Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034 Sehemu ya Tatu
KIJASUSI

Ep 03: Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034

SIMULIZI Vipepeo Weusi Mkakati Namba 0034
Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034 Sehemu ya Tatu

IMEANDIKWA NA: THE BOLD

*********************************************************************************

Simulizi: Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034

Sehemu ya Tatu (3)

Tukainuka na kuanza kunyoosha miguu pale yard.

Kuna muda kwa kiasi fulani nilitamani kama siku zote humu gerezani ziwe za utulivu kama siku ya leo.

Siku amabayo hakuna mipango ya siri, hakuna pilika pilika za kuchoma moto vitu vya watu, hakuna mipango ya kuhatarisha maisha.

Lakini si sahihi kuruhusu hisia hii ya kutamani utulivu initawale. Sikuja humu ndani gerezani ili niwe na utulivu.

Lakini bado nikiri kuwa kuna muda nilitamani utulivu kama wa siku hii ya leo uendelee.

“Faridi Mkudeeeeeeeee! Eeeee faridi mkudeeeeeeee”

Mfungwa maalumu ambaye ‘kitengo’ chake kilikuwa ni kuchukua majina ya wageni na kuja kutangaza wafungwa wanaohitajika kwenda kuonana na ndugu zao, alipita yard anaita majina ya wafungwa.

Roho ikapata tumaini. Saa nne ilikuwa imewadia na Mungu akipenda muda wowote kuanzia sasa naweza kupokea ugeni wa Cheupe na Issack.

“Kaburu umemuona asubuhi hii” nikamuuliza Godi bado tukiwa tunaendelea kunyoosha miguu pale yard.

“Yuko sehemu ya kupumzika wagonjwa”

Godi akanijibu huku akinifahamisha kuhusu sehemu alilopo Kaburu sehemu ya kupumzika wagonjwa ambayo ipo sehumu ya upande wa gereza kule mbele liliko jiko.

“Yule mjinga leo lazima inabidi afunguke” nikaongea kwa sauti serious.

“Hao ndugu zako ndio waje na info za maana sasa! La sivyo tutakufa jela humu maana ni suala la muda tu kabla watu hawajafahamu tulichokifanya juzi”

“Yeah ofcorse unajua…….” Kabla sijamaliza kuongea nikasikia jina langu linaitwa kwa nguvu na yule mfungwa mtangaza majina ya kwenda kuwaona wageni.

“Eeeeeeehh Rweyemamu Charles! Eeeeeehh Rweyemamu Charles…” Yule mfungwa alikuwa anapayuka.

“Nipooooooooo” nikaitika kwa sauti ya juu.

“Kilala kheri boss” Godi akaongea huku ananipigia saluti kwa utani..

“Yeah!” Nikamjibu kwa kifupi huku naondoka kwa mwendo wa kasi kuelekea upande wa gereza kule mbele kwenye vyumba vya maofisi ambapo pia kuna upande maalumu wenye chumba cha kuongea mfungwa na mgeni wake.

Utaratibu ni kwamba jina lako likiitwa unakuja hapa unaingia moja kwa moja kwenye chumba cha kuonana na wageni na kusubiri. Wageni wako waliokuja kukuona wakikamilisha taratibu huko nje nao wanaletwa katika chumba hiki wanakukuta hapa kisha askari anaondoka , mnaendelea na mazungumzo yenu.

Katika muda ambao wageni waliokuja kuwaona wafungwa wakiwa wengi mnaweza kujikuta hata wafungwa watatu au watano mmeingia humu kwa pamoja ili kuzungumza na wageni wenu.

Nilishukuru kwa wageni wangu kuja mapema kwani hii ilihakikisha kuwa titakuwa na faragha ya kutosha mimi na wao kuzungumza.

Nilisubiri kama dakika mbili hivi nikiwa nimekaa kwenye kiti, ndipo mlango ukafunguliwa na askaria kisha wakaingia Hasnat, Cheupe akiwa ameongozana na Issack.

Sikujua ni nini ila nilijikuata nasimama wima kutoka kwenye kiti baada ya kumuona cheupe.

Ubaya wa chumba hiki kama nilivyoeleza huko nyuma ni kwamba katikati kimetenganishwa na wavu mkubwa. Yani mnakuwa mnaonana lakini hamuwezi kuwa na “physical contact”.

Zilikuwa karibia siku sita pekee toka nionane ma Cheupe, lakini nilijihisi ninakaribia mwaka mzima sijamuona Cheupe wangu. Nilitamani ning’oe ule wavu kisha kimkumbatie so tightly Cheupe wangu.

Nikajikuta tu naweka kiganja cha mkono kwenye ule wavu. Cheupe naye akaweka kiganja upande wa pili wa nyavu. Tukawa kama tumegusana viganja vya mkono lakini hatuja gusana kutokana na ule wavu kati kati.

Nikamtazama Cheupe kwenye macho. Nikaona ni jinsi gani amenimiss, ni jinsi gani anatamani nimkumbatie sekunde hii. Lakini pia nikagundua ni kiasi gani alikuwa anajitahidi kujikaza asilie mbele yangu na kunitia huzuni zaidi. Lakini pia Nikaona hofu iliyopo ndani yake.

“Hujambo Cheupe” nikamsalimia roho yangu kwa hisia kubwa.

“Sijambo baba! How are you?” Akanisalimia pia Cheupe akiongea kwa hisia karibu machozi yamdondoke.

“Niko poa mama! Am doing great”

“Na mimi sijambo pia jamani!!” Issack akatukatiza salamu zetu za hisia.

Wote tukageuka kumuangalia na kutabasamu.

“Niaje Issack?” Nikamsalimia.

“Poa Kichwa! Ishu vipi”

“I’m great!” Nikajibu kwa kutabasamu.

“You are not great!! You are in a prison.. Hebu tumalize huu mpango wako haraka utoke humu.. I tottaly don’t like this” Issack akaongea kwa kukereka.

“Ok! Si mnajua kuna muda maalumu wa mazungumzo hebu tuongee fasta kabla hamjatolewa nje!! What do you got??” Nikaongea kwa shauku huku nakaa kwenye kiti na wao wakakaa.

“Well kama ulivyonieleza kuwa nianze kumchunguza Kaburu kwa kuanzia kwenye kesi yake na huko ndiko nilikoanzia” Issack akaongea kwa kunong’ona japokuwa tulikuwa peke yetu watatu tu ndani ya hiki chumba.

“Ok! Kuna chochote interesting mmekipata kwenye kesi yake?” Nikamuuliza.

“Actually tumepata a lot” Issack akaongea kwa tabasamu la ushindi.

Shauku yangu ikazidi.

“Ok! I’m listening” nikakaa sawa sawa kwenye kiti nimsikilieze.

“Hii kesi ya Kaburu alituhumiwa kumuua mpenzi wake Veronica Nyaulingo nadhani unakumbuka hilo” akaniuliza.

“Yes! Nakumbuka vizuri tu” nikamjibu.

“Ok! Sasa kabla ya kuanza kufukunyua kesi yenyewe na vitu vingine, tukajiuliza huyu Veronica Nyaulingo ni nani hasa? Na alikutanaje na Kaburu mpaka kuwa wapenzi” akaongea kisha akanyamaza kidogo kuniangalia na kuendelea “Tukafahamu kuwa alimaliza kidato cha nne sekondari ya Songea girls mwaka 2005, kisha akajiunga na Sekondari ya Kilakala na Kumaliza kidato cha sita mwaka 2008 na baada ya hapo akajiunga na chuo kikuu cha Dar es Salaam na kuchukua shahada ya Mass Communication na alihitimu mwaka 2011.! Kisha mwaka uliofuata akaanzisha kampuni yake ya consultation kuhusu masuala Public Relations na moja ya clients wake akawa ni kampuni ya Ndeshema Safaris ambayo inamilikiwa na Eric Kaburu na tunaamini hivyo ndivyo walivyo kutana” akanyamaza tena kidogo na kuniangalia.

“Ok!” Nikamjibu nikihisi kama bado kuna taarifa anataka kunipa.

“Ni taarifa nzuri, right??” Issack akaniuliza huku anatabasamu.

“I guess!” Nikamjibu kwa kifupi.

“Well ni taarifa mzuri except for the fact kwamba hakuna mtu anayeitwa Veronica Nyaulingo” Issack akaongea kwa kunishtuliza.

“Whaaaaat?? Sikuelewi!!” Nikauliza kwa mshangao.

“Ni hivi Ray! Binafsi nilikuwa curious kidogo kwa record zake jinsi zilivyo.. Ameenda Songea girls akapasua akapelekwa Kilakala nako akapasua akaensa UD nako anahitimu na ghafla tu mwaka ukiofuata anamiliki kampuni yake!! Its inspiring but binafsi nikawa curious” akaongea Issack kwa tabasamu la kujidai.

“Nakusikiliza” nikaongea tena kwa shauku.

“Nikaingia kwenye mtandao wa baraza la mitihani kuangalia usahihi wa hizo taarifa, na nikazikuta zipo tena kwa usahihi kabisa bila kukosewa hata spelling!! Lakini sikuridhika, Kuna mtu yuko Songea nikamtumia picha ya huyu mpenzi wa Kaburu nikamwambia aende Songea girls pale kuuliza kama wana kumbukumbu zozote za huyo mwanafunzi!! Kilichoonena kwenye mavitabu yao ya shule ni kwamba ni kweli kulikuwa na jina la mwanafunzi anayeitwa Veronica Nyaulingo mwaka huo lakini walivyoonyeshwa picha ya mpenzi wa Kaburu wote walidai kuwa hawakumbuki mwanafunzi mwenye mwenekano huo katika darasa la 2005!! Kisha mimi na Hasnat tukaenda hapa shule ya Kilakala na tukakumbana na kitu hicho hicho.. Kwenye kumbukumbu za shule yupo mwanafunzi mwenye jina la Veronica Nyaulingo lakini tulipowaonesha picha wote wakadai hawakumbuki mwanafunzi mwenye muonekano huo hapo shuleni..!! Hatukutaka kufukunyua sana ili tusije kuwatia mashaka, tukaona kama tukihitaji taarifa nyingine basi tutarudi siku nyingine.. Sasa nina rafiki yangu amesoma UD na alikuwa pale mwaka huo aliohitimu Veronica 2011..,akanitafutia mawasiliano na mtu aliyekuwa anasoma Mass Communication mwaka huo na nilipompata huyo mtu na kumuonyesha picha ya Veronica guess what he said?? Akasema yes anamkumbuka huyo binti walisoma naye mwaka huo!! Unajua hii maana yake nini??” Issack akaniuliza huku anatabasamu.

“Ameiba ‘identity’ ya mtu..” Nikamjibu huku natizama chini najaribu kufikiri.

“You got that right!! My theory ni kwamba kulikuwa na Veronica Nyaulingo mwenyewe ambaye alisoma Songea girls na Kilakala.. Lakini hapo kati kati akapotea na ‘identity’ yake ikachukuliwa na huyu binti ambaye alikuja kuwa mpenzi wa kaburu!! Swali ni je, Veronica Nyaulingo halisi alienda wapi?? Na kwanini huyu mpenzi wa Kaburu aibe Utambulisho wa mtu?? Na je hii ni coincidence mwizi wa utambulisho wa mtu kwenda kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanachama wa The Board.??” Issack akaongea na kuuliza safari hii akiwa serious kweli kweli.

Nilihisi kichwa kinazunguaka bila hiari yangu. Kulikuwa na karibia mawazo mia moja yanapita kichwani mwangu. Sikujua niwaze lipi au nishike lipi. Sikutegemea taarifa ya utata kiasi hiki.

“Ok ok ok! Najua hapa hamjaruhusiwa kuingia na makaratasi.. Binafsi licha ya kuisoma sana kesi ya kaburu kwenye vyombo vya habari lakini nimesahau vitu vingi hata Veronica mwenyewe sikumbuki anafananje! Nadhani kwamba ……….” Sikumalizia sentesi yangu nikamsikia Issack ameanza kuongea na kunikatisha..

“Ni kwa vile cheupe amekudatisha sana ndio maana humkubuki Veronica.. Ila hakuna mwanaume anayeweza kumuona Veronica na kumsahau.. Mtoto mkare utadhani toto la kitusi hahah” akaongea kwa utani na kucheka.

Lakini kwangu sentesi yake hii ya utani iliwasha taa kichwani mwangu. Nikabaki nimeduwaa.

“Umesemaje” nikauliza kwa mshangao.

“Nimesemaje kuhush nini” Issack akanijubu kwa kunishangaa.

“Umesemaje kuhusu mwonekano wa Veronica” nikamuuliza tena kwa mshangao.

“Ni mtoto mkali unaweza kudhani mi mnyarwanda” akanijibu huku ananishangaa.

Sikuamini kile nilichokibaini kwa taarifa hii iliyowash taa kichwani mwangu na kung’amua kilichojificha. “Unaweza kudhani ni mnyarwanda”, nikajikuta hii sentesi inajirudia tena na tena kichwani.

Sikutaka kuamini kile nilichong’amua.

“Nadhani naweza kuwa nimebaini siri iliyo nyuma ya huyu ‘Veronica’ feki” nikawaeleza huku nashusha pumzi.

Wote wawili, Issack na Cheupe wakabaki wamenikodolea macho kwa mshangao.

“Una maana gani kuwa umeshajua Veronica feki ni nani!” Issack akaniuliza kwa mshangao.

“Mnakumbuka nilivyo waambia nilipochukuliwa na Maafisa wa Usalama wa Taifa na kunipeleka maeneo ya Mbezi walikuwa maafisa wanne na mmoja ni mwanamke??” Nikawauliza.

“Yeah nakumbuka” wote wakaitikia kwa pamoja.

“Sasa yule mwanamke alikuwa ni Mnyaruanda. Hata kiswahili hajui kukiongea ingawa anakielewa, na nikawa najiuliza sana kwanini Maafisa Usalama wa Tanzania washirikiane na Mnyaruanda na Rwanda wana maslahi gani mpaka watume mtu huku?? Sasa kidogo nimeanza kuelewa!”

“Well, na umeelewa nini” Issack akauliza.

Nikasogea karibu na nyavu na kuongea kama nawanong’oneza.

“Nina hakika kuwa kuna kitu nchi ya Rwanda inachunguza kwenye mtandao wa The Board. Kwahiyo ninachokihisi ni kwamba Veronica ni mwanausalama wa nchi ya Rwanda na akatatumia mbinu kuanzisha uhusiano na Eric Kaburu ili aweze kupepeleza na kupata hiyo taarifa wanayohitaji. Ndio maana Rwanda mpaka leo hii wako interested na hii ishu ya The Board”

“Wow! Ina make sense kabisa. Nadhani ndio sababu kwanini Kaburu akamuua, itakuwa alikuja kubaini Veronica ni Afisa Usalama” Issack aongezea.

“No sidhani kama alimuua.” Nikamjibu.

“Kwanini unasema hivyo” akauliza kwa mshangao.

“Nimekaa hii karibia siku ya sita gereza moja na Kaburu, nimeongea nae ana kwa ana na kumsoma ni mtu wa aina gani. Trust me, Kaburu sio dizaini ya mtu mwenye uwezo wa kuua! So nina uhakika kabisa hakumuua Veronica.” Nikamfafanulia.

“But Kaburu mwenyewe alikiri kuwa amemuua!”

“Whaaaat??” Nikajikuta nauliza kwa mshangao.

“Yes kipindi kesi inasikilizwa mwanzoni kabisa mwa kesi, Kaburu akakiri kutenda hilo tukio! Ndio sababu kwanini kesi iliisha haraka haraka”

Nikashikwa na butwaa. Nikahisi hapa kuna jambo zito limejificha. Inawezekanaje mtu akiri kuua alafu ahukumiwe adhabu ya kuua bila kukusudia na apewe miaka saba pekee jela. Nikawa na uhakika kabisa kuna jambo limejificha hapa.

“Veronica alikuafaje?” Nikamuuliza Issack, licha ya kesi hii kuandikwa sana lakini nilikuwa nimesahau matukio mengi kuhusu kesi hii.

“Walikuwa Nyumbani kwa Kaburu, wakaanza kugombana na baadae Kaburu akaanza kumpiga! Inaelezwa kuwa akampiga mpaka akapoteza fahamu kisha akamchoma moto.. Na kwa mujibu ya magazeti yalivyoandika kipindi kile… Wanaeleza kuwa kisa ni wivu wa mapenzi” Issack akanifafanulia.

Taa ikazidi kuwaka kichwani mwangu. Nikahisi naanza sasa kuungajisha dots na kupata picha kamili.

“Wow! Ok ok, wow” nikajikuta naongea huku natikisa kichwa baada ya dots kuanza kuungana.

“What is it!” Cheupe akauliza kwa shauku.

“They fell in love” nikamjibu huku nawaangalia kwa tabasamu kwa furaha.

“Who fell in love?” Cheupe akauliza tena.

“Kaburu na Veronica! They fell in love!” Nikawajibu huku bado natabasamu.

“How? Kaburu amekiri kuwa alimuua?” Issack akauliza kwa mshangao.

“No hakumuua! Hicho ndicho Kaburu anachotaka watu wa amini.. Na amefanikiwa kuwaaminisha watu.. But the truth is hakumuua.. They fell in love”

Nikaongea huku natabasamu lakini niko serious.

“Oyaaaaa! Muda wenu ushaisha.. Tokeni huko” nikasikia sauti ya askari inaitilia nje ya chumba.

“Leo nitaongea na Kaburu na najua nimbane vipi ili aongee na mimi kwa hizi taarifa mlizonipa.. Nahitaji kesho mje tena hapa kuna maagizo tupene tena nina hakika nikiongea naye lazima nitapata kitu amabcho nitahitaji mkakifanyoe kazi huko nje”

Nikaongea huku tunainuka kwenye viti kwenye kile chumba cha kuongea na wageni.


Nilikuwa nimeketi mbele ya Kaburu kwenye upande wa gereza ambao kuna kisehemu cha wagonjwa kupumzika.

Kaburu alikuwa amekaa hapa ametandikiwa godoro amepumzika baada ya kutoka zahanati ya magereza kutokana na kipigo kizito cha virungu juzi.

“I’m impressed! Sikudhani kama unaweza kufanya kama kitu ulichokifanya juzi” aliongea akikumbushia tukio la juzi. Ni dhahiri alikuwa amegundua kuwa mimi ndiye niliyeufanya ule mchezo wote.

“Na hapo haujaona hata nusu ya kile ninachoweza kukifanya my friend” nikamjibu seriously nikimkazia macho.

“Ni nini unachoweza kukifanya?” Akaniuliza kwa dharau.

“Nina uwezo wa kukufanya uongee na mimi na unambie ninachokitaka kwa hiari yako au kwa kukulazimisha ufanye hivyo” nikajibu kwa kiburi.

“Hahahahaha!! Wooow, i’m really scared!” Akaongea huku anacheka kwa dhihaka.

“Unajua kipindi nasoma advance Sekondari ya Tambaza!! Kulikuwa na jamaa mmoja hivi ambaye alikuwa na tabia za kishenzi sana.. Kutukana watu, kupigana, uonevu wa kijinga jinga.. Sasa kuna siku akajichanganya akanitukana mbele ya darasa zima!! Unajua nilianyaje” nikamuuliza huku nimemkazia macho.

“Ulifanyaje” akaniuliza.

“Nikamfuata faragha akiwa peke yake, nikamwambia nampa siku tatu aniombe msamaha mbele ya darasa zima na asipofanya hivyo atajuta kwa kitakachomkuta”

“Alikuomba msamaha?”

“Hapana! Alinitukana tena hapo hapo.. Lakini unajua nini kilifuata?” Nikamuuliza.

“Ukampiga ngumi?”

“No! Wiki moja baadae akafukuzwa shule kwa kosa la kusambaza picha za uchi za demu wake” nikamueleza huku nimemkazia macho na kumsogelea.

“Wow! Kumbe hii michezo ya kuwafanya watu waonekane wamefanya vitu ambavyo hawajavifanya umeianza zamani sana kijana” akaongea huku anang’ata midomo kwa hasira.

“Ninachojaribu kukwambia ni kwamba, I always get what i want.. Nikitaka kitu kitokee akili yangu itapata namna ya kufanya ili nipate hicho kitu”

“And unahitaji nini kutoka kwangu?” Akaniuliza huku amenikazia macho.

“Nahitaji unieleze kila unachokijua kuhusi The Board” nikamjibu huku pia nimemkazia macho.

“Hahahahaha! Unaota kijana.. Kirahisi tu hivyo?? Hahahaha, endelea kuota” akajibu huku anacheka kwa dharau.

“Well, sio kirahisi rahisi tu… Itabidi unieleze ninachohitaji ili nikae kimya nisiwaeleze watu wa Usalama kwamba Veronica bado yuko hai” nikaongea kwa kusogelea karibu kabisa nikitoa sauti kama nanong’ona.

Nikauona mshtuko wake kwenye macho yake. Nilikuwa nimegusa ‘ikulu’.

“Umeanza kuchanganyikiwa Dogo” akanijibu kwa sauti ya woga huku anajigeuza kwenye gorodo na kuangalia pembeni.

“Really?? Nimechanganyikiwa? Una hakika?” Nikaongea huku nazunguka godoro kwenda upande ule aliogeukia. Nilikuwa nataka niongee naye huku namuangalia usoni ili maneno yangu yawe na effect niliyoitaka.

“Sikiliza Kaburu” nikaanza kuongea mara bada ya kuwa upande ule mwingine tunaangaliana. “Nafahamu kuwa Veronica Nyaulingo sio jina la mpenzi wako ambaye watu wanaamini amekufa. Amechukua jina la mtu ambaye mpaka sasa najiuliza amepoteaje huyo mtu. Ninachokiwaza ni kwamba wewe na wenzako The Board, kuna kitu mlikuwa mnakifanya nchini Rwanda na serikali ya Rwanda ikaja kugundua. Baada ya kugundua ndipo wakampandikiza afisa usalama wao ambaye alichukua ‘identity’ ya Veronica Nyaulingo ma kujiweka karibu na wewe na matokeo yake mkawa wapenzi. Naamini kuwa baada ya muda ingawa hii kwake kuwa na wewe kimapenzi ilikuwa ni assignment lakini akajikuta amekupenda kikweli kweli na wewe ukampenda. Na kama watoto wa sekondari vile mkajikuta mpo kwenye mapenzi mazito. Sasa lazima ikafika kipindi The Board wakagundua kuwa Veronica ni ‘spy’ na amepandikizwa kwenye maisha yako ili akupeleleze. Nina hakika kuwa kuna siri nyingi tayari alikuwa amezijua kuhusu wewe na The Board, kwahiyo The Board lazima wakafikia uamuzi kuwa inabidi auwawe. My guess is, wewe Kaburu ukawaambia wenzako kuwa wakuachie wewe hiyo kazi ya kumuua Veronica.” Nikanyamaza kidogo na kumuangalia usoni. Nikaona jinsi haya maneno yanavyomgusa moyoni. Niakaendelea.

“Najiuliza sana mwili ulioichoma moto uliutoa wapi. Na ni mwili wa nani, lakini nafahamu na nina uhakika kabisa sio Veronica Nyaulingo. Mpenzi wako Veronica kwa kutumia uzoefu wake wa ushushushu ukaenda kumficha mahali salama kabisa ambako anaishi mpaka leo hii, lakini huku nyuma ulimwengu mzima ukaamini kuwa wivu wa mapenzi umekufanya umempiga mpenzi wako na kumchoma moto!! Sasa wanasema kuwa ‘you can fool some people for some time but can’t fool all the people all the time’! Nina hakika kuwa watu wa usalama kutoka Rwanda wakaja kugundua mchezo ulioufanya wewe na mpenzi wako, na si wao tu peke yao bali pia The Board nao wakagundua kitu ulichokifanya. Ndio hapo sekeseke lilipoanzia. Watu wa usalama wa Rwanda wanahitaji afisa wao wampate lakini pia nina hakika kuna taarifa muhimu wanaamini anayo ambayo wanahitaji waipate. Lakini pia The Board wamegundua kuna taarifa muhimu mno wanaamini utakuwa nayo na ni taarifa ‘vital’ mno kwao na hii ndio sababu mpaka leo hii upo hai hawajakuua.!”

Nikanyamaza tena kumuangalia. Alikuwa amenikodolea macho haamini ni namna gani nimeweza kuchekecha akili na kung’amua haya ninayomueleza. Sikutaka kumchelewesha, nikaendekea.

“Sasa basi, kama wanavyosema watu.. Mapenzi ni upofu, mapenzi yanatia ukichaa ndicho hicho ninachokiona kati yenu wewe na Veronica! Veronica akaamua kuwasaliti wanausalama wenzake ili awe na wewe, na wewe ukawasaliti wenzako The Board ili uishi maisha ya furaha na Veronica. Ndio sababu kwanini ulikiri mahakamani kuwa umemuua. Ulikuwa unaogopa kuwa mtaani baada ya tukio lile kutokea. Nina hakika The Board walimuhonga Jaji ili asikutie hatiani uachiliwe urudi uraiani ambapo wenyewe wanajua ni namna gani wataipata hiyo taatifa uliyo nayo. Kwahiyo kabla kesi haijaenda mbali sana ukaamua ukiri kuwa ulimuua ili kumnyima nafasi Jaji asikuachie huru mwisho wa kesi. Kwa hiyo Jaji ambaye nina hakika labda alikuwa anatumiwa na The Board licha ya kutamani kukuachia huru urudi uraiani ambapo The Board wanakusubiri wakudhibiti, ikabidi akupe kifungo chepesi cha miaka saba tu kwa hukumu ya kuua bila kukusudia”

Nikanyamaza tena na kumkazia macho.

“Umeongea maneno mengi bado haujaniambia point ni nini dogo?” Akaniuliza kwa hasira.

“My point is. Kwa hii hukumu yako ya miaka saba gerezani, tukiondoa ‘remission’ ya magereza maana yake unatumikia kama miaka minne na nusu pekee, na ukizingatia umeshakaa karibia miaka miwili na nusu that means umebakisha miaka miwili pekee urudi uraiani. Najua wewe ni mtu makini lazima umeshaweka mipango ni namna gani utawaepuka The Board ukiachiwa baada ya miaka miwili. Sasa unaonaje nikifanya figisu ushtakiwe upya kwa kosa la ule mwili uliouchoma moto safari hii iwe kesi halisi kabisa ya kuua na ulimwengu mzima ujue udanganyifu mlioufanya wewe na Veronica wako? Na amini mahakama safari hii itakusweka humu miaka mingi uozee humu humu maisha yako yote huyo veronica uwe unamuona kwenye ndoto pekee badala ya miaka miwili kutoka sasa?”

Kama kawaida nikanyamaza ili nione reaction yake. Alikuwa ameng’ata midomo kwa hasira. Maneno yangu yalikuwa yanamgusa penyewe kabisa. Sikumchelewesha tena, nikaendelea.

“Kama hiyo haitoshi, unaonaje nikiwamegea siri Usala wa Taifa au The Board kuhusu mahali Veronica alipojificha? Naomba nikuhakikishie kuwa kama unavyoona nywele zako zilivvyo karibu karibu ndivyo nilivyo close kufahamu Veronica alipo” nikampiga mkwara.

“Wenzako watu wa Usalama na The Board, mwaka wa pili wanakimbiza kivuli tu hawajui Veronica yuko wapi” akaongea kwa hasira.

“Well, mimi sio Usalama au The Board, mimi ni Rweyemamu Charles Kajuna!! Na kama nilovyomuonya yule jamaa niliyekwambia shuleni Tambaza, nakuambia na wewe na wala sikupi wiki au siku tatu, nakupa chance sasa hivi! Nieleze ninachokubembeleza siku zote hizi.. La sivyo help me God, usinilaumu kwa nitakacho kifanya” nikaongea kwa hasira nimemkazia macho huku nimemsogelea karibi pua zigusane.

Kaburu akashusha pumzi na kisha kuanza kuongea.

“He was right you know!”

“Who was right?” Nikamuuliza kwa kukereka.

“Dr. Shirima! He was right!” Akaongea.

“Right about what??” Nikamuuliza kwa hasira nikiona kama anataka kuhamisha magoli.

“Miaka mitatu kama na nusu hivi iliyopita nilikuwepo kwenye kikao ambacho alipendekeza kuwa tumuingize kwenye michakato yetu mwanafunzi wake anayeitwa Rweyemamu Charles Kajuna. Nakumbuka namna ambavyo alikuwa anasifia. Kuwa ni kijana genius na persistent! Kwamba unapontential hata tunaweza kukutengeneza ukawa kiongozi mzito huko mbeleni. Nilipokuja kupewa file lako na kulisoma nilikuwa impressed sana na ni moja ya watu ambao waliunga mkono pendekezo la Dr. Shirima kuwa tukuingize kwenye michakato yetu! Kijana genius ma persistent!”

Kaburu akaongea huku kwa kiasi fulani akiwa ana maanisha anachokisema na kuna kiasi Fulani alikuwa ananiinjoi.

“Thank you for your vote of confidence” nikamjibu kwa kumuinjoi pia.

“Except for one thing kijana! Kuwa king’ang’anizi kwenye maisha ni asset na pia ni liability.! Ni asset pale tu unapokuwa king’ang’anizi kwenye jambo sahihi na ni liability pale unapokuwa king’ang’anizi kwenye jambo lisilo sahihi. Na kwenye hili hauko sahihi kijana.. No one can take down The Board! No one”

Akaongea huku amenikazia macho.

“Don’t worry about that! I will take my chances.. Hilo halikuhusu kabisa! Just tell what I want to know” nikamjibu kwa hasira nimiona kama anazunguka mbuyu tu.

“Ok! Nahitaji unisaidie kutoroka humu gerezani!” Akaongea akinikazia macho.

“What?” Nikamuuliza kwa mshangao.

“Nahitaji unisaidie kutoroka gerezani! Nataka uchekeche hizo akili zako kama unavyojigamba.”

“Ok! Na unaweza kuniambia kwanini unataka kutoroka” nikamuukiza tena kwa mshangao.

“Humu sio mahali Salama tena kwangu, umeshaharibu kila kitu. Huo utaratibu tu aliouweka Mkuu wa gereza kuwa kuanzia jumatatu nianze kwenda shamba mi hatari kwa usalama wangu.. Na si hivyo tu! The Board wanajua uwezo wako wa kupanga mipango na ulivyo king’ang’anizi, wakihisi tu kuwa naweza kukupa taarifa muhimu nakuapia kwa Mungu watatumaliza wote wawili ili waondoe udhia once and for all”

Kaburu akaongea huku nikihisi hofu iliyokuwa kwenye sauti yake.

“Ok! Nitafikiria hilo but first things first.. Naomba info ninazozitaka kwanza” nikamkazia macho.

“Ok! Unapaswa kufahamu kuwa ndani ya The Board ni watu wawili pekee wanaojua kila kitu kinagaubaga. Hao wawili ndio wanaojua akaunti zote za siri, majina yote ya vibaraka wao serialini, kwenye vyombo vya usalama, majina ya wanachama wote walio hai na waliokufa, na mikakati yote kuanzia wa kwanza mpaka mkakati wa sasa wa 34!!”

Akaongea huku anafumba macho. Nilihisi kuwa alikuwa anajijutia kwa haya mambo anayonieleza.

“Ok! Ni nani hao wawili” nikauliza kwa shauku kubwa.

“Ni chairman na kuna mtu tunamuita The Book Keeper! Chairman huwezi kumpata na wala siwezi kukuambia lakini The Book Keeper una mfahamu vizuri sana” akaongea huku anafumbua macho baada ya kuyafunga alipokuwa anaongea.

Moyo ukaanza kunienda mbio.

“Ni nani?” Nikaukiza kwa shuku kubwa.

“Vincent Mallya” akaongea kwa kifupi huku akifumba tena macho.

“Whaaaaatt!” Nikapigwa na mshangao.

“Yes, Vincent Mallya” akaongea kwa kifupi tu huku bado amefunga macho.

“Vincent Mallya Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRBB??” Nikamuuliza kwa mshangao.

“Yeah! That’s him, ndiye The Book Keeper wa The Board.! Yeye ndiye anatunza kumbukumbu zote za The Board ambazo nimekueleza. Na kumbukumbu hizi haziwekwi kwenye vifaa vya digitali kama computer kuogopa watu kudukua.. Taarifa zote zinahifadhiwa kwenye karatasi na mafaili na yapo mahali yamehifadhiwa ambapo naweza kukuelekeza ukaenda kuyachukua kama unaokota dodo kwenye mwembe, but first inabidi unitoroshe humu gerezani.” akaongea akiwa amenikazia macho kweli kweli.

Moyo ulienda kasi kweli kweli. Nikatafakari karibu vitu mia kwa wakati mmoja. Mbele yangu nimebakiza hatua moja tu nitimize lengo langu la kunileta humu. Lakini hatua yenyewe ni dhahiri ilikuwa ni impossible.

Maneno ya Kaburu yalinishitua sana. Kwanza nilishtushwa na taarifa ya Vincent Mallya kuhusika na kujishughulisha na The Board. Vinncent Mallya alikuwa ni moja ya watanzania wanaoheshimika zaidi hasa kutokana na umahiri wake katika sekta ya kibenki, ambapo aliweza kuikuza kimtaji benki ya CRBB kutoka kuwa Benki ya kawaida tu mpaka kuwa benki inayoongoza nchini kwa huduma za kifedha.

Pamoja na hilo pia, mtihani wa kumtorosha Kaburu kutoka gerezani sio tu kwamba ulikuwa hauwezekani bali pia ulikuwa kama mpango wa ukichaa. Inawezekana vipi mtu kutoroka sehemu inayolindwa kiasi hiki? Hata gereza lenyewe likivyojengwa lilizingatia kwa kiwango kikubwa mtu asiweze kutoroka. Kuta zilikuwa kubwa na ndefu na zenye nyaya za miiba juu yake.

Nikamuangalia tena Kaburu ambaye muda wote alikuwa amesimama tu mbele yangu akiniangalia ninavyoumiza kichwa kuchambua kile alichonieleza.

“..ok! Tuseme kwa mfano nikapata namna ya kukutorosha humu, then what?” Nikamuuliza.

“Nikikanyaga tu salama nje ya hii ngome, nakupa hiyo taarifa na kila mtu anaelekea njia yake!” Akanijibu.

“Nitakuwaje na uhakika kwamba utatimiza hii ahadi unayosema?”

“Well, hakuna namna unaweza kuwa na uhakika, lakini nitatimiza”

“Ok! Let me think about this..” Nikamjibu.

“Na si hilo tu, kuna kitu kingine nahitaji pia”Akaongea huku hata yeye mwenyewe anajishtukia.

“Oooh God, what else? Usije ukasema unataka mikupeleke peponi” nikaongea kwa mzaha wa kumkejeli.

“Kuna nyaraka zangu muhimu nahitaji nizipate mpaka kufikia kesho jioni” akaongea kwa kumaanisha.

“Nyaraka gani? Kutoka wapi?”

“Nahitaji uwasiliane na mtu unayemuamini huko nje, kuna document iko kwenye e-mail nataka ‘aiprint’ kisha adelete kule kwenye e-mail na hizo nakala atakazo print nizipate kesho jioni”

“Hivi tuseme kwa mfano nikapata namna ya kukutorosha humu! Kwanini usisubiri mpaka ukiwa huko nje ili ufanye hiyo kazi mwenyewe?” Nikamuuliza kwa hasira kidogo.

“Nina maana kuzihitaji kesho!” Akanijibu.

“Maana gani?”

“Its non of your business! Au labda tu kwa kifupi nikudokeze, nahitaji hizo nyaraka kabla ya jumatatu kuanza ratiba aliyoisema mkuu wa gereza kwamba nianze kupelekwa shamba”

“Ok! Na hiyo email ni ipi?” Nikamuuliza.

[email protected]

“Password?”

“veronica123100%”

“Wow! Mahaba niweke password hahaha” nikamuinjoi.

“Hahah umekariri?”

“Yeah got it! guy thirteen at gmail dot com, na password ni veronica one, two, three, one hundred percent..!” Nikamjibu huku natabasamu.

“Genius!” Akanisifia kwa kuniinjoi.

“Fu*ck you” nikajisikia tu kumtukana.

“Kesho nahitaji hizo documents Ray! Sio kesho kutwa, sio mtondogoo… Nazihitaji kesho” akaongea kwa msisitizo mkubwa.

“I will do my best” nikamjibu huku nageuka kuondoka eneo hilo.

Kengere ya chakula cha mchana ilikuwa inalia kwahiyo ndani ya dakika chache watu watajaa upande huu wa gereza ili waweze kwenda jikoni kuchukua chakula.

Nikatembea mpaka pale kwenye mlango mkubwa ukutani ambapo kuna mlango wa kwenda yard namba moja na kusubiri.

Kama dakika mbili baadae wafungwa na mahabusu wakaanza kumiminika wakipita hapo kuelekea jikoni.

“We fala ulikuwa wapi muda wote huu nakutafuta?” Godi akaniukiza baada ya kufika hapo mlangoni na kunikuta akiwa anaelekea jikoni.

“Nilivyotoka kuonana na Cheupe nikaenda moja kwa moja kuongea na Kaburu” nikamjibu huku tukiongozana kuelekea jikoni.

“Vipi Kaburu amefunguka hizo info?” Akaukiza kwa shauku.

“Kiasi tu! Kama asilimia hamisini bado asilimia hamsini hajaniambia”

“Na hizo info zilizobakia anakwambia lini?”

“Hata leo hii anaweza kunambia nioitimiza tulichokubaliana”

“Usinambie kuwa anataka umpe tigo hahahahah!!” Akaongea kwa mzaha na kuanza kucheka.

“Mseng* wewe!! Bora hata angetaka tigo ninhekuja kukushawishi umpe.. Anachokitaka hata hakiwezekani!!” Nikamjibu pia kwa mizaha.

“Anataka nini?” Akaniuliza akiwa ameacha kucheka sasa.

Nikamsogelea karibu na kumnong’oneza, “anataka nimsaidie kutoroka humu gerezani.”

Godi akapiga mluzi wa mshangao kwa sauti ya chini, “mamaeeeeee! Kazi unayo.. Nasubiri nione huo muujiza wa karne ya ishirini na moja”

Tukapanga foleni na kisha kuelekea jikoni kuchukua chakula.

Zilikuwa ni siku sita pekee tangu miingie humu gerezani lakini moja ya mateso makubwa ilikuwa ni chakula.

Sio kwamba ulikuwa unapewa chakula kidogo au hakuna chakula, hapana bali ilikuwa ni aina ya chakula chenyewe ma ratiba ya kula.

Ratiba ilikuwa kwamba mnakunywa uji saa moja au moja na nusu asubuhi. Baada ya hapo chakula cha mchana mnakula saa nane mchana. Basi siku ndio imeisha. Milo miwili tu. Uji saa moja asibuhi na chakula mchana saa nane.

Pia chakula chenyewe kilikuwa ni mtihani mwingine. Lilikuwa ni dona lakini ni dona ambalo sikuwahi kuliona maishani mwangu mwote na wala sikufikiria kuna dona la dizaini hii.

Dona lilikuwa na rangi fulani hivi kama njano lakini imechanganyika na rangi nyeusi. Mwanzoni nilipoingia gerezani niliuliza labda yawezekana wanatumia mahindi ya njano ambayo wazee wetu wanatusimulia kuwa yalikuwa yanagaiwa kipindi cha njaa enzi za nyerere? Nikaambiwa sio mahindi ya njano, nj mahindi ya kawaida tu ila ni jinsi hilo dona linavyoandaliwa ndio linafanya kuwa na rangi hiyo.

Nikaelezwa kwamba. Katika usagaji wa hilo dona, yanachukukiwa mfano magunia matatu ya mahindi ambayo hayajakobolewa, kisha yanachanganywa na gunia moja la vibunzi tupu. Yaani vibunzi ambavyo vimeoukuchuliwa hazina mahindi. Kisha vinasagwa pamoja. Ndio unaoatikana ungwa wa dona linalopikwa magereza.

Kinachochosha zaidi ni kwamba dona hili kulila ni kila siku. Kila siku ni dona hili la ajabu na maharage. Na hayo maharage yenyewe yalikuwa ni kiroja kingine.

Unapoenda pale jikoni kuchukua chakula, kuna madirisha makubwa matatu.

Dirisha la kwanza unakabidhiwa “berenge”! Hili ni bakuli kubwa la bati ambalo nahisi kipimo chake unaweza kujaza chakula sahani tatu kutoka kwenye sahani za kawaida.

Ukishachukua berenge, unahamia dirisha la pili ambapo unampa mpishi lile berenge na anakujazia dona mpaka juu.

Kisha unahamia dirisha la tatu ambalo unapewa kikombe cha bati kilichojazwa mboga. Maharagwe.

Kikombe kinakuwa kimejaa “mchuzi” mpaka juu lakini unaweza kuzamisha kiganja kizima cha mkono kuyatafuta maharage na usiyaone. Kuna siku nilipopewa hiki kikombe cha maharage na kurudi yard kula, nikafanya uchizi kidogo! Nikamimina mchuzi wote chini ili niyaone hayo maharage.

Nikayakuta yametuama chini kabisa. Nikayahesabu nikapata punje 12 za maharage. Hiyo ndiyo mboga unayotakiwa kukia dona ulilojaziwa kwenye berenge.

Nikachukua dona langua na tukaondoka na godi kwenda yard kula.


SIKU YA TANO

Ilikuwa jumapili, siku nyingine ya wafungwa na mahabusu kuja kutembelewa na ndugu zao, jamaa na marafiki.

Nilishukuri kwa jinsi Cheupe na Issack walivyokuwa wanakuja mapema sana kuniona. Kama nilivyosema hii ilitupa mwanya wa kuwa peke yetu kwenye chumba cha wageni.

Jina langu lilikuwa limeitwa na sasa ndio nilikuwa nimeingia ndani ya hiki chumba nankukaa chini nikisubiri wageni wangu wakiwa wanakamilisha taratibu za kujiandikisha huko nje ili wapewe ruhusa ya kuingia.

Nilikuwa namsubiri kwa hamu kubwa Cheupe wangu! Walau kumuona tu roho yangu ilikuwa inapata faraja na kunipa nguvu ya kupambana zaidi.

Mara mlango ukafunguliwa na wageni wangu wakaingia! Lakini ajabu ni kwamba hawakuwa wageni, Bali alikuwa ni mgeni.

Nikishikwa na butwaa na mshtuko kwani sikutegemea hili. Dr. Shirima ndiye aliyeingia kwenye hiki chumba.

“Hujambo Ray?” Akanisalimia kwa tabasamu kama kawaida huku anaketi kwenye kiti.

Nilishindwa kumuitikia, nikabaki nimemkodolea macho tu.

“Ulipata Ujumbe wangu?” Akaniuliza baada ya kuketi kwenye kiti.

“Ujumbe gani?” Nikajikuta nimemjibu pasipo mwenyewe kutaka kimjibu.

“Ujumbe wangu kuhush kikao cha kumi na nne, tukutane kwenye makazi ya askofu? Uliupata?” Akaniuliza tena.

“Yes niliupata!” Nikamjibu kwa mkato.

“Kwanini haukutokea?”

“Well, labda kama hujagundua hapa sio Kempiski!! Niko gerezani na siwezi kutoka tu kama naenda sokoni” nikamjibu huku nimekereka kweli kweli.

“Hahaha! Ray, upo gerezani kwa kuwa umetaka kuwa gerezani” akanijibu huku anatabasamu tena. Hili tabasamu lilinikera kweli kweli.

“What do you want??” Nikamuuliza kwa hasira.

“Hahaha! What do i want?? Lets see, haujawahi kukosa kuhudhuria hata kimoja nilichokuita.. Lakini kikao hiki cha 14 haukuja.. So nikahisi labda umechoka kuja ninapokuita.. So nimeona labda itakuwa vyema mimi nikija ulipo” akaongwa kwa kejeli huku anatabasamu.

“Bulksht!! What the fuk do you want?” Nikamuuliza kwa hasira.

“What do I want?? Hahaha, what the fu*k you think you are doing?” Akaniuliza pia kwa hasira. Akaendelea “chochote kile ambacho watu wa Usalama walichokushawishi mpaka ukakubali uwanyie kazi jua kwamba wanakudanganya na kukurubuni”

“I’m not working for anyone! Not you motherfu*ckers, not them” nikajibu kwa hasira mpaka nikasimama kutoka kwenye kiti.

“Then get the hell out! Unanisikia Ray, chochote ulichokipanga kichwani kwako nakupa nafasi kwa mara ya kwanza na ya mwisho.. Get out of here, na ukitoka moja kwa moja nataka uje nilipokuelekeza katika ujembe wa kikao namba 14” akaongea kwa hasira pia huku anasimama.

“Only in you dream dr. I’m done with you guys!” Nikaongea huku naanza kugeuka ili nitoke kwenye hiki chumba.

“Jumatatu italetwa hati ya dharura hapa kwa ajili yako ili upelekwe mahakamani! Ukifika mahakamani kesi itafutwa.. Baada ya hapo nataka uje moja kwa moja ulipoelekezwa kwenye ile karatasi.. Usijifanye shujaa.. Fikiria mara mbili mbili before its too late, huwezi kupambana na The Board!! Watakupoteza.. So acha kuwa mjinga na mbinafsi, Fanya ninachokuambia kwa ajili yako, kama sio kwa ajili yako Fanya kwa ajili ya cheupe, na kama sio Cheupe fanya kwa ajili ya mtoto aliye tumboni kwake”

Nilishikwa na mshtuko, moyo ulinipasuka nusura nidondoke chini.

“Umesemaje??” Niligeuka kutoka mlangoni nilikokuwa naelekea na kumtazama Dr. Shirima usoni na kumuuliza kwa hasira na mshangao.

“Umenisikia vyema tu naamini! Think about it” Dr. Shirima akaongea huku anaondoka kutoka kwenye chumba cha wageni.

Nilibaki nimesimama nimeganda kwa mshangao akili ikizunguka. Ile sentesi ikawa inajirudia kichwani, “fanya kwa ajili ya mtoto aliye tumboni kwake”. Sikuamini masikio na macho yangu. Moyo ulienda mbio kijasho chembemba nikaanza kukisikia kinaanza kunitoka.

“Rweyemamu usitoke una wageni wengine” nikamsikia askari wa mapokezi anaitilia.

Nikaketi chini kwenye kiti. Akili bado ilikuwa inanizunguka. Ile sentesi ya Dr. Shirimanilikuwa inajirudia tena na tena kichwani mwangu. “fanya kwa ajili ya mtoto aliye tumboni mwake”.

Mlango ukafunguliwa na Cheupe na Isaack wakaingia.

“Niaje kichwa?” Issack akanisamia mara baada ya kuingia kwenye chumba cha wageni.

Tukasalimiana na Issack. Kisha nikasalimia na Cheupe.

Baada ya hapo Issack kuna kitu akaanza kunielezea nadhani kuhusu ile akaunti ya Foundation kutoka Australia. Lakini akili yangu yote ilikuwa haifanyi kazi, nilikuwa nafikiria tu ile kauli ya De. Shirima, “fanya kwa ajili ya mtoto aliye tumboni mwake”.

Cheupe alikuwa amekaa lakini kwa namna Fulani hivi nilimuona hakuwa na raha na uchangamfu kama kawaida yake. Na kila nilipomuangalia machoni alikuwa anakwepesha macho.

“Umepanga uniambie lini?” Nikauliza huku namuangalia Cheupe.

“Whaaaatt???” Issack akakatisha alichokuwa anaelezea na kuduwaa.

“Is it true?” Nikauliza tena huku namuangalia Cheupe.

“What is it Ray?” Cheupe akaniuliza huku ameshangaa.

“Are you pregnant?” Nikamuuliza.

Wote wawili wakashtuka ghafla. Wakatoa macho.

“Umejuaje?” Issack akaropoka.

“Haijalishi nimejuaje!! Is it true?” Nikauliza nikiwa na hasira kidogo iliyochanganyika na furaha.

“Aaahh wiki nzima hii Hasnat alikuwa anaumwa umwa na juzi hapa akaanza kutapika tapika na hali ikazidi kidogo.. So usiku tukaenda town hapo hospitali ya Agha Khan na baada ya vipimo vipimo.. ndio ikabainika kuwa ni mjamzito” Issack akaongea huku ana tabasamu.

Nilishikwa na furaha ya ajabu nikatamani niruke nioenye kwenye zile nyavu na kumkumbatia Cheupe.

“Kwanini hamkuniambia toka jana” nikafoka kwa furaha huku nimesimama kutoka kwenye kiti.

“Well, niliona na wewe kuwepo humu gerezani alafu nikupe taarifa za ujauzito naweza kukuchanganya hata mipango unayoipanga akili ikashindwa kutulia nankuifanya” cheupe akaongea kwa woga kiasi Fulani lakini akiwa na furaha.

“Haijalishi niko wapi au nina hali gani, that’s my son lazima unipe taarifa” nikafoka tena kwa furaha..

“Your ‘son’?? Macho yako yana ultra sound au?? How do you know its a boy??” Cheupe akaongea huku anacheka kwa furaha.

“Ok ok ok guys mtapata muda wa kusheherekea.. Let’s get down to business.. Hivi huyo tuliyepishana naye hapo nje si ni Dr. Shirima??” Isaack akauliza kwa mshangao.

“Yes ni yeye! Akikuja kunipiga mikwara” nikamjibu huku nikaa tena kwenye kiti baada ya kuinula kwa furaha.

“Amesemaje?” Cheupe akauliza.

“Akichosema sio muhimu ni mikwara tu” nikamjibu huku najitahidi kuficha uongo wangu wasigundue kuwa nawadanganya. “Kuna jambo la muhimu nataka mlifanye.” Nikaongea kwa utulivu huku nawatazama.

“Jambo gani?” Akaniukiza cheupe.

Nikawaeleza kuhusu ile email ambayo wanatakiwa wakaprint document iliyopo na kisha kudelete hiyo document kwenye email. Na pia nikawaeleza kuwa wanatakiwa document hiyo ifike hapa gerezani leo jioni kabla hatujaenda kulala. Hivyo nilichowaelekeza ni kwamba wakiileta hiyo document hapa magereza wakamkabidhi askari anayeitwa ‘Obama’ na yeye Obama atajua namna gani ya kunifikishia hiyo document kwa siri.

“Kitu kingine ni kwamba nahitaji jumatatu mje mahakamani! Niatapelekwa mahakamani na kuachiwa huru”

“What? Kesi yako si ni tarehe 8 wiki ijayao” akauliza cheupe.

“Yeah, italetwa hati ya dharura kunipeleka mahakamani.. Nahitaji muwepo.. Msiumizw kichwa nini kinaendelea, I just want you to be there! Sawa?”

Nikamuangalia Cheupe.

“Honey, nahitaji use strong mama’ngu.. We are very close kulimakiza hili.. Tafadhali sana mama be strong for me and for our baby” nikaongea kwa hisia Kali huku nimemkazia macho Cheupe.

“Najitahidi baba! But am really scared” Cheupe akaongea huku vimachozi vinamlenga lenga kwa mbali.

“Cheupe unakumbuka ile stori niliyokwambia kipindi tuko sekondari mzew wako alipotaka kukufukuza kwasababu ya kuwa na uhusiano na mimi?” Nikauliza kwa hisia.

“Yes nakumbuka” Cheupe akaongea huku machozi yanamtoka taratibu.

“Tell me that story”

“Ray noooo! Pleaseee” Cheupe akalia zaidi.

“Please naomba unambie ile srori” nikajikuta kwa mbali machozi yananikaribia kutoka.

Cheupe akafumba macho kwa hisia na kuyafumbua kisha akaanza kusimulia.

“Uliniambia kuwa kulikuwa na panya wawili wametumbukia kwenye glasi ya maziwa.. Baada ya kutumbukia wakaanza kutapa tapa kwa kupiga piga miguu ili wasizame chini.. Wakafanya hivyo kwa karibia dakika kumi nzima.. Panya mmoja akamwambia mwenzake kuwa hakuna point ya kupiga piga miguu hivyo kwasababu mwisho wa siku watachoka na watazama na kufa.. Hivyo ni bora tu wafe kwa amani bila kutapa tapa.. Yule panya mmoja akaacha kupiga piga miguu na akazama kwenye glasi na kufa.. Lakini yule panya mwingine akaendelea kupiga piga miguu na kutapa tapa ili asizame… Akafanya hivyo kwa dakika kumi nyingine kwa maumivu makubwa kwa kuwa alikuwa amechoka sana..

ingawa yule panya alikuwa hajui ila ni kwamba maziwa yakikaa yametulia muda mrefu na ukaanza kuyatingisha kwa nguvu ghafla yanatengeneza margarine.. Yani mabonge mabonge ya siagi.. Kwa hiyo baada ya muda kadiri yule panya alivyo tapa tapa na kupiga piga miguu, maziwa yalitengeneza mabonge mabonge ya margarine na hatimaye yule panya akayatumia kuyakanyaga juu yake na kutoka kwenye glasi na kuendelea na maisha, akiwa hai na salama”

Cheupe akieleza kwa ufasaha kabisa hadithi ya kumtia moyo niliyomweleza miaka mingi sana iliyopita tukiwa wanafunzi wa sekondari.

“That’s the spirit honey! We don’t ever give up.. Please stay strong for me.. Karibia tunalimaza hili.. Stay strong please”

Nikaongea kwa hisia kubwa na Cheupe wangu.

“Yes! Honey I will do that.. for us and and for this baby” Cheupe akaongea huku anapapasa tumbo lake.

Baada ya hapo tukaagana na wakaondoka. Nikatoka mle ndani nikiwa na nguvu mpya na usongo zaidi. Kwamba sasa napaswa kupambana si kwa ajili ya baba yake Cheupe tu, au kwa ajili ya Cheupe tu bali napaswa kupambana kwa ajili ya mwanangu.

Tayari ilikuwa inakaribia majira ya saa tisa alasiri, tulikuwa tumeshamaliza kula chakula na muda huu nilikuwa natoka katika ofisi ambapo niliitwa na yule askari wanayemuita Obama.

Asubuhi ya siku hii nilipo maliza kuongea na wageni wangu, Cheupe na Hasnat nilirejea yard kumcheki Godi nikoongea naye mawili matatu na kumpa mrejesho juu juu pasipo kuingia kwa undani sana kuhusu nilichoongea na Isack na Cheupe kisha baada ya hapo tukaanza kusubiri kuona kama Hasnat na Isack watafanikisha kuleta document ambayo Kaburu alikuwa anaitaka ziletwe kwake kabla ya siku hii kuisha.

Cheupe na Issac hawakuniangusha, kwani majira ya kama saa nane na nusu mara tu baada ya kumaliza kula chakula, nikaitwa ofisini na Obama, kisha akanikabidhi hizo document zikiwa kwenye bahasha ya kaki, nikazisweka ndani ya suruali na ndio sasa nilikuwa natoka ofisini kwake kuelekea yard.

Baada ya kufika yard nikamtaarifu Godi kuwa niliitwa kwenda kuchukua documents na ndio sasa natakiwa nifanye mpango kumkabidhi Kaburu.

Kwahiyo Godi akaenda moja kwa moja mpaka yard namba moja ambako Kaburu alikuwa amepumzika na kumtaarifu kuwa nataka nionane nae.

Mimi nikatangulia mpaka pale uchochoroni panapo unganisha yard ya kwanza na ya pili.

Dakika kama tatu baadae Kaburu akafika akiwa anatembea kwa kuchechemea. Inaonyesha bado alikuwa na maumivu ya virungu vya juzi.

“Umefanikisha?” Akaniuliza kwa sauti ya chini mara baada kufika kwenye uchochoro.

Sikusema chochote. Nikaingiza mkono ndani ya suruali na kuibuka na bahasha ya kaki.

“Hizi hapa” nikaongea huku nimezigandamiza document kifuani kwake. “Nadhani sasa tumebakisha suala moja tu”

“Umeshapata wazo unanitoaje humu” akaongea huku anazisweka ndani ya suruali yake haraka haraka zile documents.

“Nina wazo, ila ni wazo nusu tu! Nadhani mpaka kesho asubuhi naweza kuwa nimepata wazo kamili.!” Nikaongea huku nageuka kuondoka kwenye uchochoro.

“You better come up with something fast, la sivyo wote sidhani kama tutamaliza wiki tukiwa hai” akongea huku naye akigeuka kutoka uchochoroni.

Nikoaondoka kutoka pale uchochoroni na kurejea yard huku kichwani napiga mahesabu makali sana. Ni namna gani naweza kumtorosha mfungwa kutoka gerezani?? Hivi vitu nimekuwa naviona kwenye sinema tu lakini sasa natakiwa nivifanye mimi kwenye maisha halisi.

Katika sinema mara zote watu wanaotoroka ufanya hivyo kwa urahisi sana au tuseme kwa ujanja ambao unahusisha matukio machache tu kisha anafanikiwa kutoroka.

Lakini kila nikiangalia ulinzi wa hii jela, ambapo hapa yard kwenyewe , kila yard ina maaskari wanne wa doria.. Wawili wanakaa nyuma mwishoni kabisa kwenye yard na wawili wanakaa mbele ya yard.

Pia nikiangalia jinsi zile kuta zilizozunguka gereza jinsi zilivyokuwa ndefu, pia nyuma ya hizi kuta huko nje kila upande una askari wawili wenye silaha wanaofanya doria.

Pasina shaka, suala hili lilikuwa haliwezekani.

Lakini siku zote katika maisha hakuishi kuwa na vitendawili vinavyotutaka tufanye yasiyowezekana ii tuendelee kuishi au kupata tunavyovihitaji.

Mara zote katika maisha unatakiwa utende miujiza ili ufike pale unapopataka.

Watu wamekariri katika akili zao kuwa, miujiza ni labda kupaa juu angani, labda kutembea juu ya maji, au labda kumfanya mfu afufuke au kubadilisha karatasi kuwa hela.

Na ndio maana wamejaa wahubiri wenye kujigamba kutenda miujiza, kufanya viwete watembee, viziwi wasikie na mabubu kuongea. Na ajabu zaidi sasa wameanza kuibuka “mashehe” wenye kujigamba kuwa nao wanafanya dua ili kutoa watu “majini” yaliomo ndani yao, kuleta bahati, kupata Mali na kuponya magonjwa.

Binafsi, kama Rweyemamu ni mkristo safi kabisa na mwenye kuamini katika Mungu na kuijua imani yangu.

Lakini mara zote haijalishi niko mahali gani nimekuwa nikijizuia kuchangia mijadala kuhusu dini na imani kwa sababu imani maoni yangu ni tofauti kabisa na watu wengi.

Maisha yangu yote nimekuwa na mtazamo tofauti kabisa na hivi vitu watu wanavyoviona kuwa ni miujiza. Binafsi sivioni kama miujiza bali naviona kama mazingaombwe. Yes, ni mazingaombwe sio miujiza.

Miujiza ni mfano wa mama mjane anayekaa uswahilini kabisa. Anaishi kwa kupika maandazi au chapati.. Lakini anamudu kuwalisha watoto wake watatu au wanne milo yote mitatu kila siku.. Anamudu kuwanunulia sare za shule na mahitaji mengine na bado anamudu kuwalipia watoto wake ada ya shule na anafanya jukumu hilo kwa miaka kibao mpaka watoto wake wanafika Chuo kikuu.

Hiyo ndio mijuiza.

Miujiza ni pale ambapo kijana Charles Odhiambo, mtoto yatima wa mitaani nchini Kenya anaanzisha biashara yake ya kuuza maji ya kufunga ambayo tunaita jina la utani “dripu”, na anaifanya biashara hiyo kwa mwaka mzima akitunza faida yake kiduchu kidogo kidogo. Kisha anajifunza namna ya kufanya purification ya maji ya mvua na kuyasindika kwenye chupa.

Anachukua faida yake kiduchu akiyoitunza mwaka mzima na kununua chupa kadhaa za kusindikia kutoka “SIDO” na kimashine kidogo cha kusafisha maji.

Miaka mitatu baadae kijana huyu biashara yake hii ya kuuza maji imekuwa kubwa na kuwa kampuni inayoitwa “Sky Drop” ambayo hatimaye inapata uwekezaji wa dola laki tatu kutoka kampuni nyingine ya usindikaji maji kutoka Ulaya na kumfanya kijana Charles Odhiambo mwenye miaka 23 tu kutoka kuwa mtoto wa mitaani na kuwa moja ya vijana waliofanikiwa zaidi barani Afrika.

Hiyo ndiyo miujiza.

Miujiza ni mfano wa rafiki yangu mwanadada maarufu mjini Morogoro kwa jina la “Mama Halima”, baada ya kufanya kazi za ndani kwa miaka mingi, hatimaye anapata “bahati” ya kuolewa. Licha ya kuolewa na mwanaume mwenye kipato cha chini kabisa lakini mme wake huyo anampa mtaji wa shilingi elfu hamsini ili afanyie biashara aipendayo. Anachukua elfu hamsini hiyo na kuunganisha na akiba yake ya elfu ishirini na kuwa elfu sabini na kisha ananunua cherehani na kuanza kujifunza kushona.

Leo hii miaka takribani saba baadae, dada huyu ndiye “Top Designer” kwenye mji wa Morogoro akimiliki ‘brand’ kubwa na maarufu inayojilukana kama “Mama Halima Collections”

Hiyo ndiyo miujiza. Sio mazingaombwe tunayoaminishwa kwenye vipindi vya televisheni na watu wenye kujigamba kuwa wao pekee ndio wamejaliwa “vipawa” vya kufanya miujiza.

Mungu alipotuumba sote, aliweka uwezo wa ajabu wa kutenda makubwa ambayo hayaelezeki kwa akili ya kawaida.

Nikageuka huku na huko kuangalia pale yard. Nikawaangalia wale maaskari wa doria walioko mbele ya yard na nyuma. Nikaangalia zile kuta ndefu za kutisha zilizo zunguka yard. Hakika nilichokuwa nataka kukofanya kilikuwa hakiwezekani.

Nikavuka pumzi ndefu ndani na kuitoa nje. “Natakiwa kufanya muujiza”, nikaiambia nafsi yangu. Hakuna namna nyingine kama nataka kilichonileta humu gerezani kikamilike, basi sina budi kuchekecha akili na kufanya kile kisichowezekana.

Na natakiwa nifanye hivyo sio kwasababu yangu na cheupe tu, au baba yake cheupe tu, hapana! Natakiwa nifanikishe kisichowezekana kwa sababu ya mwanangu.

“Kaba seloooooooooooooo”

Nilishtushwa kutoka katika dimbwi la haya mawazo na mipango kichwani mwangu, na sauti ya nyapala akitangaza muda wa kulala.

“Oiii” kuna mtu akiniita nyuma yangu.

Alikuwa ni Godi anakuja pale nilipokuwa nimesimama.

“Siamini kama unapanga kile ukichinieleza Jana” akaongea huku tunaongozana kuondoka hapo yard kuelekea selo.

“Kitu gani?” Nikamuuliza.

“Nimekuona muda mrefu tu umesimama anaangalia kila kona ya yard na kila upande wa ukuta unazunguka ‘ngome’. Nina hakika ulikuwa kichwani unapanga kuhusu kumtorosha Kaburu” akaongea kwa sauti ya chini.

“Yeah! Sina jinsi.. Inabidj nifanye hivyo” nikamjibu.

“Haahaha! Sijawahi kusikia mtu ametoroka hii ngome.. Dah nasubiri nione hiyo miujiza aisee” akaongea kwa mzaha huku anacheka.

“Yeah! Uko sahihi kabisa.. Utakuwa ni muujiza” nikajibu kwa kutabasamu nikikumbuka kuwa na muda mchache tu nilikuwa nawaza kuhusu miujiza.

“Alafu unakumbuka kuwa tunadaiwa shilingi elfu kumi na deadline ilikuwa leo na hatujalipa!! Sijui tutambebea mbeleko gani yule nyapara kesho..” Godi akaongea huku anashusha pumzi kwa kuogopa hicho kitakachotukuta kesho.

“Usijali! Hiyo pia ni fursa kwenye mpango wangu” nikamueleze huku natabasamu lakini nikimaanisha ninachomueleza.

“Nini?” Akaniuliza kwa mshangao.

“Subiri utaona” nikamjibu kwa kifupi tu.

Tulikuwa tumeshafika nje ya selo. Tukavua mashati na kuchuchumaa kusubiri kuhesbabiwa na kuingia kwenda kulala. Siku ilikuwa imeisha.


SIKU YA SITA

Licha ya siku hii kuwa naitegemea kugubikwa na sinto fahamu nyingi, lakini ilikuwa imeanza kwa uchangamfu mkubwa. Labda ni kutokana na haya mazoezi ya asubuhi, na hapa ndipo naemdelea kusema na kuamini huyu aliyebuni utaratibu wa mazoezi kila asubuhi gerezani alifikiria kwa ufahamu wa sita.

Yule afande mwingine alikuwa amemaliza kutuimbisha nyimbo za halaiki.. Sasa ulikuwa umewadia muda pendwa wa Msauzi kuimbisha nyimbo za “kihuni”.

Ile kupanda tu pale juu kwenye kibaraza, wafungwa kama kawaidawakaanza kushangilia na kupiga miluzi.

“Wiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii”

“Waaaaaaaaaaaaaaaa” wafungwa wakaitikia.

“Wiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii” akasalimia tena.

“Waaaaaaaaaaaaaaa”

Akarudia hivyo karibu mara tano, kisha akaanza kuimbisha.

“Nenda kalitoeeeeee nenda kalitoeeeeee”

“Kama ulitaki hill busha nenda kalitoeeeeeeeeeee” wafungwa wakaitikia kwa makelele na furaha.

“Nenda kalito, nenda kalito, nenda kalitoeeeeeee”

“Kama hutaki hilo busha nenda kaliyoeeeeeeee”

Wafungwa walichangamka kweli kweli. Wanajinwaya mwaya utadhani wako kwenye klabu ya usiku.

Msauzi sijui alikuwa amekula nini leo, maana akatubadilishia “gia angani” akaanza kutuimbisha nyimbo za ‘Kiluguru’. Lakini hii haikufanya wafungwa waacje kujimwaya mwaya na kuimba kwa furaha.

“Lidomo fulemu mijino biasharaaaa” akaanzisha nyimbo.

“Oooooohh tumalize kesi mamaaaaaaa” wafungwa wakaitikia kwa furaha na kwa sauti ya juu.

“Nunu nunu nunu nunu nunuuuuuu”

“Oyaaaaaaaaaaaa”

“Unamnunia nani?”

“Oyaaaaaaaaaaaaa.!”

“Kamnunie mkeo!”

“Oyaaaaaaaaaaaaa”

“Aliyekuleta jelaaaaaaaa”

“Oyaaaaaaaaaaaaaa”

Alafu anaanza tena kuanzia mwanzo wa wimbo.

“Lidomo fulemu mijino biasharaaaaaa”

“Oooooooo tumalize kesi mamaaaaaa” wafungwa kama kawaida wakashangilia na kuimba.

Nyimbo zikaimbwa na watu wakafurahi.

Leo hii ndio siku ambayo Dr. Shirima alinieleza kuwa italetwa hati ya dharura ya kunihitajo mahakamani, ambako alidai kuwa kesi itafutwa na alitaka niende moja kwa moja kwenye makazi ya askofu kuonana naye.

Utaratibu wa hapa magereza nimba, mkimaliza kunywa uji kila siku.. Anapita askari magereza kwenye yard zote mbili ambapo, anasoma majina ya mahabusu ambao wanatakiwa kwenda mahakamani siku hiyo kusikiliza kesi zao.

Baada ya kunywa uji, askari alipita na kuita majina ya wanaotakiwa mahakamani siku hiyo.. Ni kweli jina language lilikuwepo pamoja na wemzangu wengine wanne.

“Daaaahh kwahiyo kuna uwezekano usirudi humu mwanangu!” Godi akaniluza huku ananiangalia kijicho cha wivu.

“Yeah! Nadhani sitarudi humu” nikamjibu.

“Naamini hautasahau ishu yangu” akaongea huku amenikata kijicho cha wasiwasi.

“Siwezi kusahahu aisee! Uzuri ishu yako ni simple.. Unahitaji wadhamini tu.. Nitakutafutia wadhamini”

“Ma ukumbuke nataka wadhamini wa…..”

Nikamkatisha kabla hajamaliza sentesi.

“Yeah yeah nakumbuka yote hayo.. Unataka wadhamini wa kijiwe cha stendi cha chamwino.. Nikawalipe hela wao wana vitambulisho bandia na hizi ndio Mishe zao zinawaweka mjini, wanajua wafanyaje kuweka picha za uongo kwenye hati za dhamana na blah blah nyingine.. So unataka hivyo ili ukitoka ukimbie kesi usionekane tena..! Nakumbuka vyote hivyo don’t worry”

Nikamjibu kwa kirefu kumuelezea ili abaki na amani kuwa nakumbuka tulichokubaliana.

“And nakukumbushwa kuwa tunadaiwa elfu kumi na Nyapara.. Sijui inanichaje humu.. Sitaki kuoleqa kwa lazima”

“Nimekwambia toka jana kuwa hiyo ni fursa nataka kuitumia ili kufanikisha ishu ya Kaburu”

“Mwanangu umeanza kuvuta bangi humi jela au?? Tangu lini deni likawa fursa ya kumtorosha mtu jela” akang’aka huku akoongea kipande cha mwisho cha sentesi kwa sauti ya chini.

“Tuliza mshono Dogo, utaona na utaelewa” nikamjibu huku naanza kuinuka. “Naenda kumcheki Kaburu kuna maagizo nataka kumpa kabla sijaondoka”

“Kilala heri jini mipango hahahahah” akaongea kwa mzaha na kuanza kunicheka.

Sikumjibu chochote, nikageuka nikamuonyesha kidole cha kati na kuondoka. Hakina jela ilishaanza kunikaa kwenye damu. Sikumbuki ni lini mara ya mwisho nilimnyooshea mtu kidole cha kati.

Nilipofika kwenye uchochoro wa kuelekea yard namba moja nikakutana na Kaburu anatembea haraka haraka kuja yard namba mbili.

“Unajifanya mjanja sana sio” kaburu alifoka baada ya kuniona. Mkononi alikuwa ameshika ile bahaasha ya kaki niliyompa jana.

“Ujanja wa nini?” Nikauliza huku nimeduwaa.

“Hiki nini?” akaongea kwa mkato huku ananionyesha bahasha aliyoishika mkononi.

“Hiyo imefanyaje” nikauliza nikiwa bado nimeduwaa.

“Hizi documents sio zenyewe” akaongea huku akitoa kwa hasira karatasi kutoka kwenye bahasha na kuniwekea mkononi mwangu kwa hasira.

Nikapepesa macho kwenye zile karatasi, kisha nikamuangalia tena Kaburu.

“Sielewi unanichanganya ujue” nikaongea kwa mshangao mkubwa.

“Dogo usinifanye mimi mpumbavu, hizi documents umenibadilishia, hiki sicho kilichopo kwenye email nilichokwambia watu wako wakaprint na kuniletea” Kaburu akaongea kwa hasira nusura aanze kunikunja shati.

“Hey, wait.. hebu kuwa mtulivu kidogo! Mimi nikubadilishie hizo documents alafu nizifanyie nini?”

“Basi ni hao wenzako wamezibadilisha”

“No way! Hawawezi kufanya hivyo”

“Kama wewe haujabadilisha na wenzako hawajabadilisha, ni nani aliyezibadilisha na ziko wapi?” kaburu akaongea kqa hasira huku anahema.

Taa ikawaka kichwa. Shiiiiit!!

Hizi documents zimepita kwenye mikono mitatu kabla ya kumfikia Kaburu. Zimepita kwangu, kwa kina Cheupe na kwa Obama ambaye alikabidhiwa anipe mimi kwa siri.

Mimi sikubadilisha hizi documents, na nina hakika Cheupe na issack hawakuwa na sababu ya kubadilisha, kwahiyo dhahiri aliyebadilisha atakuwa ni Obama.

“Oooohh shiiiiitt.! No no no noooo.” Nikalalamika na kufumba macho, mwili ukakosa nguvu nilitamani nikae chini.

“Whaaaatt!” Kabutu akauliza kwa kukereka na hasira.

“Obama ndiye amebadilisha!” Nikamwambia kwa kifupi.

“What?? Obama anahusikaje kwenye hili?” Akauliza tena kwa hasira.

“Yeye ndiye alipewa bahasha na watu wangu ili aniletee” nikamfafanulia.

“Na kwanini abadilishe??” Kaburu akauliza.

Ilinibidi nikae chini ili nisidondoke kutokana na mshtuko nilioupata. Hapa ndipo nikang’amua kosa kubwa nililolifanya, na kosa hili nilianza kulifanya tangu siku nne zilizopita.

SIKU NNE ZILIZOPOTA (ALHAMISI)

Nilikuwa nimeondoka yard namba mbili na kumuacha Godi kwa kumpa maagizo kuwa ahakikishe sinyorita yuko karibu nikitoka hukj kwenye ofisi ya magereza ili niweze kuongea naye.

Mpango niliokuwa nao kichwani kuhusu namna nitakavyo fanikisha kumuondoa Kaburu kutoka kushinda ofisini kwa mkuu wa gereza na aanze kushinda yard, mpango huu ulokuwa unahitaji wahusika kadhaa na mmoja wao nilimlenga Sinyorita. Lakini pia nilikuwa nahitaji msaada wa askari yule mstaarabu wanayemuita Obama.

Nilikuwa nimefika upande huu wa gereza wenye jiko ambao unaungana na maofisi. Kwenye mlango wa kutoka hapa kuelekea kwenye maofisi kulikuwa na askari wa doria.

“We mseng* unafanya nini huku?” Yule askari akaniuliza baadabya kuniona.

“Nimekuja kumuona Obama ameniita” nikamdanganya.

“Subiri hapo hapo” akaongea huku anaingia ndani kule kwenye maofisi.

Dakika mbili baadae akarejea.

“Ingia… Si unajua ofisi yake ilipo?” Akaniuliza akiniruhusu kuingia kule kwenye maofisi.

“Yeah najua”

Kama dakika moja baadae nikawa mbele ya ofisi ya Obama. Nikagonga mlango na akaniruhusu niingie.

“Wow! Hahah, nilijua lazima iko Siku utaniomba msaada kuhusu jambo lolote humu gerezani lakini sikudhani kama itakuwa haraka hivi.. Karibu uketi” akaongea huku ana tabasamu kama kawaida yake.

Nikaketi. Sikusema chochote mpaka mda huu. Kichwani nilikuwa natafakari ni namna gani niongee kile nilichokuja kuomba msaada hapa.

“Sijui nikusaidie nini Ray” akaongea kwa utulivu akinitazama.

Nikajisemea rohoni liwalo na liwe. Kama nitakuwa ‘wrong’ katika hisia zangu jinsi nilivyohisi basi na iwe hivyo. Ni bora kujaribu kuliko kutojaribu kabisa.

Nilitafakari ni namna gani nifungue maongezi yangu na Obama ili walau anipe nafasi ya haya mawazo ya ajabu niliyokuwa nayo kichwa ayasikilize.

“Unakumbuka siku ya kwanza nilipokuja humu?” Nikafungua maongezi kwa swali.

“Umekuja juzi tu hapa Ray, nakumbuka kila kitu mpaka jina lako nakumbuka” akanijibu kwa utulivu.

“Ulisema kwamba ‘asset yeyote inapaswa kulindwa’! Unakumbuka?” Nikamuuliza tena.

“Unataka nini Ray?” Akaongea na kubadilika na kuwa ‘serious’.

“Well tusema sasa ndio umefika wakati wa kuilinda ‘asset'”. Nikaongea kwa mafumbo nikiamini kuwa kama Obama alikuwa ni mtu ninayemfikiria kuwa ndiye basi atanielewa.

Hisia zangu zilikuwa zinaniambia kuwa Obama alikuwa ni kibaraka au tuseme ni afisa ambaye anatumiwa na Idara ya Usalama wa Taifa kuwapa taarifa wanazozihitaji kutoka humu gerezani. Hisia hii niliipata baada ya siku yangu ya kwanza humu gerezani, Obama alipotamka sentesi inayofanana kabisa iliyotamkwa na baba bite dakika chache kabla sijaletwa gerezani. “asset inapaswa kulindwa.”

Na kwakuwa baba bite alionyesha dalili ya kwamba Usalama wa Taifa wana nia ya kunilinda humu gerezani basi nilikuwa na imani kama niko sahihi Obama ni pandikizi la usalama wa taifa, basi atakubali kunisaidia.

“Nakusikiliza!” Obama akanijibu tena akiwa na uso mkavu.

“Nahitaji funguo ya selo namba 46” nikaongea kwa uso mkavu.

“What?” Akaniuliza kwa mshangao.

“Nahitaji funguo ya selo namba 46! Selo ya Blaki” nikamueleza tena usoni nikiwa mkavu kweli kweli.

“Ya nini?” Akaniuliza huku bado akiwa na mshangao.

“Well, nadhani jambo la muhimu unalopaswa kufanya ni ‘kukinda asset’, hayo mengine niachie mimi!” Nikaongea kwa kujiamini sana kwa kuwa sasa nilikuwa naamini Obama ni pandikizi la Usalama wa Taifa hapa magereza.

“Ok! Hicho kitu unachokihitaji ni kitu sensitive sana kwahiyo angalau ungenieleza unakihitaji kwa ajili gani?”

“Na kwa Bahati mbaya hicho sicho pekee ninachohitaji.!!”

“Kuna lingine tena??” Akaniuliza kwa mshangao zaidi.

“Yes! Nahitaji umruhusu Msauzi aingize mzigo mkubwa wa bangi weekend hii.!!”

“Whaaaaaaaaa???” Obama alishtuka mpaka anainuka kutoka kwenye kiti.

“Siku kadhaa zijazo demand ya bangi humu jela itakuwa kubwa sana kwasababu kesho kuna kiasi kikubwa cha bangi kitateketea!! Kwahiyo ni fursa kwa Msauzi kufanya biashara wiki hii na kina blaki… Na kabla hujaniuliza chochote! Niseme kwamba, kwa siku hizi kadhaa ambazo nimekuwa ndani ya hili gereza nimejaribu kusoma vitu kadhaa humu! Bangi inapatikana kwa wingi sana, humu ndani ni mtu tu kuwa na hela ya kununulia au vipande vya sabuni.. Kwa upatikanaji huu kwa wingi wa bangi ni lazima kutakuwa na askari ambaye anafanya mchongo na blaki! Mzigo wa bangi ni wa huyo askari, lakini blaki kazi yake ni kuwauzia wafungwa.! Sasa ukiniuliza nifanye a wild guess ni askari gani anayeingiza humu bangi, basi nitakujibu ni Msauzi.. Yeye ndiye askari pekee mwenye personality na connection na wafungwa kumuwezesha kufanya hiyo biashara!”

Nikamdadavulia kwa kujiamini kabisa.

“Na tuseme kwa mfano nikapata namna ya kumsaidia Msauzi kuingiza bangi humu!! Sisi tunanufaikaje?” Akaniuliza.

Kwanza nikapenda akivyotumia neno “sisi”. Nikahisi somo limeanza kumuingia.

“Nahitahi kesho umpange lindo la hapa jikoni muda wa mchana, na umpe maagizo afanye kile nitakachomuelekeza” nikamjibu kwa ufupi tu.

Obama akaitingishwa kichwa akiwa aamini kile ninachomueleza. Ni dhahiri kuwa alikuwa hajapenda mpango niliokuwa nao kichwani, lakini alikuwa anaonyesha dalili za mtu ambaye yuko tayari kukubali kufanya kile ninachopendekeza hata kama hapendi.

“And sijamaliza!” Nikaongea mwa kujishtukia huku natabasabu.

“Kumamaeee!! Bado kuna kingine??” Obama akatukana kwa hasira. Nikagundua kuwa alikuwa amekasirika kweli maana hakufanania na mtu mwenye kutukana tukana hovyo.

“Sinyorita” nikaongea kwa mkato.

“Hahahaha.! Unataka nikutongozee sinyorita??” Akacheka na kunikejeli kwa makusudi kupunga hasira zake.

“Trust me, sihitaji msaada wa kutongozewa.. Humu gerezani kuna kitu wanaita maharage ya kuoka! Nadhani unafahamu naongelea nini! Nataka umuwekee bili ya maharage ya kuoka kwa mwezi mzima angalau.!” Nikaongea huku natabasamu nikikaribia kucheka.

“Maharage ya kuoka kwa siku ni buku, so kwa mwezi ni thelathini hiyo tunaongelea” akaongea huku amekodoa macho.

“come on man!! Askari mwenye nyota mbili begani elfu thelethini kitu gani??”

“Alafu Sinyorita anatusaidia nini?”

“Utaona kesho!” Nikamjibu kwa mkato.

“Ray, unajua ungenieleza walau huo mpango wako nina weza kukusaidia mawazo!”

“Ubaya ni kwamba sihitaji unisaidie mawazo.. Nahitaji unisaidie kutekeleza mawazo yangu!” Nikamjibu huku naanza kuinuka pale kwenye kiti.

“Kesho mchana ikigonga kengere ya chakula, nitakuwa yard namba mbili nasubiri funguo ya selo namba 46.”

Nikaongea kwa kujiamini huku nainuka na kuanza kuondoka kutoka ofisini kwa Obama.

“Fuuuuucccckk” nikamsikikia anajilalamikia.

Nikatoka kwenye ofisi huku natabasamu kimoyo moyo. Nikajua hapa nishapiga goli la tik tak.

Nikaelekea moja kwa moja mpaka yard namba mbili.

Nilipofika nikaanza kuangaza macho huku na huko kumtafuta Godi ambaye nilimuagize ahakikishe anakuwa na Sinyorita ili niongee naye.

Baada ya kutazama tazama sana, hatimaye nikawaona wamekaa nyuma ya mwembe pale yard. Nikatembea haraka kwenda mahali walipo.

“Wooow! Mnapendeza kinoma!” Nikawatania.

Sinyorita akaanza kutabasamu kwa aibu aibu kama mtoto wa kike, huku Godi akizungusha macho kwa kukereka.

“Ok! Sinyorita ndio huyu hapa, ongeeni ukimakiza utanikuta kule.” Godi akaniharakisha niongee na kuondoka akionekana dhahiri anakereka na sisi kuonekana tumesimama na Sinyorita.

Nikaanza kumuelezea Sinyorita kila ninachotaka akifanye. Nikamueleza kwa taratibu sana na kwa tahadhari ili aendelee kunisikiliza mpaka mwisho asije akanikatisha kwa kuniporomoshea mitusi na kuondoka.

Maelezo yangu, nilianzia na ofa ya maharage ya kuoka mwezi mzima.

Ifahamike kuwa, humu gerezani kero kubwa ya chakula kuliko zote ni mboga. Kama ambavyo nilieleza awali kuhusu hali halisi ya maharage humu jela, unajaziwa kikombe kizima mchuzi lakini huyaoni maharage na ukiyabahatisha yametuama chini hazizidi punje kumi.

Dona linazoeleka na halikeri sana japokuwa linasagwa na vibunzi. Lakini dona bila mboga ya kulilia ni mtihani.

Kwahiyo wapishi jikoni (ambao ni wafungwa pia) kwa kushirikiana na askari anayesimamia jiko wameunda mradi wa magendo wa kupika maharage kidogo pembeni kwa kuyaunga kwa uzuri kama yanavyopikwa nyumbani. Maharage haya ndio yamepewa jina la utani ‘maharage ya kuoka’ humu gerezani na wanayauzwa shilingi elfu moja au vipande vitano vya sabuni.

Kwahiyo hiyo ndiyo ilikuwa chambo changu nilichokuwa natumia kumshawishi Sinyorita anisaidie katika mpango wangu. Kwamba atapata maharage ya kuoka mwezi mzima kila siku.

“Kwahiyo anifile kwasababu ya maharage ya kuoka?” Sinyorita akaongea kama anabana pua.

“Nooooo! Sio kukufila… ****! Nimekwambia unavua nguo tu ili askari wawakute wewe ukiwa uchi” nikaongea huku nasikia ukakasi mdomoni jinsi tunavyolitumia neno ‘kufila’ kirahisi rahisi.

“Mi staki bwana, naweza kuvua nguo akanifila kweli” Sinyorita akaanza kuleta mapozi.

Ilibidi sasa nianze kumbembeleza kama vile ‘natongoza demu’. Nikatumia kama dakika ishirini nyingine kumshawishi mpaka hatimaye akakubali.

“Haya poa, ila nataka na ubwabwa kila jumamosi na jumapili.. Kama hutaki basi.” Akaongea tena kwa kudeka kama anabana pua.

“Ok ok! Its done.. You got it” nikajisahau na kuropoka kingereza.

“Ndo nini?” Akakunja sura.

“Namaanisha poa! Nimekubali, utapata ubwabwa kila weekend”

“Nyoko zako! Ukiongea na mimi usiniletee vingereza vyako fala wewe!” Akanifokea kishangingi.

“Kuna lingine?” Akaniuliza huku ananiangalia kwa kunilegezea macho.

Nikajikuta nimeshikwa na aibu na kigugumizi. “No! Hakuna lingine”

“Una uhakika?” Akaniuliza tena huku amelegeza macho zaidi.

“Nishakwambia hakuna lingine! Muhimu tu usisahau kesho kengere ya chakula……..” Kabla sijamaliza akanikatisha.

“Eeeeeee babu weeee hebu nitue! nshakuelewa msyuuuuuuuuu” akongea na kumalizia na sonyo kisha akageuka na kuanza kuondoka kimiss.

“Fuuuucccckk! I really need to get out of here” nikajisemea kwa sauti ya chini chini nikimwangalia Sinyorita akiondoka baada ya kushuhudia vituko vyake.

Uzuri ni kwamba, sasa walau nilikuwa na uhakika mpango wangu unaweza kutekelezeka. Kila nilichohitaji, kilikuwa “kimeelekea kibla”.


LEO

“Nimefanya mistake kubwa sana kumuamini Obama! ****..!! alinizidi akili” nikaongea kwa hasira huku natoka pale uchochoroni kuelekea yard namba mbili. Kaburu alikuwa ananifuata nyuma.

“Una maana gani sikuelewi”

“Kuna vitu alinisaidia, ikanifanya nimuamini! Nikaamini ni mshirika wa watu fulani kumbe sio na nimeanza kuwa na hisia kwamba Obama ni kibaraka wa The Board” nikaongea kwa sauti ya chini, tulikuwa tumeshatokea yard namba mbili.

“Unataka kunambia kuwa documents zangu zitakuwa mikononi mwa The Board muda huu?? Are you kidding me??” Kaburu akahamaki.

Godi alitusogelea mahali tulikokuwa baada ya kuingia yard namba mbili. Kwahiyo sasa tulikuwa tumesimama watu watatu pamoja.

“Inabidj tutekeleza plan yetu kwa haraka kuliko nilivyokuwa nimepanga” nikaongea huku nawaangalia wote wawili.

“Nakusikiliza” kaburu akaongea kwa hasira.

“Kukutorosha kutoka humu ni ngumu, inabidi nikutoroshe ukiwa nje”

“What? Sikuelewi” Kaburu akauliza.

“Hii Zahanati ya magereza nimegundua kuwa hailazi watu na haitibii ishu serious.. Kama mgonjwa anaumwa serious na anahitaji kulazwa au uangalizi wa karibu zaidi wa daktari anapelekwa hospitali kubwa chini ya ulinzi wa askari magereza” nikanyamaza kidogo kuwaangalia kama wananielewa, kisha nikaendelea. “Nahitaji keshi upelekwe hospitali kubwa ili nikutoroshe” nikaongea kwa sauti ya chini.

“What the **** are you talking about?? Mimi ni mfungwa, siwezi kuwaambia tu wanipeleke hospitaki kubwa” Kaburu akafoka.

“Hawatakupeleka tu na wala hautawaomba wakupeleke.. Watakupeleka wenyewe”

“Una maana gani?”

“Tunadaiwa shilingi elfu kumi na Nyapara na hatujamlipa mpaka sasa na tulitakiwa kumlipa jana.. Sasa muda wowote najua atakuja na wapambe wake kumdai Godi hela.. So akija nataka uwe shujaa umtetee Godi… Na nina hakika baada ya hapo lazima upelekwe kulazwa” nikaongea nikitabasamu lakini nikimaanisha ninachoongea.

“Dogo umedata nini? Unataka waniue au??” Kaburu akaanza kufoka kwa hasira.

“Mkuu kama una wazo zuri zaidi naomba kulisikia! Na kama huna Fanya ninachokwambia.. Nahitaji kesho uwe hospitali kubwa” nikaongea huku nikimvimbia na mimi.

“Mahakamaaaaaaaaaaaaaaa” mfungwa wa matangazo alipita yard anapayuka akitangaza kuwa muda umewadia kwaa mahabusu wenye kesi zao leo kwenda mahakamani.

“Wakuu naona tunaitwa huko! So mimi nawaacheni” nikaongea huku nawatazama.

“Usinisahau katika ufalme wako mkuu” Godi akakumbushia suala lake la dhamana.

“Usijali Godi, kitaeleweka tu” nikamjibu kisha nikamgeukia Kaburu na kuongea naye kwa sauti ya chini lakini ya ukali huku namsonta kidole kifuani “Nahitaji kesho uwe hospitali.! Don’t forget that”

Nikaongea na kuanza kugeuka kuondoka.

“Kilala heri chief” Godi akaniaga huku anapiga saluti.

Kwa mara ya kwanza tangu aanzishe hizi swaga za kupigiana saluti, nikajikuta na mimi nimemjibu kwa kumpigia saluti fupi kwa kama nusu sekunde tu.

“I got this”

Nikageuka na kuondoka.


Kikichokuwa kinaendelea leo mahakamani niliona kama maigizo tu na ngonjera.

Ilipofika zamu yangu ya kesi kusikilizwa, nikapelekwa mpaka chamber court. Kisha wakaanza “maigizo” yao.

Mwendesha mashitaka akasimama na kuanza kuongea. Akataja nambabyangu ya kesi, shitaka linalonikabili, blah blah blah… Mwisho akaeleza kuwa Jamuhuri haina nia tena ya kuendelea na shauri hili.

Baada ya hapo Mheshimiwa hakimu naye akaanza blah blah blah.. Akataja lundo la vifungu vya Sheria… Sijui nini nini.! Alafu mwishoni akamalizia “…..hivyo basi mahakama hii inalifuta shtaka hilo na inakuachia huru kuanzia sasa”

Sikusema chochote, nikaweka mkono kifuani na kuinama kidogo kama ilivyo desturi kuonyesha heshima kwa mahakama kisha nikageuka na kutoka nje ya Ofisi ya Hakimu.

Koridoni, kulikuwa na cheupe na Issack pekee. Baba bite na wenzake hawakuwepo kama ilivyokuwa siku ya kwanza.

.

Nikamtazama Cheupe wangu kwa shauku kubwa. Damn, sijawahi kutamani kumkumbatia kiasi hiki. Nilitamani nimkumbatie kwa nguvu nisimuachie kwa hata wiki nzima.

Lakini huu haukuwa muda wala eneo sahihi kufanya hivyo.

Nikamshika mkono Cheupe na kuanza wakaongoza nje kwa haraka.

“Its a trap” nikaongea tukiwa tunatoka nje ya jengo lenye ofisi za mahakimu.

“What do you mean its a trap??” Cheupe akauliza kwa shauku.

Sikumjibu chochote. Nikawaongoza mpaka sehemu ndani mule mule kwenye viunga vya mahakama kulikuwa kama uchochoro unaotenganisha open court na jengo lenye ofisi za mahakimu.

Tulipofika hapo nikaangalia huku na huku, na nilipohakikisha tuko peke yetu nikaanza tena maongezi.

“Its a trap” nikarudia tena.

“What trap Ray” Issack akaukiza pia.

“Dr. Shirima juzi alinieleza kuwa nitaachiwa na nikiachiwa anataka niende moja kwa moja kwenye makazi ya askofu.. So obviously siwezi kufanya hivyo! So naamini kuna mtu amewekwa hapa atufuatile tukitoka hapa tunaenda wapi! Hawawezi kuniteka hapa mbele ya mahakama na polisi lakini nikikanyaga nje tu ya jengo la mahakama nina hakika lazima waninyakue kama kifaranga”

Nikawaelezea huku wote wametoa macho.

“So tunafanyaje?” Cheupe akauliza.

“Umekuja na simu yangu?” Nikamuuliza Cheupe.

Akaingiza mkono kwenge mkoba wake na kutoa simu na kunikabidhi.

Nikawasha na kuanza kutafuta namba niliyokuwa naitaka. Nikapekua pekua mpaka nilipoipata namba iliyoandikwa ‘Taxi Bonge’.

Baada ya kuipata nikapiga.

“Niaje mzee wa saundi hahahah? Uko wapi….. Ok ok njoo mahakamani hapa mahakamani ila njoo na taxi nyingine mbili…. Yeah ingieni ndani…… aaaaahh wewe mzee wa saundi bhana utajua somjo utakayowapiga getini wakuruhusu kuingia……. Poa poa kaka” nikakata simu.

“Umeagizia taxi tatu??” Cheupe akashangaa.

“Yeah! Nataka tumvuruge akili huyo waliyemuweka atufuatulie”

Dakika tano baadae Taxi tatu zikaingia zikiwa zimeongozana. Nikampigia simu Bonge tena kumuelekeza waje na Taxi mpaka kwenye upenyo unaotenganisha jengo la ofisi za mahakimu na open court.

Taxi zote tatu zikaja. Nikamuomba karatasi na peni cheupe nikaandika kitu fulani kisha nikamoa dereva taxi mmoja.

“Ok, hiyo karatasi nataka upeleke Njia Panda ya Kilakala kwenye makazi ya Askofu wa Jimbo, ikabidhi kwa mlinzi getini muambie amfikishie Askofu… Issack utapanda hii taxi nyingine na uelekee nyumbani mazimbu… Mimi na Hasnat tutapanda taxi ya Bonge..!! Ila nataka taxi zote zitoke pamoja na tukiyoka getini tu kila mtu apite njia yake.. “

Wote wakaniangalia tu kwa mshangao wasielewe kinachoendelea.

“Don’t worry Issac you going to be fine! Its me who they want!” Nikamfariji huku nikitumia kingereza ili wale madereva taxi wasielewe kinachoendelea.

Wote tukapanda kwenye magari kama nilivyowaelekeza kisha tukaondoka.

Nje ya geti taxi aliyopanda Issac ikapinda kushoto kufuata njia inayoelekea Central Police, taxi ile amabayo haina mtu pamoja na hii niliyopanda mimi na cheupe tukapinda kulia mpaka kwenye round about ya mnara wa mashujaa kisha ile taxi tupu ikapinda kulia kuelekea kilakala huku taxi niliyopanda mimi nikimuelekeza bonge anyooshe kama tunaelekea jengo la Manispaa.

Akanyoosha moja kwa moja mpaka tukatokea round about ya masika.

“Tunaelekea wapi mkuu” Bonge akauliza.

“Mikese” nikamjibu kwa ufupi tu.

Mimi na cheupe tulikuwa siti za nyuma.

“Whats your plan honey” Cheupe akaniuliza.

“My plan is very simple! Misdirect. Confuse. Deflect” nikamjibu huku namuangalia nikitabasamu.

Cheupe naye akatabasamu, kisha akainuka na kunikalia juu akalala kifuani. Nikampakata kama katoto kadogo huku nimekumbatia kwa nguvu kwa jinsi nilivyommsiss.

Kama dakika ishirini na tano baadae tulikuwa tumefika mikese.

Cheupe akamlipa elfu arobaini, tukashuka.

Baada ya Bonge kuondoka, tukavuka bara bara mpaka karibu na mizani. Tukaisimamisha gari ya aboud kisha tukapanda kurudi mjini.

Uzuri wa gari za Avoid unaweza kushukia stendi msamvu au unaweza kwenda kushukia mjini ambapo gari za Aboud lazima ziende ofisini kwao zikitoka safari.

Kwahiyo hatukushuka msamvu. Tukaenda na gari mpaka mjini na kushukia kwenye ofisi za Aboud zilizopo kati kati ya mji.

Hapo tukachukua bajaji mpaka stendi ya Hiace. Tulipofika stendi tukachukua dala dala inayoelekea nje ya mji maeneo ya Mkundi (Dodoma Road).

Mkundi tukashuka na kupiga mkono hiace zinazoelekea Dakawa. Tukapanda hiace mpaka dakawa.

Tulipofika, tukapumzika kidogo kwenye bar ilitopo pembeni ya bara bara. Nikaangalia kuona kama kuna dalili yoyote ya watu wa kutia shaka. Nilipojiridhisha kuwa tuko salama hakuna anayetufuatilia nikamwmbia Cheupe tuelekee bara barani.

“Are we running away from them??” Cheupe akauliza.

“Hell no! Najaribu kukata tail waliyotuwekea pale mahakamani na naamini tumefanikiwa.. Now its a time to put a tail on them” nikatabasamu na kumbusu kidogo cheupe wangu.

Tukafika barabarani, nikapiga mkono Lori ambalo naamini lilikuwa linaenda nje ya nchi. Naamini lilikuwa linaenda Rwanda. Lori likasimama.

“Mnaenda wapi” Dereva akauliza kwa sauti.

“Dodoma” nikamjibu.

“Aaaaahh mi nachukua abiria wa mbali bhana”

Kabla hajageuka nikatoa noti Tatu za elfu kumi na kumuonyesha.

“Elfu thekathini hii, unatuacha dodoma tu hapo”

Dereva akatabasamu kwa uroho. “Pandeni” akaongea huku anatufungulia mlango.

“So how are you going to put a tail on them?” Cheupe akauliza tukiwa tunapanda kwenye Lori.

“Usijali mama! Utaona” nikamjibu kwa kifupi.


Tulingia Dodoma takribani majira ya saa mbili usiku.

Dereva wa Lori alitushusha katikati ya mji. Baada ya kutushusha tukachukua taxi mpaka mtaa wa Airport ambapo tukafikia kwenye lodge ya Samali.

“Oooooopps! Angalau sasa tupumzike kidogo” Cheupe akashusha pumzi kwa nguvu nikiwa nafungua mlango wa chumba namba 0207.

Nikafungua mlango, tukaingia ndani.

“Haujanipa update yoyote kuhusu mzee” Nikamuuliza Cheupe huku naketi kwenye kitanda na kuanza kuvua viatu.

“Ooohh! Bado wanasumbua sana.. Hata tukienda Wizara ya Mambo ya ndani wanatuambia kuwa tuwe watulivu watatuita”

“Aisee! Tunahitaji kulimaliza hili suala haraka iwezekanavyo” nikatupa viatu pembeni baada ya kuvivua.

“Mmmmmhh! Hebu leo jaribu kutuliza akili kidogo upumzike baba.. Alafu mpaka muda huu hujaniuliza chochote kuhusu mimi au mwanao”

Cheupe akaongea huku anapanda kitandani na kuja kunikumbatia mgongoni na kunishika shika mabega kwa kunimasaji.

“Oooooooohhh! Awwww, that’s sweeeeeett” nikasikia mwitikio wa neva zangu baada ya Cheupe kunichokoza kwa kimasaji hiki mabegani.

“So how is my boy” nikamuuliza kwa kumchokoza.

“Heeeyyy! Mbona umeng’ang’ania sana ‘its a boy’ am sure ‘its a girl’ hahahah” Cheupe akaongea huku anaendelea kunikanda mabegani.

Nikageuka na kumuangalia. Yeye alikuwa amepiga magoti juu ya kitanda na mimi nilikuwa nimesimam kawaida.

Nikamshika kiuono, kisha nikamvuta karibu yangu.

“Walisema mimba ina muda gani” nikamuuliza huku nambusu kwenye paji la uso, machoni, puani.

“Kama wiki tatu hivi” akanijibu huku naye anarudisha mabusu.

“So unajisikiaje! Katoto kanacheza cheza tumboni? Hahah”

“Honeeeeeyy! Khaaaaa, wiki tatu tu.. Najisikia kawaida tu yani kama siku zote. Labda sometime tu nasikia kizungu zungu kidogo”

“Woow! Im so happy finaly Kichwa Junior anakuja duniani hahah”

“Hahahah, lakini una miezi tisa ya kusubiri”

Cheupe akainuka kutoka kitandani na kuelekea kwenye moba wake na kuanza kupekua pekua.

Nikachukua remote na kuwasha TV.

Nilivyogeuka pembeni kumuangalia tena cheupe, alikuwa amevua nguo zote na kubaki na chupi tu. Akachukua taulo na kujifunga.

Kwa kuwa mataulo ya hotelini yanakuwaga na size ndogo, kwahiyo alipojifunga taulo ilikuwa kana kwamba amevaa kigauni kifupi sana chenye kutega.

Mwili ukanisisimuka kumuona akiwa namna ile.

Cheupe akageuka na kuniangalia jinsi nilivyokuwa namtazama. Akatabasamu.

Akaenda mpaka mbele ya kioo nankuanza kujitazama akijibinua binua makusudi ili “kuniumiza”.

Kisha akageuka tena na kuniangalia. Akatabasamu. Ila tabasamu ka safari hii lilikuwa tofauti kidogo. Alitabasamu huku kama amelegea hivi.

“Bye, naenda kuoga” akanikonyeza na kufungua mlango wa bafuni.

Sijui labda ni kwasababu ya kukaa jela wiki nzima na kushindwa kupata fursa angalau kumuona mtoto wa kwa wiki nzima, au ni huu uchokozi aliokuwa ananifanyia cheupe.. Nianchokijua ni kwamba mwili wangu ulisismuka na kuwaka joto la kutamani kumvua ile chupi cheupe na kumchezesha mchaka mchaka usiku mzima.

“Damn it” nikavua tisheti haraka haraka. Nikafungua mkanda kiunoni na kuvua jeans..

Nikaanza kutembea haraka kuelekea bafuni, nilipokaribia mlango wa bafuni nikatabasamu kidogo… Nikasimama na kuvua boxer na kubaki uchi kabisa.

Nikausogelea mlango wa bafu na kugonga kwa uchokozi. Tararibuuuu..

“Karibu!” Cheupe akanijibu kwa sauti ya chini sana iliyolegea.

Nikafungua mlango kiduchu na kuchungulia.

“Are you sure?” Nikamuuliza kwa uchokozi kwa sauti ya chini kimahaba.

“Njoo uniogeshe Ray” Cheupe akaongea bila kuniangalia akiwa amegeuka upande mwingine.

Hakuna kitu chenye nguvu kama maneno. Kitendo cha kusikia Cheupe akiniambia nikamuogeshe, nilisikia uume ukisimama kwa nguvu.

Haijalishi ni mara ngapi nimemuona Cheupe akiwa bila nguo, lakini kila siku nyingine nikiuona mwili wake ukiwa uchi kabisa bila nguo ndani yangu najisikia kana kwamba ni mara yangu ya kwanza Cheupe kunivulia nguo.

Alikuwa amefungulia ‘bomba la mvua’ huku amewasha heater kwahiyo maji yalitoka na ndani bafuni kulikuwa na kama kimvuke fulani hivi cha kuvutia! Jinsi maji yalivyokuwa yakitiririka mwilini mwake huku bado ameguka amenipa mgongo.

Jinsi maji yalivyokuwa yanatiririka mwilini mwake na kutengeneza kama mfereji kutoka mgongoni na kupita katikati ya makalio yake ilizidi kunisisimua na uume kusimama zaidi kwa nguvu. Joto la mwili lilikuwa juu sana.

Sio kwasababu Cheupe ni soulmate wangu, lakini hiki ndicho nilichoamini kwamba sidhani kama kuna mwanamke duniani mwenye umbo zuri kumshinda Cheupe wangu.

Kuanzia makalio ambayo hayakuwa makubwa sana lakini pia hayakuwa madogo, yakiwa yameambatana na hips zilizochomoza kiasi na kiuno chembamba kabisa.

Mwili ulisisimka na joto likazidi kupanda na uume ukiwa umesimama haswa.

Vile alivyogeuka na kunipa mgongo nikatamani nikamkumbatie vile vile, nipitishe mikono yangu kwa mbele na kumminya chuchu zake.

Nikafungua mlango wote na kuingia bafuni. Cheupe hakugeuka, akaendea tu kunipa mgongo.

Nikamshika kiuno na kumvuta kwangu.

Nikamsikia jinsi mwili wake ulivyosisimka baada ya uume wangu kumgusa mgongoni na kwenye makalio. Nikamvuta karibu zaidi na kumkumbatia.

Nikapenyeza mikono yangu kifuani kwake na kuanza kumminya chuchu. Nikazidi kuusikia mwili wake ulivyosisimka zaidi.

Akaanza kulegea zaidi. Akalaza kichwa chake begani kwangu.

Bomba la mvua lilikuwa linaendelea kututiririshia maji kwa pamoja. Taratibu nikaanza kumyonya shingoni huku naendelea kumminya chuchu zake. Akazidi kusisimka na kulegea.

Nikawa namyonya lips na kumnyonya shingoni. Cheupe alilegea kabisa kama vile amepoteza fahamu.

Nikaona ngoja niipeleke hii shughuli level nyingine.. Nikiwa naendelea kumnyonya shingoni na mkono wa kulia nikimminya chuchu.. Taratibu nikashusha mkono wangu mpaka katikati ya mapaja yake.. Mkono wangu ulipofika katikati ya mapaja yake cheupe akatanua miguu zaidi, nikaingiza mkono kwa ndani zaidi naniuanzq kumpapasa sehemu pendwa.. Nikampapasa sehemu pendwa kwa taratibu na nilipomuona anasisimuka zaidi nikajipa ruhusa ya kupenyeza kidole changu ndani yake… Nikausikia mwili ukizidi kuwa nyang’anyang’a vidole vikiwa vimelowa haswa huko vilipo viingiza.

Kadiri alivyokuwa anazidi kuwa nyang’anyang’a, ndivyo ambavyo nilimtamani zaidi na uume ulisimama na kukakamaa zaidi.

Nikamshika shingoni kama nimemshika kuku.

Kuna kipindi nilipokuwa teenager, niliamini kwenye falsafa ya “love her like a queen, fck her like a btch”.. Ndicho nilichotaka nikifanye leo! Kwa jinsi nilivyokuwa na hamu, nilitaka nimtomb* kama vile simjui.

Nikamshika tena shingoni kama kuku kisha nikamgandamiza ukutani.. Alafu nikashikilia ‘bolo yanki’ nakumsokimezea kwenye uchi taratibu mpaka ilipozama yoteeee!

Nikaanza kumpiga punc za taratibu na kila niliposikia misuli ya uke wake inarelax nikaungeza uzito wa punch na kumpiga punchi nzito nzito.. punch za ‘dona sato’!

Kwa jinsi ambavyo nilimbananisha pale ukutani, Cheupe hakuwa na ujanja zaidi ya kulilia kama katoto kadogo.. Kiluo cha utamu aliokuwa anasikia!

Nilipiga punch mfululizo kama mbwa mwitu na ndani ya kama dakika tano nikahisi mwili wa cheupe kama unapasuka vipande vipande.. Alikuwa amefika juu ya kilele cha mawenzi!!

Nikamuachia kidogo kumgandamiza ukutani, nikamvuta kwangu na kumkumbatia. Akageuka kwa nguvu na tukaanza kunyonyana mate.. Mimi nilikuwa sijatoa wazungu bado, kwahiyo uume bado ulikuwa na hasira, umesimama kwa ukakamavu kabisa.. Kwahiyo tulikuwa tunanyonyana mate huku amenishika uume anauchezea kama vile abanipigisha puli.. Walahi cheupe ni “mwana laana”, ananijuilia haswaaa!!

“Please usiniache tena peke yangu Ray” cheupe akaninong’oneza sikioni kimahaba sikioni huku anaendelea kuuchezea uume.

“I’m right here with you honey! I’m not going anywhere” nikamnong’oneza kimahaba na mimi.

Kwa kuwa nilikuwa bado sijawapeleka wazungu kwao, kwahiyo hii shughuli ilikuwa ndio kwanza imeanza. Nikaona tubadili uwanja wa mauaji.

Nikambeba Cheupe juu juu huku naendelea kumnyonya mate nankutoka naye bafuni.

Nikaenda kumtupa juu ya kitanda.

Cheupe akaanza kujinyonga nyonga pale kitandani kabla hata sijamgusa.

Nikiwa nimesimama vile vile nikamuinua miguu na kuanza kumbusu unyayoni mpaka kwenye vidole.

Kisha, kama ambavyo Mussa alivyoigawanya bahari Shamu, ndivyo nilivyomgawanya miguu yake na kumpanua mapaja kisha nikazamisha kichwa changu kati kati ya mapaja na kuanza kumnyonya sehemu pendwa.

Cheupe alikuwa anajinyonga nyonga na kupumua juu juu kama anataka kukata roho.

Nilipomuona amekuwa nyang’anyang’a tena taratibu nikaanza kumbusu kitovuni, kisha kwenye chuchu mpaka nikafika midomoni.. Nilipofika kwenye midomo nikawa nambusu na wakati huo huo huku chini taratibuuu namungiza ‘bolo yanki’ sehemu pendwa.!

Shughuli ikaendelea, punch za dona sato kama mbwa mwitu.

Utamu ulipotukolea wote wawili, sijui Cheupe alitoa wapi nguvu za ghafla.. akaniiunua kama ananisukuma na kunilaza pembeni kisha akaja kukaa juu yangu.

Sio kwamba tu alikaa, alikuwa kama amechuchumaa.. Alafu akawa anakaa, anainuka, anakaa, anainuka.. Hivyo hivyo, na kadiri utamu ulipokuwa unazidi, na kasi ya kukaa na kuinuka ikazidi.

Kama dakika tano baadae nikaanza kuhisi wazungu wanakaribia kupata uhuru.. Nikajiinua na kumbatia kwa nguvu Cheupe nikwa kama nimempakata.

Cheupe naye alikuwa anakaribia kilele cha mawenzi kwa mara nyingine.. Nikahisi kama alikuwa na mota kiunoni kwa jinsi ambavyo ‘bolo yanki’ alikuwa anakatikiwa.

Wazungu wakafika mlangoni, na cheupe alizidi kutapatapa kadiri anavyokaribia kilele.

Nikawaruhusu wazungu watoke.. Na walitoka kwa fujo na kasi kama risasi.. Cheupe akanikumbatia kwa nguvu zake zote kwa utamu wa kilele na wazungu waliokuwa wanamtekenya ndani yake…

Wote tulihema kama tumetoka kukimbia marathoni ya kilometa mia.

Sijui tuligandiana vile kwa muda gani.. Ila fahamu zangu ziliporudi tulikuwa tumelalia mto kitandani tunanyonyana mate huku tunatazamani uso kwa uso.!

Damn! Nilikuwa nimemmiss Cheupe wangu..


Ilikuwa tayari inakaribia majira ya saa tatu kasoro asubuhi.

Nilikuwa kwenye taxi natoka katikati ya mji wa Dodoma naelekea mitaa ya airport kwenye lodge ya Samali ambayo tumefikia.

Kwenye kimfuko cha nailoni nilichokuwa nimekibeba nilikuwa na vitu kadhaa nilivyonunua.

Kulikuwa na kamera aina ya kodak ya kizamani ya kupiga picha mnato (still poctures), Kulikuwa na mkasi, waya wa kuchomeka kwenye cable, kulikuwa na soldering iron (solda waya kama wanavoita mafundi redio/TV), bisibisi (screw driver) na ‘gun’ ndogo ya kuchomelea solda waya.

Pamoja na vitu hivi, pia nilikuwa nimenunua situ sita za tekno za elfu ishirini na tao kila moja.

Cheupe yeye nilikuwa nimemuagiza aende bank. Kwanza aende kwenye akaunti yake atoe fedha nyingi iwezekanavyo, pia achukue kadi zangu za ATM pia atoe hela nyingi iwezekanavyo. Nilikuwa nataka tuwe na fedha cash walau milioni tano kutokana na mpango niliokuwa nimeupanga.

Dakika kumi baadae tulikuwa tumefika Samali lodge, nikamlipa dereva na kuingia ndani. Nikashukuru kumkuta cheupe naye amerudi.

“Umefanikiwa?” Nikamuuliza.

“Yeah! Nimefanikiwa” akanijibu.

“Umefanikiwa kutoa jumla shilingi ngapi kwenye akaunti yako na kwangu ATM?”

“Milioni tano na laki nane”

“Na vile vitu umenunua vyote?”

“Yeah vile pale! Nguo zetu za kubadilisha, mabaibui mawili na begi la mgongoni” akanijubu huku ananionyesha begi moja kubwa sakafuni na lingine dogo la mgongoni.

“Well done cheupe! Sasa oga kabisa mimi nipe kama dakika kumi na tano nitengeneza ‘kombora’ langu” nikamueleza huku nakaa kwenye kiti na meza vilivyomo mle ndani.

“Na unaweza kunidokeza hilo kombora unalolitengeneza ni nini?” Cheupe akauliza huku anaanza kuvua Nguo ili aende kuoga.

“You will love it.!! Umewahi kuona kwenye TV kwenye nchi za wenzetu unakuta askari anamkamata muhalifu na kama muhalifu anakuwa analeta usumbufu na kuwa violent huwa wanatoa kifaa fulani hivi muundo wake kipo kama tochi alafu anampiga shoti muhalifu?” Nikamuuliza.

“Yeah! Nishaona mara kibao.. Na akishampiga shoti muhalifu anaweza kupoteza fahamu kwa muda mchache kama dakika moja au mbili hivi..”

“Exactly… Sasa ile inaitwa Taser au kwa jina lingine mtaani wanaita ‘stunt gun’! Inatumia mfumo wa kielektroniki kutoa shoti ya umeme ili kumdhibiti muhalifu kwa kumfanya azimie kwa muda mchache bila kumletea madhara mengine.. Ndicho hicho nataka kutengeneza hapa”

Nikamjibu huku natabasamu nikitoa vitu kutoka kwenye ule mfuko wa nailoni na kuviweka mezani.

“Wow! And can you tell me why we need a ‘stunt gun’?” Akaniuliza huku anajifunga taulo.

“Utaona kazi yake leo hii hii” nikamjibu huku natabasamu kwa kujidai.

“Ok! Karibu tuoge” akaaongea huku anatembea kwa madaha kwenda bafuni.

“Hahahaha.! Cheupe please usinifanyie kusudi mama, nitageuka kuwa ‘Ngoswe’ ujue… inabidi nikamilishe hii haraka tuondoke hapa” nikamjibu kwa kicheko.

“Haya shauri yako hahahah” akaingia bafuni.

Japokuwa nilitamani nijumuike naye bafuni, lakini tulikuwa nyuma ya muda. Napaswa kutengeneza hili ‘kombora’ haraka na kisha tuondoke.

Nikaichukue ile kamera ya Kodak na kuifungua nati kisha kutoa kasha lake la juu.

Kama nilivyoeleza kuwa hii ilikuwa ni ile Kodak ya kizamani, kwahiyo ukiondoa kasha la juu linalofunika kamera unakutana na ‘mkanda wa picha’ (film). Huu nao nikauondoa na kuuweka pembeni.

Kisha nikandoa kwa uangalifu betri zake. Kamera za Kodak za kizamani zina uwezo mkubwa sana wa kutunza umeme kwahiyo hata ikiwa imezimwa ukigusa gusa ndani bila tahadhari unaweza kupigwa shoti ghafla.

Baada ya kuondoa betri nikafungua nati kadhaa na kuitenganisha pembeni kadi yake ya umeme (circuit board).

Nikageuza kadi kwa nyuma ili niione Capasitor kubwa ilipo.

Baada ya hapo nikachukua nyaya nilizozinunua na kuzinyongorota mizunguko mingi sana ili kutengeneza ‘transformer’ ndogo ili iniwezesha kuboost voltage.

Wenye kujua kidogo fizikia wataelewa zaidi namna ambavyo unaweza kutengeneza ‘transformer’ kwa kutengeza ‘coil’ ya mizunguko ya nyaya.

Baada ya kutengeneza hiki ‘kitransformer’ nikakiunga na kukichomelea na solda waya kwenye Capasitor kwa utaratibu na ustadi. Kisha nikafunga kwa ‘sole tape’ vile nyaya ili zisigisane.

Baada ya hapo nikaiondoa buld kwenye kamera. Hii ni ile bulb inayotoa ‘flash’ wakati wa kupiga picha, umeme mwingi wa kamera unatumika ili kuifanya bulb iwake kwa mwanga mkali na kutoa ‘flash’. Kwahiyo nikaiondoa hii bulb.

.

Baada ya hapo nikachukua waya ule unaotumiaka kuchomeka kwenye ‘extension cable’ na kuunganisha kwenye kifaa cha umeme.

Nikaukata na kubakisha kipisi kidogo chanye urefu wa kama kidole cha mwisho cha mkono.

Kisha nikatumia ‘solda waya’ kuuchomelea na kuunganisha kwenye nyaya zinazotoka kwenye Capasitor na kupitia kwenye kile kitransfoma.

Baada ya hapo nikatoboa kasha la Kamera vitundu viwili vidogo kuwezesha ile miguu miwili ya waya kupita.

Kisha nikarudishia betri zake na kasha juu nankuanza kuifunga.

Baada ya kuifunga, Kamera ilikuwa na muonekano wa kawaida kabisa, lakini ukitazama kwa makini pembeni unaona vile vumiguu viwili vimechomoza.

Nikamsikia Cheupe anatoka bafuni.

“Its done! Vaa fasta mama tuondoke” nikaongea huku nakusanya vitu.

“Wow! So how does it work?” Cheupe akaukiza.

“Simple tu! Unabonyeza kwa muda mrefu hapa kwenye button ya kupigia picha kisha unagusisha hivi vimiguu vilivyochomoza kwenye mwili wa mtu”

“Yani simpo tu kiasi hicho?” Akauliza tena.

“Yap! Its that simple.. Hebu nipe hicho kijiko” nikamuambia anipe kijiko kilichokuwa kwenye sahani ya ‘breakfast’ tuliyoletewa hii asubuhi.

Aliponipa nikabonyeza button ya kamera kwa kama sekunde ishirini hivi bila kuiachia.

“Skia kitu hicho” nikamsikilizisha sikioni jinsi Kamera ilivyokuwa inatoa mlio fulani hivi kwa ndani kama mluzi unaosikika kwa mbali.

Ilikuwa ni Capasitor na transfoma ‘vinajichaji’ kwa kulimbikiza umeme mwingi ili viweze kuuachia.

Kisha nikagusisha vile vimiguu viwili kwenye kijiko.

“Paaaaaaaaaaaaaa” kijiko kilipiga bonge la shoti lililoambatana na mwanga.

“What the fuuuuccck” Cheupe bado alikuwa anaogopa ogopa utadhani nataka kumoiga shoti na yeye.

“Oooohh yeah! Today am going to blow someone to hell..!!” Nikaongea huku nikitoa tanasamu la kifedhuli.

Tukakusanya vitu vyote na kuondoka mpaka mapokezi. Tukalipa hela nankuwaomba watuitie Taxi.

Dakika kumi baadae tulikuwa stendi kuu ya katikati ya mji. Tukaelekea mpaka upande wanaopaki Noah. Nikamvuta dereva mmoja pembeni.

“Nataka unipeleke Moro! Niko mimi na mkewangu tu.. Itakuwa shi ngapi?”

“Wawili tu peke yenu? Daah kibingwa tutafanya mia hansini bro”

“Acha ujinga sasa, mia hamsini wapi? Nakupa mia kamili”

Tukabishana bei hapo kama dakika tatu hivi, mwishoni tukakubaliana laki na ishirini.

“Nataka yendeshe kama umetoka kulazwa Mirembe jana.. Sasa hivi ni saa tatu na dakika ishirini, kabla ya sita kasoro nataka tuwe tumeingia Morogoro” nikamuelekeza nikiwa nafunga mlango.

“Usiwaze kaka mkubwa”

Siti za mbele tulimuachia dereva peke yake, mimi na Cheupe wangu tukakaa siti ya katikati.

Nikamlaza cheupe wangu mapajani alale usingizi aondoe uchovu wa shughuli ya jana usiku, pia na mimi mwenyewe nipate wasaa wa kutafakari mikakati ya namna tutakavyoweza kutekeleza mipango iliyopo mbele yetu.

.


Tulikuwa tumeshawasili Morogoro na nilimuelekeza dereva atupeleke moja kwa moja Chamwino stendi ya hiace.

“Dakika sifuri tu” nikawaaga nikitoka nje ya gari.

Niakenda moja kwa moja mpaka kwa wajamaa Fulani kama kumi hivi waliokuwa wamekaa kwenye mabenchi.

“Niaje wakuu” nikawasilimia.

“Poa Boss! Niaje” wakaniitikia.

“Poa kabisa! Nahitaji wadhamini.!” Sikutaka kuzunguka mbuyu, nikaenda moja kwa moja kwenye point yangu.

“Umepata Boss.! Unahitaji wadhamini wangapi, kesi inahusu nini na unawahitaji lini.?” Akaniuliza jamaa mmoja ambaye ni mtu mzima kidogo kuliko wenzake. Alikuwa na muonekano fulani hivi wa mfano wa wajamaa ‘wajuaji wajuaji’ uswahilini.. Mwenye amechomekea shati lake ambalo halijapigwa pasi.. Na chini amevaa viatu vyeusi vya ‘foengo’ ambavyo sijui vilikuwa na miezi mingapi havijapigwa kiwi.

“Kuhusu jina la ninayetaka mumdhamini, kesi yake, na maelezo mengine yote nimewaandikia humu” nikamkabidhi karatasi.

“Pia kuna namba hapo mwishoni mpigie huyo jamaa anaitwa Issack ndio atawalipa hela na maelezo mengine.. Nataka kesho tu huyu mtu awe uraiani so ni vyema muanze process zenu za barua leo.. Na hii hapa muweke vocha” nikazama mfukoni na kutoa noti mbili za elfu kumi na kumpa.

“Usijali boss! Limeisha hili” akaongea kwa kujiamini yule mzee, akazikunja noti na kuweka mfukoni.

Hakuniliza maswali kwanini nimekuja mimi kuwatafuta wao akafu nawaambia mtu mwingine ndio atakuwa nao kusimamia hilo suala, jamaa alikuwa ni mtoto wa mjini haswa.. Alinielewa kuwa nina sababu za kunifanya nisifuatilie hilo suala mimi mwenyewe.

.

“Twende ukatuache Roby Hotel” nikamuelekeza dereva baada ya kupanda kwenye gari.

“Roby Hotel ya mtaa wa mlapakolo?” Akauliza.

“Yes! Ni hiyo” nikamjibu.

Akatupekeka moja kwa moja mpaka kwenye Hoteli fulani ndogo iliyopo katikati ya mji mtaa wa mlapakolo.

Ilikuwa kama saa saba kamili hivi. Nikaona huj ni muda muafaka kabisa kwa sisi kutekeleza mpango wetu.

Tukiwa humo ndani hotelini, wote mimi na Cheupe tukabadili mavazi na kuvaa yale mabaibui cheupe aliyonunua Dodoma.

Tulivaa haya mabaibui katika mtindo ambao yalificha mwili mzima kasoro uso tu.

“Damn! I really hope Kaburj yuko hospitali” nikamueleza Cheupe huku najifunga vizuri kitambaa cha usoni.

“Kwanini una uhakika kuwa atalazwa?” Cheupe akauliza akiwa ameamua anisaidie kufunga kile kitambaa.

“Unajua kipigo cha askari magereza ni tofauti na kipigo cha mfungwa mwenzako.. Askari magereza anapiga kwa tekniki.. Wamefunzwa namna ya kupiga! Wanapiga kwenye vifundo miguuni, magotini na mikononi..!! Lakini kipigo cha mfungwa mwenzako hakina formula, tena ukizingatia kipigo cha Nyapara na waoambe wake.. Kwahiyo nina hakika kama Kaburi alifuata ushauri wangu wa Kumteteta Godi, basi leo atakuwa amelazwa hospitali kubwa ya Mkoa” nikamfafanulia.

“Aisee I hope Mme wangu haujavaa hili baibui bure.. Umependeza though hahahahah” akanitania.

“Acha ujinga hahah!” Nikamgonga kikonzi cha kimahaba.

Nikatoa simu moja kati ya zile sita na kuiwekea laini. Alafu nikampigia Issack.

“Hellow”

“Damn! Kichwa.. I was so worried.. Are you guys ok?”

“Tuko poa kabisa, sijui wewe Issack?”

“Niko poa kabisa.. Mko wapi?”

“Usijali kihusu hilo.. Vipi mazingira yakoje hapo home?”

“Hawa wasenge wananifuatilia aisee.. Kuna gari imepaki hapa nje iko tangu jana haiondoki”

“Ok! Wanafuatilia nyendo zako wanaamini at some point utakuja kuonana na sisi ili watunyakue.. Sasa skia nataka ufanye kitu kimoja…”

“Nakusikiliza kichwa.!”

“Chukua gari sasa hivi endesha mpaka msamvu.. Ukifika pale paki kwenye kituo cha mafuta cha Puma kisha wewe nenda kapande Hiace kwenda mjini.. Ukifika mjini panda hiace kwenda mzumbe.. Alafu ukifika Mzumbe tafuta sehemu upumzike kusubiri maagizo yangu.. Sawa Issack!”

“Nimekusoma kichwa”

Nikakata simu. Kisha nikavunja vunja simu na laini na kuviweka kwenye dustbin.

“Mzumbe unataka akafanye nini?” Cheupe akaniuliza.

“Haendi kufanya chochote!” Nikamjibu huku natabasamu.

“Whaaat?”

“Hao watu wanaomfuatilia kumbuka wanamfuatilia Issack sio gari… Kwahiyi nina uhakika akishuka kwenye gari na kuliacha pale wataendelea kumfuatilia Isaack mpaka mzumbe.. Na sisi tutapata gepu la kwenda kulichukua na ili tutumie katika hiki tunachoenda kukifanya.. Remember?? Misdirect. Confuse. Dialect.!!”

Nikamkonyeza na kutabasamu.

Tukabeba tena mabegi yetu mpaka reception ya Hoteli. Tukalipa na kuomba watuitie taxi.

Kama dakika saba baadae tulikuwa mbele ya geti la Hospitali kuu ya Mkoa.

Ujinga wa hapa huwa hawaruhusu magari kuingia ndani.. Kwahiyo ikabidi tuhonge elfu mbili kwa mlinzi ili haturuhusu alafu akatueleza tukiulizwa huko ndani kwanini ameturuhusu? Tujibu kwamba tunamchukua mama mzazi hali yake ni tete.

“Sawa! Na majeruhi huwa wanalazwa wodi ngapi?” Cheupe akauliza.

“Namba Tatu” akajibu mlinzi.

“Shukrani”

Tukaingia na gari mpaka ndani.

“Geuza gari kama tunatoka na usizime injini” Cheupe akamueleza dereva huku tunashuka.

Tukaelekea moja kwa moja mpaka wodi namba Tatu.

Japokuwa tulikuja hapa kufanya Jambo la hatari lakini moyo wangu ulilipukwa kwa furaha mara tu tukipokanyaga ndani ya wodi namba tatu.

Mwishoni kabisa mwa wodi, kitanda cha mwisho kabisa alikuwa amelazwa Kaburu na Nguo zake za kifungwa.

Alikuwa amefungwa pingu mkono mmoja na na kungwa kwenye kitanda.

Pembeni yake kulikuwa na kiti ameketi askari magereza mwenye bunduki.

Nikatabasamu na kumnong’oneza Cheupe.

“Its show time.!!”

Baada ya kuingia tu wodi namba tatu, nikaishika vizuri Kamera yangu ya Kodak kujiandaa na ninachotaka kukifanya.! Nikaibonyeza pale kwenye button ya kupigia picha, nikaanza kusikia ikipiga mluzi hafifu kwa mvali “siiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii”.. Ilikuwa inakusanya ‘chaji’ ili iweze kuachia umeme..

Nikaanza kutembea kwa haraka kuelekea mwisho wa wodi kwenye kitanda cha mwisho kabisa ambacho alikuwa amelazwa Kaburu na pingu mkononi.

Cheupe alikuwa ananifuata nyuma yangu.

Yule askari alikuwa bado amekaa kwenye kiti akituangalia tunavyokuja.

Kadiri tulivyokuwa tunamkaribia alizidi kutukazia macho, mpaka tukawa tumemkaribia karibu kabisa.

Kadiri tulivyokuwa tunamkaribia huyu askari sura yake nikaanza kuikumbuka. Huyu ndiye yule askari magereza mtemi aliyekuwa anatupekua siku yangu ya kwanza nilipopelekwa gerezani. Ni huyu askari ambaye aliniambia nibong’oke ili anipekue matakoni. Ni askari huyu ambaye nilipokataa alinishamhulia kwa makofi, ngumi na vifuti vya tumbo.

Hatimaye leo ameingia kwenye ‘anga zangu’.! Nikatabasamu na kujisemea kimoyo moyo, “karma is a bitch”

“Hey amruhusiwi huku” akaongea yule askari huku anainuka kwenye kiti.

“Tunaomba picha” Cheupe akamueleza huku mimi nimeinua mkono kumuonyesha kamera bila kusema neno lolote. Sikutaka sauti yangu ya kiume kusikika kuepuka kushtukiwa.

“Hamruhusiwi kupiga picha hapa” yule askari akaongea huku anaanza kunisogelea.

Kidole changu bado kilikuwa kimebonyeza button ya kamera na kwa mbali bado nilikuwa nasikia mlio ikijichaji.

“Picha moja tu!” Cheupe akaongea tena.

“Nimewaambia hakuna kupiga picha” akaongea kitemi yule askari magereza huku anazidi kunisogelea.

Akafanya kosa.

Akanininyokshea mkono ili anisukume kifuani. Kabla mkono haujanifikia nikainua kamera na kumgusisha vile vimoguu viwiki vya nyaya.

“Paaaaaaaaaaaaaaaaaa” mlio mkali wa shoti ya umeme ukalia.

“Mamaaaaaaaaaaaaaaaaaa” yule askari alitoa mlio mmoja tu wa kilio na kudondoka chini na kuanza kupapalika kama mtu mwenye kifafa au mwanamke aliyefika kileleni.

“Ole wake mtu yeyote hata atingishike” Nilimsikia Cheupe anaongea kishujaa kwa sauti ya juu.

Nikageuka kumuangalia. Sijui alikuwa amepaa au ametembea kwa kasi gani, lakini alikuwa amesimama ule tukioingilia.

Uzuri wa hii wodiilikuwa na mlango mmoja tu.

Cheupe hakuwa ameshika kitu chochote, lakini ule mkwara aliowapiga na jinsi tulivyomzimisha huyu askari hakuna mtu ndani ya wodi aliyesogea hata hatua moja. Walibaki wamegansa kama sinema imewekwa “Pause”!

Nikamgeukia tena yule askari anaye gara gara pale chini.

“Hii kwa ajili ya kutaka kunipekua na mingumi uliyonipiga siku ile” nikamgusisha tena vimiguu miwili shingoni. Akapaparika kama kuku bila kutoa sauti. Alikuwa amezirau tayari.

Nikainuka na kumrushia kamera cheupe kama tunacheza marede. Cheupe akaidaka alafu akawanyooshea watu mle wodini kama vile ni bastola.

Tungekuwa tupo kwenye mazingira mengine, lazima ningeangua kicheko kwa huku kujitutumua kwa Cheupe.

Nikamgeukia tena yule askari magereza na kuanza kumshachi mifukoni. Nikazipata funguo.

“Wow wow wow! You full of suprises dogo!” Kaburu akaongea nikiwa namfungua pingu mkononi.

“Shut the **** up!” Nikamfungua pingu.

Nikamnyanyua kutoka kitandani.

Alikuwa anatembea kwa kuchechemea kidogo, hivyo ikanibidi nimuweke mkono wake mmoja kuzunguka mabega yangu ili nimepe ‘sapoti’ kutembea.

“Taratibu dogo” Kaburu akaongea huku anagugumia maumivu.

Nikamtembeza haraka haraka mpaka kutoka nje ya wodi. Cheupe naye akatufuata na kwenda kufungua mlango wa nyuma ya gari kwa haraka.

Nikaingia na Kaburu siti ya nyuma na Cheupe akazunguma akapanda siti ya mbele.

“Eeeeeeeeehh vipi tena” dereva akang’aka huku anamshangaa Kaburu. Naamini alikuwa anamshangaa zile Nguo zake za kifungwa.

“Endesha gari kum* weweeee” nikamfokea na kumtukana kitemi.

Dereva akashtuka kusikia sauti ya kiume ikitoka kwenye baibui. Tangu atuchukue hotelini ni cheupe ndiye ambaye alikuwa anaongea naye. Mimi nilikuwa kimya muda wote.

Naamini aliposikia sauti ya kiume inaongea kutoka kwenye baibui akaelewa hii ni “ishu siriazi”.!

Akang’oa gari kwa haraka tukatoka hospitalini.

“Tunaelekea wapi?” Dereva akauliza kwa woga.

“Msamvu, na nataka uendeshe kwa spidi zote” nikamuamuru.

“Wow! Sikutegemea kama utafanikiwa dogo” Kaburu akaanzisha maongezi.

“Nimekwambia funga mdomi wako” nikamfokea na yeye. Sikutaka aongee chochote mbele ya huyu dereva.

Nikavua tisheti yangu avae juu na avue ile shati ya magereza ya rangi ya chungwa.

Dakika tano baadae tulikuwa Msamvu. Tukashuka kwenye gari. Cheupe akatoa kwenye gari mabegi yetu yale mawili, begi la mgongoni na begi begi kubwa, kisha akampa dereva noti mbili za elfu kumi kumi.

Yuke dereva akapokea huku ametoa macho hakudhani kama “majambazi” sisi tungemlipa.

Tukamsubiri dereva Taxi alipoondoka na kutokomea ndipo tukavuka bara bara kuelekea kituo cha mafuta cha PUMA.

“Unajua hata usingemlipa hela wala asingetudai nauli kwa jinsi akivyoshikwa na hofu” nikamwambia cheupe huku natabasamu tukiwa tunavuka bara bara.

“We are not thieves Ray!!” Cheupe akanishushua.

.

Nikaliona mahala ambapo Issack alikuwa amepaki gari.. Tukatembea kulifuta.

Tulipolifikia, tukaweka mabegi yetu, tukapanda ndani. Nikakaa kwenye usukani, Kaburu akaa siti ya mbele pia na Cheupe akakaa siti ya nyuma.. Nikang’oa gari kwa mwendo wa kasi tukaondoka.

Nikaendesha kwa kasi kama tunaelekea Dar es salaam mpaka kmtukafika maeneo ya Nane Nane kwa mbele kidogo kwenye Chuo kikuu cha Jordan kuna barabara inachepuka kutoka barabara kuu kwenda chuoni, nikaifuata barabara hiyo.

Mbele kidogo nikapaki gari pembeni.

“Ok! Nadhani nimeshatimiza wajibu wangu, now its your turn!!” Nikaongea nikimuangalia Kaburu.

“What unamaana gani?” Kaburu akaongea kwa mshangao.

“Tulikubaliana nikutoroshe gerezani, na nimekutorosha gerezani!! Now its you turn kunipa taarifa kuhusu The Board” nikafoka huku nimemkazia macho.

“Tulikubaliana pia unisaidie kuzipata documents zangu ambazo zimechukuliwa na Obama” Kaburu akoangea kwa hofu na hasira.

“Yeah nitakusaidia ila kabla ya hapo nahitaji taarifa kuhusu The Board”

“Ray documents Obama ameziiba toka jana na tukichelewa zinzweza kufika mikononi mwa The Board na wakiziona hakuta kuwa hata na maana ya mimi kuwa uraiani.. Sacrifice yangu yote ya kukubali kukaa jela miaka miwili yote hii itakuwa haina maana.. Kwa ufupi hizo documents zina mambo Mengi na zina taarifa kuhusu alipo Veronica” Kaburu akaongea wa hofu iliyochabganyika na hasira.

Nikaona huyu anataka kuniletea ujinga..

“Sikiliza Kaburu, nimevunja Sheria za nchi, nimehatarisha maisha yangu, nimehatarisha maisha ya mpenzi wangu na nimehatarisha uhai wa mwanangu… Usianze kuniletea ngonjera!! Unanijua nikiamua kuwa Mafia ni nini naweza kukifanya.. Hizo documents tutazitafuta!! Nipe taarifa za The Board!!” Nikafoka kwa hasira mpaka natetemeka.

“Ray pleeeaase! Naomba uelewe.. Maisha ya veronica yako hatarini mpaka muda huu!! Najua nikikupa taarifa unazotaka huwezi kujisumbua tena kusisaidi.! Please Ray.. Tusaidiane tupate hizi documents.!”

Kaburu akaongea kwa sura ya huruma kabisa mpaka imani inaanza kunijaa.

“Ok! Ok… Ok! Unamfahamu vipi Obama?? Jina lake na mengineyo.?” Nikamuuliza huku nachukua begi dogo la mgongoni kutoka siti ya nyuma na muanza kupekea pekua nikitafuta moja ya zile simu nilizonunua Dodoma.

“Aaaah jina lake hakisi anaitwa… aaah… anaitwa Rashidi… Rashidi aaah Rashidi Namahal! Yes Rashidi Namahala… Pale gerezani alihamishiwa kama mwaka na nusu uliopita! Sijajua alitokea gereza gani ila kama mwaka na nusu uliopita alihamishiwa pale… Kwa hiko kilichotokea na amini alipandikizwa pale na The Board ili afuatilie nyendo zangu.

“Ok.!” Nikamjibu kwa kifupi huku naweka line kwenye simu mojawapo ya zile nilizonunua.

“Unataka kumpigia nani?” Kaburu akauliza kwa wasiwasi.

“Nataka nimpigie mtu wa Usalama wa Taifa naamini wao wanarasilimali watu wa kutosha na ujuzi wa kudili na hili suala” nikaongea huku nawasha simu.

“No no no no! You can’t do that.. Ukiwapigia simy na wakizitia mkononi hizo documents wakaona mambo yaliyo ndani ikiwemo location ya Veronica lazima watawasiliana na Idara ya Ujasusi ya Rwanda na wakifanikiwa kumpata Veronica lazima watamfunga gerezani kwa kuasi Idara na ncho yake!”

“Skia Kaburu! Nadhani ni bora walau kama ikitokea bahati mbaya Veronica akatupwa gerezani ina afadhali kuliko The Board wakikuwahi na kumtia mikononi, lazima watamuua!! So namba ukubaliane na hili, Usalama wa Taifa ndio watu sahihi wa kudili na hii ishu.. Wana uwezo wa kumtrace Obama kwa haraka zaidi na kuzipata hizo documents!! Ok??”

Kaburu akavuta pumzi ndefu na kuishusha. “Ok! Do it.

Nikabofya bofya simu na kisha nikabonyeza kitufe cha kupiga. Kama sekunde ishirini hivi simu ikapokelewa.

“Hallo”

“Halo”

“Ray hapa”

“****! Kwanini unanipigia simu si tulikuambia ukitaka tuonane unatakiwa ufanyaje?” Baba bite aliongea upande wa pili wa simu.

“Yeah nakumbuka ila ni suala urgent ndio maana nimepiga simu”

“Kitu gani?? Na nimepewa taarifa na watu wetu wa Morogoro kuwa Kaburu ametorshwa gerezani leo!! Vipi unahusika na hilo??”

“Thats not importnat na naomba mjitahidi hizo habari mzidhibiti zisitokee kwenye media!!”

“Na kwanini tukusaidie kiasi hicho??”

“Kwa sababu ndani ya masaa machache yajayo naweza kuwa na mafaili yenye siri zaa The Board mkononi mwangu”

Baba bite akakaa kimya kwa sekunde kadhaa. Nilihisi hii habari ya mimi kuwa karibia kuoata files za The Board jinsi ilivyomkuna.

“Ok! Unakata nini?” Hatimaye akauliza.

“Kuna askari magereza pale gereza kuu la Morogoro anaitwa Rashidi Namahala au maarufu kama Obama! Jana kuna documents alitakiwa azifiishe mahali lakini kwa makusudi akabadili hizo documents na kuweka nyingine na zile documents halisi bado yuko nazo.. Sasa imani yangu ni kwamba huyu ni kibaraka wa The Board na hizi documents zitaleta kizaazaa kikubwa kikubwa sana.. Kwahiyo naomba mtumie kila mbinu mliyo nayo kumnyakua huyu bwana na kumbana awape hizo documents kabla hazijafika sehemu zisipotakiwa na naomba ukizipata unikabidhi mimi kwasababu zinahusu masuaka binafsi na sidhani kama zitakuwa na faida kwenu huko kwenye Idara.” Nikamfafanulia kwa mapana.

“Ok! Ngoja niwasiliane na watu wa Morogoro” akanijibu.

“Na naomba mkizipata hizo documents unisaidie kitu kimoja.. Ndani yake zinaweza kuwa na taarifa nyeti kuhusu mtu Fulani ambaye anatafutwa na marafiki zenu wa Rwanda.. Naomba ufahamu kuwa mtu anayetusaidia kupta mafaili ya The Board anafanya hivi ili kulinda usalama wa mtu huyo anayetamaniwa na wenzenu wa Rwanda.. Lakini sidhani kama ni interest ya Taifa la Tanzania kusaidia taifa la kigeni kudili na ‘mizimu’ yao.. Kwahiyo naomba utumie busara zako zote na huruma zako zote kulinda usiri wa hiyo taarifa mtayoipata.. Najua interest yenu kwenye hii ishu ni kupata mafaili ya The Board.. Naomba hilo ndilo libaki kuwa lengo kuu moyoni mwako.”

Nikaongea kwa mafumbo na busara zangu zote ili kubembeleza huruma ya Baba bite akinde taarifa kuhusu Veronica zisiwafikie Idara ya Ujasusi ya Rwanda.

Nikakata simu. Kisha nikaivunja vunja na kuitupa.

“Ok! Naamini ndani ya masaa kadhaa watakuwa wamemnyakua! Now its you turn Kaburu!! Napataje hizo files za The Board?”

Kaburu akashusha pumzi kwa nguvu.

“Ok! Unakumbuka nilikwambia kuwa kumbukumbu zote za The Board haziwekwi kwenye mifumo wa kompyuta, kwamba taarifa zote zinatunzwa kwenye hardcopy ili kuepuka udukuzi??” Akaniuliza.

“Yes, nakumbuka!” Nikamjibu nikiwa na shauku kubwa.

“Now, kama nilivyokwambia kuwa mtunza kumbu kumbu huyu ambaye The Board wanamuita Book Keeper, ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRBB Bw. Vincent Mallya.. Na kumbu kumbu hizi anahakikisha ziko naye muda wote haziondoki kwenye uwepo wake” akaongea huku anafumba macho na kuangalia juu.

“Sijaelewa una maana gani??” Nikauliza tena kwa shuaku kubwa zaidi.

“Namaanisha documents ziko na Vincent Mallya muda wote”

“Sikuelewi Kaburu”

Akavuta tena pumzi ndefu ndani na kuishusha kwa nguvu.

“I cant believe that am telling you this” Kaburu akafumba macho kwa nguvu kwa woga.

“Stop playing around! Where are those damn files??” Nikafoka kwa shauku.

ITAENDELEA

Vipepeo Weusi : Mkakati Namba 0034 Sehemu ya Nne

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment