Sikuachi Baby Sehemu ya Kwanza
CHOMBEZO

Ep 01: Sikuachi Baby

SIMULIZI Sikuachi Baby
Sikuachi Baby Sehemu ya Kwanza

IMEANDIKWA NA: JUMA HIZA

*********************************************************************************

Chombezo: Sikuachi Baby

Sehemu ya Kwanza (1)

Ilikuwa ni siku ya jumamosi majira ya saa kumi kamili za jioni, hali ya hewa ilikuwa ni ya mvua ya wastani sanjari na baridi kali. Nilikuwa ndani ya chumba changu nimejilaza kitandani huku nikiwa nimejifunika mashuka mawili kwa mpigo nikiamini hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee ya kupambana na baridi iliyokuwa ikiendelea kunitafuna mifupa lakini haikuwa kama nilivyokuwa nikidhani, baridi ile iliendelea kunishambulia vilivyo.

“Aaagghh, hii baridi nayo,” niling’aka kisha nikajisemea maneno niliyoyasindikiza na tusi mubashara. Hiyo ilikuwa ni kawaida yangu hasa pale lilipotokea jambo la kunikwaza nilikuwa mwepesi sana wa kutukana.

Licha ya tabia yangu hiyo ambayo naweza kuiita ilikuwa ni tabia ya kipumbavu lakini nilijaaliwa kuwa miongoni mwa vijana ambao walisifika sana kuwa wapole na heshima.

Sijui ni nini kilitokea ila nilijikuta nikipokea sifa kedekede kutoka kwa ndugu, jamaa pamoja na majirani niliyokuwa nikiishi nao, walikuwa wakinisifu juu ya upole wangu ati! Mwenyezi Mungu alinibariki muonekano wa upole na kila mtu alivutiwa na upole wangu.

Kwa kweli sifa ambazo walikuwa wakinisifia hazikuendana kabisa na mimi, kuna kipindi nilikuwa nikihisi labda walikuwa wakinikejeli hii ni kutokana na tabia chafu zilizokuwa zimejificha ndani yangu, hakukuwa na mtu aliyekuwa akinifahamu undani wangu, sifa za upole zilizokuwa zimetawala pale mtaani nilipokuwa nikiishi zilinisaidia kuficha maovu niliyokuwa nikiyafanya nyuma ya pazia na hiyo ndiyo ilikuwa sababu kubwa iliyochangia mpaka watu wasifahamu kile kilichokuwa kikiendelea katika maisha yangu.

Labda nikuambie kitu ndugu msomaji mbali na sifa zangu za upole zilizokuwa zimetawala kila kona lakini nyuma ya pazia kulikuwa kuna mambo yalikuwa yakiendelea yasirisiri ambayo hakukuwa na mtu ambaye alikuwa akiyafahamu.

Nilikuwa nikifanya kazi ya udereva wa bodaboda kazi ambayo ilinifanya nikutane na wasichana wengi sana ambao mwisho wa siku nilikuwa nao kimapenzi, miongoni mwa hao wasichana niliyokuwa nao kimapenzi mwisho wa siku wamefanya niwe kilema, niishi maisha ya kukisubiri kifo changu kwa maana siwezi tena kutembea wala kufanya lolote.

Kila nikikumbuka yale niliyoyafanya nyuma katika maisha yangu kwa kweli kuna muda nakiri kuwa hata kwa ukilema huu niliyokuwa nao ni haki yangu kabisa wala sitakiwi kumlaumu mtu yoyote yule.

Japo nimeamua kukusimulia kwa mfumo wa chombezo lakini naomba unifuatilie kwa umakini kuna vitu naamini utajifunza na kama kuna sehemu itatokea nitakuwa nimekukwaza basi utanisamehe bure.

Tuendelee na chombezo letu…..

Wakati mvua ikiendelea kunyesha huku baridi nayo ikiendelea kunishambulia nikaamua kuamka kwa ghadhabu pale kitandani, uso wangu nilikuwa nimeukunja vilivyo kwa hasira zilizokuwa zimenijaa kichwani.

Tatizo kubwa lililokuwa likiniweka katika hali hiyo ilikuwa ni mvua iliyokuwa ikinyesha, ilikuwa ikinizuia kwenda kumchukua mteja wangu aliyekuwa akijulikana kwa jina la Samira. Nilikuwa na kazi ya kumpeleka kila siku kazini kwake maeneo ya Posta na kumrudisha nyumbani kwake Tandika Azimio, alikuwa akinilipa kwa siku.

Niliamini kwa mvua ile iliyokuwa ikiendelea kunyesha bila kuwepo dalili zozote za kukata basi niliamini nilikuwa nikienda kuikosa hela ya Samira msichana ambaye nilikuwa nikiishi naye mtaa mmoja.

Niliichukua simu yangu aina ya Tecno R6 nikaiwasha, nikaitoa pattern kisha nikaingia katika uwanja wa kuandika ujumbe mfupi, nilikuwa nikimuandikia ujumbe Samira.

“Mambo my.”

“Poa Metusela niambie.”

“Kama kawa vipi bado uko kazini?”

“Ndiyo nakusubiri sikuoni.”

“Na mvua hii nakujaje sasa?”

“We njoo hivyo hivyo bhanaa.”

“Au uchukue bajaji?”

“Bajaji sitaki.”

“Au daladala.”

“Sitaki pia.”

“Unataka nini?”

“Nataka uje unichukue na pikipiki yako.”

“Jamani sasa nitakujaje huko?”

“Wewe tafuta njia yoyote ya kuja mimi siondoki mpaka uje unichukue,” alinitumia ujumbe huu Samira kisha huo ndiyo ulikuwa mwisho wa chatting zetu.

Mpaka kufikia wakati huo nilikuwa nimeshapagawa, sikujua nilitakiwa niende vipi mpaka posta kwenda kumchukua, nilipoitazama saa yangu ilikuwa ni saa kumi na nusu. Nilizidi kuwa katika hali ile ya ghadhabu huku kila wakati nikichungulia nje kutazama kama mvua ilikuwa imepungua.

Kama utani vile ilipofika saa kumi na moja kasoro dakika tano hatimaye mvua iliweza kukata, sikutaka kupoteza muda tena nilichukua koti langu nikalivaa kisha nikatoka nje nikaielekea pikipiki yangu na sasa safari ya kwenda posta nikaianza.

Barabarani nilikuwa nikiendesha pikipiki lakini nilikuwa nikiufikiria ule uzuri aliyokuwa nao Samira, moyoni sikutaka kuamini kama kweli alikuwa bado hajaolewa maana alikuwa ni msichana mrembo haswaaa.

Alikuwa na sura ya kuvutia, macho legevu ya kurembua, kifua chake kilibarikiwa chuchu za kusimama mithili ya ncha ya mkuki, umbo lake lilikuwa limejengeka vyema na kuunda namba nane. Alivutia mno kutazama si kwa nywele zake ndefu alizokuwa amezifunga kwa nyuma, mwendo wake wa maringo wala kwa sauti yake laini ya kubembeleza.

Kwa mwendo wa dakika kumi nilikuwa tayari nimeshafika Posta nje Kampuni ambayo alikuwa akifanya kazi Samira, nikampigia simu kumjulisha kuwa nilikuwa nje kwa wakati ule nikimsubiri, haikuchukua sekunde akaweza kutoka nje.

Alikuwa amevalia mavazi yake ya kiofisi, sketi nyeusi fupi iliyoyaacha vyema mapaja yake wazi kwa juu alivalia T-shirt nyeupe iliyokuwa imeandikwa jina la kampuni yake kwa maandishi ya rangi nyeusi.

“Umenisubiri sana?” nilimuuliza alipokuwa amesimama mbele ya pikipiki yangu aina ya Boxer huku akiwa amekishikilia kiuno chake kilichokuwa kimebonyea kwa ndani mithili ya kiuno cha mdudu nyigu.

“Ndiyo nimekusubiri sana muda mrefu yani mpaka nikakata tamaa,” aliniambia Samira kwa suti ya kudeka.

“Tatizo ni mvua yani isingekata sijui ingekuwaje?”

“Na mimi nisingeondoka kabisa ofisini.”

“Kisa nini?”

“Hujaja kunichukua,” aliniambia kisha nikacheka.

Niliendelea kuutazama uzuri wa Samira na kila nilipokuwa nikiyapeleka macho yangu kwake nilizidi kukiri alikuwa ni mrembo kupitiliza.

“Kumbe mpaka jumamosi unaingia ofisini?” nilimuuliza.

“Hapana kuna kazi zilibaki jana leo ndiyo nimezimalizia,” alinijibu.

“Hapo sasa nimekuelewa vipi twende zetu sasa maana hili wingu jinsi lilivyofunga muda wowote mvua itashuka tena,” nilimwambia.

“Usijali Metusela ila nahisi baridi sana unaweza kuniazima koti lako?” aliniuliza.

“Hakuna shaka,” nilimwambia halafu nikavua koti langu nikampatia kisha akalivaa baada ya hapo akapanda kwenye pikipiki kisha tukaondoka zetu.

                                           ****

Nilimfikisha nyumbani kwake salama salimini jambo ambalo lilimfurahisha sana, alipenda sana kunisifia kutokana na uhodari wangu katika kuendesha pikipiki kisha akaichukua pochi yake akatoa hela halafu akanilipa kama ilivyokuwa kawaida yake.

Nilimshukuru sana lakini ajabu hakupendezewa na kitendo kile, aliniambia kuwa sikutakiwa kufanya vile mbele yake kwani kile alichokuwa akinipa kilikuwa ni haki yangu yani jasho langu hivyo sikutakiwa kumshukuru sana.

“Oooh, halafu nilitaka kusahau,” aliniambia huku akionekana kusahau kitu.

“Ulitaka kusahau nini?” nilimuuliza.

“Koti lako halafu nimejisahau kabisa nimelifanya kama langu.”

“Usijali hilo naweza kulichukua siku yoyote,” nilimwambia kisha sikutaka kupoteza muda nikamuaga halafu nikaondoka eneo lile.

Nilipofika nyumbani kwangu bado niliendelea kuteseka na hisia za mapenzi ambazo zilianza kuniingia ghafla! moyoni, nilijikuta nikiutumia muda mrefu sana katika kumfikiria Samira msichana ambaye nilitokea kumpenda sana.

Sikujua nilitakiwa kuanzia wapi kumueleza ukweli wa siri iliyokuwa ikinitesa moyoni, nilimpenda sana na nilitamani alifahamu hilo.

Wakati nilipokuwa nikiendelea kumuwaza nikaichukua simu yangu nikaingia whatsApp na kitu nilichoamua kukifanya ni kulitafuta jina lake na kuanza kumuangalia profile picha ambayo alikuwa ameiweka. Alikuwa ameweka picha aliyopiga kipindi yupo kazini.

Nikazidi kudata na muonekano wake uliyonivutia kupitiliza. Picha yake ilionekana nusu tena akiwa amekaa, ilianzia kumuonyesha sura yake mpaka usawa wa mapaja yake. Nikamtazama kwa umakini kila kiungo chake nilichokuwa nikikiona katika picha hiyo, alikuwa amekaa hakika alinivutia mno.

Hali ya hewa bado ilikuwa ni ya ubarini iliyohamasisha sana kufanya mapenzi, nilizidi kumtazama Samira pichani na hakukuwa na kitu kingine nilichokuwa nikikifikiria zaidi ya mapenzi. Hisia za mapenzi zilizonijia zilikuwa ni juu yake na hata katika upande wa kifikra nilimuwaza yeye.

Wakati nilipokuwa nikiendelea kumuwaza Samira ghafla! Simu yangu iliingia ujumbe mfupi, nilipoufungua na kuusoma ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Sesilia msiichana ambaye nilikuwa katika mahusiano naye ya kimapenzi, alikuwa amenitumia ujumbe wa kunijulia hali lakini kutokana na chuki nilizokuwa nazo juu yake sikutaka kumjibu lolote.

“Metu mpenzi wangu vipi uko salama?” alinitumia ujumbe mwingine ambao sikutaka kuujibu hata aliponipigia simu pia sikutaka kupokea.

Nilimchukia sana Sesilia, nilimfanyia kila aina vituko, kila siku tulikuwa tukiingia katika mgogoro ambao chanzo kilikuwa ni mimi. Hakukuwa na usalama wa penzi kila siku nilikuwa ni mtu wa kuwaza kumkwaza, nilikuwa tayari nimemchoka na hii ndiyo sababu iliyonifanya mpaka hisia zangu za mapenzi nikazihamisha kwa msichana mwingine.

Alikuwa ni Samira msichana mrembo ambaye niliamini siku moja nitampata na angeweza kuufurahisha moyo wangu ambao ulikuwa tayari umeshamtamani. Niliamini kushinda katika hilo hivyo sikuwa na shaka hata kidogo.

Huyu Sesilia ambaye ni mpenzi wangu mwanzoni kabla ya uhusiano wetu alikuwa ni abiria wangu kama walivyokuwa wengine. Nakumbuka niliwahi kumpeleka sehemu nyingi sana ambazo alikuwa akihitaji nimpeleke na alikuwa akinilipa.

Hakukuwa na mazungumzo mengine kati yetu zaidi ya udera na uabiria. Alikuwa ni msichana ambaye alionekana kuwa na msimamo sana pia alikuwa akijiheshimu hata katika upande wake wa mavazi alikuwa akivaa nguo za heshima ambazo zilimuweka katika muonekano wa kuheshimika kila wakati.

Macho yangu ya matamanio kwa wasichana hayakuacha kumtamani Sesilia ambaye nilimuingilia na gia ya kumuoa kabisa endapo angeweza kunikubali na kunikabidhi moyo wake wa mapenzi.

Nilianza na kumpa ofa ya kutonilipa pesa yake pale ambapo alihitaji usafiri wangu na hii ndiyo ilikuwa kama kilainishi cha kumfanya azidi kuniona nampenda sana.

Kama utani akaweza kunikubalia ombi langu na akazidi kuleweshwa na ahadi zangu za kutaka kumuoa kabisa. Sikutumia nguvu nyingi sana ya kumpata Sesilia bali ni akili na utundu fulani kidogo niliutumia.

Washikaji zangu wengi ambao nilikuwa nafanya nao kazi hii ya udereva wa bodaboda walishindwa kuelewa kwa kile kilichokuwa kikitokea katika maisha yangu, kumiliki watoto wazuri kila siku na kila msichana niliyekuwa naye alikuwa akimzidi mwenzake kwa uzuri. Waliamini nilikuwa natumia kizizi katika kuwang’oa wasichana wazuri jambo ambalo halikuwa na ukweli ndani yake.

Kichwani nilikuwa nimenyoa kiduku huku ukifuatiwa na muonekano wangu wa kawaida ambao ulisindikizwa na utanashati, nadhani hii pia ilikuwa ni sababu nyingine ilyowafanya wasichana wavutiwe na mimi. Sikuwa ni mtu wa kuongea sana kwanza nilikuwa nina aibu sana hata lilipofikia suala la kumueleza ukweli msichana nilipata kazi kubwa mno lakini mwisho wa siku mambo yalikuwa katika mstari.

Nilikuwa katika mapenzi na Sesilia huku akijaribu kuwa msichana wa tofauti sana katika maisha yangu, alikuwa akijaribu kunibadilisha kutokana na muonekano ambao nilikuwa nao, hakuupenda hata mara moja na kila wakati nilipokutana naye ulikuwa ni kama wimbo wataifa, alinisisitiza sana nijiweke katika muonekano wa kuheshimika.

“Sipendi hata mara moja jinsi unavyojiweka Metu,” aliniambia Sesilia huku akiwa ameukunja uso wake. Nilifahamu alikuwa amechukia hivyo nilitafuta maneno ya kumwambia ile niweze kumuweka sawa, wakati huo alikuwa amenifuata ghetto majira ya usiku.

“Usinune mpenzi unajua najiweka hivi ili kuvutia abiria wapende kupanda pikipiki yangu au hupendi mumeo nizidi kupiga pesa kila siku?” nilimwambia kwa sauti ya upole kisha nikamuuliza swali ambalo niliamini jibu lake ni ndiyo.

“Napenda lakini mimi sipendi hivyo unavyojiweka,” alinijibu.

“Usijali basi nitabadilika siunajua mimi ndiyo mumeo?”

“Ndiyo najua.”

“Basi usininunie.”

“Sawa sikununii tena,” aliniambia.

Kwa muda ambao alikuwa amenifuata ni wazi kuwa kuna kitu alikuwa akikihitaji na hakukuwa na kitu kingine zaidi ya mapenzi. Nililifahamu hilo kutokana na machejo aliyokuwa akiyaleta.

Alianza kunitekenya pale kitandani tulipokuwa tumekaa huku akizidi kujivuta na kuwa karibu na mimi. Tukaanza kucheza ile michezo ya kitandani ya kukumbatiana, kupapasana huku tukibadilishana mate yasiyokuwa na idadi.

Sesilia uvumilivu ulimshinda mwisho akaanza kunitoa nguo moja baada ya nyingine, nikabaki mtupu akanitazama kwa macho yaliyogubikwa na aibu kisha hapo hapo akauelekea mtarimbo wangu uliyokuwa umesimama wima kama nguzo ya umeme.

Kitendo kilichofuata mahali hapo alianza kuunyonya mtarimbo wangu mithili ya mtu aliyekuwa akinyonya koni au lambalamba, alihakikisha kila eneo analipitia vyema kwa ulimi uliyotambaa taratibu na kuniacha katika msisimko wa hali ya juu.

Wakati huo nilikuwa bado sijachojoa nguo zake, alipofikia wakati wa kutembea na ulimi mwilini mwangu hakika sikutaka kuendelea kuwa shuhuda wa kushuhudia sinema ya ngono ambayo mwisho wa siku ningeweza kuwa msimuliaji.

Nilianza kumchojoa nguo zake na mara baada ya kumaliza sikutaka kuremba mambo nilimkamata na kumlaza chali kitandani kisha nikayapanua mapaja yake yaliyokuwa yamenona kiasi.

Nilipata wasaa wa kutalii katika mwili wake uliyokuwa umegubikwa na kila aina ya kiungo kilichokuwa kikiniita. Niliutazama mdomo wake mpana wa kunyonya, shingo yake, kifua chake, tumbo lake, kitumbua chake, mapaja yake pamoja na miguu yake.

Nilitaka kumuonyesha ufundi na ustandi niliyokuwa nao katika kufanya mapenzi, kwa wakati ule ambapo alikuwa amelala chali kitandani nilipaga kuanzia kwenye nyayo zake kupanda kwa juu.

Nilitumia viganja vyangu katika kumpapasa nyayo zake, kitendo hicho kikamfanya atokwe na kicheko huku akijirusharusha pale kitandani, nikaanza kupanda taratibu kwa kutumia viganja vyangu na nilipofika katika kitumbua chake niliamua kuweka kambi kidogo, kama unavyojua tena sehemu hii ndipo panapotoaga watu roho, nikaamua kutumia upole, nikaanza kupasugua taratibu huku nikimtazama usoni Sesilia, alionekana kunogewa mwisho akaanza kutokwa na sauti za miguno ya ajabu ajabu.

“Metu nahitaji please, ingizaaa,” aliniambia kwa sauti iliyokosa uvumilivu na mimi kwa masifa sikutaka kuingiza mapema nikazidi kutembelea kiungo kimoja baada ya kingine, nilipanga kumkoleza na utamu wa penzi ambalo niliamini hakuwahi kulipata mahali popote pale.

Niliendelea kupanda kwa juu taratibu mpaka pale nilipofika mdomoni na kuanza kubadilishana naye mate. Alikuwa amelegea mwili mzima, nikazidi kupata upenyo wa kufanya lolote na kila nilivyomuweka alijiweka kama nilivyotaka.

“Metu please naomba unipee njoo ingizaa naumiaa,” aliniambia kwa sauti ya kunong’ona huku akitokwa na mihemo. Alichokuwa akikihitaji ni mechi dhidi yangu na yeye.

Niliporidhika kuwa nilifanikiwa kumlainisha kila sehemu ya mwili wake sasa nikaamua kuingia uwanjani huku nikiwa nimejipanga kwa kushindana na timu pinzani.

Wakati Sesilia akiwa katika staili ya kulala chali, taratibu nilianza kumuingiza mchezaji wangu uwanjani, sikutaka kuweka mbwembwe sana, niliamini kuwa mshindi katika mchezo huo.

Alianza kutokwa na miguno ya utamu kipindi mchezaji wangu alipokuwa akiingia. Miguno yake ikanifanya nianze kupandisha wazungu weupe lakini nilijitahidi kuwazuia wasitoke mapema, niliogopa kuonekana dhaifu wa mchezo.

“Ooooh, Aaaaaiiisshhhh tamuuu tamuuu Metuuu ingiza yoteeee,” alizidi kutokwa na miguno ya kimahaba.

Mchezaji wangu alipofanikiwa kuingia ndani ya uwanja nilitokwa na mguno wa msisimko niliyokuwa nimeupata. Nikaanza kumchezesha huku nikijitahidi kukaba kila kona na nilikuwa katika kasi ya ajabu sana, nilikuwa namuingiza ndani na kumtoa nje, kama muda wa dakika tano nikawa tayari nimesha funga goli lisilokuwa na kasoro yoyote, goli la dume la mbegu.

“Ooooohh Babyyyy aaaaaahhhh nimwagiee ndani mwaga babyyyy,” alisema Sesilia huku akitokwa na miguno ile ile ya kimahaba, alikuwa amenikumbatia kisawasawa.

“Tayari babyyy,” nilimwambia huku nikigugumia kiume, nilikuwa nimepandwa na mizuka.

Mchezaji wangu hakuonekana kuchoka hata kidogo na baada ya kumaliza kufunga goli nikaendelea kumcheza kwa kasi ileile ya bila kupumzika. Akazidi kupagawa na aina ya uchezaji wangu wa bila jezi wala namba, nikazidi kumtawala huku jasho likiwa linanitiririka kwa wakati huo.

Haikuchukua muda Sesilia akaanza kufunga magoli mfululizo, akajikuta amefunga magoli mawili ya bila kuyategemea, akanitazama kwa macho ya huba, nikamtazama, macho yetu yakakutana. Wakati huo nilikuwa juu ya kifua chake chenye matiti makubwa. Mchezaji wangu bado alikuwa ndani ya uwanja.

“Vipi niendelee?” nilimuuliza huku nikimtazama.

“Hapana baby utaniua nimechokaa,” alinijibu kisha akavuta pumzi ndefu na kuziachia kwa pupa.

“Kwahiyo?” nilimuuliza.

“Tupumzike kidogo,” alinijibu kisha nikafanya kama alivyoniambia, tukapumzika kidogo huku nikiendelea kumtomasatomasa sehemu mbali mbali za mwili wake, alizidi kuonekana bado anauhitaji mchezo na tena kwa wakati ule ambao alikuwa amenifunga magoli mawili huku mimi nikiambulia goli moja la ushindi, yaani ndiyo kwanza alizidi kunipandisha wazimu, nikatamani kumrukia niuendeleze mchezo lakini nilighairi kufanya hivyo, sikutaka azidi kuniona nina thamini sana kufanya naye mapenzi kuliko kuzijali hisia zake. Niliendelea kusubiri huku muda wetu huo wa mapumziko ukisindikizwa na stori za kuchombezana.

“Vipi sasa?” nilimuuliza mara baada ya kupumzika kama dakika kumi.

“Una hamu sana na mimi?” aliniuliza.

“Ndiyo mpenzi sasa unataka hamu zangu nikazipeleke wapi?” nilimuuliza kisha nikaamka kitandani, nikaenda kukaa katika kochi dogo, nikamuita, aliponikaribia nikampa ishara ya kunikalia huku mapaja yake akiwa ameyatanua vyema. Tukatenganeza herufi “N” pale tulipokuwa tumekaa.

“Oooohhh baby tamuu sanaaa,” alianza kutokwa na miguno nilipokuwa nampandisha juu na kumshusha taratibu kwa chini mpaka pale alipozoea, akaanza kukinengua kiuno chake mithili ya mtu aliyekuwa akifuata mapigo ya ngoma.

“Oooh babyyy sikuachiii babyyy aaaaahhh tamuuuu,” aliendelea kutoa miguno ya raha alizokuwa akizipata.

Tuliendelea kusakata rumba huku tukibadilisha staili tofauti tofauti na mpaka mwisho wa mchezo nikawa nimefanikiwa kufunga magoli matano wakati Sesilia alikuwa amefunga magoli manne.

Tulipomaliza tulikuwa hoi bin taabani, bila kwenda kuoga tukalala pale kitandani tukiwa vilevile uchi na ni katika siku hiyo ambayo Sesilia aliniambia kuwa alitaka kulala ghetto kwagu, nilimruhusu baada ya kuniambia kuwa nyumbani kwao alikuwa anaishi na dada yake na siku hiyo alimdanganya kwa kumuaga kuwa anaenda kwenye sherehe ya kumbukizi ya kuzaliwa rafiki yake.

“Asante mpenzi wangu kwa kuniridhisha, nakupenda sana,” aliniambia Sesilia tulipokuwa tumelala kitandani.

“Usijali hata mimi nakushukuru sana, umenipa mapenzi ya mwendo kasi,” nilimwambia kisha nikambusu katika kifua chake, akatabasamu.

Kitu nilichokuwa nimepanga kumfanyia Sesilia ni kuhakikisha nafanya kila niwezalo katika mapenzi ili asifikirie kuniacha kirahisi hata kama ingefika siku nikaamua kuachana naye basi isingekuwa rahisi kuweza kukubaliana na maamuzi yangu.

“Niambie kitu Metu mpenzi,” aliniambia.

“Nikuambie kitu gani?” nilimuuliza.

“Kitu chochote kizuri, nataka kusikia maneno mazuri kutoka katika kinywa kwako,” aliniambia.

“Mimi sina kitu kingine cha kukuambia zaidi ya nakupenda na nakuheshimu pia,” nilimwambia kisha akatabasamu.

“Nakupenda pia mpenzi naomba usinifanyie ujinga wowote na sitapenda itokee siku ukanisaliti nitaumia sana.”

“Siwezi kufanya hivyo.”

“Wewe sema huwezi halafu siku nije kusikia una mwanamke mwingine tutagombana.”

“Hakuna siku itakayotokea kama hiyo labda ndotoni,” nilimwambia kwa kumuaminisha kisha tukalala. Siku hiyo ikapita.

                                                 ****

Mapenzi yangu na Sesilia yalizidi kupamba moto kila siku na hakukuwa na tatizo lolote, niliendelea kufanya kazi yangu ya bodaboda huku ulipofika wakati wa kuwa na Sesilia niliweza kuwa naye.

Lilipofika suala la kwenda kunitambulisha nyumbani kwao maeneo ya Keko alipokuwa akiishi na Dada yake ambaye ndiye alikuwa akimsomesha chuo nilionekana kusita kidogo, sikuwa na ndoto za kuja kumuoa Sesilia katika maisha yangu hivyo kile alichokuwa akinieleza kilichukua sura mpya katika ufahamu wangu.

“Unasemaje?” nilimuuliza.

“Nataka nikakutambulishe kwa Dada yangu halafu tayari nimeshamueleza kila kitu kuhusu wewe anataka akufahamu,” aliniambia Sesilia maneno ambayo yalinishangaza sana.

“Mbona imekuwa mapema sana!” nilimuuliza huku nikiwa nimekumbwa na bumbuwazi.

Nilizidi kushangazwa na maneno ya Sesilia aliyokuwa akinieleza kwa wakati ule, alionekana kumaanisha kila kitu na hakuwa katika utani kama nilivyokuwa nikihisi.

Nilitafuta mada nyingine ya kumpotezea lakini kabla ya kukolea alinirudisha katika mada ile ile ya mwanzo, aliniambia anataka nikajitambulishe kwa dada yake.

“Sesilia lakini si ungesubiri kwanza?” nilimuuliza.

“Nisubiri nini Metu wakati sisi tayari ni wapenzi,” alinijibu.

“Hata kama lakini suala la kwenda kujitambulisha sio la kukurupuka kama unavyodhani,” nilimwambia.

“Tatizo kwani liko wapi?” aliniuliza.

“Wewe hulioni?”

“Metu au huna mpango wa kuishi na mimi ndiyo maana unakataa kwenda kujitambulisha niambie au una mwanamke mwingine umempata?” aliniuliza kisha nikakaa kimya, sikutaka kumjibu kwa maana nilianza kupandwa na hasira.

Kwa muda ambao nilikuwa nimekaa kimya akarudia kuniuliza swali hilohilo, nikazidi kupandwa na hasira za ajabu hata sikujua zilitoka wapi. Nilijikuta nikifyatuka na kwenda kumpiga kofi moja upande wa shavu la kushoto halafu nikaanza kumtolea maneno makali ya kumkaripia, haikuchukua hata muda machozi yakawa tayari yameshatawala mashavuni mwake, alikuwa akilia.

“Tena naomba unyamaze kwani kuna ulazima wa mimi kwenda kujitambulisha kwa dada yako,” nilimwambia kwa sauti ya ukali kisha nikamtukana tusi moja la nguoni. Akanyamaza kisha akayafuta machozi yake. Akaniomba msamaha kwa kosa ambalo hata halijulikani, nikamsamehe maisha yakaendelea.

                                                   ****

Nilijikuta nikianza kumchukia Sesilia kutokana na itikadi alizokuwa akiniletea. Katika kumbukumbu zangu sikumbuki kama kuna siku niliwahi kupanga au kuwaza siku moja nitakuja kuishi na mwanamke ambaye nitamuoa na mwisho wa siku nitatengeneza naye maisha. Huo nakumbuka ulikuwa ni ugomvi mkubwa na Mama yangu, kila siku alikuwa ni mtu wa kuniambia nitafute msichana mmoja wa kumuoa lakini maneno yake naweza kusema yaliingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia. Nakumbuka kesi za wanawake niliyokuwa natembea nao zilipozidi kuwa nyingi Mama yangu aliniambia nihame nyumbani nikapange chumba changu na hiki ndiyo kilikuwa chanzo cha mimi kupanga chumba Tandika Azimio huku nikimuacha Mama yangu ambaye alikuwa akiishi Mbagala Kizuiani. Alichoka na aina ya maisha ambayo nilikuwa nikiishi.

Furaha yangu ilikuwa ni kuona nakuwa na msichana katika mapenzi ambaye mwisho wa siku nafanikiwa kumvua nguo yake ya ndani na kisha kufanya naye mapenzi. Hiyo ndiyo ilikuewa furaha yangu wala hakukuwa na kingine ambacho nilikuwa nakipenda katika mapenzi, ni kufanya ngono na kuhakikisha namteka mwanamke kimapenzi ili asifikirie kuniacha katika maisha yake.

Baada ya kumfanyia visa na mikasa mpaka kufikia hatua ya kumpiga, niliamini mpango wangu ulikuwa umetimia. Licha ya kuwa nilimchukia ghafla! na kumkinai kwa mapenzi yake lakini nilizidi kujiona kidume ambaye sikutumia pesa, dawa wala kitu chochote katika kumteka kimapenzi Sesilia. Ufundi wangu wa kitandani pamoja na ahadi zangu za kufikirika ndizo zilizomteka Sesilia, akabaki akiamini kuwa mimi ndiye mwanaume wa maisha yake, hakutaka kunipoteza na kila baya nililokuwa namfanyia aliweza kulipokea kwa mikono miwili na kwa uvumilivu huku akiamini kuwa kuna siku nitaweza kubadilika.

Chuoni alipokuwa akisoma wanaume hawakuacha kumsumbua na kila mwanaume ambaye alikuwa akimtongoza hakuacha kuniambia, aliniambia huku akiniaminisha kuwa alikuwa akijiheshimu na kujilinda hivyo nisijali kuhusu yeye.

“Sasa kama anakutongoza unaniambia ya kazi gani?” nilimuuliza kwa ukali wakati aliponipigia simu na kunieleza juu ya Lecture ambaye alikuwa akimsumbua.

“Metu mbona hivyo lakini?” aliniuliza.

“Mkubalie sasa unamwachaje kwa mfano,” nilimwambia.

“Hivi nitaanzaje kumkubalia wakati mimi nipo na wewe.”

“Kwahiyo.”

“Kwahiyo nini?”

“Wewe unaniigizia upendo, huko chuo najua una wanaume wako.”

“Metu huniamini?”

“Siwezi kumuamini mwanamke katika maisha yangu,” nilimwambia kisha nikamsikia akianza kulia, sikutaka kukisikiliza kilio chake, niliamua kukata simu.

Kesi za kila siku juu ya wanaume waliyokuwa wakimsumbua ndizo nilizozitumia kama fimbo ya kumuadhibu, nilimwambia kuwa simuamini hivyo asiendelee kuniaminisha upendo wake niliyoufananisha na gazeti kila mtu anasoma.

Kuna muda nilijisikia kufanya mapenzi, nilimtafuta na kumuigizia upendo, alipokuja nilimfungia ghetto siku hiyo na hakukuwa na kitu kingine tulichokifanya zaidi ya kufanya mapenzi, nilifanya naye kila aina ya staili unazozijua na nyingine usizozijua.

Baada ya kumtumia sana kimapenzi nilianza kumuacha kimya kimya. Nilikuwa simtafuti tena kama ilivyokuwa hapo awali, alipokuwa akinipigia simu na kunitumia ujumbe mfupi sikuweza kumjibu kwa wakati na nilipokuja kumjibu nilisingizia kazi yangu ya bodaboda ndiyo iliyokuwa ikinifanya nikose muda wa kuwasiliana na yeye wakati, hilo hakujali na kama haitoshi akawa ananitumia ujumbe kila siku, sikutaka kumjibu kwa maana tayari nilikuwa nimeshamchoka.

Katika kipindi hicho ambacho alikuwa akinitumia ujumbe mfupi na kunipigia simu bila kuchoka nilikuwa tayari nimeshakutana na Samira msichana ambaye nilikuwa nimempenda, kazi yangu ilikuwa ni kumpeleka kila siku kazini kwake Posta na kumrudisha.

Nilichokuwa nimekipanga kwa wakati huo ni kufanya mabadiliko makubwa sana ya kimapenzi, nilipanga kuachana na Sesilia na kuanza kumfukizia Samira.

ITAENDELEA

Sikuachi Baby Sehemu ya Pili

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment