Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Kwanza
CHOMBEZO

Ep 01: Dokta Mimi Siumwi Huko

SIMULIZI Dokta Mimi Siumwi Huko
Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Kwanza

IMEANDIKWA NA: 2JIACHIE

*********************************************************************************

Chombezo: Dokta Mimi Siumwi Huko

Sehemu ya Kwanza (1)

“Ulikwenda hospitali mke wangu?” Masofa alimuuliza mke wake Sulee.

“Nilikwenda, lakini daktari kasema mimba nitapata tu ndani ya mwezi mmoja.”

“Ndani ya mwezi mmoja utapata mimba? Inawezekana kweli? Hujamwambia kwamba tumehangaika kutafuta mtoto kwa miaka nane, sasa ndani ya mwezi mmoja mimba itapatikana vipi?”

“Mimi sijui Masofa.”

“Mh! Haya, kwa sababu tumeambiwa na mtu tunayemwamini tuangalie, labda kweli daktari yule atatusaidia. Hakusema uende na mimi?”

“Hakusema Masofa, ila alisema kama naweza kesho na keshokutwa niende usiku saa moja ili anipime vizuri.”

“Alikupa dawa?”

“Dawa atanipa kesho.”

Masofa alichukua simu akampigia rafiki yake Miraji…

“Ee bwana Miraji, yule dokta uliyemsema kasema ‘waifu’ aende kesho saa moja usiku, wewe si unamwamini?”

“Yule hana neno, aende tu. Bwana Masofa we hukumbuki jinsi mimi na shemeji yako tulivyohangaika kutafita mtoto?”

“Nakumbuka.”

“Sasa kama si huyo daktari wa wanawake unadhani tungepata mtoto?”

“Oke, nimekuelewa bwana Miraji.”

“Sawa Masofa.”

Masofa alikata simu, akaendelea kukaa chumbani. Akili yake ilikuwa nzito sana kumruhusu mkewe arudi hospitali kesho yake, tena usiku wa saa moja…

“Sasa huyo daktari wa watoto ni kwa nini anataka mke wangu arudi usiku? Ni tiba gani hiyo ya usiku wa saa moja?”


Siku ya pili iliingia, saa moja jioni Sulee alikuwa kwa daktari wa wanawake anaitwa Dokta Kisarawe.

Dokta Kisarawe alikuwa amekaa ndani ya chumba cha utabibu kwenye zahanati yake huku akimwangalia Sulee kwa macho yenye huruma…

“Kwa hiyo tatizo kubwa ni mtoto tu anti yangu?”

“Ni mtoto tu.”

“Miraji unamjua?”

“Ndiyo, ni rafiki wa mume wangu Masofa kwani vipi dokta, mbona umemtaja huyo?”

“Ah! Nimeangalia kwenye maelezo yako, nikagundua kuwa mnatoka eneo moja kwa maana ya ubalozi…,” Dokta Kisarawe alijibu huku akimuangalia Sulee kwa macho ya kumkagua f’lani hivi.

“Ooh…!, maana nilishangaa ni kwa nini umuulize huyo na umejuaje kama ninafahamiana naye…,” Sulee alihoji huku akiyakimbiza macho yake pembeni baada ya kukutanisha na ya Dokta Kisarawe.

“Hata mkewe alikuwa na tatizo kama la kwako, lakini aliponea kupitia mikono hiihii…”

“Kweli dokta…?”

“Kweli nakuambia, niamini mimi.”

“Mm!, sawa lakini nimesumbuka sana kwani naumia kukosa mtoto jamani…,” alisema Sulee safari hii akionesha sura ya upole zaidi, hali iliyomfanya Dokta Kisarawe amkazie macho zaidi.

“Kwani mmehangaika kwa muda mrefu sana anti…?”

“Yaani wee acha tu dokta, ikishindikana na hapa itabidi niridhike tu kuwa sikupangiwa kuzaa kabisa…”

“Ndoa yenu ina muda gani sasa…?,” Dokta Kisarawe alizidi kumdadisi Sulee huku muda nao ukizidi kuyoyoma na tayari saa iliyokuwa ukutani ilisomeka saa mbili na dakika nne.

“Miaka mitatu sasa dokta…”

“Mm..!”

“Mbona unaguna dokta jamani, au huamini?”

“Hapana anti, naguna kwa kushangaa mwanamke mzuri kama wewe hujapata mtoto…!,” alijibu Dokta Kisarawe huku akimkazia macho Sulee hasa maeneo ya kifuani na mapajani kutokana na sketi aliyokuwa amevaa kupanda hadi kuvuka juu ya magoti.

“Kwani mimi mzuri ja..ma..ni…?,” aliuliza Sulee lakini safari hii kwa sauti iliyokatakata.

“Dah! Wewe ni mzuri sana anti, nashangaa hadi sasa hujapata mwanaume wa kukupa mimba…!”

Hapo Sulee hakusema neno zaidi ya kuendelea kumtumbulia macho Dokta Kisarawe aliyekuwa bize na kumungalia.

Alipoona Sulee yuko kimya, Dokta Kisarawe akazidi kumsifia huku akimhakikishia ni lazima atapata mimba.

“Yaani mwanamke umeumbika haswa, ona maeneo kama haya ya kifuani jamani…,” Dokta Kisarawe aliendelea kumchombeza Sulee huku sasa akionesha kwa vitendo na kuyagusa maeneo ya kifuani ya mwanamke huyo mrembo wa sura na umbo achilia mbali rangi yake ya chokoleti.

“Kwe…kwe…lii dokta jamani…?,” Sulee aliuliza kama kweli anaweza kuzaa lakini kwa sauti ya mkwamo kutokana na mkono wa dokta kugusa maeneo nyeti ya kifuani.

“Duh! yaani anti na nido nzuri kama hizi halafu huzai…!”

“Mm!,” Sulee aliishia kuguna huku akijikunja kiaina kwani safari hii vidole vya dokta viligusa kisawasawa nido zake kutokana na blauzi nyepesi aliyoivaa mwanamke huyo.

“Hujapata tu mwanaume rijali…”

“Kwa nini unasema hivyo dokta jamani…,” Sulee aliuliza katika hali ya kutojiweza, huku macho yake yakianza kubadilika rangi na kuwa mekundu kiasi.

“Mimi ni daktari si kwa matokeo ya mtihani bali kwa kukidhi vigezo, ina maana nina uwezo wa kujua tatizo la mgonjwa hata kwa saikolojia tu, yaani wewe unahitaji mwanaume rijali tu, kweli tena nakuambia,” Dokta Kisarawe alizidi kutoa maelekezo kwa vitendo zaidi na safari hii mikono yake ikiparaza juu ya mapaja ya Sulee.

“Aah! Sasa huyo mwanaume rijali nitampata wapi jamani mbona haya ni majaribu sana dokta…?”

“Kha! Mbona wapo wengi sana, huko mitaani au hata mimi…”

“Mimi wa mitaani naogopa, mume wangu ni mkorofi sana…”

“Basi mimi…,” Dokta Kisarawe alipasua ukweli wake huku mikono yake ikiwa na kazi ya kumpapasa na kumbinya kimtindo Sulee, kuanzia maeneo ya kifuani, mapajani hadi mgongoni na kumalizia kwenye kiuno kipana na cha mviringo cha mwanamke huyo.

Kutokana na joto la mikono ya dokta, Sulee alikuwa akipeleka upinzani hafifu na kuruhusu mikono hiyo izidi kutalii kadri iwezavyo na kumuacha akilalamika kimahaba huku akitamka maneno ya kukolea penzi.

“Aaah, jamani dokta lakini mimi siumwi huukooo…,” Sulee alilalama huku akitoa ushirikiano kwa dokta.

Baada ya kuona amekolea, Dokta Kisarawe hakuwa na ajizi zaidi ya kumuandaa na kumsogeza hadi kwenye kitanda kilichotumika kwa wagonjwa kulazwa wakiwemo wale wa kujifungua.

Dakika chache kila mtu akawa ameiva na kuhitaji kukabiliwa na mwenzake, vilio na miguno ya kimahaba vikatawala ndani ya chumba hicho cha Dokta Kisarawe.

Haikuchukua muda mrefu, Sulee akatangaza kufika mwisho wa safari na dokta akimkaribisha kwa bashasha zote.

Baada ya shughuli pevu, dokta alimtaka Sulee arudi siku ya kesho kwa ajili ya vipimo zaidi kwa wakati huo, muda ulikuwa umekwenda.

“Ahsante sana dokta jamani, wewe ni tofauti sana…,” alisema Sulee baada ya kuagana na dokta na kisha kuondoka huku akiangalia nyuma.


Masofa ambaye ni mume wa Sulee alikuwa sebuleni akimsubiri mkewe ambaye alichelewa sana kurudi kutoka kwa dokta.

“Ina maana huyu hadi sasa ni tiba gani hiyo…,” alijiuliza Masofa akiwa na hasira.

Wakati akiwaza hayo, alisikia hodi na kwenda kufungua akakuta ni mkewe.

“Jamani mke wangu Sulee, hadi saa hizi ulikuwa kwa dokta tu…?”

“Sasa kumbe nilikuwa wapi tena jamani mume wangu…?,” alijibu Sulee huku akitupia mkoba wake kwenye kochi.

“Dokta alikuwa na watu wengi, ndiyo maana nimechelewa kwani sasa hivi saa ngapi?”

“Angalia saa mwenyewe…”

“Mm! yaani saa tano kasoro mara hii…!”

“Haya, niambie huyo dokta amesema nini…?”

“Kwa leo amenipa ushauri tu wa kisaikolojia, amesema nirudi tena kesho muda kama wa leo…,” alijibu Sulee.

“Mm!, ina maana leo amekupa ushauri tu…?”

“Ee mume wangu…”

“Inabidi kesho twende wote…,” alisema Masofa na kumuacha Sulee ametumbua macho.

“Sasa mbona umekaa kimya, umenielewa…?” aliuliza tena Masofa akiwa amemkazia macho Sulee aliyekuwa bado amemtumbulia macho ya mshangao.

“Mm…!,” aliguna Sulee kabla ya kukubaliana na uamuzi wa mumewe, hapo moyoni alibaki na maswali mengi juu ya hali itakavyokuwa baada ya kufika kwa dokta siku inayofuata.

“Sawa,” aliitikia huku akitingisha miguu mahali alipokuwa amekaa.

“Sawa, ndiyo nini…?”

“Kha!, si nimekubaliana na ulichosema…!,” alisema Sulee huku akimwangalia mumewa kwa jicho la ‘usinichoshe bwana’.

Masofa alibaki kimya kidogo, akaanza kuondoka kuingia chumbani huku akigeuka na kumwangalia Sulee.

Muda mfupi badaye, Sulee aliungana na mumewe chumbani ambapo bila hata kuvua nguo alijitupa kitandani.

“Aah, nianche bwana…,” alikuwa ni Sulee akimjibu mumewe aliyekuwa bize kwa kumshika sehemu mbalimbali za mwili hasa maeneo ya nyuma akiomba kutafuna tunda.

“Sasa nikuacheje jamani mke wangu…?”

“Mimi nimechoka bwana…”

“Umechoka na nini…”

“Kha! si kazi jamani, au watu huchoka na nini…?”

Masofa hakujibu kitu zaidi ya kusitisha alichokuwa anakiomba.

Walipitiwa na usingizi hadi asubuhi ambapo Masofa alikuwa wa kwanza kuamka kabla ya Sulee aliyekuwa bado akiufaidi usingizi wa asubuhi uliokuwa ukisindikizwa na kibaridi cha alfajiri.

Masofa alijiandaa na kuelekea kazini, hakutaka kumsumbua Sulee akihofia mzozo usiokuwa na maana kwani aliyakumbuka vyema majibu yake ya jana.


Sulee aliendelea kulala hadi saa tatu na nusu aliposhituka ghafla. Akakurupuka na kukimbilia bafuni ambako alioga kabla ya kuanza kuandaa kinywaji.

Akiwa anakunywa chai, ghafla mazungumzo na majibizano yake ya jana na mumewe Masofa yakaanza kujirudia kichwani mwake.

“Haya, niambie huyo dokta

amesema nini…?”

“Kwa leo amenipa ushauri

tu wa kisaikolojia, amesema

nirudi kesho muda

kama wa leo…,” .

“Mm!, ina maana leo

amekupa usahauri tu…?”

“Ee mume wangu…”

“Inabidi kesho twende…”

Kufika hapo, Sulee akaishiwa nguvu kimtindo.

“Sasa huyu naye anataka twende wote kwa dokta ili iweje?, wengine wanasumbuliwa na wivu, sasa kama yeye kazi hawezi si awaachie wenzake…”, aliwaza Sulee.

Akaendelea na majukumu mengine kama mama wa nyumbani, huku moyoni akiombea mumewe apatwe na dharura yoyote ili asiende naye kwa Dokta Kisarawe!

Mawazo yakampeleka hadi kwa Dokta Kisarawe ambaye tayari hisia za mapenzi zilishaanza kuchipuka baada ya kupatiwa raha ya ajabu jana yake.

“Nakupenda, nakutaka, nakuhitajiiii….moyo wangu wakuwazaaa… mpenzi uko mbali namii….,” Sulee alijikjuta akiimba wimbo huo wa Lady Jay Dee uitywao Distance baada ya hisia juu ya Dokta Kisarawe kuzidi kumuwaka vibaya…!”

Hatimaye muda wa mumewe kutoka kazini uliwadia, ambapo maandaliazi ya kwenda kwa dokta yakaanza.

Ilipotimu saa moja na nusu, Masofa akiwa na mkewe walikuwa njiani kuelekea kwa Dokta Kisarawe.

Wakamkuta dokta akiwa peke yake kwenye chumba chake akiwa bize na ukaguzi wa mafaili mbalimbali ya wagonjwa.

Dokta Kisarawe alipomuona Sulee, mapigo ya moyo wake yakaongezeka, ikabaki kidogo tu aropoke jambo ambalo lingeharibu kila kitu.

“Jamani hon…,” alijikuta akikomea njiani japokuwa lile neon hon alitaka kutamka haoney, lakini akajikuta akibadili haraka baada ya machale kumcheza haraka.

“Hata haujachelewa, aisee unazingatia sana muda…”

“Kawaida tu dokta…,” alijibu Sulee huku akijifanya kuvaa sura ya ubize kidogo.

“Ehee, naona umekuja na mgeni…”

“Siyo mgeni, huyu ndiye mume wangu…”

“Ooh, karibu sana….”

“Ahsante…,”aliitikia Masofa huku akimuangalia Dokta Kisarawe kwa jicho la “si utoe tiba tuondoke.”

“Dokta Kisarawe naye akamwangali kama anayesema “Mbona umekaa kitemi sana.”

“Ok, sasa sikiliza anti, nadhani jana uliyaelewa maelekezo yangu…”

“Ndiyo dokta…”

“Kuna dawa nitakupa kwa leo, ambazo utazitumia kwa siku tatu mfululizo kabla ya kurudi tena…”

“Sawa, dokta…”.

Dokta Kisarawe akainama na kutoa kopo f’lani lililokuwa na dawa za vidonge, pamoja na zingine za maji!

“Hizi dawa ni muhimu sana, katumie kwa mtindo niliokuelekeza jana…”

“Sawa.”

Baada ya maelekezo hayo, waliagana kwa kupeana mikono huku Dokta Kisarawe akimpa moyo Masofa kuwa mkewe atapona na kuondokana kabisa na tatizo la kutozaa.

“Usijali, mkeo atapona tu…”

“Ahsante sana dokta…,” alisema Masofa huku akipeana mkono.

Wakaachiana mikono lakini Dokta Kisarawe akawa anamtupia jicho Sulee aliyekuwa kimya muda wote.


Toka siku hiyo, Dokta Kisarawe akawa anashinda akila karanga pamoja na kunywa mchuzi wa pweza kwa wingi, yote hiyo akiwa amempania Sulee atakapokuja siku ya tatu, kwani aliamini kwa vyovyote vile ni lazima aende peke yake.

Kila mara Dokta Kisarawe hakuacha kumkumbuka Sulee…!

“Dah, yule ni mwanamke bwana…,” aliwaza Dokta Kisarawe jioni moja akiwa amejipumzisha.

“Halafu, si nilimwambia aje baada ya siku tatu…?,” aliendelea kujiuliza maswali mengi.

“Eeh bwana…Ina maana kesho yupo hapa…Afadhali, kesho nitabimbilika naye tena…,” akaendelea kujikumbusha mwenyewe ndani ya chumba hicho.

“Twende mbele, turudi nyuma, aisee yule ni demu…Na hata muumba aliposema nitakufanyia msaidizi, alimaanisha yule…Kweli tena, fuatilia sana…,” Dokta Kisarawe akazidi kuzama kwenye mawazo hayo ya kujibizana na nafsi yake.

Dozi kali ya mchuzi wa pweza na karanga mbichi kwa wingi alizokuwa akizitumia Dokta Kisarawe, ziliendelea kumuweka sawa kwa ajili ya mechi kali ya kukata na shoka siku atakapokutana na Sulee.

“Mume wangu si unakumbuka dokta alisema nirudi baada ya siku mbili…?,” Sulee alimuuliza mumewe baada ya siku hiyo kufika.

“Kha!, sasa mimi na wewe nani anapaswa akumbuke…?,” Masofa alimjibu kwa mkato na sauti ya kishari.

“Wote…,” Sulee naye akajibu kishari huku akimtupia jicho.“Halafu wewe siku hizi mtata sana…”

“Nakumbuka basi, unasemaje…?”

“Basi ni leo…”

“Sasa ulikuwa unauliza au kunitaarifu…?,” Masofa alijibu lakini safari hii akiwa ‘siriasi’ zaidi.

Maisha ya Sulee na Masofa ndani ya ndoa yao, yalikuwa yameshaanza kuingia dosari.

Hii ni kutokana na hali ya Sulee kutopata ujauzito.

Sulee alinyamaza na kuendelea na shughuli zake. Masofa naye akaondoka kwenda kwenye mihangaiko yake ya kila siku.

Jioni ilipofika, Sulee alijiandaa kwa ajili ya kwenda kuonana na Dokta Kisarawe, moyoni akiwa amepania sana kupata tiba ya uhakika.

Akaianza safari ya kuelelekea kwenye zahanati ya daktari huyo. Alipofika alimkuta akiwa na mwanamke mwingine ndani, ikabidi asubiri nje.

Dakika moja baadaye, yule mwanamke aliondoka na kumpa nafasi Sulee kumuona Dokta Kisarawe…

“Niambie jamani…,” alisema Sulee huku akipanua mikono yake ili kumruhusu Dokta Kisarawe amkumbatie.

“Safi tu, mbona una furaha sana…?”

“Aah!, si nimefurahi kukuona jamani, au hupendi…?,” Alijibu Sulee wakiwa bado wanaendelea kukumbatiana.

“Sijasema hivyo, vipi kwema lakini…?”

“Kwema tu, naona ulikuwa na mwanamke humu, naye ana tatizo kama la kwangu…?”

“Hapana, kuna dawa nilikuwa namuelekeza, vipi mume mwenzangu mzima…?,” Alijibu Dokta Kiasarawe lakini mikono yake ikianza kukosa utulivu mwilini mwa Sulee.

“Aah!, jamani sa…saaa…,” Sulee alijaribu kuuliza lakini tayari joto la miili yao lilikuwa likimuendea ndivyo sivyo.

“Sasa kwani nini tena jamani…?,” Dokta Kisarawe aliuliza huku mikono ikiendelea kuutalii kwa utundu wa hali ya juu sana mwili wa Sulee.

“Aaa….h, mmh…,” Sulee alishindwa kuvumilia utundu wa mikono ya Dokta Kisarawe ambaye sasa alikuwa amemsogeza karibu kabisa na kifua chake kuliko hapo awali.

Mikono ikashuka hadi kwenye kiuno cha Sulee kilichobinuka vyema na kujitenga kwa juu.

Akawa kama anakibinya kimtindo, hali iliyomfanya Sulee apige ukelele wa kuashiria kuguswa yalipo maruhani yake.

Dokta Kisarawe hakuishia hapo, sasa akawa anaparaza kifuani na kuzigusa nido kimtindo…

Sulee akawa anajinyonga huku naye akirudisha mashambulizi kwa kummiliki Dokta Kisarawe.

Ikafika wakati kila wakishikana, wanakuwa wanalegezana nguo taratibu, baadaye kila mmoja alijikuta akiwa kama alivyokuja duniani.

Dokta Kisarawe akamuweka sawa Sulee kwa chini na kuanza kuchimba chumvi kisimani hali iliyozidisha uraha wa ajabu kwa Sulee.

“Yes, yesiii..yee..eee…siiiiii…..,” Sulee alizidi kuitikia kila alichoulizwa na Dokta Kisarawe.

Wakati akichimba chumvi, mikono ya Dokta Kisarawe ikawa bize na kifua cha Sulee, alizishika nido na kuzizungusha, Sulee akawa hana cha kufanya, akatoa macho yake meupe na kuyazungusha huku na kule.

Sulee aliposhindwa na uzalendo, akamgeuza Dokta Kisarawe na kuikimbilia maiki yake, akaishika vyema na kuanza kuimba nyimbo mbalimbali tamu.

Dokta Kisarawe akawa anasikilizia utamu wa mashairi ya Sulee kwa kufuatisha alivyokuwa akiimba.

Muda wa sebene ukawadia, kila mmoja akamuweka sawa mwenzake. Mechi kali ikaanza.

ILIKUWA ni furaha ya aina yake kwa Dokta Kisarawe japo kwa Sulee ilitegemea na biti kwani wakati mwingine aliisikia sauti ikimwambia…

“Lakini wewe ni mke wa mtu, unalijua hilo?”

Sulee alishindana na akili zake kuhusu hilo, lakini sasa mapigo ya Dokta Kisarawe yalimfanya asitishe kwa muda kuwaza mambo hayo na kumpa ushirikiano mzuri…

“Dokta,” aliita Sulee lakini hakuitikiwa kwani dokta alijitahidi ili amalize haraka na kuwahudumia wagonjwa wengine.

Hivyo alijitahidi kupiga mipira ya karibu. Sulee alikuwa hoi, kwa sababu alisimama, miguu iligoma kufanya kazi, akataka kukaa kwenye kiti lakini nafasi hiyo haikupatikana kwa Dokta Kisarawe.

Ni Sulee huyohuyo ndiye aliyeanza kutangaza hali ya hatari golini kwake, dokta akambana vizuri zaidi ili kumkinga na anguko lolote…

“Dokta…dokta nipe mtoto basi,” alisema Sulee akitaka kujitoa kwa dokta baada ya kupasua dafu lake lakini dokta ambaye alihamasishwa na lugha hiyo alimzuia na yeye akatangaza kushuka chini ya mnazi na kuvunja dafu lake, wote wakavunja madafu yao.

Mlio wa pangaboi ndani ya chumba hicho cha dokta ndiyo uliosikika pekee huku kila mmoja akiwa hana la kumwambia mwenzake. Sulee alikaa kwenye kiti na kuinamia meza, dokta alisimama, mkono mmoja ulishika sehemu ya juu ya suruali yake akiiziba njia.

“Wewe Sulee wewe, hivi kweli umekuja kutibiwa au kutibua?” Sulee alisikia sauti ikimwambia hivyo…

“Nimekuja kutibiwa,” eti Sulee aliijibu ile sauti kwa kujiamini.

Sasa alikaa vizuri, dokta naye alikuwa kwenye eneo lake la kiti akimwangalia mwanamke huyo, aliyeumbika sawa na mapenzi ya muumba.

Wote walijikuta wakicheka, lakini Sulee akakatisha kicheko kwa swali…

“Hivi mfano dokta…”

“Ee…”

“Ikitokea nimepata mimba mtoto wa nani?”

“Si wa kwako!”

“Hutamtaka?”

“Ha! Nimtakie nini wakati mimi nina mke wangu na watoto watatu, nimtake mtoto wako sijitaki kwangu?”

“Kwa hiyo unaniahidi?”

“Nakuahidi Sulee wala usiwe na wasiwasi.”

Siku hiyo Dokta Kisarawe hakumpa dawa yoyote Sulee, akamwambia akaishi kwa siku thelathini kamili halafu arudi tena…

“Noo dokta, mume wagu ataniuliza dawa ziko wapi?”

“Oke…oke, basi chukua hizi, akikuuliza muoneshe…” Dokta Kisarawe alimpa Sulee vidonge vya kutibu mifupa, maarufu kwa jina la ‘indosidi’.

“Hapo sawa.”

Sulee aliondoka akiwa mwepesi sana, alitembea kwa madaha kurudi nyumbani kwake.


Usiku wakiwa kitandani, mume wake alimuuliza…

“Vipi hospitali?”

“Nilikwenda.”

“Walikupa dawa?”

“Ndiyo.”

“Dawa gani?”

“Mi sizijui, sijui zinaitwaje!”

“Ziko wapi?”

“Sulee alitoka kitandani kwenda kuzichukua, akampa mumewe…

“Hizi siyo za kuongeza damu?”

“Mi sijui, alisema niwe nameza vidonge viwili kwa siku mpaka mwezi mmoja uishe halafu niende tena.”

“Sawa. Tutaona, kama hakuna matumaini itabidi tuachane naye,” alisema mwanaume huyo akiwa amelala anaangalia juu.


Mwezi mmoja na siku mbili, siku hiyo Sulee alijiandaa vilivyo, si kama anakwenda kwa daktari kupata tiba ili anakwenda kwa mpenzi wake. Kama mumewe angekuwepo nyumbani angemzuia kuvaa alivyovaa…

“Hapa niko sawa, mwenyewe akiniona atajua mimi ni mwanamke wa nguvu. Lakini Dokta Kisarawe naye, mh! Sijui alikwenda chuoni!”

Sulee alikuta wagonjwa wengine, akapanga foleni akiwa ni mtu wa kumi na saba mpaka kuingia chumba cha daktari. Alipita nesi…

“Samahani anti, mwambie Dokta Kisarawe nipo hapa nje.”

“Mh! Unadhani ataweza kuwaacha wenzako wote hawa akakuwahi wewe tu?” alihoji yule nesi.

“Sijasema awaache, nimekwambia mwambie nipo hapa nje.”

“Umesema nani vile?”

“Sulee.”

“Haya, subiri.”

Nesi aliingia kwa dokta, aliweka cha kuweka kabla hajatoka akamwambia…

“Kuna dada anaitwa Sulee, anasema amefika.”

“Kwa hiyo?”

“Kasema nikwambie.”

“Oke, mwambie umeshaniambia, asubiri. Yeye anadhani ni wa maana kuliko wenzako siyo?”

Nesi alitoka akafunga mlango huku macho yake yakikutana na macho ya Sulee…

“Nimemwambia anti, lakini hajanijibu kitu.”

Sulee kuna kitu kiligonga kichwani mwake…

“Au wanawake wote hawa ni wake, kwa hiyo kila mmoja ana umuhimu kwake? Maana kama mimi tu ndiyo mtu wake angetoa jibu lolote lile, isitoshe hatujaonana siku nyingi, mwezi na kitu sasa.”

“Aingie mwingine,” alisema Dokta Kisarawe akiwa amesimama mlangoni, alikutana macho na Sulee lakini hakuonesha uchangamfu wowote ule.

Dakika tano baada ya huyo mwanamke kuingia, vicheko na kugongeana mikono kulisikika kutoka kule ndani.

Sulee akaamua kunyanyuka mahali alipokuwa amekaa na kusogea karibu kabisa na mlango.

Akawa anategesha sikio kusikia zaidi kinachoendelea ndani ya chumba cha Dokta Kisarawe.

Vicheko viliendelea kusikika, kugongeana mikono kukazidi kuchukua nafasi kubwa….!

Sulee alirudi hadi alipokuwa ameketi awali, nakuanza kujiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu.

“Hivi, wanaweza kuwa wanafahamiana kweli…?”

“Kha, lakini nami bwana, sasa kama hawafahamiana wanawezaje kucheka na kugongesheana mikono namna hiyo…?”

“Kwa vyovyote vile watakuwa wanafahamiana tu, ngoja nifuatilie sana…!

“Sasa kama wanafahamiana, kuna uwezekano huyu dokta kuwa anatuchanganya…?”

“Yawezekana…”

“Lakini ni sisi wanawake yawezekana ndiyo tunajichanganya…,” Sulee aliendelea kujisemea juu ya hali aliyoiona kwa siku hiyo.

“Ina maana kila mwanamke mwenye ugonjwa kama wangu, ni lazima atembee na huyu dokta ndiyo apone…?”

“Sasa kama ni hivyo atakuwa ametembea na wangapi?”

“Kama ndiyo mtindo wake, kwa nini sisi wanawake tusishituke ?”

“Kuna uwezekano wanawake wengi wanajua, lakini nani wa kuvujisha siri kama anapokea dozi ya maana ya Dokta Kisarawe…? Halafu sasa unakuta wengi wao ni wake za watu, lakini sisi wanawake bwana…!

“Sisi wanawake siyo, wewe tufuatilie sana, siyo kwa sababu haiwezekani wote hawa tutembee na mtu mmoja na siri isijulikane…,” maswali yakazidi kumchanganya Sulee mahali alipokuwa amekaa.

Lakini kwa wakati wote huo akiwa amekaa kwenye ile foleni, macho yake hayakuwa yanabanduka kwenye mlango wa ofisi ya Dokta Kisarawe…

“Lakini mimi naye bwana, sasa nimethibitishaje kuwa ni wapenzi labda huenda wanafahamiana tu na umepita muda mrefu bila kuonana?”

“Lakini, kufahamiana gani huko wanacheka hadi kugonganisha mikono kwa sana…?”

“Sasa kwani kugongeana mikono kuna maanisha nini…?,” Sulee akazidi kujihoji na kujijibu mwenyewe, hali ilishaanza kuwa tete ndani yake. Moyo haukuwa na amani tena na kidonda cha wivu kilishaanza kumnyemelea.

“Yaani kweli mambo anayonifanyia Dokta Kisarawe, anaweza kumfanyia mwanamke mwingine kweli?”

“Eee, inawezekana kwani kama aliweza kwako ni kivipi asiwafanyie wengine…,” ilisikika sauti ikimjibu kutoka upande wa pili wa moyo wake.

“Ila kweli, hilo nalo neno.”

Sulee aliendelea kujihoji na kujijibu mwenyewe. Hali haikuwa hali. Dokta Kisarawe alikuwa amemuingia moyoni mwake, sasa alikuwa haambiliki wala kusikia chochote juu yake.

“Haya mapenzi bwanaaa, hayana maana….,” wimbo wa Diamond ulisikika masikioni mwake baada ya kushindwa kuhimili vishindo vya maumivu ya wivu wa mapenzi.

Muda mfupi baadaye, Sulee aliamua kusogea tena karibu kabisa na mlango wa ofisi ya Dokta Kisarawe. Lengo la safari hii ni kusikia nini kilikuwa kikiendelea ofisini humo.

Sulee alishituka baada ya kusikia sauti za kunong’ona kwa chini sana tofauti na awali ambapo Dokta Kisarawe na mteja wake walikuwa wakizungumza kwa sauti ya juu.

Safari hii alisikia watu wakibusiana, moyo ukazidi kumuuma…

Akajishika kifuani kwa upande wa kushoto ulipo moyo, mapigo yakazidi kumuenda mbio.

Dakika mbili baadaye, alianza kusikia miguno na sauti ya meza na kiti vikisogea…Moyo ukazidi kumuuma kuliko kawaida.

“Kuchiii…..kwaguuu…vegeeee….vegeeee…..vigi…vigiiiii….,” milio ya kiti na meza viliendelea kusikika na kuzidi kumpa maswali mengi sana Sulee…

Mbali na milio ya samani hizo, miguno na mihemo ya chini ikazidi kusikika, kila dalili ya watu kula mua ikawa inajionesha wazi…

Sulee akashindwa kuvumilia, akarudi kwenye kiti. Dakika tano baadaye yule mwanamke akatoka. Dokta Kisarawe naye akatoka nje na kumuita mwanamke mwingine. Lakini wakati akimuita mtu mwingine, macho yake na ya Sulee yalikutana lakini hakuonesha dalili yoyote ya kumchangamkia (Sulee). Hali hiyo ikazidi kumchanganya kabisa Sulee.

Kuna kipindi akataka kuondoka lakini akazidi kujipa moyo na kuendelea kusubiri aone hatma ya mchezo wa siku hiyo.

“Kha, au kuna kitu nimemkosea ndiyo maana kachukia namna hii, au niondoke? Lakini nikiondoka wakati nimeshafika hapa itakuwa si busara. Ngoja niangalie mwisho wa hii sinema…,” akawaza moyoni Sulee.

Hatimaye wote wakaisha na kubaki kwenye benchi peke yake. Akadhani sasa zamu yake imewadia. Lakini alishangaa kumuona Dokta Kisarawe akitoka huku akifunga mlango wa ofisi yake kwa ufunguo.

Kuona hivyo, Sulee akahamaki na kumuuliza kulikoni iwe hivyo na vipi kuhusu tiba yake kwa siku hiyo?

“Haa, sasa Dokta mbona unaondoka vipi kuhusu mimi jamani…?

“Kuhusu wewe nini tena…”

“Si tiba yangu…”

“Ipi…”

“Ya siku zote, ina maana umesahau kabisa…?”

“Hebu acha maneno yako wewe…,” alijibu Dokta Kisarawe huku akimalizia kufunga kufuli la mlango.

“Kuhusu wewe nini tena…”

“Si tiba yangu…”

“Ipi…?”

“Ya siku zote, ina maana umesahau kabisa…?”

“Hebu acha maneno yako wewe…,”

“Kha, dokta mbona sikuelewi…?”

“Hunielewi kivipi wewe….?”

“Si hivyo, ina maana kweli juhui kilichonileta…?”

“Sasa kama ningekuwa sijui si ningekuuliza…?”

“Sikiliza, nina mazungumzo na wewe nje ya mazingira haya ya kazi, ndiyo maaana sikutaka kukuita toka mwanzo.

“Hapo sawa, kwa hiyo tunaelekea wapi…?”

“Wewe tulia, si uko na mimi sasa wasiwasi wako nini…?

Ikabidi atulie.

“ngoja nione mwisho wa safari hii…,” akawaza moyoni huku akiegemea kwa nyuma.

Safari ikaendelea, mbele kidogo dereva alianza kupunguza mwendo, Sulee alipochungulia kupitia kioo, akasoma bango lililoandikwa Utulivu Gest House.

Moyo ukamlipuka, akajua nikilichokuwa kinaendelea.

Baada ya kuteremka, dokta alimlipa dereva pesa yake na kumruhusu aondoke zake lakini akamwambia angempigia simu baaadaye kwa ajili ya kwenda kuwapokea. Alionekana kuwa ni mtu wake wa karibu sana, ndiyo maana Dokta Kisarawe alikuwa anamuamini kwa kiasi kikubwa namna hiyo.

Wakazama hadi mapokezi ambapo baada ya kukamilisha taratibu zote, wakapewa chumba.

Walipoingia tu, Dokta akaanzisha mazungumzo.

“Umeona mwisho wa safari yetu…?”

“Nimeona, umeshinda bwana…”

“Ulikuw ana wasiwasiii….?”

“Mmh…”

Dokta Kisarawe alimwambia Sulee kuwa alikuwa mjamzito jambo lililomshangaza sana Sulee.

“Unasema kweli dokta…?”

“Wewe niamini mimi…”

“Kweli…?”

“Ili uhakikishe, naomba kesho ukapime kwa daktari mwingine halafu uje uniambie.”

Waliongea mengi lakini mwisho wa siku wakaelekea kwenye uwanja wa fundi seremala ambapo shughuli ilikuwa pevu, Sulee alijiachia na kutamka maneno yote aliyoyajua. Hatimaye walifika pamoja mwisho wa safari yao.

Baada ya shughuli hiyo, Sulee aliingia bafuni kujiweka sawa, na kisha kutoka ambapo alichukua usafiri hadi nyumbani kwake.

“Mbona leo umechelewa sana kurudi…?,” Mumewe Sulee, Masofa alimuuliza akiwa amekunja ndita.

Ilikuwa ni kama saa mbili na dakika kumi usiku kwa wakati huo.

“Watu walikuwa wengi sana, halafu nina habari njema sana mume wangu…”

“Habari gani hiyo…?”

“Nina mimba…”

“Amekupima…?”

“Sasa asingenipima ningejuaje…?”

“Ok, mimi siamini labda twende kwa daktari mwingine…”

“Sawa…”

Waliongoz

ana hadi kwenye zahanati ya jirani, na kumkuta daktari akiwa peke yake.

“Karibuni jamani”

“Ahsante…”

Walieleza shida zao, taratibu zikafanyika na baada ya dakika ishirini, waliitwa na daktari huyo.

Jamani sasa naomba muwe tayari kwa ajili ya kupata majibu yenu…,” yule daktari akafungua uwanja wa mazungumzo.

“Sawa daktari, tuko tayari…,” mumewe Sulee Mr. Masofa alijibu kwa sauti ya unyenyekevu na wasiwasi mkubwa.

“Hongereni sana…”

Aliposema maneno hayo, akatulia na kuwaangalia kwa zamu.

“Mkeo ana ujauzito wa mwezi mmoja, hongereni sana…,” yule daktari alirudia tena na kuwapa mikono ya furaha kwa pamoja.

“Jamani mke wangu, kumbe ni kweli, hongera sana…,” Masofa alisema huku akimkumbatia kwa furaha kubwa mkewe.

“Ahsante sana mume wangu, hata mimi sikuamini nilipojua…”

Waliendelea kufurahia kwa muda mrefu kabla ya kuagana na daktari.

Walipofika nyumbani, furaha iliendelea, kila mmoja wao akijitahidi kuonesha upendo wa hali ya juu kwa mwenziye.

“Mume wangu Mungu ni mkubwa sana…”

“Kweli kabisa mke wangu…”

“Kwa jinsi tulivyohangaika kutafuta mtoto, hakika Mungu yupo mume wangu…”

“Uko sahihi kabisa mke wangu, tumshukuru kwa pamoja.”

Furaha iliendelea kati ya Sulee na mumewe Masofa. Usiku mzima waliendelea kubadilishana mawazo ya hapa na pale ili mradi tu kukamilisha furaha hiyo.

Siku iliyofuata, mumewe Sulee alidamka mapema na kuwahi kibaruani akiwa mwenye furaha tele.

Sulee aliendelea kuchapa usingizi huku akimfikiria sana Dokta Kisarawe. Mapenzi yake juu ya dokata huyo yaliendelea kushamiri hasa kwa kitendo cha yeye kunasa ujauzito.

“Ina maana hapa mwenye matatizo ya uzazi ni huyu mume wangu Masofa…,” Sulee alianza kujisemea muda mfupi baada ya kuamka na kuketi kitandani.

“Kweli kabisa, ni lazima atakuwa ni huyuhuyu, kwa sababu kama ningekuwa ni mimi nisingeweza kunasa hii mimba,” mawazo hayo yakaendelea kujirudia kila mara akilini mwake.

Aliamka na kuanza kufanya usafi wa ndani baadaye akaenda kuoga. Alipomaliza akabandika chai jikoni huku akiendelea na ufuaji wa nguo chache zilizokuwa chafu.

Akamaliza kazi zote na kuanza kunywa chai huku akiwa ndani ya khanga moja iliyolichora thabiti umbo lake la namba nane.

Baada ya kunywa chai, aliingia ndani na kubadili nguo ambapo alivaa viwalo vikali vilivyomtoa sana.

Akaamua kwenda kwa rafiki yake mmoja aitwaye Monica aliyekuwa na tatizo la kutozaa kama alilokuwa nalo yeye.

“Hodi jamani hapa, hodi jamani…,” Sulee alibisha hodi kwa mbwembwe na uchangamfu wa hali ya juu.

“Mm! Karibu sana jamani…,” aliitikia Monicha huku akimshangaa Sulee kwa jinsi alivyokuwa amechangamka.

“Mzima shoga yangu…?”

“Mzima sijui wewe…?”

“Salama…”

“Karibu, naona una furaha kubwa kulikoni…?”

“Tayari shoga yangu, tayariii…”

“Tayari nini tena, mbona sikuelewi…!”

“Nimenasa…”

“Umenasa…?”

“Eee, nimenasa…”

“Umenasa nini Sulee, mbona sikuelewi?”

“Mwenzio nina mimba Monica…”

“Hamna, acha utani wako bwana…”

“Siyo utani Monica, nina mimba…”

Waliendelea kuzungumza mengi huku Monica akishangaa ni kwa namna gani ameweza kupata ujauzito wakati wote kwa pamoja walisumbuliwa na tatizo moja la kutopata ujauzito. Kwa upande wa Monica tayari alikuwa amekata tamaa.

“Umepata wapi hiyo tiba mwenzangu…?”

“Kuna daktari mmoja mtaalamu sana, yaani ameponesha wengi.”

Sulee aliendelea kummwagia sifa Dokta Kisarawe.

Kwa muonekano, Monica alikuwa mwanamke mrembo mno kupita Sulee. Alikuwa mweupe, mrefu mnene kiasi huku nyuma akiwa ‘amejazia mzigo wa maana.’

Mwili wake ulinakishiwa kwa vinyweleo nadhifu vilivyolala, pua nyembamba ndefu wastani huku maeneo ya kifuani yakiwa yamepambwa kwa ‘nido’ ndogo kiasi zilizochongoka.

Mara nyingi alipendelea sana kuvaa nguo za kubana na kusababisha mateso makubwa kwa wanaume wakware.

Miguu yake minene wastani, kila alipokuwa akikanyaga hatua moja, mzigo wa nyuma ulitingishika kiaina.

“Sasa na mimi utanipeleka lini nikamuone huyo daktari…?”

“Wewe unapenda twende lini…,” Sulee alimuuliza Monica huku akiwa amemkazia macho.

“Hata sasa hivi, au unasemaje…?”

“Kwa leo itakuwa ngumu, maana inahitaji maandalizi…”

“Maandalizi gani Sulee jamani mimi nina shida, kama ni fedha ipo bwana…,” Monica alizungumza huku akizidi kuliangalia kwa umakini sana tumbo la Sulee.

“Kesho uje unipitie nyumbani jioni ya saa moja na nusu, sawa…?”

“Saa moja na nusu…?,” Monica alihoji kwa mshangao mkubwa.

Ee, saa moja jioni ndiyo, mbona unashituka Monica…?,” Sulee alihoji kwa sauti ya kishari f’lani hivi.

“Mmh!, nimeshangaa muda huo ni daktari gani anatoa huduma ya tiba kwa uzazi…!”

“Kha! Monica vipi kwani wanaojifungua huwa hawaendi kuzaa usiku…?”

“Umeshasema kujifungua, sasa mimi naenda kujifungua…?” alisema Monica huku akitingisha mguu mmoja na kulifanya wowowo lake litikisike kwa kitetemeshi cha kuvutia…

“Kama unataka tiba, utakuja nikupeleke na kama hutaki basi bwana nimeshaona una wasiwasi,” alisema Sulee akijiandaa kuondoka.

“Hapana shoga yangu, nitakuja bwana…”

“Oke, utanikuta ila usichelewe…”

“Sawa shoga yangu…”

Waliagana lakini moyoni Monica akabaki na maswali yasiyokuwa na majibu.

“Saa moja na nusu jioni tiba gani ya uzazi hiyo…?”

“Lakini kwani tiba huwa ina muda maalum, na mimi bwana…!”

“Lakini ngoja, sasa hiyo saa moja na nusu kuna kuwa na wagonjwa wengine…?”

“Ee, sasa si pale ni hospitalini…?”

“Mmh! Itajulikana hukohuko kesho…,” Monica alizidi kuwaza na kuwazua moyoni mwake.

Kesho yake Monica aliamka mapema asubuhi na kuanza kufanya kazi ndogondogo za pale nyumbani. Hamu kubwa ni kufika muda alioambiwa na Sulee wa kwenda kumuona Dokta Kisarawe.

Ilikuwa mara aingie jikoni, mara sebuleni wakati mwingine mara aguse hiki na kuacha kile. Lengo likiwa ni kusukuma muda.

Saa kumi na mbili kamili jioni, Monica alijiandaa vizuri. Akaingia bafuni na kujisafisha kwa umakini mno. Hata maeneo ambayo hakuwa ameyasugua kwa muda mrefu, siku hiyo aliyaosha kwa ustadi.

Kuanzia ndani ya kucha za miguuni, katikati ya vidole na kwingineko, ilimradi tu aonekane bomba zaidi.

“Hapa sasa ngoja nikajipigilie pamba za maana…,” Monica aliwaza wakati akimalizia kujifunga taulo kabla ya kutoka bafuni…

Aliingia chumbani kwake na kuanza kuchambua nguo zote alizozipenda. Kila aliyoijaribisha aliona kama haikumfaa kwa siku hiyo…

“Eehee, hii ndiyo nilikuwa naitaka sasa ngoja niitupie…,” alisema Monica na kuiweka pembeni nguo hiyo.

Lilikuwa gauni jekundu , lakini lilibana sana maeneo ya nyuma na kuufanya mzigo wa Monica ujitenge vizuri kila alipolivaa. Kwenda chini lilikomea chini kidogo ya magoti…

Alipojiridhisha, alifungua droo ya upande wa kitanda na kutoa pafyumu kali aina ya Red door, ambayo hutumiwa na wanawake wengi wa mjini ambao mambo yao yako bomba.

Akachukua sendozi za rangi nyeusi na kumechishia na mkoba wake, hakika alitokelezea kama wasemavyo vijana wa siku hizi.

Saa moja na nusu jioni, tayari Monica alikuwa sebuleni kwa Sulee akimsubiri waende kwa Dokta Kisarawe.

“Nimekuweka sana shoga yangu…?”

“Wala usijali, tayari…?”

“Eee, twende sasa…”

Waliongozana hadi kwa Dokta Kisarawe. Walipofika walikuta dokta huyo akimalizia kutoa maagizo fulani kwa mgonjwa mmoja.

Baada ya muda mfupi, Sulee alimpeleka Monica kwenye chumba cha daktari.

Dokta Kisarawe baada ya kumuona tu Monica, alishituka kwa uwazi na kuwafanya wote wauone mshituko huo.

“Ooh, karibuni sana…,” alisema Dokta Kisarawe huku akijiweka sawa kwenye kiti chake kirefu cha kuzunguka.

“Ahsante,” aliitikia Sulee kwa sauti ya uchangamfu.

Baada ya utambulisho, Dokta Kisarawe alimuomba Sulee awaache na Monica ili aweze kumsikiliza kwa umakini mkubwa.

Sulee alitoka nje na kukaa kwenye benchi, lakini moyo na akili yote vikabakia chumbani kwa Dokta Kisarawe na Monica.

Kilipita kimya kidogo bila kusikia sauti yoyote achilia mbali minong’ono…

Akaendelea kukaa huku akijiuliza maswali.

“Sasa mbona sisikii wakiongea…?”

“Au…mh!…,” Sulee hakumalizi sentensi yake na kuishia kuguna.

Kimya kikazidi kupita. Giza nalo likazidi kutanda, lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kumsubiri Monica aliyekuwa akipata tiba maalum.

Kuna wakati alitamani avamie ndani ili kuona kilichokuwa kinaendelea kati ya Dokta Kisarawe na rafiki yake Monica, maana tayari alishaanza kuhisi wivu f’lani hivi hasa akikumbuka jinsi yeye alivyoanzisha uhusiano na Dokta Kisarawe.

Wakati akiwaza hili na lile, ghafla alishituka baada ya kusikia kitu kama meza au kitanda kikilia kuashiria kama kuna mtu anakisogeza.

Akanyanyuka alipokuwa amekaa na kwenda hadi mlangoni.

Kwa kutumia tundu la komeo la mlangoni, Sulee alichungulia ndani.

“Duh! Yaani kweli…?” Sulee alitamka maneno hayo baada ya kuona kwa ndani.

Akarudi na kukaa tena kwenye benchi kama zamani, lakini akawa hatulii sehemu moja…

Kila mara alikuwa akiinuka kukaa, mara asogee mbele na nyuma, hakika wivu ulikuwa ukimpeleka vibaya…

“Haiwezekani, huyu Dokta Kisarawe anaweza kutuchanganya na rafiki yangu kweli? Hapana haiwezekani…,” Sulee akawa anawaza moyoni.

Baada ya muda mfupi, kilisikika kimya kutoka chumbani kwa Dokta Kisarawe. Baadaye akatoka Monica lakini uso wake ulikuwa haueleweki.

Kwa mbali alionekana mchovu kwa shughuli fulani lakini pia wakati mwingine alionesha uso wa uchangamfu na kuzidi kumchanganya zaidi Sulee.

“Vipi…,” Sulee alimuuliza Monica wakati wakiongoza njia ya kurudi nyumbani.

“Safi tu…”

“Umeonana na dokta…?”

“Sijaonana naye…,” Monica alimjibu Sulee huku akimkazia macho.

“Hujamuona…!?,” Sulee akauliza kwa sauti ya mshangao mkubwa.

“Sulee bwana, sasa wewe unajua kabisa niliingia ndani kwa dokta tena wewe ndiye uliyenipeleka, sasa unaponiuliza kama nimemuona dokta ulitaka nikujibuje? Basi sijamuona…,” Monica alijibu huku akimtazama Sulee kwa jicho la ‘Uwe unafikiri kabla ya kuuliza swali’.

Sulee akakaa kimya na kumuangalia Monica kama anayesema ‘Leo umeniweza’.

Wakaendelea na safari yao, lakini Sulee hakuwa amejiridhisha na majibu ya Monica hivyo akaendelea kumdadisi zaidi kujua kilichoendelea kati yake na Dokta Kisarawe.

“Oke, kasemaje…?”

“Amenipima na kunipa dawa hizi, lakini ameniambia nirudi baada ya siku mbili…,” Monica alimjibu Sulee na kumuonesha dawa ambazo alikuwa amepewa na Dokta Kisarawe.

Moyoni Sulee alijisikia wivu zaidi kwani hata yeye mara ya kwanza kuonana na Dokta Kisarawe alipimwa na kisha kupewa dawa na kuambiwa arudi baada ya siku mbili.

Hisia za Dokta Kisarawe kufanya kama alivyomfanyia yeye zikazidi kumgubika moyoni.

“Siku ya kurudi utaniambia ili twende wote, sawa…?”

“Sawa…,” Monica alijibu kwa mkato na sauti ya chini mno.

“Mbona kama umeishiwa na raha Monica…?”

“Hamna, mbona niko kawaida tu Sulee…”

“Au umeambiwa nini na Dokta Kisarawe…?”

“Hakuna kitu Sulee, niko sawa…”

Waliendelea na mazungumzo ya hapa na pale, lakini Monica alionesha wazi kuwa hakuwa sawa kabisa, jambo ambalo lilizidi kumuweka njia panda Sulee.

Baadaye waliagana na kila mmoja kwenda nyumbani kwake kwani tayari ilishakuwa usiku wa saa tatu kama na robo hivi…

Monica akiwa njiani, alianza kuwaza mambo mengi sana, lakini kubwa ni kwa nini Sulee aendelee kung’ang’ania kwenda naye mara ya pili wakati alishamuelekeza.

“Aah wapi, naenda peke yangu, si ameshanionesha…?” Monica akaendelea kuwaza na kufikia uamuzi wa kutokwenda na Sulee mara ya pili.


Baada ya siku mbili, Monica aliamua kwenda kwa Dokta Sulee peke yake bila kumtaarifu Sulee…

Baada ya kutimu saa moja na nusu karibia saa mbili, Sulee akazidi kushangaa kwa nini Monica hakumpitia kama walivyokubaliana.

“Huyu mbona hajafika hadi sasa hivi, au kaghairi…?” Sulee alizidi kuwaza baada ya kuona muda unazidi kusonga mbele bila kumuona rafiki yake Monica.

Akachukua simu na kujaribu kumpigia ili amuulize kama alikuwa ameghairi kwenda kwa dokta.

Simu ya Monica iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa licha ya Sulee kurudia tena zaidi ya mara tano. Akazidi kuchanganyikiwa.

Akampigia Dokta Kisarawe, naye akawa hapokei. Akaamua kumpigia mume wake na Monica ili kujiridhisha. Mume wake Monica alimwambia Sulee kuwa rafiki yake huyo alikuwa ameenda kwa dokta.

Sulee akatulia. Baada ya kupita saa nzima, simu ya Sulee iliita na alipoitazama, alikuwa ni mumewe Monica akimtaarifu kuwa Monica amepokea na kumueleza kuwa anajiandaa kurudi. Sulee hakujibu kitu zaidi ya kulala.

Kesho yake, aliamua kwenda kimyakimya nyumbani kwa Monica. Baada ya kuzungumza, walikubaliana kwenda pamoja siku hiyo huku Sulee akimlaumu kwa kumuacha jana yake.

“Nilichelewa nikaona nitakusumbua shoga yangu,” alijibu Monica lakini akikimbiza macho yake chini kwa aibu f’lani hivi.

Ilipotimu jioni, waliongozana pamoja hadi kwa Dokta Kisarawe, walikuta wagonjwa wengine wamepanga foleni.

Mlango ukafunguliwa na Dokta Kisarawe akatoka, alipowaona haraka akamuita Monica na kuwaacha wagonjwa wengine, akafunga mlango. Sulee kuona vile, akasogea hadi mlangoni na kuanza kuchungulia tena.

Kwa mbali akaanza kusikia tena vitu vikisogezwa. Mara kikatokea kimya cha ajabu.

Baadaye kidogo, Sulee alisikia sauti ya kulalamika ya Monica akisema

Dokta mimi siumwi huko jamaniiii, mmh!.

Moyo ukazidi kumwenda kasi Sulee, alijua kilichokuwa kikiendelea kati ya Monica na Dokta Kisarawe.

“Yaani kweli Kisarawe anaweza kunifanyia hivi…?.,” Sulee alijikuta akisema kwa sauti na kuwafanya baadhi ya wagonjwa waliokuwa wamekaa kwenye benchi wamwangalie kwa jicho la kumshangaa kutokana na sauti yake.

“Haiwezekani, nasema haiwezekani hapa ni lazima nifanye kitu…,” akazidi kuwaza huku akiwafikiria njia ya kuzuia kilichokuwa kikiendelea kati ya Monica na Dokta Kisarawe.

Kitendo cha Dokta Kisarawe kumuita Monica aliyefika mwishoni na kuwatangulia baadhi ya wagonjwa kilileta kero kwa baadhi ya wagonjwa na kuanza kumjadili kwa tabia yake hiyo.

“Mh, ina maana huyu dokta hajaona kama kuna wagonjwa wengine hapa tuliowahi…?” alihoji kwa sauti ya juu mama mmoja aliyekuwa amekaa kwenye benchi la wagonjwa.

“Shangaa, halafu kila akiingia na mwanamke ni lazima afunge mlango,” alishadadia mwanamke aliyekuwa ameketi jirani kabisa na Sulee.

Mjadala juu ya tabia ya Dokta Kisarawe ulizidi kupamba moto baina ya wale wanawake waliochukizwa hasa kwa kitendo chake cha kumuita Monica licha ya kuwakuta baadhi yao wakiendelea kusubiri zamu yao ifike.

“Hapo kutakuwa na kitu, siyo bure nyie niaminini mimi,” alisema mwanamke mwingine aliyeonekana kuwa na umri mkubwa kuliko wote.

“Mama yangu vile, haiwezekani watu tumewahi kufika halafu mwingine anafika na kuitwa, hapo kuna jambo, nyie fuatilieni sana,” alisema dada mmoja aliyeonekana kuwa na haraka kutokana na kukosa pozi maalum, ilikuwa mara asimame, mara akae, kifupi alikosa utulivu.

Sulee alizidi kuwaza mambo mengi sana, kwanza moyoni alianza kujilaumu ni kwa nini alimuonesha Monica kwa Dokta Kisarawe. Alijua kamwe hawezi kuukwepa mtego wa dokta huyo kwani licha ya yeye mwenyewe kuwa mgumu hadi wanaume wengi mtaani kwao kushindwa kumpata, lakini kwa Dokta Kisarawe alishindwa kupindua, hivyo aliamini hata Monica hawezi kukwepa.

Fujo za Dokta Kisarawe zilizidi kumchanganya Monica kule chumbani, kwani alipokuwa akimpima mikono yake ilikosa staha hivyo akawa anayagusa maeneo hatarishi ya mwanamke huyo mrembo.

Mwanzoni alionekana kuwa mtulivu huku akimuuliza Monica maswali ya kutaka kujua kama tatizo liko kwake au kwa mumewe.

“Kweli kabisa na urembo wote huu, bado hujapata mtoto Monica…?” Dokta Kisarawe alianza kuuliza maswali yake ya mtego.

“Nimeshapata…,” Monica alijibu kwa sauti kavu tena isiyokuwa na masihara hata kidogo.

“Umeshapata…?” Dokta Kisarawe aliuliza kwa mshangao aliposikia kuwa Monica alikuwa ameshapata mtoto.

“Ee, unajua dokta nakushangaa sana, sasa kama ningekuwa nimeshapata muda ningekuwa niko hapa…?”

“Mh, hapa nimepatikana, lakini atalainika tu, mimi ndiye Dokta Kisarawe bwana…,” Dokta Kisarawe aliwaza moyoni baada ya kugundua kuwa Monica alikuwa mwanamke mtata kuliko alivyokuwa akifikiria.

Oke, sasa hebu kaa hapo…,” Dokta Kisarawe alisema na kumuonesha Monica kiti kilichokuwa karibu yake.

Monica alikaa kwa utulivu na kumwangalia dokta kwa macho ya ‘nakusikiliza’.

“Ni wanawake wengi sana walikuja na tatizo kama la kwako, lakini kupitia mikoni hii waliondoka hapa wakiwa na furaha…,” alisema Dokta Kisarawe na kumfanya Monica atabasamu japo kwa mbali.

“Kweli kabisa dokta…?” aliuliza Monica.

“Mama yangu vile…”

“Unafanyaje…?”

“Mimi siyo daktari kwa matokeo ya mtihani, bali ni mtaalam wa taaluma…,” Dk. Kisarawe alijibu.

Dokta alisogeza kiti karibu kabisa na alipokuwa amekaa Monica, alianza kumshika tumboni na maeneo mengine.

Mwanzoni Monica alionekana kutulia lakini kadiri mikono ya Dokta Kisarawe ilivyokuwa ikikosa staha, ndivyo alizidi kuhisi kitu cha ajabu kikimtokea.

Dokta alimsimamisha Monica, akawa anamshika kifuani na kumwambia kuwa alikuwa anaangalia kama mishipa ilikuwa ikipeleka vyema damu.

Kwa kuwa Monica hakujua chochote kutokana na taaluma ya kidaktari kumpita kushoto, ilibidi atulie na kumuacha Dokta Kisarawe aendelee na utaratibu wake.

“Aaah, sasa Dokta mbona unanishika huko tena…,” Monica aliuliza baada ya mikono ya dokta kushika yale matunda mawili yaliyokuwa yamesimama wima kifuani kwa Monica, wakati akisema hayo alikuwa akijigeuza na kusababisha kiti alichokalia kizidi kutoa mlio wa kuashiria kitu kisicho cha kawaida.

Licha ya kulalamika kwa kitendo cha Dokta Kisarawe kumgusa maeneo hatari, Monica hakuwa na upinzani mkubwa kwa mashambulizi ya daktari huyo mzoefu kwa kuwakwangua wanawake wasiokuwa na msimamo na ndoa zao, hakika Monica alikuwa amepatikana.

“Oooh, ophhhhuuu…,” Monica alianza kulalamika kwa sauti ya kubana tofauti na alivyokuwa akilalama kwa sauti ya juu, sasa alianza kuhema kwa nguvu huku akigeuza macho yake makubwa na meupe.

Dokta Kisarawe akazidisha mashambulizi kwa kushika na kupapsa kila eneo alilohisi ni hatari kwa mwanamke huyo mrembo kuliko wote ambao dokta huyo aliwahi kuvunja nao amri ya sita.

“Kwa nini jamani dokta…?,” Monica aliuliza huku akimtazama Dokta Kisarawe kwa macho ya ‘sasa umenibakiza nini? Si umalizie tu…’

“Aah, kwani nini tena jamani Monica…?”

“Sasa mbona unanishika huko bila lidhaa ya….nguuu….,” Monica alihoji lakini hakuimalizia sentensi yake kwani tayari Dokta Kisarawe alikuwa amelishika tunda lake la upande wa kushoto na kulibinya huku akilinyonya mithili ya maembe nyonyo yale ya Tanga…

“Sasa si usubiriiiiii….,” Monica akazidi kulalamika na kuongeza manjonjo ya kujikunja hali iliyomfanya Dokta Kisarawe alizidisha utundu mwilini kwa mwanamke huyo ambaye hakuwahi kuchubuliwa kwa mkwaruzo wa aina yoyote.

“Ok, sasa kama unataka mchezo si useme jamani dokta kuliko kuendelea kupeana mateso makali namna hii…,” alilalamika Monica huku akizidi kuhisi hali ambayo hata kama ungekuwa wewe ni lazima uhitaji huduma tena ile ya haja.

“Kwani wewe hujui hadi niseme jamani…,” alihoji dokta, lakini safari hii Monica hakujibu chochote zaidi ya kuanza kutoa sauti ya kugugumia kutokana na utamu wa sukari guru aliyokua akionjeshwa na Dokta Kisarawe.

“Aaah, hapo sasa jamani dokta, umejuaje jamaniiiii…, Monica alilalama baada ya Dokta Kisarawe kushika maeneo ya nyonga na kufanya kama anayekamua jipu kwa staili ya kubinya kwa mapozi yasiyosimulika.

Baada ya mashambulizi ya dokta kumzidishia raha ya ajabu, Monica akaona isiwe taabu kwani tayari akilini mwake alikuwa ameshahisi kuwa hakukuwa na jambo jingine ambalo Dokta Kisarawe alihitaji zaidi ya mchezo wa baba na mama.

Akaanza kujibu mashambulizi kwa kujibu mapigo ya utundu wa ajabu. Kwanza alimuangalia Dokta Kisarawe kwa macho ya karibu tena bila kupapasa, akamkazia na kusogeza kabisa kinywa chake karibu na cha Dokta Kisarawe, hapo akatoa ulimi wake mpana uliojaa mate ya uchu.

Hakuishia hapo, akausogeza kabisa karibu na midomo ya Dokta Kisarawe na bila kujali harufu ya sigara iliyokuwa ikitoka kinywani kwa mwake, Monica alitumbukiza ulimi wake mdomoni na kuanza kuuviringisha kila kona.

Utalaamu alioutumia kuchezesha ulimi wake kwa mbwembwe zaidi mdomoni, hali hiyo ilimtia wazimu Dokta Kisarawe na kuanza kugugumia kama dume la njiwa lililotoka malishoni.

Dokta Kisarawe akazidi kutoa sauti ambayo haikueleweka.

Monica naye akiwa na hali mbaya ya mhemko kutokana na kuchezewa kwa muda mrefu na mikono ya Dokta Kisarawe ambayo alikuwa akiipitisha maungoni kwake kwa ufundi na umaridadi wa kiwango cha juu.

Bila kutarajia, wailjikuta wakiwa wameegemea kitanda cha kulaza wagonjwa huku kila mmoja akiwa anahema kama aliyetoka kukimbia mbio ndefu za marathoni.

“Baby…,” Monica aliita huku akiushika mkono wa kushoto wa Dokta Kisarawe na kuupitisha katika tunda lake la kulia na kuanza kumwelekeza jinsi ya kulipikicha kwa ustadi mzuri, kitendo cha dokta huyo kuanza kupita juu ya eneo jeusi lililokuwa likizunguka kikonyo cha tunda hilo.

“Basi, basiiiii, basiiiiii jamaniiii…,” Monica uzalendo ulimshinda na kuanza kujinyonyoa manyoa bila ya kutakiwa kufanya hivyo, alipomaliza kujipembua, huku akilalamika kwa sauti ya kudai huduma, haraka alimvuta Dokta Kisarawe na kumlalalia kifuani mwake, akajiweka sawa tayari kwa mechi kali ya watani wa jadi.

Kila mmoja wao alikuwa na hali ya uhitaji wa huduma.

Refaa na wasaidizi wake wakaingia uwanjani na kuruhusu mechi kuanza…

Kila upande ulianza kwa kasi kubwa na mashambulizi ya kushitukiza kwenye lango la upinzani, hali iliyowafanya washangiliaji wa pande zote kulipuka kwa mayowe kila mara.

Si Dokta Kisarawe aliyekuwa akifungua kinywa kusema chochote zaidi ya miguno na mihemko ya raha kusikika.

“Mmh! Jamani doktaaa…” Monica akajikuta akichombeza baada ya kuzidiwa na manjonjo ya Dokta Kisarawe…

“Nini tena jamani Monica, aaah, basi bwana mama…” Dokta Kisarawe naye akawa anagugumia kwa raha baada ya mikono laini ya Monica kupapasa maeneo hatari ya mwanaume huyo.

Monica alikuwa akitembeza vidole vyake kwenye bustani ya kifuani ya Dokta Kisarawe, akawa anavitanua vidole na kuvikutanisha kama mkasi ukatavyo nguo, wakati mwingine vidole hivyo vikawa vinagusa hadi vinundu viwili vya kifuani hapo hali iliyomfanya daktari huyo wa tiba za akina mama aanze kuangua kilio cha raha ya ajabu.

Monica hakuishia hapo, sasa mikono ikawa inatambaa kwa kasi katika sehemu mbalimbali za mwili wa Dokta Kisarawe.

“Jamani mama, si tumesema tuanze…”

“Nakusubiri baba…”

“Oooh, nasikia hali ya tofauti sana mama…,” Dokta Kisarawe aliendelea kulalama huku mechi ikiendelea kuchezwa.

Kuna wakati Monica alimzuia Dokta Kisarawe kuendesha gari lake, na kumtaka atulie ili yeye kunyonga la kwake bila bughudha.

“Tuliaaa, tuliaaa jamaniii…,” Monica alisema huku akimshikilia kwa nguvu Dokta Kisarawe.

Monica akawa anajizungusha peke yake huku macho yakiwa yamefumbwa, muda mfupi baadaye akaanza kutoa miguno mfululizo huku ulimi akiutoa nje.

Akawa anakunja mapaja na kunyoosha miguu kama kuku aliyekuwa akijinasua kutoka kwa mchinjaji.

“Aaa, aaaah, aaaahaaa…,” Monica alitoa kelele hiyo na kutulia baada ya kufika mwisho wa safari yake.

Kuona hivyo, Dokta Kisarawe naye akakazana na muda si mrefu naye akatangaza kufika mwisho wa safari yake ndefu na ya kuchosha.

“Ooooh, oooffffuuu…” alihitimisha huku akijinasua maungoni mwa Monica.

Baada ya mechi hiyo, haraka sana Monica alinyanyuka na kukaa juu ya kitanda hicho cha kulaza wagonjwa na kujiinamia huku akitoa kwikwi za kilio hali iliyomshitua sana Dokta Kisarawe.

“Haa, mbona unalia tena jamani?” Dokta Kisarawe alihoji huku akimalizia kuvaa suruali.

“Kwa nini mimi jamaniiii?” Monica akazidi kutoa kilio cha malalamiko na kujifuta machozi mengi yaliyokuwa yakitiririka kwa kasi ya ajabu mashavuni mwake.

“Kha, sasa mbona unalia na kuhoji kwa nini wewe, maana yake nini sasa…,” Dokta Kisarawe akawa anauliza na kumsogelea mahali pale, akamgusa begani.

Monica akauondoa mkono wa Dokta Kisarawe kwa kasi hali iliyomjulisha daktari huyo kuwa hali si shwari kwa mrembo huyo.

“Kwa nini nimemsaliti mume wangu mimi?” Monica akawa anasema kwa sauti ya juu na kumshitua Dokta Kisarawe aliyekuwa akihofia watu waliokuwa nje kusikia.

“Sasa Monica, unaposema hivyo kwa sauti ya juu kiasi hicho maana yake nini jamani, au unataka watu wafanye mambo humu ndani?”

“Kwa nini umenishawishi na kumsaliti mume wangu jamani dokta?” Monica akazidi kuhoji huku akitafuta nguo zake na kuanza kuvaa huku akijisonya.

“Sikiliza Monica, wote tumejikuta katika hali hiyo, hakuna wa kumlaumu hapa, sasa nakushangaa sana kama utaanza kunilaumu mimi wakati kama ni raha tumezipata wote…”

“Raha gani, raha gani dokta nakuuliza, au unataka nikujazie watu chumbani kwako?” alilalama Monica.

“Sasa kwa nini ufikie huko kote, halafu unaposema nilikushawishi nashindwa kuelewa, hadi naanza kukushawishi ulikuwa wapi?”

“Wewe ndiyo chanzo cha usaliti, kwani mimi nilikuambia naumwa huko, ulipoanza kushika sehemu ambazo hazihusiani na ugonjwa wangu nilikuambia kabisa kuwa dokta mi’ siumwi huko, lakini hukusikia, lengo lako lilikuwa nini…?”

“Unajua Monica hatupaswi kulaumiana sana kwa hili?” alisema Dokta Kisarawe huku akionesha uso wa huzuni japo moyoni alikuwa akifurahia na kujipongeza kwa kitendo cha kufanikisha kula tunda la mtoto mzuri kama Monica.

“Unasemaje wewe, hivi una akili kweli?” Monica aliendelea kung’aka chumbani humo.

Kutokana na maneno matamu na kuonesha heshima aliyokuwa akiyatoa Dokta Kisarawe, kwa kiasi fulani yalichangia kumlainisha Monica na kuanza kushuka taratibu.

“Sawa lakini siyo vizuri bwana”

“Sawa jamani, naomba tuchukulie kama bahati mbaya mama,” alisema Dokta Kisarawe.

Kitendo cha daktari huyo kutumia jina la mama wakati wa kumuita Monica, kilimfurahisha sana mrembo huyo kwani tangu aolewe hakuwahi kuitwa kwa jina hilo na mumewe.

“Poa, nimekuelewa, nimekuelewa baba;” Monica naye alijibu kwa sauti ya chini lakini alijikuta akimalizia kwa neno la baba hali iliyomshangaza na kumchanganya sana Dokta Kisarawe.

Kwa pamoja walivaa nguo zao huku kila mmoja akikumbuka utundu na utaalamu wa mwenzake.

“Ila twende mbele turudi nyuma, huyu dokta ni kiboko kwa mambo ya chumbani, sasa kama amenifanyia utundu wote huu kwenye eneo lisilokuwa na uhuru kama hili, vipi kama tukikutana ndani ya chumba tukiwa na muda wa kutosha, itakuwaje?” Monica aliwaza huku akimalizia kuvaa nguo yake ya ndani kabla ya kumalizia kwa zingine.

“Dah! Hata Mungu aliposema nitakufanyia msaidizi, aisee alikuwa akimaanisha huyu, mama yangu vile nakuambia…,” Dokta Kisarawe alijisemea kimoyomoyo huku akifunga mkanda wa suruali yake pana kiunoni.

“Sasa kwa hiyo kuhusu tiba dokta;?” Monica alimuuliza Dokta Kisarawe huku akimuangalia kwa macho ya; Ila unayaweza sana.’

“Aaah, kuhusu tiba inabidi uje baada ya siku mbili lakini kwa sasa nitakupa vidonge f’lani, sawa?” alijibu dokta huku akimuangalia Monica kwa jicho la hata hii si ni sehemu ya tiba?’

Baada ya muda waliagana na Dokta Kisarawe akampa Monica vidonge f’lani vya rangi nyekundu na kumpa maelekezo ya namna ya kuvitumia.

“Basi sawa, lakini dokta nitakushukuru mno kama nitapona na hatimaye kupata mtoto, ujue nina hamu sana ya kuitwa mama jamani;,” Monica alisema huku akimtolea macho Dokta Kisarawe hali iliyobadili kabisa hali ya mzunguko wa damu wa daktari huyo mwenye uchu wa warembo wazuri kama alivyokuwa Monica.

“Usijali Mamie, mimi ndiyo Dokta Kisarawe bwana, si umeona mfano kwa rafiki yako Sulee, naye alikuja hapa akiwa haamini kama wewe lakini kwa sasa ni mama kijacho…”

“Mmh! Sawa kama kweli basi mimi naenda bwana”

“Sawa, tutaonana”

Monica alifungua mlango na kuwakuta wateja wengine wakingojea huduma ya Dokta Kisarawe.

Walimtupia Monica macho ya chuki kwani kitendo cha kuitwa yeye kwanza na kuwaacha waliokuwa wametangulia kiliwakera na kuwaudhi vibaya mno.

“Muone kwanza, watu wengine wanajirahisi kwa madaktari wakidhani ndiyo njia pekee ya kutibu magonjwa yao sugu;,” yalikuwa mazungumzo ya akina mama wawili waliokuwa wamekaa kwenye benchi la kusubiri zamu huku wakimuangalia Monica kwa jicho baya.

Monica alimkuta rafiki yake Sulee amenuna bila kujua chanzo na sababu ya yeye kufanya hivyo. Moyoni akawaza huenda kilichomuudhi Sulee ni kitendo cha yeye kuchelewa chumbani kwa dokta.

Hali ilikuwa tofauti kabisa kwa upande wa Sulee, wivu wa mapenzi ya Dokta Kisarawe ulikuwa umemkaba hadi shingoni na sasa alikaribia kuzimia kwa hasira.

Kitendo cha kusikia meza na viti vikitoa sauti ya kusukumwa kila mara kilichangia kwa asilimia nyingi sana kwa Sulee kuamini kuwa ni lazima kwa vyovyote vile Monica atakuwa ametembea na Dokta Kisarawe jambo ambalo lilimuumiza kuliko ncha ya wembe kupita kwenye kidonda kibichi.

“Vipi rafiki yangu mbona unaonekana umenuna sana, pole kwa kuchelewa mwaya, “Monica alijibalaguza huku akimshika begani Sulee bila kujua hali mbaya ya wivu iliyokuwa ikimtesa mke huyo wa mtu.

“Ina maana kweli Monica unaweza kunifanyia hivyo;?” aliuliza Sulee kwa sauti ya kukwaruza.

“Nimefanya nini tena Sulee, si nimekuomba msamaha kwa kuchelewa jamani?”

“Si umetembea na Dokta Kisarawe wewe;,” alijibu Sulee kwa sauti ya juu na yenye hasira.

Je, nini kitatokea kuhusu penzi la Dokta Kisarawe na wawili hao?⁠⁠⁠⁠

ITAENDELEA

Dokta Mimi Siumwi Huko Sehemu ya Pili

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment