Hujuma Sehemu ya Kwanza
NEW AUDIO

Ep 01: Hujuma

Hujuma Sehemu ya Kwanza

IMEANDIKWA NA: RICHARD MWAMBE

*********************************************************************************

Simulizi: Hujuma

Sehemu ya Kwanza (1)

Bahari ya hindi

MANOWARI ya kijeshi kubwa kabisa ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kikosi cha wanamaji cha Kigamboni ilikuwa ikikata maji kwa kasi, ikitokea Tanzania kuelekea Urusi. Ilikuwa ni safari ya kusafirisha makombora kumi na mbili ya kisasa, makubwa yenye nguvu, makombora ya kisasa ambayo Urusi na Tanzania zilishirikiana kuyaunda ndani ya ardhi ya Tanzania. Kiwanda kikubwa kilikuwa kimejengwa maeneo ya pwani ya Mtwara eneo la Msanga mkuu, maalum kwa kazi hiyo.

Baada ya uchunguzi wa muda mrefu uliochukua takribani miaka kumi na tano hatimaye wataalamu wa milipuko wa jeshi la Urusi na wale wa Tanzania walikuwa wamekamilisha kuunda makombora hayo yenye nguvu aina ya R-36 ambayo teknolojia yake ni ya kule Urusi tangu miaka mingi ‘Intercontinental ballistic missile’, yenye urefu wa mita 32.2 (futi 106) na kipenyo cha mita 3.05 (futi 10), linaloweza kusafiri kwa kasi ya kilomita isiyopungua 7.9 kwa sekunde. Ni makombora yanayokwenda kasi ya ajabu na yenye mlipuko usio wa kawaida. Baada ya kuundwa katika kituo hicho maalum huko Msanga mkuu, Mtwara, sasa yalikuwa yakipelekwa kwa majaribio katika jangwa kubwa la Ryn lililoko Kusini Mashariki mwa Urusi, Maghalibi mwa Khazakistan, Kaskazini mwa bahari ya Caspian. Manowari kubwa ya Tanzania Kirov Class yanye urefu wa futi 827 iliyotengenezwa kati ya miaka ya 1970 na 1990 huko Urusi na kuiuza kwa serikali ya Tanzania ndiyo ilifanya kazi hiyo ya kubeba makombora hayo makubwa kumi na mbili kuyapeleka huko bahari ya Caspian kwa majaribio.

Wanamaji waliokuwa ndani ya meli hiyo walikuwa wakiendelea kula raha kwa kucheza michezo mbalimbali kama bao, karata, draft na mingineyo mingi huku manaodha nao wakiwa kwenye kebini yao wakabadilishana mawazo. Wengi wa wanamaji hao walikuwa kutoka Tanzania na wacahache walikuwa kutoka Urusi, jumla yao ilikuwa ni kama ishirini na tano hivi. Ilikuwa ni wakati wa pekee wa wapiganaji hawa kubadilishana uzoefu wa kazi yao, ukiachilia wanamaji hao pia kati yao kulikuwa na wataalam wa milipuko nao walikuwamo. Siku hizo kulikuwa na wimbi kubwa la utekeji meli za mizigo, mafuta na nyinginezo katika bahari ya Indi hasa eneo la Somalia.

Usiku wa manane kila mtu akiwa kasinzia katika lile saa la shetani yaani saa nane kwenda saa tisa, kila mmoja alijibwaga ndani ya kitanda chake akiwa kabebwa na usingizi wa ajabu, kwa kuwa chombo hicho kilikuwa kikijiongoza kwa mitambo maalumu ya kompyuta hakikuwapa tabu waongozaji kujipumzisha japo kwenye viti vyao.

Mara ghafla kioo kikubwa katika chumba cha nahodha kilipasuka na kumwagika sakafuni, nahodha mmoja alishtuka kwa kelele za kioo hicho na upepo mkali ulikuwa ukiingia ndani ukipeperusha karatasi huku na kule, wasaidizi wa nahodha huyo nao wakaamka lakini kabla hawajakaa sawa, mmoja alibamizwa ukutani alikuwa amerushwa kwa risasi nzito ya mdunguaji, damu ikaanza kumwagika, kabla nahodha hajaminya ile nobu ya kengele ya hatari, naye alijikuta chali kifua chote kikiwa fumu kwa risasi nyingine ya mdunguaji.

Msaidizi mmoja aliyebaki akaona isiwe tabu akaamua kutimua mbio kutoka chumba cha nahodha ili kuwahi mlango wa kuingia ndani ambako wengine walikuwa wamelala, alipotoka tu kwenye deki akajikuta akimulikwa na mwanga mkali sana uliomfanya ajizibe macho asiweze kuuona. Helkopta kubwa ya kijeshi ilikuwa angani si mbali sana na uwanja wa meli hiyo ambao uliweza kuruhusu helkopta kama hiyo kutua juu yake, alipotaka kukimbia tena la haikuwezekana, alitunguliwa risasi ya mgongo na kujibwaga chini kwa kiwewe kilichomshika akakimbia na kujitumbukiza baharini, lile helkopta likashuka taratibu na kukanyaga sehemu ya juu ya manowari hiyo.

Giza nene likaivamia meli hiyo ghafla, kila mtu akashtuka ndani ya meli hiyo na kukurupuka kujiweka sawa kujua kulikoni, wamechelewa. Kila kona kulikuwa kumetanda watu walioficha nyuso zao wakiwa na silaha nzito za kisasa za kivita, walikuwa ni wengi maana mara tu baada ya ile helkopta kutua zilifuata boti nyingi ziendazo kasi zikaizunguka manowari ile, Maharamia. Kiongozi wa wale maharamia akatoa amri ya kuikagua ile manowari, na kuhakikisha kila binadamu mwenye uhai anateremshwa.

Wale wapiganaji wote wakatolewa nje na kuwekwa mstari mmoja huku wakimulikwa na taa kubwa la ile helkopta.

“Karibuni sana Somalia, hii ndiyo Pwani ya Shetani, asikwambie mtu, hapa kila goti litapigwa,” yule Kiongozi alikuwa akiongea kwa kujigamba huku mkononi mwake amekamata bunduki kubwa yenye kilo nyingi, usoni akiwa kijifunika na soksi jeusi ili hasionekane uso wake, akatoa amri myingine na wale wafuasi wake wakawafunga kamba wale wapiganaji na kuwavisha kila mmoja soksi usoni baada ya kuwavua makombati waliovaa juu. Kishapo wakawapakia kwenye boti zao na kuondoka nao eneo lile. Maharamia wanaojua kuongoza vyombo kama hivyo waka shika usukani wa Manowari hiyo kubwa kabisa na kuigeuza kuipeleka pwani ya Somalia, Mogadishu.

MOGADISHU

Maharamia waliwafikisha mateka wao katika pwani ya Mogadishu na kuwashusha wakiwaswaga mpaka kwenye malori yaliyokwisha andaliwa kisha wakaondoka nao kuelekea kusikojulikana.

Alkadhalika, ile manowari nayo ilifikishwa Mogadishu na mara moja usiku ule ule ilianza kazi ya kupakuwa yale makombora na kuyaficha kwenye ghala kubwa lililojengwa chini ya maji karibu kabisa na bandari kuu ya Mogadishu, yalifichwa hivyo ili kama wakija kuwakomboa wenzao basi waikute meli tupu kisha wale maharamia nao wakaondoka eneo lile.

§§§§§

Jamhuuriyadda Federaalka Soomaaliya, ‘Jamhuri ya Shirikisho la Somalia’, ni nchi iliyoko katika pembe ya Afrika, sehemu kubwa upande wa Mashariki ni bahari ya Indi. Somalia ni nchi iliyokuwa katika mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi kirefu na vikundi mbalimbali vya kigaidi kama Al-Shabab walitokea ndani ya nchi hiyo kutokana na tofauti za kisiasa.

Wimbi la utekaji vyombo vya majini liliibuka katika pwani ya nchi hiyo na kulaaniwa na kila taifa, kila serikali, kila taasisi ya kibinadamu duniani zikitoa wito kwa mataifa makubwa kukomesha uharamia huo.

Ilikuwa ni vigumu sana kutimiza lengo hilo la kukomesha wimbi la utekaji vyombo vya majini, haikujulikana sababu ni nini hasa ya kushindikana kwa juhudi hizo. Ilikuwa ni kitendawili kisicho na mteguaji. Hali kwa ujumla ilikuwa ni ya kuogofya katika eneo hilo, maharamia wa Somalia walikuwa hawaogopi hata sheria za maji makubwa, wao walichojua ni kuteka meli ilimradi wapate pesa, ukiwaona maharamia hao wanavovaa utasema ni masikini wakutupwa, lakini majumba hayo wanayomiliki ndani ya mji wa Mogadishu na viunga vyake ni kufuru kwa nchi hiyo isiyo na serikali kwa kipindi kirefu, kila mtu akiwa anajiamulia madaraka yake mkononi.

§§§§§

Jazeera Palace Hotel

Saa 2:10 asubuhi

Pembezoni kabisa mwa barabara ya Uwanja wa ndege ‘Airport road’,gari aina ya Jaguar nyeusi ilikuwa ikikunja kona kuingia katika hoteli ya Jazeera Palace asubuhi hiyo, moja kwa moja ikaingia katika maegesho na kuegeshwa sawasawa kabisa. Bwana mmoja wa makamo akateremka kutoka katika katika gari hiyo ya kifahari na kuuendea mgahawa wa hotel hiyo akachagua siti moja na kuketi. Haikupita hata dakika tano akaja mtu mwingine mnene kiasi mwenye upara unaong’aa ulioonekana wazi baada ya kuvua ile balaghashia yake na kuiweka mezani.

“Nipe habari,” yule bwana mwenye upara akamwambia Yule mwingine.

“Kila kitu tayari mzigo tunao, kilichobaki ni kuhesabiana tu, sisi wenyewe tunajua jinsi ya kuifikisha mahali husika,” alijibu bwana Shalabah, kiongozi wa maharamia. Ilikuwa ni biashara kubwa ya pesa nyingi za kigeni, nah ii ndio hasa waliokuwa wakiifanya maharamia hawa, safari hii walikuwa wamefanya biashara kubwa ya makombora hayo mazito.

“Ok, hatuna muda wa kupoteza, pesa iko tayari lini?” bwana Shalabah alimuuliza Yule mwenye upara.

“Pesa, pesa kitu gani? Kama wewe tayri una mzigo basi pesa utapata,” Yule mwenye upara alijibu.

“Kuna makombora 12, yenye uzito wa hali ya juu, ukipiga New York mpaka Ontario watatetemeka kwa hofu,” bwana Shalabah alimweleza Yule mwenye upara umadhubuti wa makombora hayo.

“Umenishtua sana, usijali nitwasiliana na washika dau ili tuyachukue yote 12 tuyapeleke huko maskani, sasa yako wapi japo niyaone,” Yule mwenye upara akamwambia Shalabah.

”Huwezi kuyaona, na wala hutakiwi kujua yako wapi, unachotakiwa kufanya wewe ni kuwasiliana na watu wako ili tufanye biashara, basi, hakuna kingine,” Shalabah alimueleza. Kisha akavuta mkoba wake na kufungua, akatoka kijitabu Fulani wakaandikiana mawasiliano yao na kisha wakaagana, kila mtu akachukua hamsini zake.

Shalabah akaikunja miguu yake na kuiweka kwa mtindo wa nne na kuagiza kinywaji kikali, alipoletewa alikuwa akinywa taratibu akisubiri miadi mingine, mara hii ya watu wake. Haikupita hata saa moja vijana watatu warefu, wembamba wakaingia na land cruiser pick up, wakateremka na kuungana naye katika kinywaji hicho.

“Mmekuja?” akawauliza wakati akiwaona.

“Ndio, mkuu, tumeitika wito,” wakajibu

“Sasa, nimeona kazi mliofanya, hongereni sana, lakini kama kuna jambo nataka kuwaambia ni kuimarisha ulinzi pale gahalani, silaha za safari hii hawa jamaa hawatakubali zipotee hivihivi lazima watakuja, hivyo muweke ulinzi wa kutosha kwa maana jamaa wako tayari na wanataka kuchukua mzigo wote kwa pesa iliyotakata sana. Mimi jioni ya leo nitakwenda kuonana na Top ili tuone mgao wenu mpaka hapa mlipofanikisha unakuwaje,” Shalabah alikuwa akiwaeleza wale vijana mpango ulivyo kwa ujumla.

Maharamia hawa walikuwa tayari kufanya biashara ya makombora hayo na kikundi kimoja kinachoendesha mapigano yasiyokoma huko katika jangwa la Pakistan mpaka Afghanistan, kutokana na kuishiwa na silaha nzito waliingia mkataba na maharamia hawa ili wawatafutie silaha nzito na zenye nguvu ili kuwaadabisha mahasimu wao, safari hii wakazipata. Pesa waliokubaliana kuyanunua ilikuwa ni pesa ambayo inaweza kulisha Tanzania nzima kwa miezi kumi na moja kwa milo mitano ya mlo kamili kwa kila mwananchi bila kujali mtoto au mtu mzima. Ilikuwa ni biashara haramu kuliko haramu yenyewe.

Mr SHALABAH aliendelea kuketi pale alipoketi mara baada ya kuiachana na wale vijana wake, akiwa katika kuburudika na kinywaji chake mara akajikuta hayupo peke yake katika meza hiyo, mbele yake kulikuwa na kijana mkakamavu aliyevalia suruali ya jeans na shati jepesi, usoni akiyaficha macho yake kwa miwani nyeusi iliyomkaa sawia.

“Biashara imeenda?”Shalabah akauliza.

“Kama kawaida, hakuna kinachoharibika hapa,” Yule kijana akajibu.

“Ok, mzigo uko kamili?” Shalabah akarusha swali lingine.

“Mzigo hauna shaka, uko sawa, mmetusaidia sana na mapinduzi yanaendelea,” Yule kijana akajibu. Akaisukuma briefcase ilikuwa chini kwa mguu wake wa kushoto, ikamgusa Shalabah, Shalabah akaitazama na kuiinua akaiweka mezani, akaifungua na kuchungulia kidogo, manoti ya dola za kimarekani yalikuwa yamejipanga kwa mtindo wa kupendeza, akatabasamu na kutikisa kichwa. Akaingiza mkono katika mkoba wake mdogo na kutoa kamashine kadogo, akabofya hapa na pale akatoa kijikaratasi Fulani na kukiweka saini kisha akampa Yule kijana na kuagana naye. Alipohakikisha amepotelea nje, akanyanyuka na kuibeba ile briefcase naye akaielekea gari yake aina ya Jaguar aliyoiacha kwenye maegesho na kuondoka kwa kasi katika hoteli hiyo.

Ndani ya mji wa Mogadishu. Jumba hilo ambalo nyuma yake lilikuwa limepakana na bahari ya Indi lilikuwa limejitenga na majumba mengine, lilikuwa mbali kabisa na makazi. Shalabah alikunja kona na kulifikia geti kubwa la jumba hilo, na mara lile geti likafunguka lenyewe na kuruhusu Shalabah aingie, akakanyaga mafuta kuifuata barabara inayoelekea katika jumba hilo ambalo lilijengwa umbali wa kilomita moja kutoka getini, aliegesha gari yake katika eneo maalumu, akashuka na ile briefcase mkononi na kuelekea mlango mkubwa wa jumba hilo. Vijana wawili wenye bunduki kubwa zenye nguvu walikuwa wamesimama katika mlango huo, mmoja huku na mwingine kule, walimkagua Shalabah na kuhakikisha hana silaha yoyote mwilini mwake, wakamruhusu kuingia ndani ya jumba hilo.

Jumba lote lilikuwa kimya kabisa, ni viatu vya Shalabah tu vilivyokuwa vikisikika wakati huo, akapanda ngazi kuelekea juu mpaka ghorofa ya kwanza, akapita tena katika korido ndefu iliyopambwa kwa sakafu na kuta za mbao safi ambazo polishi iliyopakwa na kung’aa sawia ilikufanya mpitaji ujione pande zote nne. Baada ya milango kama sita hivi, Shalabah alifika katika mlango wa saba akageuka na kuutazama, kulikuwa na kidubwasha chenye tarakimu tisa, akabofya tarakimu hizo kwa mtindo anaoujua yeye na mara ule mlango ukafunguka, Shalabah akaingia ndani ya kijichumba hicho kidogo na ule mlango ukajifunga, kisha kile chumba kikaanza kuteremka chini, kikaiacha ile mandhari ya mbao na kubaki kioo tupu, Shalabah aliweza kuona samaki aina mbalimbali na mandhari nzuri ya chini ya bahari, mara kile chombo kikaingia tena katika mandhari nyingine ya mbao zenye kung’aa kama zile za mwanzo, mara ikasikika sauti Fulani ikabip, ule mlango ukafunguka na Shalabah akateremka na kuifuata njia nyingiine ndefu mbele kulikuwa na mlango mwingine, ukafunguka kabla hata ya kuugusa, akaingia na kujikuta kwenye sebule pana yenye vitu vya thamani sana.

“Karibu Mr Shalabah,” sauti ilimkaribisha. Shalabah akaketi katika moja ya viti vilivyomo katika sebule hiyo. Mbele yake katika ukuta kukajitokeza luninga kubwa ‘flat’ na hapo aliweza kumuona Yule anayeongea naye.

“Ndiyo Mr. Shalabah, nipe ripoti kwa ujumla,” Yule mtu kwenye ile screen alimwambia Shalabah.

Shalabah alitoa taarifa kamili ya mchakato mzima wa utekaji wa manowari ya kijeshi iliyotoka Tanzania, pia akamweleza kuhusu pesa aliyolipwa na Yule kijana kwa biashara nyingine waliyokuwa wameifanya siku chache za nyuma.

“Vizuri sana,” Yule bwana kwenye ile luninga akajibu, kisha akaendelea, “Sasa kuna mpango gani kuhusu hizi silaha za sasa?” akuliza.

“Kwanza wale jamaa walitaka makombora lakini hawakusema idadi, sisi tumepata makombora makubwa kumi na mbili na silaha nyingine nyingi za kufaa,” Shalabah alieleza.

“Ok, hakikisha kila kitu kinakwenda sawa, imarisha ulinzi ijapokuwa naamini hakuna wa kutuumiza kichwa kwani kwa taarifa ambazo ninazo mpelelezi mkorofi wa Tanzania hayupo kazini kwa kipindi kirefu na nafasi yake imechukuliwa na mwingine, hakikisha kila mtu anayekuja kuhusiana nah ii shughuli unamuua, hakuna kumpa mtu nafasi hata ya robo sekunde, weka watu kila mahali, kila sehemu nyeti hakikisha umeweka kinasa sauti kilicho hai na Yule mdunguaji niliyekwambia umkodi ulimpata?” Yule bwana kwenye luninga alijaribu kupanga na kuuliza.

“Bila shaka mzee, nimempata na leo jioni nitaingia naye mkataba,” Shalabah akajibu.

“Sasa umwambie mkataba wetu utakwisha pale tu jamaa hawa watakapochukua mzigo wao, na hao mateka hakikisha tunawauza kwa vikundi vya ugaidi kwani nao ni silaha nzuri sana,” yule mtu kwenye luninga alimaliza na kisha ile luninga ikadidimia chini, pale ilipokuwapo pakatoakea picha kubwa ya mwanamke aliyelala uchi. Mlio wa bip ukasikika, Shalabah akainuka na kuiacha ile briefcase palepale akatoka na kuingia katika kijichumba kile alichotokea mwanzo, kikampandisha na kumleta juu kabisa, akashuka na kuondoka zake huku akiliacha lile jumba nyuma yake likifanya mandhari safi inayolipamba jiji la Mogadishu.

Shalabah alikanyaga mafuta mpaka eneo linguine kabisa la mji, hapo palikuwa na jengo kama shule kubwa, Shalabaha akaingia na kupita moja kwa moja kwenye jengo linguine lililokuwa limejengwa ndani yake.

“Karibu sana bwana mkubwa, tukusaidie nini?” mlinzi wa eneo hilo aliuliza kwa sauti ya majigambo huku akimtunishia kifua Shalabah.

“Nahitaji kumuona bosi wako,” Shalabah akajibu.

“Unaitwa nani na umetoka wapi?” Yule mlinzi akauliza.

“Shalabah, kutoka Uranus,” akajibu. Yule mlinzi akainua simu na kupiga sehemu fulani, kisha akaongea maneno machache na alipoirudisha simu hiyo mahala pake, akamruhusu Yule bwana kuingia ndani. Shalabah alijikuta kwenye uwa mkubwa uliokuwa na watoto wengi waliokuwa katika mafunzo makali ya karate na kungfu, mkufunzi wao aliyekuwa mbele kabisa alionekana kuwa stadi sana kwa minyumbuliko aliyokuwa akifanya akiwaelekeza jinsi ya kukunja mikono na jinsi ya kusimama kimapambano. Shalabah alipitishwa kwenye ujia mrefu mpaka katika mlango mmojawapo kati ya mingi, akaingizwa ndani na kuketi katika sebule kubwa lenye nakshi za kuvutia, zuria la gharama liliificha sakafu safi ya terrazzo, Shalabah alikuwa akiitalii sebule hiyo kubwa ya kuvutia iliyokosa kitu kimoja tu, muziki, muziki mororo ambao ungemfanya aliyeketi katika moja ya matandiko hayo ama achezeshe mguu au kichwa kufuatisha midundo ya muziki huo. Shalabah akiwa katika mawazo hayo mara akasikia mlango ukifungwa nyuma yake, akageuka lakini hakumuona mtu, aliporudisha uso wake mbele alikutana na mtu aliyekwishaketi tayari katika tandiko moja wapo mbele yake. Mtu aliyevalia juba la kibuluu lililoficha mwili wote na kuaacha macho mawili tu yaliyokuwa yakionekana kwa taabu kidogo. Shalabah hakujua kama mtu huyo ni mwanamke ama mwanaume kutokana na vile alivyovaa vazi lake hilo.

“Mr Kalabah, karibu sana katika himaya yangu,” Yule mtu alimkaribisha, Kalabah alimtambua kuwa ni mwanamke kutokana na sauti yake.

“Nimekwishakaribia, shukrani,” kalabah alishukuru.

“Tusipoteze muda, niambie shida yako,” Yule mwanamke alimweleza.

“Bimekuja kutoka Uranus, nina shida ya kikazi kama ofisi ilivyonituma,” Shalabah akiwa aneleza lililomleta, akaktishwa na sauti ya nhuyo mwanamke.

“Kazi au biashara?” akauliza.

“Si biashara kwa kuwa hakuna tunachotaka kukuuzia, ila kazi kwa kuwa tunataka ututekelezee jambo Fulani,” Shalabah akaeleza.

“Ok, linahusu damu ya mwanadamu?” Yule mwanamke akauliza.

“Ndiyo, litahusisha,” Shalabah akajibu.

“Sikila Mr. Shalabah, kwa hilo unalotaka tuongee hapa si mahali pake, nitakuelekeza wapi tuonane, hatuwezi kufanya biashara ya damu katika kasri hili tukufu, kasri la marehemu baba yangu alilotumia kuabudu, wewe nenda na mimi nitakujulisha wapi tuonane,” Yule mwanamke akamaliza kuzungumza na kuinuka kutoka pale alipokuwa ameketi akatokomea katika mlango mmoja wapo. Shalabah akainuka tayari kutoka ndani ya jumba lile, msichana mrembo wa uso alikuwa tayari kumwongoza kumtoa nje ya kasri hilo.

Shalabah alitolewa nje ya jengo lile kwa kupitia njia ileile lakini mara hii ali[pofika kwenye ule uwa akasimama na kushangaa anachokiona, mara ya kwanza alikuta watoto wakifanya mafunzo ya kungfu na karate, lakini mara hii alikuta uwa wote umeota nyasi na wanyama kama mbuzi walikuwa wakiburudika, alishindwa kuuliza akaamua kupitiliza mpaka nje ambako aliagana na Yule msichana akalielekea gari lake. Alipoketi nyuma ya usukani ndipo alipoiona kadi ndogo nyeupe ikining’inia katika swichi ya kuwashia vifuta maji (wipers) vya gari hiyo, akainyakuwa na kuisoma.

‘…Dar es salaam Club, saa 3:00 usiku…’

Makao makuu ya jwtz

Lugalo – dar es salaam

TAARIFA za kupotea kwa manowari ya jeshi la Tanzania na wapiganaji wake zilifika katika makao makuu ya jeshi hilo pale Lugalo mnamo majira ya saa tatu ausbuhi muda ambao manowari ile ilitakiwa kuwa imefika katika moja ya vituo vyake kabla ya kuwasili katika bahari ya Caspian siku mbili zinazofuata. Jeshi la Urusi lilipowasiliana na lile la Tanzania ilionekana wzi kuwa manowari hiyo imepotelea katika bahari ya Indi usiku uliotangulia, kwani kila walipojaribu kuitafuta kwa vifaa vya kisasa walishinda kabisa kuiona ilipo lakini waliweza kuona ilipoishia safari yake.

Wakipiga picha ya eneo hilo wanakuta ilikuwa sehemu za Somalia ijapokuwa ilikuwa katika maji makubwa, maji ya kimataifa.

Mkuu wa majeshi, brigedia jenerali Kamsumi alikuwa ameketi na viongozi wake wa ngazi ya juu kabisa jeshini wakijaribu kujadili juu ya upotevu wa manowari hiyo. Ulikuwa ni mkutano mzito ambao kila mshiriki alionekana kushikwa na jazba au hasira.

“Hao ni maharamia tu, si wengine, siku hizi wamekuwa wakiteka meli nyingi bila kujali sheria za kimataifa kuwa meli hizo ziko katika maji ya kimataifa, kwa nini tunawadekeza?” alilalama mmoja wa washiriki aliyekuwa katika jopo hilo.

“Meli sio tatizo, lakini vipi kuhusu makombora hayo ambayo gharama tu ya kuyatengeneza ilikuwa ni kubwa ijapokuwa tumepata ufadhili wa asilimia Fulani ya Warusi, tukiyaacha hawa jamaa si watatugeuka wenyewe?” Mjumbe mwingine alieleza.

“Hivyo vyote havina maana, wapiganaji wetu, watoto wetu wametekwa au kupotea pamoja na manowari hiyo kwa nini tuvumilie? Tuna makomandoo hapa tutume japo wawili tu wakaitafute hiyo meli kisha tuikomboe,” mjumbe wa tatu alikuwa akiongea mpaka anatoa machozi.

Baada ya majadiliano marefu na yaliyokuwa hayana mwisho, muada ulifika wa kufanya video conference na amiri jeshi mkuu. Luninga iliyokuwa ukutani ikachukua uhai na moja kwa moja mbele yao akainekana mheshimiwa Rais. Mkuu wa majeshi akaeleza kwa kifupi waliyojadiliana wajumbe katika kikao kile.

“Sikilizeni, hatuwezi kuvumilia wala kuwapa nafasi, ile ni pesa ya kodi za Watanzania, kwa nini ipotee hivihivi? Isitoshe kuna watoto wetu, vijana wetu na wapiganaji wetu, lazima waokolewe kwa gharama yeyote,” amiri jeshi mkuu aliongea kwa ukali sana, “Ninyi mna kitengo cha upelelezi ndani ya JW, haya mara moja chagueni mtu au watu wakafanye kazi hiyo, nitahitaji ripoti haraka,” mwisho wa maneno hayo ile luninga ikazimika. Kila mshiriki alishusha pumzi ndefu. Ilikuwa ni sentensi ndefu kidogo iliyowatetemesha wakuu hao wa jeshi waliokuwa wakibishana bila kupata muafaka katika lipi la kufanya. Kutokana na kauli ya aamiri jeshi mkuu, hakukuwa na mjadala mwingine kilichoangaliwa kilikuwa ni nani apewe kazi hiyo.

“Lakini jamani ee, tuiangalie hii kazi kwa ugumu na upana wake,” kiongozi mmoja alisema.

“Yeah ni kweli kuliko kudharau na kupeleka mtu ambaye atafika na kushindwa kufanya lolote. Nani tumtume akafanye kazi hiyo, kazi yan hatari kuliko hatari mwenyewe. Chekecha chekecha ikapita, Jamil Semindu, komandoo aliyemeliza mafunzo yake siku si nyingi nchini Cuba, jina lake lilipitishwa tayari kwa kazi hiyo. Mchana wa siku hiyo kijana huyo aliitwa makao makuu ya jeshi kutoka kambi ya Lugalo kule Mwenge. Naye hakukataa wito bali aliamini msemo wa wahenga, ;usikatae wito kataa neno’.

Majira ya saa nane mchana, Jamil Semindu alikuwa amesimama wima kiukakamavu mbele ya mkuu wa majeshi. Hakuwa peke yake, pembeni yake kulikuwa na mtu mwingine wa makamo, aliyavalia nguo nadhifu ya kijeshi.

“Jamil Semindu, Gwamaka Mwakajinga, tunatambua umuhimu na mchango wa kazi yenu katika jeshi letu tukufu la wananchi wa Tanzania. Nimekuiteni hapa kuwapa kazi maalum ambayo inatakiwa kuanzwa mara moja, kama mnavyojua au milivyosikia, manowari yetu ya jeshi la Tanzania, Kirov Class, ndani yake ikiwa na wapiganaji ishirini na tano pamoja na makombora kumi na mbili ya R-36 imepotea katika maji ya kimataifa huko Somalia, inahisiwa kuwa huenda ikawa imetekwa na maharamia kama iloivyotokea kwa meli zingine za mizigo. Tunawatuma muende mkafanye kazi, kwanza mkawaokoe wapiganaji wetu, pili mkaokoe makaombora yetu, tatu mkailete na meli yenyewe, mambo yote yamekwisha andaliwa mkitoka hapa tu mtaelezwa cha kufanya,” alimaliza mkuu jeshi. Wale wanajeshi wawili wakapiga salute na kisha kutoka nje ya ofisi hiyo.

Gwamaka Mwakajinga alikuwa mpelelezi wa kijeshi aliyeaminika sana hasa kwa kuzisoma nyanyo za adui, na kujua wapi alipo. Kijana huyu ndiye aliyewaongoza wenzake katika vita ya ukombozi huko visiwa vya Komoro, vita ya kumng’oa madarakani aliyekuwa rais wan chi hiyo. Alishiriki pia kupeleleza vizuri sana makazi ya waasi wa M23 pamoja na kujua maisha yao ya kila siku, mwisho wa siku aliwapa ramani yote majeshi ya Umoja wa Mataifa yakiongozwa na Tanzania na kuwafutilia mbali waasi hao. Jopo lililokaa kuchagua wawili hao liliangalia mambo mengi na tofautitofauti.

Gwamaka na Jamil wakapeana mikono na kusalimiana wakati wakiwa nje ya jengo hilo, kisha wote wawili wakaelekea katika jengo linguine kama walivyoongozwa.

“Unaonaje Meja, hawa vijana watawaweza wale maharamia wanaokunywa damu?” Luteni kanali Gogo alimuuliza mwenzake aliyekuwa naye, kapteni Kamazima.

“Wataweza tu, tuweke imani,” Meja Kamazima alimjibu.

“Maana wale maharamia kuwapata ni kazi, nao pia wamejikamilisha kwa silaha na upiganaji wa silaha,” Luteni Kanali Gogo alionesha waziwazi wasiwasi wake katika hili.

“Wataweza tu usihofu,” Meje Kamazima alimjibu na kumtia moyo mwenzake.

Taratibu zote zilikamilishwa za safari za hao jamaa, na siku iliyofuata kwa kutumia ndege ya shirika la ndege la Ethiopia waliondoka Tanzania kuelekea Somalia kupitia Addis Ababa.

“Sijacheza michezo hii siku nyingia sana,” Jamil alimwambia Gwamaka.

“Michezo midogo sana hii, nilikuwa Kivu juzijuzi tu kuwasaka M23 hivyo bado damu ya moto,” akazungumza Gwamaka. Walibadilishana mawazo wakiwa katika ndege hiyo safarini kuelekea Mogadishu.

“Sasa sikia Jamil, unajua hawa jamaa ni wajanja sana, kwa vyovyote lazima wanajua kama tunakwenda, tukifika naomba tushuke kila mtu kivyake na tusijuane isipokuwa tuwasiliane kwa simu tu kila mtu atakapofikia,” Gwamaka alijaribu kupanga mpango.

“No, tufikie hotel moja lakini tutofautishe vyumba kwa umbali mrefu kama kuna ghorofa basi mmoja ya juu mwingine ya chini,” Jamil naye akatoa pemdekezo ambalo lilikubaliwa na wote.

“Tutafanyaje operesheni yetu?” Jamil akauliza.

“Kutokana na kazi zetu, mi nitakuwa nafanya uchunguzi nakupa information na wewe unakwenda kumaliza kazi maana we ni jeshi la mtu mmoja,” wote wakacheka na kugonga viganja vyao.

RAMADA PLAZA HOTEL

Ramada plaza hoteli, ni hotel tulivu iliyo jirani na bahari katika jiji la Mogadishu, ikitazamana na bandari ya zamani ya jiji hilo. Mandhari safi, chakula na mazingira ya kuvutia viliwafanya wapiganaji hawa kuvutiwa na mahali hapo.

Alikuwa Gwamaka wa kwanza kuingia katika hotel hiyo, akapanga chumba ghorofa ya tatu juu. Baadae jamil nae akafika na kuchukua ghorofa ya chini kabisa, wakiwa tayari kikazi na wamekamilika.

Kutoka ghorofa ya tatu Gwamaka aliweza kutumia darubini yake kuangalia upande wa baharini kila baada ya nusu saa na kuandika kwenye kidaftari chake mambo anayoyajua mwenyewe. Jioni ya siku hiyo wakiwa chakulani walibadilishana mawazo hili na lile na kupanga nini cha kufanya.

§§§§§

DAR ES SALAAM CLUB

SHALABAH aliegesha gari yake katika maegesho ya club hiyo ya usiku, akateremka na kuufunga mlango nyuma yake. Kisha kwa hatua za taratibu aliuendea mlango mkubwa. Kwa upande wa nje zaidi ya walinzi walioonekana kuangalia usalama wa mali za wateja, hakukuwa na vurugu wala hakukusikika kelele yoyote ya kitu chochote, mtaa ulikuwa kimya kabisa. ni wale tu waliokuwa hawafuati sawasawa misingi ya dini yao ndiyo waliokusanyika katika klabu hiyo pamoja na wageni kutoka Katika nchi za pembezoni na zile za mbali.

Shalabah alizipanda ngazi na alipofika katika mlango wa kuingilia alisimamishwa na akatakiwa kusalimisha kama ana aina yoyote ya silaha, alikuwa na bastola moja na kisu cha kukunja, akaviacha na kuandikisha, akapewa namba na kuingia ndani.

Tofauti na nje, ndani ya klabu hiyo kulikua na kila aina ya starehe, muziki laini ulikuwepo na wale waliopenda disco walitakiwa kuteremka chini kabisa. watu walikula na kunywa wakifurahia maisha. Shalabah alijipenyeza taratibu katika makundi ya watu mpaka akaifikia kaunta kubwa.

“Nikusaidie nini?” akauliza mtu aliyekuwa kaunta. Shalabah hakujibu isipokuwa alitoa sigara na kumuonesha, kisha yule jamaa akatoa kiberiti na kukiwasha lakini hakuiwasha ile sigara. Sekunde chache tu mwanadada mrembo aliyekuwa na nywele mpaka kiunoni alimjia Shalabah na kumshika begani. Shalabah akamfuata. Wakapenya penya katika makundi ya watu, wakapita nyuma ya jukwaa la wacheza uchi wakaingia kwenye pazia la kumetameta, ndani ya mlango mkubwa na mzito wa kioo, hakukuwa na kelele yoyote, palikuwa kama nyumbani, huko kulikuwa na vyumba vingi sana.

809, yule mwanadada akasimama na kubofya kitufe Fulani, mlango ukafunguka, wakaingia. Ndani ya chumba hicho kulikuwa na chumba kimoja kidogo na mwanadada mrefu aliyekuwa na upara kichwani mwake huku akivuta mtemba kinywani mwake alikuwa amekunja nne kwenye sofa moja pana na kuiachia nguo yake yenye mpasuo mrefu kumwagika kwa chini na kuruhusu mapaja yake laini kuonekana kwa ukamilifu.

“Karibu Kijana,” yule mwanamke akamkaribisha.

“Asante sana,” Shalabah akajibu.

“Haya tuna dakika tano tu za kuzungumza, nipe mzigo, nikupe kipimo,” yule mwanamke mwenye upara akamwambia Shalabah.

“Nafikiri unatufahamu, sasa tuna biashara nzito sana ya kufanya, ijapokuwa hatuna hofu na usalama kutokana na biashara zetu zilizopita, ila hii tumetahadharishwa sana, kuna watu tunatakiwa kuwaondoa haraka iwezekanavyo lakini pia tunahitaji usaidizi wa kiteknolojia katia kuyatambu makombora kumi na mbili tuliyoyateka,” Shalabah alieleza.

“Ha ha ha ha nyie watu mna biashara za hatari sana, kwa kuwa tuliingia mkataba huo tangu mwanzo na tajiri wenu hamna tabu, haya kazi ya kwanza itafanyika, nipe picha za hao watu na wapi wamefikia, kuwatungua si tatizo, kisha tutaliona la pili,” yule mwanamke mwenye upara akaeleza. Shalabah akatoa Ipad yake na kuparazaparaza vidole vyake kwenye kioo cha chombo hicho, kisha akamkabidhi yule mwanamke. Akachukua na kutazama, naye akaparaza hapa na pale na zile picha zikahamia kwenye simu yake ya kisasa kwa njia ya Bluetooth.

“Ok Mr. kila kichwa dola 1000 za kimarekani, nimemaliza, fanya mchakato kama tunavyofanya kila wakati,” yule mwanamke akanyanyuka na vazi lake likamfunika vyema, akafungua mlango wa nyuma yake na kutokomea. Shalabah alitoka ndani ya chumba kile na kutembea taratibu kurudi ukumbini, kisha akatoka nje ya klabu ile.

§§§§§

Ndani ya bahari ya Indi katika bandari ya zamani ya Mogadishu, maharamia wateka meli walikuwa katika ulinzi wa aina yake. Walionekana ni watu masikini kimavazi lakini ukiwatazama silaha walizobeba mikononi mwao utakubali tu. Wapo waliokuwa juu muda wote wakitazama usalama kwa kujifanya wana shughuli mbalimbali. Na daima walikuwa wakifuatilia sana nyendo za wageni wanaoingia Somalia hasa wale kutoka nchi za maghalibi kwa maana walikwishateka meli kadhaa za mataifa hayo na kuwaweka mateka wanajeshi wao. Hata zile nchi zilipojaribu kutaka kuwapata watu hao ilikuwa ngumu kutokana na nchi ya Somalia kutokuwa na serikali ambayo unaweza ukafanya mazungumzo nao.

Wapiga mbizi kadhaa walikuwa ndani ya maji wakikagua makombora hayo, upande wa wale wanaouza ambao ni hao maharamia na wale wanaouziwa wapiganaji waasi kutoka huko Pakistani na Afghanistani, walikuja na wataalamu wao na wakati huo maharamia hao nao walikuwa na mtaalamu wao wa silaha, mwanamke yule mwenye upara. Ukaguzi ulifanyika chini ya maji kwa muda takribani wa dakika thelethini, kisha wapiga mbizi hao wakatokea ndani kwa ndani na kuingia katika chumba kilichojaa maji ambacho kuna ngazi unapanda na kutokea chumba cha juu kisicho na maji. Hapo wakavua mitambo yao walioibeba migongoni na kubaki katika nguo zao za kawaida. Kisha wakafuatana kutoka na kuingia katika gari iliyoandaliwa wakaelekea mjini.

Kepteni Gwamaka Mwakajinga akashusa darubini yake kutoka katika uso wake akaichia ining’inie kifuani.

“Wametoka,” Gwamaka akawasiliana na Jamil aliyekuwa kwenye gari nyingine.

“Wasindikize, unambie wanapoishia,” Jamil akamwambia Gwamaka. Kwa mwendo wa taratibu Gwamaka akaingiza gari barabarani na kuendessha kuelekea kule ambako gari ile ilikwenda. Alihakikisha haipotezi kabisa gari hiyo katika macho yake.

Aliendelea kuwafuata akiwa peke yake ndani ya gari.

“Gwamaka, kuna gari imenipita kasi sana hapa hebu iwekee tahadhari,” Jamil aliwasiliana na Gwamaka wakati gari hyo aliyoisema ikiwa mbele yake kama mita kumi tu. Walipoiacha barabara ya Corso Somalia na kuupita mzunguko kisha kuikamata barabara ya Jidka Jannaral Daud ndipo komandoo Jamil alipoona hila ya watu hao, akajua wazi kuwa wako matatani na hana budi kumsaidia mwenzake aliyekuwa mbele.

“Nimeiona,” akajibu.

“Kaa tayari, jamaa wameandaa silaha nahisi wanataka kufanya shambulizi la ghafla,” Komandoo Jamil alimwambia Gwamaka.

“Natafuta mbinu ya kufanya,” Gwamaka akamwambia Jamil.

Haikupita sekunde thelathini, wakati wanakaribia kabisa shule ya sekondari ya Jan Daud, ile gari nyuma ya Gwamaka ikaovateki ghafla na kukaa upande wake wa kushoto, Gwamaka akawa tayari amekwishaiona, akaipa sekunde mbili ilipokuwa tayari inakaribia nusu ya gari yake kuovateki, nae akaitoa gari yake kushoto, na kusababisha dereva wa wale jamaa kuyumba, ile gari ikagonga nguzo ya umeme, cheche zikawaka na transifoma la jirani likalipuka.

“Usisimame, wafuate,” Komandoo Jamil akamwambia Gwamaka kwa simu yake ya upepo yeye akiwa katika gari iliyokuwa nyuma yao umbali wa mita kama hamsini hivi, aliishuhudia ile gari ikigonga nguzo na ule moto wa umeme uliolipuka ukafanya gari ile kushika moto. Jamil alishuhudia watu wale walivyokuwa wakijaribu kutokea madirishani.

“Safi sana Gwamaka!!!!” Komandoo Jamil aliikubali mbinu iliyofanywa na Gwamaka, akaongeza mwendo na kuzipita gari mbili zilizo katikati yake. Akapunguza mwendo na kushuhudia wawili wakiungua vibaya kwa kushindwa kutoka ndani ya gari, na mmoja akiwa ndiye anajinasua dirishani. Komandoo Jamil, akaegesha gari pembeni na kuteremka kwa minajiri ya kutoa msaada, akamuendea yule wa dirishani na kumnasua katika kioo, akambeba na kumtia kwenye gari yake.

“Wapi Hospitali?” akawauliza watu waliokuwa eneo lile kwa lugha ya kiarabu ambapo walielewana vizuri, hilo halikumfanya yeyote kutia mashaka juu ya Jamil, akaondoka kwa kasi mapaka njia panda ya Siinay akakunja kushoto na kuendesha gari hiyo kwa kasi ya ajabu, mpaka akauacha mji na kufika maeneo yaiyo na watu, jangwa lilianza kumkabili, akaegesha gari pembeni, akamshusha yule jamaa.

“Hapa ndo hospitali?” yule majeruhi aliuliza kwa tabu kidogo.

“Aliyekwambia mi mwezi mwekundu nani hata nikupeleke wewe hoapitali?” Jamila akajibu na kumvuta akambwaga kwenye mchanga ulioshika joto kali la jua. Akamkanyaga pajani ambapo palikuwa na donda kubwa la moto.

“Nani mwajiri wako?” akamwuliza. Yule jamaa hakujibu isipokuwa akamtolea macho Jamil. “Nakuuliza nani unamfanyia kazi? Aliyewatuma kuifuatilia ile gari,” akaongeza swali linguine, yule jamaa akawa mgumu kujibu, Jamila akamuinamia na kuchomoa kisu, akachoma mchomo mmoja kwenye paja. Yuele jamaa akatoa yowe la uchungu sana.

“Nitakwambia, nitakwambi, nitakwambia,” akapiga kelele.

“Haya nambie,” Jamil akamsikiliza.

“Sharon, Sharon, kamanda Sharon,” akajibu.

“Ndiyo nani?” akauliza tena Jamil.

“Kiongozi wetu, aliwaona mkitufuatilia, akatutuma tumuue yule mwingine, wewe hakukuona,” yule bwana akajibu huku akilia kwa uchungu.

“Anaishi wapi huyo Sharon?” Jamil akahoji. Yule bwana akawa jeuri kujibu, kila alipolazimishwa hakujibu. Jamil akashika kile kisu kilichodinda katika nyama ya paja la yule jama na kukizungusha, yowe kali lilimtoka tena yule bwana akalia mpaka akawa akipigapiga ngumi kwenye mshanga.

“Jidka Dabaqayn,” akajibu huku akilia. Jamil akamuacha na kuchomoa kile kisu. Kitendo cha ghafla yule jamaa kutoka pale chini akajinyanyua na kutaka kumvamia Jamil, Jamil akaliona hilo haraka, akaachia makonde mawili makali yaliyomrudisha chini na kumtoa roho. Akamuendea na kumsukasuka kwa mguu wake, ameshakufa. Akampekua mifukoni hakuna cha maana alichokipata zaidi ya picha moja ya msichana mbichi aliyepiga akiwa uchi wa nyama, akaichukua na simu yake pia na akaondoka navyo. Jamil akaliendea gari lake na kuondoka akiuacha mwili wa yule jamaa palepale jangwani yeye akarudi mjini.

§§§§§

Gwamaka aliendelea kuifuata ile gari mpaka pembezoni mwa mji, ikaingia katika jengo moja kubwa lililoonekana kama kiwanda Fulani, yeye akapitiliza na kwenda kuegesha gari mbele kidogo. Akateremka na kurudi polepole mpaka kwenye mgahawa uliokuwa ukitazamana na jengo lile. Akaketi upenuni mwa mgahawa huo na kuagiza kinywaji huku macho yake yakitazama mara kwa mara jengo lile. Moqdisho textile, ni maandishi yaliyolipamba godown lile kwa upande wa juu, Gwamaka akachukua kijidafutari chake na kuandika jina hilo, jina la barabara na namba ya kiwanja, akahifadhi mfukoni mwake. Akaendelea taratibu kupata kinywaji chake. Akiwa bado anaendelea mwanadada mmoja alitoka ndani ya mgahawa huo na kuketi katika kiti cha mbele yake, wakasalimiana, ijapokuwa Gwamaka alikuwa akibabaisha kusalimiana kwa lugha yao. Akabadilisha lugha na kuanza kuongea kiingereza.

“Inaonekana ni mgeni wewe hapa?” yule mwanamke akamwuliza Gwamaka.

“Ndiyo, ni mgeni hapa, nimesimama kidogo nipate kinywaji, si waona jua lilivyo kali,” Gwamaka akamweleza.

“Aa yah ni kweli, wewe watokea wapi?” yule mwanamke akamwuliza.

“Mimi ninatokea Kenya naitwa Charles Musungu,” Gwamaka akajitambulisha kwa jina la bandia.

“Oh, jina zuri, mi naitwa Fatma, huu mgahawa hapa ni wa familia,” Fatma akaendelea kuzungumza, baada ya hapo mazungumzo mengi yakaendelea kati ya wawili hao, Gwamaka akachukua kadi ya kibiashara ya Fatma na kuihifadhi. Wakati wakiendelea kuzungumza, aliiona ile gari aliokuwa akiiangalia akaiona ikitoka na kuondoka.

“Fatma, maadam nina namba yako, basi nitakupigia jioni, vipi unaweza kuungana nami jioni ya leo?” Gwamaka akamwambia Fatma huku akiwa amenyanyuka tayari kuondoka.

“Bila shaka Charles,” Fatma akaitika huku akimshuhudia Gwamaka akaiziacha ngazi za mgahawa huo na kuingia mtaani, aliichuku gari yake na kuondoka kwa kasi kuifukuza ile gari, si mwendo mrefu aliikuta, akaipa nafasi gari ile na kuifuata taratibu.

“Braza,” sauti ikaita katika earphone yake.

“Hey Jamil,” Gwamaka akajibu.

“Uelekeo,” Jamil akauliza.

“Bado nawinda, nitakucheki,” Gwamaka akajibu.

“Copy,” Jamil akaitikia.

Msafara wa ile gari ukaelekea uwanja wa ndege moja kwa moja. Gwamaka akaendele kuwatazama watu wale wakiagana, akachukua kamera yake na kupiga picha kadhaa. Aliporidhika na zoezi hilo akaingia kwenye gari yake na kurudi mjini.

Gwamaka alikuwa akiendesha gari taratibu huku akipiga mruzi, mbele yake akaona kibao kilichoandikwa SHELL, alipotazama mshale wa mafuta ulimuonesha tanki lake liko mbioni kumalizika, akawasha indiketa ya kulia na kuingia katika kituo hicho cha kujazia mafuta. Moja kwa moja akaegesha katika moja ya pampu sita zilizofungwa hapo.

“Full tank tafadhali,” akamwambia kijana aliyekuwa akihudumia pampu hiyo, na kijana yule akafanya kazi yake kama ilivyotakiwa. Gwamaka akalipa na kuondoka eneo lile kurudi hotelini kwake. Akaingia kwenye maegesho ya magari na kuliweka gari lake vizuri, akatulia kwanza kabla ya kushuka, baada ya dakika kama kumi hivi akateremka na kuvuta hatua ndefundefu huku mikono ikiwa mfukoni na, akazipanda ngazi za hotel hiyo mpaka katika chumba chake, alipofika mlangoni akatulia kidogo akatzama mitego yake akagundua ama kuna mtu aliingia au ameingia, akachomoa bastola yake na kuishika barabara kwa mkono wake wa kulia kisha taratibu akanyonga kitasa na kuufungua mlango huo, akaingia ndani na kutazama huku na kule, akaangalia kila kona ambayo anajua kama imeguswa au la, kwa jinsi alivyokiacha chumba chake alijua tu kuna mtu aliyepekuwa kitaalamu sana kiasi kwamba kwa amtu ambaye ni wa kawaid hatoligundua hilo lakini haikuwa kwa Gwamaka. Alipojiridhisha kuwa usalama upo akaketi kitandani na kuvua fulana aliyokuwa ameivaa. Akaliendelea dirisha ambalo alikuwa amefunga darubini yake ya jicho moja, akachungulia kuona nini kinaendelea upande wa bandari ya zamani ya Mogadishu ambako inasemekana huko ndiko maharamia wale wanakoficha nyara zao. Hakuna jipya zaidi ya kuona walinzi walewale wakivuta bangi na kuendelea kulinda maeneo yao. ‘Nchi isiyo na serikali ni shida tupu’ akajisemea wakati akitoka pale dirishani.

§§§§§

Mwanamke mwenye upara akashusha darubini yake iliyokuwa ikimwangali Gwamaka alipofika chumbani kwake, akaiacha ining’inie kifuani mwake.

“Amerudi,” Fasendy akawaambia vijana wake machachari. Wakanyanyuka mara moja, “hakikishenu mnamleta mzima, tunataka tumtoe sadaka kesho ijumaa,” akaongezea maneno hayo kisha akavuta kiti akaketi na kuwasha sigara akaipachika kinywani. Wale vijana walifanya kama walivyoagizwa, wakafika Ramada hotel na kukamata kila mtu kona yake kisha wawili kati yao wakaingia ndani na kupanda ghorofani kukifuata chumba cha Gwamaka. Hawakugonga hodi wala kuuliza, wakapiga teke mlango nao ukafunguka, wakajitoma ndani kwa ustadi ikiwa na kutanguliza mtutu wa bunduki, hakuna mtu. Wakaingia mpaka ndani na kutazama kila mahali lakini bado hawakuona mtu, uvunguni kwenye makabati kote Gwamaka hayupo. Wale jamaa wakashusha pumzi ndefu kung’uta mashuka yote inua kitanda, hakuna Gwamaka.

“Aisee, huyu mtu ameondoka hayupo hapa,” mmoja wao akasema kumwambia mwenzake, kisha wakatoa taarifa kwa redio na kutoka nje ya chumba kile.

Gwamaka aliibuka kutoka katika beseni kubwa la kuogea lililojengewa pembeni kabisa mwa bafu hilo, wakati jamaa hao walipokuwa wakipekua kumtafuta, yeye tayari alikwishajizamisha kwenye beseni hilo lililojaa maji ya sabuni ambayo haiukuwa rahisi mtu kuona kilichopo ndani yake.

Alitoka na kusimama pembeni huku nguo zake zikimwagika maji, akatulia kimya akisubiri kuona kama watu hao wamekwishatoka au la. Alipoona ukimya umetawala akampa taarifa Jamil aliyekuwa bado hajafika mahala pale.

Plaza hotel iliwekwa chini ya nuangalizi wa siri na wapiganaji maharamia wakiwahofia watu hao kutoka Afrika Mashariki, walidhamiria kuwamaliza vijana hao, kwa maana walishaona hatari itakayosababishwa nao. Waliizingira hotel ile kwa siri, wengine wakijifanya kuja kula, wengine wakifanya jambo hili au lile ilimradi tu ni kutaka kujua kama watu hao wapo au hawapo ili watekeleze azma yao.

“Usitoke ndani, jamaa inaonekana bado wapo,” Jamil alimwambia kwa simu ya upepo. Gwamaka akaendelea kutulia chumbani mwake, akisubiria asikie nini ataambiwa na Jamil ambaye alikuwa nje ya hotel hiyo.

Jamil alikuwa akiegesha gari yake nje ya hotel hiyo alipojikuta akiwekewa mtutu wa Short Machine Gun sikioni mwake.

“Sihitaji kukuuliza wala kuniuliza, shuka kwenye gari,” Jamil aliamrishwa na mtu mmoja mwenye bunduki hiyo aliyeishika madhubuti mkononi mwake, ikiwa imefungwa kwa mkanda uliomzunguka nyuma ya bega lake. Jamil hakuwa na ujanja kwani aliona wazi kuwa jamaa huyo hana masihara hata kidogo, alikuwa ni mwembamba mrefu mwenye macho mekundu, kinywani mwake alikuwa akitafuna mirungi. Jamil akateremka kutoka katika gari lake, lakini kabla hajatoka kabisa alidondosha vikolokolo vyote alivyochukua kutoka kwa yule mateka wake aliyemuua jangwani, kisha akatoka nje.

“Weka mikono kichwani,” aliamuriwa, akafanya hivyo na kuswagwa mpaka kwenye jeep moja iliyokuwa upande wa pili wa barabara, Jamil alipokuwa akipanda kwenye hile jeep akafanya hila ambayo hawakuigundua, akabofya kitufe cha redio yake ambayo iliunganishwa kwa ndani ya shati lake juu karibu na mdomo, wakati huo alikuwa amevua zile earphone zake, hivyo moja kwa moja ikaunganisha kwa Gwamaka. Gwamaka akaanza kusikia lugha ya kisomali ikiongelewa na watu waliokuwa wakibadilishana mawazo.

“Hatari nimetekwa,” Jamil alinong’ona na sauti ile ilisafiri moja kwa moja mpaka kwa Gwamaka.

“Unaongea na nani?” akauliza mtu mmoja aliyekuwa na rifle mkononi mwake, akaiinua na kumpiga kwa kitako cha bunduki hiyo, jamili akaenda chini ndani ya bodi ndogo ya gari ile.

“Shiiit,” Gwamaka akang’aka, akachukua bastola zake mbili, na kuziweka magazine na nyingine akajaza mifukoni katika jeans, akatoka mlangoni, bila hadhari yoyote akitaka kuwahi kujua jamil anapelekwa wapi. Lilikuwa ni kosa kubwa sana alilolifanya, hakuna kingine alichokihisi zaidi ya maumivu makali kichwani mwake, kizunguzungu kikafuatia, akadondoka chini.

Mwanamke mwenya upara alisimama pembeni yake.

“Mlivyosema hayupo na huyu ni nani?” akawauliza wafuasi wake. Hakuna aliyejibu, wakamnyanyua Gwamaka na kutoka naye kupitia mlango wa nyuma, wakampakia kwenye gari yao na kuondoka naye.

§§§§§

SHALABAH alitulia kitini akinywa taratibu kahawa yake. Gari moja nyeusi aina ya Toyota Nadia ilisimama mita chache kutoka pale alipokuwa ameketi. Mwanamke mrefu akateremka, aliyevaa kininja, akavuta hatua ndefundefu mpaka pale alipoketi, akavuta kiti na kukaa.

“Sina maneno mengi, ila unajua kuwa nimekwsihamaliza kazi uliyotaka nifanye, nimefata hundi yangu,” Fasendy akamwambia Shalabah.

“Usijali, niliketi hapa kukusubiri wewe, ili kukukamilishia malipo yako lakini pia kuna kazi nyingine ya kufanya,” Shalaba akamwambia Fasendy huku akimpatia bahasha nyeupe ambayo ndani yake kulikuwa na hundi hiyo. Akaifungua na kutazama akaiona ni sawa, akaifutika ndani ya nguo yake.

“haya, ongea linguine,” Fasendy akamwambia Shalabah.

“Nifuate,” Shalabah akamwambia Fasendy kisha akanyanyuka na kuingia ndani ya jengo hilo lililoonekana kama gofu, lililotelekezwa kwa muda mrefu sana, wakapita koridoni mpaka kwenye moja ya chumba, wakaingia na kukatiza milango kama mitatu hivi, mlango wan ne ulikuwa mlango wa kioo safi uliozungukwa na kamera za cctv ili kulinda usalama wa eneo hilo. Shalabah akabonya kitufe na mara mlango ule ukafunguka, wakaingia ndani.

Kilikuwa ni chumba kidogo lakini chenya kila kitu kinachohitajika katika ofisi yoyote duniani. Shalabah akamkaribisha Fasendy na wote wawili wakaketi katika viti vyenye vono safi. Katika meza iliyokuwa mbele yao kulikaliwa na mtu mmoja mnene mwenye mwili mkubwa aliyejaa katika suti kali nyeusi, kichwa chake kilionekana kuungana na kiwiliwili, hakuonekana shingo yake kama ilikuwepo au ilimezwa na unene huo.

“Karibu sana mwanamke,” akamkaribisha Fasendy, akajikohoza na kuendelea, “ kwanza nikupongeze kwa kazi ngumu nay a hatari uliyoifanya ya kutuletea wale watu wawili wanaojifanya kufuatilia nyayo za samba. Nafikiri malipo yako umeshayapata, lililobaki huku mbeleni tuachie sisi tunajua cha kuwafanya, lakini nina jambo moja, hawa Watanzania wakishaona wenzao hawapatikani kwa mawasiliano kwa vyovyote watatuma mtu mwingine au watu wengine kuja kuwatafuta, sasa nataka nikupe kazi nyingine ya mkataba wa miezi mitatu, ya kuhakikisha kila anayeingia hapa ni kumpoteza moja kwa moja kama tulivyofanya kwa wale Waamerika waliojifanya waandishi wa habari, upo tayari?” yule mtu akauliza.

“Wewe unajuaje kama watatuma watu wengine?” Fasendy akauliza.

“Mimi najua, ninalokwambia ndilo hilo, kumbuka tuna wanajeshi wao ishirini na tano, na hawa wawili, unafikiri watavumilia? Tunataka kuhakikisha biashara yetu inakwenda safi kabisa,” yule Bwana akamaliza.

Fasendy, akatulia kimya akiitafakari uzito wa kazi hiyo.

“Sawa, hamna tabu,” akajibu Fasendy. Yule mtu mnene akasimama na kumpoa mkono Fasendy kisha akamruhusu aende. Shalabah akamsindikiza hadi nje na kuagana naye.

“Sharon,” yule mtu mnene akaita. Sharon akajitokeza kutoka katika mlango Fulani pembenzoni mwa chumba kile, akasimama akisikiliza, “Boss ansema uhakikishe wale mateka wawili wanajutia walichokifanya na upeleke onyo kali kwa waliowatuma, kisha simamia biashara nzima, wateja wetu wamesema watakuja baada ya siku tatu kuangali makombora yaliyobaki, kama kuna shida yoyote wasiliana na Shalabah, yeye ndiye mwenye uwezo wa kuwasiliana na mimi na Mr Lonely kwa utatuzi wa mwisho,” yule Bwana akamaliza na kuagana na watu wake, kisha akabaki yeye na Shalabah tu.

§§§§§

MOQDISHO TEXTILE

Jamil alikuwa amefungwa kamba na kuning’inizwa kichwa chini miguu juu, hakuweza kufanya lolote kwani pembeni yake alikuwa akilindwa na vijana wawili wadogo waliokuwa na silaha za maana zilizodungwa mkanda mrefu wa risasi, hawakuona taabu kummiminia yeyote atakayeleta shida katika himaya hiyo. Walikuwa ni vijana wawili wenye kukadiriwa umri wa miaka kumi na tano na kumi nane. Vinywani mwao waote walikuwa wanakula mirungi. Jamil aliwatazama kwa zamu ili aone kama kuna jinsi ya kujiokoa lakini hali ilikuwa siyo, kwa kuwa mlango wa chumba hicho ulikuwa ni wa chuma madhubuti kabisa. Jamil alitulia palepale huku akiwaza ni wapi Gwamaka atakuwapo kwani alimuacha hotelini.

Mara mlango ukafunguliwa, Sharon akaingia ndani na vijana wengine wawili waliovaa kiraia lakini wakiwa na silaha nzito. Jamil aliona wazi hawa jamaa hawajui matumizi ya silaha kwamba silaha hii nitumia vitani na sio kutembea nayo nah ii nitumie wapi, ilikuwa haishangazi kumkuta mjini au sokoni begani mwake amejitwika RPG huku akitalii akitazama hili na lile.

“Mfungue, umtoe hapa,” Sharon aliamuru, kijana mmoja akaja na kisu na kukata kamba iliyofunga miguu ya Jamila, akaanguka na kutanguliza kichwa, akajipiga kwenye sakafu na kubwagika chini kama mzigo. Jamil akatoa mguno hafifu wa maumivu, kisha akatulia kimya. Wakamfungua kamba za miguu na kumuinua, akasimama wima lakini akiegemea ukuta maana alikuwa akisikia kizunguzungu cha hali ya juu.

Sharon akamsogelea Jamil.

“Komandoo, koamndoo utakuwa wewe? Hiyo serikali yenu bora iombe msaada niwape hawa watoto wawili tu ni sawa na vikosi vyenu kumi vya kijeshi, na sasa utajuta, kukamatwa na sisi, sisi hatuna serikali kwa taarifa yako, na sasa utaenda kushuhudia ndugu yako anavyouawa na hiyo ndiyo salamu kwa serikali yako, mataifa ya magahribi yameshindwa itakuwa ninyi, ninyi ni nani hata mjifanye mna uchungu?” Sharon alimwambia Jamil, alipomaliza tu kusema akageuka na kuwaamuru watu wake kumuongoza Jamil upande wa pili wa jengo. Wakamto ilhali akiwa na kamba mkononi mwake.

Ulikuwa ni ua mkubwa sana wenye malori kadhaa yaliyokuwa yameegeshwa. Watu wenye silaha walikuwa wengi, vijana, watu wazima, walikuwa na silaha nzito nzito.

“Simama hapa” Jamila aliambiwa na wale waliokuwa wakimlinda, akasimama pamoja na watu wengine wawili, wazungu walioonekana kuchoka sana. Mara akachukuliwa mmoja wao na kupelekwa katikati ya ule uwanja, kelele zikaanza kusikika, kelele za mashangilio, huku wakipiga risasi hewani, yule aliyempeleka pale akachomoa jambia na kumkata shingo, akamchinja na kutenganisha kabisa kichwa na kiwiliwili. Kwa kitendo hicho wenzake wakashangilia sana, ilikuwa ni kama tafrija kwao. Jamil alishindwa kutazama kitendo hicho, aliinama na kufumba macho.

“Watu makatili sana hawa, sidhani kama ni binadamu wa kawaida,” Jamil aliongea kwa sauti ya chini. Kisha yule jamaa aliyemchinja yule mtu akaja kwa Jamil na yule mwingine, akasimama mbele yao.

“Burudani yetu ni kuwachinja watu kama ninyi, siku yenu bado,” akamaliza na kuondoka. Jamil na yule mwenzake wakachukuliwa na kufungiwa ndani ya chumba kisicho hata na dirisha isipokuwa tundu dogo kama shimo la panya lililoweza kuingiza hewa kwa tabu na mwanga kidogo sana.

Kufungiwa ndani ya chumba hicho kwa Jamil haikuwa mateso, bali kukaa bila kujua Gwamaka yuko wapi hilo ndilo lilikua teso kubwa kuliko yote, alibaki hivyo akitafakari bila jibu, hakuwa na jinsi ilimpasa kutulia.

JUA kali la saa saba lilikuwa likichoma kwelikweli, mji wa Dar es salaam uligubikwa na joto kali, kila umuonaye kama hana kitambaa mkononi cha kufuta jasho basi alikuwa kifua nusu wazi ilimradi apate kaupepo hako kadogo. Lakini wote waliokuwa wakiteseka na joto hilo ni wale watu wa KCC yaani Kima Cha Chini, lakini kwa mwenye nazo daima jiji la Dar es salaam ni jiji lenye baridi sana kiasi kwamba kila muda anatembea na suti ya vipande vitatu.

Jiji linalosifika kwa uzuri na linalovutia watalii kwa historia yake ya utulivu na amani. Kila kijana wa Tanzania anaamini kuwa katikan jiji hilo ndiko maisha yanakoanzi hivyo huwafanya wengi kukimbilia huko ili kuanza maisha mapya wakiamini watatajirika. Lakini hali huwa tofauti sana wakifika katika jiji hilo, mwisho wake ndio vibaka, wabwia unga, makahaba kuongezeka katikati ya jiji na kwenye viunga vyake. Ijapokuwa kila mara wanasomba na polisi na kuwekwa mahabusu lakini wakitolewa tub ado huendelea na shughuli zao hizo hizo wanaacha kwenda vijijini wakawekeze katika kilimo na ufugaji, lakini siwalaumu wao, ila nailaumu serikali inayoshindwa kuwawekea mafunzo thabiti ya ujasiriamali tangu wakiwa shule ya msingi, hata somo la sayansi kilimo lililokuwapo shuleni siku hizi hata haliko katika mitaala, basi waache vijana wajikimbilie mjini na taifa kuwa taifa la vibaka.

Katika ofisi ya wizara ya ulinzi na jeshi lakujenga taifa, Mwenge, Mlalakuwa hali ya utulivu ilikuwa imetawala, ni bendera tu ya Taifa iliyokuwa ikipepea huku na huko kadiri ya upepo ulivokuwa ukiitaka. Geti lilifunguliwa taratibu na mwanajeshi aliyekuwa lindoni siku hiyo.

“Kuna mzigo wenu hapa,” kijana mmoja aliyekuwa juu ya pikipiki aina ya Yamaha alikuwa akiwaambia walinzi hao.

“Ok, nenda mlango ule pale kuna mwanadada pale mkabidhi,” yule MP akampa maelekezo baada ya kusoma anwani na kukuta imeelekezwa katika ofisi ya waziri mwenyewe.

Katibu muhtasi wa wizara, Miranda, alisaini kitabu cha dispatch cha kijana huyo kamba ameupokea mzigo huo katika hali ya usalama. Kisha wakaagana.

Kilikuwa ni kikasha cha mbao, kilicho tengenezwa vizuri na kupigwa vanish safi, pembeni anwani yake ilikuwa imeandikwa kwa maandishi ya chuma yaliyokuwa yaking’aa sana, na kwa sababu kilikuwa na anwani ya ofisi haikuwa tabu kwa Miranda kukifungua kujua ndani kuna nini kwa kuwa ni mzigo wa kiofisi, akachukua kijinyundo kidogo na kubabazua mfuniko wa kikasha hicho nao ukafunguka, ndani yake akakuta kitu kama box hivi, alipoligusa lilikuwa la baridi kama lina barafu ndani yake, akaondoa gundi iliyofunga box hilo na kulifungua ndani, huko akakuta kasha maalum sililoruhusu barafu kuyeyuka akaondoa mfuniko wake.

“Aaaaaaaaaaaaaaaiiiiiiiiiggghhhhhhhhh!!!!!!!” ilikuwa ni kelele moja kali kutoka kwa Miranda, mara ikakatika ghafla na kishindo cha kikasikika, Miranda akaanguka na kupoteza fahamu.

Mp aliyekuwa getini alisikia kelele ile na ukinya uliofuata akamwachia mwenzake lindo akakimbia kutazama kuna nini, alipoingi alimkuta Miranda chini hana fahamau, akaomba msaada haraka na wengine wakatoka maofisini kuja kumsaidia kwa huduma ya kwanza, hakuna aliyejua ni nini kimeamfanya aanguke. Ni pale mwanajeshi mmoja aliposogelea lile box akabaki kaduwaa, kinywa wazi. Hakutaka kuyaamini macho yake kwa kile yanachokiona. Kichwa cha binadamu, kichwa cha Gwamaka kilikuwa kimetulia ndani ya box lile, hakuongea kitu alitoka nje na kulia sana. Kila aliyeingia ndani ya ofisi hiyo alitoka akilia kwa uchungu.

§§§§§

Brigedia jenerali Kyambassa alikuwa hatulii ofisini, alitoka kona hii ya ofisi na kwenda ile kule, akishika hiki na kuacha kile, kama umemzoea ungeweza kumjua wazi jinsi alivyoshikwa na hasira kwa ndita zilizojipanga katika paji la uso wake, na kufanya kama matuta ya kuwalazimisha madereva kupunguza mwendo barabarani. Hakuwa na amani mwilini wala moyoni, kijasho kililowesha suti yake ya kijeshi yenye rangi ya kijani kibichi, kama haikutosha hata viatu alivyovaa vilionekana kumbana ghafla, akavilegeza gidamu zake na kuendelea kuizungukan ofisi hiyo bila kuchoka, hakuweza kukaa kwani alihisi kiti ni cha moto.

“Hii ni dharau, dharau iliyopita kipimo,” Kyambassa aliongea kwa ukali kuwaambia watu wachache waliokuwamo katika ofisi hiyo. Kwa ujumla hakuna aliyeongea kila mtu kama si kutiririkwa na machozi basi alibaki katumbua macho akitazama lile kasha la mbao safi lililotumwa kwao likiwa na zawadi ya kichwa.

“Afande, kiukweli ni swala linaloumiza sana, sasa kama huyu wamemfanya hivi ni vipi kuhusu Jamil, komandoo wetu, kwa maana tunajua thamani ya komandoo mmoja, sisemi Marehemu Gwamaka hakuwa na thamani ila yeye tayari tumeshampoteza hatuwe zi kuimjadili, lakini vipi huyu aliyebaki ambaye hatuna mawasiliano naye na wala hatujui yuko wapi, pia na vipi wale wanamaji wetu ishirini pamoja na wale Warussia watano?” aliongea kwa uchungu Kanali Hosea Mlawa. Ukimya ukatawala tena.

“Hapa tutajadili lakinin jibu halitapatikana, mi nafikiri sisi kama wapiganaji ambao usalama wa watoto wetu uko mikononi mwetu tuamue jambo moja, tuiongie kijeshi Somalia, tukawatwange hao wanaojiita maharamia tuwachukue ndugu zetu,” aliongea kwa jazba mwanamama pekee aliyekuwa katika jopo hilo la watu wa juu kabisa wa JW.

Brigedia Jenarali Kyambasa, alionekana kujifuta machozi kila wakati, mara hii alikuwa ameketi katika kiti chake cha kazi ambacho mbele yake kilizungukwa na na viti kadhaa vyote vikiwa vimekaliwa na watu waliofura mpaka mashavu yao yakavimba, hakika kama angetokea Msomali hapo angegombaniwa kama mpira wa kona.

“Ukiona mtu mzima analia waziwazi mbele za watu, ujue kuna jambo, mimi ndugu zangu, nimehuzunishwa sana na kitendo hiki, nimekerekwa tangu ndani, ningekuwa na uwezo ningeshusha kombora moja na kuipoteza hiyo nchi katika uso wa dunia,” Kyambassa alizungumza.

Ukimya bado ulikuwa ukichukua nafasi kila wakati kati ya jopo lile kwa maana simanzi ilitawala kuliko maamuzi.

Mjadala uliochukua takribani masaa mawili haukuzaa matunda, ilibidi uhairishwe kwanza ili kila mjumbe akatafakari kuhusu hilo, lakini kwa wakati huo iliazimiwa kichwa cha Gwamaka kikahifadhiwe katika hospitali ya jeshi ya Lugalo na shughuli za mazishi zisiwepo mpaka ufumbuzi utakapopatikana ili mpiganaji huyo mahiri azikwe kishujaa. Swala lilibaki ni kumuokoa Jamil kama bado yuko hai na wengine ishirini na watano waliokuwa wakisafiri na meli hiyo.

Ilibidi Brigedia Jeneral Kyambassa akaonane na mkuu wa majeshi ili kuona wao wawili tu wafanyeje. Bado hata walipokutana mjadala kati ya wawili hao haukuwa na muafaka na ikaonekana wazi kuwa shauri hilo la kuingia katika nchi nyingine kwa nguvu linaweza kuleta shida katika uhusiano wa kimataifa kwani aliyewatenda hayo ni kikundi tu Fulani na maamuzi ya mwisho kikatiba kutangaza swala hilo au kulisaoni ni Rais tu mwenye mamlaka.

“Hapana Kyambassa, najua nia yako lakini tusifike huko, tunahitaji amani na majirani zetu, ni kweli usemavyo kuwa hatuwezi kufanikisha hili kidiplomasia kwa sababu nchi yenyewe haina serikali, kila mtu anaamua anavyotaka, lakini tutumie mbinu nyingine, mi nadhani peleka makomandoo wengine wawili wakamalize hiyo kazi,” alimaliza kuzungumza Jenerali Mubah aliyekuwa mkuu wa majeshi mwaka huo, yeye hakukubaliana na uamuzi wa kuingia kijeshi ila akatoa mbinu mbadala ya kufanya.

Brigedia Jenerali Kyambassa akakubaliana na mkuu wake wa kazi, akampigia saluti na kuondoka ofisini hapoi kurudi ofisini kwake ili kuongea na wale aliowaacha ambao walikuwa wanasubiri jibu kutoka kwa mkuu.

Jopo lilirudi tena mezani chini ya Kyambassa, wakapewa mrejesho wa kikao chake na mkuu, kila mmoja alionekana wazi kutoridhiswha na uamuzi huo lakini waliombwa subira ichukue nafasi, swali likawa gumu, nani aende akashike kazi hiyo katika nchi ya Somalia. Jopo likamteua Komandoo mchanga kabisa Daudi wa Daudi akisaidiana na mwingine Sebeki.

Daudi alikuwa ndiyo kwanza anamalizia mafunzo yake huko Cuba na Sebeki alikuwa tayari nchini akiendelea na majukumu mengine ya kitaifa.

§§§§§

Daudi alipokea barua kutoka kwa mkuu wake wa kikosi akitakiwa kufika Somalia moja kwa moja ili kuifanya kazi hiyo, barua ilimpa maelekezo ya nini kilichotokea na nini anachotakiwa kufanya. Kwa kuwa tayari alikwishakuwa mwana wa jeshi hakuwa na la kukatata bali jibu kwa mkuu wake wa mafunzo hapo Havanna, Cuba lilikuwa ni “Yes, Sir!” na siku iliyofuata aliagwa rasmi na kuondoka Havanna kuelekea Mogadishu kuokoa jahazi.

§§§§§

BANDARI YA ZAMANI-MOGADISHU

“Mimi watu wabishi nawapenda sana, hivi wao hawakuwahi jiuliza kuwa kwa nini wenzao wenye nguvu huko Maghalibi wametelekeza meli zao?” Sharon alikuwa akizungumza katika kikao kidogo na vijana wake ndani nya kijichumba kimoja katika bandari ya zamani ya Mogadishu huko Somalia. Tayari walikwishajua kuwa kuna makomandoo wawili kutoka Tanzania wameingia nchini mwao kwa minajili ya kuokoa wenzao.

“Hii ni vita Sharon,” Shalabah alimwambia Sharon kutoka pale alipokuwa ameketi.

“Kama ni vita basi tutapigana mpaka mwisho, wanamkanyaga nyoka mkia, wanafikiri walivyompiga Idd kule Uganda mpaka leo wana uwezo ule? Wameumia, hapa ndipo watakapofia na kuzikwa,” Sharon alikuwa akiongea huku akishikashika kisu chake kikali alichokichomoa kutoka alani mwake.

“Kwa hiyo mkuu unatuambiaje?” kijana mmoja mwembamba mrefu kana kwamba anakula saruji alisimama na kumuuliza Sharon, mgongoni mwake alikuwa na bunduki kubwa AK 47 na kujizungushia mkanda mrefu wa risasi.

“Hakuna linguine, haina haja ya kuwaacha hai, muwasake mkiwapata muwaue hapohapo wala msiniletete mimi,” Sharon alimaliza na kuwataka vijana hao kutawanyika.

Fasendy alishusha sigara yake kutoka kinywani mwake ilimokuwako kama dakika mbili mfululizo, aliitazama kama imesiha lakini ilikuwa bado inafaa kuendelea kuvutwa, akapiga pafu moja na kuteremsha mkono, akaweka kishungi hicho ndani ya kibompoli maalum kwa kazi hiyo. Akashusha pumzi ndefu na kisha akajimininia glasi moja kubwa iliyojaa maji. Akaendelea kutega windo lake palepale, maana alijua wazi kuwa windo hilo litapita tu tena muda si mrefu sana. Pembeni akiwa na bunduki kubwa ya masafa marefu maalum kwa kudunguli lenye kuingia risasi moja tu, aliendelea kusubiri akiwa juu kabisa ya jengo la ghorofa lilikuwa likitazamana na hoteli ya Somali Hotel, katikati ya mji wa Mogadishu. Fasendy alikuwa akimfuatilia komandoo Sebeki tangu siku aliyoingia pale uwanja wa ndege bila ya yeye kujua.

Sebeki hakujua kama Daudi kafika na wapi yupo alkadhalika kwa Daudi nako ilikuwa hivyohivyo, Fasendy alijua ujio wa Sebeki lakini hakuujua wa Daudi, hivyo alimweka kwenye uangalizi wake kwanza ili ajue mtu huyo atafikia wapi na uwezo alionao katika shughuli hiyo.

Sebeki ye akiwa hana hili wala lile, aliendesha maisha kama raia wa kawaida, akifuatili chinichini kujua ni wapi yalipo maficho ya maharamia hao ili asababishe vurugu ambayo itawaachia historia. Kwa ujumla aliwapania sana. Hii ilikuwa ni mbinu yake anapotaka kuvamia sehemu, kujichanganya na wakaazi na kufanya kila kitu pamoja nao lakini akiwa na wazo moja tu kichwani mwake, kulipa kisasi kabla hawajamuwahi kwa maana hapo alijua wazi kuwa ni lazima mmoja amuwahi mwenzake ili shughuli inoge.

Wakati maharamia wameamua kuwa wakimuona basi ni kumuua tu nay eye alijiseme atakayejipendekeza nayeye atahakikisha anatenganisha mwili na roho. Alikuwa akitembea taratibu kwenye vijia vya hotel hiyo. Muda wote Sebeki alikuwamo katika pembe za hotel hiyo akipata chakula cha mchana pa si na wazo lolote. Alipokwishamaliza, aliondoka na kuelekea katika chumba chake, wageni walikuwa ni wengi sana katika hotel hiyo hivyo kulikuwa na nyendo nyingi za hapa na pale.

Fasendy katika angalia angali zake alimuona Sebeki, kama alivyoelekezwa akaweka sawa bunduki yake akaitazamisha kule kunako lengo lake na kutumbukisa jicho lake katika kiona mbali kilichofungwa juu kidogo ya bunduki hiyo, akajaribu kutafuta shabaha lakini ilikuwa ngumu kwa Sebeki alikuwa akipishana na watu mbalimbali. Dole la shahada la mkono wa kulia la Fasendy lilikuwa tayari katika kifyatulio, likiminya kidogo na kuachia mara kadhaa.

“Shiit!” aling’aka pale alipomuona Sebeki akiingia kwenye mlango Fulani na kupotelea humo. Akaiachia ile bunduki yake na kutoka pale alipolala, akachukua sigala yake nyingine na kuiwasha kabla ya kuanza kuivuta kwa fujo.

“Idara ya usalama Tanzania imeishiwa, mpaka inawatuma hawa, mi ilitegemea kumuona Kamanda Amata hapa, na angekuja yule nakwambieni kweli Mogadishu pangekuwa padogo kama kidonge cha pirton,” Fasendy akamwambia kijana mwingine aliyekuwa nae hapo.

“Kwa nini unasema hivo?” yule kijana akauliza.

“Eh, we acha tu, yule shetani, ana mbinu za kijasusi ni hatari, na sijui kapatwa na nini mpaka simuoni kwenye mkasa mkubwa kama huu,”

MOSCOW – URUSI

Maofisa wa jeshi walikuwa wamekusanyika katika makaburi, wakiwa kwenye ibada maalumu ya mazishi ya kiongozi wa juu wa jeshi hilo ijapokuwa alikuwa amestahafu lakini bado alikuwa na heshima yake kubwa katika jeshi la nchi ya Urusi.

Akiwa katika kumalizia ibada hiyo, mkuu wa jeshi la Urusi Bwana Vladimir Kalachinikov alipenyezewa kijibahasha mahali alipokaa, alipokichuku na kusoma juu kilikuwa kimeandikwa kwa lugha ya kiingereza, Confidencial.

Akiwa anvuta hatua fupifupi akitoka katika eneo hilo la makaburi, Vladimir alikuwa akiifungua bahasha ile huku akihakikisha haionekani na mtu mwingine. Akaanza kuisoma taratibu huku akiendelea na mwendo wake, mlinzi wake alikuwa nyuma kidogo. Colonel Vladmir akasimama ghafla, akatzama saa yake, akashusha mkono chini, akatikisa kichwa kama kuna kitu kilikuwa kinamsumbua kwa ghafla, akaiweka ile bahasha katika mfuko wa koti lake.

Baridi ilikuwa kali sana, theruji iliganda kila mahali, miti, maua, magari, nyumba vyote vilikuwa vyrupe vikipendezesha na hali hiyo hadimu kwa nchi zetu zenye uoto wa kisavanna, hiyo yote ilihashiria kuwa Krismasi imekaribia. Akafika mahali akasimama huku amejishika kiuno, palepale alipo gari yake ikasogea na kusimama mbele yake, akaingia pamoja na mlinzi wake na kumwamuru dereva amfikishe kwa waziri wa ulinzi mara moja.

Mazungumzo yake na mkubwa wake wa kazi ambaye ni waziri wa ulinzi wan chi ya Urusi yalikuwa ni yale yale jinsi ya kuwakomboa wanajeshi wao watano waliokuwa pamoja na wengine wa Tanzania.

“Unajua, Colonel Vladimir, wale jamaa sio wa kuwaongia ovyo kama unavyofikiri, ni wanyama wabaya kuliko wanyama wenyewe,” alizungumza waziri wa Ulinzi akimweleza Colonel Vladimir Kalachinikov.

“Sasa tunafanyaje kiongozi, na unajua hali halisi iliyopo kule ni karibu wiki sasa, watu wetu wanateseka,” alilalamika Vladimir.

“Ok, fanya hivi, chagua mtu mahiri anayeweza kuifanya kazi hii kwa umakini, umtume, mwambie afanye kazi hiyo kwa siri maana akijulikana tu, wale jamaa watafanya kweli,” Waziri wa ulinzi akamaliza hapo. Colonel Vladimir Kalachinikov akasalute na kutoka ofisini hapo.

KAMBI YA JESHI YA SARATOV-URUSI

COLONEL Vladimir Kalachinikov, alikuwa ameketi kitini katika ofisi ndogo anayopenda kuitumia mara kwa mara kama anakuwa na mambo magumu ya kuamua juu ya idara hiyo ya ulinzi. Siku alikuja hapa na ujio wake ulikuwa ghafla hata kwa viongozi wa kambi hiyo ya mambo ya anga na milipuko mikubwa ya jeshi la Urusi inayojulikana kama ‘Eagle Air Force Base au Eagles – 2’.

Alikuwa ameketi kimya akiwa hajui la kufanya, alishika hapa na pale lakini yote hayo yalikuwa ni bure. Baada ya dakika kama kumi hivi, mlango ukafunguliwa na wanajeshi wengie sita wenye vyeo vya juu waliwasili ofisini hapo, wakatoa salute zao na kila mmoja kuchukua kiti chake, wote waliweka kofia zao juu ya meza kwa mtindo wa kupendeza.

“Karibuni sana makamanda, najua mtashangaa sana leo nimewaita mje Saratov badala ya Moscow tuliyoizoea, kuna jambo moja la kuamua kwa pamoja, na hili si jipya ni lile ambalo mnalijua, juu ya ile Manowari ya Tanzania iliyotekwa kule Somalia ikiwa na makobora kumi na mbili ambayo yalikuwa yakija hapa bahari ya Caspian kwa majaribio, ukiachana na hilo, tuna wanajeshi watano wako pale wanashikiliwa na hao Maharamia, sasa kwa sauti yetu moja, tunafanyaje kwenda kuwakomboa watu wetu?” colonel Vladimir alimaliza kuzungumza. Wajumbe wakabaki kimya kwa muda, wakitafakari jambo au mambo Fulani.

“Colonel, mi nafikiri hili swala tulishalizungumza, na tukaona kwa kuwa Tanzania imechukua hatua, basin a tuangalie wanafikia wapi vinginevyo kama watahitaji msaada wetu, ila kwa idara ya usalama Tanzania nawaaamini asilimia 95, wanaweza kazi, labda tungepata ripoti kwanza,” akazungumza mkuu wa jeshi kutoka Tupolev.

“Makamanda, kule hali ni tete sana, komandoo mmoja wa Tanzania amechinjwa, na mwingine hajulikani alipo, ijapokuwa wizara ya ulinzi ya Tanzania imeamua kupeleka wengine wawili, lakini kule ni kule tu,” Colonel Vladimir alitoa majibu kwa kifupi. Baada ya mabishano makali, akasimama mkuu wa kikosi cha wanaanga wa Saratov.

“Mimi sioni haja ya kucheka na hawa watu, watatusumbua mpaka lini? Nchi nying za maghalibi meli zao zimetekwa mpaka sasa wamekaa kimya hakuna jitihada wanazofanya, haya bora wao ni meli za mizigo, sasa hii ya sasa ni ya kijeshi, ina uhusiano mkubwa sana na sisi, hatuna haja ya kucheka nao, tufanye uchunguzi, tuone walipo mi ntatuma ‘tai’wawili tu wanatosha kufagia hao mende wote,” kila mtu katika mkutano huo akacheka baada ya kauli hiyo iliyotoka kwa bwana

Makubaliano yakapitishwa, mchunguzi apelekwe akafanye uchunguzi wa eneo zima, wapi hao jamaa wanajificha na wapi wanafanyia shughuli zao, awape maelekezo kwa vipimo vya ardhini, na baadae wakafanye kazi ya kuwakomboa wenzao. Hilo likapita kwa wajumbe wote. Kikao kikavunjwa na colonel Vladimir akapeleka mapendekezo wizara ya ulinzi ili kuanza mara moja, ijapokuwa hakuwa na uhakika kama litakubaliwa kwani kutuma ndege vita kwenye nchi ya mwenzako kwa sheria za kimataifa ni uvamizi.

MOGADISHU

SEBEKI alikuwa akitoka kuoga, mara tu alipofika katika chumba chake cha kulala akasikia hodi, mlango ukigongwa mara kwa mara, akajiweka tayari, akachukua bastola yake na kuikamata sawia, akauendea mlango na kuufungua, kabla hajamkaribisha aliyegonga akaingia ndani.

“Vipi, mbona unavamia vyumba vya watu?” Sebeki akauliza huku bastola lake likiwa limemtazama mwanadada huyu.

“Usiniue, nina kitu cha kukwambia,” akasema yule msichana.

“Sema haraka, kabla sijabadili mawazo,” Sebeki akamwambia yule dada.

“Ndugu yako, ndugu yako amekamatwa na maharamia, nenda kamsaidie watamuua vibaya,” yule msichana aliongea huku akikatakata maneno.

“Wewe, kama ni maigizo sisi Watanzania ndio tuna chuo cha sanaa hiyo, mi kwetu sina ndugu, na nani aliyekutuma?” Sebeki akamuuliza, akamkamata kwa kono lake moja la kushoto na kumsokomeza bastola mdomoni, “Nafumua ubongo wako, sijaja kucheza huku!” akamalizi kusema na kuitoa ile bastola kinywani mwa yule msichana, akamwacha akitetemeka pale chini. Sebeki aligeuka na kuliendea kabati, yule msichana alitumia nafasi hiyo, alichomoa bastola yake iliyopachikwa juu kabisa mapajani kwa ndani ya nguo, kwa haraka alimlinga Sebeki. Sebeki aliposikia mliowa kiondoa usalama akajua tayari, kumbe alifanya hivyo kwa makusudi mazima, alijirusha upande wa pili wa kitand na ile risasi ikamkosa. Akanyanyuka kama umeme akatuliza guu lake kichwani mwa yule msichana na kumbamizia ukutani, akamnyanyua mzima mzima kwa mikono yake miwili, kifua chake kilichokuwa wazi kilituna na misuri ilidinda kwenye mikono yake, akamrusha yule msichana katika dirisha la kioo na kudondokea nje.

Kelele za alam za magari zilisikika baada ya ule msichana yule kudondoka juu ya gari zilizokuwa maegeshoni. Sebeki akakung’uta mikono yake, na kufungua kabati, akavaa nguo zake haraka haraka na kuchuku bastola zake mbili, akajiandaa kuteremka chini ili aone nini kinaendelea.

Akashuka chini na kuzunguka upande wa pili wa ile hotel, akatazama watu waliokuwa pale wakimsaidia yule msichana aliyedondoka kutoka ghorofa ya tatu, akachukuliwa na kupakiwa kwenye gari moja iliyochoka sana, na wale waliompakia walionekana wazi si wema sana. Sebeki akili ikamcheza, ‘lazima niwafuatilie’ akajisemea, akachomoka pale alipo na kuikimbilia gari yake.

“Nooooooooooo!!!!!!!!!!!!” sauti kali ya mtu ilisikika nyumaya Sebeki umbali kama wa mita mia moja, Sebeki hakuifuatilia kwani hapo palikuwa na mkanganyiko wa watu. Akaingia na kujifungia mlango, mara akasikia kioo cha gari yake kikipigwa kwa ngumi, hakumjua mtu huyo. Sebeki akawasha gari, lo, kumbe maharamia wale walikuwa wametega bomu kwenye injini ya gari ile, na vitendo vyote hivyo Daud aliviona kwani aliwafuatilia toka mbali.

Mlipuko mkubwa ukatokea, anga yote ikawa nyekundu na moshi mzito, ile gari ilinyanyuliwa juu na kugeuzwageuzwa kama kiberiti, ikaanguka na kutua juu ya gari nyingine nazo zikadaka moto, kizaazaa. Kwa kishindo kile, Daudi aliwahi kulala chini, lakini msukumo wa mlipuko ule ukamsukuma na kumbamiza kwenye gari ya jirani, Daud, akajiviringa na kutumbukia kwenye mtaro wa maua na kushuhudia ule moto ukiwaka hewani.

“Kazi imekwisha! Nimeshaingiza pesa,” Fasendy alizungumza na kugeuka akiuacha mlipuko ule ukiendela nyuma yake, akatembea taratibu kuelekea gari iliyoandaliwa kumchukua, akiwa anavuka barabara ndipo akamuona Daud akiwa hajiwezi, anahangaika ndani ya ule mtaro.

“Usipofanya jitihada za kuondoka ndani ya masaa manne nakuua,” Fasendy akamwambia Daud kisha akaingia kwenye gari na kuondoka zake.

§§§§§

Tarumbeta maalum ya maazishi ilimaliza kupulizwa, amri ya kijeshi ikatolewan risasi kadhaa zikapigwa hewani huku wanajeshi wengine wakiwa wamepiga salute kama heshima yao ya mwisho kwa wapiganaji hao Sebeki na Gwamaka ambao walikuwa wakizikwa rasmi katika makaburi ya Kinondoni.

Ilikuwa siku ya huzuni sana kwa familia zao, na wapiganaji wote kwa ujumla, hasira na uchungu zilitawala miongoni mwa wale wenye dhamana. Manyunyu ya mvua yalinyurunyuta na kufanya hali ya hewa ya jiji la Dar es salaam kuwa tulivu kama wakazi wenyewe ambao walikuwa wakifiuatilia habari hiyo ama kwenye Tv au redioni, kila mtu alishikwa na hasira.

Siku hiyo gumzo kwenye vyombo vya habari lilikuwa hilo, wahariri wakaandika kwenye tahariri zao,vipiondi vya kuruhusu watu wapige simu navyo vikawa ni shida, kila aliyepiga alilaumu, na alipendekeza hata kama jeshi basi lipelekwe likafanye kazi hiyo kwa mapana yake.

§§§§§

Brigedia Jenerali Kyambassa alifuta machozi, na kuiangalia jopo lake lote, hakuna aliyekuwa na furaha.

“Tumepoteza askari 1600 na 1600 wengine hatujui walipo, nafikiri mmenielewa kwa lugha hiyo, kwa maana komandoo wetu mmoja ni sawa na battalion moja, yaani askari 800, hawa jamaa yumkini kama si mashetani basi wana mbinu za ajabu sana kwenye mashambulizi yao,” Kyambassa aliongea kwa ukali.

Akiwa katika kikao hicho, mara katibu wake akaingia na moja kwa moja akamwendea, akamnpng’oneza kitu.

“Naombeni mnisamehe kidogo makamanda,” Kyambassa akatoka na yule katibu wake wakaingia ofisi ya pili. Kyambassa akakutana na Miranda, katibu muhtasi wa wizara ya ulinzi.

“Karibu Miranda,” akamkaribisha. Miranda akatoa bahasha moja ya serikali na kumkabidhi. Kyambassa alitetemeka akajua hapo tayari hana kazi na hakuna kitu kingine, akaipokea na kuanza kuifungua taratibu huku mikono yake ikitetemeka.

Kyambassa akashusha pumzi ndefu, akamtazama Miranda usoni, Miranda nae alikuwa kakaza macho kwa mzee huyo aliyechafuka kwa vyeo vya kijeshi.

“Ok, Nimeelewa,” akamwambia Miranda kisha akainuka na kurudi kikaoni. Akawakuta wajumbe wakiwa wanabadilishana mawazo, alipoingia wote wakarejesha ukimya. Kyambassa akaenda palepale alipokuwa kwanza, akajiweka sawa na kuwatazama wajumbe wa kikao.

“Ndugu wajumbe, nimepata taarifa sasa hivi ya kiofisi, kusitisha mara moja operesheni yoyote inayohusiana na utagutwaji au uokozi wa watu wetu huko Somalia, hivyo sina budi kusema kikao hiki hakina haja kuwepo mpaka tutakapopata taarifa nyingine, mission aborted,” Brigedia Jenerali Kyambassa akawaambia wajumbe wake. Kikao kikavunjika na kila mtu akarudi kuendelea na majukumu yake ya kulijenga taifa.

§§§§

GINA binti Komba Zinga Zinga alikuwa ametulia tuli katika ofisi ya AGI investment, ndani ya jengo la JM Mall, ghorofa ya tano. Akiwa anaangalia televisheni, ni kipindi kirefu sana alikuwa ndani ya ofisi hiyo bila boss wake kamanda Amata ambaye mara tu alipoachishwa kazi miezi sita iliyopita alijikita kwenye kilimo huko kwao Lindi. Ni mara chache sana alikuwa akija kutembelea ofisi hiyo, hata yeye Gina alikuwa akija mara chache sana, mara nyingi alikuwa akifanya kazi zake za kiofisi katika kituo cha polisi cha kati kwa kuwa yeye alikuwa ni muajiriwa wa jeshi la polisi.

Simu ya ofisini hapo iliunguruma kwa fujo, Gina akaitazama simu hiyo ambayo ni siku nyingi hakuwahi kuitumia, aliitazama na kuinyakuwa pa si kuotea ni wapi intoka, kaiweka sikioni na kusikiliza.

“Hello, Gina!” iliita sauti ya upande wa pili mara tu Gina alipoiweka simu ile sikioni. Ilikuwa ni sauti ngeni hakuwahi kuisikia kabla.

“Ndio mimi, unasemaje?” Gina akajibu.

“Unaongea na idara ya usalama wa taifa kitengo maalumu kisicho na mipaka, TSA,” ile sauti ilimwambia.

“Nakusikiliza,” Gina akajibu.

“Unatakiwa kufika katika ofisi hii kesho saa mbili asubuhi, asante sana,” ile sauti ikatoa agizo na kukata simu bila kusubiri jib u la ndio au hapana. Gina akatahayari kwani alijiuliza ni vipi watu hao wamejua kuwa yuko ofisini hapo mpaka watumie simu ya ofisi kuweza kumpata. Akaitua simu na kuiweka kwenye kikalio chake kisha akaketi kitini, akaitazama ofisi hiyo ambayo ilikuwa bado haijapata mtu wa kukaa kama boss baada ya Amata kutoka. Ilikuwa ni ofisi maalumu ya kitengo cha usalama lakini ikionesha kuwa inafanya kazi za kijamii kumbe ndani yake kuna kikubwa kinachoendelea.

Ni Kamanda Amata aliyempendekeza Gina kuwa kama katibui muhtasi ndani ya ofisi hiyo miaka kadhaa nyuma pindi tu kilipoanzishwa kitengo hicho. Gina alikuwa ni polisi (WP), ambaye kwa kipindi cha miaka mitatu alikuwa akisomea sheria katika chuo kikuu cha Dar es salaam.

Gina alishtushwa na wito huo, ‘Kwa nini asipige Madam S au mtu mwingine ninayemfahamu?’ akajiuliza. Kichwani mwake alihisi kuchanganyikiwa, hakujua kama ni wito wa kweli au ni mtego kwake, maana ni siku nyingia hakuingia kwenye kashkash za namna hiyo. Akachukua simu yake ya mkononi na kuimpigia Madam S.

“Yes madam, shikamoo!” alimsabahi.

“Marhaba Gina, mbona kimya sana mwanangu, upo?” madam aliuliza katika simu.

“Nipo mama niende wapi?” Gina alisema, akatulia kidogo na kupisha mazungumzo ya hapa na pale na Madam S huku moyoni akiwa na shaka kumuuliza juu ya ile simu lakini mwishowe akaamua kuuliza.

“Aaaa Gina, we fanya kama simu hiyo ilivyokuelekeza, usiwe na wasiwasi,” Madam alimtoa hofu binti huyo na simu ikakatika. Gina akpigwa na butwaa, ‘kuna nini?’ alijiuliza.

SIKU ILIYOFUATA saa 2 asubuhi

OFISI YA T.S.A

MADAM S, au H.O.T (Head Of TSA) alikuwa na shughuli maalumu siku hiyo katika ofisi ya TSA, akiwa nadhifu katika suti yake ya rangi ya udongo, nywele alizotengeneza katika saluni kubwa ya kisasa, alikuwa amesimama mbela ya meza yake kubwa kabisa ya ofisi, mezani hapo kukiwa na kikasha kimoja cheusi kimetulia. Pembeni ya Madam S kulikuwako Chiba, Dr Jasmine, Scoba na Gina. Dr Jasmin alikuwa amesimama akitazamana na Madam S. ukimya ulitawala kati ya wote.

“Dr Jasmine, baada ya kufanya kazi kwa kipindi kirefu na ofisi ya TSA, leo hii ofisi hii, kwa mamlaka iliyopewa na ofisi ya Rais, inakuteua kuwa mmoja wa wanaunda idara hii nyeti, ukiwa kama daktari bila kupoteza taaluma yako, sasa utatambulika kwa utambulisho maalum, TSA 3, utasaidia ofisi hii kwa kila jambo linalohusisha utabibu,” Madam S aliongea maneno hayo huku akimtazama Dr Jasmine aliyekuwa kasimama mbele yake kiukakamavu. Madam S Litoa baeji maalum ya rangi ya dhahabu, yenye nembo ya serikali na chini yake ikipambwa kwa maandishi yenye nakshi ya kuvutia, Tanzania Secrety Agency 04. Madam S hakuishia hapo, alikinyanyua kile kikasha cheusi pale juu ya meza na kukifungua.

“Na hizi ndio zana zako za kazi tangu leo, hutakiwi kuiacha nyuma, unatakiwa uibebe kila uendapo, kwa utii na uangalifu ili itumike pale tu inapobidi,” madam S akamkabidhi kile kikasha, ndani yake kulikuwa na bastola moja ya kisasa na risasi nane, pembeni yake kulikuwa na kiwambo cha sauti kwa ajili ya bastola hiyo. Dr Jasmin akakipokea kikasha hicho na kurudi alipokuwa mwanzo. Dr Jasmine kabla ya kuwa daktari alikuwa ni muajiriwa kati jeshi la kujenga taifa, baada ya kuacha kazi hiyo akajikita katika udaktari zaidi chini ya wizara ya afya akiwa ni muajiriwa, Kamanda Amata alipenda sana kumtumia daktari huyu katika mambo yake hasa yakihitaji taaluma ya kiganga, alimuamini kwa kuwa alikuwa msiri, jasiri na asiye na woga, Madam S alipopewa pendekezo la kumtumia mwanadada huyo hakuwa na kipingamizi na Kamanda, alimruhusu aendelee kumtumia.

“Gina binti Komba Zinga Zinga, baada ya kufanya kazi kwa kipindi kirefu na ofisi ya TSA, leo hii ofisi hii, kwa mamlaka iliyopewa na ofisi ya Rais, inakuteua kuwa mmoja wa wanaounda idara hii nyeti, ukiwa ni muajiriwa wa jeshi la polisi na ofisi hii inalitambua na kuliheshimu hilo, sasa utatambulika kwa utambulisho maalum, TSA 5, utasaidia ofisi hii kwa kila jambo utakalotakiwa kufanya, kuanzia sasa nafasi yako katika jeshi la polisi haitakuwepo tena kwa mujibu wa sheria iliyowekwa juu ya kuunda na kuteua wadau wa ofisi hii,” Madam S vilevile, kama alivyofanya kwa Jasmine alimkabidhi beji maalum Gina iliyoandikwa Tanzania Secret Agency 05. Kisha akamkabidhi vifaa vile vile kama alivyofanya kwa Dr Jasmine.

Baada ya shughuli hiyo walipiga picha ya pamoja, Madam S, Chiba TSA 02 idara ya teknohama, Scoba TSA 03 idara ya usafirishaji na uokoaji, Dr Jasmin TSA 04 idara ya afya, Gina TSA 05 asiye na idara maalum. Timu ilikuwa imekamilika, lakini bado ofisi hiyo ilikuwa haijapata mtu wa kushika beji ya TSA 01 ambayo mwanzoni ilikuwa na Kamanda Amata.

Tafrija fupi ndani ya idara hiyo nyeti ilikuwa ikiendelea, mara mlio wa chombo cha mawasiliano ukasikika, Madam S akabofya kitufe Fulani na screen maalum iliyo katika ukuta wa ofisi hiyo ikapata uhai, picha iliyoonekana hapo haikuwa nyingine ni ya waziri wa ulinzi.

“Ndiyo mheshimiwa,” Madam S aliitika.

“Nakuhitaji ofisini kwangu mara moja, bila kuchekewa,” Waziri wa ulinzi alimwambia Madam S kupitia chombo kile.

§§§§

“Madam S, nimekuita mara moja kuna dharula ambayo tunahitaji ofisi yako iweze kutusaidia,” Waziri wa ulinzi alikuwa akimwambia maneno hayo Madam S aliyekuwa ameketi kitini, akisikiliza neno moja baada ya jingine. Mheshimiwa waziri akaendelea, “Manowari yetu kubwa Kirov Class, imetekwa Somalia na maharamia, leo ni wiki ya tatu, tumepelea makomandoo lakini wawili wameuawa kikatili na wawili hatujui walipoa, ndani ya manowari hiyo kulikuwa na wanajeshi 25 Watanzania isihirini na Warusi watano pamoja na makombora makubwa kumi na mawili, tunahitaji ufumbuzi wa jambo hili, haraka iwezekanavyo”.

Madam S aliendelea kumtazama waziri wa Ulinzi hata baada ya kumaliza kuongea, alitamani kumuuliza jambo lakini aliamua kuacha.

“Sawa nimekusikia, lakini unajua wazi kuwa ofisi yangu imepungukiwa tena imepungukiwa nguvu kubwa sana, unafikiri nitawezaje kulifanya hili kwa sasa? Kama mmetuma makomandoo na wawili wameuawa, we unaionaje hiyo kazi?” madam S akauliza.

“Ni kazi ngumu inayohitaji umakini sana,” akajibu waziri.

“Na unafikiri mtu makini ni nani wa kuweza kuikamilisha kazi hiyo?” Madam akauliza. Waziri wa ulinzi akamkazia macho Madam, akamtazama kwa hasira, maana alielewa kile anachokizungumza, kabla hajaongea kitu Madam S alikuwa amekwishanyanyuka na kutoka kwenye ofisi ile. Kichwa kilizunguka, hakujua nini cha kufanya, ugumu wa kazi aliyopewa na serikali aliuona ukimwelemea waziwazi, akitazama kwenye jopo lake hakuna amtu wa makabiliano ya ana kwa ana na mwenye wepesi na akili za haraka kama Kamanda Amata ambaye sasa hayupo kazini.

Alirudi ofisini akawakuta vijana wake bado wanagalipo wakiendelea na viburudisho vilivyo hapo. Akawaita wote mbele ya meza yake na kuwaketisha.

Kabla hajaongea kitu alijiinamia kwanza kwa dakika kadhaa akifikiria jambo.

“Tuna kazi ya kufanya Somalia, kuirudisha manowari iliyotekwa na wanajeshi waliopotea,” madam aliwaambia, wote wakatazamana, na minong’ono ya hapa na pale ikatawala.

“Samahani Madam, hapa katika hili tusifanye masihara hata kidogo, hii kazi ni ngumu sana na kiukweli bila Kamanda Amata tumefeli,” Gina alieleza na kuungwa mkono na wote waliopo katika kikao hicho.

“Kumbukeni Kamanda hayupo kazini, hivyo tunapoteza muda sana kumzungumzia kuliko kujipanga,” Madam S aliwaeleza na kuwaacha hapo yeye akatoka nje ya ofisi.

“….Siwezi kufanya kazi bila Kamanda Amata, we mwenyewe unajua uzito wa kazi,” ilikuwa sauti ya Madam S alipokuwa akiongea kwa simu, hakuna aliyejua ni nani anayebishana nae humo simuni.

Baada ya kama dakika kumi na tano hivi, Madam S alirudi ofisini akiwa katika hali tofauti na mwanzo, akaketi kitini. Akavuta simu yake na kuipiga namba Fulani kisha, akatulia kusikiliza.

“Scoba, chukua helkopta, sasa hivi kamlete Kamanda Amata, Gina atakuongoza anajua ni wapi alipo, nawasubiri hapa,” Madam alimaliza. Scoba na Gina wakachomoka, na kuingia garini, safari ilikuwa ni katika kituo cha polisi Oyserbay ambapo helkopta yao ya ofisi ilikuwa anaegeshwa hapo, baada ya kusainiana na ofisa anayehusika, Scoba na Gina walioondoka.

ITAENDELEA

Hujuma Sehemu ya Pili

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment