KIJASUSI

Ep 01: Jinamizi

Jinamizi Sehemu ya Kwanza

IMEANDIKWA NA: HASSAN O MAMBOSASA

*********************************************************************************

Simulizi: Jinamizi

Sehemu Ya Kwanza (1)

Hekaheka za uchaguzi zilikuwa zimepamba moto nchini Tanzania,kampeni zenye majigambo zikiwa zimeshika nafasi yake ndani ya ardhi hii yenye amani. Vyama tofauti vilikuwa vikihaha huku na kule ndani ya nchi hii ili viweze kujizolea kura kwa wananchi, wagombea urais,ubunge na udiwani a vyama hivyo walijinadi wawezavyo ili kuwashawishi wananchi wawapigie kura. Hakika zilikuwa ni kampeni za aina yake zilizoleta upinzani katika vyama viwili tofauti, kimoja kikiwa ni chama tawala na kingine kikiwa ni kikuu cha upinzani nchiniTanzania. Upinzani huu ulipelekea hadi wawe wanachafuana kupitia vyombo vya habari, huku wanachama wake wakiwa katika makundi yenye uhasama mkubwa. Hakika hii ilikuwa ni kipato tosha kwa wanahabari wenye tamaa ndani ya nchi hii, wanahabari hawa walidiriki kuandika habari za uongo zilizoleta uhasama baina ya vyama hivi.

Kampeni ziliendelea kuendeshwa sehemu mbalimbali za nchi hii huku serikali ikitoa fungu kwa kila chama ili kiweze kujimudu vyema, kampeni za vyama vyote zilikuwa za kawaida ila chama tawala na chama kikuu cha upinzani kampeni zao zilikuwa zimeimarika zaidi ya vyama vyote.

Chama tawala kilitumia pesa za wanachama wake matajiri waliojitolea kukifadhili chama kipindi cha kampeni ,huku wapinzani wao wakuu wakiwa hawajulikani ni wapi walipopata fedha za nyongeza za kuweza kufanya kampeni zenye gharama kuliko uwezo wa chama chao. Utata wa chama hiki uliwavuta sana waandishi wa kikundi cha kujitegemea kutoka nchi za Afrika ya mashariki kuingia kazini, walianza kulifuatilia suala hili kwa undani sana ili wapate ukweli juu ya chama hiki.

Chama hiki cha wanandishi kinachojulikana kama WAHANGA kiliundwa na waandishi watano wenye roho zisizo na hofu na jeuri ya kupuuzia vitisho , kiliundwa na watu watano kutokana nchi tano za Afrika ya mashariki amboa ni Norbert Kaila wa Tanzania,Davis Elius wa Kenya,Joseph Kiiza wa Uganda,Hilda Alphonce wa Rwanda na Allison Frank kutoka Burundi. Hawa ndio waliojulikana kama vichwa ngumu na baadhi ya vigogo, walikuwa wakitoa jarida lao lenye kuumbua mambo mengi maovu ndani ya Afrika ya mashariki. Hadi muda huo wa kampeni walikuwa tayari wameshaingia nchini Tanzania kwa siri,bwalifanya uchunguzi wa chini kwa chini huku kampeni zikiwa zinanaendelea. Uchunguzi wao ukiwa unaendelea ndio uhasama baina ya vyama hivi ukizidi kushika hatamu nchini, mauaji ya mgombea ubunge wa chama kikuu cha upinzani katika jimbo la Kahama yanatokea katika kampeni za chama hicho wilayani Kahama mkoani Shinyanga. Mgombea huyu aliyeitwa Gerald Geofrey alipigwa risasi ya kichwa akiwa jukwaani akijinadi kwa wananchi , hali ya sitomfahamu ilitokea baina ya chama cha upinzani maarufu kama PTP(people of Tanzania party) na chama tawala RPP (revolutionist political party) . PTP walikuwa wakiishutumu RPP ndio waliohusika na mauaji ya mgombea katika vyombo vya habari, hali hii ilipelekea RPP watumie muda wao mwingi kujitetea katika kampeni huku wenzao wakijinadi kwa wananchi. Hadi uchaguzi unakaribia tayari RPP walikuwa wameshapoteza idadi kubwa ya wafuasi na PTP walikuwa wameshajipatia wafuasi wengi tofauti na ilivyokuwa awali, RPP walijikuta wakipigwa kwenye kampeni zao karibu kila mahali.

Hatimaye uchaguzi ukawadia ukawadia na ikawa ni siku ya mapumziko siku hiyo ya uchaguzi ili kuwapa fursa wananchi wapige,uchaguzi ulifanyika katika hali ya utulivu na amani nchi nzima.



Waandishi wa WAHANGA nao walikuwa tayari wameshafanya uchunguzi na sasa wapo katika hata za mwisho kabla hawajalilipeleka jarida lao mtamboni ili liweze kuchapishwa na hatimaye liingie mitaani, walipolimaliza tayari uchaguzi ulikwisha fanyika na ilikuwa yanasubiriwamatokeo ya uchaguzi kwa hamu kubwa ili mshindi ajulikane. Binti pekee wa WAHANGA Hilda Alphonce ndiye aliyechukua jukumu la kupeleka nakala za jarida lao ili liweze kuchapishwa,alipeleka kiwanda cha EAPL(east africa publishers limited) tawi la Dar es salaam. Kutoka ofisini kwao hadi zilipo ofisi za kampuni ya EAPL hakukuwa mbali kwa mwendo wa miguu ingawa Hilda aliamua kutumia gari la umoja wao ili awahu kurudi aweze kuendelea na kazi kama kawaida,alifanikiwa kufika zilipo ofisi hizo mtaa wa Libya jirani na kituo cha mafuta kisha akaenda kwa mtu wao maalum anayewachapishia majarida yao wakiwa jijini Dar es salaam. Hakuwa na muda wa kukaa tena maeneo hayo baada ya kukabidhi vitu muhimu kwa ajili ya uchapishaji, aliondoka ofisini hapo. Wakati akiwa anatoka nje ya jengo hilo alipishana na kijana mwenye suti nyeusi nadhifu akiingia ofisini humo.

Hakutaka kumtilia shaka yoyote kwa muonekano alionao, alimuona kama mteja wa kawaida kama alivyo yeye ktika kampuni hiyo.


*. Kijana aliyepishana na Hilda aliingia moja kwa mojahadi katika ofisi inayohusika na kupokea nakala zawaandishi , alimkuta mhusika wa upokeaji wa nakalahizo akiwa ameegemea kiti huku miguu ikiwamezani. Aliongea pasipo kuketi katika cha watejakilicho jiranj yake, ” we Daud huyu malaya kaletanini” Daud alijibu bila ya kumtilia maananuanayezungumza naye, “ni nakala za jarida lao ambalo linahitajika kuchapishwa”. Yule kijana aliingiza mkono katika mfuko wa koti la suti yake,alipoutoa ulikuwa na burungutu la pesa ambalo aliliweka juu ya meza kisha akasema, “hizi pesa ni zako zote ikiwa utanipatia hizo nakala kabla hazijafika mitamboni”. Daud alikaa sawa kisha akamtazama yule kijana kwa umakini, alizitazama na pesa pia kwa macho ya tamaa kisha akasema “siwezi kuharibu kazi yangu kisa tamaa”. Yule kijana akatia mkono katika mfuko nyuma wa suruali yake,alipoutoa ulikuwa umeshika pochi ya kuwekea hela iliyotuna mithili ya nyoka mwenye hasira.

Aliifungua zipu ya pochi hiyo kwa majivuno kisha akatoa noti kadhaa na kuzihesabu, aliporidhika nazo aliziweka juu ya meza huku akisema “maisha yako unahitaji uyajenge zaidi ya hapa ulipo rafiki,sasa wewe jifanye mzalendo ukale dona na dagaa”. Daud alizipokea pesa zote kwa pupa kisha akaziweka halafu akaziweka katika mkoba wake wa kazi,alipofunga zipu ya mkoba wake alifungua mtoto wa meza yake kwa funguo. Alitoa karatasi zote alizokuja nazo Hilda na kumkabidhi yule kijana akiwa ametabasamu, “dona na dagaa ni mlo mbaya kwa masikini ila kwa Tajiri ni chakula bora” Daudaliongea kwa mzaha na kupelekea wote wacheke.

Waliagana kwa furaha kisha yule kijana akaondoka ofisini hapo akiwa na nakala hizo za WAHANGA. Mnamo desemba mwaka huohuo matokeo ya uchaguzi huo yalitarajiwa kutangazwa katika ukumbi wa tume ya taifa ya uchaguzi,tarehe na saa za kutangazwa kwa matokeo hayo ilitajwa mapema sana. Hatimaye siku ya siku ikawadia na ukumbi huo ukawa umejaa wagombea tofauti huku wagombea wa urais wa kila chama wakawa wamekaa katika viti vilivyo katika safu moja iliyopo mbele karibia na jukwa kuu . Ilipotimu saa nne kamili za asubuhi matokeo hayo yalitangazwa na mwenyekiti wa tume hiyo mhe Ramadhani Gumbo kwa kutaja asilimia za kura kwa kila mgombea,hakika ilikuwa ni shangwe kwa chama cha upinzani PTP huku chama tawala RPP kikipitwa kwa kura nyingi sana. Vyama vingine vilivyobakia vilikuwa na upinzani mdogo hivyo havikuweza kufua dafu kabisa. Mgombea urais aliyeshinda alipeana mikono na wagombea wote kwa tabasami kuu,nao wagombea wengine waliupokea mkono wake kuonesha hawana kinyongo na wamekubaliana na matokeo hayo.

Mwisho akapeana mkono na mpinzani wake mkubwa mheshimiwa Dominic Mtalemwa wa RPP, walipeana mikono wakiwa tabasamu kisha wakakumbatiana kwa furaha yao ya maigizo.

Wakiwa wamekumbatiana mhe Filbert Ole ambaye ni mshindi aliongea kwa sauti ya chini, “bado ni chekechea kwenye siasa usishindane na aliye chuo kikuu”. Maneno hayo ya dharau hayakusikika na mtu yoyote isipokuwa Mtalemwa mwenyewe ambaye hakuhisi kama ipo siku atadharauliwa namna hiyo. Hata hamu ya kukaa eneo haikuwepo ndani ya nafsi yake kutokana dharau aliyooneshwa,kwake ilikuwa ni kuaibishwa ingawa hakuna mtu aliyeiona. Alitoka hadi nje ya ukumbi katika eneo la maegesho akiwa na wapambe wake wote,aliingia ndani ya gari alilokuja kisha akamuamuru dereva aendeshe kurudi nyumbani kwake.


Ukimya wa kampuni ya uchapishaji ya EAPL katika kuchapisha jarida la WAHANGA ulizua hali ya sintofahamu miongoni mwa waandishi hao wa kimataifa, kuzungushwa na mtu aliyepokea nakala zao kuliwashangaza sana kwani haikuwa kawaida kwa jambo kama hilo kutokea.

“nashauri tuifuatilie nakala yetu” alishauri Norbert katika kilichowekwa juu ya suala hilo. “hata mimi naona tufanye hivyo” Davis alimuunga mkono Norbert “hapana tusifanye hivyo ” Joseph alitoa rai ya kupingana na mawazo ya Norbeert na Davis kisha akawaambia “hili suala halijakaa kama mnavyofikiria nyinyi jamani, kumbukeni tulimchezea simba sharubu akiwa amesinzia na sasa amezinduka lakini ametutisha tu pasipo kutung’ata”. Kauli hiyo ilimuacha kila mmoja njia panda, hali hiyo Joseph aliibaini haraka sana na ikamlazimu kuwafafanulia “namaanisha hivi kama jarida lingetoka tungekuwa tumechokonoa mahali pabaya,bsasa ili kutuonesha mhusika anaweza kufanikiwa kufanya lolote ndio amezuia kazi yetu”.

Wote waliafiki kwa kutikisa kichwa kuashiria wamekubaliana na hoja ya Joseph. “jambo ulilolisema Mr Kiiza nakubaliana na wewe kwa asilimia mia moja na sasa inatubidi tusitishe kazi ya kuchunguza tukubali kazi yetu imepotea tu” aliongea Allison kwa mara ya kwanza baada ya kuwasikiliza wenzake. Akaendelea kuwaambia “cha msingi ni kuangalia kazi nyingine baada ya hapa, ila kwa sasa tukubali tumeshindwa kuwazindua wanachi usingizini”.

Baada ya wote kutoa mawazo yao walikaa kimya na kumtazama Hilda, “hakuna kilichoharibika jamanu katika suala hilo mimi nahisi tuwaache wasahau kisha tuwaumbue” Hilda kwa mara ya kwanza aliongea baada ya kuona anatazamwa na kila mmoja.

“unamaanisha nini kusema hivyo?” .Alphonce alimuuliza kwa pupa. Hilda alianza kuifafanua kauli yake kwa kusema “baada ya kukamilisha uchunguzi nakala zile nilivutiwa sana nazo,hivyo nilitoa vivuli vyake kisha picha za ushahidi nikazihamisha kwenye santuri nikavihifadhi mahali ili ziwe kumbukumbu kwangu”. Wote walitoa tabasamu na kufufua tumauni jipya mioyoni mwao….

“aisee we mwanamke sijui una….” Norbert hakumalizia kauli yake hiyo ya kimasihara baada ya kicheko cha ghafla kumshika, hali hiyo ilikuwa kwa wenzake pia waliopo eneo hilo kwa kitendo alichokifanya Hilda. “sasa nimekuwa kikatuni jamani, maana mnavyonicheka ” aliongea Hilda baada ya kuona vicheko vimezidi. Vicheko vya wote vilipotulia Joseph alisema “aisee sikutegemea kabisa kama utafanya hivi, hivi ulioteshwa nini kama kuna tatizo litatokea?”. “labda mzimu wa kitusi ulimfungulia njia” Allison naye alidakia na kusababisha wenzake wote wacheke.

“khaa jamani kuwa mtusi nayo imekuwa mada” Hilda aliongea kwa mshangao baada ya kusikia utani uliotunbukizwa na Allison. Mjadala uliikatika kwa muda na utani ukachukua nafasi yake dhidi ya Hilda, binti wa kitusi aliyeishi Tanzania kwa muda mrefu ingawa makazi yake ni Rwanda. Utani huu ulidumu kwa muda kisha Davis akawarejesha kwenye kwa kusema “sasa jamani suala limeisha au sio?” “hata mimi nadhani hivyo” Norbert naye akaafiki kauli ya Davis. Wote kwa pamoja wakakubaliana wasubiri joto la siasa litulie kisha waitoe kazi yao kwa mara ya pili kwa kutumia kampuni nyingine na sio ile ya awali. Wakitawaliwa nyuso zenye tabasamu baada ya kufufuka tumaini jipya la kazi yao, waliamua wapumzike siku hiyo ili wakaitulize furaha yao.


Januari mwaka uliofuata rais mpya wa jamhuri ya

muungano wa Tanzania mheshimiwa Filbert Ole

aliapishwa katika uwanja wa uhuru jijini Dar es

salaam, hafla hiyo ya kuapishwa rais Ole

ilihudhuriwa na maelfu ya watu kutoka sehemu

mbalimbali za jijj la Dar es salaam huku wachache

wakitoka mikoani kuja kushuhudia hafla hiyo.

Wanadiplomasia mbalimbali pamoja na viongozi

nao walialikwa katika sherehe hizo, viongozi wa

mataifa mbalimbali barani Afrika nao hawakuwa

nyuma katika uhudhuriaji wa sherehe hizo. Hadi

muda wa kuanza sheria hizo unakribia tayari

uwanja mzima ulishafurika watu walioalikwa huku wasioalikwa wakiwa nje ya geti, hali hiu

iliwalazimu watu wasioalikwa kukaa nje ya uwanja

huo kutokana na kutokana na ulinzi ulio ndani ya

uwanja. Ulinzi wa wanausalama nao haukuwa wa

kulegalega, ulinzi huu ulikuwa imara sana na

wenye kuridhisha sana kwa viongozi wa eneo hilo.

Muda mfupi kabla ya sherehe kuanza rais

anayemaliza muda wake Prof Athumani Kisiga

aliingia uwanjani akiwa katika gari la wazi kisha

akauzunguka uwanja huku akipungia mkono watu,

baada ya hapo alienda kusimama katika jukwa la

kiapo kisha mizinga ishirini na moja ikafuata. Rais

mstaafu alishuka kukagua gwaride la majeshi

yote, alipomaliza alipanda jukwaa na kuketi mahala

pake huku bendera ya rais ikishushwa kuashiria

kuisha kwa utawala wake. Hatimaye shughuli ya

kuapishwa kwa rais Ole ilianza mnamo saa tano za

asubuhi, rais mtarajiwa alipanda katika jukwaa la

kiapo baada ya rais mstaafu kupanda tayari wakiwa

pamoja na jaji mkuu. Shughuli za kuapishwa

ziliannza na kufuatiwa na kuapishwa kwa makamu

wa rais Dk. Hilary Jamadin, ukaguzi wa gwaride

maalum ulifuata kuhitiimisha shughuli hizo. Ratiba

nyingine zilifuata baada ya shughuli hiyo

kukamilika.


Muda huo huo sherehe zikiwa zinaendelea kwenye

mitaa ya jiji la Dar es salaam watu walikuwa

wakishuhudia kupitia kwenye luninga tofauti,

vikundi mbalimbali vya watu vilikuwa vikiijadili

sherehe hiyo ya kitaifa. Mijadala hiyo ilijadiliwa

katika makundi tofauti ndani ya mitaa ya

jiji , wengine walikuwa wamekaa majumbani mwao

wakiendesha mijadala hiyo. Hali hiyo pia ilikuwa imo

ndani ya nyumba moja ya kisasa maeneo ya

mikocheni. Huzuni ya watu humo ndani ilishaanza

kusahaulika

kwa watu wote isipokuwa mama mwenye nyumba

hiyo ambaye ni mjane, watoto wake wakiwa

wanafurahia kuangalia rais wao mpya waliyempigia

kura yeye alikuwa amezama katika dimbwi zito la

mawazo. Hakuwa mwingine bali ni mke wa

aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la kahama

bwana Gerald Geofrey aliyeuawa kwa kupigwa

risasi, mwanamama huyu alionekana ana dukuduku

zito moyoni wake na kila akiangalia sherehe hizo

za kumuapisha rais zilikuwa zinamchefua.

Hakuweza kustahimili kuziangalia sherehe hizo

tena kwani machozi yalishaanza kumtoka, akaingia

chumbani akilia kwa uchungu. Hali hiyo

iliwashangaza sana watoto wake ingawa

hawakuthubutu kumuuliza chochote, walimuacha

kama alivyo hadi atakapokuwa sawa.


Baada ya sherehe za kuapishwa kuisha na hatimaye

rais Ole kukabidhiwa majukumu ya urais na rais

mstaafu, shughuli za kimaendeleo ziliendelea kama

kawaida. Rais huyu aliooingia madarakani aliteua

baraza lake la mawaziri ndani ya muda mfupi tu,

baraza hili la mawaziri lilikuwa na mchanganyiko

wa mawaziri wapya na wa awamu iliyopita. Baada

ya mwaka mmoja tu toka rais Ole aingie

madarakani tayari nchi ilisheheni miundombinu ya

kila aina, pia huduma za kijamii zikaimarishwa

ndani ya muda huo. Hii ilisababisha wananchi

wazidi kumpenda na kumuamini sana rais wao,

hata wale waliokuwa sio wanachama wa chama

chake walianza kuwa na imani nae. Wizara zote

zilionekana zikifanya kazi ipasavyo na kupelekea

awamu hii ya urais iwe ya kipekee.

Ndani ya mwaka huohuo utafiti wa madini ulifanyika

wilayani kondoa katika mji kuu wa nchi hii, kiwango

kikubwa cha madini aina ya almasi kiligunduliwa

ndani ya eneo la kijiji cha Chambalo, madini hayo

yenye thamani kubwa yaligunduliwa ndani ya eneo

hilo na ripoti ikapelekwa kwa waziri wa maliasili na

utalii Dk. Jumanne Mdoe. Habari hizo pia

zilisambaa kwa wananchi wa kawaida ndani ya nchi

nzima, wengi wa wananchi kupitia vyombo vya

habari walitaka mgodi huo utumike kwa manufaa ya

nchi yao tu. Baada ya siku mbili waziri wa maliasili

na utalii alieleza uamuzi uliochukuliwa na wizara

yake juu ya madini. “hakika hii ni bahati ambayo

Tanzania imetuangukia na tunapaswa tuitumie

kama bahati ndani ya nchi yetu. Kumbukeni bahati

haiji mara ya mbili na tunapaswa tusiipoteze bahati

hii bali tuitumie kwa manufaa ya Tanzania yetu,

hivyo mimi na wizara nzima ya maliasili na utalii

tutaitumia bahati hii kwa ajili ya manufaa ya

watanzania na si vinginevyo. Hivyo watanzaniwa

watarajie mazuri kutokana na bahati hii na wawe

na imani ya kupata matunda bora ya bahati hii”

hayo ndiyo maneno ya waziri wa maliasili na utalii

juu ya matumizi ya hayo madini. Maneno hayo

yalimfurahisha kila raia aliyeyasikiliza kupitia

kwenye vyombo vya habari na ikawa ni kama

bahati kuwa na kiongozi kama yeye, watu walikuwa

wanangojea kwa hamu hayo matunda ya maliasili

iliyogunduliwa nchini mwao. Baada ya mwezi mmoja kupita toka hotuba ya

waziri huyo katika mkutano wake na waandishi wa

habari , ajali kubwa ilitokea maeneo ya

msata baada ya gari ndogo aina ya Land cruiser

kugongana uso kwa uso na Fuso lililobeba mkaa

likitokea mkoani Tanga kuja jijini Dar es salaam.

Dereva wa land cruiser alifariki papo hapo huku bosi

wake akiwa ni majeruhi hivyo kulazimika

kukimbizwa hospitali iliyo jirani kwa ajili ya

matibabu, askari wa usalama barabarani walifika

eneo la tukio mapema na kupima ajali. Upande wa

fuso lililobebe mkaa dereva wake hakufahamika

alipo hadi muda huo, ilikuwa ni mshangao mkubwa

sana kwa maaskari hao na walipoangalia gari aina

ya land cruiser ndio walipopata mshango zaidi.

“aisee hii si gari ya mheshimiwa” aliuliza mmoja

wa maaskari hao mwenye V moja begani. “kostebo

una uhakika maana hata majeruhi aliyekutwa

haujamtambua kutokanana majereha yaliyopo usoni

mwake” mwenzake alimwambia huku akitazama namba

za gari hilo pamoja na stika za gari hiyo. “aisee ni

lenyewe na nahisi hata majeruhi aliye kwenye hilo

gari ni yeye maana leo alikuwa anasafiri kuelekea

Tanga kuangalia hifadhi ya mkomazi” aliongea tena

yule askari baada ya kukagua namba za gari lile

kwa umakini. Walipomliza waliamua waliamua

kuwasiliana na wenzao waliongozana na gari la

wagonjwa la hospitali ya tumbi lililofika hapo kwa

ajili ya kuchukua majeruhi na mwili wa dereva

kwenda kuihufadhi.


Joseph Kiiza wa WAHANGA akiwa safarini akitokea

mkoani Kilimanjaro alikuta ajali kubwa iliyotokea

maeno ya Msata mkoani pwani, akiwa kama

mwanishi wa habari mwenye vifaa vyote

alisimamisha gari ya ofisi yake aina ya toyota

harrier na kuanza kuanza kuelekea eneo la ajali.

Hadi muda huo tayari utepe ulikuwa

ushazungushiwa eneo na askari walikuwa wamefika

wengi sana, alipojaribu kuuvuka utepe huo alizuiwa

na askari hali iliyomlazimu atie kitambulisho chake

na kuwaonesha maaskari hao. Maaskari

walimruhusu apite eneo hilo lenye utepe,

alipouvuka huo utepe alianza kupiga picha

mbalimbali kisha akafanya mahojiano na baadhi ya

maaskari wa eneo hilo. Akiwa anaendelea kupiga

picha mbalimbali za ajali hiyo kamba ya kiatu

ilimfunguka na kumlazimu ainame ili aifunge akiwa

jirani na fuso lililopata ajali, alipoinama tu alisikia

mlio wa bati la fuso ukitobolewa eneo ambalo

kichwa chake kilipokuwa wakati amesimama.

Hakuhitaji elimu ya ziada kutambua kuwa alikuwa

amelengwa na risasi ambayo ilimkosa baada ya

kuinama na kufunga kamba za viatu. Alijibiringisha

chini toka pale alioo kuelekea pembeni huku

maaskari wakiwa tayari wameelekeza silaha zao

ilipotokea risasi hiyo.

Hawakuweza kuambulia chochote zaidi ya vichaka

vilivyopo eneo hilo, baadhi ya askari waliamua

kuelekea ilipotoka risasi hiyo wakiwa wameweka

silaha zao kwa namna ya tahadhari. Joseph naye aliinua

kwa tahadhari pale chini alipokuwa amelala baada

ya kujibiringisha pembeni, alikimbia kwa haraka

hadi alipoliacha gari lake kisha akaingia na akakilaza kiti

chake pamoja na yeye kulala akiwa anahema mfululizo kwa tukio

lililomkuta. Hakutaka tena kutoka nje kwa kuhofia

usalama wake, akiwa amejilaza hapo alisikia mlio wa

pikipiki aina ya bajah ukitokea barabara ya vumbi

iliyo jirani na eneo hilo. Pikipiki hiyo ilifuata njia iendayo

Chalinze kwa mwendo wa kasi, mwendo wa pikipiki

hiyo pamoja na makelele yake ulimvuta Joseph na

kumfanya ainue kichwa na kuitazama. Aliiona ikiwa

ina mchoro wa chui katika bango lililokuwa

linaning’inia nyuma, aliipuuzia kisha akarudi na

kujilaza kwenye kiti cha gari yake. Baada ya muda

wale maaskri walirudi pasipo kuambulia chochote

cha ushahidi zaidi ya bunduki aina ya sniper rifle

iliyotelekezwa, Joseph aliinua kiti kisha akaiwasha

gari yake. Maaskari hawakushughulika naye kabisa

hata alipowaambia anaondoka wao walimruhusu

aende, Joseph alifuata barabara iendayo chalinze

kwa mwendo wa wastani kisha akaongeza mwendo

ili awahi aendapo. Alifanikiwa kufika Chalinze ndani

ya muda mfupi tu kutokana na kutumia mwendo

mkali, alifuata njia iendayo Dar es salaam kwa

mwendo ule hadi kibaha . Hapo alifuata barabara iliyo upande wenye kibao

kilichoelekeza mahali ilipo hospitali ya tumbi toka

barabara ya morogoro katika eneo ambalo zamani

lilijulikana kama Tamko. Baada ya kuingia barabara hiyo alienda mwendo mfupi tu

alipishana na ile pikipiki aina ya baja ikitokea mahali

anapoelekea, sasa alimuona dereva wa pikipiki hiyo

alivyo ingawa alikuwa amevaa kofia ya kujikinga

kichwani. Alikuwa ni mtu mrefu na mwembamba

mwenye mavazi yaliyomkaa vilivyo na mikononi

alivaa glovu za kuendeshea pikipiki, kumuona hapo

kwa mara ya pili hakukumshtua Joseph zaidi ya

kuvutika kuuangalia jinsi alivyo. Alipofika hospitali ya tumbi alipitiliza

hadi mapokezi , alijitambulisha kisha akumuulizia

majeruhiwa ajali aliyefukishwa hospitalini hapo.

Joseph alipelekwa kwa mganga mkuu wa hospitali

hiyo kwani manesi na madaktari wengine

hawakutakiwa watoe taarifa yoyote juu ya majeruhi

huyo, alipofika alijieleza kwa mganga huyo shida

yake iliyomleta kisha akaomba ushirikiano katika

jambo hilo.

“kusema ukweli muda si mrefu tumepokea majeruhi

wa ajali ambaye alikuwa ni mheshimiwa, ninasikitika

kukutaarifu kuwa hatunaye tena duniani hadi sasa”

aliongea mganga mkuu Joseph akinakili maelezo

hayo, alimsaili mganga huyo kwa maswali

machache kisha akaondoka eneo hilo baada ya

kuwaaga wenyeji wake.



Taarifa za kifo cha waziri wa maliasili na utalii

zilisambaa kama moto wa kifuu, karibu sehemu

zote za jiji la Dar es salaam na majiji mengine

yalishazipata taarifa hizo kabla hata vyombo vya

habari havijaitangaza. Maelfu ya wananchi

walihuzunika na kifo cha mtumishi wa umma

mwenye kuijali kazi yake, taarifa hizo zilipofika ikulu

zilipokelewa kinamna nyingine ingawa rais Ole alitoa

salamu za rambirambi kwa familia ya waziri wake.

Ilikuwa ni huzuni isiyoelezeka kwa familia ya

marehemu, hata watu wa karibu waliomjua vizuri

waziri huyo. Siku iliyofuata mwili wake uliletwa jijini

Dar es salaam kisha ukaenda kuhifadhiwa katika

hospitali ya taifa ya Muhimbili, hadi mwili

unaingizwa katika chumba cha kuhifadhiwa maiti

tayari hospitali hiyo ilifurika waandishi wa habari

waliokuwa wakisaka habari na utbibitisho juu ya hilo

suala. Joseph na Nobert wakiwa miongoni mwa

waandishi hao, walitumia taaluma yao vizuri jambo

lililowawezesha wapate picha za uthibitisho wa tukio

hilo. Waliporidhika waliondoka hadi walipoacha gari

ya kikundi chao aina ya toyota Noah ya rangi nyeupe, walipanda

wote huku Norbert akiketi nyuma ya usukani kisha

wakaondoka hospitalini hapo. Walifuata njia iendayo

kituo cha zimamoto, wakiwa wanamalizia kona ya jengo la Swiss kuingia

katika barabara ya umoja wa mataifa Joseph aliangalia

nyuma kupitia kioo cha pembeni kilicho upande

wake. Hapo ndipo alipoingiwa wasiwasi kwa kile

alichokiona aliiona pikipiki aina ya baja ikiwa nyuma

yao baada ya magari mawili, alipomtazama dereva

wa ile pikipiki alikuwa mrefu na mwembamba kama

aliyekutana nae jana msata na hospitali.

“Norb huyo jamaa mwenye pikipiki huko nyuma sina

imani nae” alimwambia Norbert

“yupi? huyo kwenye baja au boxer maana wapo

wawili huko nyuma na wote wamevaa suti nyeusi”

alisema Norbert na kumfanya Joseph ageuke

aangalie vizuri, alipoangalia aliona pikipiki ya tatu

ain ya suzuki ikija kwa kasi kisha ikaungana na wale

wawili hali iliyofanya waonekane wapo watatu

kiidadi. Alipowatazama vizuri aliona wote ni

wembamba na warefu tena wamevaa mavazi

yanayofanana.

“wapo watatu Norb inabidi tufanye kitu aisee ili

tuwakwepe” aliongea Joseph.

“punguza uoga Jose” aliongea Norbert.

“Norb niliwaambia jana nimekoswa na risasi kisha

nikaiona pikipiki aina ya baja ikiendeshwa na mtu

mwembamba na mrefu baada ya kukoswa na risasi

na nilipokuwa naenda hospitali ya Tumbi, sasa mimi

sina imanu nae huyo” alifafanua Joseph na

kumfanya Norbert aifuate barabara ya morogoro kwa

mwendo wa kasi punde tu alipofika katika makutano

ya barabara yaliyo jirani na kituo cha zimamoto

maarufu kama fire, aliifuata barabara hiyo kwa

mwendo wa kasi huku akiangalia nyuma. Zile

pikipiki tatu nazo bado zilikuwa zinawafuatilia kwa

mwendo wa kasi lakini hazikuwapita wao, hali hiyo

ilimsababisha Norbert aifuate barabara iendayo Ilala

baada ya kufika makutano ya barabara yaliyo jirani

na msikiti wa kichangani maeneo ya magomeni

mapipa. Akiwa katika mwendo uleule huku akiyapita

baadhi ya magari, aliifuata barabara hiyo hadi

mzunguko wa kigogo kisha akafuata barabara ya

mkato iendayo ubungo kupitia kigogo. Hadi muda

huo tayari ilikuwa ni muda wa saa saba muda huo

watu walikuwa wakiswali swala ya

adhuhuri katika misikiti. Norbert alifuata njia hiyo ya

mkato iendayo ubungo kisha akaingia katika

maegesho ya magari ya msikiti mmoja wa ghorofa

uliopo upande wa kulia mkabala na dhule ya msingi ,maegesho hayo ya msikiti yalikuwa

yana magari ya waumini wachache. Kulikuwa kuna

gari aina ya Noah zenye kufanana na gari la akina

Noerbert, hakika huo ulikuwa mwanya kwa akina

Norbert kwani nao waliegesha gari kisha wakalaza

siti walizokalia. Baada ya muda walisikia milio ya

pikipiki tatu tofauti huku makelele ya pikipiki aina ya

baja ikiwa inavuma zaidi, pikipiki hizo zilisimama

kwa muda mfupi kisha zikaondoka kuendelea mbele.



Vijana watatu wa kundi hatari la three devils kutoka

Marekani walikuwa wapo maeneo ya hospitali ya

taifa ya muhimbili, walikuwa hapo kuhakikisha kama

mwili ulioingizwa hapo ni wa mheshimiwa waziri

aliyepata ajali siku iliyopita. Wakiwa na vitambulisho

feki vya usalama wa taifa, waliweza kuiona maiti

baada ya kujitambulisha wao ni usalama wa taifa na

walikuwa kwenye uchunguzi. Walipotoka mmoja wao

alipiga simu na kuongea, “ni yeye bosi” kisha

akakata simu na kuwaashiria wenzake waondoke.

Wakiwa wanatoka waliwaona Norbert na Joseph

wakiwa pamoja, walipotaka kuondoka kuondoka

mmoja wao akawaambia wenzake wawili, “ni

sehemu ya kazi yetu, au mmesahau”. Walitazamana

kisha wakaenda kuziegemea pikipiki zao huku

wakiwasubiri wakina Norbert, baada ya muda

Norbert na Joseph waliingia ndani ya gari lao na

kuondoka hospitalini. Three devils nao waliingia

kwenye pikipiki zao na kuanza kuwafuatilia wakiwa

katika namna ya kufuatana katika mstari ulionyooka,

mwenye pikipiki aina ya bajah akiwa mbele kisha

akafuata mwenye pikipiki aina ya boxer na mwisho

akaja mwenye pikipiki aina ya suzuki. Kwa

walivyopangana ilikuwa ni vigumu sana mtu kujua

kama wapo watatu kwa muonekano wa mbele,

walitembea hivyohivyo hadi walipofika jirani na

makutani ya kituo cha kuzimia moto jirani na shule

ya jangwani. Hapo mwenye boxer alitoka pembeni

kisha mwenye suzuki akafuata na kukaa nyuma ya

mwenye bajah kwa upande wa kushoto na kulia.

Hapo ndipo gari ya akina Norbert iliongeza mwendo

kuifuata barabara iendayo magomeni,

“wamegundua

hawa,tuwafuate hivihivi hakuna kuwaacha” aliongea

mwenye bajah kuwataarifu wenzake kupitia simu zao

ndogo zilizokuwa ndani ya sikio. Waliwafuata

wakiwa na mwendo wa wastani ili kuwaondoa hofu

wakina Norbert, walipofika magomeni walifuata njia

iendayo Ilala kisha wakapunguza mwendo ili

kuwapumbaza wakina Norbert na kuhakikisha

hawawapotezi. Hadi wakina Norbert wanaingia

mzunguko wa kigogo na kuelekea upande wa kulia wao walikuwa

wamewaona ila walikuwa mbali kidogo, hapo ndipo

walipokuja kupigwa chenga ya mwili na Norbert

baada ya Norbert kuegesha gari jirani na msikiti

kwenye magari yanayofanana na gari lao. Three

devils walipofika hapo kwenye kona yenye barabara

inayopita msikitini hapo, walisimama kwa muda

kisha wakayaangalia magari hayo kwa umakini

halafu wakaondoka.

Walienda hadi ilipo shule ya sekondari ya Loyola

kwa mwendo wa kasi, hapi ndipo walibaini

wamepigwa chenga ya mwili. Baada ya kubaini

wamepigwa chenga ya mwili, waligeuza pikipiki zao

kisha wakatazamana kila mmoja halafu wakarudi

kule walipotokea. Walipofika kigogo kwenye msikiti

mkabala na shule ya msingi, walikuta bado watu

hawajamaliza kuswali swala ya adhuhuri na moja ya

magari haikuwepo eneo lile. Hali hiyo iliwafanya

wamuite kijana mmoja muuza maji aliyepo jirani,

“hey njoo mara moja!” alipaza sauti mwenye pikipiki

aina ya bajah. Kijana huyo alifika mara moja akiwa

na deli lake la kuuzia maji baada ya kusikia wito

huo, “mambo vipi?” alimsabahi huku akitoa noti ya

shilingi elfu moja kisha akampatia yule kijana. “safi

braza unataka ya shilingi ngapi?” muuza maji

aliitikia salamu kisha akamuuliza maji anayoyataka.

“nipe ya mia saba, halafu samahani naomba

nikuulize” aliongea huku akiweka stendi ya pikipiki

halafu akashuka.

“usihofu braza uliza tu” aliongea muuza maji huku

akimpatia maji.

“eti hujaona gari yoyote aina ya Noah ikija kuegesha

hapa msikitini wakati watu wanaswali”.

“nimeiona braza sema imeondoka kitambo kidogo bila

hata kutoka mtu”.

“poa poa kaka ngoja sisi tuwahi” aliongea huku

akiuma meno yake kwa hasira. Alichukua maji hayo

pasipo kuyanywa kisha akaenda kwenye pikipiki

yake, alipofika akaiwasha kisha akawaashiria

wenzake waondoke, alitia gia kisha akaondoa

pikipiki hiyo huku mkono mmoja akiwa ameshika

maji aliyoyanunua. Alienda hadi kwenye mzunguko

wa kigogo kisha akayatupa maji hayo kwenye mtaro

halafu akavuta mafuta kuelekea njia iendayo Ilala.

Jim ndio jina lake na ndio anavyotambulika hata

kwa wenzake, ni mmarekani aliyeingia Tanzani

miaka miatu iliyopita kwa agizo maalumu la mkuu

wake anayejulikana kwa jina la Eagle kutoka Miami

jijini Marekani. Kijana huyu ni muuaji wa hatari na

wakuaminika wa kundi la Three devil , yupo nchini

Tanzania kwa miaka hiyo ili aweze kutimiza lengo

maalumh aliloamriwa kulitimiza. Jim ameingia

Tanzania kama mfanyabiashara aliyeamia Tanzania

kwa ajili ya kuwekeza, akiwa nchini kwa muda wote

huo amefanikiwa kujifunza lugha ya kiswahili kama

inavyozungumzwa na makundi tofauti ya watu

nchini kulingana na umri na kazi zao. Hadi mwaka

wa tatu ndipo alipoongezewa wenzake wawili wa

kundi lake wakiwa tayari wameshajifunza kiswahili,

sasa wapo kazini na wameshafanikisha sehemu ya

kazi waliyotumwa. Akiwa peke yake amefanikisha

mauaji ya waziri kwa kutengeneza ajali dhidi yake,

pia alijaribu kumuua mwandishi wa habari ingawa

mpango huo ulifeli. Michael na Morris ndio

wamarekani wengine wanaounda kundi la Three

devil wakiwa chini ya Mr Eagle wa Marekani.

Mpango wao wa kwanza toka waanze kufanya kazi

pamoja umefeli baada ya kupigwa chenga ya mwili

na Norbert, sasa wana hasira na wanaelekea yalipo

maskani yao kujipanga upya.



Norbert aliinua kiti cha gari kisha akawasha gari

baada ya zile pikipiki kupita na milio kufifia, alirudi

hadi kwenye mzunguko wa kigogo kisha akafuata

barabara iendayo ilala. Alipofika mataa ya Ilala boma

alikuta taa za upande wake zikiwa zimeruhusu na

kumlazimu kunyoosha moja kwa moja hadi yalipo

mataa ya keko, hapo napo ikawa ni kama bahati

baada ya kukuta askari wa usalama barabarani

akiwa ameruhusu magari ya upande wake. Alikata

kona kuingia barabara ya mwalimu nyerere iendayo

Tazara halafu akaongeza mwendokasi wa gari,

walipofika yalipo mataa ya makutano ya barabara

maarufu kama Tazara aliamua kufuata barabara ya

Mandela iendayo vetenari. Alitumia dakika takribani

tatu akawa ameshavuka vetenari na sasa alikuwa

anakata kona kuingia upande wa kulia kufuata

barabara iendayo mtoni kwa azizi ally kupitia

temeke. Hapo alienda kwa mwendo wa kasi

kutokana na uchache wa magari hadi usalama kisha

akaingia upande wa kulia kwenye barabara ya vumbi

ipitayo shule ya msingi Muungano eneo la temeke,

aliendelea hadi alipoivuka shule ya msingi

muungano kuingia

kushoto kisha akaenda moja kwa moja hadi katika

nyumba moja yenye geti kubwa jeusi kisha akapiga

honi. Ndani ya dakika moja geti lilifunguliwa kisha

akaingiza gari hafi kwenye maegesho ya nyumba

hiyo, alikanyaga breki kisha akazima gari halafu

wote wakashuka kwa haraka huku wakihema kama

wamekimbia mbio ndefu. Wakiwa na mwendo wenye

papara kama wamekuja kwa shari, waliingia ndani

ya nyumba hiyo kupitia mlango wa uani hadi katika

ukumbi wa nyumba hiyo unaopendeza kuutazama.

Waliwakuta wakina Hilda, Davis na Allison wakiwa

wapo kwenye meza ya inayotumika kwa chakula

iliyopo katika ukumbi wa pili jirani na ukumbi wa

sebule wa nyumba hiyo, Joseph alijitupa kwenye

kochi huku akihema mfululizo na Norbert alibaki

kasimama huku mikono yake ikiwa imeshika kiuno

chake na kichwa akiwa anakitikisa kwa masikitiko.

“nyie wanaume vipi kwema?” aliuliza Hilda baada ya

kuwaona wakiwa katika hali hiyo.

“ni kinyume cha kwema” alijibu Norberr huku

akintoa kitambaa mfuko wa nyuma wa suruali yake

kisha akajifuta jasho katika uso wake.

“kulikoni” aliuliza Hilda huku akigeuza kiti

kuwatazama Norbert na Joseph.

“yule jamaa niliyemuona msata na kibaha

tumuona tena muhimbili leo akiwa na wenzake

wawili” aliongea Joseph halafu akajiweka sawa

kwenye huku

akihema kisha akasema ,”walikuwa wanatufatilia

pasipo sisi kujua, na hata tulipojua Nor aliongeza

mwendo wa gari na wao wakaongeza mwendo wa

pikipiki zao kutufualia hadi sehemu moja yenye

msikiti wa ghorofa. Hapo ndipo Nor akawapiga

chenga wakapotea”.

“pongezi kwako mr Transporter kwa kucheza na

usukani kama unamkimbia aduo kuu” aliongea Allison kumfananisha Norbert na

muigizaji Jason Statham wa Uingereza aliyeigiza

filamu ya The transporter. Wote walicheka humo

ndani kasoro Joseph.

“yaani nyie sisi tumekimbia umauti mnatucheka, na

wewe Nor unacheka wakati ulikuwa unawindwa”

alipngea Joseph huku akijigeuza kwenye kochi kisha

akalala chali kuangalia dari la nyumba hiyo.

“Jose na wewe umezidi uoga” Davis alisema huku

akicheka

“ndugu kifo kitu kingine kabisa msilete mzaha”

Joseph alisema akiwa anajiinua kivivu kwenye kochi

huku wenzake wakicheka, aliposimama wima alienda

moja kwa moja hadi kwenye jokofu lililopo jirani na

meza ya chakula. Alitoa pombe kali kisha

akaifungua halafu akaipeleka kichwani, alikunywa

funda moja halafu akawatizama wenzake na

kuwaambia “mimi leo wacheni nipumzike mpaka

kesho, mnaweza mkaendelea”. Joseph alifuata

ukumbi mwembamba

unaotenganisha vyumba vya humo ndani kisha

akfungua mlango mmoja wa vyumba halafu akaingia

ndani na kuufunga. Huku katika ukumbi wa

unaotumika kama sehemu ya chakula Norbert

alivuta kiti kilicho jirani na Hilda kisha akakaa karibu

ya Hilda, “mahaba niue hao wapo pamoja” aliongea

Davis kuwatania Norbert na Hilda.

“we ulitaka tuwe mbalimbali kwani?” Hilda alisema

akiwa

ameweka mkono wake katika bega la Norbert.

Waliendea kuongea huku wakitaniana kwa muda

mfupi kisha ukimya ukatawala huku Norbert na Hilda

wakiwa wanakumbatiana na kupigana na mabusu

hapo mezani.

“ngoja tuwapishe nyie mahaba niue”

aliongea Davis akivuta kiti nyuma kisha akasimama

halafu akaondoka eneo hilo, Allison naye alisimama

akaondoka kumfuata Davis. Wakiwa wamebaki

wenyewe hapo ukumbini Hilda alinyanyuka katika

kiti chake kisha akaenda kukaa katika mapaja ya

Norbert miguu yake akiipitisha kiunoni mwa kijana

huyo. Hapo waligusanisha mapaji yao uso wakawa

wanatazamana kwa ukaribu, hakika walionekana ni

watu waliozama kwenye mapenzi mazito sana kwa

mkao huo waliokaa.

“kuna simu leo kutoka kwa CE imeingia leo

asubuhi” aliongea Hilda kwa sauti ya chini

“mh! huyo kibabu anasemaje?” aliuliza Norbert kwa

sauti ya chini.

“anataka kuongea na wewe, amesema ukirudi

nimpigie”

“mh! Kuna jipya limezuka nini?” Norbert aliuliza

swali hilo kisha akamnyonya ndimi Hilda huku

akimpapasa mgongo baada ya

Joseph kutokea eneo hilo.

“wa mahaba subirini kwanza nichukue kinywaji ndio

muendele”

Joseph aliwaambia kwa sauti iliyochangamshwa na

pombe halafu akafungua jokofu, alitoa

pombe kali ya pili kisha akaondoka..

Hapo Norbert aliacha kunyonya ndimi ya Hilda huku

akiwa amegusanisha paji la uso kama alivyokuwa,

alihema kwa nguvu kisha akasema, “hizi kazi hizi

aisee ni tabu kila siku kama wacheza filamu”. Kauli

hiyo ilimfanya Hilda acheke kwa sautu ya chini

akiwa tayari ameshaingiwa na aibu zake za kike.

“Nor inabidi umpigie CE leo hii maana unamjua yule

mzee akisema ujue kuna jambo” Hilda aliongea

huku ameelekeza macho yake pembeni kwa aibu.

Norbert alimshika kidevu halafu na kumfanya Hilda

amuangalie kwa macho malegezo. Walitazamana

kwa muda mfupi kisha Norbert akambusu Hilda

mdomoni jambo lililosababisha binti huyo afumbe

macho kwa hisia.

“Nor bwana ushaniweka katika wakati mgumu

mwenzio kumbuka tupo kikazi acha tafadhali” sauti

ya kudeka na yenye kubembeleza ilitoka kinywani

mwa Hilda, muda huo tayari Hilda alikuwa ameibana

miguu yake kwa nguvu katika kiuno cha Norbert.

“najua mama ila hapa imebidi tuwe hivi” aliongea

Norbert huku akinyanyuka na Hilda pamoja akiwa

amembeba kama anampeleka mtoto aliyelala

kitandani. Hilda naye alikuwa amepitisha miguu

kiunoni mwa Norbert na mikono ikiwa shingoni kwa

Norbert huku vifua vyao vikiwa vimegusana. Norbert

alitembea kuufuata ukumbi mwembamba

unaotenganisha vyumba vya kulala katika nyumba

hiyo, alipofika katika mlango wa chumba ulio

mkabala na chumba alichoingia Joseph alinyonga

kitasa huku mlango ikikaidi amri ya kufunga na

ukatii amri ya kufunguka. Alimuingiza binti huyo

ndani kama anaenda kumlaza mtoto, alienda hadi

kwenye kitanda kisha akamuachia kitandani ili arudi

kufunga. Hadi muda huo Hilda alikuwa yupo

amelazwa kitandani ila hataki kutoa miguu kiunoni

mwa Norbert wala mikono shingoni.

“no Hil wacha nifunge mlango kwanza” aliongea

Norberr na kupelekea Hilda amuachie, Norbert alienda

kufunga mlango kisha akarejea kitandani hapo

alipomuacha Hilda. Muda huo tayari Hilda alikuwa

amelala chali akiwa amejiweka huru kabisa, Norbert

alipanda juu ya kifua chake kisha wakagusanisha

ndimi na kupelekea wote waingie kwenye

ulimwengu mwingine tofauti na sayari hii ya dunia.

Hakika kila mmoja alionesha kumuhitaji mwenzake

na hakuna aliyekuwa kumuacha mwenzake kwa

muda huo, kazi yao waliiweka pembeni kwa muda ili

kuhitimisha kazi hiyo isiyo rasmi. Baada ya masaa

mawili walikuwa wameshakamilisha kazi yao na

sasa wamepitiwa na usingizi mzito wakiwa

wamejifunika shuka moja, ilipotimu saa kumi na

moja jioni usingizi wao ulikatika baada ya simu ya

mkononi inayotumiwa kwa ajili ya kazi kuita.

Norbert aliinuka kivivu huku akiangalia mpigaji wa

simu hiyo akiwa na uchovu mwingi, jina la mpigaji

lilimuondoa uchovu kisha akaipokea simu hiyo kwa

pupa kisha akaongea ,”N001 hapa naongea”.

“njoo ofisini haraka ukiwa na HI002” ilisikika sauti

ya mpigaji ikitoa amri kisha simh ikakatwa. Norbert

akaiweka simu kwenye mtoto wa mtanda kisha

akampiga Hilda kibao katika kalio lake halafu

akamwambia, “CE katuita sasa hivi, jiandae twende

ofisini kwake”, kisha akaokota kaptula yake

aliyoitupa wakati wanaanza kasheshe na kuivaa

mwilini. Hilda naye alishaamka na alikuwa

anajinyoosha akiwa hana nguo yoyote mwilini.

“aisee kama siyo kazi tungekesha leo, maana

nikikutazama mh!” aliongea Norbert na kusababisha

Hilda amtizame jicho la upande kisha akasema

“looh! Lionee”. Hilda alijifunga taulo kisha

akamshika Norbert mkono, alimuongoza hadi bafuni

pasipo Norbert kuleta pingamizi lolote. Huko

walioga kisha wakatoka baada ya kumaliza,

walijiandaa kisha wakatoka humo chumbani hadi

sebuleni wakiwa wameshikana mikono kiupendo. Sebuleni waliwakuta Allison na Davis wakiangalia luninga na kuwaaga kisha wakatoka hadi nje kwenye banda la

gari lililopo jirani maegesho ya gari ndani ya

nyumba hiyo, walifungua milango ya banda hilo

halafu wakaingia ndani kulifuata gari aina ya suzuki

ya rangi nyekundu. Waliingia wote kwa pamoja huku

Norbert akiwa ndio dereva wa gari hilo, mlio wa

kuwashwa kwa gari hilo ulisikika kisha matairi yake

yakaanza kujongea taratibu na kusababisha gari

litoke kwenye banda la gari na kufuata uelekeo wa

getini. Geti lilifunguliwa na mlinzi kuruhusu gari hilo

litokee nje ya nyumba hiyo kwa mwendo wa

taratibu, mwendo uliongezwa baada ya kuingia

katika barabara ya vumbi inayopita shule ya msingi

muungano kuelekea usalama kwenye barabara ya

lami.



Ndani ya nyumba ya ghorofa iliyopo maeneo ya msasani kwenye moja ya mitaa ya msasani ambayo huwa wanaishi watu wenye kipato cha juu, kulikuwa na kikao cha dharura katika moja ya chumba cha mikutano cha nyumba hiyo na wahudhuriaji wake walionekana ni watu wenye kujiweza kiuchumi na wenye kauli.

Mmoja akiwa ni kigogo maarufu wa Tanzania anayetumia jina KL akiwa sehemu kama hizo, mwingine akiwa ni kiongozi maarufu anayejiita FI na wengine ni vijana wa kundi la Three devils. Suala lililokuwa linajadiliwa katika mkutano huo ni kuhusu mpango wao madhubuti wa kupunguza vikwazo katika mambo yao. Hadi muda huo wote walishapeana salamu na sasa walikuwa ndio wanaanza kujadili, “wakuu napenda mjue kuwa tushapunguza moja ya magugu katika kubakikisha shamba letu linastawisha mazao yetu” Jim aliongea kwa kutumia lugha ya mafumbo kutokana na uwepo wa wafanyakazi waliokuwa wakiwahudumia wahudhuriaji wa mkutano huo.

“vizuri Jim sasa naona kuna gugu jingine nitaliweka katika anga zenu ili muliondoe upesi kama ilivyokuwa kwa gugu la kwanza mtindo ni uleule” aliongea FI kumpongeza Jim kisha akampa kazi nyingine hapohapo.

“pia ningependa ningependa wale kenge watano waondolewe haraka maana ni hatari sana” KL alitoa wazo hilo kwa kutumia lugha ya isiyo ya mafumbo baada ya wafanyakazi wote kutoka katika chumba cha mkutano. “hao ni kiporo kwanza kwa sasa tushughulikena hawa wenye kauli huku tukifunga midomo kupitia kwa wachapishaji” aliongea Michael kwa mara ya kwanza.

“wazo zuri hilo Michael sasa baada ya huzuni kutulia nitaweka gugu jingine jirani na jembe ili liweze kulimwa haraka” FI aliongea kisha akavuta bilauri yenye kinywaji iliyopo halafu akapiga funda moja. “sasa huko tumemaliza ila kwa sasa inabidi tufanye juu chini tuwajue wanausalama wa kampuni ya upelelezi ya EASA walioingia nchini kwa kazi maalum ambayo bado hatujaijua mpaka saea , yaani siba imani nao kabisa” KL alibainisha jambo geni ambalo halijukani kwa wenzake waliopo haoi kwenye mkutano.

“KL hiyo ni habari nyingine ila hawa vijana nina uhakika wataimaliza,sasa mimi na KL tunawahi sehemu mra moja. Tutakuja siku nyingine kuwapa maelekezo kama yakihitajika” FI aliongea baada ya simu yake kuita kisha akanyanyuka akiwa na KL ambaye alishanyanyuka tayari. Walitoka ndani ya chumba hicho cha mkutanina kuwaacha Jim,Michael na Morris wakiwa wanajadiliana mamboyao mengine.



ITAENDELEA

Jinamizi Sehemu ya Pili

Also, read other stories from SIMULIZI;

Leave a Comment