni dokta wa mapenzi au wa mwili. Kama ofisini kwake tena chapchapu ni vile. Je, tungekuwa chumbani?” Monica alijikuta akiwaza mengi sana kuhusu dokta na mazingira yote yaliyotokea. Ilikuwa mara yake ya kwanza kumsaliti mumewe na akahisi kuna tofauti kubwa kati ya mumewe na Dokta Kisarawe.

“Kwanza mume wangu hana pawa sana kama dokta. Halafu mume wangu utadhani hahemi, dokta anatoa mhemo mpaka unajua mwanaume yuko kazini,” alisema moyoni Monica.


Dokta Kisarawe alikaa kwenye kiti akimuwaza Monica…

“Huyu mwanamke ni mzuri sana kuliko wengine. Da! Bonge la mwanamke. Sijawahi kukutana na mwanamke mzuri kama huyu, ngozi nzuri, laini, hana kipele wala manundunundu kama wengine,” aliwaza moyoni daktari huyo ambaye inawezekana mpaka kwa Monica ni mwanamke wa mia mbili tangu aanze kutoa tiba.


Usiku wakiwa kitandani, mume wa Monica ndiye aliyeanza mazungumzo…

“Mke wangu, kwa dokta kuliendaje leo?”

Monica moyo ulimlipuka, alihisi aliulizwa swali lile kwa maana kwamba mumewe amesikia alitembea naye palepale kazini.

“Kwani vipi mume wangu?” Monica aliuliza kwa sauti ya chini.

“Ulikwenda hukwenda?”

“Nilikwenda dear.”

“Si ndiyo nakuuliza kulikuwaje?”

“Ooo, alinipa dawa akasema nitumie nikimaliza nirudi kumwambia.”

“Basi, tusubirie. Asubuhi unioneshe hizo dawa.”

“Sawa.”


Nyumbani kwa Sulee, mumewe alikuwa akilishikashika tumbo la Sulee akijifanya ndiyo anaulea ujauzito huo kwa mapenzi ya dhati…

“Natamani uzae hata leo mke wangu.”

Sulee alicheka huku moyoni akisema…

“Ungejua mtoto si wako, wala usingejipongeza, mwenzako mwenye nguvu za kusababisha mtoto ndiyo amehusika.”


Asubuhi, mume wa Monica akiwa ameshajiandaa kutoka kwenda kazini alikumbuka kitu, akamwita mkewe…

“Abee.”

“Nipe zile dawa.”

Monica alikwenda chumbani, akatoka na kipakti…

“Tena dokta alisema nikitaka kuzinywa lazima niwe nimekunywa chai ya kutosha,” alisema huku akimpa dawa hizo mumewe…

“Khaa! Mbona ni dawa mpya za mafua mke wangu, vipi kwani?”

“Dawa mpya za mafua?”

“Ndiyo. We hukumbuki siku zile mama alipokuja akawa anasumbuliwa na mafua nilinunua dawa hizi?”

“Mh! kweli? Kwani zile si zipo, ngoja nikazilete.”

Monica alikwenda kwenye bakuli kubwa la plastiki, akachakurachakura na kuona kipakti cha dawa hizo.

“Kweli mume wangu, si hizi hapa!”

“Si ndiyo sasa.”

“Mh! Ina maana Dokta Kisarawe kaniingiza mkenge siyo?”

“Haya, kumbe dokta mwenyewe anaitwa Kisarawe! Kisarawe si walaya ya mkoa wa Pwani, tangu lini likawa jina la mtu! Makubwa haya.”

Monica alifedheheka, akaanza kuhisi Sulee amemwingiza mkenge kwa kumpeleka kwa daktari feki na si yule aliyemsaidia yeye…

“Lakini kama ni feki, mbona pale nje palikuwa na wanawake wengine wengi tu tena wasiofahamiana na Sulee. Au..?” alishindwa kumalizia.

Baada ya dakika tano mumewe kuondoka, Monica alishika simu, akampigia simu Dokta Kisarawe…

“Dokta za leo, mimi Monica…”

“Ooo, Monica mpenzi, umeamkaje? Vipi, umenimisi my dear?” “Sikiliza Dokta Kisarawe…”

Enhe, nakusililiza baby.”

“Umenipa dawa gani?”

“Lini?”

“Jana.”

“Si za kusaidia kutunga mimba!”

“Mh! mbona ni dawa za mafua?”

“Sikiliza mpenzi wangu, mimi siwezi kukupa dawa sizo. We endelea kutumia hizo dawa halafu baada ya siku ishirini utaniambia matokeo,” alisema Dokta Kisarawe.

“Mh! Sijui, yangu macho.”

“Kwani uko wapi Monica mpenzi?”

“Nyumbani.”

“Unafanya nini?”

“Ndiyo nimeamka.”

“Naomba tuonane leo nje ya nyumbani kwako au nje ya hapa hospitalini kwangu.”

“Unataka nini tena? Jana si ulifanikiwa?”

“Nilifanikiwa lakini si kwa uhuru nilioutaka.”

“Uhuru gani? Kwani ulitaka uhuru au ulitaka kutimiza haja yako?”

“Haja na uhuru.”

“Kwanza nimegundua kitu, wewe na Sulee ni wapenzi, unabisha dokta?”

“Si kweli, kama mwenyewe Sulee amekwambia hivyo basi ujue ananitaka maana nilishawahi kuona dalili za kunitaka lakini nikampotezea, unajua lazima upende kilicho kizuri kama wewe.”

“Kwani mi mzuri dokta?” Monica alianza kulainika sasa, hata lugha aliyotumia iliashiria hivyo…

“Sana, Sulee atasubiri sana kwako.”

“Mmmh! Ya kweli hayo?”

“Mimi nakwambia ndiyo maana nimeomba tuonane na wewe nje ya nyumbani kwako au nje ya hapa kazini kwangu.”

“Saa ngapi?”

“Sema wewe unataka saa ngapi?”

“Mimi jioni siwezi kutoka kwani nakuwa naandaa chakula cha mista mwenyewe, muda wangu ni asubuhi mpaka kwenye saa sitasita hivi.”

“Basi tukutane asubuhi hii.”

Walipanga kukutana kwenye gesti ya Kivumbi na Jasho nusu saa mbele ambapo Monica palepale aliingia bafuni kuoga na kuvaa. Kwa vile ilikuwa ahadi maalum, Monica alivaa sana siku hiyo.

Alipigilia gauni jepesi la kufika magotini na hivyo sehemu kubwa ya mapaja kuwa wazi. Hakuacha pafyumu kwa kujipulizia kwa wingi.

Midomo aliichora kwa rangi nyekundu huku nyusi akizipunguza kwa staili ya kukatia na kusiliba kwa wanja.

“Hapa naamini dokta ndiyo atazidi kukubali uzuri wangu. Si amesema mimi ni mzuri kuliko Sulee. Leo atajua mimi pia ni mzuri kuliko Kleopatra wa Misri.”

Alibeba kipochi cha begani kilichokuwa na kanga pea moja ndani yake, akachukua Bajaj hadi kwenye gesti hiyo ambapo dokta alishafika kama dakika kumi nyuma.

Alisimama nje ya gesti akamtumia meseji…

“Nipo nje.”

“Ingia namba kumi.”


Monica alishaingia chumbani na alikuwa amelala kwenye mapaja ya Dokta Kisarawe akimkunakuna mgongoni huku akizidi kumsifia sana…

“Baby wewe umeumbika bwana, kama hujui naomba ujue sasa.”

“Kweli dokta?”

“Kweli kabisa.”

Kule kushikwashikwa kulimpandisha mashamsham Monica, akaanza kuchaji. Hata kuhema kwake kulibadilika, pozi zilikuwa na kutegatega. Yeye mwenyewe akatoka kwenye miguu ya kwa dokta na kusimama, akajivua gauni, akabaki na kufuli tu, dokta akabahatika kuona uzuri wa mapaja ya mwanamke huyo.

Naye alikurupuka, akasimama, akavua suruali huku akichekacheka kama fisi aliyeona mbuzi akikatizia jirani yake kule porini.

“Lakini leo lazima dokta utumie kinga.”

“Khaa! Monica unataka mimba hutaki mimba? Kinga ya nini tena wakati unasema hujawahi kunasa ujauzito?”

“Ndiyo, lakini sitaki ujauzito wa kwako au mwanaume mwingine nje ya mume wangu.”

“Unaamini yeye anaweza kukuzalisha?”

“Si umenipa dawa!”

Dokta Kisarawe alikosa cha kuongeza, akabaki amemkodolea macho mwanamke huyo lakini kutoka moyoni hakupenda kutumia kondom kwake.

“Please my dear, twende uwanjani bila viatu,” alisema dokta huyo huku macho yake yakiwa yanakosa nguvu polepole.

“Hapana dokta, siwezi, tutumie viatu ili nisichomwe na miba. Kama ni miiba nataka ya mume wangu tu.”

“Nikwambie kitu Monica?”

“Niambie dokta.”

“Ujue raha ya mchezo kama huu ni kuingia uwanjani pekupeku, mguu kwa mguu, nyasi kwa nyasi,” hapo sasa Dokta Kisarawe alikuwa amemsogelea Monica na kumshika, akamvutia kwake…

“Noo dokta.”

“Please, nikubalie Monica,” dokta alisema huku akisogeza midomo yake kwenye sikio moja la mwanamke huyo na kumpumulia kwa karibu hali iliyomchanganya Monica ghafla…

“Aaa…dokta…”

“Nini tena Monica jamani?”

“Acha!”

“Kwani unaumia Monica?”

“Dokta bwana, unaniteke…”

“Mmm, polepole Monica wangu,” alisema dokta kwa sauti nene huku akizidi kumhemea, maskini Monica alikosa nguvu ghafla na kulegea.

“Do…do…dok…taaa.”

“Ee.”

“Kwa…kwa…ni…ni..?”

Dokta Kisarawe alimbeba Monica na kumpandisha kitandani, akamfuatia kwa haraka ili asimtoe kwenye ile hali ya msisimko.

Kuanzia hapo, Monica hakusema tena, alimwacha dokta huyo afanye kila alichotaka na yeye alikuwa tayari.

Miguno ilimtoka kinywani mrembo huyo kila pasi ya mpira ilipopigwa kwake, macho yalijaa giza jekundu huku mwili ukiwa mwepesi hasa sehemu ya katikati ambayo inaruhusu mwili kujimega sehemu moja na nyingine, hasa juu kwenda kifuani na chini kwenda magotini.

Wakiwa wazimawazima, wote walijikuta wakitangaza kila mmoja kujipatia pointi moja kwa mkwaju wa nguvu kuliko ule wa penati, wakatulia Monica akijikunjakunja kama samaki aliyerushwa nchi kavu kutoka majini na mvuvi mwenye utaalam wa hali ya juu.

“Iloo, lione kwanza,” Monica alimwambia Dokta Kisarawe huku akijua kwamba alizidiwa na kujikuta akishindwa kusimamia msimamo wake wa kucheza mechi na viatu, akakubali kucheza bila viatu.

“Umedhurika nini sasa mpenzi wangu Monica?” aliuliza dokta huku akichekacheka kimtindo.

“Madhara yapo. Je, nikinasa?”

“Hupendi kunasa?”

“Nilishasema nataka kwa mume wangu.”

“Huwezi kunasa, mi najua. Utanasa kwa mumeo tu.”


“Mambo Sulee?” Monica alimsalimia shoga yake huyo siku saba baada ya siku thelathini na moja za mwisho wa mwezi.

“Poa Monica, niambie.”

“Hivi unajua nimepita siku kama kumi na moja?”

“Kweli?”

“Eee.”

“Basi piga vigelegele Monica, tayari.”

“Inawezekana kweli?”

“Kabisa.”


Monica aliamua kwenda kwenye zahanati ya jirani na kwake ili akathibitishe kama kweli amenasa…

“Mh! Kama kweli atakuwa mume wangu tu. Siku ile si dokta alisema hakukuwa na uwezekano.”

Monica alipima haja ndogo, akasubiri majibu yake huku kiroho kikimdunda! Hakuwa amemwambia mume wake kuhusu kupitisha muda huo wote na mume naye siku hiyohiyo alikwenda kwenye hospitali moja kubwa kwa ajili ya kucheki mfumo wake wa uzazi kama upo sawa au la!

Wakati mumewe akiwa kwenye benchi akisubiri majibu, yeye alikuwa kwa dokta akipokea na alipanga asimwambie mkewe kwa majibu yoyote yale…

“Ndugu nani…katika maisha yako uliwahi kupata ajali ya gari hivi?” dokta alimuuliza mume wa Monica.

“Yeah! Mwaka elfu mbili na tatu.”

“Ulikuwa hujaoa?”

“Yah!”

“Sasa bwana sikiliza nikwambie, wewe mfumo wako wa uzazi ulivurugika baada ya ajali hiyo. Kwa hiyo huwezi kumpa mimba mwanamke.”

“Kweli dokta?”

“Ndiyo vipimo vinavyosema.”


“Mrembo majibu yako yapo sawa. Una ujauzito wa siku kumi na moja sasa. Hongera sana, mwambie mzee pia nampa hongera

ake,” daktari wa zahanati aliyokwenda Monica alimwambia.

“Kweli dokta?”

“Ndiyo kipimo kimesema hivyo mrembo. Wewe ni mjamzito.”

“Jamani, kweli Mungu mkubwa. Asante Mungu wangu. Mume wangu atafurahije?”

Monica alitoka akiwa na furaha iliyopitiliza, moja kwa moja hadi nyumbani, akafikia sebuleni ili ampigie simu mumewe na kumpa habari njema.

Simu ya mume wake iliita kwa muda bila kupokelewa, ikakatika akapiga tena…

“Khaa! Huyu vipi kwani? Simu hapokei, yuko wapi?”

Akajaribu kama mara tatu mpaka nne bila kupokelewa, akaamua kutuma meseji akiamini kwamba kama mumewe yuko mbali na simu, akiifikia atakutana na ujumbe wake mzuri…

“Baby, Mungu mkubwa mume wangu. Nimekwenda kupima nimeambiwa nina ujauzito. Da! Kweli Mungu hamtupi mja wake.”

Baada ya kutuma meseji hiyo, Monica alikaa nusu saa bila kujibiwa hali iliyompa wasiwasi, alianza kuhisi mumewe amepata matatizo makubwa mahali, akapiga tena simu, haikupokelewa.

“Mmh! Siyo kawaida,” alisema moyoni Monica lakini hakuchukua hatua yoyote. Ile furaha yake ikachanganyika na wasiwasi.


Mume wa Monica alikaa kwenye mgahawa mmoja na mume wa Sulee wakizungumza. Mume wa Monica alikuwa akimsimulia alichoambiwa na daktari baada ya kupima eneo la uzazi…

“Kwa hiyo ndiyo hivyo bwana, mimi sina uwezo wa kuzaa tena kwa mujibu wa yule daktari. Nimeumia, lakini nimeikubali hiyo hali, sina jinsi.”

“Da! Sasa shemeji yeye huko anakohangaika kwa Dokta Kisarawe ina maana anapoteza muda tu?”

“Kiukweli anapoteza muda ndugu yangu.”

Meseji nyingine iliingia kwenye simu ya mume wa Monica, mume wa Sulee akamshauri azisome…

“Kaka, kuna simu zimepigwa na meseji zimeingia, ungesoma hata meseji ujue nani, pengine madili ya hela.”

Mume wa Monicha aliivuta simu ilipokuwa, akaitumbulia macho…

“Shemeji yako amepiga mara kibao, halafu kuna meseji yake hapa, anasemaaa…baby, Mungu mkubwa mume wangu. Nimekwenda kupima nimeambiwa nina ujauzito… Da! Kweli Mungu hamtupi mja wake.”

Mume wa Sulee alishtuka kusikia hivyo, mume wa Monicha akaishiwa nguvu kabisa…

“Au dokta amekudanganya ndugu yangu, uko fiti!”

“Noo! Sidhani, huyu atakuwa na mimba ya mwanaume mwingine, kweli kabisa.”

“Hapana bwana, itakuwa yako.”

“Kaka, mimi nimemwamini dokta. Unajua nilishawahi kuwa na demu kabla ya Monica hakuwahi kunasa ujauzito wangu, lakini nilipomwacha tu, akaenda kunasa kwa jamaa mpya. Huoni kama ni kweli sina uwezo wa kuzalisha?”

“Mh! Shemeji anaweza kufanya hivyo?”

“Ndugu yangu, wanawake wanaweza. Tena unajua afadhali na mwanaume anayeweza kuzaa mtoto akamwacha kwa mama yake huko wapi sijui, lakini wao mtoto unalala naye kitandani lakini si wako.”

“Sasa unadhani iweje ili kubaini ukweli au uongo wake?”

“Itabidi nifanye uchunguzi.”

“Dah! Aisee, kama mimi nigundue mke wangu amebeba mimba ya mwanaume mwingine kwa kweli nadhani naweza kufanya jambo baya sana ulimwengu ukanishangaa.”

“Ni kweli. Lakini wewe mwenzangu si uwezo wa kuzaa unao kama hivi shemeji ni mjamzito na ulishawahi kumpa mimba yule mtoto wa mjumbe ukaitoa.”

“Eee, mimi ni mzima kaka, si Diana mtoto wa mjumbe tu, kuna demu anaitwa Maureen naye nilishampachika mimba ikatoka yenyewe,” alisema mume wa Sulee kama anayejitapa kwa mwenzake.

“Mimi bwana nitakwenda hadi kwenye DNA kutaka uhakika, niko tayari kutumia gharama yoyote ile lakini najua mwisho wa siku mtoto si wangu, naamini.”

“Mimi nitakuwa pamoja na wewe.”

Waliagana, kila mmoja akaelekea nyumbani kwake.


“Za kazi mume wangu?” Sulee alimsalimia mumewe.

“Nzuri tu.”

“Mbona kama haupo sawa?”

“Nitakuwa sawa kivipi wakati kumbe mnatusaliti?”

“Kivipi tena?”

“Monica amekwenda kupima akagundulika ana ujauzito…’

“Usiniambie, mbona hajania…”

“Sikiliza wewe, mbona unadandia kwa mbele.”

“Enhe?”

“Wakati yeye amekwenda kupima, mumewe naye alikwenda kupima, akabainika hawezi kumpa mimba mwanamke, sasa hiyo ya Monica ameipata wapi?”

“Mh! yamekuwa hayo?”

“Ndiyo maana yake. Nadhani hata hiyo ya kwako si yangu mke wangu.”

“Hamna my dear, mimba yako hii wala usiwe na wasiwasi,” Sulee alisema huku sura yake ikichora alama ya unyonge, alivuta picha kuhusu Monica akaamini hisia zake kwamba alitembea na Dokta Kisarawe ni za kweli.

“Lakini baby, unajua niliwahi kuhisi kwamba Monica anatembea na yule dokta aliyetupa dawa.”

“Dokta Kisarawe?”

“Ndiyo.”

“Kama ametembea naye yeye basi hata wewe umetembea naye maana ndiye uliyempeleka.”

“Wala, mimi hawezi.”

“Hawezi wewe mkali, mgumu, mjeuri au mwanaume mwenzake?”

“Hawezi tu.”

“Sikia Sulee…

Nakusikilia mume wangu.”

“Mimi si mjinga kama mume wa Monica, mimi mjanja sana.”

“Najua sana lakini siwezi kukusaliti mume wangu, amini.”

“Lakini si mlikuwa mnapelekana wote?”

“Ndiyo, lakini sijatembea na Dokta Kisarawe.”

“Je, nikigundua umetembea naye?”

“Nifanye lolote lile.”

“Sawa.”


Mume wa Monica alifika nyumbani akiwa amechoka sana. Mkewe alipomwona alitoka mbio kumlaki…

“Pole na kazi mume wangu.”

“Asante sana.”

“Sasa ikawaje, mbona hujajibu meseji yangu wala hujapokea simu?”

“Niache Monica.”

Monica alishtuka sana kwani si kawaida mume wake kumwita kwa jina la Monica, alizoea darling au mke wangu, wakati mwingine alimwita mama. Akajua pana jambo zito limetokea…

“Kwani kuna nini?”

“Umenitumia meseji kwamba una limimba?”

“Ha! Baby, nina limimba au nina mimba?”

“Una limimba, mimba kwani kitu cha kufurahia wakati unajua kila kitu?”

“Kwani mume wangu kuna nini?”

“We! Mimi siyo mume wako.”

“He! Yamekuwa hayo jamani, kwa nini kwani?”

“Hilo limimba ni la nani?”

“Si yako.”

“Wewee, mimi sijakupa mimba wewe.”

“Kanipa nani sasa?”

“Unamjua, tena nitakupiga sasa hivi.”

Monica alimkwepa mumewe na kwenda kukaa sehemu nyingine lakini akiwa amejaa mawazo…

“Au kajua kuhusu mimi na Dokta Kisarawe?”

“Lakini kama kajua, kajuaje? Mbona hakuna mawasiliano kati yake na dokta?”

“Mh! Labda Sulee kamwambia hisia zake maana Sulee sijawahi kumwambia kwamba nimetembea na dokta, sasa?”

“Ha! Liwalo na liwe bwana, sasa nitafanyaje?”

“Monica,” aliitwa na mumewe Monica tena sauti iliyotumika ilikuwa kali sana.

“Abee.”

Monica aliinuka, akatembea kwa kasi mpaka kwa mumewe…

“Nataka tukapime DNA…”

“DNA ndiyo nini mume wangu?”

“DNA ni kipimo kitakachoweza kusema ukweli kama hilo litumbo lako ni la kwangu kweli au la!”

“He! Mume wangu jamani, umefikia huko?”

“Ndiyo.”

“Mh! sawa.”

“Kesho tutakwenda.”

“Sawa.”

Alipoondoka, Monica alimtumia meseji Dokta Kisarawe na kumuuliza kama amewasiliana na mwanaume yeyote anayeitwa David…

“Hapana.”

“Kwani vipi?”

“Nahisi mume wangu amejua natembea na wewe na ana wasiwasi na ujauzito wangu.”

“Unasema kweli?”

“Dokta kwa nini unauliza kama nasema kweli, ina maana hata wewe unajua huu ujauzito unaujua si wake?”

“Sijasema hivyo.”

“Sasa?”

“Nimeshtuka kusikia mtu ana wasiwasi na mimba yake.”

“Kasema kesho tunakwenda kwenye DNA sijui.”

“Mh! amefikia na huko?”

“We acha tu. Sina amani hapa nilipo.”


Usiku akiwa sebuleni, mume wa Monica alimpigia simu mume wa Sulee ambaye naye alikuwa amekaa sebuleni na mke wake…

“Haloo, kesho bwana nakwenda kwenye ile DNA, nakwenda na shemeji yako, nadhani imefika mahali ukweli ujulikane.”

“Sawasawa, naunga mkono.”

“Je, utakuwa tayari unisindikize?”

“Unataka niwepo kaka?”

“Muhimu sana.”

“Basi hakuna shida, nitakuwa na wewe.”

Baada ya kukata simu…

“Unaongea na nani umsindikize?” Sulee alimuuliza mume wake.

“David, kesho anampeleka mkewe wake kupima DNA ili ajue kama kweli ile mimba ni yake au la!”

“Mh!” aliguna Sulee.

“Unaguna nini, au unajua si yake kweli?”

“Hapana, nimeguna kuona amefikia huko.”

Palepale, Sulee alishika simu na kumtumia meseji Monica…

“Mwenzangu unalo, mpaka kwenye DNA?”

Monica aliposoma meseji ya shoga yake huyo alishtuka sana, lakini pia aliumia moyoni…

“Ina maana mume wangu amemwambia Sulee kuhusu hili?”

“Mbona siamini! Mume wangu na Sulee wapi kwa wapi mpaka amwambie mambo mazito kama haya?” aliwaza moyoni Monica huku akiseti namba za Sulee ili amtwangie…

“Ee…”

“Sulee, nani amekwambia?”

“Ni kweli si kweli?”

“Ni kweli ndiyo, lakini nani amekwambia?”

“Mume wangu.”

“Kaambiwa na nani?”

“Si kaambiwa na shemeji.”

“Kamwambia tu au?”

“Kamwambia amsindikize hospitali.”

“Mh!” aliguna Monica, mapigo ya moyo yalimwenda kwa kasi ya ajabu.


Usiku wa kuamkia siku ya kwenda hospitali, Monica alimwamsha mumewe…

“Baby…baby.”

“Mh!”

“Nataka kuzungumza kidogo.”

“Kuhusu nini?”

“Hivi ni kweli kabisa umedhamiria kesho kwenda kupima DNA?”

“Hilo lilishapita na kama umeniamsha kwa ajili hiyo naomba aniache nilale vinginevyo niambie ukweli una mwanaume mwingine nje?”

Monica hakujibu swali hilo. Moyoni alijua anaye mwanaume hata kama si rasmi ambaye ni Dokta Kisarawe, lakini atawezaje kumwambia mumewe kuhusu hilo?

“Sina,” alijibu kwa mkato.

“Basi majibu tutayapata kesho kwenye DNA.”

“Mh!” Monica aliguna, akabaki kimya. Usingizi haukumpata, muda mwingi akili yake ilikuwa ikifikiria namna ya kufanya ili kuepukana na zoezi la kwenda kupima hiyo DNA…

“Au niamke mgonjwa?” aliwaza…

“Tena nataka kukwambia hivi Monica, kesho asubuhi hata ukiamka unaendesha tumboni, daktari na vipimo vyake atakuja hapahapa nyumbani,” alisema mume wake na kuuza mawazo kwamba aamke anaumwa japokuwa naye alitoa kauli ya kumchimba mkwara tu.


Asubuhi Monica ndiyo alikuwa wa kwanza kutoka kitandani, hakupata usingizi kwa usiku kucha huku akiendelea kuwaza kitanzi kilicho mbele yake…

“Za asubuhi?” alimsalimia mumewe.

“Nzuri, jiandae tuwahi.”


Saa mbili na nusu walifika hospitali yenye kutoa huduma ya DNA ambapo pia walimkuta mume wa Sulee…

“Za leo mkubwa?” mume wa Sulee alimsalimia mume wa Monica…

“Salama kaka, mzima?”

“Mzima sana. Naona tumewasili.”

“Sana tu.”

Sura ya Monicha ilionesha wazi kwamba haikutaka kusalimiwa na wala haikuwa tayari kupokea salamu kutoka kwa mtu mwingine.

“Shemeji vipi?” mume wa Sulee alijipa kichwa ngumu na kumsalimia hivyohivyo tu, aitikie, agome angejijua mwenyewe.

“Salama,” Monica aliitikia kwa mkato, mumewe aligundua lakini hakuhusika naye kumuuliza kuna nini mpaka ameitikia salamu kwa staili hiyo.

Walipata huduma kwa kuchukuliwa vipimo muhimu ambapo Monica alichomwa sindano ya tumbo na kuchukuliwa sampo ya maji huku mumewe akichukuliwa vipimo vya kawaida.

“Majibu mje baada ya wiki mbili,” alisema dokta.

“Sawa dokta, hakuna neno.”


Mchana wa siku hiyo, Monica alikuwa kwenye chumba cha Dokta Kisarawe kwa mazungumzo muhimu…

“Kwa hiyo dokta kama nilivyokwambia, hapa sijalala. Mawazo yote ni kuhusu hicho kipimo je, kitasema mtoto wa nani wakati yeye kaenda kupima akaambiwa hana uwezo wa kuzaa?”

“Mimi ninavyojua, mtoto huyo tumboni ni kweli si wa mume wako.”

“Nini dokta? Unamaanisha ni wa nani sasa? Maana mwanaume pekee niliyekutana naye kwa mwaka huu nje ya mume wangu ni wewe.”

“Inaweza kuwa ya kwangu.”

“Aaah! Dokta, lengo lako ni nini?”

“Ilitokea tuu!”

“Ili?”

“Unajua mazingira yalikuwa si ya kutafuta kinga Monica, sasa tungejikingaje? Halafu we shida yako si ilikuwa kupata mtoto kwa sababu mumeo hakuwahi kukupa ujauzito…”

“Sasa ndiyo we unipe kwa njia ya ukweli dokta?” alihoji Monica huku akianza kulia machozi.

“Ndiyo njia ninayoitumia Monica, hata rafiki yako Sulee pia ana ujauzito wangu.”

“Ha! Kweli dokta?”

“Sana tu.”

Kidogo Monica alijiona kama amepoa kusikia Sulee naye ni mjamzito…

“Sasa utanisaidiaje mimi kuhusu maji ya DNA?”

“Rahisi sana, ila kama uko tayari kusaidiwa twende gesti sasa hivi.”

Mh! halafu?”

“Aah! Kwani Monica hujui tukienda gesti halafu ni kitu gani?”

“Ina maana dokta bado unataka?”

“Si sana, ila kwa ajili ya kuburudika mwili wangu.”

“Hivi dokta huoni kama sitajisikia vizuri kutokana na matatizo?”

“Ni akili tu Monica, unaweka pembeni mawazo yote. Kwani si nimekwambia nitakwenda kuongea na daktari wa DNA kwenye ile hospitali?”

“Utamwambiaje?”

“Najua mimi.”

“Nihakikishie kwanza ili kama nikiona kweli inawezekana tunaweza kwenda huko gesti.”

“Nitamwambia ayapindishe majibu. Yawe ni kweli mimba ni ya mumeo.”

“Lakini si amepimwa imeonekana hawezi kuzaa?”

“Bwana wewe Monica, kila kitu kinawezekana, ujue hilo kwanza ili mengine yaendelee.”

“Mh! Dokta huo ni mtihani mkubwa kwangu. Lakini poa twende.”

“Sasa sikia, wewe tangulia kufika kwenye ileile gesti ya siku ile.”

“Usichelewe.”

“Ndani ya dakika sifuri nitakuwa nimefika na mimi.”

Monica alikwenda gesti bila kupenda, lakini angefanyaje wakati aliitaka ndoa yake. Dada yake wa kwanza aliachika, wa pili pia, watatu hajaolewa, wa nne kaachika na uzee juu, sasa ilikuwa lazima yeye ajichunge.

Wakati anaingia gesti hiyo, mume wa Sulee akamwona akiwa ndani ya teksi…

“Haa! Yule si shemeji Monica?”

Alichofanya mwanaume huyo alimpigia simu mkewe, Sulee ili amsimulie lakini namba ikawa haipatikani hewani…

“Khaa! Huyu naye vipi? Mbona hayupo hewani!”

Alijaribu mara mbili tatu, mwishowe akaamua kumpigia simu mume wa Monica…

“Mshikaji wapi saa hizi?”

“Job, niambie…”

“Mh! Kuna ishu moja hivi lakini naona kama haijakaa sawasawa.”

“Ipi hiyo tena?”

“Nimepita kwenye gesti moja hivi, nimemuona shemeji akiingia. Mna mgeni yeyote ambaye amefikia gesti?”

“Hapana! Ni wapi?”

“Hapa Kinondoni Mkwajuni.”

“Nakuja, nisubiri hapohapo ulipo.”

“Poa.”

Mume wa Monica alikodi teksi akamuomba dereva aendeshe kwa kasi hadi Kinondoni Mkwajuni. Hakutaka kumpigia simu mke wake asije akapoteza ushahidi. Alikutana na mume wa Sulee ambaye alihama kwenye teksi akaiacha iende na kuingia kwenye teksi aliyofika nayo mume wa Monica.

“Vipi mshikaji, gesti gani?”

“Ile pale yenye maua. Lakini ni vyema umpigie umuulize aliko si ajabu si yeye, nilifananisha tu.”

“Hapana, nikimpigia nitapoteza ushahidi.”

“Huwezi, kwani akiwa yeye kweli na sisi tumesimama hapa nje atajiteteaje?”

“Lakini kweli.”

Mume wa Monica aliiseti simu yake akampigia mke wake, simu iliita kwa muda mrefu mpaka ikakatika…

“Hapokei,” alisema mume wa Monica kwa sauti iliyoambatana na mtetemesho wa ghadhabu kama siyo hasira za kupitiliza.

Mara Dokta Kisarawe akatokea, mume wa Sulee anamjua alishakutana naye siku moja…

“Ha! Mshikaji, huyo anayeshuka kwenye gari ndiye Dokta Kisarawe ambaye anawatibu wake zetu.”

“Mh! Au ndiyo jamaa mwenyewe?”

“Huenda.”

“Sasa?”

“Tusubiri hapahapa nje.”

Mara, simu ya Monica iliingia kwa mume wake…

“Huyo anapiga.”

“Pokea.”

“Haloo.”

“Ee my husband, nimeona missed call yako hapa.”

“Uko wapi kwani mpaka hukupokea simu?”

“Kwani we uko wapi?”

“Khaa! Mimi nakuuliza na wewe unaniuliza, una akili kweli wewe?”

“Mimi nipo jirani na nyumbani kwa mama Mariam.”

“Oke, sawa.”

Upande wa pili, yaani kwa Monica ikakata simu haraka.

“Sasa sikia, tukisema tukavamie vipi?” aliuliza mume wa Monica.

“Mawili. Kwanza niambie, kama kweli ni yeye utachukua hatua gani mzee?”

“Talaka tu.”

“Una uhakika?”

“Mungu vile ni talaka tu.”

“Okey, kama ni talaka basi tusivamie, tukae mpaka watoke sisi tushuke kwenye gari tukiwa wawili hivihivi.”

“Sawa, niko tayari.”

Mara, mume wa Sulee alimpigia

mke wake…

“Enheee, Sulee hebu njoo hapa Kinondoni Mkwajuni haraka sana, chukua Bajaj,” alisema mwanaume huyo.

“Kuna nini tena?”

“Nimesema njoo, utajua hapahapa.”

Sulee kwa sababu alikuwa amevaa gauni, alichofanya ni kubeba khanga moja tu, akatoka mbio na kuchukua Bajaj mpaka Mkwajuni. Alimpigia simu mumewe, akamwambia alipo. Ile anafika tu na kumwona mume wa shoga yake Monica akahisi kitu tayari kuhusu Monica mwenyewe…

“Hapana lazima Monica amefanya kitu,” alisema moyoni lakini alishindwa kumpigia kwa sababu tayari alikuwa mbele ya wanaume hao walioonesha sura za kuchukia…

“Kuna nini kwani? Eti shemu kuna nini?”

“Ingia kwanza ndani ya gari,” mume wake alimwambia akiwa ameshamfungulia mlango…

“Rafiki yako ameingia gesti ile…”alisema mume wa Monica.

“Na nani? Ameingia na mwanaume gani?”

“Hatujajua, lakini tumemwona yule Dokta Kisarawe naye akiingia,” alisema mume wa Sulee…

“Mungu wangu, ina maana Dokta Kisarawe ndiyo wa kwake siku hizi siyo?”

“Hatujathibitisha.”

“Sasa kwa nini msiende?”

“Tumeona hakuna haja ya kwenda shemu, ila tukae hapa mpaka watoke ndipo na sisi tujitokeze,” alisisitiza mume wa Monica.

“Mh! Makubwa,” alichoka kabisa Sulee. Moyoni alikuwa na mambo mawili, kwanza shoga yake kuingia kwenye mkenge huo, pili ni wivu wa dokta kutembea na Monica jambo ambalo aliwahi kulihisi lakini akakosa ushahidi wa moja kwa moja.

“Lakini mkuu je kama shemeji atatoka peke yake na Dokta Kisarawe naye peke yake itakuwaje?” alihoji mume wa Sulee hoja ambayo ni ya kweli kwani kama angeanza kutoka mmoja wao, mfano dokta wangemuingizaje kwenye tuhuma za kumfumania?

“We sikiliza, hata kama itakuwa hivyo bado ni tatizo, ishu hapa ni yeye kuja gesti, iwe na dokta iwe na mwanaume mwingine lakini hoja ni moja tu, sijapenda. Halafu ananidanganya kwamba yuko nyumbani,” alilalamika mume wa Monica.

Nusu saa ilikatika, hakukuwa na mtu yeyote aliyetoka ndani achilia mbali Dokta Kisarawe na Monica. Sulee akashauri…

“Mimi shemeji nashauri kwamba, kama inawezekana mimi niende kuingia, nikaulizie…”

“Hapana,” alikataa mume wa Sulee, akataka uendelee utaratibu uleule kwani ufafanuzi ulikuwa tayari kwamba, awe amenaswa laivu au la, ishu ni yeye kuingia katika gesti hiyo.

Dakika sitini zilionesha kwenye saa zao za kwenye simu na mkononi, walitoka watu wawili, mwanamke na mwanaume lakini wakiwa wamepishana kwa dakika kama tatu hivi. Aliyeanza ni mwanaume.

“Loo! Shemeji naona shoga yako kaamua kumkinaisha Dokta Kisarawe, lisaa limoja sasa,” alisema mume wa Monica…

“We acha tu, mi mwenyewe nashangaa, muda wote huu?”

“Ungekuwa wewe ungetumia dakika ngapi?” Sulee aliulizwa na mume wake lakini kicheko cha mume wa Monica kukalifanya swali hilo kuwa jepesi zaidi.

“Mimi sina mpango huo kwanza, sijui yeye ametolea wapi haya mawazo,” alijibu Sulee.

Mume wake akaendelea…

“Nimekuuliza kwa sababu umesema unamshangaa yeye kutumia muda mrefu hivi, ndiyo maana nikataka kujua ungekuwa wewe ungetumia muda gani?”

Kabla jibu halijapatikana, ndani ya gesti hiyo alitokea mwanaume mmoja, si Dokta Kisarawe. Alikuwa akifunga vifungo vya shati vizuri huku uso ukionekana kuwa na jasho kwa kazi ya chumbani.

“Jamani, inawezekana yule mwanaume ndiyo alikuwa na Monica chumbani?” alisema kwa mshtuko mume wa Sulee…

“Haa! Halafu namfahamu, ni jirani yangu bwana. Anaitwa baba Anode, atakuwa yeye,” alisema mume wa Monica huku akianza kufungua mlango ili atoke, tayari alikuwa amekasirika kuona kumbe anayemwibia ni jirani yake.

Kabla hajatoka, msichana mmoja naye wa nyumba ya jirani na mume wa Monica alitoka kwenye gesti hiyo hivyo kutoa picha kwamba, alikuwa na baba Anode.

“Yule msichana anaitwa Mwasiti, ina maana anatembea na baba Anode?” alihoji mume wa Monica akionekana kushangaa sana.

Tena ili kudhihirisha kwamba kweli walikuwa wote gesti, Mwasiti alikazana na kumfikia baba Anode ambapo walishikana mikono na kutembea kwa maringo kama wapo fungate.

Baada yakuona kimya hawatoki Mume wa Monica na mume wa sulee waliamuwa kuingia ndani nakuwakuta Monica na dokta wakiwa chumbani

Monica kumwona mumewe akadondoka chini

nakupoteza fahamu kwa presha aliyo kuwa nayo.

Wanasema anayefumaniwa hupoteza nguvu hata kama ni baunsa uwa mdhembe, mume wa Sulee licha ya wembamba wake lakini aliweza kumkwida Dokta Kisarawe na kumtembeza hadi lipokuwa Sulee,

Monica alikuwa hajazinduka

Dokta Kisarawe akawekwa chini akae pembeni ya Monica huku kazi ya kumpepea Monica ikiendelea ili azinduke… “Katika hali kama hii shemeji halafu mwanamke aje kuniambia eti mimba ni yangu inawezekana kweli?” Mume wa Monica alimwambia Sulee…

“Kweli lakini shemeji. Inauma sana!” Dokta Kisarawe aliinua uso na kumwangalia Sulee kwa sura inayosema…

“Hata wewe unaongea maneno kama hayo wakati mimba yako pia ni yangu?”“Unaniangalia nini, kwenda huko?” Sulee alimkandia daktari huyo kwani alijua kwa pale hakuwa na ujanja wa kumfanya chochote wala kutoboa siri. Atoboe siri ale mkong’oto! Katika hali isiyotarajiwa, mume wa Monica alimvaa Dokta Kisarawe kwa kumpiga teke la tumbo na mangumi ya kichwani hadi naye akaanguka na kupoteza fahamu…

“Siwezi kumlegezea mtu kama huyu, ameharibu ndoa yangu,” alisema mume wa Monica huku akitaka kumwongezea kipigo lakini mume wa Sulee akazuia. Watu walianza kujaa eneo la tukio. “Jamani kuna nini kwani?” Walihoji watu huku wengine wakiwa tayari wameokota mawe kutaka kumpiga Dokta Kisarawe. “Ha! Jamani huyu si Dokta Kisarawe?” Mwanamke mmoja aliuliza kwa mshangao mkubwa.

“Ni yeye bwana,” mwenzake alijibu halafu akaendelea kusema…

“Halafu mi nilijua tu jamani kwamba iko siku moja dokta atafumaniwa. Kutibu gani wagonjwa kila siku uko na wake za watu?” “Mimi mwenyewe siyo siri niliacha kwenda kwake baada ya kunitongoza kila nikifika. Wengine dokta hatujaumbwa hivyo. Wewe kila mwanamke unadhani anaweza kukukubali?”

Mazungumzo ya wanawake hao wawili yalitoa mwanga mpya kabisa kwa akina Sulee, mume wa Monica akasema anataka kummaliza dokta kwa kumpiga risasi… “Noo…nooo, usifanye hivyo,” mume wa Sulee akamzuia.

Alipoona amezuiwa kwa tendo hilo, mume wa Monica akaomba watu watawanyike ili abaki yeye, Sulee na mume wake. Watu walitii, wakaondoka lakini wengi walionekana kumkandia daktari huyo. Wapo waliodai wamewahi kusikia kwamba kuna daktari anapenda ngono na wake za watu. Wakati huo Monica alishaamka. Sasa walibaki sita tu, wakamuomba dereva wa teksi aondoke akakae mahali ili wao waingie ndani ya gari. Walimbeba Monica hadi ndani ya gari, wakamwingiza na Dokta Kisarawe. Walikaa wote wakaenea… “Dokta,” alianza kwa kuita mume wa Monica…

“Naam.” “Ni kwa nini unatembea na mke wangu tena mpaka umempa mimba?”

Dokta Kisarawe aliangalia chini tu. Alijua ukweli wa madai ya mwanaume huyo…

“Monica,” mumewe alimwita…

“Bee.” “Ni kwa nini uliamua kunisaliti kwa kutembea nje ya ndoa hadi kupata mimba?”

“Nisamehe mume wangu ni shetani tu.”

“Sawa, labda nikuulize kitu kingine. Ni kwa nini uliamua kusema mimi ndiye mwenye mimba?”

Monica alibaki kimya, akaulizwa tena pia akabaki kimya. Kidogo mume wake amchape makofi…

“Si nakuuliza wewe mbwa.” “Monica si useme tu ukweli, kama kusamehewa usamehewe, unakatakata maneno ya nini?” Alisema Sulee, Monica akakasirika sana na kusema…

“Jamani, haya yote sababu kubwa ni Sulee.” “Ha! We Monica mwogope Mungu, sababu kubwa ni mimi kivipi?

“We si ndiyo ulinipeleka!”

“Halafu nikakutongozea kwa dokta?”

“Unajua mwenyewe.” “Sikia Monica, sidhani kama mimi ni mjinga kiasi hicho. Wewe mzigo wote huu ni wako, hakuna ubishi. Unapotaka kumsukumia mwenzako ni kutapatapa tu.”

“Mwambie shemeji, nahisi kama anataka tufe wote.” “Siyo nataka tufe wote, kwani na wewe si una mimba ya Dokta Kisarawe.”

Mambo yaliharibika! Monica alisema kauli nzito na mbaya, ni kama alichochea kuni kwenye moto wa kuni ulioanza kuzimika. “Unaona Sulee…unaona? Sikukwambia mimi kwamba nahisi hata wewe hiyo mimba ni ya Dokta Kisarawe?” Mume wake alikuja juu.

“Jamani maneno ya Monica si ya kuyaunga mkono, amechanganyakiwa huyu mume wangu,” alijitetea Sulee, msala ulishamwangukia. Mume wake alimvaa mume wa Monica na kumnyang’anya bastola, akamwelekezea mke wake, lakini mume wa Monica akamuwahi na kumpiga mkono, ikaanguka chini. Kuona hivyo, mume wa Sulee alitoka ndani ya gari, akaenda kuokota jiwe kubwa akawa anakwenda nalo kwenye gari ili ampige nalo mke wake. Yeye hakuonekana kuwa na haja na Dokta Kisarawe…

“Naua mimi, naua nasema,” alilirusha jiwe hilo likatua kwenye mlango jambo ambalo mle ndani hakuna aliyetegemea… “Mume wangu jamani siyo kweli,” alisema Sulee akianza kulia. Tayari gari sehemu ya mlango ilikuwa nyang’anyang’a kwa lile jiwe na mwenye gari alikwenda mbali kidogo kwa vile..

ITAENDELEA

Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Tatu

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment