Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Tatu
CHOMBEZO

Ep 03: Dokta Mimi Siumwi Huko

SIMULIZI Dokta Mimi Siumwi Huko
Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Tatu

IMEANDIKWA NA: 2JIACHIE

*********************************************************************************

Chombezo: Dokta Mimi Siumwi Huko

Sehemu ya Tatu (3)

kwa vile mahali aliposimamisha gari hakukuwa na njia nyingine ya kutokea zaidi ya ile aliyoelekea yeye kwa miguu… “Mtasha mbona umekuwa mstari wa mbele sana kunizuia mimi nisifafanye uhalifu, inakuwaje wewe unashindwa kujizuia?” Mume wa Monica alisema akimwita mwenzake huyo kwa jina lake la utani.

Mara, mwenye gari alitokea

Alishtuka kuona gari lake limeharibika sehemu ya mlango huku timbwili likiendelea…

“Jamani vipi tena?” aliuliza kwa mshangao mkubwa.

Majibu aliyoyapata yalimfanya ajutie lakini akaahidiwa kulipwa fedha ili kwenda kutengeneza gari hilo japokuwa alikubali lakini kwa shingo upande.

Baada ya utulivu kurejea lakini huku wanaume wote wakiwa na hasira ya wivu, waliamua kwenda polisi ambapo Dokta Kisarawe aliwekwa ndani ili kupisha uchunguzi wa madai ya wanaume hao kwamba ametembea na wake zao na kuwapa ujauzito.

Baada ya kuandikisha maelezo, walirudi nyumbani. Wote walifikia nyumbani kwa Mtasha, mume wa Sulee ambapo kikao kilikaa na misimamo ilitolewa…

“Mimi bwana kwa upande wangu nasema wazi kwamba sina haja ya kuwa na mke kama huyu,” alisema mume wa Monica huku akimwangalia mkewe kwa macho yaliyojaa uchungu…

“Hata mimi, Sulee nakuandikia talaka zako tatu sasa hivi,” alikuja juu Mtasha na kutaka kumpiga tena mke wake kwa hasira…

“Sasa Mtasha si umeshasema unamwandikia talaka si ufanye hivyo, achana na kumpiga bwana,” alisema mume wa Monica.

Wanawake hao wawili waliangua kilio huku kila mmoja akimlaumu mwenzake kwamba alimsababishia lakini lawama za Monica kwa Sulee zilikuwa za kweli kwani yeye alipelekwa na shoga yake huyo ambaye alikuwa akiijua tabia chafu ya Dokta Kisarawe…

“Bila wewe Sulee mimi yasingenikuta haya. Ulijua Dokta Kisarawe ni mwingi wa habari ni kwa nini hukuniambia maana hata wewe ulishapitiwa…

“Halafu nilimwambia dokta. Alikuwa akipenda kunishikashika sehemu zisizohusika na matatatizo yangu, nikamwambia dokta mimi siumwi huko yeye hakusikia,” alilalama sana Monica…

“Monica ni shetani, hata mimi nilimwambia dokta mimi siumwi huko wakati akipeleka mikono yake kwenye matiti yangu lakini hakutaka kunisikia. Tusameheni jamani.”

“Hakuna msamaha hapa… Ala!” wanaume wote walijikuta wakijibu kwa pamoja bila kutaarifiana…

“Kwanza ni muhimu kwenda kupima afya zetu maana kama mna mimba ina maana mlikuwa hamtumii kinga,” alisema mume wa Monica…

“Huko kuchepuka kwenu ndiyo faida yake mnaiona sasa,” alisema mume wa Sulee huku akikohoa. Hapo alikuwa akisaka karatasi ya kuandikia talaka mara moja.


Siku ya pili, Mtasha, yaani mume wa Sulee na mume wa Monica walikwenda kupima virusi vya Ukimwi. Walikutana na wake zao huko wakiwa na shangazi wa Sulee ambaye aliomba kuzungumza na Mtasha kabla ya kuingia kwa dokta. Kwa heshima Mtasha alikubali na akatoka pembeni…

“Baba najua unaniheshimu sana…”

“Kweli shangazi…”

“Mwenzio kanijia na talaka analia. Lakini aliponisimulia kisa hata mimi nilikuunga mkono mwanangu…”

“Nashukuru sana kusikia hivyo shangazi…”

“Enhee, lakini sasa nina ombi moja tu kwako…”

“Lipi hilo shangazi?”

“Msamehe Sulee.”

Mtasha palepale alijishika kichwa na kujikuna huku akitumbua macho, akakumbuka mema aliyowahi kuyafanya shangazi huyo kwake maana ana uwezo si wa kitoto.

Kuna mwaka Mtasha alipata kesi mbaya sana, uchumi wake ukayumba sana akajikuta hana hata pesa ya kula. Shangazi huyo wa mkewe akawa ndiye mfadhili wake kwani alikuwa akimpa pesa ya kula na pia alimsimamia kwenye kesi hiyo kwa kumuwekea wakili na akashinda.

Baada ya kushinda alimpatia mtaji akaendelea na miradi yake iliyosimama…

Wakati wa maongezi hayo, shangazi mtu hakumkumbusha kitu chochote Mtasha. Alimwacha ajipime mwenyewe tu…

“Da! Shangazi kusema ukweli umenipa wakati mgumu sana,” alisema mume wa Sulee…

“Kwa nini mwanangu? Kusameheana kumewekwa na Mungu na ukimsamehe mwenzako hata Mungu atapenda na kukubariki.”

“Ni kweli, lakini shangazi unalionaje hili la ujauzito?”

“Hilo unaweza kuliacha mikononi mwangu nikashughulika nalo.”

“Utafanyaje shangazi? Maana mimi kusema kweli siwezi kuishi na mke mwenye ujauzito wa mwanaume mwingine.”

“Ndiyo maana nimesema niachie mimi kuhusu hilo.”

“Shangazi maamuzi yako ni mema na nakuheshimu wewe sana, je vipi kuhusu kupima Virusi vya Ukimwi?”

Muda wote huo, mume wa Monica alipokuwa amekaa alikuwa akimtumbulia macho mume wa Sulee kama anayemwambia asithubutu kukubali hata siku moja maneno ya shangazi wa Sulee…

“Ndiyo maana tupo hapa! Wewe unadhani Sulee ana virusi?” alisema shangazi mtu huyo…

“Siwezi kusema anavyo au hana, ila kupima ni muhimu shangazi.”

“Kwa hiyo kama atakuwa salama utakuwa umepokea ombi langu siyo?

“Naamini hivyo.”

“Basi turejee kusubiri zoezi likamilike.”

Walirudi kwenye fomu. Mume wa Monica akamuuliza mume wa Sulee mazungumzo yao yalihusu nini…

“Shangazi anataka nimsamehe Sulee.”

“Uko tayari kwa hilo?”

“Mh! Nimemwambia kama atakuwa hajaathirika naweza.”

“We unataka kumrudia Sulee?”

“Unajua nini mshkaji? Huyu shangazi amenisaidia sana katika maisha yangu kuliko mtu mwingine yeyote…”

“Kwa hiyo?”

“Kwa hiyo naweza kuangalia upya cha kufanya.”

“Mh! Nadhani sijakuelewa.”

“Kivipi?”

“Yaani pamoja na mambo yoote waliyotufanyia hawa Malaya wewe unakubali tuwasamehe, Mungu aniepushie hilo mawazoni mwangu,” alisema mume wa Monica na kumfanya mume wa Sulee kuwa na mawazo nusunusu tofauti na alivyoongea na shangazi mtu.


Majibu ya vipimo yalitoka, waliitwa mtu mmoja mmoja lakini huku wakiruhusiwa kwenda na watu wao kama wapo walioongozana nao.

Sulee alikwenda na shangazi yake huku akidondosha machozi kwa kuwa muda wa zamu yake ulifika. Alikuwa akitetemeka sana.

Monica, mumewe na mume wa Sulee walibaki nje lakini mume wa Sulee aliuliza kama itakuwa busara na yeye aende kwa vile yanaweza kutoka majibu ambayo yamechakachuliwa na shangazi huyo kwa vile alitaka ndoa ya Sulee iendelee kudumu.

“Noo, achana nao bwana. Wewe mbona hueleweki? Kwanza kama wao walitaka uwazi na ukweli kwa nini wasikwambie muingie wote?” alihoji mume wa Monica mpaka mwenyewe akaona ni kweli, akabaki kwenye fomu.

Baada ya dakika kama kumi, kilio kikubwa kikasikika kutokea chumba cha daktari…

“Uuuwi, Mungu wee nisaidie. Nitakwenda wapi mimi?” ilikuwa sauti ya Sulee…

“Ngoma tayari hiyo mwanangu, hakuna kurudiana wala kwenda mbele,” alisema mume wa Monica huku akichekelea. Alijua mpango wa shangazi mtu kuirejesha ndoa hiyo haupo tena.

Kwa upande wake, Monica alionekana kuwa mtu mwenye mchecheto zaidi kwani kila wakati alikuwa akisimama na kukaa. Aliamini kama Sulee ‘aliungua’ hata yeye yumo ndani ya ‘moto’ huo.

“Mmh! Sasa kama Sulee analia amegundulika kuwa na virusi je mimi? Maana mwanaume aliyemwambukiza yeye ndiyo huyohuyo ametembea na mimi,” alisema moyoni Monica huku akimtupia macho ya wizi mumewe.

“Monicaaa…” aliita jina muuguzi kabla hajamalizia, Monica mwenyewe alisimama haraka sana. Mara Sulee na shangazi yake wakatokea huku Sulee akichuruzika machozi.

“Pole Sulee,” alisema Monica lakini hakuitikiwa hata shangazi yake hakusema kitu.

“Baba tunaondoka, uamuzi wako ubaki kuwa palepale,” alisema shangazi mtu akimwambia mume wa Sulee. Alipita kwenye korido kwa aibu kubwa akiwa amejiinamia mpaka kwenye gari lake akifuatwa na Sulee kwa nyuma.


“Eee, thanks God. Asante Mungu, wewe ndiye muweza wa yote. Oooh! Si kwa nguvu zangu bwana bali kwa neema tu. Mimi Monica mimi kwamba sina virusi?” sauti ya Monica ilisikika kutokea kwenye chumba cha daktari.

Ilifika mahali akapiga na vigeregere kufurahia majibu ya vipimo vyake.

Mumewe alianza kuhisi ganzi akiwaza kwamba endapo mkewe yuko fiti halafu yeye akakutwa na ngoma itakuwaje?

“Itakuwa poa tu kwani maisha bado yataendelea,” alisema moyoni mume wa Monica huku akiangalia chini kwa mawazo.

“Mkubwa unasikia huko ndani? Shemeji yuko ngangari,” mume wa Sulee alisema.

“Eee, ndiyo sherehe inaendelea ndani.”

Mara Monica alitokea…

“My dear niko fiti, sina virusi wala vijidudu,” alisema Monica huku akirukaruka kwenye miguu ya mumewe…

“Kwa hiyo?” mumewe alimuuliza…

“Heee! Hujapenda?”

“Hata nikipenda, kwani kuna nini? Si umekutwa upo fiti tu.”

“Hunisamehi?”

“Haitatokea Monica.”

Monica aliangua kilio mbele ya watu huku mumewe naye akiitwa kuchukua majibu yake. Kumbe Sulee na shangazi yake hawakwenda mbali, walikuwa kwenye gari wakisubiri matokeo ya mume wa Sulee, mume wa Monica na Monica mwenyewe.

“Mshkaji mimi nataka twende wote,” alisema mume wa Monica baada ya kuitwa jina lake na muuguzi mmoja.

Walizama wote mpaka kwa dokta na wakasema wote wamefika kwa kupima…

“Kwa hiyo majibu mnasikiliziana?” alihoji dokta.

“Ndiyo.”

Alianza kwa kuwashauri huku akiweka majibu ya wote sambamba, karatasi ya mume wa Monica ikianza juu.

“Sasa kwa kuwa mpo wote na wote mmepima na majibu yote yapo hapa baada ya ushauri niliowapa, wote mpo vizuri hakuna mwenye virusi vya Ukimwi,” alisema dokta. Walisimama, wakakumbatiana. Wakampa mkono dokta na kutoka nje huku wakicheka kwa furaha…

“Mungu anajua cha kufanya mshkaji, wale wanawake siyo kabisa,” alisema mume wa Monica…

“Lakini kama wewe huna na shemeji hana si mnaweza kurudiana?” alihoji mume wa Sulee.

“Na ile mimba?”

“Si utailea tu.”

“Mimi nilee mimba ya Dokta Kisarawe?”

“Kwani mshkaji kuna nini?”

“Haitatokea. Mara kumi angenibambika nisijue kuliko kujua.”


Sulee na Monica walikumbatiana kwenye gari huku wote wakilia. Kilio kikubwa kilikuwa kwa Sulee kwani alikutwa ameungua wakati mwenzake yupo fiti.

“Mwanangu nyie naona mambo mazuri maana naona vicheko,” shangazi wa Sulee alimuuliza mumewe…

“Mungu hamtupi mja wake shangazi. Mungu mkubwa bwana,” alisema mume wa Monica huku wakiondoka zao kwa mbwembwe wakicheka na kupigiana mikono na wakitembea kwa ujasiri wa hali ya juu.

Wake zao walikuwa wakiwatazama kwa macho yanayoendelea kujaa machozi wasijue la kufanya. Ghafla waliangua vilio mpaka watu wakajaa lakini hakukuwa na jinsi, waume zao walishaamua. Walijuta na kujuta kwa usaliti wakati waume zao walikuwa wakihangaika kusaka maisha

na siyo uhuni kama walio

kuwa wakifanya wakezao.

“shangazi mimi sijuwi kwa nini

jamani Yani nimetembea na Monica kwa mwanaume mmoja

lakini mwenza hana shangazi”

“pole Sulee Nimipango ya Mungu

wala usijari”

“Monica ladhima nijari

Moyo wangu una umia sana najuta na juta”

lakini shangazi yake sulee

hakuwa na wasiwasi kabisa

kuhusu suara hilo

“Sawa Sulee mimi narudi

kijijini nikaanze maisha mapya”

alisema Monica huku

akitokwa na Machozi sana”

“sikiliza Monica baki nasi hapa hapa mjini sawa utakaa na sisi”

“kweli shangazi oooh Asante Mungu wangu”


baada ya miezi2:

Dokta kisarawe

alihama Dar na kuamia Morogoro

huko alikutana na kijana mmoja

aliye itwa Adams j maryo jr.

Aliye kuwa mfanya biashara

hapo Morogoro Dokta kisarawe

aliacha kazi ya udokta na kuanza kufanya biashara anazo fanya

Adams za Magari kutoka

japani Maisha yalisonga sana

kisarawe alikuwa mwembamba sana lakini alikuwa kaninepa vibaya ndani ya miezi mi3 tu

mambo yake yalikuwa safi

kutokana na Elimu yake kuwa kubwa sana alikuwa msaidizi

katika kampuni ya Adams Maryo.

Adams alikuwa akimtumia kisarawe katika mahesabu na hata akwenda nae japani

“Unajuwa safari moja tu nimeona

mabadiliko katika biashara yangu

kaka kisarawe”

“unajuwa kwa nini”

“hapana sijajuwa”

“tatizo lugha ulikuwa huiwezi

walikuwa wakikuibia sana bei ya gari moja walikuwa wakikuibia zaidi ya laki7 ya tz”

“sasa umenifungua akiri

kaka sasa kivipi”

“kulikuwa kuna pesa inayo tolewa

katika jumla ya manunuzi

wewe ulikuwa hujuwi”

“ok asante nakutegemea

kaka”

“tupo pamoja”


Sulee alikuwa mtu waku lia kila

Mara Monica alikuwa ndiye Mtu wa kumliwaza Muda wote

Mimba zao zote zilikuwa za miezi 7 kila Mtu Sulee alikonda sana

alishindwa kula Hakuwa na Furaha kabisa Moyoni mwake

alimchukia kabisa dk kisarawe

kwaku sababisha Ndoa yake

kuvunjika :

“Monica nina siri kubwa sana

kuhusu Sulee”

“siri gani hiyo Shangazi…

Ila wewe inaonekana haujatulia

kabisa unaweza ukamwambia”

“Shangazi wewe ndiyo nguzo

yangu katika maisha yangu yote kwa sasa siwezi kumwambia kabisa shangazi naumia

sana kumwona sulee akiwa katika

hari ile”

“Hata mimi najuwa

sana kutoa mimba nikosa sana

lakini je ukimsababishia

nidhambi pia?”

“shangazi mh hapo sijuwi

ila ni dhambi siyo kubwa”

“huna uwakika Monica”

“ndiyo”

“basi kuna jambo ambalo

nataka itoke ikitoka

Nahuakika sulee mwanangu atakuwa na Afya njema”

“sasa shangazi ni jambo gani hilo

nijuwe maana mimi na wewe ni walezi wake sasa kila siku

hari yake ina zidi kuyumba

ona anavyo pungua hata kama na H I V. Ni miezi michache sana

hawezi kuwa ana dhohofika

kiasi hiki huyu hata mawazo

yana changia”

“ngoja kesho takwambia”

“shangazi sawa”

“acha niende kazini

badae”

“kazi njema Mama”

“leo unaniita mama”

“yah kuanzia leo

takuita mama nasiyo shangazi

naomba ukubali”

“sawa maana wanangu wote

wapo makwao hapa sina

mtu wakunipa mahaba ya kuniita mama nita furahi sana”


Baada ya siku moja:

“Monica”

“Naam sulee”

“hivi imekuwaje wewe huna ukimwi na mimi ninao”

“kwa nini wauliza hivyo”

“nawaza sana sijuwi

kwa nini maana wote tumetembea na mtu mmoja

Dokta kisarawe mwenye

ukimwi”

“hata mimi sijuwi

ila punguza mawazo mpezi angu

una niliza sana napo kuona”

“hapana Monica najuta sana

Mume wangu tulikuwa tukipendana sana sana ujinga wangu umeniponza nilifanya vile

kuokoa ndoa yangu kumbe ndiyo

nilikuwa naipoteza jamani

hiii hiii mmh”

“nyamaza wangu

usilie Sulee”

“ina uma sana”

“jikaze sulee angalia upo katika

hari mbaya siyo vizuri kulia lia

kila mara”

Hari ya Sulee ilikuwa mbaya sana

Monica alitoka inje nakumwita dereva ili wampe msaada :

“dereva sulee kadondoka

hari yake mbaya sana twende tukampe msaada”

Monica dereva pamoja na mlinzi

waliingia ndani nakumkuta

sulee damu zikimtoka

kwa wingi ukeni”

“jamani jamani nisaidieni

kumchukua kumpakiza kwenye gari tumpeleke hospital”

walimchukuwa

nakumwingiza katika gari nakumpeleka hospital

kwa matibabu”

“shangazi sulee kazidiwa

sana na damu zinamtoka sana ukeni kapoteza fahamu”

“mko wapi sasa”

“tupo hospital kubwa hapa”

“ok nakuja”

Monica alishangaa sana

alipo kuwa akiongea na shangazi/Mama kwakuto jari sana

angekuwa mwingine ange piga kelele (uwii jamani mwanangu)

lakini ilikuwa tofauti kabisa”

“kutokana na kupanda kwa bp

kwa kiwango kikubwa sana

imesababisha mimba kutoka

sasa mlikuwa mkiishi vipi na

huyu hamkujuwa kama mama

mwenye mimba anatakiwa

usi muudhi wala kufanyishwa kazi ngumu”

“dokta hari ya mgonjwa

imebadilika ghafra sana”

“basi ni hivyo ila kuna vipimo

vingine bado havijaja subiri

sawa mgonjwa mleteeni ndizi laini na uji ok bado anawekewa damu”

“sawa daktar”

“Mama ila

hari yake inaendelea poa

ila mimba imetoka”

“yes”

“shangazi yes wakati kiumbe

kimetoka mbona sikuelewi”

“Monica ni story ndefu kidogo

Nihivi Mimi na doktar Tuli….

Tuli Ongea adanganye

kuwa sulee ana HIV ili

Mumewe amuache nilikuwa

sipendi Sulee akae na Mumewe

kwani alikuwa hana Hadhi ya kuwa na sulee kwakuwa

walipendana na kuwa na ndoa

sikuwa na jinsi ya kuwatenganisha kabisa niliamuwa iwe hivyo tulijuwa

sulee atakuwa katika

mawazo sana na kupandisha BP

itakayo sababisha kujifungua

kwa kupewa dawa ya kukisukuma kiumbe au kutoka mimba mpaka hapo safi atarudi katika hari yake ya kawaida”

“lakini shangazi ulivyo fanya siyo

vizuri kabisa unajuwa”

“nyie mmefanya vizuri au unaongea tu”

“hapana shangazi kuuwa na kumsariti mwenzako

dhambi hazi fanani shangazi”

“kwahiyo mimi ni muuwaji

eeh”

shangazi alifoka kwa hasira sana

mpaka Monica aka shtuka na kujiludi chini.

“sina mana hiyo shangazi

namaanisha kuwa”

“kuwa nini eeh”

“kuwa dhambi ni dhambi tu”

“umeona sasa mbona mimi namuokoa sulee awe na maisha safi wewe unataka kusema mimi

nina kosa wewe Moni nini”

“aah shangazi ila naona upo sahihi tu sijuwi na mimi nitoe hii mimba”

“hapana usitoe takusaidia kuilea sawa sulee nimehangaika nae

tangia mtoto wa miezi mi4 wazazi wake walikufa hivi unajuwa mimi siyo shangazi yake wa damu”

“sijuwi kabisa nilijuwa ni dada wa baba yake wewe”

“hapana baba yake alikuwa dereva tax alikuwa ana nibeba kutoka kazini mpaka nyumbani

tukawa kaka dada baba yake ni mtu wa kenya na mama yake ni mtu wa kenya nae walikutana hapa hapa dar wakawa wapenzi

mpaka waka owana na kumzaa

Sulee, walikufa kwa ajari ya gari

wakitokea Bagamoyo”

“ooh kumbe sasa sulee ana juwa kuhusu hilo”

“hapana kuhusu kufa ana juwa

kuhusu kama mimi siyo shangazi wa damu hajuwi naomba kuhusu suala hili usimwambie sawa”

“nimekuelewa”

baada ya miezi 3:

Sulee alikuwa fiti kama zamani

japo kuwa alikuwa hana furaha kabisa alijaribu kuwasiliana na Mumewe lakini haikuwa poa kwakuwa Sulee aliasirika

Mumewe na sulee mwenyewe walijuwa hivyo

isinge kuwa Rahisi kurudiana

kuwa wapenzi au wana ndoa.

Shangazi alikuwa akimletea

dawa ili ameze kama dozi

ya HIV kumbe zilikuwa za BP

kwakuwa alikuwa hazijuwi dawa

alikuwa akimeza tu Nae Monica

hari yake ilikuwa siyo zuri

kutokana na miezi9 kutimia

ghafra uchungu uka mshika

saa6 usiku ya juma tatu alikimbizwa hospital kufika tu nakulazwa kitandani alipiga kelele sana kuomba msaada kwakuwa uchungua aliusikia

manesi na madaktar walimchukuwa nakumpeleka

katika chumba cha kujifungulia

walimsaidia na kufanikiwa kuzaa

mtoto wa kike.

“hongera sana umejifungua

mtoto wa kike yupo salama”

“ooh asante Mungu”

“sasa wewe pumzika kwanza

sawa mama”

“sawa”

“jamani mzazi wenu

amejifunguwa salama mtoto wakike”

Sulee alifulahi sana kusikia hivyo

“Monica hongera sana mwenzangu fungu lako limekuja

kama wewe”

“sulee asante mwaya”

“sulee hongera sana”

“asante shangazi”

“mh hata mimi sijuwi

angekuwa wakike”

Swali hilo lilimfanya MONICA atoe

machozi

“Monica mbona una lia

acha uchuro badala ufurahi una lia”

“Monica nakumbuka mengi sana

siyo kwaajiri ya mtoto Mume wangu Sulee”

sule aliwaza sana nae alianza

kudondosha machozi kwa sababu

tatu moja ana, hiv mbili kaachika, tatu mimba imetoka:

“jamani mna lia na mimi nifanyeje eeh”

Aliuliza shangazi

bila kupewa jibu Monica na sulee walikumbatiana huku wakilia.

**

Maisha ya mume wa sule yalizidi kuwa magumu kifedha alitamani

kwenda kwa shangazi yake Sulee lakini aliona aibu kwenda kuomba

alivumilia lakini ilizidi sana

kuwa mbaya maana alizoeya

kupewa na shangazi

Nae mume wa monica

ali Rudi kijijini kutokana na maisha kuwa magumu aliingia katika madeni makubwa benk wakataifisha nyumba na gari

lake

**

Sulee kwa nini usiende kupima

tena ujuwe afya yako”

“mimi nasubiri kufa tu”

“hapana sulee nenda wewe

mimi hainiingii akirini eti mimi sina ukimwi na wewe unao

wakati mwanaume mmoja

tumetembea nae”

“inatokea hivyo monica”

“jaribu wewe nakushauri tu

uwenda Mumeo alifanya njama

tu kwa dokta ili akuambie una virusi ili akuache maana aibu tume wapa”

“mh ina wezekana eti lakini haku paswa kufanya hivyo.

“sulee haina haja ya

kufikiria kwa sasa maji yamesha

mwagika kuyazoa haiwezekani kabisa sawa”

“sawa ngoja kesho niende kupima tema hospital kama 4 kwauwakika zaidi uwongo Monica”

“fanya hivyo mpenzi wangu maana unaweza kuishi kwa mawazo wenda huna tatizo hilo

wangu”

“asante Monica”

“ila usimwambie shangazi

kama unaenda kupima sawa”

“kwa nini Monica”

“hupaswi kuuliza kwa nini

fanya hivyo”

_____­­__________­

Dokta kisalawe alimsimulia Adams

Historia yake ya maisha aliyokuwa akiishi Dar najinsi alivyo kuwa akiwa fanyia wanawake za watu:

“Nihivyo Adams nilikuwa nikifanya dhambi kabisa

na sasa nimeamua kuokoka

sitaki dhambi tena”

“Uwamuzi wako mzuri sana

nakupa hongera sana mke wa mtu ni sumu kali sana usipende kupenda au kufanya mapenzi/sex nao utakufa mapema sana, ona mimi sina mke lakini sijihusishi na Mapenzi mpenzi wangu mimi ni kazi/pesa KISARAWE”

“Kweli nakuamini ndugu yangu”

“basi akiri yako wekeza kwenye

kazi jifunze nacho fanya sawa

usiwe na tamaa katika Mari yangu

ukiiba tu nikigundua nakupoteza asee sikutishi nakupa ukweli

angalia ulio wakuta wako vipi”

“sawa Adams nakuahidi sita fanya hivyo”

“asante kama itakuwa kweli”

_____­­__________­

Kisarawe alizidi kuomba Mungu

na kutubu Dhambi zake zote yeye alikuwa mtu wakufunga na kusari

Mpaka Adams alishangaa sana

kubadilika sana alikuwa mkimya

sana hakupenda kabisa ku share na wanawake” Kisarawe vipi

mbona uko hivyo siku hizi”

“kivipi Boss”

“Hapana niite Adams inatosha

kaka”

“ok Adams”

“naona unabadirika sana

mkimya hupendi kukaa na akina dada”

“Adams nimeamua kubadilika

kidogo sipendi kukaa nao nataka

nisahau kabisa matukio yangu ya zamani nikikaa nao nitakumbuka

yaliyo pita na kuanza upya”

“Hivi ulishakuwa na mke”

“kwa nini una uliza hivyo”

“namaana yangu”

“Hapana sikuwa na mke”

“ndomaana ulikuwa ukitembea

na wake za watu”

“kwa nini”

“Ulikuwa huoni uchungu

wa mke ungekuwa na mke

usinge fanya hivyo, tuachane

na hayo kesho Naenda Dar

kuna kampuni moja nimeongea nao kuhusu gari wana hitaji”

“sawa Adams kwahiyo

kuhusu mpango wa sua kuhusu

trekta zile kumi inakuwaje

wamefika milioni95 kila moja”

“ooh nilisaha wambie waongeze 20”

“sawa”

_____­­__________­_

ADAMS akiwa maeneo ya mbezi

alihisi tumbo likimuuma

ndani ya gari yake alikuwa

na Dereva aliye mkodisha

kuendesha gari yake kutokana

na kuto zijua vizuri njia na msongamano wa magari

kama unavyo lijuwa jiji la dar

alikuwa akilala mika sana

dereva alishauri waende

hospital ya Amana

kupima/kupewa matibabu

dk10 walifika na kuchukuliwa

vipimo wakati wakiwa

katika chumba cha kupumzikia wagonjwa walikuwa wengi

wakisubiri majibu yao ya

vipimo walikuwa wakiangalia video iliyo kuwa ipo juu ya ukuta

wote wagonjwa walikuwa wakitazama juu katika video hiyo

lakini kwa Adams ilikuwa tofauti kidogo.

Macho yake yalikuwa kwa Binti

mrembo sana aliye kuwa kakaa upande wa kushoto kwake.

“kaka vipi mbona hivyo”

ilikuwa sauti ya dereva wake

iliyo muuliza:

“ona yule dada alivyo”

“aah kaka mbona kama hao wengi tu wapo hapa Dar tena wazuri kushinda huyo mgonjwa

pesa yako tu kama upo tayali niambie nikupeleke viwanja”

walikuwa wakinong’onezana

masikioni ili watu wengine wasisikie.

“hapana asee Roho yangu

imetua pale asee”

“sasa kaongee nae basi”

“poa subiri hapa hapa”

“Adams alivaa kiheshima sana

ilikuwa suti kwakuwa kulikuwa na joto sana alivua koti na kubakia na shati nyeupe na tai shingoni alipendeza sana.

“samahani kaka”

“bila samahani”

“Naomba nikae hapo ulipo

kaa nataka kuongea na huyu dada”

“ooh sawa kaa”

_____­­__________

Dada habari za kwako

nadhani una umwa maana naona

una mawazo sana muda wote naona umeinama chini”

“Matatizo kaka angu “

“pole sana, samahani kuna kitu nataka kuku uliza kidogo

naomba tukae pembeni kidogo”

“sawa labda wapi”

“kwenye kiti kile ile kama daktar ataita majina iwe lahisi kusikia”

“ok”

“Naitwa Adams j maryo jr.

Naishi Morogoro ni mfanya biashara”

“oh asante kuku fahamu”

“ok, nilikuona Muda wote upo

na hudhuni sana vp nini tatizo”

“Ni Afya yangu tu kaka:..

“Namba 11 ingia”

Ilikuwa sauti ya daktar

iliyo sikika hakuwa mwingine ni yule dada aliye kuwa akiongea na Adams aliinuka na kwenda.

“kaka ngoja niingie nisubiri”

“aliingia ndani kwa doktar..

Habari yako Dada”

“nzuri Doktar,Nipe majibu yangu

ilinijuwe kitakacho endelea katika Maisha yangu”

“Mbona una Haraka sana”

“Doktar ni umuhimu wangu

kujuwa”

“ok unaitwa Sulee siyo”

“ndiyo”

“ok Sasa mbona umekuja peke yako kupima”

“sina Mume wala mpenzi nipo mimi mwenyewe”

“Mh kwanini je mmeachana”

“ndiyo”

“kipindi gani tokea muachane”

“kama miezi 9 na siku kazaa”

“pole sana pole sana”

“doktar nina nini”

“hayo ni maisha yakawaida sana

leo wewe kesho mimi hupaswi kujutia Mungu ana kila sababu kwenye jambo lolote sawa sulee ona wewe ni mzuri sana lakini

leo hii una dosari katika maisha yako usikate tamaa kabisa Dada angu Mungu atakupa nguvu Na..

_____­­__________

Monica Alikuwa ana furaha

kubwa sana Moyoni kwakupata Mtoto japokuwa alikuwa akimkumbuka sana Mume wake

aliumia sana kwa kufikiria sana Jinsi Mumewe alivyo kuwa ana mjari na kumpenda

alijikuta akimuangalia Mtoto wake

huku machozi yakimtoka sana

alianza kumchukia Mtoto wake aliye fanana sana na Kisarawe

alitamani kumtupa au amtelekeze

yule mtoto kwa shangazi

lakini aliona Mtoto hana Hatia

kabisa alizidi kumtunza na kujitahidi kumpenda sana.

_____­­______

Mume wa Monica Aliamuwa kuwa mkulima katika kijiji cha mlali kilichopo mkoa wa Morogoro

alilima mazao lakini yalimgomea

kabisa alikuwa akivuna kidogo sana”Hii itakuwa Radhi ya mke wangu tu kuachana tu maisha yamekuwa magumu sana kila ninacho kifanya kwangu siyo

imekuwaje sijuwi niende kwa Mganga, lakini hapana hapana

siwezi kufanya hivyo kwakuwa huku kijijini hawajuwi kama tumeachana na mke wangu ngoja ni rudi dar nika mtafute mke wangu tujetuishi wote lakini anaweza kukubali kuja kuishi huku sijuwi”

Hayo yalikuwa Mawazo ya

Mume wake na Monica

aliyo kuwa aki waza

_____­­______

Nakushauri Usichoke kutafuta

sawa sulee”

“Doktar doktar sikuelewi”

Sulee aliulza kwa ukali kidogo

huku machozi yakilenga lenga

huku akitetemeka kwa uwoga na presha kupanda”

“hapana sule kuachika siyo mwisho wa kuto pendwa au kupenda utapata Mume bora

na aliye sahihi kwaku kazana kuomba Mungu atakuonyesha”

“doktar nime asirika tawezaje kukaa na Mtu asiye na virusi”

“nani kakwambia kuwa ume Asirika eeh”

“soma hivi hapa vyeti”

“mh Hapana sule vipimo vyetu havisemi hivyo upo salama kabisa

sulee”

“hapana doktar hostpital iyo siunaijuwa nikubwa sana

itadanganyaje hivyo”

“huwezi kujuwa wenda kuna sababu kama ulivyo niambia kuwa umeachika miezi9 naa, wenda ninjama ya mumeo”

“sasa unanishauri vp doktar”

“kapime hospital mbili tena

utapataje majibu”

“asante doktar”

“haya karibu tena”

Sulee alitoka nje hakuwa na kumbukumbukama kuna kijana

nje aliye kuwa na maongezi naye

alitoka huku akielekea mlango wakutokea nje kabisa

“sulee mbona hivyo

jamani”

“nisamehe sana Adams”

“ehee ina kuwaje maongezi yetu”

“ooh tuakae pale”

Kabla ya kukaa

doktar akasikika akisema namba 25 ingia” ilikuwa ninamba ya Adams j maryo jr.

“sulee ni namba yangu hiyo

je uta nisubiri niingie”

“sawa usichelewe sana”

“sawa”

“Pita tu”

“Habari yako doktar”

“salama tu ,wewe ni Adams”

“ndiyo”

“tatizo lako ni mchafuko wa Tumbo tu utaenda Dukani

uta chukuwa dawa hizi nilizo andika sawa”

“sawa kwaheri”

“pita huku “

ADAMS ALIPITA NJIA NYINGINE

NASIYO ILE ALIPO TOKEA SULEE

ADAMS ALICHUKUWA DAWA DUKANI NAKURUDI PALE ALIPO MUACHA DEREVA NA SULEE.

“vipi dereva yuko wapi yule dada

yuko wapi”

“kaondoka mda kidogo kaka”

“khaa sasa sijuwi tampataje

asee”

“kaacha namba yake ya simu

hii hapa”

“afadhari sana ,bac twende zetu

asee”

_____­­__________­_Sule hakutaka kurudi nyumbani

alienda hospital 3 tofauti kupima

tena mpaka saa3 usiku alikuwa akisubiria Majibu hospital zote3

Na majibu yote yalikuwa ni mamoja hana Virusi alikuwa na amani moyoni japokuwa aliambiwa arudi tena kupima baada ya miezi mi2/3

kiuwakika zaidi alirudi nyumbani

huku ana furaha sana.

“vp sulee mbona hivyo

una furaha”

“yani Mungu ashukuriwe

sina Virusi Monica”

“sasa iwe siri usimwambie shangazi sawa”

“mh kwa nini tena”

“utajuwa ukweli badae”

Monica alimwambia sulee vile

ili uadui usitokee kati yao na Shangazi yao

_____­­__________

miezi mi2 sulee alienda tena kupima alipata majibu tena kuwa hana virusi aliwaza sana ninani aliye fanya kitendo hicho cha kuambiwa ana h,i,v aliamuwa kwenda katika hospil ile aliyo ambiwa kuwa ana Virusi ilikumbana doktar yule

ajuwe ukweli.

Alipo fika alimkuta daktar wakike

“zakazi daktar”

“nzuri tu”

“nina shida”

“kiafya au kiofice

“kiofice”

“karibu”

“kuna siku nilikuja hapa kupima…

Kupima H.I.V. Na vyeti vya vipimo vyangu ni hivi hapa unaweza ukasoma.

“Yes inaonyesha umeasirika

Dada angu”

“ooh vizuri je nitarehe ngapi

hapo ina sema”

“eeeeeh eeeeeh ni 21/5/2014, mbona unaniuliza maswali sana”

“asante sana,uta juwa tyuu

usiwe na haraka, Je unaweza

kunisomea katika fairi la ofice hii alikuwepo nani tarehe iyo”

“aah kuna kazi nyingi zakufanya

sahizi niache nihudumie wagonjwa wengine”

Sulee aliingiza mkono

katika pochi yake nakutoka na

wekundu/pesa kazaa nakumpa yule dada/doktar akapokea

nakuweka katika Matiti yake.

“sasa naomba nisaidiye

kumjuwa ninani alikuwepo”

“ok subiri”

Baada ya dk5

Alisha pata jibu alikuwa ninani

“nimeona alikuwa ni

doktar john nimnene mweusi

ana nywele nyingi hivi”

“huyo huyo”

“sasa kafanyaje”

“habari ndefu sana wangu

angalia hivi vyeti nausome”

Doktar huyo alisoma

vyote vi nne alitoa pumzi

uphuuuu kisha akamtazama

kwa huzuni sana sulee kisha akainuka

nakumshika bega.

“sulee pole sana hiyo nikawaida yake huyo doktar hafai hata kwa dawa nakushauri fanya unavyo taka kufanya”

“ok nataka kujuwa ukweli tu

aliyemtuma afanye hivyo ninani”

“sawa”

Sulee alianza kufanya mipango:

alianzia Mahakamani

moja kwa moja kwakumshtaki

doktar john kwakumpa vipimo vyauwongo.

Kesi ilisumwa kort chemba

sulee hakutaka yawe makubwa

kwa doktar yeye alitaka ajuwe tu ninani alifanya vile tu.

Monica alikuwa akihisi kuwa ni Mume wangu ili tuachane, Lakini mbona alisema nisimwambie Shangazi kuhusu ilo suara.

Sulee alijiuliza moyoni

Doktar alibanwa sana mwisho akakubali kuwa alipewa pesa

na shangazi yake sulee adanganye majibu kuwa sulee ana ukimwi

ili aachane na Mumewe,(japo kuwa shangazi na sulee alikubaliana na Mume wa sule kuwa kama watakuwa wazima wote Mume wa sulee ange msamehe sulee)

“ok vizuri sana”

Kutokana na sifa za doktar huyo

kuwa mbaya anahusika na utoaji mimba NK. Mahakama iliamuwa kumfungia kazi kwa muda usiyo julikana.

Sulee ali Rudi nyumbani

huku akiwa na hasira sana

alikuwa ana hamu sana amkute shangazi yake

Lakini hakumkuta.

“kweli Monica doktar kakubali

kumbe shangazi ndiye kafanya tukio langu hilo eti kisa tuachane

na mume wangu, tulikubaliana

kama tutakuwa hatuna Virusi tungeendelea kukaa wote licha

yakuwa na mimba siyo yake”

“Sasa utafanyaje sulee”

“nataka kumchana live”

“Hapana Sulee kumbuka

hatuna pakwenda”

“potelea mbali liwalo na liwe

nimesha pagawa kasababisha kutoka kwa mimba yangu inauma sana nilikuwa nikikaa kwa Huzuni kama naumwa nilikonda kama

kweli na ngoma Monica siwezi kumsamehe Mimi”

“Sulee huoni kama ndiyo utakuwa

mwisho wetu wakukaa hapa”

“mmh popote mimi takwenda kukaa mimi”

“na mimi je”

“najuwa atanifukuza mimi

tu siyo wewe”

“hapana sulee atajuwa nime kwambia mimi hiyo siri”

“siri siri siri gani tena hiyo

Monica”

“kuwa wewe hauna ukimwi”

“mh mbona unanichanganya inamaana hata wewe ulikuwa ukijuwa kuwa mimi sina ukimwi

Monica mbona haukuniambia

mimi kwa nini kwa nini Monica

hukuniambia mapema

mpaka mimba yangu imetoka

Monicaaaaaa….

ITAENDELEA

Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Nne

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment