Jiue Mwenyewe Sehemu ya Tano
IMEANDIKWA NA : RICHARD MWAMBE
Simulizi : Jiue Mwenyewe
Sehemu Ya Nne (4)
Gina alijisikia vizuri kiasi chini ya matibabu ya hali ya juu kutoka kwa Dr. Jasmine, aliweza hata kusimama na kutembea kidogo japo alilalamika kuwa kichwa ni kizito sana. Kila mtu alifurahi.
โWalinipiga kichwani kama si rungu basi gongo kubwa sana, niliona sayari zote tisa kisha giza,โ akamweleza Jasmine, โKamanda Amata yuko wapi?โ akahoji.
โYupo, yeye ni mzima na sasa yupo kazini kama kawaida,โ Jasmine akamjibu.
โDr Jasmine, wale jamaa ni wauaji, naomba nikamsaidie Kamanda, atakuwa matatani sasa,โ Gina alikuwa akiongea kama anayeweweseka.
โHapana, we ni mgonjwa bado, pumzika kwanza,โ Jasmine alimshika mkono na kumlaza kitandani kisha akamchoma sindano ya usingizi ili apate kumpumzisha mwili wake, Gina akalala fofofo.
Simu ya mezani ikaita kwa fujo, Dr. Jasmine akaiwahi na kuiweka sikioni.
โHello!โ
โYeah, unaongea na Kamanda Amata, Chiba yuko wapi? (โฆ) mwambie afanye juu chini anione usiku huu nina shida naye nyeti sanaโ.
โUmesomeka Kamanda,โ Dr Jasmine akajibu na kukata simu.
CLUB BILICANAS โ saa 6:23 usiku
KULIKUWA NA WATU WENGI kila kona ya jumba hili la starehe, jumba linalotikisa jiji zima la Dar es salaam kwa umaarufu wake. Wavulana wa kisasa na wadada wao walijazana, wanaocheza disco twende wanaovuta sigara au bangi sawa tu, wanaouza miili wakiwa nusu uchi kila kona walikuwa wakijivinjari kutega mawindo yao. Hapa ndio palikuwa mahala pa kila uovu, wapo waliokuwa wakipanga mbinu za kuvunja, kutia mimba, kutoa mimba na kila jambo lilizungumziwa humo.
Akiwa ndani ya suruali yake ya cadet nyeusi, fulana nyeusi na kizibao cheusi juu ambacho ndani yake kilisheheni zana za kijasusi za kuua na kutoa pumzi za watu, kwenye soksi zake akiwa kabana bastola mbili, moja huku na nyingine kule, akapanda juu ya kiti kimoja kirefu, kati ya viti vingi vilivyokuwa hapo mbele ya kaunta hiyo kubwa ya kisasa, akiangalia kushoto, na kulia kila mmoja alikuwa na kinywaji kizito mkononi mwake, ama akinywa yeye au akimnywesha binti aliyekuwa naye hapo, kisha wanapigana mabusu. Akawatazama kwa wote kwa tuo, akawaona jinsi walivyo safi, hakuna mwenye mawaa yoyote zaidi ya funguo za gari mfukoni au sarafu za mia mia na mia mbili mia mbili, akatabasamu, akaishusha miwani yake na kuiweka kwenye mfuko wa kile kizibao, kisha akatoa kofia pama yake iliyokunjwa huku na kule kama ya Marlboro, mandevu yake yalimfanya aonekane kama jambazi sugu. Kila mtu alimgwaya kwa mawazo kama si kukaa mbali naye.
Kama kawaida ya warembo, mmoja akajipitishapitisha ili apate chochote kwa mtu huyo, lakini kama angejua kuwa mtu mwenyewe kaja kwa kazi zake asingepoteza muda.
โUnataka nini?โkamwuliza yule binti.
Binti akamtazama usoni mtu huyo na kumrembulia macho.
โSihitaji hiyo biashara, chukua unachokunywa upotee,โ yule mtu akamwambia yule binti, kisha akageukia kaunta.
Nipe Tonic Water na Konyagi ndogo, usisahau vipande vya barafu,โ akaagiza, na kinywaji kikaletwa.
Mara akahisi anaguswaguswa mgongoni, akaelewa maana yake nini, akainua glass na kujimiminia kinywani, kisha akateremka na kuacha vinywaji pale kaunta na noti ya elfu kumi, akamfuata huyo aliyemgusa. Wakatoka pamoja mpaka nje. Wakaingia kati kichochoro kimoja.
โKamanda! Hata mimi sikukujua,โ Chiba alizungumza.
โKawaida tu, leo nina kazi kubwa kaka, nataka uwe nami,โ Kamanda Amata akamwambia Chiba.
โUsijali nipo jirani yako,โ akaingiza mkono katika kimkoba chake, akatoa bastola moja nyeusi safi kabisa, ukiitazama unaweza kusema ni ya plastiki. Kamanda akaitazama, akatikisa kichwa.
โYa Kirussia,โ akatamka.
โNdiyo, lakini nimekaa chini nikaimodifai tena, sasa ni ya Kitanzania,โ aliposema hayo Chiba waote wakacheka, โtazama hapa,โ akashika katikati mahala kwenye tumbo panapojaa risasi kabla hazijafyatuliwa, akapazungusha kwa namna yake na kufyatua kitu kama pini akakiamishia mahala pengine lakini vyote hivyo alivifanya kwa mkono mmoja.
โUkishaweka hapa, Kamanda, Umejiua!โ akamwambia. Kamanda Amata akaitazama na kujaribu kufanya vile alivyoambiwa, โsafi sana Chiba, tunajivunia kuwa na mtu kama wewe.โ Akaipachika ile bastola katika kizibao chake.
***
Majira kama ya saa saba hivi, Amata alikuwa akiambaa ambaa na korido za maduka na maofisi, akaufuata mtaa wa Samora na kuipita picha ya Askari akaikuta barabara ya Pamba na kukunja kulia, kisha akaingia kwa ndani kidogo akapita kituo cha mafuta na kuibukia katika ukuta wa hoteli anayoitaka, Motel ya Agip.
Kama mwenyeji, aliingilia mlango wa nyuma ambao hutumika na watu wa usafi kuingilia ndani, akapenyapenya mpaka alipoukuta mlango wa pili akautikisa umefungwa, akachukua funguo zake na kuchezesha kidogo tu, mlango ukakubali, alipoufungua ili apite, kulikuwa na watu wanatokea upande huo, akaurudishia na kujibana nyuma yake. Walipopita naye akafuata, viatu vyake havikufanya kelele hata kidogo, akazikwea ngazi mpaka mlango namba 206. Akasimama kwa sekunde kadhaa, akatzama huku na huko, hakuna mtu, zaidi ni miungurumo ya mashine za kupoza hewa zilizokuwa zikiunguruma ndani ya vyumba hivyo, ukiacha hiyo ni sauti za watu walio kwenyea raha zao, wakipiga kelela za malalamiko ya raha. Akachukua kamera ndogo yenye umbo ka waya na akaipenyeza kwenye tundu la ufunguo mpaka upande wa pili, akapiga picha na kuitoa, akachomeka katika simu yake na kutazama, ndani kote ni salama, hakuna mtu. Akairudisha, akatia funguo na kuufungua mlango na kuingia ndani. Alipohakikisha kila kitu kipo sawa, na usalama wa kutosha, akavuta kiti akaketi nyuma ya mlango akitazama kitandani, pembeni akajiwekea pombe kali akinywa.
Mwanga hafifu ulikuwa ukimulika ndani ya chumba hicho, akiwa kajibana nyuma ya mlango kwenye kiti kidogo, akachomoa bastola yake kwenye soksi, akaiweka chini sakafuni kisha kwenye kizibao chake akatoa kiwambo cha sauti akaichukua ile bastola na kuifunga barabara ili isilete kelele itakapokuwa kazini. Akaitazama saa yake, inakimbilia saa nane usiku.
Mara akasikia sauti ya viatu ikija upande huo kutoka kwenye korido upande wa nje, akaiinua bastola yake na kuiweka tayari, lakini akili yake ilitambua kuwa sauti ya viatu hivyo ni kama vya kike na pia mwendo akautambua kuwa ni wa kike, akasubiri aone maana alijua wazi kuwa Mc Field ana uwezo wa kujifanya hata Mwanamke ili tu atimize lengo lake.
โUlinitoroka kipindi kile leo huchomoki,โ akajisemea huku akijikuta hasira zikimtawala taratibu. Mara funguo ikapachikwa katika tundu lake, ikafungua mlango, Kamanda Amata akatulia kungoja kuona nani anayeingia.
Mwanamke, aliyeonekana kama Mwarabu, mweupe, mrefu kiasi, mikononi alikuwa na mkoba, vazi jeusi linalometemeta lilikuwa limefunika mwili wake juu kabisa ya mapaja na kuishia juu kidogo ya matiti. Kamanda Amata akameza mate, kisha akalegeza mkono ulioshika bastola yake. Yule Mwanamke akaiendea swichi, alipotaka tu kuwasha, akashangaa taa ile inawaka sekunde mbili kabla yeye hajawasha, akashtuka. Mara akasikia kitu kama glass ikiwekwa mezani, akageuka na kukutana uso kwa uso na domo la bastola ya Amata. Mwanamke yule akaanza kutetemeka.
โUsiniue nakusihi!โ aliongea kwa sauti ya woga na kubembeleza.
โHuwa siui warembo kama wewe, jibu maswali yangu mawili tu,โ Kamanda akamwambia huku akiweka sawa kofia yake aina ya pama kichwani, โwewe ni nani?โ
โAaaa! Aaaa! mimi naitwa Amba,โ akajibu, lakini lafudhi yake ilionesha kabisa kuwa hakuwa Mtazania.
โSwali la nyongeza kabla ya la pili, unatokea wapi na unafanya nini hapa?โ akamuuliza.
โMimi natokea Afrika ya Kusini, nipo Tanzania kwa miaka miwili sasa, nafanya kazi Las Vegas Cassino, huyu ni mteja wangu tangu afike hapa miezi mine ilopita, huwa nakuja kumstarehesha kwa ujira mnono, nafikiri umenielewa, niache niende,โ akajibu haraka haraka huku akirudishia viatu vyake miguuni tayari kuondoka.
Amata akamuoneshea ishara ya kuwa hawezi kuondoka.
โSwali la pili, mteja wako yuko wapi?โ akamhoji tena.
โAnakuja, amesema kuna kazi anamalizia kufanya lakini anakuja akanambia mimi nitangulie huku anikute,โ akajibu kwa ufasaha.
โGood girl, sasa huwezi kuondoka, panda kitandani umsubiri mteja wako, tena tulia kimya, lete mkoba wako hapa,โ akamwamuru, yule Mwanamke akaupeleka mkoba, Kamanda akaukagua ndani, akakuta vipodozi, simu, pedi, helleni, pete ya dhahabu na mikufu, bangili za kisasa, kitita cha pesa za kigeni na funguo za gari.
โOk,โ akauweka ule mkoba chini huku mkononi akiwa kabaki na simu ya yule Mwanamke, โMsubiri mteja wako kama ulivyopanga kumsubiri,โ akamwambia. Lakini yule Mwanamke akabaki haelewi anachoambiwa.
โHuelewi? Vua nguo zako panda kitandani jifunike umsubiri, mi sina shida na wewe nina shida na mteja wako ambaye hata mimi ni mteja wangu vilevile,โ akamwambia. Yule mwanamke akavua kigauni chake, akabaki na sidiria nyeusi, na chupi mchinjo ya rangi hiyo hiyo. Akavua sidiria, lo, Amata akaona akili ikimwenda mbio maana titi zilizojaa vizuri zilikipendezesha kifua chake, wekundu wake uliweza kumfanya Mwanaume yeyote rijali apate shida katika suruali yake, akaondoa na ile chupi akabaki kama alivyo, Kamanda Amata alilisanifu umbo mwororo la Amba. Yule Mwanamke akapanda kitandani na kuvuta shuka mpaka kidevuni, Amata akazima taa.
Majira ya saa tisa usiku, Kamanda Amata alihisi mlango ukitikisika, mara ukafunguliwa kwa kasi kwa minajiri ya kumbamiza pale alipo. Mc Field aliingia haraka bastola mkononi na kuwahi kutazama nyuma ya mlango, hamna mtu, isipokuwa chupa ya pombe na bastola.
โShiit!โ akashangaa na kutamka kwa sauti ya chini. Wakati huo Amba nae alikuwa amekurupuka kwa kishindo kile.
โTulia vivyohivyo, umeingia mikononi mwangu tena,โ Sauti ya Kamanda ilisikika nyuma yake.
Kumbe Kamanda Amata baada ya kuhakikisha kuwa Amba amepitiwa na usingizi alitoka pale alipo na kujificha bafuni akiwa amejua wazi hila za adui wake kwani alishajua kwa vyovyote huko aliko anafuatilia mazungumzo yake na mwanamke huyo, na alijua kwa vyovyote atajua ni wapi alipokaa kutokana na vyombo vyake vya mawasiliano jinsi alivyoviunganisha. Mc Field alijikuta hana ujanja, amewahiwa, akataka kugeuka kumtazama mtu huyo.
โTulia, weka bastola yako chini. No! No! usiiname irushe chini,โ akamwambia, maana alijua kujitikisa kidogo mtu huyo anaweza kuleta madhara makubwa, โsafi sana, umekuwa kijana mpole sana siku hizi na si mtukutu kama zamani,โ maneno hayo ya dharau yalimtia hasira Mc Field. Alitamani amrukie Amata lakini alijikuta hana ujanja, alibakiwa na mbinu moja tu na alikuwa akitafuta jinsi ya kuitumia.
โGeuka, mikono yako ikiwa juu,โ akamwamuru. Mc Field akageuka.
โHa ha ha ha leo una sura ya Kihindi, hivi wewe kwa nini umekuwa mwoga namna hiyo siku hizi? Umeanza kuzeeka ee? Basi leo ndiyo mwisho wako, roho yako nitaitia kwenye mfuko wa ruruali yangu. Nani amekutuma kuja huku tena? Kufanya nini?โ akamtupia maswali baada ya kumkejeli.
โHilo hupaswi kujua mbwa mweusi kama wewe, waume zenu wanaowalisha ndiyo walionituma, nimetumwa kuua, kukuua wewe!โ alipojibu tu, akashusha mkono haraka, Kamanda Amata alikuwa keshaona hiyo, aljirusha akabiringita upande wa pili wa chumba, risasi nyembaba ikapiga kwenye kabati la vioo likatawanyika. Amata akajinyanyua haraka, alipotulia tu, ngumi kali ya Mc Field ikatua shavuni, ya pili ikadakwa sawia.
Amba alikurupuka kutoka pale kitandani akajikunyata kwenye kona ya chumba. George Mc Field akatumia kichwa kumpiga Amata, Amata akamwachia ule mkono, akayumba na kuanguka chini, akajibamiza ukutani, akamwona Mc Field akimjia na kisu mkononi, akavuta stuli ndogo na kuirusha kwa mikono ikampiga Mc Field usoni, kisu kikamtoka mkononi. Kamanda akanyanyuka, akapiga round kick, miguu yake ikamchapa Mc Field sawia kichwani ikampeleka mpaka kitandani. Mc Field akajirusha upande wa pili wa kitanda kulikuwa na ua la plastic lililowekwa katika bilauri kubwa la kioo, akaliinua na kwa kutumia mkono wake wa kulia uliojaa vizuri akalirusha kwa Amata. Hakika kama angekuwa mtu wa kawaida bilauri lile lingemuumiza vibaya lakini Amata alilipiga kiustadi kwa mikono yake na likatawanyika vipande vipande, akamwona Mc Field hewani akija kama Mbogo aliyejeruhiwa, Amata akamuepa, jamaa akatua chini peke yake.
Mzungu huyo akatega mikono yake katika mtindo mahili wa kung fu kumkabili Amata, miguu yake aliipanga katika namna ya kupendeza na mikono yake ilizunguka taratibu ikionesha jisi pigo lijalo litakavyomaliza kazi. Usoni mwake tayari damu zilikuwa zikitiririka. Kamanda Amata naye akaweka mtindo mwingine wa Kung fu naye akasimama kwa namna yake kumkabili Mc Field, hakuna aliyetabasamu wala kucheka, kila mtu alikuwa na โpepo la mautiโ.
Amba, alinyanyuka pale kwenye kona na kuiwahi bastola ya Mc Field iliyokuwa chini, Kamanda Amata akaona hilo, alipogeuka kidogo tu, maana alijua hatari inayokuja, alijikuta akipata mapigo matatu ya Kung fu ambayo hakuweza kuyakinga hata kidogo, maumivu makali yakalifikia bega lake akahisi kama limevunjika. Mc Field akaanza kumpelekea mashambulizi ya haraka haraka ambayo yalimpoteza kabisa Amata, akaanguka chini kama gunia la karanga, akajigeuza na kulala kifudifudi.
โMwisho wako umefika, unafikiri kila mtu ni wa kuchezea, sasa leo Tanzania itakuomboleza wewe na Rais wako,โ Mc Field alimwambia Amata kwa hasira huku akiuma meno, alikuwa akimsogelea taratibu pale alipo.
โInuka, nikumalize, mbwa mweusi we! Akamkamata ukosi wa kizibao alichovaa na kumburuza, nitakuuwa kwa kukuchinja, nitatenganisha kichwa na kiwiliwili chako,โ alimwambia huku akimburuza kumpeleka bafuni. Amata alikuwa hoi, mkono wake ulikuwa umevimba, damu zikimtoka upya kwenye jeraha lake, lakini hakuona haja ya kuuawa kikondoo. Aliukamata mguu wa Mc Fiel kwa mkono uliobaki, Mc Field akashtuka na kuinama kumtazama, kwa kutumia mkono uleule uliovimba alimdaka shati na kumvuta mpaka chini kisha akamshindilia konde zito la kwenye koromeo, Mc Field akalegea na kukohoa sana.
โVipi?โ Madam S aliuliza.
Chiba akamtazama kabla ya kumjibu, โsaa kumi inakaribia,โ akajibu. Scoba bado alikuwa kwenye usukani akiendesha taratibu.
โGari ya Mc Field hii hapa maegeshoni,โ Chiba akamwambia Madam.
โKamanda yuko kwenye mtanange,โ akamwambia Madam S huku akiweka bastola yake vyema, โnisubirini hapa,โ akawaambia Scoba na Madam S.
Utulivu ulitawala katika mitaa ya katikati ya jiji, na hata katika Motel. Hata wahudumu wa mapokezi walionekana wanasinzia kwenye makochi wakiangalia TV, hakuna aliyejua wala kuhisi nini kinatukia muda huo ghorofa ya pili, ya jengo hilo. Maana mapambano ya watu wazima yalikuwa ni mapambano ya kimya kimya.
Madam S alikuwa na mawazo mengi sana usiku huo, maana alijiuliza maswali yasiyo na majibu, umri nao ulimfanya ashindwe kupata majibu ya haraka haraka. Alikuwa ametulia tuli katika gari kiti cha nyuma.
โBora hata sikuwahi kuolewa!โ akasema. Scoba akamtazama na kucheka, โkwa nini?โ akamwuliza.
โNamna hii si ngeshaachika maana hata huyo mume angenipa talaka, saa tisa hii mwanamke niko nje sihudumii ndoa,โ akaongea huku akicheka.
โHivi Madam huna hata mtoto wa dawa?โ Scoba akauliza.
โNinao!โ akajibu.
โWangapi?โ
โWatano,โ
โWatano!โ Chiba akashangaa.
โNdiyo, watano, wa kike wawili na wa kiume watatu ila ni watukutu balaa, ndio wananifanya mi nisilale mpaka sasa,โ akawajibu. Wote wakacheka kizungu bila kutoa sauti.
Chiba akiwa katika kujiandaa kuelekea katika ile motel, mara walisikia sauti ya kioo kinachovunjika na sekunde chache kitu kama jiwe au furushi kilitua juu ya gari moja iliyokuwa imeegesha upande mmoja wa motel hiyo.
โNini ?โ Madam akauliza. Akaivuta bastola yake na kuelekea kule alikoenda Chiba, Scoba alibaki nje ya gari akitazama lakini akiwa tayari kwa lolote.
Amata akatazama dirisha lililopasuka ambalo Mc Field alipita hapo baada ya kuchezea kichapo kikali.
Baada ya kumshindilia lile konde pale chini, Mc Field alijifanya bado ana uwezo mkubwa wa mapambano, ndipo alipojikurupua na kumbwaga Amata kando, lakini kabla hajajiweka sawa, alichezea karate kali zenye mapigo ya kifo kutoka kwa Amata kiasi kwamba aliona hawezi kujitetea hasa alipopigwa pigo kali na kuvunjwa mbavu tatu, aliamua kujiokoa kwa kujirusha dirishani lakini hali yake tayari ilikuwa mbaya.
Akarudisha macho kwa yule mrembo, Amba, โvaa nguo zako!โ akamwambia huku akijitazama ule mkono uliovimba. Amba akavaa harakaharaka. Saa ya Kamanda Amata ikaanza kumfinya mkononi, akaingiza mkono kwenye moja ya mifuko ya kizibao chake na kutoa kifaa maalum cha mawasiliano.
โYes!โ akatamka.
โTupo, tumefika!โ ilikuwa sauti ya Madam S.
โOk, kama unaweza panda 206 haraka uone cha kuona. Chiba hifadhi huo mwili kama hauna uhai,โ akamaliza.
โWe mwanamke, usipende kuwa na wapenzi usiowajua, angekuua huyu, ni jambazi,โ Amata akamwambia Amba.
Mlango ukagongwa na Madam S akaingia.
โPole Kamanda, naona mkono wako umepata shida,โ Madam alisema.
โNdio, nahisi kama mifupa imepishana,โ akajibu.
โScoba akuwahishe kwa Jasmine ukapate matibabu, hili la hapa niachie mimi na Chiba,โ Madam akamwambia Amata.
โSawa!โ akajibu na kumtazama yule Amba, โtwende huku,โ akamwamuru huku moyoni akimmeza mate.
Madam S ndipo akagundua kuwa kuna mtu wa tatu mle ndani, akamtazama binti huyo kwa tuo, โnani huyu?โ akauliza.
โAh, wafanyabiashara hai,โ Amata akajibu huku akimswaga nje Amba. Wakafika mahali pa mapokezi wakakutana na mhudumu wa hapo. Kamanda Amata akamatzama bila kuongea kitu.
โUnalala sana, unaweza kuvamiwa na kuuawa hivihivi!โ akamwambia, โhaya, sasa hakuna kupokea wageni kwenye hotel hii mpaka mpate kibali kingine cha serikali, tunaiweka chini ya uangalizi kwa masaa machache na kufanya ukaguzi wa chumba kwa chumba naomba uhakikishe wageni wote wasitoke kuanzia sasa,โ Kamanda akatoa amri huku akimwonesha kitambulisho uinspekta wa polisi.
โSawa, lakini ni swala la kumwambia meneja, maana wengine wana ndege alfajiri hii,โ yule mhudumu akamwambia Amata.
โMpigie simu meneja mwambie afike hapa haraka,โ alipomalisa kusema hayo akaongoza nje, akamchukua Amba na kumtia kwenye gari.
โUlifikiri safari hii utatoroka tena? Utafia hapa hapa,โ alimwambia Mac Field aliyekuwa hoi na pingu mkononi ilhali mnyororo miguuni mwake.
โMtie kwenye buti,โ Kamanda akamwambia Scoba, Mc Field akatiwa kwenye buti ya gari, kisha yeye na Amata wakaingia ndani.
โShamba,โ akamwambia Scoba.
โNa huyu mwanamke?โ akauliza.
โHapana, huyu tunamtupa shimoni hapo mbele,โ Amata akajibu na gari ikaondolewa, mtaa wa kwanza, wa pili.
โSimama hapa,โ akamwambia Scoba kisha akamtazama Amba, โteremka, ondoka na usimsimulie mtu chochote ulichokiona,โ akamwambia kisha akaketi vizuri. Amba akateremka na kukimbilia mitaani.
Gari ya Scoba ikaegeshwa vizuri mahala pake, Kamanda Amata akateremka na kufungua buti, wakamshusha Mc Field kisha wakamkokota na kumwingiza kwenye chumba kimoja kisicho na madirisha wala ndani hakikuwa na chochote isipokuwa sakafu na choo tu.
โKaa humu, nakuja unijibu maswali yangu kabla sijakuua,โ Kamanda akafunga mlango kwa namba maalumu.
Dr. Jasmin akampokea Kamanda na kumpa tiba zote zinazowezekana, akamfunga bendeji maalum mkononi na kumwekea kamba ya kuvalia shingoni.
Dakika arobaini na tano baadae, Madam S na Chiba waliwasili, wakiwa na begi moja na suitcase kubwa, wakaliweka mahali. Kisha likafunguliwa kila mtu akiwa anaona.
โMnaona kazi hii?โ Madam aliwaeleza vijana wake. Ndani ya begi hilo waligundua vitu vingi sana vinavyotumika kujibadili sura, dawa za kunenepesha kwa muda mfupi na kukondesha kwa muda mfupi, vitambulisho zaidi ya hamsini vya idara mbalimbali kilichowagusa zaidi ni kile cha dereva wa Rais, hati za safari za nchi mbalimbali, maburungutu ya Kitanzania na za kigeni, silaha za kila aina, bastola, viwambo vyake na silaha nyngi za kijasusi.
โHii ni hatari sana,โ Gina aliongea kwa sauti ya chini. Wote walibaki midomo wazi, begi hilo lilikuwa limetengenezwa kwa malighafi ambayo ukilipitisha kwenye mashine za ukaguzi zinazotumia x-rays itakuonesha tu ndani kuna nguo na vitabu hata kama ndani hamna kitu, na hii ilimfanya mtu huyu kuweza kupenya kwenye vizuizi vya viwanja vingi vya ndege.
โKamleteni hapa!โ Madam akatoa amri. Chiba na Scoba wakaenda kwenye kile chumba kumleta Mc Field, wakamkamata huku na huku na kwenda naye. Wakamtupa sakafuni na kuchomoa bastola zao, risasi ya kwanza ya Chiba ikapiga kanyagio la mguu wa Mc Field, yowe la maumivu likamtoka.
โSasa tutuambie lengo zaidi la kuja hapa ni lipi, na nani kakutuma?โ Kamanda Amata alimwuliza Mc Field aliyekuwa akigugumia kwa maumivu ya mguu wake pamoja na mbavu zake, hakujibu kitu.
Amata akamwendea pale chini, โhutaki kujibu sio? Niambie aliyekutuma na madhumuni yakuja hapaโ. Badala ya kumjibu akamtemea mate usoni. Amata akashikwa na hasira, akampiga teke la kilo nyingi na jamaa akarudi chini chali, akatulia tuli huku povu likamtoka mdomoni.
Chiba akamuwahi na kumbana mashavu yake kwa vidole, maana alijuwa kuwa tayari mtu huyo anajiua kwa kidoge cha sumu. Hakuna aliyemwona wakati gani kameza kidonge hicho.
โShiiit!โ Chiba akapiga ukelele alipomwona mjinga huyo keshalegea na macho kumtoka, akawatzama wenzake waliokuwa kimya, โlimejiua!โ akasema.
โAwasalimie babu zake,โ Madam S akasema.
11
ONTARIO โ CANADA
WAKATI HUKU KWETU ILIKUWA ni alfajiri ya saa kumi kule kwao ilikuwa saa mbili usiku. Sir Robinson Quebec alikuwa akiweka sawa miwani yake akiwatazama wale washirika wake wa karibu sana katika sakata lao hilo. Kila mmoja likuwa na shauku ya kusikiliza nini kimejiri huko Afrika Mashariki.
โUsiku wa manane, ambapo kule ni asubuhi ya saa nne, ukurasa wa mwisho wa mkataba wetu na yule mheshimiwa utafungwa,โ akawaambia.
Yule mjumbe mweusi naye akatoa taarifa yake, โNa pia alfajiri hii kutafanyika tukio lingine katika mgodi wa Tanzanite kule Mererani kwa kupata kasha zingine tano za madini hayo, kila kitu kipo sawa unasubiriwa muda tuโ.
โKwa ujumla tumepata ushindi kwa kutekeleza makubaliano ya mkataba wetu, upande mmoja umeshindwa na sisi tunatekeleza kile tulichokubaliana, hakuna wa kutulaumu, kama tulivyofanya Congo, Liberia, hivyo hivyo tu,โ akaeleza yule mjumbe wa tatu.
Watu hawa watatu walikuwa ni matajiri sana huko ughaibuni, walifadhili nchi nyingi sana na kutengeneza Marais wengi sana hasa Afrika na Asia wakikuwezesha upate utawala na wao uwape sehemu ya mali asili ili wafaidi, kurudisha gaharama zao na kupata faida juu. Kwa jina lingine ni โKing Makersโ.
Walipanga kukutana siku hii ili kupiga mstari mwekundu kati yao na yule waliyemweka madarakani katika nchi ya Tanzania, kwa kuwa alikuwa amekiuka makubaliano. Waliketi hapo wakisubiri taarifa mbili, moja ni wizi mwingine wa madini huko Arusha Mererani, pili ni kifo cha mtu wao, mteja wao, Rais wa nchi. Kila mara walikuwa wakiangalia saa, masikio yao yakiwa makini kusubiri mngurumo wa simu iliyotegwa mezani hapo.
IKULU saa 4:00 asubuhi
NJE ya jengo la Ikulu, Makao Makuu ya Rais kulikuwa na watu wengi wakiwa kwenye viti na wengine wakiwa wamesimama hapa na pale. Walijulikana kuwa ni waandishi wa habari kwa kamera walizokuwa wamebeba mabegani mwao, wengine wakionekana kuandika hiki na kile. Bado katika lango kuu kulikuwa na wengine wanaongia, wakikaguliwa kila kona na vijana wa jeshi la polisi na askari kanzu waliowekwa hapo kuhakikisha ulinzi unakuwepo.
Watu wa televisheni nao walitega kamera zao hapa na pale ili kuhakikisha wanapata picha nzuri kadiri iwekanavyo, wakirekebisha vinasa sauti vyao na huku magari yao makubwa yenye mitambo ndani yake yakiwa tayari kupeleka maangazo hayo moja kwa moja kwa wananchi.
Huko majumbani nako kila mmoja alifanya kazi harakaharaka ili awahi kutazama au kusikiliza nini Rais wa nchi anataka kuliambia taifa. Na hali hii ilitokana na utata wa mambo makubwa mawili, kudunguliwa msafara wa Rais kule Bunju na wizi wa almasi uliofanyika Mwadui ukimhusisha Waziri wa Nisahati na Madini. Ilikuwa siku ya aina yake. Kila mtu aliisubiri saa nne na nusu ifike. Kwenye migahawa, mabaa, maofisini wote walikuwa tayari kusikiliza hotuba ile, na kila mmoja akisubiri jibu la maswali yake.
Kila mtu alikuwa tayari kajipanga kwa tukio hilo, hawakuwa na amani kabisa ijapokuwa Mc Field alikuwa tayari marehemu lakini bado hawakufanikiwa kumpata mshirika wake.
โNina wasiwasi anaweza akafanya maajabu hapa,โ Kamanda Amata akawaeleza wengine.
โNdio, daima inabidi tuwe katika tahadhari,โ Chiba akaongezea. Punde tu Madam S akawasili ofisini.
โPoleni najua mmenisubiri sana lakini foleni za jiji letu mnazijua na sote ni wahanga, haya bila kuchelewa, si mnajua Mkuu atahutubia asubuhi hii? Basi tujiweke tayari. Chiba kazi yako unaijua, hakikisha unakamata mawimbi yoyote ya sauti chochote katika maeneo hayo, hakikisha unakata mawimbi yote ya simu kilomita nne za mraba. Scoba utakuwa tayari kuratibu usafiri kama itahitajika, Gina unajisikiaje sasa?โ Madam akakatisha maelekezo.
โNiko sawa Madam,โ Gina akajibu.
โOk, Gina na Kamanda nawarudisha katika kazi yenu, mtakuwa kwenye viwanja vya Ikulu kuangalia kila kinachoendelea, mimi nipo hapa wala sitoki, mawasiliano yasikatike mpaka itakapoamriwa. Chiba kumbuka usikate frequency tunayoitumia, sawa?โ Madam akamaliza.
Wote wanne ukimuacha Jasmine ambaye alibaki ofisini na Madam, walichukuwa vifaa vyao vya mawasiliano na kupachika masikioni, wakajaribu vyote na Chiba akawapata sawia kabisa, wakabeba bastola na vifaa vingine muhimu katika kazi zao kadiri walivyoweza.
Taksi yenye rangi ya kijani, ilisimama karibu kabisa na lango la Ikulu, eneo ambalo liliandaliwa kwa waandishi wote kushuka hapo. Mwanamke mwenye shepu tamu kwa kuiona kwa macho aliteremka akiwa na video kamera kubwa mkononi mwake, akalifikia lango akasimamishwa kwa ukaguzi. Ndani ya chumba kidogo alikaguliwa na kuonekana yuko sawa hakuwa na silaha wala kitu chochote cha hatari. Kitambulisho chake kilionesha kuwa ni mwanahabari kutoka kituo kikubwa cha luninga duniani NBC. Akapita na kuungana na waandishi wengine.
Katikati ya kamera nyingi akaweka ile ya kwake na kuhakikisha amekwishaiweka sawa kwa kazi.
Saa nne na nusu kama ilivyopangwa, Rais wa Jamhuri alijitokeza na kukaribishwa kwa makofi baada ya kutoonekana kwa takribani siku tano.
Mbele ya jopo la waandishi na wanausalama, Rais alianza kutoa hotuba yake iliyojawa na maneno mazuri na matamu.
Tracy Tasha aliingiwa na wasiwasi, kila alipojaribu kumtafuta Mc Field hakumpata simuni, mpango waliopanga ilikuwa wakutane hapo, lakini alishangaa kutomuona swahiba wake, akajua kwa vyovyote atakuwa tayari katika kona aliyomwambia atamkuta. Kupitia kamera yake alikuwa akiitembeza kuangalia wote waliokuwa mbele, licha ya Rais na walinzi wake walioonekana kuwa makini katika kutazama huku na kule, alimwona mtu ambaye alimfanya moyo wake ulipuke.
Kamanda Amata alisimama pembeni kabisa mwa jukwaa kuu, akiwa na ile plasta yake kubwa mkononi na mkono huo kuuningโiniza shingoni, Tracy akatabasamu, akajua hapa hana mkono mmoja hawezi chochote. Akatazama na wengine wote akaona walivyojipanga na jinsi walivyojiweka bastola zao ndani ya makoti yao. Tracy alitazama tena kwa makini sana hali nzima ya usalama, akaangalia wapi na wakati gani ataweza kuifanya kazi yake, akakumbuka maelekezo ya Mc Field wapi pa kutokea pindi akikamilisha hilo.
Kamanda Amata, alitulia kama sanamu, macho yake yaliyofichwa kwa miwani nyeusi yalikuwa yakimtalii kila aliyekuwa mbele, ilikuwa ikipiga picha, ikivuta na kurudisha na kuhifadhi katika kadi sakima ndogo iliyokuwa imepachikwa katika kona moja ya miwani hiyo.
โPoint one, ova!โ Chiba akaita
โPoint one, Clean, ova!โ sauti ya Kamanda Amata ikajibu na wote wakaisikia vizuri.
โPoint two, ova!โ
โPoint two, Clean, ova!โ Gina akajibu kutoka juu dirishani ambapo aliweza kuwaona watu wote kwa chini.
Chiba alikuwa akiangalia kila tukio kupitia luninga zake ndogo ndani ya gari aliyoiegesha nje ya ukuta wa Ikulu, picha zote alizipata kupitia miwani ya Gina na Amata. Alikuwa akikamata mawimbi mbalimbali ya mawasiliano yaliyokuwa yakikatisha eneo hilo, alizima mawasiliano yote ya simu kilomita nne za mraba, aliweza kuchuja kila frequency inayokatiza usawa wake. Tracy aliiangalia saa yake mara kwa mara. Kitendo hicho kilimfanya Kamanda Amata kumuona na kumtambua, aliishika miwani yake na kumvuta karibu, picha yake haikuwa ngeni hata kidogo.
โGround zero! Ground Zero! Ova!โ akaita. Chiba akaipokea na kutazama kwenye kijiluninga chake, akaona sura ya Tracy Tasha akiwa nyuma ya kamera kubwa ya video.
โRoja, point one kazini, Ova!โ Chiba akaita lakini ilikuwa ni kupeleka ujumbe.
โCopy, point one kazini, ovaโ Kamanda akajibu.
โPoint two, stand by! Ovaโ Chiba akatoa ujumbe tena.
โCopy, point two standby, ova!โ Gina akajibu, akashusha mkono chini na kuinua bunduki aina ya SR 25 iliyotengenezwa huko USA. Bunduki ya maana, maalumu kwa kudungua, ilibuniwa na Eugene Stoner yenye urefu wa inch 44.0. Gina aliipachika dirishani na kuweka jicho lake katika lensi iliyofungwa juu yake na kumwangalia vizuri yule mwanamke.
Tracy Tasha aligeuza kamera yake na kumtazama tena Kamanda Amata, hakumuona. Alihisi akili yake inaganda ghafla, alitazama kwa chati huku na kule lakini hakumuona Amata mahala aliposimama, akahisi kuchanganyikiwa. Hakuhitaji kupoteza muda, hakuona sababu ya hilo, aliigeuza kamera yake kwa Mheshimiwa Rais, akamweka vizuri katika kioo chake cha kuvuta, akakijaza kifua cha Mkuu huyo, kisha kidole chake chembamba kikabonyeza kitufe chekundu cha kuiruhusu kamera hiyo ianze kunasa picha. Kizaazaa.
Ni nukta ileile, Rais alitupwa hewani, walinzi wake walichanganyikiwa, wale wa nyuma walijitahidi kumdaka lakini wote sita wakarudi chini bila kipingamizi, wale wa mbele wakageuka mara moja, na kumwendea Mkuu, haraka sana tayari eneo lile likawa katika hali ya taharuki. Waandishi wa habari walihaha kupata picha ya hiki na kile, askari wa FFU waliingia na kuzingira eneo lile kujua nini kimetokea.
Tracy Tasha, alijishika kiuno katikati ya watu waliokuwa wakihaha huku na kule. Alikuwa akiangalia nini cha kufanya. Macho yake yalitazama juu ya jengo la ikulu na kujikuta akitazama na domo la SR 25, akajua pamenuka, akabinya kijitufe kingine kwenye ile kamera yake na yote ikalipuka na kutoa moshi mzito uliowafanya watu kuchanganyikiwa na kukohoa huku wengine wakitokwa na machozi yaliyochanganyika na kamasi jembamba.
Gina alitoa jicho lake katika lensi ya lile bunduki kwani alishachelewa kupiga, Tracy alipotea katikati ya ule moshi.
โShiiit! Mwanaharamu wa kike,โ Gina alingโaka alipojikuta kazidiwa kete na Tracy. Aliendelea kutazama kwa lenzi mtu mmoja baada ya mwingine huku kinywani mwake akiendelea kutukana matusi anayoyajua yeye mwenyewe.
Kamanda Amata alipata wakati mgumu, alikuwa akimfuatilia Tracy kwa utaratibu maalumu kabla hajafanya kile anachotaka kufanya, mara kizaazaa kilipoanza alijikuta akibabaika, hakujua amuendee Tracy au arudi kumsaidia mheshimiwa, ilikuwa ngumu. Lakini alipokuwa akitafakari hilo, ni nukta hiyohiyo aliposikia kishindo cha pili kilichozua mtafaruku, moshi mzito uliomfanya hata yeye achanganyikiwe ulizagaa.
โPoint one, point one!โ Chiba aliita.
โHali tete, mheshimiwa kaangushwa!โ kamanda Amata alijibu haraka.
โMan down!โ Chiba alipigwa na butwaa.
โAmetoroka! Ametoweka!โ Gina alipeleka ujumbe.
Kamanda Amata bastola mkononi, alihaha kutafuta huku na kule akiwa tayari ameweka miwani yake usoni ili kumtambua mtu huyo hakumuona.
Madam S alikurupuka katika kiti chake, โJasmin, nifuate haraka chukua silaha!โ akatoa amri nia Dr. Jasmine akafanya hivyo, hawakuwa na haja ya kutumia gari.
โVipi Madam, kuna nini?โ akauliza.
โMkuu wa nchi amedunguliwa,โ akajibu huku akimalizia kuchomeka bastola katika kiuno cha suruali yake ya suti. Wakatoka nje na kuvuka barabara, kizaa kilionekana, gari za polisi zilikuwa zikipiga vingโora kwa fujo zikitanda katika njia zote, kila mtu aliye karibu na ukuta wa Ikulu aliondolewa na aliyetiliwa mashaka alitupiwa kwenye gari za polisi. Mitaa ilichafuka, kuanzia Hazina Ndogo mpaka Magogoni kuzunguka mpaka hospitali ya Ocean Road, kwa ujumla kila upande ulimwagwa askari wakipekuwa mpaka kwenye vichaka.
Madam S aliingia getini na kukuta kizaazaa bado kikiendelea, waandishi wote walikamatwa na kuwekwa mahala pamoja. Ilibidi kwa haraka lifanyike gwaride la utambuzi.
Kamanda Amata aliifuata gari ya polisi iliyokuja na mbwa, akamwomba askari mmoja ashuke na mbwa wake. Wakafuatana mpaka pale kwenye mabaki ya kamera ya Tracy, yule mbwa alinusa hapa na pale huku akitoa kilio chake cha ajabu, kisha akaanza kufuata uelekeo fulani, Kamanda na yule polisi walifuatana kumfuata mbwa huyo. Mbwa aliwaongoza mpaka kwenye ukuta, umbali wa mita kama 200 hivi kutoka eneo la tukio, kisha yule mbwa akasimama mahala na kuendelea kunusa hapa na pale bila kwenda popote.
Tracy alipoona tayari domo la SR 25 linamwelekea yeye alijuwa wazi kuwa sasa mambo yameharibika. Kamera yake ambayo ilikuwa na bunduki ndani yake yenye kubeba risasi tatu tu, pia ilifungwa mabomu mawili ya machozi, akayafyatua mara moja, ikatawanyika vipande vipande. Tracy alijiangusha chini na kubiringita kisha akaibukia nyuma ya waandishi wa habari. Wakati watu wakiendelea kukohoa, na kutokwa machozi, Tracy alivuta hatua ndefu na kuufikia ukuta kisha bila hata kuugusa alijirusha sama soti akatua nje ya ukuta huo. Lakini alijikuta na wakati mgumu sana pale alipojua kuwa Mc Field alitakiwa kuwa hapo, hakuwepo. Akachanganyikiwa, hivyo ikabidi ajiokoe mwenyewe kwa nguvu zake, alivuka barabara ya Magogoni kwa haraka na kuingia katika Chuo cha Utumishi wa Umma, akiwa jirani na ofisi za chuo, alikutana na mwalimu mmoja wa kike, akamwita na kumwambia kuwa ana shida naye ofisini, wakaingia.
Tracy alitoka nje ya ofisi hiyo akiwa na mavazi ya yule mwalimu. Wakati wanafunzi na wafanyakazi wakikimbilia mbele ya jengo hilo kujua kulikoni, Tracy alipita katikati yao na kutokomea. Vingโora vya polisi vilimchanganya kiasi Fulani, alishindwa upande gani aelekee, akapita jengo la kwanza na la pili, akaibukia nyuma, hakuona njia nyingine ya kutoroka, akaivuta hijab aliyoipata kutoka kwa yule Mwalimu, akajiweka vizuri kichwani mwake.
Kamanda Amata akiwa na mbwa wa Polisi, walizunguka nje ya ukuta na mbwa yule akaipata tena harufu ya Tracy na kuvuka barabara mpaka kwenye ofisi za Chuo cha Utumishi, walipoingia ofisini, walimkuta yule Mwalimu akiwa hana uhai, nguo zote za Tracy zikiwa pembeni, na yule Mwalimu alikuwa kama alivyo.
โShiit! Katuweza, Mtuhumiwa ameruka kihunzi!โ aliongea kwenye kinasa sauti chake.
โLazima akamatwe!โ Gina akajibu.
โPoint one! Upande wa Mashariki tafadhali, kuna mtu anayejaribu kujipenyeza katika kundi la wachuuzi wa samaki akielekea upande tofauti na wengine wote,โ Chiba alitoa hadhari hiyo, akiwa anakamata picha kutoka katika satellite.
โPoint One kazini,โ Kamanda akajibu.
โPoint two, ongeza nguvu tafadhali,โ Chiba akaomba.
โPoint two kazini,โ Gina akajibu.
โGround zeroโฆ. Ground zeroโฆโ sauti ya Madam ilifika kwa wote, aliyekusudiwa akajibu.
โNakusoma,โ akajibu Chiba.
โNipe dira yako!โ akamwambia.
โMashariki, soko la samaki, usawa wa bahari,โ
โCopy!โ Madam S akajibu.
Tracy, alijitahidi kupenya kwenye kundi la watu kwa minajiri ya kufika baharini, aliamini akifika tu baharini, kamanda na kikosi chake hawatamwona tena kwani mbinu za kutoroka kwa njia hiyo alikuwa akizijua vyema. Kila alipogeuka nyuma alimwona Kamanda Amata akimfuata kwa umakini wa hali ya juu huku mkononi mwake amekamata bastola ndogo sana.
โHey! Stop!!โ Kamanda alitoa amri lakini Tracy hakusimama. Kamanda Amata akpiga risasi hewani na watu wote wakatawanyika, wengine wakianguka chini na kukanyagana vibaya. Tracy akapata kipingamizi kipya, lakini bado hakuonesha udhaifu, alichomoa bastola yake, akageuka nyuma na kumfyatulia Amata, ambaye tayari aliliona hilo, Kamanda Amata akajitupa na kubingirita chini ile risasi ikamkosa na kujeruhi mwingine nyuma yake. Akanyanyuka haraka na kumtazama Tracy, hakumuona.
Akiwa na bastola yake mkononi, akatazama huku na huku.
โPoint one, Chumba cha kuhifadhia Samaki,โ Chiba akatoa maelekezo kwani alikuwa akiendelea kumfuatilia Tracy kwa mtandao.
โPoint one kazini,โ Kamanda akajibu huku akiingia katika chumba kikubwa kilichopangwa majokofu mengi makubwa makubwa.
Ukimya ulitawala, harufu ya samaki ilikijaza chumba hicho, kelele za pepezo za pangaboi zilisikika. Bastola mkononi, Amata alikuwa makini kupekuwa uchochoro mmoja baada ya mwingine.
Katika chumba cha siri kabisa, Rais aliteremshwa kwa lifti maalum na kuingizwa ndani ya chumba hicho chenye kila aina ya mtambo tiba kwa huduma ya kwanza. Akiwa na chupa ya maji iliyokuwa ikiendelea kuingia mwilini mwake, alikuwa kimya kayafumba macho yake. Wanausalama wa Ikulu walihaha huku na kule kujaribu kuokoa maisha yake kwa maana walijua wazi kuwa Taifa liko kwenye taharuki kwani hakuna cha kuficha, hotuba ile ilikuwa ikienda moja kwa moja hewani na watu waliitazama kwa televisheni. Walimlaza juu ya kitanda na wote wakasogea pembeni kutazama kinachoendelea maana mshangao na bumbuwazi ulikuwa dhahiri shahiri nyusoni mwao.
Ni siku moja ilikuwa imepita tangu Rais ajiimarishie ulinzi wake binafsi kwa kuifumua idara ya Usalama wa Taifa na jambo hilo linatokea, kila mtu alichanganyikiwa.
Ukimya ulichukua nafasi ya kila kitu katika chumba hicho, watu wachache wasiozidi watatu ukiachana na Daktari walikuwa wamebaki, wengine walitoka nje kuhakikisha mtuhumiwa anatiwa mkononi.
Polisi nao walizingira jengo lote la Ikulu na viunga vyake, barabara za kuingia na kutoka ziloikuwa zimefungwa haikuruhusiwa gari kuingia eneo hilo wala zilizo katika eneo hilo kutoka. Kila kona mbwa wa Polisi walifanya kazi ya kukagua kwa kunusa kila gari na kila mtu. Mbwa hao wenye mafunzo maalum waliweza kutambua harufu ya kitu chochote hatari hususan milipuko.
Madam S, aliingia katika chumba alichokuwa amelazwa Rais, akifuatana na Dr. Jasmine nyuma yake. Mlango mzito ukajirudisha nyuma yao, mlango uliotengenezwa kwa madini ya kutokuingiza risasi. Walimkuta Mheshimiwa amelala kimya kabisa kitandani, daktari akiwa kasimama pembeni.
โVipi mbona hakuna tiba yoyote inayoendelea?โ akauliza.
โAmenipa ishara nimuache,โ yule daktari akajibu.
Kisha akamgeukia mtu wa kwanza ambaye ni afisa usalama wa Taifa mwenye mamlaka yote ya juu kwa Rais. Yeye alikuwa amesimama pembeni mwa kitanda, โkinachoendelea?โ
โUsafiri unaandaliwa na muda si mrefu tutaondoka kuelekea London kwa matibabu, โ akajibu. Madam S akasimama na kumtazama Mheshimiwa ambaye alikuwa kajilaza kwa utulivu na suti yake ileile ikiwa mwilini, damu nzito iliyoganda juu ya kifua chake ilitengeneza jeraha zito na la kutisha ambalo lilijificha nyuma ya au ndani ya suti hiyo.
Kamanda Amata alijikuta akipewa dhoruba kali ya mapigo ya karate yaliyodhamiria kuua, yakitokea nyuma yake, akayumba na kujiweka sawa, kisha akageuka nyuma na kukutana na mapigo mengine yaliyopigwa kiufundi, haraka haraka na yaliyomchanganya kupita kawaida.
Huyu mwanamke si wa kawaida, akawaza Amata wakati tayari yupo chini akijifuta damu iliyokuwa ikimtoka katika pachipachi za kinywa chake. Tracy akasimama sakafuni kwa mtindo wa kuvutia, akiwa tayari kwa mapigano na kijana huyo mtanashati. Wakati wanawake wenzake walikuwa wakitafuta nafasi ya kufanya nae mapenzi ili tu wajisifie, yeye alikuwa anatafuta nafasi ya kupigana naye. Kamanda Amata alijizoazoa pale chini, alihisi mkono wake kutonesheka tena. Tracy alijirusha kwa namna ya ajabu kwa minajiri ya kutua na shingo ya Amata lakini hapo ndipo alipopajutia. Amata alijitupa pembeni na Tracy akatua peke yake, alipomtazama Amata tayari alikuwa mbele yake; pigo moja la maana likapiga katikati ya sura yake nzuri, Tracy alishuhudia nyota nyingi mbele yake, kabla hajatulia pigo zito la pili likatua mbavuni, Tracy akajikuta analegea, hana la kujitetea. Pigo la tatu lililokuwa linalenga kutoboa tumbo la Tracy na kufumua takataka zote za tumboni, lilikingwa kiustadi sana. Tracy akaunyonga mkoni wa Amata ule ambao umefungwa bendeji ambao mwenyewe aliutumia bila kujali. Akaunyonga kwa nguvu, maumivu makali yakapenya kwenye mishipa ya Amata, akabana meno kwa maumivu hayo, alijifyatua na kupiga kichwa kimoja maridadi, Tracy alihisi kama jiwe limepiga kwenye mwamba wa pua, akamwacha Kamanda na kurudi nyuma, akasimama akihisi kama kitu kinatoka ndani ya pua yake, damu.
Tracy akawa kama mbogo aliyejeruhiwa, sasa alimkamia adui wake, akajiwekea yamini moyoni mwake, ama zangu ama zake. Aliruka na kutua juu ya moja ya jokofu kubwa akinuwia kushusha kipigo kwa Kamanda kutokea juu, lo, alicheza pata potea, kwani hilo adui yake alilitegemea baada ya kusoma macho ya mwanamke huyo kabla, aliunyanua mguu wake na kupiga ngwala moja safi iliyopita millimita chache juu ya jokofu hilo huku mguu mwingine bado ukiwa umesimama juu ya sakafu. Miguu ya Tracy ilitua na kukutana na mguu wa Kamanda Amata. Tracy alijikuta akirudishwa hewani sasa kwa mtindo wa kuangushwa vibaya lakini kwa ustadi wake na ufundi wa mapigano alijigeuza hewani mara ya pili na kupoteza lengo la Amata, akatua chini na kukutana na guu lenye nguvu lililotua kifuani mwake, akatupwa nyuma na kupiga mgongo kwenye jokofu. Alipokaza macho yake ambayo yalikuwa yakipoteza nuru, alimwona Amata bado akiwa kaweka mguu juu, hajaushusha chini.
Tracy alihema kwa nguvu, damu zikiendelea kumvuja puani.
โUmekamatika Tracy Tasha, muuaji mwenye taaluma, na wewe utauawa kitaalamu vile vile na amini usiamini utajiua mwenyewe,โ Amata alimwambia kwa Kiingereza safi huku akishusha mguu wake chini.
โSi-we-zi ku-fa ki-ko-ndoo,โ alijibu kwa lugha hiyo hiyo, lakini kwa shida sana, sauti yake ilikuwa ikimezwa na maumivu makali.
โSasa utanyongwa Tanzania, Mzungu muuaji wewe, uliona haitoshi kumuua Khumalo, Touzony na sasa ukaamua kuja Afrika Mashariki? Basi aliyekutuma amekuuza, alijua wazi kuwa hapa ndiyo kaburi lako kama mwenzako Mc Field ambaye tangu jana tayari yuko motoni bila shaka na wewe anakusubiri kule ili mkamuue shetani kama mnaweza kuua,โ Kamanda alimwambia Tracy.
Tracy alikunja sura baada ya kusikia kuwa Mc Field alikuwa tayari marehemu, mara picha ya karatasi ya mwili wa Mc Field ikadondoka mbele yake, akaiokota na kuitazama.
โTunakufahamu sana, na tulikuwa tunakusubiri, Serikali ya Tanzania haiwezi kuangushwa na nguvu yenu vibaraka na sasa utanambia ni nani aliyekupa kazi ili naye nikamshughulikie hata akiwa na ulinzi wa namna gani,โ Kamanda alimweleza.
โManeno mengi hayavunji mfupa,โ Tracy alijibu huku akiikunja ile picha na kuitia kinywani. Alifyatuka kutoka pale alipo na kushusha kipigo kizito kwa Kamanda Amata. Kasi aliyokuwa anaitumia Tracy kupeleka mapigo kwa mikono na miguu ilimshangaza Amata. Tangu alipoanza kupambana na watu wenye ujuzi mbalimbali huyu alikuwa tofauti. Amata alikuwa makini, alikinga mapigo yote kumi na nane na hakuna hata moja lililopata, pigo la mwisho Tracy alijinyoosha na kupiga msamba akiwa anakwepa teka kali la Amata ambalo lingetua ubavuni mwake basi bila shaka lingevunja mbavu za kutosha. Akajikuta akimkosa, akajirusha upande wa pili na Tracy aliyedha, aliyenuia kushusha pigo kwenye korodani alimkosa na kujikuta kabaki peke yake. Akanyanyuka harka na kukutana na konde zito la usoni, akapepesuka kidogo kabla hajatulia, konde la pili, la tatu, la nne, la tano, la sita, la saba, Tracy chali, sura ya urembo yote ilikuwa nyekundu.
Akajinyanyua tena haraka na kusaimama wima, akamfuata Amata kwa kasi. Mwenzake akamkwepa na kumtwisha konde la kilo nyingi lililotua tumboni, Tracy akaganda akiwa kajishika tumbo, damu ikimtoka kinywani na macho yakimtoka pima. Kamanda Amata alikuwa katulia palepale, akisubiri Tracy ajibwage chini maana alijua kwa kilo za ngumi hiyo hawezi kupona tena na akipona hatokufa tena.
Watu walikuwa wamejazana katika mlango mkubwa wa jengo hilo wakiangalia mapigano yale yaliyokuwa yakiendelea, walishangaa mwanamke huyo alivyokuwa akifanya minyumbuliko ya ajabu katika mpambano huo.
โHuyu atakuwa Cynthia Rothrock huyu!โ mmoja akamwambia mwenzake, wengine wakacheka.
Mara vingโora vya polisi vikasikika kuja eneo hilo, watu wakaanza kusogea nyuma.
โEeeee wanoko haooo!!!โ akasikika kijana mmoja mchuuzi wa samaki.
Gina akiwa na bastola mkononi, alikuwa akikimbia nyuma yake akifuatiwa na Chiba kisha polisi na maafisa wengine wa usalama wote walikuwa wakielekea huko.
Katika soko hilo la samaki kulikuwa ni mshike mshike, kila mmoja alitaka aone kinachotukia lakini gari ya FFU ilifika na kuwataka watu wote kusogea mbali na eneo.
Tracy Tasha bado alijiinamia mkono wake mmoja ukishika tumbo lake na mwingine ukiwa umeushika ule mkono wa Amata uliopiga ngumi, alitulia kwa sekunde chache, damu zikimtoka kinywani na puani.
โNani boss wako? Nani kakutuma?โ Kamanda akauliza.
Tracy hakuweza kuongea chochote, akajiachia kutoka katika mwili wa Kamanda na kuanguka chini, akiwa hana nguvu ya kufanya lolote. Amata akamtazama mrembo yule aliyelala kwa ubavu sakafuni, akamsukuma kwa mguu na kumuweka chali. Tracy akajiinua kwa tabu, akajivuta na kuegemea moja ya jokofu lililo hapo, akipumua kwa shida. Kamanda akachuchumaa akimwangalia usoni.
โBado kidogo utakufa, kama ulivyoua wengine wote, lakini kabla hujafa, nani boss wako, nani unayemfanyia kazi hii?โ akamwuliza.
โRho-bin-son Que-be-bec!โ akajibu kwa tabu kisha akamtemea Kamanda mate yaliyochanganyika na damu usoni.
โHuna maana kama mkia wa mbuzi, mwanamke hayawani kabisa! Kwa kuwa sina desturi ya kuua warembo kama wewe,โ akachomoa bastola yake aliyokabidhiwa na Chiba jana yake, โshika hii, ina risasi mbili tu ndani, jiue mwenyewe!โ akamshikisha kwenye kiganja chake. Kamanda Amata akasimama pembeni.
โJiue mwenyewe, mi nasubiri hapa,โ akamwambia. Tracy Tasha hakuwa na nguvu yoyote ya kufanya lolote. Kamanda Amata akageukia mlangoni na kuvuta hatua kuondoka eneo hilo wakati alipowaona Gina, Chiba na baadhi ya polisi wakiingia katika jengo lile.
โPole sana Kamanda!โ Gina alitoa pole huku akiipachika bastola yake kiunoni mwake, na kumwendea Amata.
โPole Kamanda na hongera sana!โ Chiba nae alitoa pongezi, lakini mara ghafla wote wakasimama na kutazama kwa mshangao kule alikokuwako mwanamke adui.
Tracy Tasha, alisimama wima, mkononi mwake akiwa na bastola inayomtazama Kamanda Amata kisogoni.
โHautapata nafasi ya kujutia kosa ulilofanya, nimehakiki kuna risasi mbili, moja itakuua wewe na nyingine itanimaliza mimi,โ Tracy aliongea kwa sauti ya kichovu. Kamanda Amata akasimama kimya, mara akasikia mlio wa kilinda usalama cha bastola hiyo kikiondolewa.
โHah! Hah! Hah! Hah! Hah! mwili wangu hauwezi kuguswa ukiwa hai na ninyi watu weusi, hamna hadhi, na we huwtopata nafasi ya kujisifu kuwa umeniua na kuandika historia hiyo duniani katika duru za usalama, adios amigos,โ Tracy aliendelea kusema huku shabaha yake ikiwa sawia.
Akapachika kidole kwenye kifyatulio na kufyatua bastola ile, bastola ikaruhusu risasi moja kutoka kuelekea kwa Kamanda Amata.
Trace alishangaa kuona bastola ile inapiga kinyume, risasi ilitokea upande wa nyuma na kupiga kifuani kwake, Tracy akatoa yowe la uchungu na kujibwaga chini, kifua chake kilikuwa kikivuja damu.
Kamanda Amata hakugeuka nyuma, โasante Chiba kwa teknolojia yako, nimekukubali,โ akampigia salute na kisha akaondoka eneo hilo.
MADAM S alijikuta akiruka kwa furaha alipopata taarifa ya kifo cha Tracy Tasha, hakuweza kuvumilia. Akampa taarifa hiyo Dr. Jasmine ambaye naye alikuwa mwenye furaha sana kwa hilo.
โUnaweza kupona sasa Mheshimiwa Rais, adui zako tumewamaliza,โ madam akamwambia Rais aliyekuwa amelala kimya kitandani. Mara akainuka na kuketi.
โAsante sana Selina, uliloliota ndilo haswa lililotokea,โ akaongea, kisha akavua shati lake kila mtu akashangaa isipokuwa Madam S. kifuani mwake alivua kitu cha plastiki chanye madonge ya damu ndani ya mapakiti, risasi moja kubwa ilikuwa imenasa katika dude hilo. Haikumdhuru, alikingwa, akalitoa na kulitupa pembeni.
โNaomba muwaambie waandishi wa habari, wasitoe habari yoyote zaidi ya kuwa Rais amedunguliwa basi, na hali yake ni mbaya, waandike hivyo hivyo,โ maneno hayo alimwambia msemaji wa Ikulu naye akatoka na kwenda chumba maalumu ambako alionana na waandishi waliokuwepo.
โโฆkwa kifupi, kama mlivyoona, Rais ameshambuliwa, ameumia vibaya na hali yake ni mbaya, hivyo Ikulu itamsafirisha mchana huu kwenda London kwa matibabu, taarifa yoyote mpya mtapewa kutoka hapa tu, asanteni.โ Msemaji wa Ikulu alimaliza mazungumzo yake, akanyanyuka. Waandishi wa habari waliokuwepo walianza kumgombania kumtupia maswali lakini aliondolewa mara moja na watu wa Usalama wa Taifa, mlango ukafungwa, na dakika hiyo hiyo gari maalumu ya wagonjwa ikawasili Ikulu, kama ilivyopangwa, akafungwa vizuri katika kitanda.
โMchome sindano!โ Madam S akamwambia daktari wa Rais. Naye akafanya hivyo na usingizi mzito ukamchukua.
Ni watu wasiozidi watano waliojua kuwa Rais ni mzima kabisa lakini wengine wote waliaminishwa hivyo kuwa Mheshimiwa ana hali mbaya.
Msafara wa gari za Ikulu ukaondoka kuelekea Uwanja wa Ndege.
***
โKamanda Amata,โ sauti iliita kutoka nyuma yake. Akageuka na kumwona Madam S akiwa na faili moja mkononi. Amata alikuwa amesimama katika sehemu ya mbele ya nyumba kubwa huko Gezaulole, mkono wake ukiwa na bandeji nyingine kubwa. Akageuka na kumtazama Madam S.
โYes Mom,โ akaitikia na kuitoa miwani yake usoni.
โMheshimiwa Rais anakupongeza kwa kazi ulioifanya, anakubali sana uwepo wako hapa nchini na hususan katika idara nyeti kama hii, nimetoka kuzungumza naye sasa hivi, tumekubaliana jambo moja,โ akamkabidhi lile faili ambalo juu yake lilikuwa limeandikwa Rhobinson Quebec na chini yake maandishi mazito โWantedโ, akatazama na kumwangalia Madam S.
โRoho yake tu wala hatumwitaji akiwa hai,โ kisha akageuka na kuondoka.
11
SIKU TATU BAADAE
โOoooh babe, you are so sweet hubby!โ Lereti binti wa Khumalo alikuwa akilalamika kitandani, juu yake Kamanda Amata alikuwa akimfanyia manjonjo ya maana.
โMmmh! Oooh yeah utainjoy sana mama!โ akambembeleza.
โAgain, pleaseโฆโ malalamiko yakaendelea, miguno ya mahaba ikachukua nafasi kila mtu alikuwa kazama katika dunia nyingine kabisa. Amata alilihusudu umbo la Lereti kwa jinsi lilivyo katika katikati na kutengeneza nane, mapaja yaliyojaa vyema na kuzungukwa kwa nyama nzito na ngozi laini yalizidi kuupeleka mbio moyo wake.
โHii ndio zawadi yangu kama nilivyokuahidi, na kwa nini hukunambia kama wewe ni mpelelezi mashuhuri Afrika na Ulimwenguni?โ Lereti akamwambia.
โAaaaa hayo hapa si mahala pake mtoto mzuri,โ akamjibu.
โSasa roho yangu kwatuuuu!!! Umemuua yule hayawani aliyeniulia baba yangu kipenzi, sasa niue na mimi niue kimapenzi,โ Lereti alibembeleza kimahaba, kwa sauti ya kitoto huku akichezea kifua cha dume hilo. Akamtazama usoni na kumyonya ulimi.
โKamanda Amata, kuua kwako kama chai ya asubuhiโ akamwambia.
โNa mapenzi kwa watoto wazuri kama pumzi ya kila siku,โ kamanda akamalizia.
โNiue na mimi โฆ.โ Akazidi kulalama huku akijinyonganyonga.
โJiue mwenyewe!โ Amata akamjibu.
MWISHO
Isikupite Hii: Jinsi Ya Kumfanya Mwanamke Akupende Kwa Mara Ya Pili
Also, read other stories from SIMULIZI;
