Mzoa Takatakata Sehemu ya Nne
CHOMBEZO

Ep 04: Mzoa Takatakata

Mzoa Takatakata Sehemu ya Nne

IMEANDIKWA NA : HAFIDHI J IKRAM

*********************************************************************************

Chombezo : Mzoa Takataka

Sehemu Ya Nne (4)

“Salumu mjukuu wangu ni kheri uishi makaburini kuliko ndani ya nyumba hii!”

“kwa nini bibi unasema hivyo?

“Siku zote usilolijuwa ni sawa na usiku wa Giza binafsi ndugu wa marehemu washaanza kukutupia makombora mazito mazito nia yao ni kukupoteza kabisa

hapa duniani. Ndani ya nyumba hii kuna vitu vya ajabu ajabu tu kinacho wazuia wao kukuondoa haraka ni kile kitabu.

Nikaangalia hiko kitabu anacho nionyeshea Bibi kumbe ni msahafu japo msikitini siendi kuswali ila kusoma Qur’an nakumbuka.

Bibi akaendelea kusema usipokuwa makini na hiki ninacho kuambia utaona matokeo yake ushaanza kulishwa vitu vya ajabu ajabu usiku.

Wakati Bibi anaongea yote hayo Mimi mwili unatetemeka vibaya mno nikahisi baridi maana kumbe nyumba haifai hii.

“Usiogope Salumu kumbuka wewe ni mtoto wa kiume utakiwi kuwa hivyo jikaze pambana naimani utashinda tu!”

“sasa bibi nitapambana vipi wakati sijui wapi pakuanzia na sina fani yoyote ya uchawi mie!”

Nilizungumza hivyo huku mchozi ukinitoka binafsi asikwambie mtu uchawi unatisha vibaya mno utakuta unabebwa kitandani usiku pasipo kujitambua ukaenda

kulimishwa ukiamka Asubuhi umechokaa mwili wote unauma hapana chezea mchawi.

Bibi akanistua kutoka katika dimbwi zito la mawazo kwa kuniambia.

Embu twende nyumbani kwangu nikakupe kitu ambacho kitawakomesha hawa wajinga wote!

Tukaongozana hadi nyumbani kwake ni kijumba kidogo hivi kilicho jengwa kwa kugandika udongo juu kaezeka makuti tu nikajiuliza hivi inapo nyesha vua iliyo

ambatana na upepo mkari huyu Bibi analala kweli. Akaniambia niingie ndani nikawa naogopa ila nikaingia nikiwa na hofu tele moyoni.

Niliweza kukitasimini kile chumba pembeni kuna kitanda cha kamba juu kimewekewa mabox tu. Nikazidi kushangaa shangaa tu.

“Mmh naona unashangaa mjukuu wangu hapa ndio nyumbani kwangu ninapo egemeza ubavu wangu. Kaa hapa wala usiogope!”

“hivi Bibi kwa nini unaishi maisha ya tabu hivi”….. hukuzaa au huna watoto ndugu jamaa marafiki wote hao wamekuacha uteseke kwa nini Bibi?”

Niliuliza maswali kwa mkupuo

Akaniambia

“Salumu kumbuka nilikwambia jambo usilo lijuwa ni sawa na usiku wa Giza kwanza kabisa ni story ndefu kidogo nahisi nikianza kukusimulia unaweza kulia

kabisa watoto ninao ndugu ninao tena kama ushawai kusikia jina la Wahida Tarq?

“ndio nishawai kumsikia hadi kumuona kwenye TV akizitangaza kampuni zake ni mmoja kati ya matajili hapa Nchini anamiliki viwanda maduka na mabasi ya

mikoani kibao tu!”

“Basi huyo Wahidi ni mmoja kati ya watoto wangu wanne niliowazaa kwa uchungu nikateseka miezi Tisa”…

Nikastuka na kuuliza Bibi unasema?”

“ndio huwezi kuamini kwa hiki nikwambiacho ila embu kaa hapa nikupake dawa kisha nikupe story ilikuwaje mpaka nikawa hivi”…

Nilikaa vizuri ili niweze kupata history ya Bibi. Akaanza kusema

“Kwajina naitwa Asma Salehe ni mtoto wa kwanza kuzaliwa kati ya watoto sita wa Mzee salehe na bibie Zulfa.

Nilizaliwa huko mkoani

Dodoma kusema kweli maisha kwetu yalikuwa mazuri sana hatukuweza kuijuwa nini shida

Wala tabu na mateso tulikula

kulala na kuvaa vizuri wazazi wangu wakatokea kunipenda Mimi kuliko wenzangu sikuweza kujuwa sababu hasa ni nini.

Nakumbuka tukio moja

Siku hiyo nilikuwa natoka shule

Nikakutana na kijana mmoja akaniita

nilitaka kumpuuza ni kheli ningefanya hivyo kuliko kuitikia wito wake

Msemo wa kubali wito kataa maneno ndio ulioniponza Asma Mimi nikaenda kumsikiliza yule kijana baada kufika

Ghafla nikajikuta nazibwa kwa nyuma. Nilijitahidi kujitoa nikashindwa

nikaanza kuona Giza totoro mbele

yangu sikujuwa nini kilicho endelea.

Nikaja kustuka na kuhisi maumivu

kila maeneo ya mwili

wangu hasa sehemu zangu za siri

nyuma na mbele macho nilifumbua kwa shida sana nilikuwa

nimefungwa kamba mikononi sikujuwa hapo nilipo ni

wapi na kwanini nimetendewa unyama kama huu nikajitahidi kupiga kelele kuomba msaada sauti haikutoka

damu zikawa zinanitoka sehemu za mbele bila shaka nimebakwa

na kutolewa bikira yangu nililia sana mpaka machozi yalikauka hakuna wa kunisaidia.

Nilikata tamaa nikajuwa ndio basi tena

Asma mimi nakufa bila kukamilisha ndoto zangu za siku moja kuwa mwana Shelia wa kujitegemea

Nikiwa nimejiinamia nikahisi kama mtu hivi kaingia kwenye kile chumba

nilicho fungiwa.

Nikainua uso wangu nikastuka kwa kile nilicho kiona mbele ya upeo wa macho yangu. Nilimuona binti

mmoja hivi akiwa kanisimamia

mkononi kashika kisu akaja mbiombio

na kukata kamba nilizofungwa akaniambia.

“fanya haraka ukimbie kabla Kaka hajarudi kutoka kazini!”

Kuna kitu niliitaji kumuuliza ila sikuweza kutamka

chochote akanisaidia kuninyanyua

nikajikaza hivyo hivyo japo

nilikuwa na maumivu kila mahali

kwa mwendo wa kuchechemea nikapiga hatua huku mabonde ya damu yakinimwagika”

“Salumu siwezi siwezi kuendelea naumia sana moyoni mwangu!”

Huku machozi yakimtoka Bibi akaniambia hivyo. Nikamfuta machozi na kumwambia pole sana!”

Akaitikia “Asante”

Akaendelea kusimulia

“Basi nikajitahidi kutembea huku nikitafuta njia ya kuelekea nyumbani hatimae nikafika nyumbani. Mama na ndugu zangu wengine waliponiona wakaja mbio

mbio nikadondoka chini na kupoteza fahamu.

Nikaja kustuka na kujikuta niko hospitali nimelazwa huku nimetundikiwa dripu ya damu nikatizama kushoto kwangu nikamuona Mama nikafumbua mdomo

wangu na kumwita.

“Mama”

akainua kichwa chake na kuja kitandani haraka huku akiniuliza

“Asma mwanangu uu mzima?”

Nimjibu nini zaidi ya kulia tu.

Siku wiki miezi ikatimia hafya yangu ikatengemaa huku police wakiwa tayari washamnasa mtuhumiwa

Kesi ikawa ipo mahakamani

Nikiwa najiandaa kufanya mitihani ya kumaliza form four

Shuleni kwetu kuna kawaida ya kupimwa mikojo kila baada ya miezi sita basi sikuwa na hili wala lile nikapeleka mkojo wangu

Majibu yakatangazwa tena mbele ya wanafunzi wote sikuamini pale Headmaster aliposema wanafunzi kama nane au tisa hivi wameitia aibu shule hii kwa kubeba

mimba pasipo kumaliza masomo yao”….

Akaanza kutaja majina

Wakwanza ni Faudhia Eva Prisca Pendo Asma. Nikastuka

kwani kila jina unatajwa na mzazi wako nguvu zikaniishia miguu ikawa mizito nikaona kizunguzungu nikaenda chini kwa Mara nyingine nikapoteza fahamu

Nikaja kuzinduka nikiwa mikononi mwa Mama akiwa analia

Baba akiwa pembeni kajiinamia baada kugundua nimeweza kurudisha fahamu zangu akanyanyuka na kuanza kufoka kwa hasira

“Wee nyau pusi kenge blue Malaya mkubwa yani Mimi napoteza pesa zangu kukusomesha wewe leo hii unakuja kunitia aibu katika familia yangu kwa kubeba

ujauzito!”

Nitamjibu nini Baba zaidi ya kubaki kimya tu ndio ana haki ya kuongea hivyo ila atambuwe mwanae nilibakwa mie!”

Akaingia ndani punde tu akatoka na begi langu.

Akanitupia huku akizidi kuongea

“Sasa kuanzia leo sitaki kukuona ndani ya nyumba yangu nenda kwahuyo aliyekupa mimba shenzi zako!”

Mama akaingilia kati na kuanza kunitetea.

“Hivi wewe Mwanaume unaakili kweri yani unajuwa kabisa binti yetu alibakwa ndio kimepelekea kushika mimba afu wewe na bange zako unataka kumfukuza

mtoto!”

“Nishasema sitaki kumuona ndani ya nyumba hii icho kisingizio cha kubakwa Mimi sikijui usikute ana Wanaume zake huko ndio wamempa hicho kitumbo

kisingizio kabakwa

Naingia ndani nikitoka nisikukute

wee Malaya

Machozi yakanitoka. Mama nae akajitahidi kunitetea ghafla Baba akatoka na panga nikatoka mbio na begi langu nikaamua kwenda kwa Shangazi nae akanitimua

kwa

madai ya kwamba asije akakatwa kichwa na Baba.

Nikaenda kwa shogaangu Zurekha nikashukuru baada kunipokea vizuri tu nikawa naishi hapo kwao wazazi wake wakatokea kunipenda na kunijali kwa kila kitu

hasa Baba yake Zulekha

Kuna siku alikuja mgeni ni Mwanamama mtu mzima hivi Zulekha aliniambia ni Mama yake mdogo basi akaonekana kunifurahia mwishoe akaniomba aondoke

na Mimi kwenda jijini Dar es salaam.

Sikuwa na jinsi zaidi ya kukubali tu

Baada siku kazaa nikawa nipo ndani ya jiji hili maeneo ya Kawe ukwamani

Nikapokelewa vizuri na familia yake

Nikiwa kama mwanae wa kunizaa vile

Nikaweza kupata marafiki wengi tu huku kitumbo changu kikiendelea kukua

Nakumbuka siku moja usiku nikiwa nimelala ghafla nikahisi kama vile kuna mtu ananishika shika nikafumbua macho yangu taratiibu hamadi ni Baba mwenye

nyumba tena akiwa uchi wa mnyama akijiandaa kuniingilia

Nikastuka na kupiga kelele akaniziba mdomo nikamng’ata

ajabu taa ikawashwa nikamuona yule Mama akiwa kashika mwiko

Na kuja kunitandika nao huku mumewe akiniacha napigwa yeye akaondoka kwa kicheko

Kumbe siku zote akufukuzae akwambii toka atakufanyia visa tu

Nikafukuzwa kama mbwa usiku wa manane Asma nililia sana sikujuwa wala kufahamu Usiku kama huu nitaenda wapi

Nikafikia hatua ya kukufuru kwa kulaani kwa nini nimezaliwa

Nimeletwa duniani kuja kuteseka why?

Mpaka kufikia hapo story ya Bibi ikanitoa machozi nikampa pole kwa mitihani aliyo pitia.

Akaniambia

“Salumu nilikwambia usilie maana ukilia nitashindwa kuendelea kingine jikaze wewe ni Mwanaume!”

“Sawa Bibi nitajikaza sitolia tena!”

Akatabasamu japo kwa kulazimisha akaendelea kusimulia

Usiku ulikuwa mkubwa sana Kawe nzima ilikuwa kimya nikaenda kumgongea mmoja kati ya Mashoga zangu anayeitwa Sikitu baada kumgongea kwa muda

akaitikia na kuuliza wewe nani?

Baada kumjibu akawasha taa na kuja kunifungulia mlango nikaingia ndani na begi langu

Hakutaka kuniuliza kitu kwakuwa ilikuwa usiku tukalala ila Mimi sikupata hata lepe la usingizi

Usiku kucha nikawa nawaza na kuwazua kuhusu mustakabari mzima wa maisha yangu. Nikajikuta mchozi ukinitoka,

Asubuhi kulipokucha

Sikitu ikabidi aniulize

“Ehee vipi tena shost kunijia Usiku usiku na mabegi?”

Sikuwa na jibu la kumpa zaidi ya kuinamisha kichwa changu chini. Mchozi sijui macho yangu hayana komeo au vipi nikajikuta nalia.

Sikitu akanibembeleza na kuniambia

sikuwa na jinsi zaidi ya kumsimuliza kila kitu,

Sikitu akabaki kusikitika tu, na kusema

“pole sana Asma hakika utaishi hapa pamoja nami

japokuwa maisha yangu ni magumu sana tutajisogeza tu hivyo

hivyo.

Tukipata tutakula tukikosa tutalala”

Sikuweza kuamini nikamkumbatia

Shogaangu huku nikijifuta machozi.

Salumu usione nimechakaa hivi

mpaka unaniita bibi,

Hapana mimi ni sawa na umri wa

Mzazi wako au mama yako mdogo.

Siku zote yaache maisha yaitwe maisha, leo

hii msichana wa kijijini akitembea pamoja na

Binti wa mjini yule mwenye kujipiga

sijui madudu gani wenyewe wanaita”…

Nikamtajia

“Wanaita Mockup,

“ehee ndio hayo basi hata kama binti wa mjini atakuwa na umri mkubwa ataonekana mdogo.

Wakijijini ataitwa bibi yote sababu ya kutopata matunzo bora,

Salumu nikuulize kitu?”

“ndio bibi niulize”…….

“hivi Mama yako mpaka sasa yupo hai nakama yupo hai ana umri gani?”

Nikamjibu

“mpaka sasa mama anamiaka 42

Tu”

Bibi akatabasamu na kuniambia

“hakika mama yako nimempita miaka sita tu

Salumu ni haki yako kuniita bibi,

Binafsi story hii nitakusimulia kila kitu kuhusu maisha yangu

sitoweza kukuficha chochote kile Nina

hakika wewe ni mtu mzima sasa.

Unaejuwa baya na zuri”……….

“basi Asma shogaangu nyamaza usilie piga moyo konde Mimi nipo Tayari kuwa pamoja nawe bega kwa bega. Niambie nini tatizo”..

Nilijisikia faraja sana kuwa na rafiki kama Sikitu alikuwa ni zaidi ya ndugu kwangu niliweza kuishi hapo kwao japokuwa katika swala la kupata chakula

lilikuwa shida sana kusema kweli Sikitu hakuwa na kazi yoyote ile yenye kumuingizia kipato.

Nahiyo nyumba wameachiwa kama urithi tu na marehemu Baba yao

Sikitu ana wadogo zake wawili wote wakike ni vibinti vikubwa tu kama Mimi kipindi hiko.

Kutokana na maisha kuwa magumu nikajikuta nadondokea mikononi mwa muuza chipsi

Sikujuwa kama ananidanganya ili mladi aweze kunitumia tu.

Aliponiambia ananipenda nikajikuta namkubali bila kipingamizi siku zote penzi linapochipukia basi yanakuwa motomoto

lakini mwisho wa siku linafifia taratibu kama mshumaa unaokwisha vile.

Kijana yule anaekwenda

kwa jina la Swedi akanilazimisha nitoe mimba kwa kisingizio cha kutaka

kuniowa hakika nikapinga

kufanya kitendo cha kinyama kama hiko

Salumu mjukuu wangu kuna matukio mengi yenye kuumiza na kusikitisha

Katika dunia hii

Yenye kutawaliwa na mambo ya kishezi unyama siku hiyo katika mtaa wetu kulikuwa na Mnanda sio sijui vigodoro kama hizi zama zenu

sie enzi hizo tulikuwa tunacheza mnanda mchiriku vanga mdundiko.

basi nikaenda kuangalia tu sikuweza kucheza sababu ya ukubwa wa tumbo langu.

Tokea nashika mimba mpaka wakati huo sikuwai kuijua krinik hakika

Mungu pekee ndie aliyekuwa akinipigania.

Nikiwa na shogaangu Sikitu na wengineo kila mmoja akaonyesha ujuzi wa kuzungusha kiuno katika

kibao kata ulizungushwa mduara hivi

nilitamani namie nicheze nikashindwa ghafla nikaja kushikwa mkono na kibwana changu Swedi

akanivutia pembeni na kuniomba nikampe dawa maana anajisikia hamu.

Nikamkatalia kwa kumwambia

“hivi wewe Mwanaume wa aina gani usiejali hali ya mwenzio ikoje kwanza siwezi kukupa usije kumtoboa mwanangu utosini bure meana ukipewa unafanya

kwa sifa embu niache!”

Swedi hakutaka kuniachia.

“Asma mpenzi ujuwe mwenzako nyege zimenizidia nakuahidi nitafanya

taratibu sitoingiza yote

twende basi baby afu kesho uje nyumbani kuchukuwa ule mzigo!”

Mmh nikacheka

Baada bibi kutaja kitu Nyege

Hahaha

“unacheka nitaacha kusimulia Ohio!”

“haya basi bibi endelea”

Akaendelea

Nikajikuta nalainika kwa maneno ya Swedi

japo nikakana kauli yake ya kutoingiza yote sababu bunduki yake

haina masikio au mapembe kusema ataingiza mwisho wa kikomeo.

Basi tukaingia kwenye mjumba fulani hivi ambao ulikuwa katika matengenezo haikuitaji maandalizi

Swedi akanivamia na

kunivua nguo yangu ya ndani. Na kuniingilia binafsi alikuwa anafanya kwa hasira baada raha nikahisi karaha

Maumivu nikayasikia ila nilivumilia ili kumlizisha mpenzi wangu

Hatimae akamaliza huku akihema akaniambia hasante sana baby akanikiss kisha akapiga mruzi nikamkataza asipige mruzi Usiku ule.

Anaweza kuita majini.

Ghafla nikastukia vijana wakiume kama 8 hivi wakiingia ndani mjumba ule hakika nilistuka sana nikijua tumevamiwa. Nikamuona Swedi akipeana nao salamu

hapo hofu ikanishuka baada kugundua kumbe mpenzi wangu anajuana nao.

Mmoja kati ya wale vijana akauliza

“Demu mwenyewe ndio huyu boss?”

Swedi akajibu

“ndio yeye ninachohitaji kazi ifanyike kimyakimya!”

Kengere ya hatari ikagonga kichwani kwangu Swedi akatoa pesa na kumkabizi yule kijana aliyeuliza swali.

Asma Mimi nikavamiwa na kuanza kushikwa shikwa kwenye maungo yangu nikavuliwa gauni langu nikajitahidi kupiga kelele nikashindwa baada kuzibwa

mdomo

Nikalazwa chini na kuanza kuingiliwa kwa zamu Giza totoro likatanda kwenye upeo wa macho yangu sikujuwa kilichoendelea.

Nilikuwa nimepoteza fahamu.

yani kupoteza fahamu ilikuwa kama hobi yangu.

Nikaja kustuka na kujikuta nipo kitandani huku nikiwa na maumivu kila mahari nikaitaji kujiinua nikashindwa nikasikia sauti ya shogaangu

Sikitu akija mbiombio huku akiita Nesi!!!

nesi!!! akaja hadi kitandani na kuniuliza

“Asma umzima Dada yangu?”

Kwa macho ya kivivu nilimtazama Sikitu machozi yakaanza kunichuruzika na kurowanisha shuka.

Ajabu nikajishangaa sina mimba tena

Nikaitaji kumuuliza Sikitu ila.doctor akaingia akiwa na kitoto kichanga mkononi kwa uso wa bashasha na tabasamu zito akaniambia

“ongera Binti kwa kujifungua mtoto wakiume”

Nilifurahi sana nikajisikia faraja kwa kuweza kupata ndugu ni kweli mwanangu ni kama ndugu ni mtoto wakiume nikampa jina la Wahidu yani ni mmoja tu!”

Nikatoka hospitali kila aliyeniona mtaani wakati narudi kutoka hospitali alikuja kunipa pole wakiambatana na zawadi za hapa na pale.

Kama Neema ya Mungu basi Wahidu alikuja nayo kumbuka baada ya ziki faraja, kuna Mwanaume wa kiarabu akajitokeza na kuitaji kuniowa

Alikuwa yupo Tayari kulea mtoto asiekuwa wake.

Sikutaka kudenguwa maisha yenyewe yako wapi nikakubali nikaolewa

hakika Mwanaume yule alikuwa na pesa kama tipa la mchanga.

kila nilichokitaka Asma nilikipata

Wahidu mwanangu akatimiza mwaka mmoja na nusu nikaweza kushika mimba ya bwana Tariq ndio Mume wangu hatimae nikaja kujifungua watoto mapacha

Wakike na kiume kutokana na Furaha aliyokuwa nayo Mume wangu akaanda bonge la sherehe

Watu walikula na kusaza nikiwa katikati ya sherehe nikajikuta nashikwa makalio yangu kwa nyuma. Kwanza nikastaajabu nani huyu anayenishika hivi”……

Maana hata Mume wangu hana tabia hiyo. Kugeuka dahaa kumbe ni Swedi

Mwanaume aliyenitendea unyama wa ajabu yani nikabakwa na Wanaume nane hasira. Zikanishika

Na kujikuta nachukuwa kisu kidogo hivi. Kwa nguvu zote nikamchoma nacho shingoni.

Hakutegema

mimi kufanya vile

kuna kitu alitaka kuongea akashindwa Asma nikajikuta nauwa

mbele ya umati wawatu

Siku zote hasira hasara nikakamatwa japokuwa Mume wangu alitumia kila mbinu kwa kuhonga pesa ila mwisho wa siku nikahukumiwa kunyongwa!”

Nikashituka na kumuuliza Bibi ulihukumiwa kunyongwa tena?”

“ndio nilihukumiwa kunyongwa

Mwanangu Wahidu alilia sana kunililia Mama yake. Ndani ya mahakama ya kisutu nikavishwa pingu safari ya kwenda segerea

ikaanza ukungu mzito ulitanda

kwenye macho yangu machozi yalinijaa nikainua uso wangu kuangalia

Mbinguni japo niongee

na Mwenyezi Mungu nimuulize kosa gani nimetenda mpaka nakutana na mitihani kama hii.

Asma nikafikishwa gerezani na

kutupwa jela nikakutana na wafungwa

waliopinda na kuchoka na maisha.

Hakika nikafanyiwa vitendo vya ajabu ajabu kwa kushikwa shikwa kimapenzi

na Wanawake wenzangu

nikagombewa kama mpira wakona

kila mmoja akitaka niwe mke wake.

Salumu usiombe kupelekwa

jela ni zaidi ya jahannam

kunatisha vibaya mno.

“Sasa Bibi kama ulihukumiwa kunyongwa imekuwaje leo hii upo hai

wakati mtu akinyongwa anakufa au walikosea kukunyonga nini?”

Lile swali likamfanya Bibi atabasamu kabla ya kujibu.

“Sijui tuseme muujiza au vipi nakumbuka nikiwa bado gerezani nangojea siku ya hukumu yangu kuna tukio moja lilitokea Usiku

baada sero niliyokuwepo Mimi kuwaka moto basi gereza zima

wakapiga kelele za moto…..moto…..

Askari jela wakaja haraka haraka na kuanza jitihada za kuuzima moto ule pasipo kufahamu chanzo chake ni nini.

Basi baadhi ya wafungwa tukaitumia

nafasi hiyo kutoroka

ndani ya gereza….

Baada kutoroka gerezani tulikimbia kutoka kwenye ile ngome nzito huku tukikimbizwa na Askari jela. Wakiwa wameongozana na Mbwa.

Hakika sikuweza kukata tamaa nilikimbia kwa juhudi zangu zote.

Baazi yetu tukaweza kuruka fensi ila wengine

wakaishia kukamatwa

Tulitoroka Wasichana kama kumi hivi ila sita wakanaswa tukabaki wanne

Tukiwa hatujui wapi tunapokwenda mmoja wetu akasimama huku akisema

Subirini kwanza ikatubidi wote tusimame.

Na kumtizama yeye kila mmoja akihema.

Akasema

“hivi naona tunakimbia tu pasipo kufahamu wapi tunakwenda!”

Hakuna aliyejibu kitu tukabaki kimya tu.

Akaendelea kusema

“Unajuwa kwa sasa Usiku umekuwa mkubwa sana mi naona tufanye jambo moja tu ili tuweze kupata usafiri utakao weza kutuondoa eneo hili!”

Nikamuuliza jambo gani hilo?”

Akanijibu ya kwamba

“Kwakuwa sie wote ni Wanawake kwanini tusijifanye kama vile Machangudoa yani tunajiuza ili tuweze kuiteka gari ya Mwanaume yeyote yule atakayejifanya ni

Mkwale!”

Kila mmoja akamtizama mwenzake tukaafikiana kufanya hivyo. Tatizo likaja kwenye mavazi yetu ya kifungwa nikajikuta naambiwa Mimi ndio niwe kama

chambo.

Kitendo bila kuchelewa wakanichania yale mavazi nikabaki na Chupi na kibrauzi tu

Salumu mjukuu wangu hapa naomba nikuambie kitu unajuwa kipindi hiko nikiwa angali Msichana nilikuwa ni mrembo

Kupita kiasi nilikuwa nina

figa ya maana popote

nipitapo vidume lazima

wageuze macho. Kunitizama mimi!”

Kwanza nikatabasamu kusikia Bibi anavyojisifia kisha nikamwambia endelea kunipa story ilikuwaje baada wewe kufanywa chambo.

Bibi akaniangalia na kusema

“Basi baada kufanywa Chambo sikutaka kukataa nikajitokeza hadi barabarani na kuanza kupungia magari.

Ndani ya dakika kama tano hivi ikasimama gari moja

aina ya Chase basi kwa mwendo wa madaha nikaikimbilia nikainamisha kichwa changu nikaweza kumuona Mzee mmoja hivi wa makamu mwenye asili ya kama

sio Pemba basi unguja, nikampa hi

Akaitikia kwa bashasha kubwa sana

Na kuniuliza

“Vipi Binti hiki kijiwe kipya nini mbona sijawai kuona Malaya katika maeneo haya?”

Nikamjibu

“Ndio boss unajuwa siku zote hizi biashara zetu zimetawaliwa na changamoto nyingi sana ndio maana tunahama vijiwe kila kukicha!”

Akaniangalia juu chini nikamuona akijiramba midomo kwa uchu hakika alitokea kunitamani ghafla

Sijui Wanaume wanaakili gani yani hakuweza hata kujistukia yakwamba kaniona eneo hilo la kutisha kidogo je ningekuwa Jini

Akaniambia tu.

“Oky ingia kwenye gari twenzetu”,,,,,,

Nikazunguka upande wa pili ghafla ukasikika ukelele wa maumivu ukitoka kwa yule Baba.

Kumbe tayari kina Agnes washafika na kumpiga na sijui Kipande cha mti au jiwe kichwani.

Maana kishindo kikubwa kikasikika mwishoe akawa kimya huku damu zikimvuja kichwani.

Nikaingiwa na roho ya imani nikaitaji kumsaidia ila nikajuwa nitaonekana mwehu tu.

Basi tukamshusha yule Mzee tukaenda kumbwaga pembeni ya barabara kisha tukaingia ndani ya gari na kuondoka eneo lile kwa speed Agnes ndio alikuwa dereva

Sikuweza kufahamu wapi tunakwenda

Kingine nikaweza kugundua kumbe wenzangu wanafahamiana.

Nikawa nimenyamaza kimya kikubwa zaidi nikimuwaza Mume wangu na watoto wangu.

Nikajikuta mchozi unanitoka pasipo kutarajia hakika maisha yangu

hayana tena thamani maana nilishahukumiwa kunyongwa. Hakika safari yetu ilikuwa ndefu sana maana tulikatiza Gongolamboto mpaka Tazara tukatokea

buguruni hadi ubungo.

Nilitamani kuuliza jamani tunakwenda wapi. Nikaona bora niwe mpole tu…..”

Hatimae tukatokea tegeta.

Sehemu zote hizo nilizifahamu kutokana na

Rafiki yangu kipenzi

Sikitu kuweza kunitembeza katika jiji hili. Safari yetu ikaishia Goba gari ikasimama kisha tukashuka mbele yetu kulikuwa na nyumba yenye geti jeusi mmoja

kati yao ikabidi aruke ukuta na kufungua geti.

Gari ikaingizwa ndani geti likafungwa yani nilibaki kushangaa tu.

Hatimae milango ya jumba lile lenye thamani sijui Billion ngapi ikafunguliwa tukaingia hadi Sebureni

Hakika nyumba ilisheheni mazagazaga kibao tu.

Hakuna aliyweza kukumbuka kuoga wakafungulia Radio yao kubwa yenye sauti kubwa na nzito utazani vigodoro vyetu vya uswazi wakaanza kuyakata mauno

friji likafunguliwa

wakatoa vinywaji vya kila aina yani pombe zile kali kali.

Nikajiuliza maswali pasipo kupata jibu hivi hawa si walikuwa wafungwa inakuwaje wanafanya mambo kama haya ndani ya jumba hili inamaana kila kitu

walikiandaa au?

Nikiwa nawaza hivyo nikastuka baada kuhisi nashikwashikwa kimapenzi nikamtizama anaye nishikashika kumbe ni Agnes huku akiuleta mdomo wake kwangu

ili aninyonye denda nikaukwepesha akanishika kwa nguvu

Ajabu akatoa na bastora

Huku akisema

“tulia hivyohivyo kumbuka umekubari

Kutoroka na sisi kwahiyo

unatakiwa ufanye kile ambacho sie tunataka ufanye kuanzia leo wewe ndani ya nyumba hii utakuwa ni Mke wetu utake usitake hiyo lazima

Kama vipi chaguwa moja tukurudishe gerezani ukasubilie siku yako ya kunyongwa au ukubari kuhudumia Wanaume watatu kwa mpigo ndani ya nyumba hii?”

Nilijikuta nakubari kuwa Mke tena Wanaume wenyewe ni Wwnawake wenzangu mbona majanga.

“Kwahiyo Bibi hao Wanawake mpaka inafikia hatu yakuwa Wamezako je hiyo neo mliozeshana wapi?”

Bibi alitamani hata kucheka ila akatabasamu tu na kusema

“Haikuwa ndoa ya Kanisani wala Msikitini yani ilikuwa ndoa ya humohumo Chumbani kila mmoja akiniitaji kwa wakati wake basi ananichukuwa na kwenda

kunifanya

Kwa kutumia midude sijui ya bandia ile

Hakika dunia ina laana kubwa sana.

Mwenyezi Mungu atusamehe huko tuendapo.

Niliweza kuvumila shida zote utakuta napigwa pasipo sababu mwishoe nikaja kuuzwa kama Kuku vile.

Wakati Mimi ni binaadamu

Nikaenda kufanya kazi kwenye familia ya wahindi

Asikwambie mtu hakika wahindi wanaroho za kinyama sana niliweza kufanya kazi kama punda

Usiku na mchana japokuwa niliweza kutangazwa kwenye vyombo vya habari Mimi na wenzangu tuliotoroka

Ajabu hakuna katika famili hii ya Wahindi yenye watu takilibani kumi na sita hakuna aliyestuka. Kama mimi ni wanted

Maisha yakazidi kusonga ndani ya mjengo ule kawaida hutakiwi kula chochote kile mpaka uakikishe kazi zote ulizokabiziwa zimeisha

Utakuta naamka saa kumi Usiku.

Wakati kulala nalala saa saba Usiku

Basi nitapewa mikazi yani kuosha vyombo kufua nguo za watu kumi na sita hao wote ni watu wazima ukichanganya na watoto shida tupu utakuta nakaa na njaa

Asubuhi mpaka mchana

Nikaona njia pekee nifunge jiwe tumboni ili kuzuia hii NJCAA

Kwani hata nikipewa Chakula chenyewe sishibi

Utakuta napewa chai. Robo kikombe na mkate nusu silesi ndio nile

Huku wao wakila mapochopocho kibao

Basi kuna Mwenzangu mmoja alishindwa kuvumilia hali hiyo

Akaamua kuvamia jikoni akala ndani yake

Si akafumwa kilicho mkuta siwezi kusimulia maana.

Bibi baada kusema vile akaanza kulia

Je nini kitaendelea?

Kumbuka Bibi bado anaendelea kumsimulia Salumu history ya maisha yake kuna mengi ya kujifunza

Katika story hii tatizo like ndogo au kwa sababu hakuna

yale mambo yetu

Assess,,,,ohoooo

mmmmm,,,,chomekaaa,,,tamuuu

Sikuwa na jinsi zaidi ya kumbembeleza kwanza bibi, hakika alikuwa na maumivu makubwa sana katika moyo wake. Nilihisi ya kwamba kama nimemtonesha

kidonda, ambacho kilikuwa tayari kishapona na kubaki kovu tu, nikamwambia

“Bibi basi usiendelee kusimulia maana naona unazidi kuumia tu!”

huku akijifuta mchozi na kaniki yake akaniambia,

“hapana Salumu ni haki yako kutaka kuijua story hii kuna sababu nyingi za Mimi kukusimulia wewe ili uweze kujuwa na kufahamu

Ulimwengu uko vipi.

Basi baada yule mwenzangu kwa jina anaitwa Sikujuwa kama lilivyo jina lake na kweli hakujuwa

Hakika alipigwa sana, akajitahidi kuomba msamaha ikashindikana kusamehewa alipigwa na Mwiko kuna Muhindi mmoja alikuja akiwa kashika pasi sikuweza

kujuwa anataka kufanya nini, kwa kiswahili chake kibovu akasema

“funua nguo hiyoo veve,,

Sikujuwa akafunuliwa gauni lake sikuweza kuamini baada ile pasi kukandamizwa kwenye mgongo wa Sikujuwa

Ndipo nikatambua ile pasi ni yamoto kwani moshi ulikuwa unatoka huku harufu ya nyama kuungua ikisikika.

Sikujuwa hakuweza kutikisika tena alikuwa kimya sijui amekufa au vipi”

Hakika story hii ilinifanya mwili unitetemeke kwa uwoga ni

Mateso gani aliyopewa huyo binti kisa chakula tu, dahaa,

Bibi akaendelea kusema,

“Salumu naomba utambuwe kitu kimoja mimi mpaka kufikia hatua ya umri huu nimepitia mambo mengi sana

Tokea siku hiyo sikuweza kumuona

Sikujuwa sikuweza kufahamu amekufa au laa

Ikabaki siri yao wenyewe wahindi,

Maisha yakazidi kusonga huku nikiishi kwa shida ndani ya jumba hilo

nilifanyishwa kazi kama punda chakula kikiwa kidogo ikafikia kipindi nikakonda vibaya mno

Mabega yakanipanda utasema kikongwe cha miaka mia moja na kitu ndipo nikapanga kufanya jambo.

Jambo ambalo mpaka leo hii naijutia nafsi yangu,

Salumu mjukuu wangu naona kigiza kinaingia itabidi uwende nyumbani kunapo majaaliwa yake

Allah kesho nitaendelea kukusimulia,

“Insha Allah bibi wacha Mimi niende kesho Asubuhi na mapema nitakuja kukuletea chai na vitafunwa kwani usiku huu unakula nini Bibi?”

“nitakula kiporo changu cha ugari!”

Nikatabasamu na kuagana nae

hakika nilienjoi sana kutokana na historia ya Bibi yenye kusikitisha na kufurahisha,

Nikapiga hatua kadhaa kisha nikasimama kuangalia nyuma

Nilimuona bibi akinipungia mkono wa kwaheli nami nikampungia

Nikafika nyumbani na kukuta kuna mzozo yani vurugu baina ya wapangaji,

Nikasogea niweze kufahamu wanagombania nini

“nishakwambia hunitishi kwa lolote wewe mbwa tu tena kijaa malaya mkubwa wewe muone kwanza sura kama mlinzi wa Monchari”

“Mlinzi wa monchwari Baba yako bwege”….kwanza jiangalie nitakupasua Ohooo!!!

ITAENDELEA

Mzoa Takatakata Sehemu ya Tano

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment