Wakala wa Giza Sehemu ya Pili
KIJASUSI

Ep 02: Wakala wa Giza

SIMULIZI Wakala wa Giza
Wakala wa Giza Sehemu ya Pili

IMEANDIKWA NA: HASSAN O MAMBOSASA

*********************************************************************************

Simulizi: Wakala Wa Giza

Sehemu ya Pili (2)

Phina aliitikia kwa kutikisa kichwa akiafukiana na kauli ya Dk Hilary.

          "Sasa basi unaweza ukawasaidia shida yao Phina" Dk Hilary aliongea kisha akawatazama Norbert na Moses akiwaashiria waongee.



           "Phina una uhakika kabisa umemuona huyo mwanamke vizuri?" Norbert aliuliza.



           "ndiyo" Phina alijibu.

          "ukiweza kumuona kwa mara nyingine utamkumbuka?" Norbert aliuliza tena.



          "Ndiyo nitamkumbuka" Phina alijibu huku akiinama chini kutokana na kutazanwa na macho ya Norbert yasiyokuwa na hata chembe ya mzaha.



       "vizuri, Dokta naomba penseli na katarasi nyeupe" Norbert alimuambia Dk Hilary ambaye alifungua faili lililopo mezani akampatia karatasi kisha akafungua mtoto wa meza akatoa penseli akampatia.



       "taja sifa zake jinsi alivyo" Norbert alimuambia Phina huku akiwa ameshika kalamu ya risasi na karatasi ikiwa mezani, Phina alianza kutaja sifa za huyo mwanamke hadi akamaliza na Norbert alitumia muda huo kumchora huyo mhusika kuendana na sifa anazotajiwa. Baada ya dakika takribani tano mchoro wa sura ya mwanamke ilikuwa ipo kwenye karatasi aliyokuwa anaichora Norbert, Norbert alimuonesha Phina ile karatasi huku akimuuliza, " anafanana na huyu?"



  Mshtuko wa ghafla ulimpata Phina baada ya kuona mchoro huo uliochorwa na Norbert, aliishia kutikiza kichwa kukubali bila hata kuulizwa suala linalimpasa akubali kwa ishara. Aliitazama tena ile karatasi iliyobeba mchoro wenye kufanana kwa kila kitu na huyo mhusika aliyemtaja, alikubali tena kwa kutikisa kichwa bila hata kuulizwa kitu kitakachomfanya akubali.



         "Ndiye huyu?" Norbert aliuliza.



        "Ndi...ndiyo yeye" Phina alikubali huku akibabaika kutokana na taaluma ya juu ya uchoraji aliyonayo Norbert kiasi cha kuchora sura ya mtu alipotajiwa sifa zake, ilikuwa ni jambo la kawaida kwa wapelelezi wa daraja la kwanza wa shirika la upelelezi la Afrika mashariki kuwa na taaluma hiyo kwani wamefundishwa kila taaluma ya wanausalama wa kawaida na wana ujuzi wa vitengo vyote  vya usalama.



  Norbert alichukua ile karatasi akamuonesha Moses ambaye naye alibaki na bumbuwazi akionekana kutoamini kile alichokiona, ilikuwa ni sura ambayo hakutarajia kuiona muda huo kwenye tukio kama hilo na sasa ameiona sura ya mwanamke yule mrembo na mwenye sura ya upole.



         "Damn!" Moses alisema kwa hasira kisha akamtazama Phina akasema, "usiondoke hapa utaondoka na sisi ikiwa umemuona huyo mtu kama ni muuaji kweli jua maisha yako yapo hatarini".



   Phina alibaki akiwa ameduwaa kabisa asijue la kufanya kwani hakuelewa walikuwa wana wadhifa gani, aliitikia kwa kichwa tu kwani aliona hawakuwa wa binadamu wa kawaida kiasi cha kumchora mtu ambaye hajabahatika kumuona akifanya tukio kwa kutumia ushahidi wa sifa na muonekano wake.



        "Dokta huyu hakikisha anapewa likizo ya muda mrefu na uongozi wa hospitali nitaongea na mganga mkuu" Moses aliongea kisha akasimama akapeana mkono na Dk Hilary halafu akaongea, " dada tufuate".



 Kwa pamoja waliondoka hospitalini hapo ili kulinda usalama wa Phina huku wakijua wapo peke yao walioona wakati wanaondoka nae, kumbe kulikuwa kuna kibaraka mmoja aliyeshuhudia ujio wao na hadi wakiwa ofisini kwa Dk Hilary. Laiti wangelijua wangelimuweka kiti moto kibaraka huyo wangepatsma mengi huyo lakini hawakujua juu ya hilo, waliondoka naye na muda huohuo kibaraka akafanya kazi yake iliyomleta.

Muda ambao Moses na Norbert wanaingia katika hospitali ya Taifa ndiyo muda ambao Leopard Queen na Panther asiyejua kuongea kiswahili vizuri walikuwa wakiingia barabara ya Umoja wa mataifa baada ya kumaliza kutekeleza kazi waliyokuwa wameazimia kuitekeleza katika hospitali hiyo. Walikuwa wamo ndani ya gari aina ya toyota Altezza nyeusi ambayo ndiyo ilikuwa ikiwafuatilia kina Norbert kabla hawajaingia chaka baada ya kupigwa chenga na Moses, furaha ilikuwa imewatawala na kupelekea kusahau kuwa walikuwa na ushahidi waliouacha huko nyuma ambao ingekuwa ni hatari sana kwao.



        "Baby nimekumbuka kitu, inabidi tumpigie Japhet aibe ripoti yote isije ikatutia matatani" Leopard Queen alimuambia Panther huku akimchezea shingoni kwa mikono yake laini, Panther alikuwa yupo makini katika kushika usukani wa gari na mwili ulianza kumsisimka baada ya kufanyiwa hivyo.



         "Oooh its true Mrembo call him" Panther aliongea na muda huo akakata kona kuingia kushoto baada ya kuimaliza barabara ya Umoja wa mataifa akaingia barabara ya Ally Hassan Mwinyi, Leopard Queen alipiga simu akatoa maelezo kwa Japhet ambaye ndiye yule muuguzi wa kiume aliyeingia ofisini kwa Dk Hilary  bila hodi pia akamkuta Norbert na Moses ofisini humo. Taarifa za uwepo wa Norbert na Moses ofisini kwa Dk Hilary pia kuitwa muuguzi aliyemuona Leopard Queen nazo ilifika kwa Leopard Queen kupitia huyo kibaraka, ilikuwa ni taarifa aliyoiona ya kawaida sana kwani hakuona uhatari wowote katika taarifa hiyo.



           "baby Norbert na Moses wapo ofisini kwa daktari aliyekuwa anawatibu wale soldiers, nesi aliyeniona kaitwa" Leopard Queen alimuambia Panther baada ya kukata simu, taarifa hiyo ilimfanya Panther acheke sana kwa kuwaona kina Norbert wajinga sana.



            "They are insane, I think they are after Doctor's report on soldiers' bodies before they died. Ha! Ha! Ha! Ha! Ha! They are lost( Wao ni wendawazimu, niafikiri wanafuatilia ripoti ya Daktari katika miili ya wanajeshi kabla hawajafa. Ha! Ha! Ha! Ha! Ha! Wamepotea)" Panther aliongea huku akicheka na kusababisha Leopard Queen naye acheke kwa nguvu kutokana na jambo ambalo aliona ni ujinga kulifanya.



             "Ngoja Japhet aibe ripoti watajua pengine pa kuanzia, wajinga" Leopard Queen aliongea  huku akicheka.



            "Ha! Ha! Ha! Ha! Fools( Ha! Ha! Ha! Ha! Wajinga) watajuta" Panther aliongea kisha akasimamisha gari akaegesha kwenye kituo cha daladala kilichopo na mwanzo wa barabara ya Kenyetta, Leopard Queen alimbusu mdomoni Panther kisha  akashuka akaelekea kwenye kutio cha daladala cha upande wa pili wa barabara. Panther aliondoa eneo hilo kwa kasi sana baada ya kuhakikisha Leopard Queen amepanda daladala tayari.

Majira ya saa tisa na nusu tayari Norbert alikuwa ameegesha gari eneo la pembeni ya barabara ya Sokoine lilpo jirani na bandari ndogo ya boti, alisubiri hapo kwa muda wa mfupi na hatimaye Josephine akaonekana akitoka nje akiwa anatembea kwa madaha sana kutokana na viatu alivyovivaa miguuni . Josephine hakuwa amemuona Norbet na alianza kutembea kuelekea kwenye kituo kikuu cha daladala Posta akapande daladala ili aondoke, aliipita gari ya Norbert hadi pale Norbert alipopiga honi ndiyo aliiona gari yake akaifuata hadi ilipo akasimama jirani na mlango wa dereva



          "ni siku nyingine tena" Norbert alimuambia Josephine ambaye aliishia kutabasamu baada ya kumuona Norbert kwa mara nyingine.



           "Norbert niambie" Josephine aliongea huku akitabasamu.



           "safi, naona promise umeisahau tayari" Norbert aliongea huku akiachia tabasamu.



           " Yaani acha tu  mambo mengi mine yaani hadi kichwa nahisi kinaelekea kupasuka kwa kuzidiwa na haya majukumu" Josephine aliongea akikwepesha macho yasitazamane na Norbert.



            "Kawaida hayo ni majukumu pigana mtoto wa kike" Norbert aliongea.



            "akhaa! Yamezidi bora niolewe tu nipumzike" Josephine aliongea huku akiegemea gari ya Norbert.



            "Kakuambia nani kuolewa kuna kupumzika si ndiyo kuna kwata za saresare kabisa" Norbert aliongea huku akimkonyeza Josephine na kusababisha kicheko cha nguvu kimtoke Josephine.



             "Afuu wewe una maneno kama nini" Josephine  huku akiwa bado anacheka.



             "tuondoke basi" Norbert alimuambia Josphine ambaye alizunguka upande wa pili kwenye kiti cha pembeni ya dereva akafungua mlango akaingia, Norbert aliweka gia akaliingiza gari barabarani kisha akaelekea barabara ya Sokoine.



     Foleni kubwa ya magari waliikuta kwenye mzunguko maarufu wa magari unaoitwa Clock tower ambao mara nyingi huwa na foleni sana majira ya jioni kutokana na askari wa barabarani anayezuia magari katika makutano ya barabara ya Kariakoo gerezani, hiyo ilikuwa ni nafasi nyingine kwa Norbert kutimiza kile ambacho hakukitimiza zaidi tu ya kupewa ahadi na Josphine. Walikuwa wapo kwenye maongezi ya kawaida lakini urefu wa foleni hiyo ulimfanya Norbert abadili maongozi, ulikuwa ni muda  muafaka sana kwake ambao alikuwa akiungoja kwa hamu sana.



     Nafasi nyingine kwake ambayo hakupaswa kuitumia vibaya na ilimbidi aitumie vizuri ili aweze kupata kile alichokuwa anakihitaji, kwa macho yaie mawili alimtazama Josephine aliyekuwa akitazama nje kisha akanyanyua mkono na kiganja chake kikatua juu ya paja la Josephine.



    Mguso wa kiganja chake kwenye paja ulisababisha  Josephine ageuke kukitazama kiganja cha Norbert kisha akainua macho juu kumtazama Norbert, macho ya Josephinee yalikutana na macho ya Norbert ambayo yalikuwa ysmeshazungumza kitu ingawa kwake ilikuwa ngumu sana kukiri kuwa ameelewa lugha ya macho ya Norbert kutokana na kutotaka kuonekana mrahisi.



 Lugha ya macho ya Norbert ilipozidi kumsihi atoe maana Josephine aligeuka pembeni kutokana na aibu, alirudisha macho chini aliutazama mkono wa Norbert uliokuwa pajani kisha akashusha pumzi akamuangalia Norbert usoni akajiandaa kutamka neno.







          "Norbert" Josephine alifungua kinywa chake akiwa anashindwa kuyatuliza macho katika uso wa Norbert, aliita jina la Norbert kisha akashindwa kustahimili kutazamana na macho ya huyo anayemuita.



Norbert naye alinyanyua nyusi moja akiashiria yupo tayari kusikiliza huo wito wa Josephine, kimya kilipozidi na hakuambiwa chochote juu ya wito alianza kuvitanua vidole vyake na kuvibana juu ya paja la Josephine akasababisha mwenye kiungo hiko amuangalie tena usoni akiwa na macho malegevu kuliko ilivyokuwa hapo awali.



             "Norbert" Josphine alitamka tena huku akizidi kulegeza macho huku pumzi akiachia kwa nguvu, wito wake wa mara ya pili ulibidi uitikiwe kwa sauti na Norbert badala ya kuinua nyusi kama alivyofanya awali huku kiganja chake kikiendelea kufanya utafiti usio rasmi juu ya paja la Josephine



             "sema bibie" Norbert aliitika huku akimtazama Josephine usoni ambaye alishindwa kustahimili kutazamwa huko akaangalia pembeni.



             "aaah hamna" Josephine alikosa cha kusema baada ya kumuita Norbert na pumzi zake zilianza kumuenda kwa nguvu ya mithili ya mtu aliyekimbia umbali mrefu, macho yalizidi kulegea na mkono wa Norbert muda tayari ulianza kusafiri safari isiyo rasmi kwa mwendo wa taratibu  zaidi hata wa mwendo wa msafara wa harusi.



 Kusafiri kwa mkono huo kuleweka vituo viwili katika mwili wa Josephine ambao ulikuwa na ulaini usiokuwa wa kawaida, kituo cha kwanza kabisa kilikuwa ni kwenye kiuno kilichobeba miguu ya mwanadada huyo chenye ulaini usio wa kawaida, mkono huo ulianza kazi ya kutalii hapo kwenye kiuno kwa kufanya kazi mithili ya kukamua jipu. Mkono mwingine wa Norbert uligusa sehemu ya jirani ya redio ya gari ukawasha kiyoyozi kisha ukasogea  jirani na mlango wa dereva ukavuta vitufe viwili vilivyosababisha vioo vya giza vipande juu taratibu sana.



 Josephine hakuwa amelitambua hilo alibaki amefumba macho kwa hisia huku akizidi kupungua nguvu za mwili wake na hatimaye akaegemea upande aliiopo Norbert, alikutana na bega la Norbert ambalo aliliegemea kisha mdomo wake ukagusa shingo ya Mwanaume huyo ukiambatana na muhemo wa pumzi zilizoonesha kutojiweza baada ya kufanyiwa ukorofi na mkono wa kiume.



  Msisimko wa ajabu ulitoka shingoni mwa Norbert akajikuta  akiachia mkono kule kiunoni lakini Josephine alimzuia asiuachie kutokana na  ladha aliyokuwa akiipata baada ya mkono huo kuwepo katika kiuno chake ukifanya utalii. Hakutaka kubishana na Josephine aliuacha mkono huo ufanye kazi yake iliyokuwa awali huku mkono mwingine ukikishika kidevu cha Josephine na kumfanya atazamane uso kwa uso na Norbert huku macho yake yakionekana ni  mtu aliyezidiwa kilevi kisichonyweka mdomoni mwa mwanadamu.



 Alitazamana na Norbert kwa shida sana na hatimaye akawa anataka kutazama pembeni lakini Norbert alimuwahi kwa kudaka papi za midomo yake juu ya midomo ya Josephine kwa muda  kisha akaachia akamtazama, Josephine alijikuta akileta mdomo wake tena baada ya Norbert kuacha kumpiga busu hilo ambalo ni maaarufu sana kutumiwa na wafaransa. Alipokelewa mdomo wake huo na hapo shughuli ya kubadilishana shurubati ya mdomoni ikaanza kwa taratibu  na hatimaye ikakolea hata wakajisahau kama wapo barabarani, mikono ya Norbert muda huo tayari ilikuwa ipo kifuani ikifanya utalii mwingine uliozidi kumletea wazimu usio rasmi katika mwili wa Josephine kusababisha atoe miguno hafifu wakati kinywa chake kikiwa kimekutana na kinywa cha Norbert.



Habari ya uwepo wao barabarani ilikuwa imeshahaulika kabisa na walijihisi wapo kwenye ulimwengu wao wa peke yao tu, magari tayari yalishaanza  kutembea  lakini wao waliendelea kuzama ndani ya dimbwi lenye kina kirefu lisilo hata na kimiminika chochote  ingawa lilikuwa linamfanya mtu yoyote asiweze kufanya kitu kingine cha kawaida.



 Walikuwa wamezama kwenye dimbwi la huba ambalo lilikuwa ni kero kwa wengine  baada ya gari hilo kutosogea. Walikuja kushtuliwa na kugongwa kwa kioo ndipo Norbert akaangalia mbele kwa jicho upande akimuacha Josephine akiwa anaendelea kuburudika na shurubati iliyomo kinywani mwake.



  Macho ya Norbert kwa mbele yalishuhudia magari yakiwa yapo umbali wa mita takribani kumi na ikamlazimu kuweka gia kwani hakuwa amelizima, aliutoa mdomo wake mdomoni mwa Josephine kisha akakata kona ya haraka akageuza gari akawa anaelekea mjini huku mkono wake mmoja ukirudi katika mwili Josephine ambaye alikuwa amejiegemeza begani kwake. Aliuvuka mzunguka wa Clock tower kisha akaendelea mbele akaingia kushoto katika barabara ipitayo katika mtaa wa Aggrey, alienda na barabara hiyo hadi alipofika katika makutano ya mtaa wa Jamhurii na mtaa wa Aggrey.



 Hapo aliegesha gari  jirani na hoteli ya New avon na alishuka kwa harska kisha akaenda kumshusha na Josephine ambaye alishuka kwa uvivu mkubwa na aliposhuka tu alimuegemea  kifuani mwake, mkono wa Norbert mmoja ulimshika Josephine kiunoni na mkono mwingine ulishika funguo ambayo aliminya kitufe cha kufunga milango kwenye gari na kupelekea taa za pembeni za gari ziwake.



 Wote kwa pamoja waliingia hadi mapokezi wakakutana na msichana ambaye hakuwapokea kwa uchangamfu sana na alikuwa akimtazama Norbert kwa jicho baya sana, Norbert alichukua chumba hotelini hapo kisha akapanda  ghorofani na Josphine kilipo chumba alichochukua ambacho kipo ghorofa ya pili ya hoteli hiyo.

Upande mwingine Moses alikuwa yupo katika nyumba ya shirika la EASA yenye kutumika kama makazi maalum kwa wapelelezi wa EASA(East Africa Security Agency), alikuwa yumo ndani ya chumba cha chini ya ardhi cha nyumba hiyo ambacho hutumiwa kwa kazi maalum. Mbele yake kulikuwa kuna viti viwili vya mateso vilivyokuwa vimefungwa watu wenye mavazi maalum ya Special force wa jeshi la polisi, pembeni yake kulikuwa kuna meza iliyofunikwa kitambaa cheupe ikionekana ilikuwa imebeba kitu ambacho hakikutakiwa kuonekana kabisa kwa watu waliofungwa kwenye hivyo viti.



Moses alikuwa akiwatazama watu wale mmoja baada ya mmoja kisha akawasogelea akiwa na tabasamu pana usoni mwake, aliwashika kila mmoja shavu kama watoto wa kike na kusababisha atukanwe matusi mazito sana mengine yaliwahusu wazazi wake. Matusi hayo yalimfanya atabasamu kisha akasogeza meza iliyofunikwa mbele yao akaifungua tararibu mithili ya mtu anayefungua meza yenye chakula kulichoandaliwa kwasababu maalum, vifaa mbalimbali vya mateso vilionekana kwenye meza hiyo ambavyo hutumiwa kutesa watuhumiwa wakubwa wakiwa wapo chini ya ulinzi.



           "Matusi yenu kwenu ni kama wimbo uburudisho ambao muda si mrefu utakuwa wa huzuni kwenu" Moses alipngea huku akivaa mipira ya kitabibu iloyopo kwenye meza hiyo kisha akauliza, "ni nani aliyewatuma?".



 Swali lake hilo halikujibiwa na badala yake alitukanwa matusi mazito  sana na wale mateka wake, matusi hayo yakimfanya atabasamu kwa mara nyingine kisha akachukua kifaa kinachofanana na koleo la kukatia nyaya ingawa kilikuwa kina makali zaidi. Alimuendea mmojawapo aliyekuwa jeuri zaidi akabana shati alilolivaa akavuta hadi likachanika kisha amtazama kwa tabasamu, jeuri ya mtu huyo wa Special force ilionekana kwani alirusha mate ambayo yalimpata Moses kwenye nguo zake kisha akaachia matusi mfululizo.



Moses aliposikia matusi hayo alitabasamu zaidi kisha akachukua lile koleo akaanza kufinya taratibu ngozi ya mtu huyo kuanzia shingoni hadi kifuani akatoa vipande vya ngozi , damu ilianza kumtoka yule akari aliyejifanya jeuri na maumivu yakafuata lakini hakuthubutu kunyanyua mdomo na ndiyo kwanza alizidi kutukana matusi ambayo kwa muda huo yalikuwa ni kama wimbo kwa Moses.



         "muda wako wa kuwa mnyonge umefika sasa ngoja uwe mnyonge" Moses aliongea kisha akaacha kumbana na koleo akarudi kwenye meza yenye vifaa vya mateso akachukua mkebe mpana uliokuwa umefungwa akaja nao hadi mbele ya askari huyo aliyejifanya mjeuri sana.



 Aliufungua mkebe huo na ndani ukaonekana unga mwingi mwekundu sana ambao hakuna kiumbe angethubutu kuweka pua zake karibu na unga huo pasipo kumletea madhara, unga wa pilipili ambao hutumiwa sana na wahindi au kwa wauza maembe ndiyo ulikuwa mbele yake.



 Moses alimuonesha unga huo yule askari kisha akamsogelea askari mwingine wa pembeni akampiga karate ya  kisogoni akazirai kisha akasema, "hupaswi kusikia mwenzako kajibu nini". Alimfuata yule askari wa kwanza aliyemkata shingoni mwake akachukua ule unga akaanza kuumwaga taratibu kwenye vidonda vyake huku akitabasamu, makelele ya maumivu kutoka kwa askari hakuyajali hata kidogo ndiyo kwanza alizidi kutabasamu huku akiendelea kimimina pilipili hiyo kifuani akitokea shingoni.



      "nani aliyekutuma?" Moses aliuliza tena huku akitabasamu akiitazama pilipili iliyobaki ndani ya mkebe, askari alikaa kimya huku akisikiliza maumivu hali iliyomfanya  Moses amuone ni jeuri na akarudi kwenye meza ya mateso akauweka mkebe na koleo la awali akachukua koleo jingine jembamba zaidi akaja nalo hadi osle alipo askari huyo.



       "Huwa siulizi swali mara tatu nitaendelea mpaka ujibu hilo swali nililokuuliza" Moses alisema kisha akalishika koleo alilikuja nalo kwa nguvu halafu akamminya askari sehemu ya  mwisho wa taya hadi akafungua mdomo wake bila kupenda, aliliingiza koleo hilo mdomoni akabana jino moja kisha akaling'oa akamuacha askari huyo akiendelea kuugulia maumivu.



Moses hakusitisha zoezi lake aliendelea kumng'oa meno  mengne hadi ya mbele yakaisha kabisa lakini askari huyo hakufungua mdomo wake kuongea chochote na ndiyo kwanza jeuri ilizidi akajaribu kumtemea mate yenye damu Moses. Kitendo kikimfanya Mosea ang'oe hadi meno yaliyofuata na yakabaki magego tu kwa yule askari na bado alijifanya kichwa ngumu hakutaka kunyanyua mdomo wake kuongea chochote.



       "Sasa nimeharibu showroom  yote ya mdomoni tuone atakupenda bibie gani na uwazi huo kama ukuta uliovunjwa" Moses aliongea kisha akarudi kwenye meza yenye vifaa vya mateso akachukua mkebe wenye  unga wa pilipili, alirudi akamsogelea yule askari akamfungua mdomo kinguvu na akauinamusha mkebe huo ili kumlisha unga huo mdomoni.



Askari huyo alionesha uso wa huruma akawa anatikisa kichwa kukataa asilishwe unga huo ambao ungeenda kwenye vidonda vyake, Moses alisitisha zoezi lake kisha akamtazama akasema "una dakika mbili za kuongea au  niendelee na kazi nyingine".

Askari huyo mapigo ya moyo hadi muda huo yalikuwa juu kwa kuhofia pilipili ambayo angelishwa kinywani mwake na Moses, ujanja tayari ulikuwa umeishia kwenye mfuko wa nyuma wa suruali yake na hakuwa na ubavu tena wa kuleta jeuri kwa kuhofia kulishwa pilipili ilihali ana vidonda mdomoni mwake vya kung’olewa meno bila ganzi. Alifunguka kwa kila kitu juu ya aliyemtuma hadi akamaliza jinsi mpango mzima ulivyokuwa, maneno hayo yalimfanya Moses ashushe pumzi kwani huo mpango huo na yeye ulikuwa unamuhusu.

            "Kwahiyo wote tulioendesha Operesheni fagio la chuma kifo ilikuwa ni haki yetu?" Moses alimuuliza yule askari.



           "Ndiyo tulivyoambiwa na jukumu tulilopewa, tuliwekwa makundi tofauti ya kuweza kuwaua nyote mliosababisha binamu wa Kaminshna auawe. Wengine walitumwa nyumbani kwako na wengine nyumbani kwa M.J Belinda kwenda kuwaua na wengine tulitumwa kuja kumuokoa Lion mikononi mwa Norbert" Askari yule aliongea huku akivumilia maumivu yaliyopo mdomoni mwake.



            "je kiini cha mpango huo ni nini ukiacha hiyo ya kutuangamiza sisi?" Alimuuliza huku akimtazama kwa umakini sana.



            "Sijui kiini ni nini sisi Kamishna alitupa kazi tu na alituambia iwe ya siri kama kikosi chetu kilivyokuwa cha siri, hatuhoji kingine kwani hatukuwa ns haki ya kupinga amri  za mkubwa wetu" Askari huyo alijibu kisha akamtazama Moses kwa huruma sana.



             "Ngoja huyo mwenzako aamke aongee tofauti na wewe nitabandika ile pasi ya mateso iliyopo pale mezani kwenye korodani zako" Mosea alisema  huku akimuonesha yule askari ilipo pasi ya umeme kwenye meza ya mateso, yule askari alimuangalia kwa huruma lakini haikumfanya abadili uamuzi wake.



   Moses alichukua simu yake akabonyeza baadhi  ya vitufe vilivyopo kwenye simu yake akaipata namba ya Norbert akampigia, simu iliita kisha ikakatwa kisha  ukaingia ujumbe mfupi wa maneno kwa Norbert.



  Gawaza alipofungua ujumbe huo na kuusoma alijikuta akicheka kisha akasema, "jamaa huyu umalaya utammaliza kwa kweli", alitoka humo kwenye chumba cha mateka akafunga mlango akazima taa akaondoka.

 Muda ambao Moses anampigia simu Norbert tayari alikuwa ameshafika kwenye mlango  wa chumba cha hoteli alicholipia, ilipoita simu alitumia mkono mmoja kuitoa kukata kisha akaandika ujumbe mfupi  huku mkono mwingine ulikuwa upo kiunoni mwa Josephine.

Aliingia ndani na Josephine kisha akafunga mlango kwa ufunguo na hapo ndipo akaanza uchokozi mwingine katika mwili wa Josephine akiwa yupo nyuma yake amemkumbatia, alitumia wasaa huo kwa kukichezea kiuno cha Josephine huku midomo yake ukiwa ipo shingoni ikifanya utalii wa ghafla ambao ulimpa kichaa cha ghafla Josephine hadi akaishiwa nguvu akabaki akikishika kichwa cha Norbert kama aliyetaka kukitoa huku akichezea akichezea kidevu cha Norbert kilichobeba ndevu ndogo zilizokatwa vizuri kwa mtindo wa kupendeza.

      "ooosiii! Norb....ert" Josephine alilalamika huku akizidi kumuegemea Norbert kwa nyuma kutokana na kuishiwa nguvu, utundu wa Norbert katika mwili wake alishindwa hata kusimama akawa anaelekea kudondoka ikambidi Norbert ambebe huku  wakiwa wamekutanisha ndimi zao akaenda kumtupia kitandani huku akiendelea na utundu wake.



 Alikuwa juu ya kifua cha Josephine akifanya utalii usio rasmi katika wa mrembo huyo ambao ulaini na joto lake ulizidi kumtia hamasa aendelee na utalii huku akipunguza stara za mrembo huyo pamoja na stara zake, ndani ya robo saa tangu waingie walikuwa wapo kama walivyoingia duniani na utundu uliendelea baada ya muda mrefu kisha wakaanza kile kilichowafanya wawepo humo ndani katika mazingira hayo.



Iliwachukua masaa takribani mawili wakawa tayari wamemaliza kile kilichowafanya wawepo humo ndani, wote kwa pamoja walijipumzisha huku wakiwa na tabasamu pana usoni mwao na wakawa wanaongelea kile kilichokuwa kikifanyika muda mfupi uliopita, walipongezana kwa kila mmoja kuonesha ushirikiano kwa  mwenzake huku wakiwa wamekumbatiana kwa upendo wa hali ya juu kama walikuwa wana muda mrefu tangu wajuane.



 Haukupita muda mrefu Josephine alipitiwa na usingizi papo  hapo kitandani akamuacha Norbert akiwa amejilaza pembeni yake akiusanifu mwili wake ambao muda huo haukuwa nakificho chochote kitachozuia usiuone moja kwa moja.



 Norbert alibaki akitabasamu alipouangalia mwili wa Josephine kisha akajikuta amepeleka mkono akashika moja ya mapambo ambayo ukubwa wake ulikuwa umeongezeka kutokana na  Josephine kifudifudi, alipoendelea kuyashika mapambo hayo mhemko mpya ulimuanza na alitamani kumuamsha Josephine lakini alisita baada ya simu yake ya mkononi  kutoa mlio wa kuingia ujumbe mfupi wa maneno na ikamlazimu aichukue simu yake ausome ujunbe huo.



 Ujumbe huo ukimfanya asikitike kisha akamtazama Josephine aliyekuwa amelala akambusu shavuni, alivaa nguo zake akaiacha simu yake kitandani akatoka chumbani humo akaelekea chumba cha tatu kutoka chumba alichopo. Aligonga katika chumba hicho mara mbili kisha akasubiri kidogo, mlango wa chumba hicho ulifunguliwa akaonekana yule msichana aliyekuwa yupo mapokezi akiwa yupo ndani ya mavazi maalum ya kulalia. Sura ya msichana huyo ilipomuona Norbert ilibadilika na kuwa isiyo na furaha hata kidogo, Norbert hakujali hilo suala yeye aliingia ndani kisha msichana huyo akafunga mlango.



          "Nor hivi kipi hukipati kwangu?" Msichana huyo alilalamika akimtazama Norbert kwa sura yenye kuonesha hakuwa amependezwa na tabia yake.



          "Nor nimekupa mwili wangu nimekupa mapenzi yangu lakini bado tu huridhiki hadi umeamua kumleta mwanamke mwingine katika hoteli hii ambayo nafanya kazi na umelipa chumba kwa ajili yetu tukutane...Aaaargh! Nor nifanye nini ujue nakupenda mpenzi wangu" Msichana huyo alizidi kulalamika huku machozi yakianza kumtoka, Norbert alimsogelea kwa taratibu huku akimtazama usoni na alipomfikia karibu akamshika bega.
           "Jamila" Norbert aliita akiwa ameshika bega lake na mkono wa pili akaupeleka shavuni mwa binti huyo.



           "niache huko" Jamila alisema kwa ukali sana kisha akautoa mikono mikono ya Norbert kwa nguvu akaendelea kulalamika, "Norbert kwanini unanifanyia hivi jamani nimechoka nasema nimecho....".



   Jamila alishindwa kuendelea tena kulalamika baada ya Norbert kumuwahi kwa kukutanisha papi za midomo yake kwa nguvu sana na akawa anapata shurubati kwa nguvu, Jamila alileta upinzani kutokana na kutotarajia jambo hilo lakini upinzani wake ulizidiwa na nguvu alizonazo Norbert katika kumdhibiti asifurukute.



   Haukupita muda mrefu sana tangu midomo yake ikitutane na midomo ya Norbert kwa ghafla tayari alikuwa amelegea na akashindwa kutoa upinzani na badala yake akatoa ushirikiano kwa Norbert, aliendelea kufanya  hivyo huku akimpapasa Norbert kufuani mwake na akiwa amekolewa kabisa na kitendo alichokuwa akikifanya Norbert.



   Maruhani yake ya kike yaliyokuwa yamelala tayari yalikuwa yameshaamka kutokana na zoezi hilo, Norbert alipotoa mdomo kinywani Jamila aliuleta mdomo wake karibu akionesha kuhitaji kuendelea na zoezi hilo. Norbert aliamua kuendelea na zoezi hilo ambalo analijua kuwa ni udhaifu mkubwa sana kwa Jamila kwani huamsha vilivyo lala, haikupita muda mrefu tayari Jamila alikuwa hajiwezi kabisa  hata macho yakawa yanafunguka  kwa tabu sana huku mihemo ikawa inamtoka akionesha kazidiwa.



    Norbert alitumia wasaa huo kumpeleka kitandani huku akiendelea na uchokozi, Jamila alionekana kuzidiwa zaidi hadi akafungua shati la Norbert akalivua halafu akadaka vishikizo vya suruali vilivyopo juu ya zipu akiwa na papara sana.



           "dah! Hawa wanawake wataniua kama natumia mafuta vile" Norbert alisemea moyoni  huku akidaka mikono ya Jamila isifungue vishikizo vya suruali kwa kuhofia kuzua mapya, alikuwa katoka kutimiza hitaji la Josephine   hivyo angefungua suruali angejua kila kitu kwani hakuwa amejisafisha kabla ya kuja humo ndani.



            "Nor please usinitese", Jamila alilalamika huku akikazanania kufungua suruali ya Norbert.



           "subiri kwanza mpenzi mimi ni wako tu usiwe na papara" Norbert alimuambia Jamila huku akiitoa mikono yake akaendelea kufanya utundu wake huku akipunguza vizuizi vinavyofanya mwili wa Jamila usionekane vizuri kwake, baada ya muda mfupi tayari na yeye alikuwa amepunguza vizuizi katika mwili wake akawa hana tofauti na Jamila. Waliianza safari nyingine iliyowachukua saa kadhaa wakawa wameshamaliza wakiwa wamechoka hasa Norbert ndiyo alichoka zaidi kwani alikuwa ameangusha magogo mawili bila kupumzika.



            "Asante Nor" Jamila huku akihema kwa nguvu sana.



            "huna haja ya kushukuru ni haki yako hii" Norbert alimuambia huku akivaa nguo zake kwa haraka kwani hadi muda huo tayari giza lilishaumeza mwangaza wa jioni.



           "Nor unaenda wapi sasa au kwa huyo kimada wako?" Jamila aliuliza huku akikunja sura kwani hakupendezwa kuondoka na Norbert muda huo.



           "Aaah! Jamila mpenzi wangu mbona wivu hivyo acha nimuwahi yule siyo kimada wangu nipo kazini" Norbert alimulalamika Jamila.



           "Etii upo kazini! Ndiyo mshikane viuno pale receiption? Haya mwandishi wa habari naona ulienda kutafuta habari kitandani na yule mwanamke" Jamila alikuja juu huku akimbania pua na hapohapo Norbert akabadilika uso wake ukawa usio na furaha hata kidogo.



           "Unajua nini? Sasa kulala na wewe kitandani inaonekana umevuka mipaka hadi unafikia hatua ya kunitusi sasa tusijuane" Norbert aliongea kwa hasira akamaliza kuvaa nguo zake akataka kuondoka, Jamila hakuweza kustahimili kuona jambo hilo kutokana na kutekwa sana na Norbert kihisia tangu waanze uhusiano wao usio rasmi. Alikimbilia Norbert akamkumbatia kwa nyuma huku akilia, Norbert alimtoa mikono yake kisha akageuka nyuma kumtazama.



            "Nisamehe mpenzi wangu ilikuwa ni hasira tu" Jamila huku machozi yakianza kumtoka kisha akaendelea kusema,"nakupenda sana Norbert ndiyo maana nakuwa hivi".

Jamila alipomaliza kuongea alibaki akimtazama Norbert ambaye alisimama akimuangalia, alipoona Norbert hajibu kitu aliamua kupiga magoti akiwa hivyohivyo mtupu aombe msamaha huku machozi yakimtoka.

  Norbert alimtazama Jamila kisha akashusha  pumzi akamuinua pale chini alipopiga magoti akamkumbatia. Aliamua kumfuta machozi akamuambia, "kilio chako ni zaidi ya msiba kwangu hivyo sipendi kukiona mpenzi wangu, kosa lako wewe kwangu msamaha hutoka haraka sana  hata kabla hujalikiri mbele yangu. Nakupenda sana mpenzi wangu".



   Jamila aliposikia maneno hayo amani ya moyo ikarudi na alitabasamu akambusu Norbert mdomoni, Norbert alitabasamu alipopewa busu hilo kisha akampiga kibao cha kalio Jamila cha uchokozi kilichosababisha Jamila ashtuke halafu amtazame Norbert.



              "Afuuu Nor unaanza sasa wakati mwenzako nimechoka sana kazi yako siyo ndogo" Jamila aliongea kisha akambusu Norbert kwa mara ya mwisho akamuambia,



              "haya mpenzi wahi".



   Norbert hakuchelewa alitoka upesi chumbani humo akimuacha Jamila ndani na alirudi katika chumba ambacho alikuwepo Josephine amelala, alipoingia ndani hakumkuta Josphine zaidi ya kusikia maji yakiwa yanamwagika bafuni na kitandani aliikuta simu kama alivyoiacha. Norbert aliichukua simu yake akawasha kioo ili aingize namba zake za siri atoe loki, alipoingiza namba za siri kwenye simu yake picha ya Josephine ikaja kwenye kioo kwa ghafla ikitoa tangazo na mfano kwenye mfumo wa simu juuvya kuchezewa simu yake.





           "intruder selfie" Norbert aliongea huku akiitazama picha ya Josephine ambayo ilipigwa moja kwa moja na siku bila Josephine kujua.

   Intruder selfie ni picha inayopigwa kwa kamera ya mbele ya simu baada ya mtu kukosea kuingiza neno la siri au kukosea mchoro wa simu(pattern) ambao ndiyo hufunga simu kwa usalama zaidi, mara nyingi mchoro huwa upo kwenye simu za kisasa zenye mfumo wa android katika program zinahusika kufunga program zingine(appslock) hasa kwa programu ya ulinzi wa simu dhidi ya virusi maarufu kama CM security.



    Ulinzi wa namna hii ndiyo ulikuwepo kwenye simu ya Norbert ambayo alikabidhiwa na shirika la EASA aitumie kwa ajili ya shughuli za kijasusi, simu hii ilikuwa ni tofauti na simu zingine ambazo mpaka uweke programu maalum yenyewe kufanya hivyo. Hii ilikuwa ina mfumo wa moja kwa moja wa ulinzi wa  simu na ilikuwa imeundwa kwa ajili ya wapelelezi wa daraja za juu sana katika mashirika mbalimbali ya wapelelezi duniani, simu hii ilikuwa imetengenezwa na kampuni ya Samsung ya Korea ya Kusini kwa agizo maalum kutoka mashirika ya kijasusi duniani.



  Hadi hapo Norbert alishabaini Josephine ndiye aliyeichezea simu yake kipindi hayupo, picha ya Josephine iliyokuwepo juu ya kioo ilikuwa ni ushahidi tosha usiopingika. Norbert alisikitika tu alipoona hiyo picha ikiambatana na maandishi yaliyoandikwa 'someone tried to snoop on your phone'. Yaliyomjulisha juu ya uchezewaji wa simu hiyo akiwa hayupo, alipuuzia suala hilo kuliweka ndani ya fikra zake kwa muda  huo.



  Aliamua kufungua sehemu ya ujumbe mfupi wa maneno kwenye simu yake baada ya kukuta ujumbe mpya umeingia kutoka kwa Moses, aliusoma ujumbe huo kisha akatikisa kichwa kuuafiki halafu akatizama ulipo mlango wa bafuni humo chumbani. Akili yake bado ilikuwa ipo imara ingawa muda huo mwili wake ulikuwa na uchovu sana kutokana na shughuli nzito aliyotoka kuifanya muda mfupi uliopita, uchovu wa mwili wake ulimfanya ajilaze kitandani huku akisikia uchovu mkubwa uliopo kwenye mgongo wake.



 Akili yake ilianza kurudi na kuwaza tukio la siku iliyopita hasa pale hospitali ya taifa ya Muhimbili alipokuwa akifuatilia upelelezi wa mauaji ya Jenerali Kulika, mchoro wa muuaji wa wanajeshi wote waliokuwa wakilinda nyumbani kwa mkuu wa majeshi huyo nao ulimrudia kwenye kichwa chake kwa sura ile anayoitambua ambayo mwanzo hakuwa ameitambua kutokana na kutodhania kwa huyo mwanamke anaweza kufanya kitu ksma hicho.  Hakika umdhaniaye siye kumbe ndiye na umdhaniaye ndiye kumbe siye, Norbert alibaki akiwa na hatiati juu ya mhusika huyo  na alijionya kuwa awe makiini kwani ashang'amua kuwa muuaji huyo anajua kwamba yupo nyuma yake akifuatilia nyendo zake.

Fikra za muuaji huyo zilipozidi kushambulia katika halmashauri ya kichwa chake aliamua kusimama wima kisha akajongea hadi lilipo dirisha la chumba, aliamua kuweka macho yake hapo dirishani yatalii eneo la barabarani kwenye makutano ya mtaa wa Aggrey na Jamhuri.

 Aliusngalia utulivu wa eneo hilo hasa nyakati kama hizo kutokana na barabara yake kutotumiwa  sana, utulivu wa mtaa huo ulizidi kuifanya akili yake iwe kwenye utulivu zaidi katika kulifikiria suala lililopo mbele yake ambalo ilikuwa ni wajibu alipatie ufumbuzi hata kabla hajaambiwa kufanya na bosi wake anayempa kazi. Hakika alitakiwa aongeze umakini zaidi hata anavyoongeza umakini wa kulinda mboni za macho akipita kwenye eneo lenye kimbunga chenye mchangayiko wa takataka na vumbi, alikuwa akigawiana kitu kimoja cha siri na muuaji huyo anayemtafuta na ameweza kumtambua kuwa huyo ndiye muuaji ambaye ni miongoni mwawauaji hao.
        "hebu" Norbert katika fikra zake alikumbuka kitu na hapo akaitoa simu yake akafungua sehemu ya ulinzi wa simu ya ambayo hupiga picha ya ghafla pamoja na kurekodi ikiwa tu itanasa sauti, alifungua katika mafaili yenye kuhifadhi picha pamoja na sauti akakuta faili la sauti likiwa na ukubwa wa megabaiti moja(1 MB). Alilitazama faili hilo kwa umakini pamoja na tarehe lililoingia na muundo wake, file hilo lilikuwa limerikodiwa muda ambao alikuwa chumbani kwa Jamila. Norbert aliligusa faili hilo kwa kidole gumba alifungue kisha akalifunga papo baada ya sauti ya mlango wa bafuni kusikika ukifunguliwa, alifunga sehemu ya ulinzi wa simu yake kwa haraka sana kisha akafungua video ya nyimbo ya msanii wa kitanzania ambayo ilikuwa ni mpya aliyoipakua mtandaoni ili aiangalie kutokana na kuwa mpenzi wa muziki.



 Josephine alionekana akitoka bafuni huku akiwa amejifunga taulo fupi  sana la rangi nyeupe lilioshia kwenye mapaja yake huku akitumia taulo jingine dogo kujifuta nywele zake, alipousikia huo muziki unaolia kwenye simu ya Norbertr alitabasamu kisha akamtazama ambaye aliinua macho yake kumtazama mara moja.



         "Yaani Norbert huo wimbo naupenda sana utanirushia kwenye simu yangu" Josephine aliongea  huku akiwa bado ameweka kichwa chake upande aweze kujifuta vizuri maji kwenye nywele zake.



       "nikurushie video au audio?" Norbert alimuuliza.



         "Zote zote halafu video sijaiona  kabisa" Josephine aliongea huku akijifungua taulo na kubakiwa hana kitu akaanza kujifuta maji.



        "video ndiyo hii naitazama" Norbert alijibu huku akimtazama Josephine ambaye hakuwa na kitu mwilini akiwa anajifuta maji, aliutazama mwil huo kuanzia juu hadi chini kisha akatikisa kichwa  huku akitabasamu.



         "weee! Usiniambie nipe na mimi niione....nini sasa Norbert mbona hivyo?" Josephine aliposikia juu ya video ya nyimbo hiyo alijikuta akipatwa na hamu ya kutaka kuitazama video hiyo, aliponyanyua uso wake kumtazama Norbert kwa mara nyingine alimuona akisanifu umbo lake na hapo ndipo alipomuuliza huku akiingiwa na aibu.



         "Wewe ni mrembo sana ndiyo maana siishi kukutazama" Norbert aliongea huku akimtazama Josephine kwa taratibu pana.



         "Norbert bwana na wewe" Josphine alisema huku akiinamisha macho chini kwa aibu akimuacha Norbert aendelee kuusanifu mwili wake huo.



        "ok, ngoja na mimi nikaoge tukale" Norbert aliongea huku akitembea hadi kitandani akaitupia simu kitandani, alivua nguo alizovaa kisha akavaa taulo  akaelekea mahali ulipo mlango wa bafuni akimuacha Josephine akiwa anajiweka sawa baada ya kumaliza kujifuta maji mwilini mwake.

 Upande mwingine maeneo ya  Kunduchi nyumbani kwa mkuu wa majeshi ya majini Luteni Jenerali Ibrahim, kikao kizito kilikuwa kimeandaliwa baada ya ripoti nzito kufika kwenye mikono ya wakubwa wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa kupitia daktari aliyechukua vipimo vya damu katika mwili wa Jenerali Kulika pamoja na wale wanajeshi kwa namna ya siri baada  ya uchunguzi wa awali kuonesha vipimo walivyotilia shaka na baadhi ya wakubwa wa majeshi akiwemo Msemaji mkuu wa majeshi hayo.



   Mkutano huo uliendeshwa ndani ya chumba cha siri  katika nyumba hiyo chenye meza ambayo kila mhusika wa mkutano huo alikuwa amekaa kwenye kiti kinachoizunguka meza hiyo. Mkuu wa majeshi ya majini L.J Ibrahim, mkuu wa majeshi ya anga na nchi kavu M.J Belinda, Mkuu wa jeshi la kujenga taifa(JKT) Filipo Marwa, Dokta Bakari kutoka Muhimbili pamoja na Benson ambaye alihudhuria kama mwanausalama ambaye amekuwa akifuatilia vifo vya watu waliokufa kwa sumu ya Quantanise aliyeletwa kwa msaada wa ngazi za juu wa Kanisa la Kiluteri ambao walimkodi kutoka shirika la kijasusi Marekani CIA. Ripoti hiyo ilipofika L.J Ibrahimu ilizidi kumtia hasira haswa kutokana na uzito wake, kifo cha mkuu wake kilizidi kumfanya jazba ipande.



         "Jamani hii ni aibu kabisa kwa mtu kama Moses Gawaza mkurugenzi wa usalama wa taifa pia mwanasayansi wa kuaminika ndani ya nchi hii, ametengeneza sumu akisema ni ya kuulia wadudu waharibifu wa mimea tena akaifungua kwa sherehe kubwa na taifa lilimpongeza  kwa kuwa mkombozi wa wakulima kumbe ni muuaji aliyetumia  kivuli cha taaluma yake kuangamiza wengine hii ni too much Dokta Bakari hebu wape maelezo wa kila ulichokibaini wewe baada ya kukuambia ufanye uchunguzi kwa mara ya pili kwa siri" L.J Ibrahim aliunguruma kwa hasira kwenye mkutano huo, Dokta Bakari aliposikia ruhusa hiyo ya kueleza kuhusu ripoti hiyo alisimama akiwa mkononi ana faili lenye makaratasi yaliyobanwa vizuri.



          "Nashukuru ndugu Luteni Jenerali kwa kunipa wasaa huu, kabla ya kuanza uchunguzi huo nilianza kupitia tafiti za uchunguzi zilizotangulia katika vifo vinavyofanana na kifo na General pamoja na wanajeshi wengine wazalendo waliokuwa wakifanya kazi ya kumlinda General. Uchunguzi wa matukio ya awali inaonesha kuwa kifo cha Bishop Edson na Mufti kilisabAbishwa na kupasuka kwa mishipa ya damu na ule wekundu uliokuwa unaonekana juu ya ngozi ni damu kuviria juu yake kiasi kwamba miili yao ilianza kuvimba  juu ya ngozi kama lengelenge kubwa katika sehemu za mbalimbali na laiti ikitobolewa kidogo basi damu ilikuwa inavuja eneo lilipotobolewa" Dokta Bakari alieleza kisha akamtazama kila mmoja aliyepo humo ndani halafu akaendelea, "sasa turejee katika uchunguzi huu nilioubaini ambao ulinitia maswali sana kabla hata sijaanza kuchunguza, ripoti za chunguzi zilizopita zilieleza juu ya kuvuja kwa damu lakini sikuwahi kuhusika kwenye chunguzi hizo. Swali langu la kwanza nililojikuta najiuliza ni kwanini General alikuwa na alama ya kutobolewa na kitu chenye ncha kali nyuma ya shingo lakini sikupata majibu hadi pale nilipopima damu yake kwa umakini nikiwa nimebaki peke yangu katika chumba cha uchunguzi majira ya usiku wa manane, kwa mujibu wa taarifa za tafiti yangu nimebaini kwamba aliyotobolewa nayo ilikuwa ni sindano ambayo ilitobolewa kwa kutumia nguvu nyingi sana hadi sehemu ya plastiki ya sindano hiyo  ikabaki ndani ya ngozi baada ya kugonga pingili za shingo sehemu hiyo ya plastiki ni hii..."



  Dokta Bakari aliingiza mkono kwenye koti la mfuko wa koti la suti alilokuwa amelivaa akatoa mfuko wa nailoni wenye kipande kidogo cha plastiki lenye rangi ya bluu, aliwapatia M.J Belinda aliyekuwa pembeni yake ambaye alikiangalia kisha akampatia M.J Marwa. Mfuko huo ulizunguka kwa watu wote  humo ndani na hatimaye ukarudi mikononi mwa Dokta Bakari ambaye aliuweka mezani, alifungua karatasi kadhaa za faili hilo kisha akaendelea kusoma, "Plastiki hiyo nilipoichunguza nilikuta ina chembechembe za kemikali za Quantanise ambazo ninatambua kuwa ni sumu ya kuua wadudu waharibifu wa mimea iliyoipa sifa nchi yetu kwa kutengenezwa kwake, sikutaka kuamini kama sumu hiyo ndiyo imemuua General pasipo kufanya utafiti ikiingia kwenye mwili wa kiumbe hai inaleta athari gani. Ili kujua athari za sumu hii niliamua kumchukua panya albino(panya weupe) nikagusa mabaki ya sumu hiyo kwenye sindano ndogo ya kupima malaria kisha nikamchoma panya huyo, nilimuweka panya huyo kwenye sanduku la peke yake kisha nimtazame atakuwa na hali gani baada ya kumchoma. Panya aliishiwa nguvu ndani ya sekunde kadhaa na hatimaye ngozi yake ikaanza na kuwa nyekundu hadi alipokufa, hivyo basi hapo nikatambua athari za sumu ya Quantanise ambazo zilitokea katika mwili wa General na hiyo ndiyo chanzo cha kifo chake baada  ya sumu hiyo kuleta athari kwenye moyo"  Dokta Bakari alipomaliza kuongea aliketi kwenye kiti chake.



  L.J Ibrahim alisimama kwa mara nyingine akasema, "nadhani mmemsikia Dokta alivyosema juu ya uchunguzi wa kifo cha mkuu wetu ambacho kinafanana kwa kila kitu na kifo cha walinzi wake, sasa nyinyi wengine miongoni mwa wanajeshi wenzangu wenye uchungu na mkuu wetu ningetaka kusikia maoni yenu, naanza na Major general Marwa".

M.J Marwa aliposikia kauli ya L.J Ibrahim alisimama akapiga saluti moja kisha akasema, ” kwa mujibu wa maelezo ya Dokta hapa hakuna ubishi juu ya suala hilo chanzo cha kifo cha General ni Professa Moses Gawaza kwani hizo kemikali nakumbuka wakati anazizindua alisema ni hatari sana kwa binadamu na itatumika kwa uangalifu maalum hapa nchini tena itatolewa kwa vibali maalum, sikuwahi kusikia kama kuna mkulima wa hapa nchini aliwahi kuchukua kibali akainunua zaidi ya kusikia sumu hiyo ilisafirishwa kwa meli kuelekea huko Ulaya zilipotoka oda za kuinunua. Hivyo basi kwa matumizi ya ndani ya nchi hii ni Moses anahusika kwani haipo kwenye mikono ya mwingine yoyote na pia muuaji ni mtu mwenye mbinu za kijasusi, Moses ndiye mhusika kwani yeye ana mbinu za kijasusi tukumbuke na ni kiongozi wa usalama wa taifa. Lazima atiwe nguvuni mara moja”.

M.J Marwa alipoongea hivyo jazba tayari ilikuwa imempanda na hadi anakaa chini alikuwa alihema sana, L.J Ibrahim alimruhusu M.J Belinda naye aongee katika mkutano huo.

   M.J Belinda alipopata ruhusa ya kuongea alinyanyuka akatoa saluti kisha akasema, "Najua nitakuwa nipo tofauti sana na nyinyi nyote ila napenda niseme hivi, kabla ya kuanza kumtuhumu Moses ningependa tuwatuhumu na Special forces wa jeshi la polisi ambao walinivamia nyumbani kwangu wakataka kunichoma sindano yenye kimiminika chekundu ila niliwahi kuwatia nguvuni na wapo kwenye basement ya kambini. Hao  tumewabana na wamekiri kutumwa kuwaua wale wote walioshiriki operesheni fagio la chuma ambayo iliongozwa na General, mtu waliyemtaja anawatuma kwa ajili ya kazi hiyo ni Kamishna ambaye hawajamtaja jina lake. Sasa mnaposema muuaji Moses wakati yeye mwenyewe alishiriki Operesheni fagio la chuma na aliwatoroka hao Special force  bado haina ushahidi kwanza tuwahoji hawa niliowakamata na hiyo sindano ikapimwe na kama ni hiyo sumu wataje wameipata vipi. Mkuu hapo tutaweza kumpata Mhusika kirahisi kutengeneza sumu na kuwa jasusi haitoshi kumtuhumu kuwa ni muuaji". Alipomaliza kuongea alikaa chini akiwaacha wakubwa wenzake  wakitafakari maneno yake, Benson alikuwa kakaa kimya muda wote huo akiwasikiliza na hakuwa amenyanyua mdomo wake kuongea.



   Baada ya kimya cha muda wa dakika kadhaa kuvamia humo ndani hatimaye Dokta Bakari alinyoosha mkono, wote kwa pamoja walimtazama na hatimaye L.J Ibrahim ambaye ndiye mkubwa kuliko wakubwa wote waliopo na ndiye mwenye kauli kuu akamruhusu kuongea.
              "Kwa maelezo ya meja jenerali Belinda ni wazi kuwa hiyo sindano aliyotaka kuchomwa ni ya Quantanise kwani hiyo sumu  ina rangi nyekundu nafikiri angeileta hiyo sindano tuifanyie ufafiti za kuhakiki" Dokta Bakari aliongea kisha akakaa chini, M.J Belinda aliposikia maneno ya Dokta Bakari alizamisha mkono wake katika mfuko wa kombati la kijeshi alilolivaa akatoa simu ya kisasa ambayo  alibonyeza kwenye kioo mara kadhaa akampatia Dokta Bakari huku akimuonesha kwenye kioo. Dokta Bakari aliangalia kioo hicho cha simu akapatwa na mshtuko sana na akaishika simu ya M.J Belinda akaweka vidole viwili kwenye kioo cha simu hiyo ya kugusa akavitanua ili kukuza(zoom) kile alichokiona hapo  kwenye kioo.



                "Hii ni quantanise ikiwa kwenye injection container(bomba la sindano) means hao watu ni wanahusika" Dokta Bakari aliongea kisha akampatia simu L.J Ibrahim ambsye aliitazama akampatia M.J Marwa halafu ikapelekwa Benson kabla haijarudi  kwa mwenyewe M.J Belinda. Maneno hayo alipoyasikia L.J Ibrahim aliweka mikono kwenye uso wake kisha akajifikiria kwa sekunde kadhaa halafu akainuka kwenye kiti, aliwatazama wote waliomo mule kisha akasafisha koo lake huku akishusha pumzi ili ajiandae kusema jambo ambalo liljia kichwani kwa muda huo.



                "Ok ok ni hivi Belinda utaongozana na Benson mkawahoji wale watuhumiwa halafu kikosi kingine cha makomandoo kitaemda kumtia nguvuni Moses kabla habari hizi hazijafika kwenye vyombo vya habari. Is that clear? Mimi ndiyo nitajua hatua gani atakayochukuliwa Moses kwani bado muuaji kwangu"L.J Ibrahim aliongea  akazidi kumshangaza M.J Belinda kwa uamuzi aliouchukua.



                "Lakini mkuu hapo hatuna uhakika wa wa ushahidi kumtia Moses nguvuni Moses apewe adhabu kutengeneza chemical hiyo siyo saba..."



                "Shut up Belinda nani mkuu kati ya mimi na wewe?! Si wewe mdogo kicheo sasa sikiliza amri zangu ninavyosema mimi ndiye mkuu kwa sasa, is that clear?!"M.J Belinda aliongea kwa kutoridhishwa na uamuzi wa mkuu wake lakini  alifokewa kwa nguvu sana L.J Ibrahim ambaye ni mkubwa kwake kicheo, alilazimika kukubali amri ya mkuu kwa kukamsa  huku akisema,"Mkuu!"



                  "Good! Sasa kazi ianze mara moja kuanzia muda  huu, kikosi cha kumkamata Moses kitateuliwa na wewe Belinda kutoka jeshi la nchi kavu. sitaki nisikie unadanganyika na hao watu uliowakamata kumbuka alama hiyo ya mabawa ya ndege yenye rangi ya silver iliyowekwa hapo kwenye mfuko wa kombati yako ya juu inamaanisha wewe ni komandoo tena kiongozi wa kikosi  cha makomandoo kuanzia hivi sasa baada ya General. Sasa ujinga huo sitaki kuusikia, Marwa hakikisha unatoa vijana wako watakaa mipakani wakishirikiana na wa jeshi l ardhini katika kuhakikisha huyu mtu hatoroki. Kikao kimevunjwa kwa sasa mpaka atakapopatikana Gawaza ndiyo tutakaa tena kikao kujadili" L.J Ibrahim aliondoka humo kwenye chumba cha mkutano huku kila mmoja akinyanyuka akiwa na fikra zake kichwani.

 Majira ya saa nne usiku Norbert alikuwa tayari ameshapata chakula cha jioni pamoja na  Josephine, muda huo walikuwa wamejilaza kitandani wakichezeana michezo ya hapa na pale mithili ya wapenzi wa siku nyingi.



  Walikuwa wamevaa nguo za kulalia wakifanya michezo hiyo mithili ya watoto na hatimaye wakaamsha wazungu waliolala kwa kila mmoja, joto la miili yao lilipanda kwa ghafla baada ya wazungu hao wasio hata na asili ya Ulaya kuamka. Hitaji la kuwalaza wazungu ndiyo lilifuata kwani hawakuwa na namna baada ya wazungu wa Josephine kuchachamaa zaidi wakihitaji kulazwa, ilikuwa ni wajibu wa Norbert kwa namna moja tu na hakuwa na namna nyingine itakayowafanya wazungu hao walale.



  Kuwalaza wazungu hao ilikuwa ni kama unamlaza mtoto, yaani uwalaze kwa namna ambayo wanataka kulala ndiyo watalala.



  Wazungu hao ambao tayari walikuwa wameshamtia  wazimu Josephine na alimkalia kwa juu Norbert aliyekuwa amelala cha huku akifungua uwazi wa mavazi maalum ya kulalia na kifua kika wazi. Alianza kuchezea lifua cha Norbert na akapeleka kinywa chake karibu na kinywa cha Norbert ambapo alipokewa na Norbert kisha akaanza kufanya utundu katika mwili wa Norbert, haikupita muda mrefu Norbert alimgeuza akamuweka yeye chini akaendelea na utundu wake kwenye mwili wa binti huyo ambao ulimfanya awe kama aliyepandwa na maruhani jinsi alivyokuwa akigaragara kwenye kitanda hiko akienda kushoto  na kulia huku akipiga makelele. Aliendelea na utundu wake kwa muda mrefu kisha akaanza tena mchezo mwingine usiohitaji musmuzi na wenye uwanja uliotengenezwa kwa bidhaa za zao la misitu, miguno ya Josephine ndiyo ilitawala ndani ya chumba hicho kwa muda wa masaa mawili. Saa sita usiku wa maneno ndiyo kelele hizo zilikoma baada ya wazungu wake kulala sasa akawa anatawaliwa na uchovu wa hali ya juu, alilala usingizi hapo kitandani akimucha Norbert akiwa anafikiria mambo mengine hadi alipopitiwa na usingizi.



Majira ya saa kumi na moja alikuja kushtuka baada ya kusikia mlio wa simu yake ikilia kwa fujo, alijinyoosha kisha akatazama pembeni hakumuona Josephine badala yake alisikia sauti ya kunong'ona ikitokea ulipo wa mlango wa kuelekea bafuni  kisha sauti ya maji yakimwagika ikasikika baada ya yeye kuzima kengele ya simu aliyokuwa ameitega kila siku ikimkumbusha(reminder) juu ya jambo ambalo aliazimia kulifanya siku hiyo.



Norbert aliamka kitandani kwa haraka kisha akakaa akafungua simu yake akaangalia sehemu ya kurekodi ilivyokuwa na akakutana kuna faili jingine la ziada likiwa limeongozeka kwenye simu yake, tabasamu la ghsfla lisiloashiria furaha lilimjia katika uso wake. Muda huo Josephine alitoka bafuni akiwa ameshika simu yake akamkuta Norbert akiwa amekaa kitandani, aliungana naye kitandani huku akionesha kutokuwa na wasiwasi wowote.



    "Network haipatikani mpaka bafuni siyo" Norbert aliongea huku akitabasamu.



         "Hamna nilienda kwenye sink kunawa ndiyo simu ikaita nikarudi kuichukua nikaenda nayo nikawa nanawa huku naongea nayo" Josephine aliongea huku akijisogeza karibu zaidi halafu akamkumbatia Norbert.



        "mapema yote hii nayo" Norbert alimuambia Josephine.



          "Norbert nawe nini sasa" Josphine aliuliza huku akitumbukiza mkono yake katika eneo lisilostahili kutimbukizwa mikono



 Norbert hakutaka ubishi aliamua kutimiza kile kilichokuwa kikimfanya Josephine aingize mikono katika eneo la milki yake asubuhi hiyo.

MBEZI BEACH

DAR ES SALAAM

Muda ambao Norbert akiwa anajivinjari na ndiyo muda ambao gari la jeshi la wananchi wa Tanzania(JWTZ) liliingia  katika lango la nyumba hiyya kifahari baada ya mlinzi wa nyumba hiyo kulazimishwa afanye hivyo, ilikuwa ni range rover  ambayo makelele yake yalitosha kuwaamsha waliomo humo ndani. Breki za gari hiyo zilipofungwa kwa ghafla na kuleta makelele tayari wafanyakazi wa nyumba hiyo walikuwa wameshaamka, wanajeshi waliovaa sare za kijeshi walishuka ndani ya gari wakiongozwa na Afisa mteule daraja la pili ambaye alitoa amri kwa baadhi kuizunguka nyumba hiyi. Wengine wakiongozwa na Afisa mteule huyo waligonga mlango wakuingia ndani kwa nguvu hadi mfanyakazi wa ndani  alipofungua ndiyo wakaacha.



                   "Yuko wapi Dokta Hilary" Afisa mteule huyo alimuuliza mfanyakazi huyo ambaye alianza kutetemeka kwa uoga.



                  "ni mimi niwasaidie nini?" Sauti kutoka ndani ya nyumba  hiyo ilisikika na hapo wanajeshi wote wakaingia wakimsukuma msichana huyo wa kazi, waliingia ndani wakamkuta Dokta Hilary akiwa kasimama na mkewe Irene akiwa na mavazi ya  kulalia.



                  "Moses yupo wapi"Afisa mteule huyo daraja la pili ambaye alijulikana kutokana na kuvaa cheo mkononi kilicho na umbo kama la saa yenye alama ya mwenge alimuuliza Dokta Hilary huku wenzake wakimnyooshea bunduki kwa tahadhari.



               "Sijui alipo" Dokta Hilary alijibu kwa kujiamini.



                 "Ok, mkamateni yeye mpaka atakapojileta Moses" Afisa mteule  huyo aliongea kuwapa amri wenzake, askari hao walisogea mbele ili wamtie nguvuni Dokta Hilary lakini walisita baada ya kusikika amri nyingine.



               "SUBIRI!" Afisa mteule ambaye ndiye kiongozi wap alipaza sauti.

Wanajeshi wote walisitisha zoezi hilo lakini hawakusitisha kuwawekea bunduki Dokta Hilary na Irene, walitega sikio kwa mara ya pili wasubiri amri ya Afisa mteule daraja la pili aliyekuwa yupo nyuma yao.

          "Hapana msimkamate Dokta Hilary kwani huyo hatashawishi Moses kujitokeza, mnajua njia rahisi ya kumshawishi Moses kujitokeza ni ipi?" Afisa Mteule daraja la pili aliongea kisha akauliza swali ambalo halikujibiwa na wanajeshi waliopo chini yake, alikuwa akimtazama Dokta Hilary kwa tabasamu mithili ya mtu aliyekuja kiamani.



  Tabasamu lake lilikuwa linaongeza hofu katika moyo wa Dokta Hilary kwani lilikuwa ni tabasamu lililofuatana na fikra chanya, fikra hizo hazikutambuliwa na yeyote hadi pale Afisa huyo alipoziweka wazi.



          "Mkamteni mke wake" Afisa huyo alisema huku akitabasamu.



         "Nini? No! No! No! Nikamateni mimi mke wangu muacheni jamani" Dokta Hilary aliongea huku akisogeza mke wake mgongoni mwake kumkinga.



         "Nikamateni mimi!" Dokta Hilaty alipaza sauti huku akirudi nyuma akiwa amemkinga mke wake, mlio wa bunduki ikikokiwa baada ya kuondolewa usalama kutoka kwa mmoja wa wanajeshi hao ulisikika papo hapo. Mwanajeshi mmoja aliyeishika bunduki yake aina ya SMG ambayo kitako chake alikiweka begani ili kuzuia isitikisike wakati anapiga; alikuwa tayari ameweka shabaha kwenye mwili wa Dokta Hilary.



        "Tufumue ubongo wako na ubongo umwagike kisha tumchukue mke wako akataabike au tumchukue mke wako tuweze kumpata tunayemtaka. Haaaaa! Dokta Hilary chaguo ni lako hapo au nikuchagulie ukiwa upo hivyo hivyo umemficha mke wako mgongoni mwake" Afisa mteule daraja la pili aliongea.



  Maneno hayo yalimfanya Dokta Hilary amtoe mke wake nyuma ya mgongo wake, uamuzi uliokuwa ukitaka kuchukuliwa na wanajeshi ulikuwa ni mbaya zaidi hata ya huo anaotaka kuufanya. Mwanajeshi mmoja alisogea mbele zaidi akamchukua Irene kwa nguvu, alimuacha Dokta Hilary akiwa hana cha kufanya zaidi ya kubaki akitazama mke anavyokamatwa na wanajeshi hao.
          "Noooo! Hilary fanya kitu mume wangu usiwaruhusu wanichukue" Irene alilalamika huku akijaribu kujitoa mikononi mwa mwanajeshi aliyemdaka, Dokta Hilary alijikuta  akipiga hatua  zaidi mbele baada ya uchungu za sauti ya mke kumuumiza moyoni mwake. Hatua zake hizo zilizuiwa kwa mara moja na bunduki nyingine kutoka kwa mwanajeshi mwingine ilimuelekea, alisitisha ghafla kupiga hatua nyingine kutokana na kuhofia bunduki hiyo isije ikatoa kikohozi cha ghafla kitachoutwaa uhai wake papo hapo.



          "Lala chini, naona unajifanya mjuaji wewe" Afisa mteule huyo aliongea, Dokta Hilary alilala chini bila ya kupenda na wanajeshi hao walitoka mmoja baada ya mmoja.



Afisa mteule ndiye aliyekuwa wa mwisho kutoka nje na alitoka na ufunguo wa mlango mkubwa kisha akaufunga kwa nje, sauti ya gari ikiondoka ilisikika na ilizidi kumchanganya zaidi Dokta Hilary. Alikimbia hadi mlangoni kisha akanyonga kitasa akiwa ametokwa na kumbukumbu ya kufungwa kwa mlango na mwanajeshi yule, alinyonga kitasa bila mafanikio ndipo akakumbuka kuchungulia kwenye tundu la funguo. Hakuweza kuona nje kwa muda huo wa alfajiri kutokana na tundu la kitasa hicho kuzuiwa na ufunguo, aligeuka nyuma akiwa amechanganyikiwa akawaona wafanyakazi wake wakiwa wanamshangaa kwa kile anachokufanya muda huo.



           "Hey! Mnashangaa nini nyinyi kaleteni  funguo za akiba sasa hivi, mkichelewa sekunde mbili kazi hamna!" Dokta Hilary aliwafokea wafanyakazi wake akiwa amechanganyikiwa kabiaa, aliweka mikono kichwani kisha akakaa chini bila ya kupenda akajikunyata mithili ya kinda la ndege lilikosa joto la mama yake kipindi cha baridi.



            "Aaaaaaaargh! Mke wangu mimi jamani" Dokta Hilary alitoa ukeleleea uchungu pamoja na malalamishi ambayo hayakuwa na mhusika wa kumlalamikia, kulia alitamani lakini kulia huko alishindwa kutokana na roho ya kiume  aliyonayo.



Macho yake yaligeuka rangi na kuwa mekundu kutokana na uchungu alioupata baada ya kutekwa kwa mke wake, sehemu ya moyo wake alihisi ikikandamizwa na kitu chenye ncha kutokana na kutiwa nguvuni kwa kipenzi chake anayemhusudu. Kutoka pale alipoikunja miguu kwa kujikunyata aliinyoosha kisha akaanza kuichezesha kwa fujo mithili ya mtoto aliyekuwa amenyimwa hela ya kununua pipi, makelele ya uchungu ndiyo yalifuata huku akiweka mikono kwenye kichwa chake.



 Alidumu akipiga kelele hizo kwa muda hadi psle alipoguswa begani akatulia ghafla akamuangalia aliyemgusa uso wake ulitua kwenye funguo za mlangoni zilizokuwa zikining'nizwa na mkono wa kike  kuashiria alitakiwa azichukue. Alipomuangalia mtu  aliyeshika funguo hizo aligundua ni mmoja wa wafanyakazi wa nyumba yake, hapo ndipo akili yake ikarudi kawaida akakumbuka kwamba aliwatuma kuleta funguo hizo.



Kuletewa  kwa funguo hakukumfurahisha na ndiyo kwanza kulizidi kumtia hasira zaidi, alimtazama mfanyakazi huyo kwa  jicho lake jekundu lenye kutangsza hasira za wsziwazi. Wekundu wa jicho hilo ulizidi kuleta hofu kwa mfanyajazi huyo, mfanyakazi huyo hakuuona utofauti wa rangi uliopo katika jicho hilo na nyanya ambazo amezoea kuzikatakata kutengeneza mboga. Tofauti ya wekundu huu ulikuwa ukimtisha na wa nyanya haukuwa ukimtisha, Dokta Hilary naye aliendelea kumtazama mfanyakazi wake huyo wa kike kwa muda wa sekunde kadhaa kisha akaachia msonyo mzito sana.



          "Bloody fool! Sasa unanionesha funguo katika uso wangu ili iweje? Kuna tundu la funguo uweze kufungua mlango, haya utie kwenye tundu la pua ufungue mlango" Dokta Hilary aliongea kwa hasira huku akimtanulia tundu la pua mfanyakazi wake autie ufunguo huo, mfanyakazi alizidi kutetemeka kwa uoga akawatazama wenzake ambao walikuwa sebuleni hapo kwa uoga.



 Wenzake walimuashiria akaufungue mlango mkubwa kwa haraka naye alifanya hivyo akiwa anatetemeka sana, aliufungua mlango huo kwa hofu kubwa sana kwa kukosea kutumbukiza funguo kwa zaidi ya mara nne.



 Mara ya tano mlango ulipofunguka aljikuta akienda chini baada ya kukumbwa na kukumbo kizito kutoka kwa Dokta Hilary hadi akaanguka chini, gauni fupi alilovaa liliweka mambo hadharani kwa wafanyakazi wenzake ambao ni jinsia moja na yeye pamoja  kadamnasi ya samani iliyopo sebuleni. Wafanyakazi wenzake walienda kumsaidia kumuinua haraka kisha wakakimbilia nje alipokimbilia bosi wao baada kumkumba kikumbo, walimkuta Dokta Hilary akiwa anayaangalia magari yake ambayo hayakuwa na upepo kwenye matairi hadi muda huo kutokana na kutobolewa matairi.



   Dokta Hilary alikaa chini  akiwa anapiga makelele kwa hasira sana huku akiwa amechanganyikiwa, alikuja kuguswa begani tena na mfanyakazi wake mwingine.



             "Bo...bosi Professa Gawaza anapiga simu" Mfanyakazi huyo alimuambia Dokta Hilary huku akibabaika kutokana na hasira alizomuona nazo, simu hiyo kwa mara nyingine ilimrudisha Dokta Hilary katika hali ya kawaida. Aliipoikea simu hiyo  kutoka kwenye mikono ya mfanyakazi wake, aliiweka sikioni kisha akaanza mashambulizi ya makombora bila hata kushambuliwa yeye.



              "Moses you are an idiot (Moses wewe ni mjinga)!  Kwa ujinga wako mke wangu ametekwa na wanajeshi na kwa upumbavu wako wewe nabaki nataabika........ nikusikilize kwa lipi Moses nitakalokuelewa.......nini? Ngoja" Dokta Hilary aliongea kwa hasira kisha akaikata simu akairudisha mikononi mwa mfanyakazi wake.



              "Asitoke mtu" Alisema kisha akatimua mbio pekupeku mpaka getini, alimuamuru mlinzi amfungulie geti na ye alitii akamfungulia.

MWANZO WA ALFAJIRI.

   Wanajeshi wa jeshi la wananchi (JWTZ) wakati wanapanga mikakati yao juu ya kumtia mikononi Moses hawakujua kama idara ya usalama wa taifa iliyopo chini ya Moses ilikuwa ina vibaraka katika sehemu zote za nchi hii. Ndani ya jeshi hilo pia vibaraka wa usalama wa taifa katika kulinda usalama wa nchi kwa kutoa taarifa muhimu walikuwepo bila ya wanejeshi wenyewe kujua, wakati mpango huo ukipangwa mwanajeshi mmoja mwenye cheo cha Koplo anayeaminika sana kwa ulengaji shabaha alihusishwa kutokana kuhitajika  sehemu kama hiyo.



 Hawakujua kama mwanajeshi huyo alikuwa yupo katika idara ya usalama wa taifa  na amepachikwa jeshini hapo kwa kazi maalum kama hizo, wakati mkutano ukiendelea Koplo huyo aliipiga namba ya Moses kisha akaiacha hewani bila wenzake kujua. Wakati wakiendelea mazungumzo tayari  mpango wao wote ulifika kwa Mosea bila wao kujua, katika mpango huo Afisa mteule daraja la pili aliyeongoza kumkamata Irene alimuita Koplo huyo kibaraka wa TISS na kumuambia juu ya kiini cha mpango huo ni kumteka Irene mke wa Dokta Hilary.



 Wakati wanaondoka kulekea nyumbani kwa Dokta Hilary tayari Moses alishafika jirani na maeneo ya nyumbani kwa Dokta Hilary, wakati wanaingia ndani ya nyumba hiyo Moses alikuwa ameshawaona na tayari aliandaa mtego mwingine utakaomuwezesha kumtoa Irene. Makazi ya Dokta Hilary yalikuwa yapo mtaa wa Flamingo huko Mbezi  beach na njia waliyoitumia wanajeshi hao kufika hapo tayari Moses aliijua na alienda kuwawekea mtego, wakati wanajeshi hao wanatoka walitumia nia ilele waliyokuwa wamekuja nayo.



 Walipita kwenye mtaa wa Busara  kisha wakafuata mtaa wa Hekima wakawa wanaelekea  kwenye barabara ya Mbaraka Mwinshehe, hawakutambua mitaa kadhaa hapo mbele yao Moses alikuwa akiwangojea kwa hamu sana na walipofika kwenye anga za Moses ghafla mipira ya matairi ya gari lao ilipasuka yote. Hapo walisimamisha gari wakashuka kwenda kuangalia kile kilichotokea hadi matairi yao yakapasuka, hawakutambua kama kushuka kwao walikuwa wamefanya kosa kubwa jingine zaidi hata ya kosa kuliko kosa la awali la kupita katika njia hiyo.



 Kitendo cha wao kushuka chupa nne zenye umbile kama chupa ya dawa ya mbu zilitupwa, hawakuwa wamezutambua kwa haraka zile chupa zilikuwa za nini kutokana na ufinyu wa mwangaza wa Alfajiri na hata walipokuja kuzitambua tayari walikuwa wamechelewa.



 Moshi mzito wenye kemikali uliwavamia kwenye macho yao pamoja na kwenye pua zao wakabaki wakikohoa sana huku macho yakiwawasha, waliishiwa nguvu kwa kukohoa huko kutokana na gesi nzito iliyokuwa imevamia, ulipokuja kuondoka moshi huo tayari Irene hakuwa katika mikono yao na  hapo ndipo wakauona ubao wenye misumari uliokuwa umetegeshwa barabarani ambao ndiyo uliotoboa matairi yote ya gari. Walibaki wakijilaumu tu kutokana na kushindwa kutekeleza kazi na wakawa na hofu sana juu ya uzembe huo, walipojitazama idadi yao ndiyo walizidi kuchanganyikiwa kwani yule Koplo kibaraka wa usalama wa taifa hakuwepo kati yao.















   (2)UTEPE

Mapambazuko ya siku mpya ya jumamosi tayari yalishashika nafasi yake kwa kuvizishwa kwa mpango wa kutaka kumtia mbaroni Moses, baada ya jua kuchomoza kwa upande mwingine katika hoteli ya New Avon Norbert alitoka akiwa na Jospehine wakaenda kupata kifungua kinywa wakiwa pamoja. Majira ya saa tano asubuhi yalipotimu Josephine alimuaga Norbert akimuacha hapo kwenye mgahawa akaondoka, alitumia usafiri wa teksi akapotea kwenye upeo wa macho ya Norbert huku akimuacha Norbert akiwa na mengi yaliyomfanya aendelee kuketi hapo kwenye mgahawa.

 Hapo aliamua  kuitoa simu yake na akaweka sauti zilizojirekodi akazisikiliza kwa umakini hadi akazimaliza, fikra ya utambuzi juu ya jambo jingine ndiyo zilifuata na hakuona umuhimu wa yeye kubaki hapo. Alinyayuka kitini kwenye mgahawa huo akarudi alipoliacha gari lake kwenye maegesho jirani na hoteli ya New Avon, hakutaka kupoteza ilimbidi aondoke eneo hilo kwa haraka sana. CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



 Aliingia ndani ya gari lake na kabla hajawasha kioo cha gari lake kiligongwa na ikamlazimu kushusha baada ya kumuona msichana mrembo aliyevaa kisasa zaidi, kioo kilipmalizika kushushwa alipokelewa na tabasamu pana zaidi kutoka kwa msichana huyo mwenye umbo matata na mrefu. Norbert alijikuta akimtazama msichana huyo kwa kiusanifu zaidi kisha akatingisha kichwa akiwa na tabasamu, alipomtazama msichana huyo mwenye sura inayofanana kwa kiasi kikubwa na wasichana kutoka nchi  ya Rwanda alijikuta akimkumbuka jasusi mwenzake Hilda Alphonce waliyefanya naye kazi kwenye JINAMIZI na SHUJAA pamoja na visa vingine.



Alitoa tabasamu lililomfanya hata binti huyo amshangae kwani hakuwa akimuelewa, alibaki akimtazama kisha  akatazama pembeni kuonesha kuwa ana aibu lakini kimtazamo wa Norbert aliona kuwa ilikuwa ni aibu geresha.



             "Habari yako kaka yangu" Alimsabahi Norbert.



            "safi mdada za kwako?" Norbert aliitikia.



            "safi tu, samahani kaka yangu sijui unaelekea wapi?" Aliuliza huku akiabza kujiumauma



            "Naelekea Keko mdada" Norbert alimjibu.



           "samahani kwa usumbufu kaka yangu" Alisema.



           "bila samahani mrembo" Norbert alimuambia



           "nahitaji nifike hapo Sofia House Keko nimesahau handbag yenye pesa yangu kwenye appartment niliyopanga" Alisema.



          "si vibaya nikakusogeza mdada , ingia kwenye gari" Norbert alimuambia, binti huyo bila kuchelewa aliingia kwenye gari akiacha sehemu zake za nyuma zikifanya fujo  ambayo ilionekana wazi kwa Norbert. Huo ulikuwa ugonjwa wake wa kupenda wanawake wenye maumbo tata pamoja na wenye sura nzuri, lakini kwa binti huyo kila akilitazama umbo lake vinyweleo vyote vilimsisimka.



 Suruali  ya kahawia yenye  kubana iliyombana kisawasawa binti huyo hadi nguo ya ndani ikaonekana bado haikumletea mvuto Norbert kwani moyo wake ulisita kabisa kuvutika naye. koti la suti akilolivaa kwa juu ambalo lilkuwa limeifunika shati ya kubana aliyoiachia sehemu ya kifuani wazi bado haikuwa imemletea mwenyekiti wa mwili wa Norbert usumbufu. Norbert alijihisi yupo tofauti na siku zote kwani hakuwa amevutiwa na mwili huo wa msichana mrembo, ushawishi wa matamanio yake  juu ya mrembo hayakuwepo kabisa. Hadi muda huo tayari mrembo huyo alishaketi ndani na alifunga mkanda, Norbert aliwasha gari kisha akaliingiza barabarani.



               "Janet, nani mwenzangu" Binti huyo alijitambulisha huku akimpatia mkono Norbert.



               "Kaila au Norbe.."



               "ohoo! Norbert Kaila ndiyo wewe, mwndishi wa habari maarufu wa kujitegemea"



               "Hujakosea"



              "Basi nafurahi kukufahamu ila nahitaji kukufahamu zaidi"



             "kiaje yaani sijakuelewa"



            "Kama hivi ujitambulishe  vizuri mbele ya rafiki" Janet alipoongea hivyo Norbert alihisi akiguswa na kitu cha baridi sehemu ya kwenye mbavu wakati mikono yake ikiwa kwenye usukani, alipoangalia eneo hilo aliiona bastola isiyo na kiwambo cha kuzuia sauti ikiwa imegusa sehemu ya mbavu.



           "IMI DESERT EAGLE original kutoka kwa Israel ndiyo hii siyo  ile ya Marekani, ukileta ujinga kidogo tu nacharanga mbavu zako hadi kwenye moyo hii" Janet alimuambia Norbert huku akiwa ameweka uso wa tabasamu.



           "Pandisha vioo tafadhali usihitaji nikumalize mapema watu wakipata faida kutoka kwetu"  Janet alimuambia Norbert ambaye alitii bila kupenda akapandisha  vioo, Norbert alijua alikuwa amekamatika kwani hakuwa na uwezo aa kumfanya chochote Janet.



  Aliwaza aongeze  mwendo halafu akanyage breki kwa ghafla lakini hiyo isingesaidia kitu, Janet alikuwa amejifunga mkanda hivyo angekanyaga breki za gari kwa ghafla mkanda ungenasa kumzuia asiende hivyo asingemfanya chochote na ingekuwa ni nafasi tosha kwa Janet kufumua mbavu zake kwa bastola hiyo yenye uwezo mkubwa.



  Alikuwa akiitambua  IMI Desert eagle uwezo wake hivyo hakutaka kuleta ubishi hata kidogo kuepuka kuleta makuu, alishikilia mikono yake kwenye usukani wa gari akijua amekamatika kabisa na hakupata nafasi yoyote ambayo angeitumia kama kosa la kuweza kumuokoa.



            "Nenda Mwembeyanga moja kwa moja"  Janet alimuambia Norbert kisha akaanza kuutembea mkono wake wa pili katika  eneo la zipu ya Norbert. Alipapasa eneo hilo kwa tararibu sana kwa mikono yake huku akimtazama Norbert, hakuridhika na hapo akafungua zipu ya suruali yake akatia mkono ndani juu ya nguo ya ndani akazidi kumpapasa hadi mwenyekiti akaleta fujo hafifu kutokana na mawazo ya Norbert kuwaza umauti tu ndiyo ulikuwa unamkabili.



           "Kumbe na wewe muoga sana mbona huyu aliyenitamani siku ile tulipokutana klabu Bilicanas hadi ukanitongoza kwenye parking ya magari leo hii mnyonge" Janet aliongea  huku akimtazama Norbert ambaye akili yake iliwaza kujiokoa tu na siyo suala jingine ndiyo maana mwenyekiti aligoma kujitambulisha kiufasaha ndani ya suruali yake, hapo alipoambiwa maneno hayo na Janet ndiyo kumbukumbu za siku nyingi zilizopita hata kabla mabalaa hayo hayajaanza alipokutana binti aliyemvutia sana akamtongoza kwenye maegesho ya magari klabu ya usiku ya Bilicanas.



           "Dorene" Norbert aliongea kwa taratibu huku  akimtazama Janet kwa jicho la kuibia.



           "Ulinifahamu kwa jina hilo lisilo halisi na leo umenifahamu kwa jina jingine lisilo halisi, kiuhalisi niite Leopard Queen  member of Cats Kingdom" Kwa mara ya kwanza alijitambulisha jina lake analolitumia ambalo lilimfanya Norbert arudishe mawazo siku ile aliyokuwa ametekwa na Cats kingdom wakiwa chini ya Panthers, alilikumbuka umbile la mwanamke aliyekuwa amevaa kinyago cha paka na hapo akabaini ndiye huyu aliyekuwa anaongea  naye. Moyoni alijilaumu kwa kuchelewa kumkumbuka hadi anaingia kwenye mtego wake, aliitukana tusi halmashauri ya kumbukumbu kwa kushindwa kumbukumbu haraka hadi amenasa kwenye mtego.



          "Kama nilivyokuambia leo tutafahamiana vizuri zaidi, nilikuwa nangojea nafasi hii adimu tangu unaingia na malaya wako pale mgahawani. Ngoja tufike tutafahamiana zaidi then Quantanise itakuondoa kama ilivyowaondoa wengine, nataka ujue hakuna wa kutuzuia hata N001 mpelelezi wa daraja la kwanza tunayemsaka tumuangamize kabla hajaanza yeye"  Leopard Queen aliongea kwa dharau  pasipo kutambua N001 anayemzungumzia ndiyo huyo yupo aliyemtia nguvuni, alikuwa akimtambua Norbert kama mwandishi wa habari mjanja anayelindwa na wanausalama  lakini hakumtambua kama huyo ndiyo mpelelezi wa hatari wanayemsaka kabla hajaanza kazi.



           "Hongereni" Norbert aliwapongeza huku akiachia tabasamu mithili  ya mtu aliyepo kwenye eneo lenye amani.



          "Norbert Kaila wewe mfu tayari tuone zile ngumi zako ulizojifunza ili ujilinde kwa ufichuzi wako utazitumia mbele ya Leopard Queen ukiwa umetoka kumtumia huyu bwana kwa yule mfanyakazi wa bandari" Leopard Queen huku akimchezea mwenyekiti wa mwili wa Norbert kwa madah, hazikupita dakika kumi na tano mwenyekiti huyo aliamka usingizini akainyanyua nguo ya ndani  ya Norbert akiomba afunguliwe.



         "Wooow! Kaamka leo namdunga Quantanise yeye" Leopard Queen aliongea na muda huo tayari walikuwa wameshaingia Mwembeyanga Temeke, alimuelekeza Norbert aende hadi kwenye geti la Ghala moja lenye maandishi yalisomeka 'Nourhern brothers warehouse'. Hapo aliamriwa apige honi na alipiga honi geti likafunguliwa, Norbert aliingiza gari ndani na geti likafungwa tena na mwanaume mwenye mwili wa  kimazoezi.



         "Shusha kioo" Leopard Queen alimuambia, Norbert alishusha kioo na hapo mdomo wa bunduki ukapenya ndani ya gari ukagusa kichwa chake.



  Leopard Queen alishuka ndani ya gari akazunguka upande wa dereva dirishani akamnyooshea bastola Norbert huku mwenye bunduki akiishusha chini akasogea pembeni, Leorpard Queen alimuamuru Norbert ashuke lakini alisita baada ya kusikia honi ya pikipiki kwa nje.



            "Gasper ni nani huyo anayepiga honi" Leopard Queen alimuuliza yule mwaneume aliyewafungulia geti ambaye alikuwa peke yake ndani.



                  "Madam ni mleta tenki nafikiri una habari ya kuletwa kwa tank mpya ya maji kwani ile ya zamani imetoboka" Gasper aliongea.



                  "Ok ficha silaha umfungulie aingize tenki upande wa kushoto kwenye parking ya malori" Leopard alimuambia Gasper ambaye alikimbia upesi akaenda kufungua geti, muda huo Leopard Queen alikuwa amemuwekea bastola Norbert akijua amemdhibiti kumbe tayari walishafanya kosa.



                   "Golden chance" Norbert alijisemea moyoni huku akitazama kwa jicho la kuibia kwenye kioo cha pembeni akaiona pikipiki aina ya Toyo yenye matairi matatu ikiwa imebeba tenki kubwa la kuhifadhia maji la lita 2000, muda huo gari ya Norbert ambalo amepewa kwa kazi hizo lilikuwa limewekwa mfumo wa automatic(moja kwa moja) na gia yake ipo herufi D (drive). Ushindi wa kukwepa mdomo wa mamba aliuona unakuja na hapo akaachia breki za gari makusudi, gari yake ilisogea mbele na kusababisha Leopard Queen amkazie macho kwa hasira.



                 "We! We! We! Weka gia hiyo kwenye  P parking haraka" Leopard Queen  alimuamrisha kuweka parking  pasipo kutambua kuwa alikuwa anafanya kosa kubwa sana kumuambia afanye hivyo, mfumo wa automatic wa gari upo mpangilio P-R-N-D-2-L.



   Mfumo huo huwezi kuweka P ambayo ni parking bila kuivuka  R ambayo ni  reverse yaani gia ya kurudi nyuma, Norbert alipoona geti lililofunguluwa lipo usawa wake alirudisha gia kama anaipeleka parking na alivyofika R alifanya kitu ambacho Leopard Queen hakutarajia kama anaweka kukifanya kwa muda huo . Kwa kasi ya ajabu alikanyaga mafuta akaachia breki akarudisha gari nyuma kwa nguvu sana akamuacha Leopard Queen akipiga risasi zilizoishia kwenye kioo chake cha gari kisichoingia risasi, alienda kuigonga ile pikipiki matairi matatu akaitoa hadi nje kutoka pale getini ikarushwa umbali wa mita kadhaa kutoka geti liliopo na hapo akaweza kutoka nje ya geti hilo.

Alirudi nyuma kwa kasi sana kisha akageuza gari kwa namna ya ajabu, aliweka gia ya kwenda mbele akatimua vumbi akimuacha Leopard akiwa ametoka nje ya geti akibaki haamini alichokifanya na hata kupiga risasi alishindwa kutokana na sauti ya bastola hiyo kuleta kizazaa katika eneo hilo. Hakuweza kuamini kama Norbert angeweza kumponyoka namna ile akiwa yupo usawa wa mdomo wa bastola yake, hasira zilimpanda zaidi Leopard Queen na alisonya kwa nguvu akaachia tusi zito sana.

 Aligeuka upande ilipo ile Toyo iliyoleta tanki hakumuona dereva wake na wala hakujua ni wapi alipo, pande zote zilizo katika usawa wa macho yake hakuweza kubaini unekano wowote wa dereva huyo aliyetumwa tenki la maji. Leopard Queen alichekecha akili yake kwa haraka sana kisha akapaza sauti, "Gasper!"



     "Madam" Gasper aliitikia kwa upesi sana.



     "ulikuwa wapi hadi huyu anatutoroka?" Leopard Queen aliuliza.



     "Madam niliweka silaha mbali halafu niliruka  pembeni,  angenigonga na mimi" Gasper alijieleza.



      "Ok! Ingiza hiyo Toyo ndani na umfuatilie huyu dereva upesi sana asije akaleta polisi hapa, tumeelewana?!" Leopard Queen aliongea kwa nguvu.



        "Madam" Gasper aliongea na kwa haraka sana akaiendea ile pikipiki, Leopard Queen aliingia mule ndani ya ghala akaketi jirani na  kibanda cha ulinzi bado akiwa haamini jinsi alivyotorokwa na Norbert.



Alibaki akijiuliza Norbert ni nani kwani hakuwa amemtambua hadi muda huo kabisa, uwezo wa Norbert wa kufikiri kwa haraka ulimfanya ahisi hakuwa mwanadamu wa kawaida hata kidogo hasa kwa jinsi walivyomkosa kwa mara mbili tofauti akiwa yupo chini ya mikono yao. Alizidi kuwaza juu ya uhalisia wa Norbert lakini hakupata jibu hata kidogo, haikuwa kawaida kwa mwandishi wa habari wa kawaida akombolewe na mtu aliye na mbinu za kijasusi siku ile walivyomteka.



Haikuwa kawaida kwa mwandishi asiye na ujuzi wowote wa kijeshi au wa kijasusi aonekane katika  katika hali ya kawaida wakati amewekewa bastola ubavu mwake, hamu ya kutaka kumjua Norbert ilipanda zaidi baada ya kukumbuka kitu kingine kilichomtia wasiwasi zaidi. Hapo wasiwasi wake dhidi ya Norbert ukamzidi na akajikuta anataka kufanya kitu ili wasiwasi huo umpungue, hakutaka kupoteza muda aliingia ndani ya chumba kidogo kilichopo ndani ya ghala hiyo akakaa kwa muda wa sekunde kadhaa na alipotoka alikuwa yupo katika muonekano mwingine kabisa wa kisura na hadi umbo.



Alikuwa amebadili sura kuvaa nyingine ya bandia, aliporudi aliikuta ile pikipiki ikiwa tayari imeingizwa ndani na Gasper tayari alikuwa ameshatoka kwa mara nyingine. Alitabasamu kwa kufurahishwa na wepesi  wa Gasper kisha akaiendea ile pikipiki, alibaki akiitazama kila mahala hasa katika eneo la mbele lililokuwa limeharibika vibaya  baada ys kugongwa na gari ya Norbert.



 Hasira za kutorokwa kwa Norbert zilimpanda zaidi na alajikuta anaipiga teke pikipiki hiyo isiyo na hatia kabisa katika suala hilo, hakika alikuwa amechezewa akili kwa namna asiyopenda yeye kuchezewa akili na mtu ambaye hakumdhania kama angeweza kumfanyia hivyo. Alijiona kafanywa mjinga sana na Norbert kwa namna alivyomtoroka na hata akimueleza Panther yoyote kati yao atalaumiwa, alizidi kujilaumu  kwa kumuarisha Norbert asimamishe gari katika eneo ambalo lipo usawa wa geti la kuingia humo ndani ambalo limemfanya atoroke kwa urahisi sana.



  Lawama za nafsi yake zilizidi kumtafuna lakini zilishindwa kummeza baada ya kusikika mlio wa gari ya toyota landcruiser ikisimama mlangoni  hapo, vishindo vya watu wakishuka ndani ya gari hilo vilifuata  ambavyo vilfanya atazame kila upande kwenye eneo hilo la uzio wa ghala kisha akaenda kujibana baada ya kusikia vishindo vya watu vikikaribia  getini.

Baada  ya kuwakimbia  wabaya wake Norbert alienda moja kwa moja Temeke nyumbani kwake ambapo aliingia ndani akabadili nguo, alijipamba kwa silaha za kijasusi zisizoonekana katika sehemu mbalimbali za mwili wake. Alikuwa yupo tayari kuingia kazini lakini utayari wake ulimezwa sauti ya simu yake ya mkononi ambayo iliita aliipokea baada ya kumbaini mpigaji, ilikuwa ni simu ambayo haipigwi pasipo kuwepo na dharura hata siku moja.



Norbert aliipokea simu hiyo kutoka tawi la EASA ambapo ilimpa habari za kuhitajika ofisini hapo mara moja, Norbert hakutaka kupoteza muda aliamua kuingia ndani ya gari nyingine akaondoka kuelekea  huko alipohitajika.





 Nusu baadaye gari aina ya Toyota Noah ilionekana ikiegeshwa kwenye maegesho ya magari katika hoteli maarufu iliyopo Ilala mtaa wa Lindi, mlango wa dereva  wa gari hilo ulionekana ukifunguliwa na Norbert alionekana akishuka. Alikuwa amefika kwenye jengo la hoteli ambalo ni makao ya siri ya shirika la kijasusi la Afrika ya mashariki(EASA), aliingia ndani ya eneo la mapokezi la hoteli hiyo akiwa kama mtumiaji hoteli hiyo. Kituo cha kwanza kukifikia ilikuwa ni mapokezi ambapo alikuta wasichana watatu warembo wakiwa wamekaa katika dawati la mapokezi,  Norbert aliwafuata wasichana hao wakiwa na tabasamu kubwa ambapo nao walipomuona walitabasamu pia.



       "Kijogoo naona leo umetukumbuka" Msichana aliyepo katikati ya wenzake wote alimuambia



        "Siyo nimewakumbuka Hidaya sema ninawakumbuka nitaendelea kuwakumbuka wake zangu" Norbert aliongea huku akitabasamu.



           "Loh! Huna haya nani mke wako wewe" Msichana aliyekuwa yupo pembeni ya Hidaya kwa upande wa kushoto alidakia na kusababisha Hidaya acheke kwa nguvu, wote kwa pamoja walicheka kicheko cha kike wakagonganisha mikono yao.



          "Basi poa kama sina wake ngoja nikaonane na meneja   kuhusu mkataba mpya wa matangazo ya hoteli, haya warembo nikitoka nitatafuta mke mwingine" Norbert alipngea huku akianza kuondoka na kusababisha Hidaya amzuie.



          "Nor bwana na wewe hutaniwi" Hidaya aliongea kwa kudeka lakini Norbert alimtoa mkono baada  ya simu yake kuanza kutetemeka mfukoni mwake.



         "Tutaongea nikirudi wacha kwanza nikaongee kuhusu mkatsba" Norbert alimuambia kisha akapiga hatua kuifuata lifti ya ghorofa hiyo ambayo ilikuwa imejitenga peke yake, aliingia ndani ya lifti akiwaacha wasichana hao ambao walijua alikuwa anaenda kuonana na Meneja wa hoteli.



Haikuwa hivyo bali alikuwa  anaenda ofisini  ambapo alihitajika na mkuu wa kazi, wafanyakazi wote wa hoteli hiyo hawakuwa wakifahamu juu  ya uwepo wa  makao madogo ya EASA  ndani ya jengo hilo zaidi ya meneja wa hoteli hiyo ambaye ndiye mkuu wa kazi wa Norbert. Kuonekana kwa Norbert eneo hilo ilikuwa kunatambulika kama yupo kwa kuonana na Meneja wa hoteli  hiyo kwani alikuwa akionekana kwa mara chache sana, siri ya ofisi hiyo ilikuwa ipo miongoni mwa watu wachache sana wenye kuaminika ambao waliweza kuitunza siri hiyo.



 Norbert alipoingia ndani ya lifti hiyo alibonyeza sehemu ambayo haijulikani kama kulikuwa kuna kitufe cha kubonyeza, lifti hiyo ilianza kushuka chini taratibu kwa kiasi cha urefu wa ghorofa mbili kisha ikafunguka baada ya kufika eneo husika. Norbert alitoka ndani ya lifti hiyo akatokea sehemu yenye korido ndefu ambayo ilimpeleka hadi kwenye mlango  ambao unafunguliwa kwa kuweka alama za kiganja, aliweka kiganja chske sehemu hiyo na taa ya rangi ya kijani iliyopo juu ya mlango ikawaka mara moja kisha ikazima.



          "Karibu N001" Sauti maalum ya kutengenezwa  kwa mitambo ilisikika kisha mlango huo ukajifungua, Norbett aliingia ndani na mlango ukajifunga tena.





Alitokea katika eneo lenye vyumba vingi vya ofisi kukiwa na watu tofauti wakifanya kazi humo, Norbert alizipita ofisi hizo akaenda kwenye mlango ulioandikwa CE ambao ulikuwa wa kitasa cha kawaida. Aliufungua mlango huo akaingia akapita moja hadi katika ofisi ya Katibu Mukhtasi, hapo alimkuta Norene akiwa yupo makini na kioo cha tarakilishi.



      "Mama watoto nimekuja" Norbert alimuambia Norene ambaye hakujibu chochote zaidi ya kumuonesha upande ilipo kamera ya ulinzi iliyounganishws na ofisi ya CE ambaye anaona kila kitu kinachofanyika hapo.



       "Vipi mbona nimeitwa ghafla tu?" Norbert alimuuliza.



       "Hilo la kukueleza sina mamlaka nalo nenda kwa mkuu mwenyewe, anakusubiria kwa hamu sana" Norene alimuambia Norbert ambaye aliishia kujishika kiuno chake kisha akahema kwa nguvu  sana, hakutaka kupoteza muda aliamua kuingia ofisini kwa CE kwani alikuwa ameshajulikana uwepo wake ofisini hapo.



 Ndani ya ofisi ya CE alimkuta akiwa amekati kwenye kiti chake akiwa na faili kubwa mezani, alitoa salamu kisha akaketi kwenye kiti baada ya kuamriwa afanye hivyo na CE ambaye alionekana na jambo lililomfanya amuite hapo.



      "N001" CE aliita kisha akampatia picha Norbert kisha akaendelea, "Jack Shaw ndiyo jina lake huyo kiongozi wa genge hatari la ualifu kutoka Ujerumani.  Kwa mujibu wa taarifa zilizopo katika ofisi hii huyu mtu  anaingia Tanzania saa tisa alasiri leo hii katika ndege  ya shirika la Qatar ambayo atakuja nayo Askofu Achim Valdermar kutoka kanisa kuu la kiluteri akija kuhudhuria maziko ya Askofu Edson yatakayofanyika mapema kesho. Ujio wa mtu hatari kama yule kutoka taifa la mbali huenda upo kwa namna au anataka kufanya jambo baya, mtu huyu ameonekana uwanja wa ndege wa Cairo lakini amepotea katika mazingira ya kutatanisha. Kwa mujibu wa taarifa za wazi ni kwamba mtu huyo anataka kuazimia jambo baya kwa Askofu Valdermar akiwa huku ndani ya Tanzania kuja kuhudhuria mazishi ya rafiki yake kipenzi, N001 nataka uwaoneshe Tanzania siyo uwanja wa kufanya uhalifu. Hakikisha Askofu Valdermar anaingia salama na anaondoka salama bila mtu yoyote kutambua kama wewe upo kwa ajili ya kazi hiyo, huyu mhalifu akikamatwa nafikiri wengine wenye akili kama zake watakuwa wamepata ujumbe kwamba EASA wapo makini kuilinda Afrika ya mashariki. Tumeelewana".



      "Mkuu, ila samahani nina ombi moja" Norbert aliongea kwa utaratibu kisha akaendelea baada ya CE kumruhusu aongee, "Ndani ya wiki hii kumetokea vifo  viwili vya viongozi wa dini pamoja na General Kulika wote  wakifa kwa namna moja kwa sumu ya Quantanise ambayo hadi sasa imemtia doa Gawaza ambaye ni mmoja wetu, uchunguzi binafsi wa jambo hilo nimefikia hatua nzuri katika kuzifikia nyayo za muhusika. Ujio wa kazi mpya utazorotesha ya zamani, hivyo ninaomba nizifanye zote kwa pamoja".



      "Kwanza nikupongeze kwa kuamua kujitosa kwenye uchunguzi bila ridhaa ya ofisi  ingawa taarifa tayari zipo kwa ajili ya kufanikisha usalama wa nchi, upo huru kuendelea ila sitaki viza na kama unajua moja itaviza acha moja tumteue N002 ambaye yupo ana kazi ndogo tu" CE aliongea.



      "Tarajia mazuri kutoka kwangu" Norbert aliongea.



       "Ok unaweza ukaenda   hakikisha Askofu Valdermar aje na aondoke salama na pia wahalifu wakamatwe, sitaki ubaki kwa mkeo asiye rasmi Norene sasa hivi uwahi uwanja wa ndege tena umwambie Gawaza asionekane katika public areas hadi kazi ikamilike" CE alitoa amri, Norbert alinyanyuka kwenye kiti akatoa heshima akaondoka.

SAA TISA ALASIRI

UWANJA WA NDEGE WA NDEGE WA MWALIMU JULIUS NYERERE

 Ndege kubwa ya shirika la ndege la Qatar aina ya Airbus 330-300  ilionekana ikishuka kwa mwendo wa kasi katika ardhi ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, matairi yake yalipogusa ardhi ilianza kukimbia na hatimaye ikasimama kwenye  eneo maalum la kusimama kwa ndege. Ulinzi katika uwanja huo wa ndege ulikuwa umeongezwa mara dufu kutokana  na ujio wa Askofu Valdermar,  mapokezi yake yaliongozwa na wakuu mbalimbali wa kanisa la Kiluteri Tanzania pamoja na  makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



 Mtu mwenye asili ya kizungu aliyevalia nguo ndefu nyeupe yenye ukosi mnene na kikoti kirefu cha kahawia alionekana akitoka ndani ya ndege hiyo huku akipunga mkono, wapokezi wake kutoka srrikalini pamoja na kanisa la kiluteri walipiga makofi kumkaribisha. Askofu Valdermar  ndiyo alionekana mbele ya wageni wake waliokuwa wakimsubiri awasili hapo, alishuka taratibu kwenye ngazi za  ndege hiyo na alipofika chini akaanza kusalimiana na viongozi mbalimbali wa kidini na wa kitaifa waliojitokeza katika mapokezi hayo ya kiongozi huyo mkubwa wa dini kutoka Hamburg Ujerumani.



 Ulinzi katika uwanja huo uliimarishwa zaidi  kwa kutumia ulinzi wa kudhihirika na macho ya watu na usiodhihirika na macho ya watu wa kawaida isipokuwa wenye ujuzi wa hali ya juu, ulinzi usiodhihirika na macho ya kawaida ulikuwa ukiwakilishwa na Norbert akiwa yupo katika muonekano tofauti kuanzia sura hadi mavazi.



 Hakuwa tofauti kimavazi na wawakilishi wa kanisa la KKKT ambao walikuja kumpokea Askofu Valdermar, msafara wa Askofu Valdermar hadi unaondoka uwanjani hapo Norbert alikuwa tayari amekuwa karibu na askofu huyo hadi kufikia kuwa katika msafara huo. Hakuna aliyekuwa amejua kwamba ndani ya msafara huo kulikuwepo majasusi wawili hatari wenye itikadi tofauti  kutoka ardhi tofauti, mmoja tayari alikuwa ameshatambulika na kalamu ya mwandishi kuwa ni Norbert aliyevaa sura ya bandia pasipokutambulika na waliomo ndani ya msafara huo.



 Jasusi mwingine ambaye tayari alikuwa ameingia kwenye msafara huo hakuwa ametambulika, msafara huo uliishia katika hoteli ya Kilimanjaro iliyopo kata ya Magogoni ambapo askofu huyo ilihitajika apumzike kabla hajajianda kuongoza ibada ya kuuaga mwili wa Askofu Edson siku inayofuata. Ulinzi katika hoteli hiyo nao uliimarika maradufu na bahati nyingine ikamuangukia Norbert ambaye aliteuliwa kuwa mtu wa karibu atakeyekuwa na Askofu Valdermar katika kipindi chote hadi anaondoka nchini, Askofu Valdermar alivutiwa sana na Norbert hadi akapenda kuwa naye karibu, hakika hakutambua kabisa kwamba alikuwa anatimiza malengo ya Norbert zaidi ya kujali yeye kutimiza malengo yake aliyoyajua mwenyewe tangu anamuona Norbert kwa mara ya kwanza pale uwanja wa ndege akiwa yupo katika kundi la watumushi wa Mungu waliokuja kumpokea.



 Majira ya saa kumi hadi  saa kumi na mbili hoteli hiyo ilikuwa ikiingia viongozi mbalimbali wa kikanisa na wa kitaifa waliokuwa wamekuja kumsalimia kiongozi huyo, Norbert alikuwa ameteuliwa kukaa pembeni ya Askofu  Valdermar akiwa yupo sambamba na watu wawili waliovaa mavazi ya watumishi ambao walifika pamoja na Askofu Valdermar. Majira ya jioni kwenye machweo ya jua Askofu Valdermar aliaga kwenda kupumzika chumbani kwake hotelini humo, Norbert hakuwa mbali  alikuwa akilala chumba cha pembeni yake huku akiwa makini katika kulinda usalama wa Askofu huyo. Alikuwa akikaa makini kila muda katika kuhakikusha kuwa Askofu huyo havamiwi, muda mwingine ilimbidi atembee kwenye korido inayotenganisha vyumba ili kuhakikisha usalama wa kiongozi huyo mkubwa wa kiroho unakuwepo.



 Majira ya saa mbili usiku baada ya kiongozi huyo wa kiroho kupata  chakula, alirudi chumbani kwake kupumzika kusubiria siku mpya ianze. Mapumziko hayo yalimfanya Norbert abaini uwepo wa kitu kingine kilichokuwa kimejificha nyuma ya pazi, ni muda ambao aligongewa mlango wa chumba chake na alipofungua akakutana na mmoja wa watumishi aliyekuja nao Askofu



          "You are needed(Unahitajika)" Alimuambia kisha akaondoka, Norbert naye alitoka akaingia katika chumba cha Askofu Valdermar akamkuta akiwa amekaa kwenye kochi akiwa amevua mavazi aliyokuja nayo.



          "Sit down(sit down)" Askofu Valdermar alimuambia huku akitabasamu akimuonedha Norbert mahali pa kuketi karibu na yeye, Norbert aliketi kwa heshima huku akiwa amekaa kwa umakini kusikiliza wito alioitiwa.



           "My son I need your help in this foreign country (Mwanangu nahitaji msaada katika nchi hii ngeni)" Askofu Valdermar aliongea huku akimtazama Norbert usoni.



           "Yes father(ndiyo baba)" Norbert alimuitikia kwa heshima akiwa yupo tayari kuusikiliza wito ws Askofu Valdermar.



          "There is another son like you in the car parking, I received his email(Kuna mwana mwingine kama wewe katika maegesho ya magari, nimepokea baruapepe yake)  Askofu Valdermar aliongea kisha akamtazama Norbert kwa umakini sana, alishusha pumzi kisha akaendelea "Go and take him  secretly, I need to see him. You will find him  in black BMW (nenda ukamchukue kwa siri, nahitaji kumuona. Utampata kwenye BMW nyeusi )".



         "Ok father(sawa baba)" Norbert aliitikia kisha akanyanyuka kiheshima akatoka humo ndani, alienda hadi nje ya hoteli hiyo kwenye maegesho ya magari.



 Haikumuwia vigumu kulipata gari alilokuwa analitafuta ambalo lilikuwa lipi katikati ya gari mbili za kifahari, Norbert aliifuata ile gari ambayo ilikuwa na vioo vya giza na alipofika aligonga katika upande wa dereva. Kioo cha gari hiyo kilishushwa taratibu na mtu aliyekuwa anahitajika amfuate alimuona na hapo moyo wote ukapiga sarakasi ya kificho kwa kumuona mtu huyo ambaye hakutarajia kama ndiye huyo aliyekuja kumfuata, alikuwa ni mtu ambaye hakuwa mgeni ambaye alimuona mara chache tu ndani  ya siku moja. Hakuwa amemsahau mtu huyo ambaye alikuwa amemuona ndani ya siku moja tu ambayo ilitosha ubongo wake kumkariri, mtu huyo alishuka ndani ya gari huku akiwa na tabasamu tele akasalimiana naye.



Alikuwa yupo katika vazi la suruali ya kitambaa  kigumu cha rangi ya kahawia na fulana ya mikono mifupi iliyofanya mkono wake kulia uonekane na kovu la mshono ambao ulizidi kuiamsha akili ya Norbert. Mtu huyo hakumtambua Norbert kutokana na sura ya plastiki aliyokuwa amevaa wala hakutambua kwamba alikuwa ametambulika vizuri na Norbert, alionekana kuwa na uchangamfu kwa Norbert ambaye alimuongoza moja kwa moja hadi ndani kwenye chumba cha Askofu Valdermar akatoka akarudi chumbani kwake baada ya kukamilisha kazi yake sasa akabaki akimfikuria yule mtu ambaye alianza kumuhisi ni mhusika nambari moja wa kifo cha Jenerali Kulika kwani alama aliyokuwa nayo  mkononi ndiyo alama ambaye mtoto mkubwa wa kike wa Jenerali Kulika aliiona kwa muuaji aliyezima taa chumbani kwake akamfungia kwa nje.



 Uhakika zaidi juu ya mtu huyo ulianza kujengeka taratibu katika fikra  zake baada ya kumkumbuka mhusika huyo alikuwa amevaa shati la mikono mirefu kwemye msiba wa Jenerali Kulika  ambalo lilificha alama hiyo, hakika aliona  mhusika mkuu wa tukio hilo tayari alikuwa amempata ilikuwa bado kumtafuta mhusika wa pili mwenye mchoro wa Kipepeo mkononi ambaye hakumjua hadi muda huo.



Alianza kumfikiria juu ya mhusika huyo na akajikuta akikataa kwa nafsi kwamba uwepo wa wauaji wawili siyo, alifikiria namna ya kutoa funguo kwa mkono ambao mgongo wa kiganja utaonekana katika chumba cha Jenerali Kulika na pia katika chumba cha watoto. Jawabu alilolipata  ni kwamba mkono uliotumika kutoa funguo na kumfungia mke wa Jenerali Kulika ulikuwa wa kushoto, mkono uliotoka funguo chumbani kwa watoto wa Jenerali Kulika ulikuwa wa kulia hivyo alijua kabisa muuaji alikuwa mmoja aliyetumia mikono yake yote katika muda tofauti kufanya hayo.



       "Vyumba vilivyopo mkabala haiwezekani kutoa funguo kwa ndani kwa sawasawa kwa kila chumba mgongo wa kiganja kuonekana, natakiwa niangalie mkono wake wa kushoto kama una mchoro nilioambiwa" Norbert aliwaza akiwa amejilaza chali kitandani na mavazi ya kiroho aliyokuwa nayo, ushindi wa kile alichokuwa akikitafuta tangu awali alianza kuuona ukimjia waziwazi.



       "Benson you are the Killer(Benson wewe ni muuaji)" Alijisemea moyoni mwake kisha akakumbuka kutafuta simu yake ilipo kutokana na uhitaji aliokuwa nao katika hiyo simu.

Wakati Norbert akiwa yupo anawaza juu ya upelelezi wake, upande mwingine nyumbani kwa Mfanyabiashara mkubwa nchini Wilson Ole mkutano ulikuwa umeitishwa mara moja baada ya taarifa ya kutoroka kwa Norbert kuwafikia kutoka kwa Leopard Queen aliyekuwa amemtia nguvuni. Panther aliyekuwa hajui kingereza ambaye alikuwa yupo eneo hilo akimuwakilisha mwenzake alikuwa amekasirika sana, Wilson Ole alibaki akifarijika kwa ujanja aliofikia Leopard Queen wa kuweza kumuwekea silaha Norbert.



Wilson Ole mdogo wa aliyekuwa rais wa Tanzania Filbert Ole tayari alikuwa ameshaibaini kazi halisi ya Norbert baada ya kupata uhalisia kutoka kwa  Jackline mwanausalama aliyetiwa mikononi na Allison secret service wa EASA kutoka Burundi baada ya kutaka kumuua Koplo Daniel Uyomo katika kisa cha JINAMIZI, asubuhi ya siku hiyo Wilson Ole alimtembelea mwanausalama huyo ambaye kwa sasa ni mfungwa katika gereza la Segerea na hapo ndipo alipobaini ukweli.



Lawama za kushindwa  kumtia nguvuni Norbert ziliangushwa kwa Leopard Queen na muda wote huo Wilson alikuwa amenyamaza, walipomaliza kumlaumu ndipo na yeye alianza kueleza.

“Jamani hatuna haja ya kumlaumu Leopard Queen kajitahidi sana awezavyo kumkamata mtu kama Norbert” Wilson aliongea huku akiwatazama kila mmoja.

        "Hapana ni uzembe aliyoufanya" Kamishna aliongea.



       "Hapana nafikiri nyinyi hamuijui rangi halisi  ya Kaila mimi nimepata kuijua nilupomtembelea Jackline yule akiyekuwa TISS kipindi marehemu Kitoza akiwa ni mkurugenzi, huyu amenieleza rangi halisi ya Kaila" Wilson aliongea kisha akawatazama wenzake ambao walijaa shauku ya kutaka kumjua Norbert kiundani, aliendelea kusema, "Kaila ni mpelelezi hatari tena mwenye uwezo wa hali ya juu wa EASA si mwandishi wa habari mjanja kama mnavyofikiria na mkae mkijua tunapambana na EASA".



       "Shit! Leopard Queen you have to be careful(Shit! Leopard Queen unatakiwa uwe mwangalifu)" Panther aliongea.



        "Hivyo basi huyo ndiyo Kaila na tukienda vibaya kwake tumeumia  hata mabosi hawatatuelewa si umesikia wote wapo ndani ya nchi hii Don kaingia jana na mke wake kaingia leo" Wilson aliongea.



        "Nauona ugumu wa kazi ila sitakubali mpaka nilipe kisasi kwa Kaila ndiyo furaha yangu" Kamishna aliongea kwa uchungu.



        "Kamishna cool down najua kama Kaila ndiyo kamuua Kitoza aliyekuwa  binamu yako, ila usiweke hasira mbele kumbuka tumepewa kazi hii kutoka kwa Don  na ikiharibika hii kazi pia Sir Shaw hatatuelewa" Wilson aliongea kisha akamtazama Panther akamuambia, "Kaila atauliwa na Leopard Queen kwa kumtegea ugonjwa wake tu, yeye si mpenda  mabinti sasa binti ndiye atakayemuua".CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Nafikiri hiyo kazi niendelee nayo mtego mmoja bado upo” Leopard Queen aliongea.

            "No! No! Stay away from him(Hapana! Hapana! Kaa mbali naye" Panther aliongea kwa uchungu sana aliposikia Leopard Queen anataka kujitosa kuendelea na kazi, uhatari wa Norbert ulimfanya awe na hofu sana ya kuendelea kumuacha mpenzi wake aingie kupambana naye.



            "Panther come on! Muache afanye hiyo kazi ikishindikana mnaingia nyinyi najua kabisa hamuwezi kushindwa kuhusu hilo" Wilson alimuambia



             "I can't(Siwezi)" Panther aliongea kwa uchungu.



              "Usiwe na hofu nami B boy nitamaliza hiyo kazi then tutakuwa na ushindi" Leopard Queen aliongea.



              "Na pia usiruhusu hisia za mapenzi zikutawale katika kazi kama hii Panther" Kamishna aliongea,





     Muda huo huo mlango ulifunguliwa na aliingia mtu aliyewafanya wote wasimame juu, walisimama kwa pamoja baada ya kuingia mgeni huyo ambaye wanamuheshimu sana mchango wake katika mpango wao.



             "Karibu jenerali mtarajiwa wa dola tarajiwa"Wilson aliongea akimkaribisha mgeni huyo ambaye hakuwa mwingine, L.J Ibrahim ndiye mgeni mwenyewe ambaye alikuwa ahudhurii sana vikao vyao lakini ni  sehemu ya mpango wao.



            "Asanteni wana mapinduzi wenzangu niambieni mpango unaendelea vipi?" L.J Ibrahim aliuliza huku akiketi kwemye kiti na wote wakaketi kwenye viti.



            "Mpango kidogo umechukua sura mpya, na kuna mapya yamezuka" Kamishna alijibu.



           "enhee nipeni ripoti kamili" L.J Ibrahim aliongea.



          "Kwanza baya zaidi ni kwamba ni kwamba EASA ipo kazini na zuri zaidi ni kwamba Don na mkewe wapo nchini hapa katika mikoa tofauti" Wilson aliongea.



   Kauli ya kwanza ilimfanya L.J Ibrahim ashtuke huku kauli ya pili ilimfanya aingiwe na tumaini kidogo, kusikia kuingia kwa mabosi wao nchini ilikuwa ni jambo la kufarijika kwake kwani aliona dalili za mpango wao zilikuwa zikielekea kutimia.



           "Napenda ufahamu kuwa Norbert Kaila ni mpelelezi hatari wa EASA na ndiye yupo kazini na tayari amemponyoka Leopard Queen kwa namna ya kutatanisha sana" Kamishna aliongezea.



          "Maelezo yenu yananipa wasaa wa kuharibu zaidi heshima ya Moses ili tuzidi kumuweka pabaya Zuber atoke pale ikulu" L.J Ibrahim aliongea akaweka kituo kisha  akaendelea kuongea, "napiga simu pale ikulu nampa siku saba atoe maelezo ya kwanini Mkuu wa idara ya usalama wa taifa aliyemteua anayemuamini kwa siri anahusika na mauaji ya General na  nitamuambia ana ushahidi gani wa kujitetea kuwa na yeye ahusiki katika mpango huo ikiwa huyo ni mtu wake wa kuaminika. Akishindwa kutoa majibu ndani ya siku tatu namtangaza Professa Gawaza ni muuaji wa General, siku ya saba tunaipindua nchi mradi wetu unaanza kwa watanzania wote tuone suala alilokuwa analipinga na amekataa kulisaini atakuwa  kalizuia vipi".



              "Good plan General but what about Kaila(Mpango mzuri Jenerali lakini vipi kuhusu Kaila)?" Panther aliuliza.



              "Kaila ni jukumu lenu na ikishindikana Don na mke wake wataingia kumtuliza, sidhani kama atatoka. Kwa sasa mimi ndiyo mkuu kati ya wanajeshi wote hivyo majeshi yapo chini ya amri yangu, mapinduzi lazima" L.J Ibrahim aliongea akiwa na tabasamu pana zaidi.



             "Njia ya kupandikiza machafuko ya kidini naona haifai kwa sasa na wale viongozi wa dini walioteuliwa kwa ajili ya mpango huo hawana kazi tena ila inabidi wabaki na siri milele, Panther  unajua nini cha kufanya kwa askofu na mufti mkuu" Wilson aliongea.





              "I know(najua)" Panther aliongea.





Mradi wa kupandikizwa Tanzania ulikuwa tayari umeanza kuonesha matumaini kwa hawa wahusika, ambapo suala la mapinduzi kwa namna ya kijeshi ndiyo ilitaliwa kufanyika kwa kutengeneza serikali mpya na kuiondosha serikali ya rais Zuber Ameir. Mbinu ya kumpandikizia hila ya kuhusika na kifo cha Jenerali Kulika ndiyo iliongelewa ili kuwaondoa imani  wananchi  kwa rais wao, kikundi hiki tayari kilikuwa kimeweka makubaliano na kundi la hatari la kihalifu la nchini Ujerumani lililopo chini ya  Jack Shaw ambaye tayari ameingia nchini  kwa kutumia mbinu ya kinyonga awapo kwenye maeneo ya hatari ili kudumisha mpango huo.



 Siri ya kuundwa kwa mpango huo ilikuwa ni mkataba feki amba uliletwa kwa kivuli cha Jumuiya ya madola, ulikuwa na hila ya kuitumbukiza Tanzania mahali pasipo stahiki lakini Rais shupavu  Zuber Ameir aligoma kusaini pasipo kujua kimetumika kivuli cha Jumuiya ya madola katika kumshawishi asaini. Haukuwa mkataba uliotoka jumuiya ya madola bali ilikuwa ni hila ya kuingiza Tanzania mahali pasipostahiki kwa kisingizio cha kuleta maendeleo nchini, Rais Zuber alipowagomea ndipo ikaundwa hila ya kupandikiza machafuko ya kidini ili kuidhoofisha serikali na hatimaye kupinduliwa na jeshi na mradi huo kupandikizwa kwa ulaini sana.



Mapinduzi yaliyokuwa yakizungumziwa yalikuwa yafanyike kwa sharti la kuondoshwa kwa Jenerali Kulika katika uso wa dunia na bila hivyo mapinduzi hayo yasingeweza kutelekelezeka hata kidogo ndani ya nchi ya Tanzania. Tayari Jenerali Kulika mwenye amri katika majeshi ameuawa hivyo hatua iliyokuwa inafuata ni kuipindua serikali ya Rais Zuber baada ya kumpandikizia chuki kwa wanachi wake kupitia mauaji hayo, hakika walikuwa ni maadui wakubwa wa Tanzania ingawa asilimia kubwa walikuwa wamezaliwa ndani ya Tanzania.



Watu wasiotaka kuiona Tanzania ikiwa ni nchi iliyokuwa ikiendeshwa kizalendo kama ilivyo hivi  sasa zaidi ya kuona ni nchi wanayoistahiki kuwa sehemu  yao kutekelezea mpango wao ambayo ingewaingizia kiasi kikubwa sana cha pesa, uzalendo alioonesha Rais Zuber kwa kukataa dola milioni 500 za kimarekani ikiwa tu ataweka saini katika mkataba alioletewa wao waliuona ni ujinga kupitiliza. Hivyo fedha hizo walikuwa wakizitaka wao kwa kupandikiza mpango wao kwa kilazima kama mabosi wao walivyowaahidi, uchu wa pesa kuliko kitu chochote  ndiyo ulisababisha wakodi  kikundi cha Cats kingdom ambacho ni sehemu ya kundi la hatari la Jack Shaw lililopo  ndani ya Afrika ya mashariki.



 Uchu wa pesa kutoka kwa mabosi wao ndiyo ulisababisha hata watanzania wenye nyadhifa kubwa  katika masuala ya ulinzi waweze kuisaliti nchi yao, pia waliweka kuwasaliti wananchi ambao walikuwa wakiwategemea sana. Hawakuona hasara ya kupoteza roho zaidi ya kuona hasara ya kupoteza pesa, hawakuona hasara ya kupoteza utu wa wananchi wao zaidi ya kujali kuingiza fedha.

KILIMANJARO HOTELI

 Baada ya Benson kuingia ndani ya chumba cha Askofu Valdermar wapambe wote walitoka nje  kutokana na amri ya Askofu huyo iliyowataka wafanye hivyo, usiri wa jambo lililowafanya watoke nje tayari walikuwa wakilitambua na ilikuwa ni kawaida  kwao kutolewa nje akiingia Benson katika eneo kama hilo. Ajenda kubwa ambayo ni zaidi hata ya kikao cha siri  iliwafanya watoke nje, ilikuwa ni siri kubwa iliyobaki miongoni mwa watumishi hao wawili waliokuja na Askofu huyo.



 Benson alipoingia ndani milango ilifungwa na Askofu huyo akabaki akimtazama kwa macho yaliyoashiria kitu, ukakamavu wa kiume alionao Askofu huyo ulipotea mara moja kuanzia sura na hata mwili. Kwa namna isiyotarajiwa Askofu huyo alilegeza macho mithili ya mtu anayesikia usingizi huku akmsogelea Benson, alipofika mbele kabisa ya Benson aliweka mikono juu ya mabega ya Benson kisha akafanya kitu ambacho hakikutarajiwa kufanywa  na mtumishi wa Mungu mkubwa kama huyu.



 Askofu Valdermar na Benson walianza kubadilishana mate  vinywani mwao mithili ya wapenzi wa jinsia tofauti, mmoja alikuwa amechukua wasaa  wa kujifanya mwanamke na mmoja alikuwa akibaki katika uanaume wake kamili. Hali ya kusikitisha na hata kuhuzunisha kwa mtu anayeonekana kwa hadhira ni mtumishi wa Mungu kama huyo kutoka barani Ulaya  akitomaswa na mwanaume mwenzake tena akitoa mihemo mithili ya binti, hali nyingine ya kusikitisha kwa mwanaume mwenye kujitambua akimtomasa mwanaume mwenzie mithili ya mwanamke. Haikustahiki kabisa kumuita Askofu Valdetmar mtumishi wa Mungu kwa kufanya kitendo ambacho Mungu  aliwaangamiza wanadamu wallikuwa wakiishi Sodoma kwa kukifanya, aibu sana kwa jinsia ya kiume kufanya kitendo kama hicho ambacho ni haramu kwa dini zote.



Benson pasipo kuwa na haya  ya kwamba aliyempa pumzi anamuona yeys alimvua vazi maalum la kulalia Askofu Valdermar akabaki kama alivyozaliwa, pasipo hata kuwa na chembe ya haya katika uso wake aliamua kumuandaa kwa ajili ya kufanya tendo hilo haramu, Alifanya kama vile anavyomuandaa mwanamke katika tendo ambalo Mungu kalibariki kufanywa na waliomo kwenye ndoa, alitumia muda  huo kumundaa huku Askofu Valdermar akitoa miguno mithili ya mtoto wa kike kwa sauti ya puani. Aibu iliyoje ilizidi kwa mtu anayeonekana ni wakala wa nuru kwa kutoa maneno mema kwa jumuiya, kumbe ni wakala wa giza anayefanya mambo yanayofanywa na watu wa giza.



 Askofu Valdermar kwa mara nyingine baada ya kumaliza kuandaliwa na yeye alizidi kufanya jambo la aibu kwa kuzitoa nguo za Benson zote kisha akaanza kumuandaa mithili ya mwanamke anayemuandaa mume kwa ajili ya jimai. Mambo mengine waliyofanya hayakustahiki kabisa kuandikwa kwa kalamu ya mwandishi, mambo hayo yaliwachukua masaa mawili wakawa wamemaliza kabisa na hapo wakajisafisha wakarudi wakavaa mavazi yao.



         "Asante sana Benson, unanipa burudani zaidi hata ya mume wangu" Askofu Valdermar yule aliyekuwa akiongea kingereza kumuambia Norbert akamuite Benson sasa hivi aliongea kiswahili fasaha kabisa tena bila kuonekana kama ni mgeni katika lugha hiyo, laiti kama ingesikika sauti yake tu pasipo kumuona yeye mwenyewe basi ingedhaniwa anayeongea ni mtu mweusi kabisa.



           "Anytime(muda wowote), nafikiri taarifa yote unayo. Don ameingia tayari yupo hoteli ya Singita Grumeti Serengeti kwa ajili ya mradi wetu" Benson aliongea.



            "Ndiyo ninayo, ninamaliza mazishi ya Edson ndiyo nitaenda kuungana naye" Askofu Valdermar aliongea.



           "Ok, Sir kuna jambo naona uliache" Benson aliongea.



            "Benson tukiwa wawili niite madam usiniite sir, ok jambo lipi?" Askofu Valdermar aliongea.



             "Naomba huyu kijana aliyekuja kunipokea asiwepo karibu nawe" Benson aliongea huku akionekana ameshikwa na wivu.



               "Hiyo siyo kazo yako Benson ana kazi yake huyo ndiyo maana nimemteua, nafikiri nikienda kwa mume wangu Serengeti ndiyo utakuwa mwisho wa kazi yake. Unaweza ukaenda" Askofu Valdermar aliongea, Benson hakuwa na ubishi zaidi ya kuondoka humo ndani kutokana na amri aliyopokea kutoka kwa bosi wake.



 Wivu wa kumuona Norbert eneo hilo ndiyo ulimtafuna na akajikuta hana la kumfanya, hakika alimuonea wivu mwanaume  mwenzake kwa mwanaume mwingine.

 Benson alipotoka  watumishi wale walirudi ndani ya chumba hicho wakimuacha Norbert akiwa anatoka na kuingia ndani ya chumba chake ili aweze kupata kile alichokuwa akikihitaji kutoka kwa hao watu. Wasiwasi juu ya Askofu Valdermar tayari  ulikuwa umeshamuingia ingawa hakutaka kupuuza agizo la ofisi pasipo kuzifanyia utafiti fikra zake zilizompa wasiwasi sana baada ya kumuona Benson akiwa na alama aliyonayo mtu aliyeonekana nyumbani kwa Jenerali Kulika siku ambayo aliuawa, nafsi yake ilimuambia anahitaji umakini sana katika kumlinda Askofu Valderamar hasa baada ya kutambulishwa kuwa  Benson yupo nchini akichunguza kifo cha Askofu Edson. Upande mwingine wa nafsi yake ulimuambia aendelee kumlinda Askofu Valdermar kama ofisi inavyomuhitaji ili asije akadhuriwa na Benson, alifikiri sana juu ya hayo.



Mwisho wake akaamua aendelee kumlinda Askofu Valdermar huku akizidi kumpeleleza Benson. Hakika mwanadamu hakuwa anayajua ya  mbeleni mwake na laiti angekuwa na utambuzi wake, Norbert angezidi kuongeza umakini wake kwani alikuwa akicheza na watu wanne tofauti wenye hatari kubwa ingawa yeye aliona anacheza na watu wawili.

SIKU ILIYOFUATA

JUMAPILI



 Kanisa la kiluteri la Azania front siku hiyo lilifurika mamia ya waumini kwani ilikuwa ni siku ya ibada, pia ndiyo ilikuwa siku ya kuagwa mwili wa Askofu Edson. Viongozi mbalimbali wa kiserikali walikuwepo ndani ya kanisa hilo wakiongozwa na Rais Zuber  katika kuhudhuria ibada ya mazishi ambayo ingeanza baada ya kumalizika kwa misa ya pili, ndani ya kanisa hilo pia Norbert alikuwepo pembeni ya Askofu Valdermar kwa kipindi chote kama agizo la ofisi yake lilivyomtaka.



Siku hiyo misa ya kanisa hilo iliongozwa na Askofu Valdermar akiwa na mkalimani wake Norbert hadi inaisha, kisha ikaingia ya pili hadi inaisha na hapo ndipo ibada ya mazishi ikaanza. Jeneza la lenye.mwili wa Askofu huyo lilikuwa lipo mbele na ibada hiyo ilikuwa ikiendelea, muda wa kuuaga mwili wa askofu Edson ulifuatia. Ulikuwa ni muda ulioibua majonzi na simanzi kwa wafiwa na hata waliokuwa wakimpenda sana Askofu huyo, muda wa kuaga ulipoisha safari ya kupeleka jeneza uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere ili usafirishwe kuelekea Musoma kwa maziko ndiyo ilifuatia. Viongozi mbalimbali wa kiserikali walitawanyika baada ya kutoa salamu za pole kwa  wafiwa wakiongozwa na Rais Zuber, baada ya hapo shughuli zingine za kawaida zilifuata huku Norbert akiwa yupo kwenye msafara wa Askofu Valdermar kwa mara nyingine ambao ulikuwa unaelekea uwanja wa  ndege kusafiri kuelekea Musoma kwenye mazishi.

Muda ambao msafara unaondoka kuelekea Uwanja wa ndege ndiyo muda ambao msafara wa rais Zuber ulikuwa unarejea ikulu baada ya kumaliza kumuaga Askofu Edson, ilikuwa ni lazima arejee ikulu kabla hajaondoka baadaye kuelekea Musoma kwa ajili ya kuhudhuria  mazishi. Msafara wake ulitumia dakika tano tu kutoka kanisa la Azania front hadi ikulu, kuwasili kwa msafara wake ikulu hapo ndiyo kulikuwa mwanzo wa kuzuka jambo jingine ambalo hakutarajia kama litazuka. jambo hilo lilimfanya asitishe  safari yake yote ya kwenda kwenye mazishi kutokana na uzito wake, simu yake ya mkononi iliita na hapo ndipo jambo lenyewe lilipoanza.



Aliipokea simu hiyo akaiweka sikioni mwake pasipo kujua dhumuni la kupigiwa simu hiyo, ilikwa ni simu kutoka kwa L.J Ibrahim ambayo haikuwa na ishara ya kuwepo kwa jambo zuri hata kidogo. Simu hii ndiyo ilimpa taarifa ya kupinduliwa kwa nchi siku saba zijazo ikiwa tu hatatoa maelezo ya kina juu ya kuhusika kwa Moses katika mauaji ya Jenerali Kulika, kitendo cha kumuamini Moses na kumfanya kuwa msiri wake ndiyo jambo ambalo lilimfanya ahisiwe anahusika na mauaji hayo moja kwa moja. Taarifa ya kupinduliwa kwa nchi ndani ya siku saba zijazo ilizidi kumchanganya sana kwani hakuhusika lolote katika mauaji hayo, alikuwa amebebeshwa gunia la misumari ambalo hakutakiwa alibebe yeye.



Rais Zuber alizidi kupagawa sana  akawa hajui nini cha kufanya kwani mtu aliyempa amri hiyo majeshi yote yalikuwa yapo chini yake, alishindwa kumpigia simu Moses kutokana na uzito wa jambo lenyewe kwani alihofia huenda Moses angeweza hata kummaliza yeye mwenyewe kwa kuficha siri hiyo ya kuhusika. Hakuwa na imani tena na Moses na aliona kama ndiyo mhusika namba moja wa jambo hilo basi akimuita anaweza kumfanyia kitu kibaya. Uamuzi wa kufanya kwa jambo hilo aliona ni kuomba msaada katika shirika la kipelelezi la Afrika ya mashariki(EASA) ili walau apate nusra ya jambo ambalo hahusiki nalo analotaka kuhusishwa nalo, hapo Rais Zuber alipiga simu  kwa CE na kumueleza juu ya tatizo hilo ambapo  kidogo alipata ahueni.

SIKU ILIYOFUATA

MUSOMA

  Baada ya  Askofu Eddson kuzikwa safari nyingine kabisa ilianza iliyomuhusisha Askofu Valdermar, Norbert na vijana wake aliokuja  nao, safari hiyo iliwachukua masaa kadhaa wakawa wamefika katika mbuga ya taifa ya Serengeti. Walifika kwenye hoteli ya kitalii namba moja duniani iiitwayo Singita iliyopo ndani ya ardhi ya Tanzania, walipokelewa kwa uchangamfu mkubwa na wahudumu wa hoteli hiyo wenye uchangamfu wa kuweza hata  kumsahaulisha mteja uchungu wa gharama za juu za hoteli hiyo inayoongoza kwa kuwa na gharama za juu  nchi nzima. Walipokelewa wakapakiwa kwenye gari maalum lililokuja kuwapokea kuwapeleka kwenye lodge ambayo walitakiwa, kutokana na ukubwa wa hoteli hii iliwalazimu watu kutumia usafiri kutoka lodge moja hadi nyingine.



 Usafiri uliwafikisha lodge walipokuwa wameichagua salama ambapo walikutana na mtuambaye alimfanya Norbert azidi kushangaa, alikuwa ni mtu ambaye yeye aliishia kumuona tu kwenye luninga. Mtu huyo ndiye aliyekuwa anawasubiri hapo jambo ambalo haliwezekani, haikutokea kwa mtu kama huyo mwenye msimamo mkali amsubiri Askofu Valdermar tena akionekana ni mchangamfu sana.



  Norbert alibaki kutoamini kwa mtu huyo kusalimiana na Askofu Edson kisha akawapungia mkono yeye na vijana wa askofu, kitendawili  kizito kilitanda ndani ya ubongo wake juu ya hali hiyo.



          "Sheikh Ahmed" Alibaki akijisemea moyoni huku akimtazama  mtu huyo ambaye alikuwa amevaa mavazi ya kiislamu, alikuwa akitazamana na mtu huyo mwenye asili ya kiarabu ambaye amefuga ndevu nyingi sana kidevuni mwake. Akiwa ndani ya kanzu safi nyekundu pamoja na kiremba cheupe chenye kizibao chekundu,  sehemu ya uso ilitangaza kwamba mtu huyo anaingia sana nyumba ya ibada  lakini mambo aliyoyaonesha yalimtia shaka Norbert.





 Sheikh Ahmed Al-Baggara  muumini mkubwa wa dini ya kiislamu na kiongozi mkubwa wa dini ambaye amekuwa akisimamia misimamo ya dini, kiongozi huyu anatambulika na ulimwengu kuwa kiongozi wa dini mwenye msimamo mkali kutoka nchini Iraq ambaye alijiapiza kutokaa wala kuongea na mkristo baada ya kutokea mtafaruku wa kidini uliohusisha kikundi cha watu waliukashifu uislam.



 Kiapo cha Sheikh huyu kilienda sambamba na kushika kitabu kitukufu  cha kiislamu ili kuonesha kuwa alikuwa anamaanisha kuweka kiapo hicho, aibu iliyoje ilikuwa kwa kiongozi huyu ambaye sasa hivi alikuwa  ameshuhudiwa na macho ya Norbert akiwa anafanya tofauti na kiapo chake. Ingawa hakuwa muumini wa dini wa kiislamu Norbert alibahatika kuwa mtu anayeijua dini hiyo ambayo siyo imani yake kutokana na kazi yake, miiko mbalimbali ya dini hiyo juu ya uvunjwaji kiapo aliitambua vilivyo yampasa mtu kufunga siku tatu mfululizo.



Hiyo ilikuwa ni sehemu ya sheria ya dini ya kiislamu lakini kwa Sheikh huyu wa Iraq anayetambuliwana dunia kwa ajili ya misimamo yake hiyo haikuwahi kutokea akavunja kiapo kama anavyoonekana hapo, Norbert alibaki akimtazama  Sheikh huyo akiingia ndani ya chumba cha hoteli akiwa amefuatana na Askofu Valdermar. Vijana wa Askofu nao walichukuliwa wakaenda kupewa vyumba vingine kila mmoja, Norbert naye alichukuliwa  akaenda kupewa chumba kingine ambacho hakikuwa mbali sana na kilipo chumba ambacho waliingia Askofu Valdermar na Sheikh Ahmed.



 Kitendawili kingine kingine kilijitega katika kichwa cha Norbert ndani ya siku hiyo na hapo ikamlazimu abebe vifaa  vyake vya kazi visivyoonekana, alijifunga vifaa hivyo kwenye mavazi yake kisha akabaki chumbani humo akiwaza juu ya Askofu Valdermar. Hapo alipata uhakika alikabidhiwa kumlinda asiyehitajika kulindwa dhidi ya mhalifu wa kimataifa, kazi aliyopewa na ofisi yake aliona haistahiki kufanywa kwa mtu mwenye kila aina ya shaka. Askofu mwenye kushirikiana na muuaji Benson na askofu mwenye kushirikiana na Sheikh aliyeweka kiapo mbele ya watu baada ya kukashifiwa mtume wa Mungu rehma na amani ziwe juu yake. Askofu ambaye aliwahi kutoa kauli nzito juu ya imani ya uislamu leo yupo na kiongozi wa dini ya kiislam aliyekuwa anajilikana kwa jinsi anavyowachukia wakristo,



 Norbert alibaki akifikiria hilo muda huo aliobaki hapo ndani na hapo onyo zito  likaja kichwani mwake juu ya hao watu. Wasiwasi wa uwepo  wa kitu kingine kinachowafanya viongozi hao kidini wawe pamoja ndiyo ulimjia Norbert, hamasa ya kuujua ukweli unaowafanya viongozi hao wa kidini wawe pamoja tayari ulishamuingia ndani ya mwili wake hadi vinyweleo vyake vikamsisimka. Wahka wa kutaka kuingia kazini tayari ulikuwa umeshaingia kwenye damu yake, kiherehere cha kuingia katika kazi yake tayari kilikuwa kimeivamia damu yake lakini alikizuia ili asifanye papara katika kazi yake hiyo.



  Muda huo aliopo peke yake chumbani aliutumia  humo aliutumia kujikagua silaha zake kuanzia bastola aliyoichomeka mguuni akaifunika vizuri na suruali yake, aliiangalia kamera ndogo aliyoichomeka kwenye nguo yake ambayo alitaka akusanye ushahidi utakaomsaidia kutegua kitendawili kinachomsumbua kichwani mwake. Alikuwa akijiandaa kuuvaa na upande  mwingine ambao haukuujua ulikuwa umejiandaa namna gani, bahati nasibu ndiyo alikuwa akiicheza ingawa mwenyewe alitambua na alihitaji umakini wa hali ya juu.

Upande wa pili katika hoteli hiyo ya Singita Grumeti katika chumba cha hadhi ya kitalii kutokana na mapambo ya kitalii na muundo wa chumba hicho kilichojengwa kiasili zaidi, samani za gharama zilizojengwa kiasili ndiyo zilionekana kuzidi kupendezesha chumba hicho. Mojawapo wa samani zilizopo humo ndani samani moja ilionekana kupata purukushani isiyo ya kawaida kutoka kwa viumbe   wawili waliopo juu yake, samani hiyo iliyobeba godoro la kisasa ilikuwa katika mtikisiko usio wa kawaida.



 Kitanda hicho ambacho kilibeba  wenye laana kiliendelea kuvumilia hao waliolaanika wamalize laana yao ambayo iliwahi kusababisha wanadamu wa kale kuangamizwa, kitanda hicho kiliumia zaidi kwa kubebeshwa laana hiyo ya waliyolaaniwa. Kitanda hicho kilisononeka muda wote ambayo waliopo juu yake  wakifanya laana hiyo, ilikuwa si mara ya kwanza kitanda hicho kubeba watu waliokuwa wakichoshana miili yao ingawa hakikuwahi kuhuzunika  hata mara moja.



Siku hiyo kitanda hicho kilisononeka kwa kubeba viumbe wa jinsia moja waliokuwa wakipashana miili yao kwa namna isiyotakiwa, miguno  ndiyo ilikuwa imetawala kwa kiumbe mmoja na mihemo ndiyo ilikuwa imetawala kwa kiumbe  mwingine. Hawakuwa wengine isipokuwa Askofu Valdermar na Sheikh Ahmed ambao walikuwa watupu kama walivyozaliwa wakifanya laana kwa kutumia njia iliyoharamishwa na Mungu muweza, walikuwa wakiitana mume na mke katika kipindi hicho wakichakarika katika kuzidi kumuasi Muumba aliyesababisha wakapata elimu ya dini kwa ajili ya kuwaongoza waumini wengine wawe kwenye mstari ulionyooka.
Aibu! Aibu! Aibu iliyoje kwa  hawa wanadamu wawili waliouvaa uwakala wa nuru kumbe ni mawakala wa giza, wanafanya mambo yanayoamrishwa kufanywa na mawakala wa giza huku wakiwa na alama zinazowaonesha wao ni mawakala wa nuru. Mavazi ya kiaskofu yalikuwa yapo kwenye sehemu maalum ya kutundika nguo yakishuhudia uharamu huo, msalaba uliokuwa umewekwa mezani pia ulikuwa ni shuhuda mambo hayo. Kanzu safi, kilemba na kizibao navyo vilikuwa vimstundikwa sehemu maalum vilikuwap vikishuhudia mambo hayo huku tasbihi ya kutaja majina ya muumba ikiwa ipo mezani ikishuhudia mbebaji wake akifanya haramu.



 Ama kweli uchamungu siyo mavazi wala kutembea na vitu vya dini muda wote bali uchamungu ni usafi wa roho, Sheikh Ahmed na Askofu  Edson hawakustahiki kuitwa wachamungu hadi muda huo kutokana kuwa ni wachafu zaidi hata ya kinyesi katika roho zao. Laiti wangelikuwa uchafu basi hata kuhifadhiwa katika tundu la choo hawakustahiki kwani walikuwa wamekizidi kinyesi kwa uchafu, hata baharini pia panapowekwa uchafu mkubwa hawakustahiki kuhifadhiwa na ardhini pia lau kama wangehifadhiwa basi ardhi ingesononeka kwa kutupiwa uchafu mkubwa usiostahiki kutupiwa. Walikuwa wakionekana ni watu ambao hawatakaa hata meza moja kuongea masuala ya kidini kwa jinsi walivyo tofauti kiimani, kumbe walikuwa ni watu waliokuwa wakijuana  tangu muda mrefu na walikuwa wameshafanya muungano usio rasmi.





Askofu Achim Valdermar na Sheikh Ahmed Al-Baggara walikutana nchini Uingereza mara ya kwanza miaka kadhaa iliyopita, Sheikh Ahmed alikuwa yupo ziarani na nchini humo na Askofu Valdermar alikuwa yupo katika mapumziko.  Askofu Valdermar kipindi hicho tayari alikuwa shoga wa kutupwa na aliyekubuhu katika ushoga na alikuwa akiwatumia wanaume maalum wanaofanya mapenzi ili kujiingizia kipato, kwa mara ya kwanza alipomuona Sheikh Ahmed alijikuta amevutika kutokana na utanashati alionao na hapo akatamani awe naye ili aweze kuonja raha za mwanaume wa kiarabu. Sheikh Ahmed naye kwa kipindi hicho alishakomaa katika kufanya usodoma kwa wanawake na alikuwa amejaribu kwa mwanaume mmoja na hapo akatamani aendelee zaidi kutumia wanaume baada ya kuona tofauti yao na wanawake aliowazoea huko kwao.



Wawili hawa waliazisha uhusiano wakiwa nchini humo na hatimaye baada ya mwaka mmoja wakafunga ndoa  ya kisheria nchini humo kwa siri, tangia hapo walianza kuitana mume na mke pasipokuwa na haya na ndiyo hadi muda bado wapo kwenye ndoa hiyo ya kishetani. Hao ndiyo wanandoa wa jinsia moja ambao walikuwa hawatambuliki na umma zaidi ya kutambulika na watu wachache tu.



  Baada ya kumalliza tendo hilo wote kwa pamoja waliingia bafuni wakaoga, walipotoka tayari kiza ndani ya eneo kilikuwa kimetanda kuashiria mwangaza wa jioni ulikuwa umeshaingia na walienda kula chakula.



 Hali ambayo Askofu Valdermar hakuitarajia sura ya Sheikh Ahmed ilikuwa ni ya hasira kwa ghafla pindi tu walipomaliza kula, alijitahidi kumuuliza juu ya tatizo lililomsibu kwa mahaba  makubwa na hapo ndipo akajua kilichokuwa kikimsibu.



              "Huyu kijana mweusi ni nani na kwanini uongozane naye?" Sheikh Ahmed aliuliza kiswahili fasaha.



             "Ni mmoja wa watumishi wa kanisa  nimevutiwa sana kuongozana naye katika safari hii ili isijulikane kama mimi ni mwenyeji ndani ya nchi" Askofu Valdermar aliongea.



             "Khaa! Sitaki kusikia huo upuuzi naondoka kwenda Musoma mjini na helikopta, nikirudi awe mfu tayari nakujua wewe unapenda sana vijana wa aina ile. Silaha zipo Scorpio na Spider watakusaidia kuhusu hilo" Sheukh Ahmed aliongea huku akivaa nguo.



            "Naenda nikirudi nitamchinja mwenyewe kwa mkono wangu ikiwa nitamkuta akiwa bado anapumua, sasa kama umeanza kuwa na mapenzi naye sitokuacha hai. Chagua umuue kwa risasi au bomu, ukishindwa nakuja kumuua mimi kwa kumchinja" Sheikh Ahmed aliendelea kuongea kwa sauti ya chini iliyojaa hasira huku akimalizia kufunga kizibao, Askofu Valdermar hakujali maneno yake alinyanyuka na kwenda kumsaidia kuweka vizuri kizibao. Alipomaliza alikutanisha mdomo wake na mdomo wa Sheikh Ahmed, alidhamiria kumtoa hasira Sheikh Ahmed lakini hasira zake zilikuwa palepale.



           "Msimamo wangu huwa haubadiliki nikirudi namchinja kwa jambia langu" Sheikh Ahmed aliongea kwa msisitizo kisha akaondoka, wivu wa mapenzi kwa mwanaume mwenzake tayari ulishaanza kumtafuna kwani alimtambua vyema huyu anayemfanya mke wake huwa ana tabia ya kutamani vijana wengine.



 Mawazo hayo ya Sheikh Ahmed yalikuwa ni kweli sana kwani Askofu Valdermar alimteua Norbert kuwa mwenyeji wake kwa lengo hilo, alikuwa amevutiwa na mwili wa Norbert pamoja na utanashati wake ambao unawatesa sana wanawake. Ndiyo maana akamteua ili tu aje kuonja ladha ya penzi haramu kwake,  alitaka amtumie kisha amkate kauli. Adhma yake tayari ilikuwa imeshagundulika na Sheikh Ahmed na akaona alikuwa ana hatiati ya kumkosa Norbert, ili kufanikisha jambo lake aliamua kuwapigia simu vijana aliongozana nao kisha akawaambia kila kitu.

 Norbert akiwa chumbani kwake alizama katika fikra sana hadi mbabe wa wababe asiyezuiwa hata na wenye bomu akaja kumdhibiti, akiwa amejilaza kitandani vile vile akiwa chali mbabe huyo alikuja kumdhibiti  akiwa hivyo hivyo baada ya kuzidiwa na uchovu. Ulikuwa ni usingizi ndiyo ulimpitia baada ya uchovu wa safari pamoja na kulala kwa mitego alivyofanya usiku uliopita amlinde Askofu Valdermar, pia hakuwa amepata muda wa kutosha wa kumpumzika tangu alipofanya mapenzi na wanawake wawili kwa siku moja zaidi ya kulala masaa  machache tu ndiyo maana usingizi ulimuonesha ubabe wake kwa njia nyepesi sana.



Miguu sehemu ya magoti hadi kwenye unyayo ikiwa ipo nje ya kitanda na mwili ukiwa upo ndani ya kitanda, hadi Sheikh Ahmed anaondoka bado yeye alikuwa amezama usingizini. Muda ambao Askofu Valdermar anawaitwa vijana wake ambao wanatambulika kama watumishi wa kanisa aliokuja nao ambao ni Scropio na Spider bado Norbert alikuwa amelala, alikuja kuamshwa na mlango wake kugongwa ambapo alikurupuka akijibua sarakasi kisha akaweka kiganja chake ulipo mguu wake alipoficha bastola yake.



 Mlango ulipogongwa  kwa mara ya pili alijicheka mwenyewe kwa kurupuka kitandani akijua kavamiwa aliposikia sauti hiyo,  mlango uligongwa tena kwa mara ya  tatu hapo akaenda kuchungulia kwenye kioo maalum  kilichopo mlangoni akamuona mgongaji wa mlango huo. Alishusha pumzi kisha akajiangalia kama kila kitu kipo sawa halafu akafungua mlango, mlangoni alimuona kijana wa askofu ambaye ndiye Scorpio akiwa amevaa mavazi mengine ya kiraia ysliyomka vyema.



            "You are needed(unahitajika" Scorpio alimuambia.



            "Ok Lets go" Norbert alijibu kisha akawa anafunga mlango huo.



           "First of all change your clothes like us (awali ya yote badilisha nguo kama sisi)" Scorpio alimuambia Norbert huku akimuonesha mahali alipokuwa amesimama Spider ambaye alikuwa mbali na mlango, Norbert alitikisa kichwa kukubali kisha akaingia ndani akatumia dakika kadhaa kubadili nguo akihamisha zana kwenye nguo nyingine.



 Alipomaliza alitoka akaongozana na Scorpio pamoja na Spider, walielekea moja kwa moja chumbani kwa Askofu Valdermar. Norbert akiwa hana hili wala lile ingawa akili yake haikuhama  aliingia ndani  akakaribishwa kuketi kitandani badala ya kwenye kochi, yote yakiendelea Spider alikuwa amesimama mlangoni na Scorpio alikuwa amesimama jirani na Norbert ambaye alikuwa amekaa sambamba na Askofu Valdermar kwenye kitanda. Maajabu mengine alianza kuyaona hapo baada ya Askofu Valdermar kujilegeza kama mwanamke kisha akaanza kumshikashika Norbert akitaka kulazimisha kubadilishana kimiminika cha kinywani, Norbert alikataa akaanza kumrudisha Askofu Valdermar.



            "What is the meaning of this Bishop(Nini maana ya hii Askofu)?!" Norbert aliuliza huku akimzuia Askofu Valdermar.



            "Iam a gay my son and I like you( Mimi ni shoga mwanangu na ninakupenda)" Askofu Valdermar aliongea huku akipeleka mkono wake kwenye zipu ya suruali ya Norbert akashika kwa juu, kauli hiyo ilimshangaza sana Norbert ingawa mshangao wake haukumtoa kwenye maigizo aliyokuwa anayafanya.



             "What! Ohh! Jesus Christ I can't do that Bishop, is against the God's rules. God created Adam and Eve not Adam end Steve, means man and woman not man and man (Nini! Ohh! Yesu Kristo siwezi kufanya  hivyo Askofu ni  kinyume cha sheria za Mungu. Mungu kanuumba Adam na Hawa siyo Adam na Steve, inamaanisha mwanaume na mwanamke na siyo mwanaume na mwanaume)" Norbert alimuambia  Askofu Valdermar kwa msisitizo zaidi.



              "Saints are not yet born in this generation my boy, even you are not Saint (Watakatifu bado hawajazaliwa kwenye kizazi hiki mvulana wangu, hata wewe sio mtakatifu)" Askofu Valdermar aliongea.



              "Yes Iam not, but you are cursed and Iam not cursed. Thats the difference, evil spirit (Ndiyo mimi siyo, lakini wewe umelaanika na mimi sijalaanika. Hiyo ni tofauti, pepo mchafu" Norbert alisema kwa kujiamini kisha akanyanyuka kwenye kitanda ili aondoke lakini alishindwa hata kupiga hatua akabaki kasimama hivyo hivyo, kitu cha baridi kilikuwa kimgusa juu ya sikio lake la kulia.



  Alipotazama upande wa kulia kwa kutumia jicho lake aliona bastola iliyoondolewa usalama okiwa imeshikwa na Scorpio, kicheko cha kejeli kutoka kwa Askofu Valdermar ndiyo kilifuata. Norbert alibaki akiwa ameganda vile vile mithili ya mtu aliyekuwa yupo kwenye mkanda wa video uliogandishwa, alibaki vilevile huku akitembeza macho kwa Askofu Valdermar akayarudisha kwa Scorpio halafu akayapeleka kwa Spider ambaye alikuwa yupo mlangoni akiea na tabasamu pana mikono kaweka nyuma.



               "Kijana hutaki siyo sasa utafanya kilazima" Askofu Valdermar aliongea kiswahili kwa mara ya kwanza mbele ya macho ya Norbert ambaye alionekana kushangaa.



               "Ha! Ha! Ha! Ha! Unashangaa kusikia naongea kiswahili? Kiswahili ni mojawapo wa lugha ninayoongea na Tanzania ni mojawapo wa nchi ninazitambua na mwenyeji sana. Nimekuambia kistarabu hutaki sasa utanifanya kwa lazima, jua nchi hii ikiwa chini yetu hii ni sheria ilimpunguze kuzaliana. Sasa utaanza kufanya wewe kabla nchi haijapinduliwa" Askofu Valdermar aliongea.



                "Siwezi kufanya hivyo" Norbert alisema kwa jeuri huku akikagua kosa lolote linaloweza kujitokeza  kwa wapinzani wake, hakuona kosa lolote kwani maadui zake walikuwa makini sana na hapo akaamua atumie mbinu nyinginr kwani maadui zake alishabaini hawawezi kumuua eneo hilo pasipo kugunduliwa.



                "Mtumishi wa Mungu Albert upo kwenye Jack Shaw sasa hivi usiniite Bishop Valdermar, kifo ni haki yako ukatae ukubali. Unakataa ushoga kama rais wako alivyokataa kusaini mkataba aupitishe nchini kwenu ili mpate maendeleo" Askofu Valdermar aliongea huku akimtazama Norbert kwa dharau sana, Norbert alipatwa na mshtuko mwingine baada ya kubaini alikuwa yupo chini ya mikono ya Jack Shaw anayejiita Achim Valdermar pia alipobaini lengo lake kwa Tanzania.
                "Nipo tayari kufa nikauone ufalme wa Mungu lakini siyo kufanya ushetani unaotaka niufanye" Norbert alizidi kuonesha jeuri huku akipindisha mdomo, jambo hilo lilimkera sana Jack Shaw akataka kumpiga pigo ambalo lingemlegeza lakini alisita baada ya hali nyingine kujitokeza kwa Norbert muda huo pasipo wao kutegemea. Norbert alinyanyua kinywa chake ili azungumze lakini alionekana kushindwa kabisa, alionekana akihangaika kuvuta hewa kwa shida kisha akaanza kukohoa kwa mfululizo huku akiwa amejiinamia. Jack Shaw na vijana wake walibaki wakimshangaa tena Scorpio akabaki akimuangalia huku akiwa amepoteza umakini ingawa bastola  yake ilikuwa imemuelekea Norbert.



          "Kumbe ana  pumu huyu si atanifia mgongoni kwangu" Jack aljongea huku akimtazama Norbert aliyekuwa anakohoa mfululizo, hawakujua kama walikuwa wamefanya kosa kubwa mbele ya mtu mwenye akili nyingi za kufikiria kama Norbert. Hawakujua kama tayari Norbert alikuwa amecheza na akili zao kwa kufanya hila ya kujifanya amebanwa na pumu kumbe macho yake yalikuwa makini kumtazama Scorpio aliyekuwa na silaha mkononi, Scorpio tayari alikuwa amefanya kosa kwa kushughulika kumuangalia Norbert anayejifanya anakohoa kama ana pumu na hapo ikawa nafasi ya pekee kwa Norbert.



  Alifanya jambo ambalo hawakulitarajia kwa kujiinua juu kwa kasi kisha akaupiga mkono wa Scorpio ulioshika silaha, alienda sambamba na kuachia ngumi  nzito ya upper cut(ngumi hii hupigwa kwa chini ya kidevu) aliyoinuka nayo ambayo ilipiga kwenye eneo la chini ya kidevu cha  Scorpio hadi akaaanguka. Ngumi hiyo nzito ilienda sambamba na teke ya kisigino maarufu kama shukrani ya punda, teke hili lilimlenga Jack Shaw(Askofu Valdermar) lakini lilikosa lengo baada ya Askofu Valdermar kuhama eneo alilokuwepo kwa kasi ya ajabu.



 Norbert alipokosa lengo na pigo ake alijianda kuleta pigo jingine lakini alijikuta akiwahiwa kwa namna ya tofauti, kabla hajatoa pigo hilo mlio wa bastola ikitoa kikohozi hafifu kama cha mtoto mdogo ulisikika na hapo akahisi bega lake  likivamiwa na kitu kilichopenya ndani zaidi. Norbert hakutaka utaalamu kujua kwamba risasi ndiyo ilikuwa imevamia bega lake ingawa maumivu yalikuwa bado hayajaanza kusikika, damu kwa taratibu zilianza kumtoka na akaacha kupambana hapo hapa aliposikia kicheko kutoka mlangoni  eneo alilokuwa amesimama Spider.



  Muda huo huo Jack Shaw naye akaanza kucheka kwa nguvu, Norbert alipotazama kule mlangoni alimuona Spider akiwa ameitoa mikono yake aliyokuwa ameificha nyuma ambayo ilikuwa ilionekana ikiwa imeshika bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti. Moshi hafifu ulionekana kutoka ndani ya bastola hiyo na hapo akatambua kuwa aliyempiga risasi alikuwa ni Spider, hapo maumivu yalianza kuja kwenye bega lake kwa taratibu na akashika sehemu iliyokuea imeumia ili damu isitoke. Ujanja wa kujinasua ulikuwa umemuisha kwani alishabaini Jack Shaw aliyekuwa anapambana naye hakuwa mtu wa ksmawaida pamoja na watu wake pia, ilimbidi awe mpole tu huku akishikilia sehemu aliyokuwa ameumia.



  Hiyo ilikuwa nafasi kwa Jack Shaw ambaye aliachia teke kali lililotua kwenye bega la Norbert lililopigwa  risasi, Norbert aliyumba kurudi nyuma baada ya kushindwa kustahimili uzito wa teke hilo. Huko nyuma alikutana na teke jingine la kuzunguka lenye uzito mkubwa kutoka kwa Scorpio ambaye tayari alikuwa ameinuka tangu apigwe ngumi na Norbert, teke hilo lilimpeleka hadi chini kisha vicheko vikazidi.



                 "Kijana huwezi kuingia kwenye mikono ya Jack Shaw ukatoka ukiwa hai hata siku moja na ukijifanya mjanja utaumia kama ulivyoumia sasa hivi, ndiyo maana nimekuambia siri yetu nikijua hutoki salama. Haya nieleze wewe ni nani hadi uwe na ujanja kiasi hicho eti unajifanya una pumu hadi utake kunipiga. Jack ni ninja wewe hapigwi  kijinga namna hiyo" Jack aliongea kwa dharau sana, Scorpio ambaye alikuwa anatokwa na damu mdomoni alipomuangalia Norbert aliamua kumfuata kwa hasira hasa alipokumbuka ngumi nzito ya Norbert iliyotua kwenye kidevu chake. Alianza kumpiga mateke mfululizo ya mbavu ambayo yote yalimpata Norbert, alizidi kumpiga sehemu mbalimbali  za mwilini mwake  hadi pale Jack Shaw alipokuja kumzuia.



                    "inatosha! Mzibeni hilo jeraha tutoke naye hadi porini tukamuue" Jack Shaw aliongea  huku akimzuia Scorpio.



                    "Kanipiga ngumi hadi nimejing'ata ulimi huyu" Scorpio aliongea kwa hasira akataka kumuongeza pigo jingine lakini Jack Shaw alimzuia na  kumsukuma pembeni.



                   "Mume wangu anarudi muda si mrefu  na team nyingine na amesema hataki kumuona akiwa mzima na akimkuta anamchinja, mzuieni jeraha tukamuue msituni huyu" Jack Shaw aliongea na vijana wake wakafanya kama alivyowaagiza wakabeba na silaha ya kumuulia, walitoka na Norbert humo ndani huku wakitembea naye kiurafiki hadi kwenye gari moja ya hoteli hiyo ambayo waliilipia hela.



  Walimuingiza ndani ya gari Norbert huku wakimdhibiti asifanye ujanja wowote, safari ya kuondoka hotelini hapo kuelekea  katikati ya mbuga ya Serengeti. Waliiingia ndani kabisa ya msitu wa Serengeti hadi eneo lenye mwembamba  ambapo  walimfunga mikono na miguu kwa kutumia pingu  pasipo hata kumpekua zaidi, walipomaliza walitoa bomu aina ya C4 ambalo huwa na saa pamoja na baruti ambazo hufungwa mithili ya karoti na walilitega muda wa kulipuka.



                    "Albert mwana wa Mungu wasalimie huko mbinguni maana ndani ya dakika tatu bomu hili ninaloliweka mbele yako litasambaratisha viungo vyako vyote" Jack Shaw aliongea huku akimuita kwa jina la bandia alilojiita Norbert, wote kwa pamoja walicheka kisha wakaingia kwenye gari wakaondoka  kwa umbali wa mitaa takribani mia tatu halafu wakasimama. Walisubiri kwa muda wa dakika tatu hadi waliposikia mlipuko mzito wa bomu ukitokea walipomfunga Norbert, hapo walijua kazi yao imeshaisha na waliondoa gari kwa mwendo wa kasi.







 Kawaida ya mpelelezi siku zote ni kubeba vitu vitakavypmsaidia kwenye  jambo la dharura, Norbert naye ilikiwa ni kawaida yake kufanya hivyo akiwa yupo mahali popote hata kama akijihisi yupo eneo la lenye amani. Mwilini mwake siku zote alikuwa na silaha alizoziita mapambo ambazo humsaidia maeneo ya hatari, siku hiyo kabla hajaenda chumbani kwa Jack Shaw aliweka silaha mbalinbali pamoja na vitu vya ushahidi kama vile kamera ndogo aliyokuwa ameifunga kwenye kifungo cha shati lake. Mguuni alikuwa amepachika bastola  ndogo yenye kiwambo kidogo cha kuzuia sauti ambayo alitaka kuitoa hata alipokurupushwa usingizini na kugongwa kwa mlango, alipoambiwa abadilishe nguo yeye alifanya kazi ya kuiweka bastola hiyo isionekane katika nguo alizovaa.



Jack Shaw, Spider na Scorpio wakati walipomfunga kwa pingu katika mti bila ya kumpekua, walikuwa wamefanya kosa kubwa bila wao kutambua kama walikuwa wamefanya kosa. Walipoondoka wakiwa wametega bomu mbele yake tayari walikuwa wameamsha akili ya Norbert katika kujikomboa na hatari, pingu walizomfunga zilimfanya Norbert mgongo wake uwe kwenye gogo jembamba la mti huo mgumu.

Mikono na miguu yake vilikuwa vimefungwa kwa nyuma, bomu lilikuwa mbele yake tena mshale wa saa unaohesabu sekunde ulikuwa ukienda kwa mwendo wake wa kawaida huku ukizidi kuzipunguza dakika tatu zilizotegwa kwenye bomu hilo. Mlio wa mshale wa dakika katika bomu hilo vilimfanya Norbert ahangaike kujivuta mbele lakini ugumu wa pingu ulimrudisha palepale alipokuwa, alijaribu kujitikisa kulia na kushoto lakini ugumu wa pingu aliyofungwa ulimfanya asogee kidogo tu kwenda upande wa kushoto na kulia.

Hapo ndipo Norbert akakumbuka kwamba alikuwa ana bastola yake ya dharura aliyokuwa ameifunga mguuni, alizitazama sekunde katika bomu hilo zinavyomaliza dakika kisha akajilazimisha kupiga magoti kwa haraka huku mapigo yake ya moyo yakimuenda mbio kila akiitazama saa ya bomu ambayo ilkuwa tayari imeshamaliza dakika moja kati ya dakika tatu na sasa ipo dakika ya pili.

Alipopiga magoti chini alijitahidi kuupindisha mgongo wake pamoja na kuipindisha mikono yake aliyofungwa pingu hadi akafanikiwa, gogo alilofungiwa lilipita katikati ya miguu yake kwenye eneo la baina ya goti ma kifundo cha miguu. Hiyo ilimuwia rahisi kuweza kuulazimisha mkono wake kufika katika mguu wake kulia juu ya kifundo cha mguu, macho yake yalikuwa yakiitazama ile saa ya bomu ambayo ilikuwa ikitoa mwanga kwenye mishale yake eneo hilo la gizani ambayo ilimfanya Norbert ang’amue dakika zilizobaki ili bomu hilo lilipuke.

Mwendo wa sekunde katika saa hiyo kulimfanya azidi kuwa na kasi ya kutaka kujinasua katika kifo hicho kibaya cha kutawanywa viungo vyake na bomu, alifanikiwa kuufikisha mkono wake pale alipokuwa akihitaji ufike na aliuingiza mkono huo ndani ya soksi yake baada ya kuisogeza juu suruali. Alipekua katika soksi yake aliyoivaa mguu wa kushoto kwa haraka akitafuta akiitafuta bastola yake lakini hakuipata, hakukata tamaa aliamua kuipekua na soksi yake aliyovaa mguu wa kulia akafanikiwa kuipata bastola hiyo akaitoa haraka.

Moyo wake ulizidi kupiga kwa nguvu alipiangalia saa ya bomu hiyo ambayo ilionesha imebaki dakika moja na nusu kabla bomu halijalipuka, hakuwa na njia nyingine ya kujiokoa zaidi ya hiyo bastola ambayo tayari alikuwa ameshafanikiwa kuitia mikononi mwake. Aliishika bastola hiyo kwa tabu akaelekeza bomba la kiwambo cha kuzuia sauti kwa juu katika pingu za mkononi, alibinya kidude cha kuachia risasi katika bastola hiyo na hapo risasi ikakata pingu ya mikononi lakini bastola ikamponyoka ikamdondoka kwa bahati mbaya kutokana na jinsi alivyoishika.

Norbert aliachia mguno wa fadhaa ingawa hakutaka kukata tamaa hata kidogo, aliamua kupeleka mikono yake nyuma na kupapasa katika giza hilo kubwa kwa muda wa sekunde kadhaa hadi akaipata bastola hiyo. Kitendo kingine cha haraka ndiyo alikifanya cha kuikata pingu ya miguuni kwa risasi halafu akasimama haraka sana, aliangalia kwenye bomu akakuta imebaki nusu dakika tu yaani Sekunde 30.

Aliamua kukimbia kwa uwezo wake wote aliojifunza wakati yupo mafunzoni katika nchi tofauti, alifika umbali wa mita takribani mia moja na hapo ndiyo akasikia mlipuko wa bomu hilo ukitokea nyuma yake. Alishusha pumzi hapo kwa kufanikiwa kujikomboa na bomu hilo kisha akaketi chini ili kutuliza akili yake katika kivuli cha mti mkubwa, mkononi alikuwa ameishikilia bsstola ambayo ndiyo aliiona imekuwa msaada yake katika kumkomboa.

Alipumzika kwa muda wa dakika kadhaa kisha akasimama akaangalia pande zote akaona kupo shwari, alianza kukimbia kwa kasi sana akiwa hana uelekeo maalum kwani hakujua ni wapi pa kuelekea kwa usiku huo. Alikimbia sana na hatimaye akachoka akapumzika chini ya mti ya mti mwingine ambao aliuona salama kumbe haukuwa na usalama, hapo chini ya mti Norbert alijishika kidevuni mwake mithili ya mtu anayetaka kujichomoa kichwa chake. Alivuta kwa nguvu akavua sura ya bandia iliyomfanya atambulike kama Albert mbele ya Jack Shaw akabaki na sura yake halisi, hapo aliamua kutazama kamera yake ndogo aliyoifunga kwenye kifungo cha shati lake akaona ipo salama.

Norbert aliendelea kupumzika katika eneo hilo lililokuwa halina usalama ingawa yeye aliliona lipo salama, hakujua kama eneo la chini ya mti juu kulikuwa kuna mwindaji aliyeona windo lake muda huo wa usiku. Alikuja kujua hilo baada ya kuhisi majani yakijitikisa huko juu kuashiria kulikuwa kuna kitu kinaanguka chini  usawa wa eneo alilopo, Norbert hakutaka kujiuliza mara mbili juu ya kitu hicho kikichojiachia zaidi ya kubiringita pembeni halafu akajiinua kwa namna ya kiufundi kabisa. Alipoangalia katika eneo alikuwa amekaa hapo awali kwa msaada wa mbalamwezo ya usiku huo alimuona chui akiwa anamtazama kwa hasira, Norbert hapo alijua alikuwa ameingia katika anga za muwindaji wa pori hilo ambaye ilimpasa kuwa makini sana. 



Chui yule alitoa mngurumo wa hasira na aliruka upande ule aliokuwa yupo Norbert akiwa ametanguliza kucha zake mbele, Norbert alikuwa ameshaliona hilo na alihama eneo alilopo kwa kasi ya ajabu kisha akaishika bastola yake vizuri. Chui alipogeuka amshambulie tena alionja risasi ambayo ilitua kwenye paji lake la uso ndiyo ukawa mwisho wa upinzani wake  kwa Norbert, chuo huyo hakufanya purukushani wakati roho yake inaachana na mwili zaidi ya kutulia papo hapo.

Eneo la mbugani hapo hakuona usalama wake kama utakuwa mzuri ikiwa ataendelea kukaa, Norbert alinyanyuka na kuanza kukimbia kuelekea upande wa kaskazini.


ASUBUHI ILIYOFUATA,

    KARATU,

    ARUSHA



Gari kubwa la kubeba mizigo aina ya Scania liliokuwa limesheheni mizigo mingi lililokuwa likitoka nchini Kenya likupunguza mwendo ili liingie kwenye kituo cha kujaza mafuta, kupunguza huko mwendo kuliambatana na kufunguka sehemu ya juu ya gari hiyo kisha mwanaume mrefu aliyevaa shati ya rangi bluu bahari lenye mikono mirefu pamoja na suruali ya nyeusi kushuka kwa haraka akatua chini pasipo kuonwa na dereva wa hilo. Mwanaume huyo hakuwa mwingine isipokuwa Norbert aliyedandia gari hilo lilipopita katika barabara inayopita mbuga ya Serengeti usiku uliopita, gari hilo lilipunguza mwendo katika tuta usiku uliopita na hapo ndipo Norbert akapata nafasi ya kulidandia pasipo kujulikana.



Hadi saa nne asubuhi tangu alipolidandia gari hilo ndiyo alikuwa amefika wilayani Karatu mkoani Arusha ambapo alishuka , alitembea kwa haraka hadi pembezoni mwa barabara  huku akiwa na tabasamu pana kama ilivyo kawaida yake akitaka kufika katika eneo lolote analotaka kufika. Mifukoni mwake bado alikuwa ana vitu muhimu ambavyo vingemsaidia  kwenye shida ikimtokea, pochi yake yenye vitu muhimu yote ilikuwa ipo mfukoni mwake.

Norbert alishukuru Mungu kwa kutopekuliwa na Jack Shaw pamoja na vijana wake kwani laiti angepekuliwa basi hata hapo asingefika, muda wa saa nne asubuhi Norbert alikuwa tayari ameshachoka hivyo alihitaji muda wa kupumzika kama ilivyo wanadamu wengine wakiwa hawakupata usingizi. Aliamua kutafuta nyumba ya wageni ya bei ya kawaida ambayo alilipa akapata chumba, Norbert alipoingia ndani ya chumba alicholipia aliamua kujitupa kitandani kutokana na usingizi kuizidi hamu ya kula aliyokuwa nayo na ndani ya dakika chache tayari alikuwa amelala usingizi mzito.


Wakati Norbert akiwa anauchapa usingizi upande wa jiji la Dar es salaam tayari mambo yalishaanza kuwa mabaya zaidi kwa Moses, muda huo tayari ilikuwa imatimia siku ya tatu tangu Rais Zuber alipopewa agizo na L.J Ibrahim la kutoa maelezo ya kutohusika kwake na kifo cha Jenerali Kulika ikiwa  Moses mtu wake wa kuaminika alikuwa anahusika. Siku hiyo ndiyo siku ambayo L.J Ibrahim aliahidi kumtangaza Moses kama muuaji aliyehusika na mauaji ya Jenerali Kulika, Askofu Edson pamoja na Mufti.

Siku hiyo ndiyo alifanya hicho hicho alichoahidi ambapo alihitisha mkutano wa dharura wa waandishi wa habari, katika mkutano huo aliamua kueleza kwa kifupi juu ya nini chanzo cha mauaji hayo. Aliitaja sumu iligunduliwa na Moses ndiyo chanzo cha kifo hicho, L.J Ibrahim alieleza juu ya umiliki wa sumu hiyo ulivyokuwa wa kimakini mno ambapo isingewezekana kwa mtu yoyote kuupata pssipo kibali maalum.

Alizidi kwenda mbali zaidi akaeleza juu ya kutonunuliwa sumu hiyo ndani ya Tanzania zaidi ya kusafirishwa nje ya nchi tena mbali na bara la Afrika, katika maelezo yake hayo alibainisha sumu hizo kwa Tanzania mtu ambaye alikuwa akizimiliki ni mwenyewe aliyezitengeneza  hivyo alihitimisha kwa kumtaja yeye ndiye muuaji mkuu kutokana na ushahidi uliokusanywa. Alieleza Professa Moses Gawaza tangu yalipotokea mauaji hayo hakuwa ameonekana kazini kwake na sumu hizo bado zipo chini ya umiliki wake, mwisho wa maelezo ya L.J Ibrahim  ilikuwa ndiyo mwanzo wa hasira za  wananchi mbalimbali hasa waumini wa dini ya kiislamu na wakristo wa dhehebu la Kiluteri.

Maandamano makubwa yalifanyika na barabara zote zikafungwa na wananchi ambao walienda kuivamia Maabara ya Umoja wa mataifa wakaharibu vifaa vyote pamoja na kupiga wafanyakazi wake, vurugu hizo zilipozidi amri kutoka kwa Rais Zuber ilipelekwa kwa IGP Chulanga ambaye aliamriwa aagize vijana wake waweze kudhibiti hilo. IGP Chulanga naye alitoa amri kwa makamishna hatimaye kikosi cha jeshi la polisi cha kutuliza ghasia nacho kikapewa amri kikaingia kazini.

Askari hao waliingia maeno ya katikati ya jiji yaliyokuwa yakiongoza kwa fujo wakajitahidi kuzuia fujo lakini walishindwa kabisa kuzuia vurugu hizo na wao wakajikuta wakizidiwa na wananchi wenye hasira kali, hata walipochukua uamuzi wa kunyoosha bendera nyekundu juu kisha wakawaua watu wachache ndiyo kwanza hasira za wananchi zilizidi wakajikuta hata nao wakirudi nyuma kwani tayari walishaanza kushambuliwa.



Vurugu hizo ziliwazidi askari wa kutuliza ghasia na hawakuwa na la ziada ya kukimbia kuokoa maisha yao kutoka kwa wananchi hao, amani ndani ya katikati ya jiji la Dar es salaam wakati Norbert akiwa amelala usingizi mwanana huko Karatu ilikuwa imevurugika. Matukio mbalimbali ya fujo hizo yalikuwa yalirushwa moja kwa moja na vyombo vya habari kupitia kwa kamera zilizokwa zimefungwa kwenye ndege, ilikuwa ni tukio liliogusa hisia za raia wengi wa nchi jirani waliobahatika kuliona kupitia vyombo vya habari.

MIKOCHENI

Eneo hili pia hali ilikuwa hiyohiyo ambapo wakazi wengi wa eneo hilo walikuwa wamejifungia majumbani mwao, nyumba ambayo inatambulika na umma kuwa ni makazi ya Moses tayari ilikuwa imevamiwa na wananchi wenye hasira kali wakiharibu vioo vya nyumba hiyo ya kisasa huku baadhi ya vibaka wakiitumia nafasi hiyo kuiba samani na vitu mbalimbali vilivyomo humo ndani. Uharibifu wa nyumba hiyo ya Moses uliendelea na kuifanya ikawa haina dirisha wala mlango, wananchi hawakuridhika hsta kidogo na uharibifu huo kutokana na kumkosa mhusika waliyekuwa wanamtafuta. Kitendo cha kumkosa Moses waliamua kuichoma moto nyumba hiyo pamoja na magari yake yote ambayo alitumia jasho lake katika kuyanunua, waliiacha nyumba hiyo ikiqa imeteketea moti hadi ikabaki gofu ndiyo wakaondoka eneo hilo.


Matukio yote yaliyokuwa yakitendeka ndani ya jiji la Dae es salaam yalikuwa yakishuhudiwa na mtuhumiwa mkuu Moses kupitia luninga iliyopo ndani  ya sebule ya nyumba ya EASA Kurasini, alikuwa akiangalia tukio hilo pamoja na Dokta Hilaty na Irene ambao walimsikitikia sana  kwa kile kilichompata. Moses aliishuhudia kwa macho yake nyumba aliyoijenga kwa fedha nyingi, alikuwa akiyashuhudia magari yote aliyotumia pesa nyingi katika kuyanunua yakiungua kwa moto. Alibaki akisikitika kupoteza mali zake lakini moyoni mwake alikuwa akihisi afadhali kwa kumuokoa mke wake kipenzi juu ya mabalaa yaliyokuwa yakikaribia kumkumba.



         "Aisee Mose pole sana" Dokta Hilary alimuambia huku akimshika bega lake.



         "Ni jambo la kawaida Hilary  kupoteza mali ndogo mojawapo ya mali  nyingi, poa ni jambo la kawaida kupotezewa heshima mbele waliyokuwa wanakuheshimu. Jambo baya kabisa ni kupoteza moyo na ndiyo nimeliepuka kwa kumsafirisha Beatrice pia na wewe nikakuepusha kwa  kumkomboa Shem Irene" Moses aliongea akiwa ameshika tamaa kwa simanzi kubwa, mawazo yalikuwa yamemzonga kichwani mwake ingawa yeye alichukulia ni jambo la kawaida. Muda huo akiwa kwenye mawazo simu yake ya  mkononi iliita na akaitoa  akaangalia jina kisha akawatazama Dokta Hilary na mke wake.



          "Beatrice huyu nafikiri taarifa kaipata" Aliwaambia kisha akasimama  akapokea simu akaiweka sikioni , "hellow honey.......nipo okay usijali mke wangu kuwa na amani........no! No! Usije mpenzi baki tu everything will be alright.... kuwa muelewa mke wangu ukija utapata matatizo....okay kuwa na amani na umalize ziara yako nitakuja kulufuata mwenyewe, subiri niongee na mama huyu anapiga"



   Moses aliikata simu hiyo kisha akapokea simu yake nyingine ya mkononi akaongea, "Naam mama....nimechezewa mchezo mama yangu sihusiki chochote.....asante sana mama.....Mke wangu yupo salama nafikiri baba atakuambia kila kitu juu yake......asante mama"



Moses alikata simu kisha akawaangalia Dokta Hilary na mke wake halafu akashusha pumzi, aliamua kujitupa kwenye kochi huku akionekana na mawazo mengi.



        "Shem vipi mbona hivyo?" Irene aliuliza.



        "Beatrice anajua kila kitu kilichotokea huku na alikuwa anataka kurudi lakini nimemkataza" Moses aliongea.



       "Sasa wasiwasi wako ni nini?"  Dokta Hilary aliuliza akamfanya Moses akae vyema kwenye kochi huku akitoa simu yake ya mkononi.



        "Beatrice nimemkataza lakini kwa jinsi minavyomtambua atakuja yule kwakuwa bado haamini, cha kufanya ni kumzuia tu" Moses aliongea huku akibonyeza namba kadhaa kisha akaweka simu sikioni mwake, "hakikisha mke wangu hapati njia ya kurudi Tanzania weka vikwazo kote"



Alipokata simu aliondoka  eneo la sebuleni akiwaacha Dokta Hilary na mke wake wakiwa hawamuelewi kabisa.

GEREZA LA UKONGA

       PUGU

Hali ya afya ya Ole ilibadilika na kuwa mbaya kwa ghafla tu akiwa yupo ndani ya chumba chake cha gereza, hali hiyo ilisababisha mkuu wa gereza hilo atoe amri ya kukimbizwa hospitalini kwani hakutaka afe mpaka yeye amuue kwa mikono yake ili ajipize kifo cha mdogo wake aliyeuawa kwa njama zake Filbert Ole kipindi alipokuwa madarakani.

Gari aina ya landrover mali ya jeshi la magereza ambayo hutumika kubeba wagonjwa ilitoka ndani ya gereza hilo ikiwa imeongozana na toyota land cruiser mbili zilizojaa maaskari ambazo zilikuwa zimekaa mbele na nyuma ya gari hilo. Msafara huo uliingia barabara ya mwalimu nyerere kwa kasi mno ukawa unaelekea katikati ya jiji, magari mbalimbali yaliyopo barabarani ilibidi yapishe msafara huo upite kutokana na kasi yake pamoja ma makelele ya ving’ora yaliyokuwa yakisikika. Msafara huo ulipita kwa kasi sana hadi kwenye kituo cha daladala cha njia panda ya Segerea ukakata kona kuingia kushoto.

Msafara huo kwa kasi ya ajabu ulipita hoteli maarufu ya kulaza magari na watu Ukonga maarufu kama Transit Motel, ulizidi kwenda mbele ukavuka mgahawa maarufu wa Salum machips ns ukawa unaekekea katika eneo ambalo barabara hiyo inakutana na reli ya kampuni ya TRC. Mwendo mkali uliokuwa unaitumia ulisababisha msafara huo ufike mapema kwenye makutano na ulipunguza mwendo ukavuka reli hizo kisha ukaendelea mbele, haukufika mbali msafara huo ulisimama kwenye njia panda baada ya gari kubwa la mizigo kuziba njia kutokana na kuharibika. Askari wenye silaha walishuka wakawa wanalinda  gari lililombeba mgonjwa huku askari wengine wakiwa wamesogea mbele kuangalia tatizo lililokuwa limetokea ndani ya gari hilo la mizigo hadi lisimame.



Askari hao wakiwa wanalinda eneo hilo hawakutambua kama walikuea wamefanya makosa sana kupita barabara hiyo kutokana na msongamano wa magari  kule Tazara ambapo iliwawia vigumu kupishwa, gari la wagonjwa walilokuwa wanalitumia hawakutambua kwamba lilikuwa lipo wazi sehemu ya chini ambapo kulikuwa kuna mfuniko ukisogezwa tundu linabaki wazi.



Mfuniko  huo ulikuwa umekaa sambamba na mfuniko wa mtaro mkubwa wa maji upitao ardhini ambapo ndani ya mtaro huo kulikuwa kuna watu chini waliokuwa wakisubiri kwa hamu nafasi hiyo waweze kuitumia. Watu hao walifungua mfuniko huo kisha wakafungua  mfumiko wa chini wa gari wakapuliza dawa iliyowalaza wauguzi wote kasoro dereva wa gari hiyo aliyekuwa amefunga kioo kulichopo nyuma yake ambacho hutumiwa kuwasiliana na wauguzi waliopo nyuma, walimshusha Ole ndani ya gari hilo kisha wakatega bomu wakafunga vilevile wakarudi ndani ya mtaro wa maji machafu wakatokomea bila kujulikana.



Maaskari wa Magereza waliona ni jambo gumu sana kupita kuendelea kwa muda huo hadi gari hilo la  mizigo liondolewe, hali hiyo iliwafanya warudi kule walipotokea ili wapitie barabara ya Mwalimu Nyerere. Iliwabidi pia wawasiliane na Askari wa usalama barabarani waliopo makutano ya barabara ya Tazara ili waruhusu magari yote ya upande waliopo waweze kupita njia ikiwa tupu.



Walizidi kuongeza mwendo wa magari yao wakijua wana mgonjaa kumbe walikuwa wamebeba hatari kubwa katika hilo gari la wagonjwa, walipofika makutano ya barabara ya Mwalimu Nyerere kwenye kituo cha daladsla cha Njia panda ya Segerea ndiyo balaa hilo lililokuwa limelala liliamka kwa ghafla.



Mlipuko mzito ndiyo uliamka ukachukua nafasi yake kweli gari lilikokuwa limebeba wauguzi askari, gari la wagonjwa lilirushwa juu zaidi nap mlipuko huo. Magari ya mengine yaliyosalia yalipoteza muelekeo ambapo la mbele lilipitiliza hadi kando ya barabara na la nyuma lilienda kugonga kituo cha daladala cha njia panda  ya Segerea.



 Raia wa kawaida waliopo eneo hilo hawakuweza kustahimili kubaki na kuangalia tukio hilo, kika mmoja alikimbia  akifuata njia anayoijua yeye au anayoona yeye inaweza kumuokoa. Baadhi yao walikimbia pasipo uelekeo maalum kutokana na kuchanganyikiwa, ilikuwa ni patadhika juu ya tukio hilo ambalo halikuwa na tofauti yoyote na tukio la ugaidi.

Muda ambao kunatokea mlipuko mzito wa bomu kule Ukonga ndiyo muda ambao Norbert anaamka usingizini katika chumba cha nyumba ya wageni alichokodi. Uchovu wa mwili wake tayari ulikuwa umemuisha na sasa alijisikia yupo imara kuliko kawida, njaa pekee ndiyo ilibaki kuwa bughudha kubwa sana kwa mwili wake na ikambidi aende kupata chakula aondokane na bughudha hiyo iliyokuwa ikishambulia tumbo lake.

Alitumia muda wa robo saa tayari akawa ameshaiondoa bughudha iliyokuwa ikiushambulia tumbo lake na sasa akabaki na bughudha moja ya taka mwili zilizopo mwilini kutokana na kutooga toka usiku uliopita alipojinasua kwenye mdomo wa kifo. Alitumia muda huo wa mchana kwenda kununua nguo mpya katika duka la nguo hapo Karatu, alioga kisha akabadili nguo zile pamoja na kuhamisha mapambo yake ya kujihami.

Majira saa kumi alasiri aliwasha simu yake ambayo aliizima kutokana na kazi zake, muda huo huo alianza safari ya kuiacha wilaya ya Karatu ili aende uwanja wa ndege wa Arusha aweze kurudi jijini Dar es salaam.

Alikuwa yupo katikati pikipiki ya kukodisha ambayo ndiyo aliona ni njia pekee ya kumfikisha uwanja wa Ndege wa Arusha haraka sana, kutokana na mwendo mkali uliokuwa unatumiwa na dereva wa pikipiki hiyo alitumia saa moja na akawa tayari yupo katika uwanja wa ndege wa Arusha.

Norbert aliingia ndani ya uwanja ya ofisi za uwanja wa ndege wa ndege eneo la mapokezi akaizima kamera yake ndogo, hapo alikutana na sura ya msichana mrembo ambaye alimtolea tabasamu la kebehi tu baada ya kumuona. Norbert naye alirudisha tabasamu na akajongea katika dawati la mapokezi uwanjani hapo, alipofika aliegemeza viwiko vya mikono juu ya dawati hilo akawa anamtazama huyo binti kwa tabasamu pana.

           "Loh! Mwanaume mbaya wewe" Yule binti alimuambia.



           "Haaaaaa! Bibie  ndiyo salamu yako hiyo" Norbert alimuambia yule binti.



           "Yaani hata hiyo hamu ya kukusalimia sina kwakweli, unaingia Arusha hadi sasa hivi najua unataka kuondoka bila kunipa taarifa" Binti huyo alimuambia Norbert huku akionekana kutopendezwa.



            "Fatma unajua nimekuja ghafla tu nisamehe mke wangu, ukininunia wewe dunia nzima chungu kwangu" Norbert alichombeza huku akimtazama usoni na binti huyo akaanza kuangalia kando.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



            "We sema tu tiketi ya Dar jioni hii siyo kuniletea hizo ngonjera zako" Fatma aliongea huku akikwepa macho ya Norbert.



             "Haaaaaa! Fatma maneno gani hayo kwahiyo mimi sipaswi kukuambia maneno mazuri tu lazima unihisi nataka kusafiri kupitia wewe unifanyie mambo marahisi, ok tufanye hivi ngoja niende ofisi za makampuni ya ndege zenyewe nitapata hata ya kesho asubuhi. Jioni njema bibie" Norbert aliongea maneno hayo kisha akaanza kupiga hatua taratibu kuondoka eneo la mapokezi akawa anaelekea nje, hakutaka hata kutazama nyuma kumuangalia Fatma.

ITAENDELEA

Wakala wa Giza Sehemu ya Tatu

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment