SAA LA 25
SIMULIZI

SAA LA 25

Saa la 25 Sehemu ya Tano

Giza liliendelea kupambana na mwanga wa taa zilizoko kwenye majumba ya wahindi katikati ya jiji la Dar es salaam, barabara hii ilikuwa nyeupe kabisa ni magari machache tu ambayo yalikuwa yakipita kwa wakati huo, hakukuwa na mbalamwezi wala nyota hazikuonekana kabisa, ulikuwa usiku wa mawingu mazito na hali ya kaupepo iliendelea kupunguza joto la jiji hili ambalo husifiwa kwa hali hiyo na kila mtu aliyewahi kufika hapa. Wengine walikuwa bado kwenye starehe zao muda huo, wakila maisha kwa kucheza muziki au kula na kunywa vinywaji aina aina, pesa ziliteketezwa tu kwa kugawa kwa wauza miili katika majumba hayo, hata hawakujua kuwa kuna kufa baada ya maisha hayo, hiyo kwao ilikuwa ni hadithi ya kufikirika tu, wengine walikuwa wako katika majumba ya filamu wakiburudisha macho yao kwa kuangalia maigizo haya ya kizungu yaliyooneshwa ka njia ya picha kwa kutumia chombo kilichofanana na baiskeli iwapo kwa fundi, wengine wakiwa wamelala wakifurahia raha ya magodoro na upepo wa mapangaboi yaliyofungwa katika mapaa yao yakining’inia na kuwapa upepo mtamu ili tu kupunguza joto la ndani, wengine wakiwa mahospitalini wakiteseka kwa magonjwa, wakiomba kila siku ee Mungu utuchukue, wengine walikuwa katika kutimiza wajibu zao za kazi katika kulijenga taifa. Maisha yaliendelea kila kona kwa jinsi zake, kwa kila mtu kwa namna yake.

Saa la 25 Sehemu ya Kwanza
Saa la 25 Sehemu ya Pili
Saa la 25 Sehemu ya Tatu
Saa la 25 Sehemu ya Nne
Saa la 25 Sehemu ya Tano

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment